Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Juma Hamad Omar (6 total)

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa Kipindi cha Januari, 2016 hadi Januari, 2017
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa fursa hii adhimu ya kuchangia taarifa hii muhimu, taarifa ya Kamati ya Bajeti, katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia Januari, 2016 hadi Januari, 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti, nadhani Mheshimiwa Mwambe amezungumza mengi sana na taarifa yenyewe ina mambo mengi sana na muhimu, sasa mimi nitachukua nafasi hii kukazia tu baadhi ya sehemu ambazo nadhani zina umuhimu wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yoyote duniani inapata sifa sana ya maendeleo ya kiuchumi ikiwa itakuwa na mambo matatu yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwanza nchi hiyo inatakiwa iwe na sera sahihi ya uchumi (Prudent Economic Policy); pili, nchi hiyo iwe na sera sahihi ya utozaji kodi (Taxation Policy); tatu, iwe na sera sahihi ya fedha (Prudent Fiscal and Monetary Policy). Sasa mambo hayo matatu yapo katika kapu ambalo linaitwa good governance and political stability. Maana hata hayo mambo matatu kama unayo, lakini kama huna good governance na political stability basi huwezi kuendelea kiuchumi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani mtakubaliana na mimi kwamba ziko nchi nyingi sana duniani, ambazo zimepiga sana hatua za kiuchumi. Kwa mfano, tuchukulie nchi za mashariki ya mbali (far east) nchi zile zimepiga sana hatua. Tukichukua kwa mfano utawala wa Mahathir Mohamad katika nchi ya Malaysia; Mahathir Mohamad alikuwa ni Fourth Prime Minister wa Malaysia, na nina hakika mtakubaliana na mimi kwamba kama kuna mtu alihuisha uchumi wa Malaysia au kama kuna mtu aliujenga uchumi wa Malaysia wa kuja na prudent economic policies, prudent of fiscal and monetary policy, prudent taxation policy basi alikuwa ni Mahathir Mohamad. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Malaysia ya leo ni nchi moja ambayo imepiga a very big economic strive, hivyo nchi nyingine za mbali ya Mashariki. Tuje hapa kwetu Afrika, Botswana ni nchi ambayo ina-enjoy the highest per capital development. Nchi ile haina resource nyingi kuliko Tanzania, nadhani kama sikosei resources zao zaidi wanazotegemea ni madini kidogo na mifugo, lakini leo Botswana ina the highest per capital income, lakini kwa nini? Botswana imefikia pale kwa sababu ya good governance and stability. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani hata ukichukua ile award ambayo ametoa Mo Ibrahim award ile imetolewa kwa Marais wastaafu ambao wamekuwa na a very good governance and good political stability. Rais wa Botswana mwaka 2008, Mheshimiwa Festus Mogae alipata zawadi ile ya dola 5000. Rais Kikwete amestaafu juzi nadhani atapata, lakini sasa kama hii imemaliza 2016 hajapata unaanza kujiuliza ni kwa nini? Kwa hiyo, good governance ni kitu muhimu sana katika yote haya. Botswana ukichukua kigezo cha uchumi cha foreign exchange value, Botswana ina foreign exchange ya kutosha kwa miezi 12. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Nigeria pamoja na kwamba ni old producing country lakini ana foreign exchange ya kutosha kwa miezi kumi kwa sababu kule ndani kumekuwa na political terms, tukija kwetu Tanzania tuna foreign exchange ya kutosha kwa miezi minne, tukija Zimbabwe rafiki yetu ambaye tunampenda sana na tunashirikiana naye sana because of lack of good governance ana foreign exchange siku saba this is amazing! Kwa hiyo, yote mifano inamaanisha kwamba haya mambo matatu, lazima yawe katika kapu la good governance, without good governance you can not make strong economic strives. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuje kwenye Pato la Taifa na tunaambiwa linaongezeka, mwaka 2016/2017 Pato la Taifa tulitegemea kwamba litakuwa asilimia saba lakini tukienda mwaka 2017/2018 itakuwa asilimia 7.2. Swali la kujiuliza infact katika hii region yetu sisi ndiyo tunaongoza kwa Pato la Taifa wanafuatia Rwanda, wanafuatia Kenya. Rwanda katika mwaka 2015 walikuwa na Pato la Taifa la asilimia 6.9; mwaka 2016 matarajio ni kwamba watakuwa na asilimia sita. Kenya ni ya tatu lakini nchi nyingine hizi kama Burundi, Uganda, Zambia, Malawi, Congo DRC zote tunazipita sana.
