Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Answers to supplementary Questions by Hon. Eng. Edwin Amandus Ngonyani (417 total)

MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Spika, naomba niseme kwamba taarifa nilizokuwanazo na ambazo ni sahihi ni kwamba daraja la Mto Kilombero lilipaswa kuwa limekamilika mwezi wa 10, 2015. Kutokana na Serikali ya CCM kushindwa kumlipa Mkandarasi kwa wakati, ameshindwa kufanya kazi hii kwa wakati.
Sasa naomba nijue ni lini Serikali ya CCM itaweza kumlipa Mkandarasi huyu ili aweze kufanya kazi yake vizuri? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali lingine. Nataka nijue ni kwa nini Mkandarasi huyu amechukua mchanga kama sehemu ya material katika maeneo ya Lipangalala bila kuwalipa fidia yoyote wananchi wa Lipangalala. Nataka nijue, kama amelipa, kamlipa nani na kiasi gani? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, fedha za daraja zinagharamiwa na fedha za Serikali kwa 100%, hizo fedha zinatokana na kodi zetu. Sasa uwezo wa Serikali na miradi yote tuliyonayo, hatuwezi kuikamilisha kwa wakati mmoja. Ndiyo maana muda wa kumaliza umebadilishwa kutoka wa kwanza wa mwaka 2015, sasa tunaongelea Desemba, 2016. Ni kutokana na uwezo wetu wa ukusanyaji wa mapato yetu ya ndani.
Mheshimiwa Spika, kama ulivyosema awali, swali lake kuhusu fidia ya eneo ambalo mchanga unachukuliwa, naomba tuwasiliane Wizarani tumpe takwimu sahihi, kwa kuwa linahitaji takwimu.
MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini pia niseme tu kwamba barabara hii katika maeneo mengi, kama ulivyokiri kwenye jibu lako la msingi kuna baadhi ya maeneo inateleza, kuna utelezi mkali. Je, Serikali ina mipango gani kuhakikisha kwamba kwa kipindi hiki cha mvua ambapo haipitiki inaweza kujengwa kwa haraka iwezekanavyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa tuna maeneo mengi sana katika nchi hii yenye matatizo ya mawasiliano ya barabara. Tumetoa maelekezo mahsusi kwa kila Meneja wa TANROADS Mkoa kuhakikisha kwamba muda wote wanapata taarifa wapi kuna matatizo na wayashughulikie haraka. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, maelekezo hayo yamekwenda Mkoa Mbeya na pengine nichukue nafasi hii kama walikuwa hawana taarifa sasa wamepata taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge, wakalishughulikie hilo eneo kwa kadri ya maelekezo ya jumla ambayo Mameneja wote wameelekezwa.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kujua barabara ya Tunduma - Mpemba yenye kilometa 12 itajengwa lini na Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi kwa sababu barabara ile inasababisha msongamano mkubwa sana wa magari kwenye Mji wa Tunduma na wananchi kushindwa kutimiza majukumu yao. Kwa hiyo, nataka Waziri atueleze ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwenye Mji wetu wa Tunduma haraka iwezekanavyo? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii inahitaji takwimu, ninamwomba Mheshimiwa Mbunge, avute subira tuwasiliane na wataalam ili tuweze kumpa jibu lililo na uhakika.
MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa kususua kwa barabara ya hizi za Busokelo inafanana sana na kusuasua kwa ujenzi wa barabara ya kutoka Dodoma kwenda Babati na hasa kipande cha Mayamaya kwenda Bonga, naomba kujua Serikali inasema nini kuhusu changamoto hiyo kubwa ambayo imechukua muda mrefu na ahadi ilikuwa mwisho wa mwaka 2015 kumalizika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba barabara ya Busokelo na anayoongelea zinafanana, lakini hii ilikuwa inaongelea matengenezo na hiyo nyingine inaongelea ujenzi. Namwomba Mheshimiwa Mbunge, anafahamu kuna Mbunge ameleta swali kuhusiana na hii barabara. Ni hivi karibuni tu tutapata taarifa kamili na tutalijibu swali linalohusiana na barabara hii ndani ya Bunge hili linaloendelea.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pia nishukuru kwa majibu ya utangulizi, lakini naomba tu kuiambia Serikali kwamba barabara hii ni muhimu sana kwa ajili ya uchumi pamoja na kijamii. Pia niseme barabara hii ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne na wakati barabara hii inaahidiwa na Rais wa Awamu ya Nne, Rais wa sasa Dkt. John Pombe Magufuli alikuwepo. Sasa hili suala la upembuzi yakinifu, ni lini hasa kwa sababu swali hapa la msingi, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami kwa kuzingatia kwamba hii ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa namna nilivyomwelewa, anasisitiza tu kwamba hii kazi ya upembuzi yakinifu ikamilike haraka ili ahadi ya Marais wetu, Rais wa Awamu ya Nne na Rais wa Awamu ya Tano wakati alipokuwa Waziri wa Wizara ya Ujenzi itekelezwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumthibitishia kwamba Wizara yetu itatekeleza ahadi hiyo kikamilifu.
MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa kuwa ujenzi wa barabara ni kichocheo kikubwa kwa shughuli za kiuchumi.
Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Tanga - Pangani - Saadani utaanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Mbunge, barabara hii ili tuweze kuitendea haki, tuwasiliane Wizarani ili wataalam nao watoe mchango wao ili tunapotoa tarehe ya lini itaanza iwe taarifa sahihi. (Makofi)
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, katika Bunge la Kumi nilitumia muda mwingi sana kufuatilia na kuuliza maswali juu ya upelekaji wa huduma hii kwenye Kata hizi za mwambao na sababu kubwa ni kwamba Kata hizi ni za mpakani, zina changamoto myingi zikiwepo changamoto za kiusalama pamoja na usafiri, barabara zake hazipitiki vizuri. Majibu yaliyokuwa yanatolewa na Serikali hayana tofauti na haya, na sasa hivi Serikali kama imejichanganya kidogo. Mara ya mwisho walikuwa wanasema Halotel ndiyo wangeweza kupeleka mawasiliano kule, sasa wanakuja na msimamo wa Vodacom jambo ambalo litawachanganya wananchi kikamilifu, na nilikuwa juzi Kata ya Ninde ambako wanasema utekelezaji umekwishaanza, hakuna dalili zozote zaidi ya kwenda kuonyeshwa site basi. Vilevile Wampembe hakuna kitu kinachoendelea, kwa hiyo nina mashaka majibu yamekuwa ni yale yale, ninaiomba Serikali ihakikishe kwamba inapeleka mawasiliano haya kama inavyoahidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, wasizoee kuahidi wanieleze leo ni miujiza gani wataifanya iwe tofauti na ahadi walizokuwa wanazitoa wakati ule?
Swali la pili, katika Jimbo langu pia hasa Kata ya Isale. Kwanza niishukuru Serikali kwa kupeleka mawasaliano Kata ya Kate, kuongeza usikivu na hatua nyingine inayoendelea kwenye Kata ya Sintali. Kata ya Isale yenye vijiji vya Msilihofu, Ntuchi na Ifundwa, usikivu siyo mzuri, na nilipata kuuliza hapa pia nikaelezwa kuna hatua na kampuni imepewa kazi ya kuboresha mawasiliano katika eneo hilo, nataka kujua ni lini kazi hiyo itakamilika? Asante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba ajue hii ni Serikali ya awamu ya Tano, ni Serikali ya kasi, ni Serikali ya hapa kazi tu. Ahadi tuliyokupa imezingatia commitment iliyotolewa na mfuko huo tunaoongelea UCSAF. Kwa hiyo ninakuahidi, kama ulivyosisitiza mwenyewe na mimi narudia kwamba ifikapo mwezi Juni 2016, Kata hizo tatu mawasiliano yatakuwa yamefikishwa na atakayefikisha ni Vodacom Tanzania. (Makofi)
Kuhusu swali lako la pili, kama unavyoniona huwa napenda kusema kitu ambacho kina takwimu. Swali hili ni jipya kwangu na nakuhakikishia baada ya saa tisa alasiri tuonane nitakuwa nimewasiliana na watu wa UCSAF nikupe majibu sahihi. (Makofi)
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, asante. Kwa jina naitwa Boniphace Mwita ni Mbunge wa Jimbo la Bunda na ieleweke hivyo, mdogo wangu Ester Bulaya ni Mbunge wa Bunda Mjini.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya Jimbo la Bunda yanafanana na matatizo ya Nkasi, kuna Kata ya Unyari, ambayo ina vitongoji vyake na maeneo yake, ambavyo ni Nyamakumbo, Manangasi, Magunga, na Nyamatutu, na kijiji cha Kihumbu vitongoji vyake na Kihumbu na Mwimwalo vina tatizo lile lile la kutokuwa na mawasiliano, na kwa kuwa maeneo haya yana wakulima wengi na wafugaji wengi, na kwa kuwa wakulima hawa wako kwenye hali hatari ya tembo.
Je, Mheshimiwa Waziri haoni kuna umuhimu sasa wa kupeleka mawasiliano maeneo hayo ili wajiokoe na hali ya ulinzi wake na pia kwa mawasiliano ya kawaida?
Kwa kuwa wananchi hao wamechoka kuahidiwa na leo wamekuja hapa Bungeni kuonana na Waziri kuhusiana na maeneo yao hayo.
Je, Waziri yuko tayari kuonana nao leo? (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mbunge kwamba nitakuwa tayari ofisini tuonane tu-discuss masuala yote aliyoyaongelea na tumpe takwimu sahihi.
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kutokana na majibu haya yasiyokuwa na tija kwa wananchi wa Temeke yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo yanatushawishi sasa kwenda kuidai haki yetu Mahakamani, naomba niulize maswali matatu ya nyongeza. (Kicheko)
Samahani naomba niulize maswali mawili ya nyongeza moja lina sehemu (a) na (b).
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mtolea nadhani utakuwa umeziangalia Kanuni kuhusu maswali, ukiuliza swali moja lenye (a) na (b) kwa sababu ni nyongeza utakuwa umeshauliza hayo mawili, tafadhali.
