Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Answers from Prime Minister to Hon. Job Yustino Ndugai (1 total)

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Hivi karibuni tumepata kuona kupitia mitandao, mwanafunzi aliyejulikana kwa jina Asia ambaye alifaulu vizuri masomo yake ya sayansi amepata division two ya point kumi na moja, lakini mwanafunzi huyu alikosa mikopo bila sababu ya kueleweka, ni mpaka baada ya kujiweka wazi mitandaoni na kulia sana ndipo Loan Board ikaweza kumpa mkopo mwanafunzi huyu.

Naomba kuiuliza Serikali; mwanafunzi huyu ambaye alifaulu vizuri, tena mtoto wa kike na masomo ya sayansi, imekuwaje akakosa mkopo na ni kigezo kipi walikitumia baadaye kumrudisha ili kuweza kupata mkopo? Ahsante sana. (Makofi)
SPIKA: Swali lako ni zuri sana Mheshimiwa Mwanaisha lakini ni very specific, linahitaji muda. Mimi namuagiza tu Mheshimiwa Waziri afanye utaratibu wa kukutafutia jibu hilo halafu mtaongea kwa wakati wenu. (Makofi)