Kwa hiyo, the first economy in our region ni Tanzania, ni asilimia Saba lakini tunategemea kupata asilimia 7.2. Swali la kujiuliza kama Pato la Taifa linaongezeka kiasi hicho hivi kwa nini hali za wananchi wetu zimekuwa duni? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nasema nikingalia tu, ni kwa sababu sekta inayo-employ watu wengi katika Tanzania ni sekta ya kilimo; na Government yetu haijafanya a big investment katika sekta ya kilimo. Sekta ya kilimo inachangia only 2.1 percent ya Pato la Taifa, sekta ya mawasiliano nadhani kama sikosei inachangia asilimia 15.5, sekta ya uchimbaji madini ndiyo kubwa inachangia asilimi 15.8, lakini sekta ya uchimbaji madini inaajiri watu wa nje. Sekta ya mawasiliano na uchukuzi sawa lakini haina direct impact na mkulima, lakini kwa sababu Serikali haija-mark very big investment over areas katika sekta ya kilimo ndiyo ukakuta leo sekta ya kilimo ambayo imaajiri watu wengi, inachangia only 2.1 percent. Hapa inaonesha kwamba hatuna a prudent economic policies kupanga ni kuchagua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija hapo hapo kwenye Pato la Taifa, mimi nakubali fine Tanzania is a fast growing economics in terms of GDP, lakini that is a nominal terms. In real terms tunakwenda chini; wakati tunazungumza Pato la Taifa linaongezeka lakini pato la kila Mtanzania linapungua in real term. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2014 kwa mfano pato la Mtanzania kwa wastani alikuwa anapata dola 1,047, lakini mwaka 2015 imeshuka anapata dola 966.
MBUNGE FULANI: Mhh!
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Ndiyo! Hii ni kwa sababu sekta ya kilimo ambayo kwa kweli ilikuwa tuweke priority na ambayo inaajiri watu wengi but government has done nothing when it comes to investment.
Sasa kama hatuja-invest kwenye sekta ya kilimo ambayo inaajiri watu wengi nakuhakikishieni in real term fine, wataalam wanatuambia Pato la Taifa linaongezeka but in nominal terms pato haliongezeki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye mapato (taxation policy); hakuna Serikali yeyote duniani ambayo inaongozwa….
MWENYEKITI: Tunaendelea!
Muswada wa Sheria ya Fedha wa Mwaka 2020 (Toleo la Kiingereza)
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Kwanza nataka nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan, kwa uono wake wa kuleta bajeti ambayo ni ya kimapinduzi. Nimekaa kwenye Bunge lako hili vipindi vinne na nikiwa Waziri katika Serikali hii; lakini sijapata kuona bajeti ambayo ya viwango kama bajeti ya Mama Samia Suluhu, kwa hiyo nimpongeze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nimpongeze sana Waziri wa Fedha, Waziri wa Fedha ni msikivu sana. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Bajeti, kama kuna Waziri ambayo amesikiliza maoni yetu basi ni Mheshimiwa Waziri Mwigulu Nchemba. Kwa kweli tulitofautiana lakini baadaye tukaja ku-make a consensus, kwa hivyo tunamshukuru sana; kaelewa matakwa yetu na yeye katupa fikra zake, lakini mwisho wa siku tumefikia malengo mamoja. Nasema nampongeza kwa hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nichangie kidogo kuhusu Ndugu yangu Mheshimiwa aliyetangulia. Mheshimiwa aliyetangulia alisema kwamba; Sheria ya Ushuru wa Bidhaa, hasa kwa vinywaji vikali; inatakiwa kwa mujibu wa kifungu 124(2) cha Sheria hii, kwamba vinywaji hivi vikali vitozwe excise duty kulinga na interest rate, lakini siyo kulingana na interest rate na viashiria vingine vya uchumi. Sasa nataka nimwambie ndugu yangu huyu kwamba lengo kubwa la kutoza excise duty ni ku-deter madhumuni ambayo yalikuwa yanaleta athari au mambo ambayo yaliyokuwa yanaleta athari kwa maisha ya binadamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pombe kali pia ni moja ya jambo linaloleta athari katika maisha ya binadamu, nafikiri atakubaliana na mimi. Kuna wengine wanakunywa pombe, mimi sinywi pombe na wala sijapata kunywa katika maisha yangu; lakini basi angalau unywe pombe hizi bia bia. Unakwenda kuchezea GIN, unakwenda kuchezea gongo na kadhalika. Hiyo inaleta athari katika mwili wako ndio maana imekuwa imposed hiyo excise duty of 30%. Bahati nzuri Serikali imependelea imerejesha to 20%. Kwa hiyo, nafikiri Serikali ingeiacha vilevile 30% ili iwe deterrent kwa wale watumiaji wa pombe kali kama hii.

