Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Emmanuel Adamson Mwakasaka (1 total)

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu.

Kwa kuwa tatizo hili la upimaji wa mchanga linaanzia kule ambako ndiko kuna machimbo yenyewe. Ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha kule origin source kunawekwa mashine ambazo sasa tatizo hili halitajirudia tena?
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Naibu Spika, moja kati ya mikakati ambayo tunayo ni kupokea wawekezaji na tumeanza kuona wawekezaji kadhaa wakija kuonesha nia ya kuwekeza kwenye eneo hili. Awali kulikuwa na usiri mkubwa wa namna ya kuwakaribisha wawekezaji hawa kuwekeza kujenga mitambo hii na ndio kwa sababu Serikali imeanza kuchukua hatua za awali kwa vile tunajua kwamba, kuna maeneo ambayo yalikuwa hayaoneshwi wazi ikiwemo na eneo la kuwakaribisha wawekezaji wa kujenga mitambo hii hapa nchini.

Baada ya muda mfupi kama ambavyo mambo yameanza kujitokeza tutaamua kuwekeza, kujenga mashine zetu hapa hapa nchini au kuwakaribisha wawekezaji au kuona uwezo wa Serikali kama tunaweza ili sasa tuweze kutatua tatizo ambalo linatukabili sasa la kupoteza mchanga ambao tunautoa hapa na kupeleka nje kwa ajili ya uyeyushaji na kupata aina mbalimbali za madini. Ahsante.