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kilwa ilijengwa chini yakiwango, na Serikali ilimwamulu mkandarasi airudie kwa gharama zake mwenyewe. Ujenzi huo wa chini ya kiwango ni pamoja na mitaro iliyo pembezoni mwa barabara hiyo, mvua zilizonyesha tarehe 14 na tarehe 15 Disemba, mitaro hiyo ilishindwa kuyabeba maji vizuri na ikapasuka ikapeleka maji kwenye makazi ya watu maeneo ya mtaa wa Kizinga katika Kata ya Azimio pale Mtongani na nyumba 40 ziliharibika vibaya.
Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuwatuma wataalam wake kwenda kufanya tathmini na kuwalipa wananchi walioathirika na tukio hilo?
Swali la pili, hivi tunavyozungumza hivi sasa kuna taharuki kubwa imezuka kwa wakazi wanaokaa pembezoni mwa barabara ya Davis Corner - Jet Rumo ambapo wananchi waliokuwa pembezoni mwa barabara hiyo wanawekewa alama za „X‟ kwamba wavunje nyumba zao ambao kimsingi zimejengwa kihalali kwa sababu wakati wa upanuzi wa barabara walilipwa mita 15 na Serikali ilikuwa haina pesa ya kuwalipa mita nyingine 15 kukamilisha mita 30 kila upande.
Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa yuko tayari sasa kuamulu zoezi linaloendelea katika Kata ya Vituka, Buza, Makangarawe na Tandika hivi sasa, lisimame mpaka yeye na mimi tutakapokwenda kukaa na wananchi na kujua nini tatizo la pale?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, maswali uliyoyauliza yanahusu masuala ya fidia ambayo inashughulikiwa chini ya sheria maalum chini ya Wizara ya Ardhi. Tumekubaliana kwamba tukutane wote sisi na Wizara ya Ardhi, tulichunguze hilo suala ulilolileta ili hatimaye tukupe majibu sahihi.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naitwa Mwalimu Marwa Ryoba Chacha ni Mbunge wa Jimbo la Serengeti.
Kwa kuwa tatizo ambalo liko Temeke ni sawasawa na tatizo ambalo liko ndani ya Jimbo la Serengeti. Katika barabara ambayo ni lami ya kutoka Makutano – Butiama - Nata - Tabora B - Loliondo na kadhalika, ilishafanyika upembuzi yakinifu na evaluation kwa wananchi ambao barabara hiyo inapita ambapo hiyo barabara haikuwepo. Tangu mwaka 2005 mpaka leo wananchi hao hawajalipwa.
Je, Serikali inasema nini kuhusu fidia ya wananchi ambao wako kando kando mwa hiyo barabara ambao walishafanyiwa evaluation lakini hawajalipwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamuomba awe na subira kwa sababu kuna swali hilo hilo limeletwa na litajibiwa katika Mkutano huu kabla haujaisha. Kwa hiyo, nitaomba muda ukifika wa kulijibu hilo swali tuyajibu hayo yote kwa pamoja.
MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nina maswali mawili ya nyongeza. Barabara ya Nkana – Kala mwishoni mwa mwaka jana ilijifunga na ikalazimika kutafuta fedha za dharura zaidi ya milioni 400 ambazo Serikali iliipatia na tukapeleka ndiyo ikafunguka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi imefanyika vizuri, naishukuru sana Serikali. Hata hivyo, lipo tatizo kwamba tusipopeleka pesa kwa sasa hivi kwa jiografia ya barabara zile ambazo zinaenda mwambao mwa Ziwa Tanganyika kwenye miporomoko, juhudi kubwa iliyofanyika na Serikali mwaka huu, haiwezi kulindwa na fedha kidogo iliyotengwa na Halmashauri ndiyo maana tuliomba fedha pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naiuliza Serikali, je, inakubaliana na ushauri wangu kwamba ili kulinda fedha zilizotumika mwaka jana inatakiwa ipeleke pesa nyingine zaidi kwa barabara hii?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, iko barabara ya Kasu – Katani – Chonga – Chalatila – Myula na ile ya Kisula - Milundikwa na Malongwe. Barabara hizi ni za Halmshauri, zimekuwa zikijifunga kila wakati na sababu kubwa ni hiyo hiyo ya Halmashauri kuwa na pesa kidogo. Ni lini Serikali itaongeza pesa kwa Halmashauri ili ziweze kumudu kutengeneza barabara katika viwango vinavyohitajika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika swali langu la msingi, hizi barabara na mazingira ya mvua tunayokuwa nayo katika misimu ya mvua siyo rahisi kuahidi kwamba, barabara hii pekee tupeleke fedha kiasi hiki. Tatizo linapotokea Serikali inashughulikia chini ya Mfuko wa Dharura ambao upo katika kila TANROAD Mkoa. Naomba tuvumiliane kwa mazingira tuliyonayo, Serikali itaendelea kuongeza juhudi, kuhakikisha inatekeleza wajibu wake wa kuhakikisha mawasiliano sehemu zote za nchi yanapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, naomba hizi barabara tukaziangalie upya na ziletewe maombi kama ambavyo hizi zingine zililetewa ili Wizara yetu iweze kuzitathmini na kuangalia vigezo vile kama vinakidhi kupandisha hadhi au kuviongezea fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mnafahamu kwamba fedha zilizoko ni zile ambazo zinapangwa hapa Bungeni na Waheshimiwa Wabunge uwezo tunaopewa ni ule ambao Bunge linaidhinisha na kiwango kile tunachopata kupitia Road Board ndicho kinachogawiwa kwa nchi nzima.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Ukarabati wa barabara pia unaendana na utanuzi wa barabara. Serikali ilikuwa inatanua barabara kuu ya kutoka Mwanza kwenda Musoma na ilifuata nyumba za wananchi na wakawafanyia tathmini, lakini kwa bahati mbaya mpaka leo hawajalipwa na kuna wazee wangu kule wanapata taabu sana, nyumba zao hazijalipwa na wanaishi kwa taabu. Miongoni mwa wazee wangu ni pamoja na baba yangu Mzee Wasira, naye nyumba yake imefanyiwa tathmini katika kijiji chetu cha Manyamanyama.