T A A R I F A

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Taarifa.

MWENYEKITI: Taarifa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Hamad ni rafiki yangu sana, lakini hoja yangu; halafu asiwe anajibu, hoja yangu ilikuwa based kwenye Sheria ya Excise Duty yenyewe anayoizungumza Kifungu 124(2) ambacho kimeelezea mazingira ambayo Serikali inatakiwa izingatie wakati inatoza excise duty. Sheria inasema inatakiwa iangalie mazingira mawili; iangalie mfumuko wa bei na iangalie shughuli zingine za kiuchumi. Nataka aelewe mimi argument yangu…

MWENYEKITI: Sasa Mheshimiwa Halima, unachangia au unatoa taarifa.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampa taarifa kwamba Mzee hii ni sheria sio mimi. Sheria iliyoletwa na Serikali na sheria ambayo...

MWENYEKITI: Haya ahsante, Mheshimiwa Hamad.

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unaweza ukaipokea au ukaipotezea tu kama ilivyo utamaduni.

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani nimefahamika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema sheria hii imezingatia suala la mfumuko wa bei na viashiria vingine vya uchumi; na kwa kweli lengo kubwa la kutoza excise duty ni ku-deter yale mambo ambayo yana athari kwa maisha ya binadamu, hilo ndilo lengo kubwa, namtaka Mwanasheria aende akasome atakuta hiyo. Sasa pombe kali ni hatari kwa maisha ya binadamu and that’s why ikatozwa excise duty to that tune; lakini bado Serikali imekuwa generous imepunguza from 30% to 20%.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo, nasema hivi, nataka niipongeze Serikali. Kwanza juzi alipokuwa ana-windup Mheshimiwa jana au juzi, alipokuwa ana-windup Waziri wa Fedha alisema wameongeza fedha za ziada, akataja kwa mfano Elimu ya Juu to the tune of 70 billion, ununuzi wa vifaa vya afya 50 million, TARURA around 322, 121 billion miradi ya maji na kadhalika. Hiyo yote ukijumlisha utakuta kwa mfano 563 billion, lakini chunk kubwa inakwenda kwenye TARURA, lakini TARURA tayari kuna vyanzo vyake vya fedha; ambavyo tumeviweka katika bajeti au vimeelezwa katika Finance Bill hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ninachotaka kusema ni kwamba; kwanza nampongeza sana kwa kiasi hicho, lakini kinyume na Mjumbe alivyosema kwa sababu Appropriation Act tumeshaipitisha, haiwezekani tena kufanyika supplementary budget, lakini hapa kitakuja kitu kinaitwa reallocation within the boards. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nisisitize kitu kimoja, kwa sababu hii ni pesa nyingi inakwenda TARURA, naomba, naomba, kwamba hii fedha iwekwe kwenye Mfuko Maalum na Mfuko huu ujadiliwe kwenye Bunge kama hizi sheria zinavyotaka na Mfuko huu uwe ring fenced; isije ikatokea kutumika katika matumizi mengine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, finance bill inapendekeza kwamba zile bidhaa ambazo kuwa zinakuja kwa ajili ya horticulture hasa haya mabarafu, kwamba zipunguziwe ushuru au zisamehewe. Nilidhani jambo sahihi kwa sababu horticulture ni mapinduzi makubwa sana katika kilimo, nafikiri wenzetu Wakenya sasa hivi wanapata karibu two billion dollars per annum kwa horticulture peke yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nafikiri sisi nafikiri tukwenda kwenue chain nzima ya hotculture sio hivi majokofu tu madogo madogo na hata hizi containerized structure ambazo huwa ni za baridi zile au suala la greenhouse pia zingesamehewa kwa sababu kuzihuisha hii sekta ya horticulture. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani kama tuna manage kupata two billion dollars hiyo ni all most our half of our foreign change raging, kwa hiyo nadhani Serikali ingekazia sana kuboresha hii horticulture. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni kwamba bajeti hii imeweka mkazo kwenye kilimo, pamoja na kwamba mchango katika bajeti katika kilimo ni mdogo sana lakini the fact kwamba imekubalika kupunguza au kusamehe ushuru katika sekta hii basi ni ishira ya kwamba tunaelekea kuzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa hivyo, nataka nipendekeza mambo maili, kwanza katika hili kilimo nadhani hii ni mapendekezo haimo kwenye finance bill. ni vizuri tukaboresha utafiti sasa hivi Tanzania utafiti wa mbegu bora, utafiti wa mitamba, utafiti wa zana bora za kilimo, sasa hivi Tanzania tuna issue za utafiti kama 10, na bajeti ya utafiti, research and development, nafikiri ni pesa kidogo sana, ni around 3.3 trilion hii ni pesa kidogo sana, kwa hiyo, ni vizuri katika bajeti zinazokuja tuboteshe kuweka fedha nyingi katika utafiti na utafiti unasaidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo China na Malesia wanatumia around 3.4 percent of the GDP kwa utafiti. Kenya wenzetu wanakaribia one, sisi hatujafika one percent of the GDP. Ujerumani na korea walitumia more than five of the GDP na ndio maana yake Ujerumani leo katika sekta ya magani, all most cars katika Dunia zinapatikana Ujerumani masadis bens, BMW, Odi. Korea ninahakika ilo si la kubishana lakini wanatoa simu hizi za Samsung ambazo ni the best in the world, kwa hiyo utafiti unasaidia, nadhani tu-concentrate katika bajeti inayokuja katika utafiti. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika kilimo, tuhimize matumizi ya bwana shamba, agriculture extension officers, sisi hapa tuna mabwana shamba wanaofika 7,000 na mahitaji 22,000. Na ni jambo la kushangaza tukilinganisha na wenzetu wa Kenya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kenya in terms of coffee production imelima less hectarage compere to Tanzania but, Kenya the yield per hector ni kubwa kuliko sisi, inamaana Kenya wanatoa kahawa nyingi kuliko Tanzania, despite the fact kwamba sisi Tanzania tuna hectarage ndogo, kwa hivyo na yote kwa nini, kwa sababu ya bwana shamba, wenzetu wa Kenya wanawatumiwa mabwana shamba wao vizuri sana, wanakwenda mkulima kwa mkulima, mti kwa mti kinyume na sisi, mabwana shamba wetu hawa tulionao 7,000 wanakaa maofisini. Sasa nadhani imefika wakati saivi kwa mabwana shamba wetu wasikae ofisini badala yake waende kwenye mashamba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kenya wao wanakwenda shamba kwa shamba, mti kwa mti, Kijiji kwa Kijiji kitu kama hicho. Sasa na sisi ni muhimu we should make use our agriculture extension officers, nasema hivi tukifanya hivi mimi ninahakika yield per hectare itaongezeka kwa mazao yote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niseme hivi kwamba nataka niunge mkono kwa dhati, finance beld ya Waziri wa fedha, na ninawaomba waheshimiwa wabunge wote tuunge mkono hii kwa asilimia mia moja, ahsante sana. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2016 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kuchukua fursa hii kukushukuru sana kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna siku nilifarijika sana katika Bunge hili ka Kumi na Moja ni siku ambapo Katibu Mkuu wetu Maalim Seif Sharif Hamad alituita kwenda kutuasa sisi Wabunge. Hiyo aliifanya baada ya kile kikao cha kuapa. Naomba ninukuu; alitueleza hivi:

