Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Stephen Julius Masele (5 total)

MHE. STEPEN J. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda hiki kina umri wa miaka 42 zaidi hata ya umri wangu na tangu kimejengwa hakijawahi kufanya kazi. Nataka majibu ya uhakika kwamba ni lini kiwanda hiki kitafanya kazi na Serikali imetoa muda gani kwa mwekezaji huyu kuhakikisha kiwanda hiki kinafanya kazi?
Mheshimiwa Naibu Spika, kiwanda hiki kimechukua maeneo na mashamba ya wananchi wa Kata za Chibe, Old Shinyanga pamoja Ndembezi. Je, Serikali iko tayari kuruhusu vijana kutumia maeneo hayo kwa kilimo cha bustani ili wajipatie kipato na ajira wakati tathmini hiyo inaendelea kwa miaka 42 ambayo wamesubiri?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naelewa concern ya Mheshimiwa Mbunge anataka ajira kwa ajili ya wananchi wa Shinyanga, lakini anataka soko la uhakika kwa mifugo yote ya Kanda ya Ziwa. Katika miradi inayonipa shida ni pamoja na kiwanda hiki, huyu mwekezaji hakufanya vizuri. Katika watu ambao katika utendaji wangu wa kazi nakuwa mwangalifu nao ni mwekezaji huyu, siyo mwekezaji mzuri, nimemkabidhi kwa Treasurer Registrar anamfuatilia, kuna masuala ya kisheria. Huyu mtu ametumia kiwanda kile akakopa pesa, sasa anategea tumnyang‟anye kiwanda kile kusudi governments guarantee na pesa aliyokopa iishe, siyo mtu mzuri. Mjomba uniache nimfuatilie kwa uangalifu ili tutakapomkamata tumalize kitu once and for all.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kutumia maeneo, huyu mtu yuko under surveillance na nimekwambia siyo mtu mzuri. Kwa hiyo, maeneo yake msiyaguse asije akasema alishindwa kuendeleza kwa sababu tuligusa maeneo yake. Hata hivyo, ni katika maeneo ambayo nataka nitoe majibu yake haraka sana. Nikueleze, hata tajiri namba moja anafuatilia suala hili.
MHE. STEPHEN J. MASELE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mwezi uliopita Mheshimiwa Rais alifanya ziara kwenye Manispaa ya Shinyanga, Jimboni kwangu na aliagiza Waziri wa Maji aje Shinyanga akiambatana na mimi tukae tujadiliane mgogoro wa bei ya maji baina ya KASHUWASA ambao ni Mradi wa Maji wa Kitaifa na SHUWASA ambayo ni Mamlaka ya Maji ya Manispaa ya Shinyanga na wananchi wa Shinyanga:-
Je, Waziri wa Maji yuko tayari kuambatana na mimi mara baada ya Vikao hivi vya Bunge ili tukakae na wadau wote hao husika tutatue mgogoro wa bei kati ya KASHUWASA, SHUWASA na wananchi wa Shinyanga? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Mradi wa KASHUWASA ni Mradi wa Kitaifa, siwezi kukubali kama Mbunge, wananchi wa Shinyanga wabebeshwe adhabu ya kugharamia mradi wa Kitaifa kwa kubebeshwa bei kubwa ya maji. Nahitaji majibu leo, Waziri kama yuko tayari twende tukashughulikie mgogoro huu.
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mhweshimiwa Spika, kwanza kabisa, kwenda Shinyanga siyo tatizo, tunaweza tukaenda, lakini tunapokwenda kule lazima tuelewane tunachokwenda kufanya. Tunakwenda kule kwanza tunarejea Sheria Namba 12 ya mwaka 2009 inayohusu uendeshaji na utoaji wa huduma ya maji. Ndani ya Sheria ile tuliweka Mamlaka ya Udhibiti inayoitwa EWURA, hii ndiyo imepewa mamlaka ya kupanga bei za maji.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais alichokielekeza ni kwamba, ni lazima tufanye ulinganifu kuangalia, je, maeneo mengine watu wanachangia maji kwa kiasi gani? Kwa Shinyanga Mamlaka ile bado ni changa. Bei ya maji inaweza ikaonekana kwamba ni kubwa kwa sababu ya wachache amboa ndio wanaochangia. Kwa hiyo, Serikali tuna jukumu la kuongeza mtandao ili wananchi wengi waingie kwenye mtandao waweze kuchangia huduma ya maji ili iweze kuwa endelevu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tutakwenda Shinyanga, lakini nataka twende huku wakijua kwamba, siyo kwamba tunakwenda kushusha bei. Tunakwenda kufanya ulinganifu wa kuona ni kipi kifanyike kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji.
MHE. STEPHEN J. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Siku nne ama tano zilizopita mradi mkubwa wa kitaifa wa maji wa KASHWASA Shinyanga ambao unasupply maji Manispaa ya Shinyanga pamoja na mji wa Kahama ulikatiwa umeme na TANESCO kwa sababu ya kutolipa bili za umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kumuuliza Waziri wa Maji nimekuwa nikishauri hapa kwamba Serikali itenge ruzuku ya kusaidia mradi huu ili kuwaondolea mateso wananchi wa Shinyanga, Kahama na Maswa, je, Waziri yuko tayari kutenga
fedha kwenye bajeti ya mwaka huu kuhakikisha kwamba KASHWASA inasaidiwa ruzuku ya kuendesha mradi huo na kuwaondolea mzigo wananchi wa Shinyanga, Kahama na Maswa?
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa kwa utaratibu mamlaka za maji tumeziweka kwenye makundi daraja A, B, na C. KASHWASA ni daraja A, kwa maana kwamba inatakiwa iwe inalipa maji
kutokana na mauzo ya maji. Sasa TANESCO wamekata deni ambalo walikuwa wanadaiwa na tatizo ni kwamba taasisi nyingi zilikuwa hazijaweza kulipa kwa wakati. Tunaendelea kusisitiza kwamba taasisi zote za umma lazima zilipe bili za
maji ili kusudi kuwezesha mamlaka zetu zilipe TANESCO. Kwa hiyo, hilo lililotokea, limetokea lakini kwa hivi tunasema wasiyazalishe madeni mapya na tutafika mahali tutaanza kukatia hata hizo taasisi za umma ambazo hazilipi bili za maji.
(Makofi)
MHE. SUSANNE P. MASELLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, mwezi wa Kwanza mwaka huu wakati Serikali ikijibu swali langu kuhusu wachimbaji hawa wadogo ilisema kwamba inatambua vikundi ambavyo nilikuwa nimewahamasisha wachimbaji hawa kuviunda na itawapatia maeneo ya kuchimba. Hata hivyo, baada ya mwezi mmoja Serikali hii hii ilienda kuwazuia wasichimbe na sasa Waziri ananiambia kwamba tena nihamasishe kwamba waunde vikundi vingine, ni vikundi gani tena hivyo? Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kutatua hii migogoro kwa sababu naona kama wanakwepa kwepa na wamekuwa na ndimi mbili mbili kuhusu huu mgogoro?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, malalamiko ya wananchi ni kuhusu huyu mwekezaji ambaye anamiliki eneo kubwa ambalo lina ukubwa wa ekari 2,250, lakini ameshindwa kuliendeleza na wananchi hawa wana nia njema kabisa ya kuliendeleza na Serikali ilikiri mbele ya wananchi kwamba mwekezaji huyu ameshindwa kuliendeleza eneo hili. Je, Serikali itatekeleza lini hii ahadi yake ambapo ilisema kwamba ingemnyang’anya huyu mwekezaji hiyo leseni na kuwapatia wananchi na si kutumia nguvu kwa ajili ya kutatua migogoro? (Makofi)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nikiri kwamba maswali ya Mheshimiwa Mbunge yana logic, lakini niseme tu kitu kimoja kwamba kuunda kikundi ni hatua moja lakini kumiliki kihalali ni hatua nyingine. Kwa hiyo kile ambacho Mheshimiwa Mbunge alishauriwa na ambacho ndicho msimamo wa Serikali ni kwamba hao vijana wakishakaa kwenye vikundi wanatakiwa pia wafanye zile taratibu za kuweza kumilikishwa kihalali na wakishamilikishwa ndio watakuwa wamekamilisha utaratibu wa kuweza kuchimba kihalali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu mwekezaji anayesema anamiliki eneo kubwa, nalo hilo lina taratibu zake naamini Wizara husika watakapokuwa wamejiridhisha na taratibu zile kukamilika kwenye maelekezo waliyokuwa wameyatoa basi wanaweza wakachukua hizo hatua.

