Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Capt. Abbas Ali Mwinyi (4 total)

MHE. KEPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa makampuni yanayotengeneza aina hizo za ndege yamesitisha utengenezaji, sasa je, Serikali haioni itakumbwa na changamoto za upatikanaji wa vipuri? Hilo ni swali la kwanza.
Swali la pili, je, lini hasa uboreshaji wa karakana hiyo utaanza? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Abbas Ali Mwinyi kwa uzalendo wake mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba viongozi wetu wa kitaifa wanasafiri katika hali ya usalama mkubwa. Vilevile nikusifu kwa kutumia utaalamu wako mzuri kama rubani mzoefu wa kuhakikisha kwamba ndege zetu zinakuwa salama. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Abbas kwa kuwa ni kweli kwamba Serikali inafahamu hilo; lakini nimhakikishie kwamba vipuri hivyo bado vinatengenezwa na kampuni hiyo hiyo ya Uholanzi ambayo ndiyo mtengenezaji mkubwa wa ndege za Fokker ambako vipuri hivyo vinapatikana kwenye unit yao iliyopo nchini Malyasia.
Mheshimiwa Spika, vilevile huko nchini Malyasia ambako ndiko vipuri vinapotengenezwa kuna unit yao ya mafunzo (training center) ambako wanafanya re-validation ya licence na kwa ndege hizo marubani wetu wote huwa wanakwenda kule kwa ajili ya ku-review leseni zao. Nimhakikishie Mheshimiwa Abbas kwamba vipuri vipo vinapatikana kwenye unit yao hiyo na tutaendelea kuvitumia na tunaendelea kuwasiliana kwa ajili ya matengenezo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili ni kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la msingi. Mara TGFA watakapotuletea makadirio basi Serikali itatenga pesa kwa ajili ya matengenezo ya hanga hilo la ndege, ahsante sana.
MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nami niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zipo baadhi ya Taasisi za Serikali ambazo zinakidhi vigezo vya mkopo kutoka katika mabenki ya kibiashara. Je, taasisi ya aina hizo ni ruksa kukopa kwa lengo na madhumini ya kugharamia miradi yao bila kuingiliwa na Serikali?

Swali la pili, zile taasisi kama alivyojibu Mheshimiwa Naibu Waziri, hazipeleki chochote na ni mzigo kwa vile ni tegemezi katika suala zima la ruzuku. Je, ni busara kuendelea na aina hiyo ya taasisi? Ahsante sana.(Makofi)
WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, kwanza napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa alivyojibu swali la msingi, lakini pili, napenda kujibu swali la Captain Abbas Ali Mwinyi, Mbunge wa Fuoni kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba zipo taasisi ambazo zinakidhi vigezo vya kukopa Serikalini, lakini taasisi hizi zina mwenyewe ambaye ni Msajili wa Hazina. Kwa hiyo, japokuwa kazi hizi zinakidhi vigezo vya kukopa bado zinahitaji ruhusa ya Serikali kupitia kwa Msajili wa Hazina kabla ya kuweza kupata mikopo ili kuweza kuteleleza miradi yake ambayo nayo inabidi ipitiwe na kupitishwa na Wizara na kuingizwa kwenye bajeti kama ambavyo tumepanga hapa.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ni kuhusu taasisi tegemezi, taasisi tegemezi tulizonazo ni zile ambazo zinatoa huduma ambazo zinategemea ruzuku ya Serikali. Kwa hiyo, ni muhimu ziendelee kuwepo kama Taasisi za Bodi za Usajili ambazo hazizalishi mapato bali zinatoa huduma kwa ajili ya udhibiti. Ahsante.
MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa chuo hiki kinatoa mafunzo ya aina mbili, yaani nadharia pamoja na practical. Sasa swali ni kwamba, je, Serikali inahakikishaje kwamba kwa wale ambao wanamaliza nadharia na wanatakiwa wafanye practical, hiyo practical inapatikana katika meli gani? Nini mchango mchango wa Serikali katika kuhakikisha kwamba upande wa pili wa practical unapatikana? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU (MHE. PATROBAS P. KATAMBI): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abbas Mwinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ameuliza katika eneo la mafunzo, hasa katika practical training. Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Wakala wa TAESA ambaye yuko chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu, tumekuwa tukitoa mafunzo hayo kwa wahitimu, lakini pia kuna mpango maalum wa chuo chenyewe wa utoaji wa mafunzo ya mabaharia ambao wanahitimiu hapo. Kwa mfano ukiangalia takriban zaidi ya vijana 3,000 waliomaliza katika chuo hicho wamepewa mafunzo. Tunatarajia baada ya marekebisho haya na ukarabati wa chuo pamoja na ongezeko la majengo tayari tutakuwa na uwezo wa kudahili vijana 4,500 hadi 6,500 na hawa wote wanaingia kwenye mpango wa mafunzo. Tumekuwa tukiwapeleka kwenye meli za Wakala binafsi au wawekezaji binafsi pamoja na zile za Serikali.