“Mnapokuwa Bungeni jaribuni kuikosoa Serikali ili ifanye vizuri na mnapoikosoa, basi mkosoe kwa maana ya constructive criticisms kwamba muwashauri, kama hili halikufanyika vizuri, basi wafanye nini?” (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili akasema, “mnapokuwa Bungeni pale ambapo Serikali inafanya vizuri, basi muisifu.” Huo ndiyo ulikuwa wasia wa Maalim Seif Sharif Hamad. Wenzangu wa CUF kama nasema uongo wanisimamishe hapa wanipe utaratibu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hiyo haitoshi, Mama Lulida amesema, tuliapa na sisi wote ni waumini wa Mwenyezi Mungu. Tuliapa kwa kutumia Biblia na Quran kwamba tutaitumikia Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa maslahi ya wananchi wetu ambao tumewawakilisha hapa. Kama hiyo haitoshi, kila siku hapa asubuhi tunasoma Dua ya kuliombea Bunge na kumwombea Rais wa Jamhuri ya Muungano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Dua zetu za kila siku, maana nataka ninukuu kipande kidogo tu: “Ewe Mwenyezi Mungu, Muumba Mbingu na Ardhi, umeweka katika dunia yako hii au katika Ardhi yako hii Mabunge au Mabaraza ya kutunga sheria na Serikali za wanadamu ili haki itendeke kama upendavyo wewe Mwenyezi Mungu. Tunakuomba sisi Wajumbe wako utupe hekima na busara ili kujadili mambo yetu kadhaa, kadhaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka nijadili hii bajeti ya mwaka 2017/2018 kwa mustakabali huu. Nafikiri ni vizuri kabla ya kujadili bajeti ya mwaka 2017/2018, tufanye tathmini ya bajeti iliyopita ili tujue what went wrong in the 2016/2017 budget, what are the challenges that we faced? Tukifanya hivyo tutakuwa tunaitendea mema bajeti ya 2017/2018. Bila hivyo, no, hatuitendei haki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa la bajeti ya mwaka 2016/2017 ni kuelekeza matumizi in such a way kwamba development budget tuitengee asilimia 40 na recurrent budget tuitengee asilimia 60. Sisi tulimpongeza sana Mheshimiwa Dkt. Magufuli kwa sababu kwa mara ya kwanza anazungumzia maendeleo ya watu na huko nyuma ilikuwa chini ya asilimia 40. Sasa tuje kwenye ukurasa wa 30 wa budget speech ya Mheshimiwa Waziri. Naomba sana kama mna vitabu mfungue ukurasa wa 30. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa wa 30 kwenye paragraph ya 41, sitaki nisome ile paragraph yote, lakini kwa ufupi anachosema hapa ni kwamba up to April, 2017 tumekusanya 20.03 trillion. Sasa hivyo kwamba tumeweza kutekeleza recurrent expenditure kwa asilimia 87.4 na tumetekeleza development expenditure kwa asilimia 38.5. Sasa Mheshimiwa Waziri waambie wataalam wako kule kwamba huku usifikiri Wabunge hawakusoma; sisi wengine tumeichambua neno kwa neno hotuba hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa if you add those two ingetufanya tupate 100 percent au tupate less than 100 percent kwa sababu hii ni mpaka Aprili lakini uki-add 87.4 percent na uka-add na 38.5 percent unapata 125.9 percent. Maana yake nini? Ni kwamba kile kilichokuwa kadirio kutumika katika bajeti hii, kimetumika na tumeongeza fedha nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye real na nominal terms; maana kuna wakati nilisema hapa, kuna vitu viwili; kuna kitu kinaitwa real terms and nominal terms. Is this budget real, ya 2016/2017? Is this real? Sasa nafikiri bajeti ya mwkaa 2016/2017 is not realistic. Angalau hii ya 2017/2018 now it is real, lakini angalau ni nzuri, it is healthier. Uki-compare bajeti mbili hizi; ya 2016/2017 na 2017/2018, hii bajeti ya sasa ni healthier kwa sababu imewalenga wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niishukuru sana Serikali kwa kubana matumizi, hilo wame-achieve vizuri, lazima tuwashukuru; lakini kwa maana ya mapato ambapo ndiyo msingi wa bajeti yote, bado tuna kazi kubwa. Nataka niwaambie, hakuna Serikali yoyote duniani inayoweza ku- survive bila tax revenue. Marekani imefika stage kwamba ikiwa wewe ni mgombea wa Urais kama ume-evade taxes, basi wanasema hufai kuwa Rais wa nchi hiyo. Kwa hiyo, naelewa umuhimu wa kukusanya kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka niseme, katika hili suala la kukusanya kodi kuna siri tatu; moja, collect taxes with minimum inconvenience to the tax payers; ya pili, kusanya kodi hizi rates za kodi ziwe affordable to the tax payers; lakini la tatu, kusanya kodi ili yule mlipa kodi aone kuna good returns katika maisha yake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niipongeze Serikali; kwa maana ya minimum inconvenience to the tax payers Serikali imefanya vizuri sana. Tuna mifumo mbalimbali ya kielektroniki ambayo sasa hivi tunaitumia; juzi Kamati ya Bajeti tulikwenda kukagua ule mtambo wa TTMS ambao kwa kweli utawezesha kujua kodi za operators wa simu hawa on timely basis, lakini pia tuna mfumo pale katika Idara ya Forodha ambao unaitwa TANCIS; ni mfumo wa kielektroniki wa kujua ni nani aliyelipa kodi na wakati gani na kiasi gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo ni kwamba ule Mfumo wa TANCIS bado ni TRA ndiyo imekuwa nao, lakini kuna wadau wengine ambao wanapaswa kukusanya kodi kwa niaba ya TRA, ule mfumo hawana. Nadhani ni vizuri tuishauri Serikali hapa kwamba wale wadau wengine nao wa-adhere to that TANCIS system.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niende haraka haraka. Kama kuna kitu ambacho kimesahaulika katika bajeti hii ya 2017/2018 ni suala la utalii. Mapato yatokanayo na utalii sasa hivi ndiyo mapato makubwa kwa maana ya foreign exchange tunayo-earn. Nafikiri kama sikosei, asilimia 17.5 ya mapato yetu ya nje yanatokana na utalii. Wenzetu wa Kenya wamechukua comperative advantage; wakati sisi tulikubaliana wote katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kwamba tutoze VAT, wao hawakutoza. Kwa hiyo, bei ya mtalii kuja Tanzania sasa hivi imekuwa ghali sana kuliko kwenda Hija. Tunakosa watalii wengi na huenda baada ya muda mdogo sana tukakuta mapato yetu yana-decline kabisa katika Sekta hii ya Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi tuna comperative advantage ukilinganisha na Kenya. Over the years kuanzia 2011 mpaka sasa hivi namba ya watalii in Kenya inapungua, sisi huku inaongezeka na inategemewa kwamba mwaka unaokuja namba ya watalii itakuwa kama milioni moja na kitu in Kenya na milioni moja na kitu hapa kwetu. Kwa hiyo, kama tutajipanga vizuri, tutaondoa kodi hii VAT on tourism, basi nina uhakika tuna uwezo wa kukusanya mapato zaidi ya Kenya. Kwa hiyo, naiomba Serikali inapokuja na Finance Bill iliangalie suala… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)
Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya SADC ya Usimamizi wa Mazingira kwa ajili ya Maendeleo Endelevu (The Southern African Development Community SADC – Protocol on Environmental Management for Sustainable Development)
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Mimi kidogo mchango wangu utakuwa ni tofauti na wachangiaji waliopita. Kwanza kabisa, naomba kuunga mkono kabisa kabisa, mia kwa mia Itifaki hizi mbili za mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono kwa sababu ni jambo ambalo linatu-affect vizazi vya sasa na vizazi vinavyokuja. Nataka nianze kwa kusema, hii ozone layer hai- belong to any state, wala siyo ya mtu binafsi. Mwenyezi Mungu alipoumba dunia akaweka ozone layer. The question now rise, why should there be no depletion of ozone layer? Ozone layer ina mambo mawili makubwa; moja, ni production of oxgen. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mtu wa chemistry, kwa hiyo, nataka niwalete kwenye chemistry. Nafikiri wale wale waliokuwa hawanifahamu, degree yangu ya kwanza ya Bachelors ni Physics Chemistry, lakini ya pili nime-specialize kwenye Chemistry. Sasa Ozone layer ni producer of oxygen. Oxygen ni hii hewa safi ambayo tunaivuta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ozone layer Mwenyezi Mungu kaiweka makusudi siyo kwa bahati mbaya ili iwe ni blanket au insulating sheets ya jua, mionzi inayotokana na jua. Mtakumbuka kwamba jua liko around 93 million miles from earth surface. Kwa hiyo, kama ingekuwa ile mionzi ya jua inatupiga direct, nafikiri hapa kungekuwa hakuna mtu tena, wala kiumbe kisingeweza kuishi katika dunia hii, lakini kwa sababu ya ozone layer ndiyo tunapata protection. Mungu atunusuru, siku za the day of eruption eeh, wanaita siku ya kufufuliwa. Inasema…