Je, ni lini mtawalipa wananchi wa Bunda kwa sababu mmeshawafanyia tathmini miaka mitatu iliyopita?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
MWENYEKITI: Lini mtawalipa.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Fedha zitakapopatikana tutawalipa.
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri napenda kumwuliza maswali yafuatayo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Tabora kwa muda mrefu umekuwa ukililia barabara hizi za lami; na tunaishukuru Serikali ya Mapinduzi imewezesha kwa kiwango ilichoweza. Sasa alipojibu Mheshimiwa Waziri kwamba tunategemea barabara ikamilike mwezi Juni. Je, haoni kuna umuhimu wa kutaja hapa ni lini fedha zinakwenda? Kwa sababu wakandarasi wapo, hawafanyi kazi kwa sababu hakuna fedha.
Naomba Serikali itamke hapa, ni lini fedha zitapelekwa ili kuiwezesha kampuni ya CHICO ifanye kazi ili kweli barabara ikamilike mwezi Juni? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Waziri kwamba barabara ya Kilometa 6.3, kutoka nje ya mji kidogo, panaitwa Ndorobo, kufika mjini na kupitiliza hadi Seed Farm haikuwemo kwenye usanifu wa barabara kubwa, ile ya msingi inayokwenda mpaka Kigoma. Lakini alipokuja Rais wa Awamu ya Nne, Mheshimiwa Jakaya Kikwete, aliahidi mbele ya Mkutano wa hadhara kwamba barabara ile ya katikati ya Urambo itajengwa na Serikali. Pia alipokuja Mheshimiwa Magufuli ambaye sasa hivi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano…
MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ndilo hili nauliza. Kwa kuwa ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu ya Nne; na kwa kuwa pia Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Ujenzi aliahidi kwamba barabara hiyo itajengwa kwa lami. Je, Serikali haioni kwamba kwa kuwa usanifu tayari na fedha zimeshatengwa, kwa nini wasiwape hao kampuni ya CHICO, inapomalizia kipande kile ambacho hakijamaliziwa, wakati huo huo wamalize na barabara inayopita katikati ya Urambo ili zote kwa pamoja zikutane eneo la Seed Farm? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu lini fedha zitakwenda, nadhani atakiri kwamba ndani ya Bunge hili Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano alishatamka kwamba fedha zimeanza kuja, tumeshapokea zaidi ya shilingi bilioni 280. Kwa kweli awamu hii naomba kumwakikishia kwamba hiyo kazi itafanyika na ahadi hiyo itatekelezwa kwa sababu fedha zimeanza kuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili nadhani anaongelea masuala ya procurement. Nina uhakika, kwa sababu CHICO wako pale, vifaa wanavyo, inawezekana kwamba bei watakazozitoa, wao watakuwa na bei rahisi zaidi, kwa hiyo, uwezekano wa wao kushinda ni mkubwa zaidi kwa sababu tayari wana vifaa pale. Naomba tu tufuate taratibu za procurement, muda utakapofika, nina uhakika watu hawa watafikiriwa.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali ya nyongeza.
Kwa kuwa barabara ya barabara ya Mbande - Kongwa – Mpwapwa mpaka Kibakwe ni muhimu sana kwa maendeleo na uchumi wa Wilaya ya Mpwapwa na Kongwa; na kwa kuwa barabara hii inaunganisha Majimbo matatu; Jimbo la Kongwa, Mpwapwa pamoja na Kibakwe; na kwa kuwa ni ahadi ya Rais Mstaafu, Mheshimiwa Jakaya Kikwete na ahadi ya Mheshimiwa Rais John Magufuli ambaye ni Rais wetu sasa. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana na mimi kwamba ipo haja sasa ya kukamilisha barabara hii kwa kujengwa kwa kiwango cha lami?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa barabara ya kutoka Mpwapwa – Gulwe kwenda Berege – Mima mpaka Iwondo haipitiki, ni mbaya sana kwa sababu ya mvua zinazonyesha. Je, Mheshimiwa Waziri ana maelezo gani kuhusu wananchi wa Jimbo la Mpwapwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la kwanza ni kama nilivyojibu katika swali la msingi. Sana sana ninachoomba kuongezea ni kwamba dhamira yetu kama Serikali ni kubwa sana. Tuna nia ya kutekeleza ahadi za Marais hao; na kwa kweli mara fedha zitakapopatikana tutaendelea na kipande hiki kilichobakia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili, Wabunge wengi ni mashahidi kwamba maeneo mengi yaliyoharibiwa na mvua zinazoendelea, vijana wetu wa TANROAD wanafanya kazi kubwa. Naomba kwa upande wa TANROAD Dodoma waliangalie eneo hili ili kile wanachokifanya katika maeneo mengine na hapa wakifanye kwa ukamilifu ili wananchi waweze kupata mawasiliano ya uhakika.