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Nimshukuru Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwa majibu mazuri. Nimwombe tu ndugu yangu Mheshimiwa Susanne Maselle tuweze kuonana ili kuweza kulipata suala hili kwa kina na kuona namna gani tunaweza tukalitatua. (Makofi)
MHE. STEPHEN J. MASELE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, katika utekelezaji wa mradi wa KASHUWASA wa kutoa maji Ziwa Victoria kuleta katika Mji wa Shinyanga na Kahama. Katika mradi ule vijiji vyote vinavyopitia pembezoni mwa bomba hilo vilipaswa kuunganishwa na maji ya Ziwa Victoria. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri alipofanya ziara na Mheshimiwa Makamu wa Rais alituahidi kutupatia pesa katika vijiji vya Bugwandege, Kata ya Ibadakuli, vijiji vya Mwanubi Kata ya Kolandoto, Chibe katika Kijiji cha Mwakalala pamoja na Kijiji cha Ihapa ambapo tank kubwa la Kashuwasa limejengwa pale lakini wananchi wale hawajapatiwa maji.

Swali langu ni kwamba, sasa ni lini zile pesa alizoahidi zitakuja na ili wananchi wale waweze kupatiwa maji kama alivyoahidi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Masele kwa kazi kubwa ambayo anaifanya. Kiukweli kama Serikali tunatambua Mkoa wa shinyanga ni moja ya maeneo yalikuwa na changamoto kubwa sana ya maji na Serikali ikawekeza fedha kwa ajili ya kuyatoa maji Ziwa Victoria na kuyapeleka katika Mji wa Shinyanga.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni kweli vipo baadhi ya vijiji ambavyo havina maji na jukumu la kuwapatia maji ni jukumu letu sisi Wizara ya Maji. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge tukutane sasa haraka na wataalam wetu ili tuangalie namna ya kuweza kutekeleza ahadi hiyo ambayo tuliahidi, ahsante sana.