MBUNGE FULANI: Rise eruption.

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Yes, rise eruption. Wanasema hili jua litakuwa karibu sana na sisi; nasi tutakaa sana kabla ya kuhukumiwa. Kwa sababu tutakaa sana, jasho lile litakalotutoka litafika mpaka kwenye mabega, wale wenye dhambi kali. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, uwepo wa ozone layer haukufanywa kibahati mbaya na Mwenyezi Mungu. I agree na maazimio haya na hasa lile Itifaki ya Motreal na marekebisho yaliyofanywa nchini Rwanda, nakubaliana nao mia kwa mia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, nadhani sisi mwanzoni tulifikiri tatizo la ozone layer kutobokatoboka, kuwa na matundu ni kwa sababu ya kemikali za aina zinazoitwa CFS (Chlorofluorocarbons), lakini baadaye tukagundua kwamba unaweza uka-get rid of chemical inayoitwa chloralfluorocarbons hasa kwenye utengenezaji wa friji, jokofu, air conditions na kadhalika kama walivyosema Waheshimiwa Wabunge. Tukaja na kemikali mbadala inaitwa hydrochlorolfluorocarbons. Hata hivyo, as we say na kwa mujibu wa protocol hii ya Montreal kuna a lot of chemicals ambazo zinasababisha mmomonyoko wa ozone layer.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo siyo la Tanzania. Nataka nisikubaliane na Kambi ya Upinzani kidogo na wale ambao walikuwa wanafikiri kwamba kuleta friji mbovu…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Muda!

MBUNGE FULANI: Mwongezee!

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe elimu.

MWENYEKITI: Kwa sababu ya field yako hiyo, natumia mamlaka yangu hayo, ongea kidogo dakika tatu zaidi. (Makofi)