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Napenda kumshukuru sana Naibu Waziri amejibu vizuri sana na amejibu kitaalamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imesema Chunya ina mazao mengi ambayo yakibebwa ndiyo yanaharibu barabara, sasa napenda nimwambie Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba wanaosomba tumbaku, magari yanayobeba tumbaku au mbao au mkaa yanabeba lumbesa, yanakuwa mara mbili, yakifika Mbeya yanagawa kwa sababu kuna mizani kule ndiyo yawe magari mawili na Serikali hapa imesema kwamba itadhibiti hiyo kwa kuweka mobile weighbridges.
Je, ni lini itaweka kwa sababu Chunya sasa hivi sijaiona mobile weighbridge hata moja? Hilo ni swali la kwanza
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nashukuru Serikali imesema kwamba ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Chunya kwenda Makongorosi karibu utaanza, napenda nimwambie Naibu Waziri kwamba Mheshimiwa Rais akiwa Makongorosi aliwaahidi wananchi wa Makongorosi kwamba atawapa kilomita nne za lami pale Makongorosi na kwamba barabara hiyo ya Chunya Makongorosi itaanza kujengwa Makongorosi kuja Chunya.
Je, hiyo barabara itanza lini kujengwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama tulivyosema kwenye jibu la msingi la swali la msingi kwamba weighbridge itaanza hivi karibuni. Naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mwambalaswa kama yeye alivyo-concerned na uharibifu wa barabara hiyo na sisi ambao ndiyo wenye dhamana hiyo tuko concerned kwa kiwango kikubwa, ninamhakikishia hiyo weighbridge inatafutwa hivi karibuni itaanza kufanya kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili naomba kumjulisha Mheshimiwa Mwambalaswa kwamba mara fedha zitakapopatikana barabara hii itaanza kujengwa na suala la ianzie wapi whether ianzie Makongorosi au ianzie Chunya nadhani ni muhimu tuwaachie wataalamu na ahadi ya kilomita Nne nayo katika eneo la Makongorosi itaangaliwa kwa umakini wake. (Makofi)
MHE. DUA W. NKURUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika wale ambao walifanyiwa tathmini ya awamu ya kwanza, wapo ambao mpaka sasa hawakulipwa, Majina yao yalirukwa katika Kijiji cha Misawaji, lakini pia wapo ambao walifanyiwa tathmini kwamba nyumba zao zitabomolewa nusu lakini zimebomolewa zote na hivi ninavyokwambia wamechanganyikiwa kabisa.
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kutuma watu tumuoneshe watu ambao wameathirika ili wapate haki yao?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara kutoka Masasi mpaka Mangaka imekamilika, hadi sasa magari yenye uzito mkubwa kutoka Songea kuelekea Masasi yanatumia hiyo barabara.
Je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kuleta mizani katika Mji wa Mangaka ili kuokoa barabara ambayo Serikali imetumia gharama kubwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana nae kwamba tutatuma watu waende wakalichunguze hilo suala na hatimaye tuweze kulipatia ufumbuzi stahiki. Ninachoomba kumhakikishia tu ni kwamba Serikali hii inafuata sheria na yeyote mwenye haki ya kulipwa fidia atalipwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili nadhani anafahamu kwamba hizo barabara anazoziongelea bado hazijakamilika na hivi karibuni nimepiata katika eneo lake ingawa kwa bahati sikumjulisha kwa sababu ilikuwa ni dharura wakati natokea Jimbo la Namtumbo. Ninamhakikishia mara barabara hizi zitakapokamilika na umuhimu utakapoonekana kwamba kuna umuhimu mkubwa wa kuweka mizani, Serikali itafanya maamuzi stahiki. (Makofi)
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa barabara ya kutoka Sumbawanga kwenda Mpanda takriban kilometa 50 zimeshatengenezwa na magari makubwa ya mahindi zaidi ya tani 60, 70 yanapita kuelekea Mpanda. Nimeshamwomba Waziri wa Ujenzi kupeleka gari ya mizani ili kudhibiti uharibifu wa barabara kabla wakandarasi hawajakabidhi kwa sababu barabara inaanza kuharibika kabla haijakabidhiwa. Je, ni lini Serikali itapeleka gari ya mizani ili kudhibiti barabara hiyo isiendelee kuharibika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Keissy na wananchi wa Sumbawanga hadi Mpanda kwamba barabara ile kwanza tutaikamilisha kuijenga. Tutakapoona umuhimu wa kuweka mizani kutokana na tathmini ya wataalam tutakaowapeleka kufanya shughuli hiyo tutaweka mizani hiyo.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Naitwa Alex Raphael Gashaza, Mbunge wa Jimbo la Ngara.