Mheshimiwa Spika, sasa katika ule mpango wa kupata meli yetu wenyewe kwa ajili ya chou, nao utasaidia katika kufanya practical training ili kuwajengea vijana wetu competence na performance katika kazi hii. Ahsante.
MHE. CAPT. ABBAS ALI MWINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Naridhika sana na majibu ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; kwa kuwa ununuzi au uwekezaji wa hizi ndege 11 lazima uendane sambamba na mafunzo kwa wafanyakazi wake. Sasa Je, kuna juhudi gani za makusudi za kuhakikisha kwamba Serikali inasomesha wafanyakazi hao na hasa marubani, wahandisi na ma-cabin crew ili kuhakikisha kwamba hizo ndege 11 zinakuwa na wataalam wa kutosha wa kuziendesha? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuna wafanyakazi wastaafu wengi wa ATCL wanadai stahiki zao ambazo kwa muda mrefu sana hawajalipwa. Pamoja na ukweli ya kwamba Serikali mwaka 2016 waliliridhia kuchukua deni hilo, lakini kwa bahati mbaya mpaka leo hii mwaka 2022 madeni hayo hayajalipwa. Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusiana na kadhia hii? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Abbas Ali Mwinyi, kama ifuatavyo : -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nitambue namna ambavyo Mheshimiwa Abbas Mwinyi kwamba yeye ni bingwa hasa kwa maana ya masuala haya ya U-pilot na ana licence aina ya ATPL. Ni kweli kwamba Serikali imewekeza sana kama ambavyo nimejibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba imewekeza zaidi ya trilioni 1.44 na kwa msingi huo Serikali imejipanga ipasavyo kusomesha wale wote ambao kwanza marubani, na hivi sasa kupitia chuo chetu cha NIT, Chuo cha Usafirishaji Serikali imetenga zaidi ya bilioni nne kwa ajili ya ununuzi wa ndege ambazo zitatumika kwa ajili ya mafunzo kwa ajili ya marubani kwa kuzingatia kwamba kozi hizo zilikuwa zinatolewa nje ya nchi na kwa bei kubwa zaidi. Tunategemea kwamba ifikapo mwezi Agosti na Septemba, kozi hii itaanza kutolewa na tayari Serikali imeshatoa hizi fedha zote bilioni nne. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la pili ambalo amezugumzia suala la maslahi hususan kwa wastaafu, ambao walikuwa watumishi wa kampuni hii ATCL na sasa wanadai maslahi yao. Ni kweli mwaka 2016 Serikali ilitoa commitment ya kulipa madeni hayo na mwaka 2017 kupitia CAG alihakiki hayo madeni.

Mheshimiwa Spika, mwaka 2021, Wizara ya Fedha kwa mujibu wa sheria pia imehakiki hayo madeni na wanadai zaidi ya bilioni nne na sasa hatua za mwisho kwa ajili ya kuwalipa wastaafu na watumishi ambao walikuwa ATCL ipo kwenye hatua za mwisho ili waweze kulipwa. Ahsante. (Makofi)