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivyo kwa sababu problem iko katika nchi zilizoendelea. Suala la haya mafriji, majokofu, kutengenezwa kwa kutumia hiyo kemikali mbadala, hydrofluorocarbon siyo tatizo. Tatizo ni kwamba nchi zilizoendelea, zenye viwanda zina a lot of emission ya hizi kemikali ambazo huwa ni distractive. We don’t want to talk of hydrofluorocarbons; na hiyo sasa imeambiwa kwamba nayo ina madhara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri kama sikosei kuna kama kemikali za aina sita ambazo zote ni destructive ya ozone layer. Ukiacha CFS, unakuja hydrofluorocarbon ambayo sasa hivi inatumika katika utengenezaji wa mafriji, lakini kuna hydrofluorobromocarbons, kuna hydrobromochlorocarbons a number of them; kuna hizi chemicals zinazoitwa halons ambazo is nothing but carbontetrachloride. Kuna a lot of chemicals sasa hivi na hizi hatuzalishi sisi, wanazalisha nchi zilizoendelea, zenye viwanda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kusema kwamba friji bovu au kifaa chakavu kitaleta emission hiyo, siyo kweli. Hata ukinunua friji zima jipya, basi kule kuna hydrofluorocarbons. Kwa hiyo, friji inavyofanya kazi, liwe jipya, liwe kongwe lina emission ya hydrofloralcarbons. Tatizo nasema tena ni nchi zilizoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, solution ni nini? Kwanza tuzibane nchi kubwa kwamba ipo side penalt clause katika ile Itifaki lakini is not punitive, wala haitekelezwi. Leo Taifa kama Marekeni, China, Japan, Italy ambazo zina viwanda tukizibana tukawaambia lazima watoe 5% of their budget kusaidia nchi changa kwa suala la kuharibiana mazingira, hilo litakuwa sawa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, au tukazibana tuwe na effort ya pamoja, tufanye reseach ili tupate kamikali mbadala. Hiyo inawezekana. Suala la AIDS, HIV, tuna research ya pamoja na mpaka sasa hivi hatujapata dawa, lakini at least kuna jitihada joint efforts ambazo zinaonekana zitazaa matunda huko baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la tatu, mataifa haya makubwa waambiwe wapunguze viwanda ambayo huwa vina-emit hizo hydrofuorocarbons otherwise suala la ozone layer litaendelea. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, again, naomba kuunga mkono azimio hilo. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue fursa hii kukupongeza sana wewe kwa kuchaguliwa kwako kuwa Naibu Spika na kumpongeza Mheshimiwa Job Ndugai kuchaguliwa kwake kuwa Spika wa Jamhuri ya Muungano. Nawapongeza kwa sababu Mheshimiwa Spika, Job Ndugai ali-participate sana katika kuandaa kanuni ambazo zina mawanda mapana; zinatufanya tufanye kazi zetu katika Bunge hili ndani na nje kwa urahisi zaidi. Na wewe ninakupongeza kwa sababu umekuwa dictionary wa kutekeleza kanuni hizi. Lakini baada ya hayo, najua itifaki inazingatiwa, nataka niende kumpongeza Rais wetu wa Awamu ya Sita, Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Ninampongeza kwa sababu ameingia katika record ya dunia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi kwa nini, sasa hivi katika viongozi wa dunia wanawake heads of states tunao 26 na sita katika hao wanatoka Bara la Europe, watano wanatoka Afrika na mama Samia akiwa mmojawapo. Nchi ambazo zilikuwa zina viongozi wanawake katika Afrika kama ninavyosema ni watano. Tunaye kiongozi wa Namibia, Saara Kuugongelwa, tunaye kiongozi wa Ethiopia Sahle-Work Zewde, tunaye kiongozi wa Togo, Victoire Tomegah Dogbe Dogbe na tuna Garbon kiongozi wake anaitwa Rose Francine Rogombe.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini baada ya kutoa pongezi hizo kwa Mheshimiwa Rais sasa nataka nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Naibu wake pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni mjumbe wa Kamati ya Bajeti kwa hivyo, sina sababu ya kutounga mkono hoja hii. Nakupongeza sana, umeleta bajeti ambayo nataka niseme wazi, katika maisha yangu ya kuwa Bungeni, sijapata kuona bajeti ambayo imeleta mapinduzi makubwa kama bajeti ya mara hii. Nimekuwa hapa vipindi vinne, kipindi cha Mzee Mwinyi nikiwa Waziri wake na kipindi cha Mheshimiwa Magufuli na sasa hivi Mheshimiwa Samia. Lakini nataka nikuhakikishie bajeti yako ni ya aina yake. Nasema ni ya aina yake kwanini, nitakuja nitaeleza vizuri. Lakini, ili hii nchi ipate maendeleo na ihitajike kuna mambo matatu makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nchi lazima iwe na Prudent Physically and Monetary Policy, la pili nchi iwe na Budgetary Policy ambayo ni imara. Yote hayo yawe katika backet/katika kapu ambalo ni la good governance, tunayo. Tumemchagua Rais wetu juzi, kwa kishindo kikubwa tu. Kwa hiyo, tunayo good governance, kama vile hii transition ya madaraka kutoka Hayati Mheshimiwa Magufuli mpaka kuja Samia, ilikuwa ni ya salama kwa hivyo, tunayo good governance. Sasa sitazungumzia Physically Monetary Policy sasa hivi, lakini zaidi kwa sababu muda wenyewe hautoshi nitajikita kwenye Budgetary Policy. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kufanya kazi zake bila la kodi, Kodi ndiyo inayoendesha Serikali. Marekani ni nchi ambayo imeendelea lakini haiwezi kwenda bila kukusanya kodi. Katika City of New York kuna road tolls pale, kuna road toll station inatozwa kodi ya barabara na kadhalika. Kwa hivyo kodi ni muhimu na siri moja ya kukusanya kodi ni kukusanya kodi with minimum inconvenience to taxpayer. Huyu taxpayer ikusanywe kodi yake bila ya kusumbuliwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hizi indirect taxes zinazopita kwenye mafuta, zinazopita kwenye simu hazinipi matatizo, hizi haziumizi hata kidogo na bajeti yetu kwa kiasi kikubwa imejikuta na indirect taxes. Katika bajeti ya Mheshimiwa Waziri mara zote, mara zote, nasema tena au mara nyingi amekuwa akipunguza kodi katika Sekta ya Kilimo, Sekta ya Uvuvi, Sekta ya Madini na Sekta ya Mifugo. Hayo ni mambo yanayogusa wananchi, maana asilimia 65 ya wananchi wa nchi hii ni hao. Kwa hivyo nasema ni mkombozi mkubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niweze ku-refer maneno mazuri sana ya Mama yetu Samia Suluhu Hassan, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwanza twendeni Ukurasa wa, kama sikosei, Ukurasa wa 127. Ukurasa wa 127, Kifungu cha 105. Mheshimiwa Mwigulu anasema:

“Amekuwa wazi kuwa Rais wetu hataki kodi ya dhuluma. Hataki kodi ya dhuluma. Hataki kuendesha Serikali kwa Mapato ya dhuluma. Ameweka wazi kusimama imara kwenye masuala ya mapato na matumizi ya Serikali. Ameweka wazi kuwa atakuwa imara kwenye vita dhidi ya rushwa.”

Hayo ni maneno ya Mama Samia Suluhu Hassan tunataka Rais wa namna gani kama si Mama Samia?

WABUNGE FULANI: Mama Samia.

MHE. JUMA HAMAD OMARI: Mheshimiwa Naibu Spika, lakini tukienda ukurasa wa 136, Mheshimiwa Mwigulu ana- windup kwa kusema:

“Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Rais amenituma, niwahakikishie Watanzania kupitia hotuba hii kuwa, tutaendelea kujenga nchi. Ije mvua, lije jua tutaendelea kujenga nchi. Uwe usiku na mchana tutaendelea kujenga nchi. Kazi inaendelea.”

Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka maneno gani ya busara kama hayo? Kwa hiyo nadhani tuna kila hali ya kumpongeza Rais wetu mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kwa hiyo naomba nijikite zaidi kwenye mambo haya ya budgetary policy. Nchi hii naifananisha na Nchi ya Malaysia, Malaysia ilipopata uhuru kutoka Uingereza mwaka 1957 ilikuwa ni nchi ya low income, basically nchi ile ilikuwa ya kilimo, walikuwa wanauza haya mazao ya kilimo ndipo ulikuwa uchumi wao. Akaja Mwanamapinduzi mmoja Mohamad Mahathir akaifanya Malaysia ikatoka kwenye low income ikaja kwenye middle income jambo ambalo kuwa na sisi Tanzania tumefanya hivyo. Tumetoka kwenye low income tumekuja kwenye middle income kiwango cha chini. Nani kafanya hayo? Ni Mama Samia na akishirikiana na Mheshimiwa Hayati marehemu Magufuli. Kwa hivyo tumetoka kwenye low income tumekuja kwenye middle income kipato cha chini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa vigezo vya Benki ya Dunia ili u-qualify kuwa uchumi wa kati kigezo cha chini unatakiwa uwe per capital income ya dola 1,036, sisi tunakwenda zaidi. Malaysia sasa hivi hawapo tena kwenye low income, kigezo cha chini, wao wapo hawapo kwenye middle income kigezo cha juu ambao wameshafika uchumi wao per capital income ya dola 4,045. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, inachukua muda mrefu sana kutoka middle income ngazi ya chini kwenda kwenye middle income ngazi ya juu. Kwenye high income itachukua muda mrefu zaidi kwa sababu you’re talking per capital high income of 12,000 dollars ambayo hiyo siyo rahisi kufika kwa muda wa karibuni. Kwa hivyo, tutakuwa hapa kwa muda mrefu najua, lakini kwa jitihada hizi, ambazo Serikali yetu inafanya, nina hakika hatuna muda tutakwenda uchumi wa kati kigezo cha juu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ninavyosema hii mimi ni bajeti yangu ya kipindi cha nne; sijapata kuona bajeti nzuri kama hii. Kwa mfano, bajeti inakwenda inapunguza kodi kwenye horticulture, wenzetu wa Kenya horticulture peke yake per annum wanapata kama two billion dollars. Sasa sisi foreign exchange yetu imeongezeka sasa hivi tunakwenda kwenye 5,000 dollars. Kwa hivyo ni dhahiri kwamba kwa sababu kuna upunguzaji wa kodi kwa vifaa vya horticulture kama vile majokofu ambayo yatajengwa Airport, nina hakika inawezekana kabisa tunaweza kuvuka dola 5,000 kwa muda mdogo sana. katika kipindi kinachokuja kidogo tu sisi tutavuka zaidi ya hiyo. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa kengele ya pili imeshagonga.