Kwa kuwa barabara ya Murugarama – Rulenge – Nyakahura yenye kilometa 85 ni barabara ambayo iliahidiwa na Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2008 kwamba itaweza kujengwa kwa kiwango cha lami na miaka miwili iliyopita wananchi wa Jimbo la Ngara walikuwa wakielezwa kwamba tayari upembuzi yakinifu wa barabara hii umeanza.
Naomba kumuuliza Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi ni lini mkandarasi atakuwepo site kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumepata taarifa kutoka kwa Waziri mwenyewe wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano juu ya upatikanaji wa fedha za kulipa madeni ya wakandarasi, kama jana mlimsikia alisema ni karibu shilingi bilioni 419 zimeshatolewa. Kwa hiyo, katika lile deni la shilingi trilioni 1.268 sasa tumeshuka tuko kwenye shilingi bilioni 800 na zaidi. Naomba kuchukua nafasi hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mara fedha zitakapopatikana kwa mradi huo, barabara yake itashughulikiwa kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. GIMBI D. MASABA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa vile nchi yetu ina uhaba wa majengo ya shule, zahanati na vituo vya afya, je, Serikali iko tayari kumuagiza mkandarasi ambaye sasa hivi yuko site kujenga majengo ya kudumu ili baada ya mradi kukamilika majengo hayo yaweze kutumika kwa ajili ya matumizi ya shule, zahanati na vituo vya afya? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara za Mkoa wa Simiyu zinaunganishwa na barabara za vumbi na kwa sasa hazipitiki kutokana na mvua zinazoendelea.
Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kutoka kwenye Mfuko wa Barabara ili kuweza kutengeneza barabara hizo na ziweze kupitika kwa urahisi tofauti na ilivyo sasa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, mkandarasi aliyeko site mkataba wake ulishasainiwa. Hata hivyo, nawaagiza TANROADS Mkoa wa Simiyu waangalie uwezekano katika mkataba huo kama inaweza ikafanyika variation au kama kifungu hicho kipo wahakikishe majengo yanayojengwa na mkandarasi huyo yaweze kuangalia matumizi ya baadaye ambayo Mheshimiwa Mbunge ameomba. Kama itashindikana, Serikali itatafuta njia nyingine kupitia Wizara husika ya Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Mfuko huo anaoungelea ndiyo tunaoutumia kujenga na kukarabati barabara zote nchi nzima. Naomba akubali mfumo tulio nao ndiyo huo, hatuna mfuko maalum kwa ajili ya barabara hii peke yake.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kuniona niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa katika Mpango wa Maendeleo wa mwaka mmoja ulio mbele yetu, miundombinu si kipaumbele.
Kwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Magufuli wakati akiomba kura aliahidi ujenzi wa barabara za lami nchini kote ikiwemo Jimbo langu la Babati Mjini ambako aliahidi ujenzi wa kilometa 20 za lami. Naomba nifahamu, ni lini ahadi hii itatekelezwa kwa wananchi wa Babati?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi zote ambazo zimetolewa kwanza na Chama Tawala kupitia Ilani yake ya mwaka 2015 - 2020 Serikali hii ina wajibu wa kuzitekeleza. na tutaitekeleza
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hiyo anayoiongelea namuomba awasiliane na TANROADS mkoa ili kuangalia vipaumbele vya sasa vilivyopo katika mkoa ule. Kama barabara hiyo ni moja kati ya vipaumbele vya mkoa, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaitekeleza katika kipindi hiki kama ambavyo iliahidiwa katika kipindi cha kampeni
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Na mimi kama swali la msingi lilivyoongea kuhusu Mkoa wa Simiyu kuunganishwa na mikoa mingine, ni wazi kwamba Mkoa wa Simiyu bado haujaunganishwa na Mkoa wa Singida ambao unapitia katika Daraja la Sibiti – Mkalama - Nduguti - Iguguno. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, je, anafahamu kwamba Daraja la Mto Sibiti ndilo kiunganishi kikubwa katika Mkoa wa Simiyu na Singida na mpaka sasa mkandarasi hayupo site? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba Daraja la Sibiti ni muhimu katika mawasiliano kati ya Mkoa wa Simiyu na Singida na ndiyo maana kazi kubwa inafanywa sasa kutokana na matatizo yaliyotokea ili kuhakikisha mawasiliano yanakuwepo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mkandarasi, kwa kuwa fedha za kulipa madeni ya wakandarasi tumeanza kupata ambapo huyu naye ni mmoja kati ya wakandarasi wanaotakiwa kulipwa ili waendelee na kazi. Mara fedha zitakapopatikana, mkandarasi atarudi site ili aweze kukamilisha kazi ambayo alisaini kuifanya.
MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba Mheshimiwa Waziri aniambie ni lini ujenzi huo utaanza? Kwa sababu barabara hii imekuwa ikizungumzwa kwa muda mrefu. (Makofi)
Swali la pili; issue hapo ni ku-sign mkataba ama ni pesa? Kwasababu tumekaa kwenye kikao cha RCC ingawa Meneja wa TANROADS Mkoa alishindwa kusema wazi, lakini kinachoonekana pesa hakuna. Kwahiyo, issue ya msingi naomba kujua; ni kwamba mkataba haujasainiwa ama pesa zinazofanya mkataba usainiwe hazipo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Tunza Issa Malapo, kwa niaba ya Wabunge wote wa Mtwara.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu walikuwa na kikao cha RCC na walikataa kuijadili barabara hii wakataka ije ijadiliwe hapa Bungeni. Naomba nikuhakikishie, hamna sababu ya kuijadili hapa Bungeni. Barabara hii imetengewa fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka 2016/2017 barabara hii imetengewa fedha tutakayohakikisha hizo kilometa 50 zinajengwa. Tunachosubiri ni taratibu za mkandarasi ku-sign mkataba kukamilishwa. Fedha zimetengwa!
MHE. MOHAMED R. CHUACHUA: Ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali yafuatayo ya nyongeza:-
Swali la kwanza, je, Serikali sasa haioni haja ya kuingilia kati na kutoa mwongozo kwa makampuni haya ambayo ni wawekezaji ili waweze kuwalipa wananchi hawa wanaotoa maeneo yao kwa kiwango kinachostahili, kwa sababu wengi wao hawajui thamani ya uwekezaji huo?
Swali la pili, katika eneo la Mji wa Masasi au Jimbo la Masasi, maeneo ya pembezoni karibu yote hayana mawasiliano, je, ni lini Serikali itajenga minara katika Kata za Marika, Mombaka, Temeke, Matawale, Surulu, Mwenge Mtapika pamoja na Chanika Nguo? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, labda nitumie fursa hii kutoa wito kwa wananchi wote wanapofanya mikataba na wawekezaji mbalimbali wapate huduma ya ushauri kutoka kwa Wanasheria pamoja na wataalam.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama mkataba umesainiwa kati ya kijiji na wananchi hata kama haukufata ushauri na pengine siyo mzuri kwa wale wanakijiji, ni ngumu kuwalazimisha upande mmoja katika mkataba kurekebisha, kwa sababu ni kinyume cha misingi ya mkataba.
Kwa hiyo, tutachunguza mkataba uliopo wa kijiji hiki kuona kama tunaweza wao wawili waliokubaliana wanaweza kukubali wakarekebisha ili waboreshe kile ambacho wananchi watakipata.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili, amenipa orodha ndefu. Kama Serikali naomba tupewe nafasi, hiyo orodha tuiwasilishe kwenye makampuni mbalimbali ambayo yanatoa hiyo huduma tuone kampuni ipi itakuwa tayari kujenga minara katika maeneo hayo au kupitia mfuko wetu wa Mawasiliano kwa Wote halafu tutamjulisha kwa maandishi.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Ahsante Mheshimiwa Naibu Spika. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya barabara hii, lakini hazipelekwi. Mara tatu mfululizo imekuwa ikitenga fedha hazipelekwi; mara ya kwanza shilingi bilioni nne; mara ya pili mwaka 2015/2016 zilitengwa shilingi bilioni 10 hazikwenda.
Je Serikali inaweza kulihakikishia Bunge hili na wananchi wa Mkoa wa Kigoma kuwa fedha zitatengwa sasa na kupelekwa Kigoma ili barabara hii iweze kukamilika? (Makofi)
Swali langu la pili, Kidahwe – Kasulu kuna mkandarasi ambaye yupo pale lakini amesimama kwa sababu hajaweza kulipwa fedha zake. Je, ni lini mkandarasi huyo atalipwa ili aweze kuendelea na kazi ya ujenzi wa barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sehemu ya swali lake la kwanza naomba kuthibitisha kwamba ndivyo itakavyokuwa.
Kwa swali lake la pili, naomba kumhakikishia kwamba wakandarasi wote Tanzania nzima tumeshaanza kuwalipa madai yao ikiwa ni pamoja na huyo mkandarasi. Kwa hiyo, muda siyo mrefu huyu mkandarasi atarudi site na kuanza kukamilisha hiyo kazi.
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, namshukuru Naibu Waziri na mimi nakubaliana naye alivyosema kwamba barabara ile ina umuhimu mkubwa hasa ukilinganisha kwamba kuna uzalishaji wa samaki katika eneo hilo, lakini vilevile ni eneo ambalo linapita nchi yetu ya jirani.