MHE. JUMA HAMAD OMARI: Mheshimiwa Naibu Spika, namalizia kwa kusema, tuna mengi sana lakini kwa sababu muda mdogo, namalizia kwa kusema tu, naiunga mkono bajeti hii na nawaomba Waheshimiwa Wabunge wenzangu hatuna sababu ya kutounga mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023
MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kuchukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa fursa hii adhimu kuwa ni mmoja wa wachangiaji wa jioni ya leo. Mheshimiwa Naibu Spika na Mheshimiwa Spika nyote mmekuwa mkitulea vizuri sana katika Bunge hili mpaka kufikia kiasi cha kusema Mheshimiwa Spika anataka Bunge hili lifanye mageuzi katika kilimo. Nasema hilo ni jambo zuri kwa sababu kilimo ni uti wa mgongo wa uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini wewe umekuwa mlezi wetu mkubwa sana kwa maana ya kujadili kwa mujibu wa kanuni na sheria tulizojiwekea. Siku zote huwa ninakuita dictionary wa kanuni kwa hiyo, nakupongezeni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo naomba nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu, Mheshimiwa Suluhu Hassan. Kwa kweli, kama kuna Rais ambaye ametu- encourage, ametunyanyua nchi hii, yeye ni mmojawapo. Na ninasema hivi kwa sababu, bado amebaki na adhma au na dhima ya kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu. Na hivi karibuni ameonesha kwamba, kweli anajali, amefanya mambo mengi ambayo nitayataja as I go through my speech, kwa hiyo, kwa kweli, tunampongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri wa Fedha. Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Mchemba mmoja katika Waziri ambao kwa kweli, nimebahatika kufanya kazi na Mawaziri wa Fedha muda mwingi sana nikiwa kama Naibu wao, lakini kama kuna Waziri wa Fedha aliyekuwa msikivu, hayuko adamant, yuko dactyl naweza ukampa mawazo na akayakubali, sisemi atakubali yote asilimia 100, lakini ni mwepesi wa kukubali yuko dactyl nakupongeza sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nataka nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Mwenyekiti wetu wa Kamati, Daniel Sillo, kwa kweli, ni Mwenyekiti mzuri sana. Kamati hii imeuchambua mwongozo huu wa mpango na imekuja na mapendekezo mazuri. Kwa hiyo, ni matumaini yangu kwamba, Mheshimiwa Waziri wa Fedha utayachukua mapendekezo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hivyo nataka niseme hivi, Kamati yetu ya Bajeti, nikiwa ni mmoja katika Wajumbe, imechunguza hali ya uchumi katika kipindi pre-covid na katika kipindi post-covid na tumeona mengi sana na tumependekeza mengi. Mmoja katika wachangiaji hapa, Dkt. Kimei amesema kwamba, Sera ya Riba ambayo inakuwa determined na Bank of Tanzania ni moja katika kigezo kikubwa cha kukuza uchumi au cha kufufua uchumi, nasema ni sawa kabisa ametueleza vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nijikite katika suala la ujazi wa fedha, money in circulation ambayo inakwenda sambamba na hii sera ya, au hii tune dhana ya kuchochea uchumi kwa maana ya riba aliyoitaja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, over some time now ujazi wa fedha umekuwa ukipungua, money in circulationa. Na kwa tafsiri pana wale wataalam wanasema M3 na ni kweli, ukienda mwaka 2019/2020 ujazi wa fedha ulikuwa kwa asilimia 10, lakini unakwenda mwaka 2020/2021 lengo lilikuwa asilimia 10, lakini ujazi wa fedha umekuwa kwa 7.6. Hii ni dhahiri kwamba, money in circulation, pesa ile inayozunguka imepungua, lakini unajiuliza kwa nini? Nadhani hilo ndio la msingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazungumza kwamba, private sector ni engine ya uchumi, engine ya kuchochea uchumi. Private sector hawana fedha za kuzungusha na kwa nini hawana fedha, nitakuja. Lakini sababu kubwa zilizotolewa ni tatu kwa nini money in circulation inapungua; moja ni shughuli za uchumi hasa katika sekta ya biashara, katika sekta ya utalii na katika uwekezaji katika private sector zimepungua. Na kwa nini zimepungua? Nadhani nakuja hapo, kuna hizo sababu tatu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kimsingi ni kwamba, private sector ambayo ndio engine ya kufufua uchumi haina access kubwa na na mikopo. Wengi hawa wanashindwa kwenda kwenye commercial banks wakakopa, wanashindwa kwa sababu interest ambazo zilikuwa zinatolewa na commercial banks despite the fact kwamba, BOT na Mama Samia hapa amefanya mambo mengi. Hawa commercial banks wengi hawafikiki katika kutoa. Sisi Wabunge ni mashahidi, sisi Wabunge tunajulikana address zetu zinajulikana, lakini tunachukua mikopo yetu at an interest rate of 15%, 16%. Hawa private sector wanapewa zaidi ya hapo, nasema hilo ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa ujazi wa fedha unapungua hilo ni tatizo maana ili fedha izunguke yule tajiri anataka awe na fedha nyingi na masikini basi humohumo anauza mazao yake naye atapata fedha, lakini kama haizunguki, kama fedha haizunguki tutauwa na matatizo tu. Kwa hivyo, nasema pamoja na kwamba, Mama yetu Rais ametusaidia sana, kwa mfano hivi karibuni katoa 1.1 billion kawapa Benki Kuu ya Tanzania. Kama hiyo haitoshi, juzi katusaidia amepata 1.3 trillion zote hizo zitatiwa ziende zikapunguze suala la ujazi wa fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo nasema pamoja na mambo mazuri anayotufanyia Mheshimiwa Rais wetu, lakini bado money in circulation ujazi wa fedha umekuwa ni tatizo. Kwa hiyo, ninapendekeza yafuatayo, ili kukabiliana na suala hili la ujazi wa fedha:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tu-encourage PPP (Public Private Partnership). Hivi tujiulize tokea sheria hii ipite ya PPP ni miradi mingapi ambayo imefanywa kwa njia ya ubia? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani kama sikosei ni Daraja la Kigamboni basi, Daraja la Kigamboni. Na Kigamboni pale ni private, lakini kwa maana ya shirika letu la hifadhi NSSF, lakini hakuna jitihada ambazo zimeelekezwa ku-encode PPP. Sasa hilo ni tatizo na ninadhani PPP katika ulimwengu huu ina play part kubwa, hasa katika miradi ambayo ni capital intensive; mradi kama wa SGR, mradi kama wa Bwawa la Mwalimu Nyerere, mradi kama wa njia nne kutoka Kibaha mpaka Chalinze. Mradi kama ule wangepata private sector tukafanya partnership nao nadhani kwa kiasi kikubwa Serikali isingekuwa na haja ya kuwekeza fedha kama hizo kwa hiyo, nadhani hiyo ni njia moja tu-encourage PPP.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, BoT, Benki Kuu ya Tanzania, lazima pamoja na kwamba, kuna kitu Dkt. Kimei amekitaja kinaitwa Statutory Minimum Reserve Requirement, pamoja na kwamba, Benki Kuu ya Tanzania imepunguza hii Statutory Minimum Reserve Requirement, lakini hii haisaidii. Inasaidia kuhakikisha benki zetu endapo zitapata matatizo zinaweza kurejesha fedha za watu kwa sababu benki haina fedha zake, benki inakusanya amana na kuna benki nyingi kwa mfano Greenland Bank kuna wakati ilifilisika kwa hivyo, Benki Kuu ikatakiwa irejeshe amana pale ikarejesha. Kwa hivyo, hii haimsaidii mtu binafsi wala haiwasaidii watu wa private sector, zaidi inasaidia kuhakikisha kwamba, benki zetu ziko liquid at a given time.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la tatu ninalopendekeza ni kwamba, lazima tukataka tusitake, private sector iende ikafanye kazi hasa katika miradi ile kwa PPP kama tulivyosema, lakini kuna kuna miradi kwa mfano, nitawapa mfano; mradi wa Mchuchuma na Liganga, mradi wa Liganga, chuma cha Liganga na makaa ya Mchuchuma. Hii miradi kama sisahau mradi wa Liganga umekuweko tokea miaka ya 1990s, mimi niko Bungeni wakati huo, Mheshimiwa Kihaule, if I can remember very well alikuwa anauzungumzia mradi huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini so far mradi huu huwezi kuamini, so far mradi huu nafikiri umetumia only shilingi 5.7 billion huu ni LNG, Mchuchuma nafikiri umetumia kidogo zaidi…

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Juma. Mda wako umekwisha.

MHE. JUMA HAMAD OMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya. Kwa sababu muda hauniruhusu naomba kuunga mkono hoja zote hizi. (Makofi)