Sasa ukiangalia toka 2009 hadi leo, zaidi ya miaka mitano ni kilometa 7.5 peke yake ndiyo barabara iliyowekewa lami, napenda kufahamu Serikali itakuwa tayari kwa mwaka huu kutenga fedha kwa ajili ya hicho kipande cha barabara ili kiweze kujengwa zaidi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naomba ikumbukwe kwamba mbali na ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali ambayo yako katika mpango lakini kutokana na umuhimu Mheshimiwa Rais mwaka jana tuliweza kumpa maombi maalum hasa kwa pale Musoma Mjini, tulimpa ombi la barabara ya kutoka Bweri - Makoko ambapo kipande kile zipo sekondari zisizopungua 14, je, Serikali sasa itakuwa tayari kutimiza ahadi hiyo kuanzia mwaka huu wa fedha?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, maswali yake yote mawili yanaongelea kutenga fedha kwa mwaka huu wa 2016/2017 kwa ajili ya kuendelea kujenga ile barabara ya Mika – Utegi – Shirati - Kirongwe pamoja na hii barabara aliyoiongelea ya Bweri - Makoko. Naomba kumuahidi kwamba hivi sasa tunavyoongea, wataalam wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, sekta ya ujenzi, wapo katika hatua ya mwisho ya kuangalia katika haka kasungura kadogo tulikokapata ni wapi tutenge kiasi gani. Kwa hiyo, naomba asubiri Bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano itakapokuja itatoa majibu sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pengine moja ningependa kusisitiza, mahitaji ya ujenzi wa barabara ni makumbwa sana sehemu mbalimbali za nchi na priority (kipaumbele) kwa mwaka ujao wa fedha ni kukamilisha miradi ya muda mrefu ili kuondokana na gharama za makandarasi wanazotudai kutokana na kuchelewa kukamilisha miradi. Hivyo, tutahakikisha kwamba barabara zile ambazo zimeanza muda mrefu lazima kwanza zikamilike kabla hatujaingia katika eneo jipya.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nauliza kwa kifupi ili na wengine wapate nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, amesema upembuzi yakinifu unakamilishwa Juni, 2016 lakini kwa uhakika niliokuwa nao kwa sababu ni miaka sita niko Bungeni na hili swali nimekuwa nikiuliuliza na wamekuwa wakisema liko kwenye upembuzi yakinifu. Kama upembuzi yakinifu unachukua miaka sita, je, lini sasa mkandarasi atapatikana na ujenzi wa barabara hii utaanza lini? Maana ni muda mrefu mno nimezungumzia barabara hii na watu wanateseka sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wananchi wa Mlimba wanasikia maana nimewaambia, kwa kuwa Jimbo la Mlimba linaunganika na Mkoa wa Njombe, lakini amezungumzia barabara ya kwenda mpaka Mlimba hukuzungumzia barabara ya kutoka Mlimba - Madeke Njombe. Ni nini mpango wa Serikali wa kujenga barabara hiyo ili wananchi wa Mlimba waunganike na wa Mkoa wa Njombe ili waweze kupata fursa za kimaisha na za kiuchumi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza la Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga anahoji dhamira ya Serikali na mimi naomba kumthibitishia kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano ina dhamira ya dhati na itatekeleza ahadi zake zote zilizoko katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 -2020. Tumepewa dhamana ya kusimamia ahadi zote ikiwa ni pamoja na kuzikamilisha shughuli zote ambazo zilikuwa zimeanza kutoka Serikali ya Awamu ya Nne. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili linahusu kuunganisha Mlimba pamoja na Mkoa wa Njombe kupitia Madeke. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Susan Limbweni Kiwanga kwamba hoja yake tutaishughulikia. Barabara hii pia imeombwa na watu wa Njombe upande ule mwingine na ipo katika mpango wa TANROADS Mkoa wa Njombe na tutahakikisha wanashirikiana na TANROADS Morogoro ili barabara hii tuikamilishe yote kwa pamoja.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Makutano – Mugumu – Mto wa Mbu imetengewa fedha kuanzia mwaka 2012 - 2013 ili kujenga kilometa 50 kuanzia Makutano mpaka Sanzate.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninavyoongea, tangu mwaka 2013, hii ni 2016, hata kilometa moja ya lami haijawahi kukamilika. Sasa kama kuanzia mwaka 2013 mpaka sasa ni miaka mitano...
Miaka mitano kilometa 50 haijakamilika. Uki-cross multiplication it will take 45 years kukamilisha kilometa 452.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa swali, nataka Mheshimiwa Waziri awaambie wananchi wa Serengeti, ni lini watakamilisha ujenzi wa lami kuanzia Makutano mpaka Mto wa Mbu?
Swali la pili, ninavyoongea, sasa hivi hakuna mawasiliano kwenye hii barabara, imekatika! Daraja la Mto Robana limekatika. Serikali iko tayari kuji-commit sasa hivi kupeleka hela zikajenge yale madaraja ambayo yamebomoka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Marwa Ryoba Chacha kwa kusimamia kwa ukamilifu Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo imekusudia na imeweka barabara hii katika Ilani yake na tunaanza kuitekeleza kwa mwaka ujao wa fedha ukiacha kile ambacho kimeshafanyika katika kipindi kilichopita. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka ujao wa fedha, bajeti yetu itakapofika, Waheshimiwa Wabunge naomba muikubali ili tuweze kutekeleza Ilani hii ya Chama cha Mapinduzi. Katika barabara hii shilingi bilioni 12 tumezitenga kwa ajili ya kujenga kipande hiki anachokiongea na shilingi bilioni nane tumeitenga kwa ajili ya kujenga upande wa pili wa Arusha ambayo nimeiongelea.
MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza, kwa kuwa, Wakandarasi wakipewa kazi huwa wanapewa na time frame ya kumaliza ile kazi, hii barabara imeshafanyika kwa asilimia 69, naomba Mheshimiwa Waziri anipe jibu asilimia 31 iliyobaki atakabidhiwa lini na Mkandarasi?
Swali la pili, kwa kuwa, Wataalam wamethibitisha tairi za super single zinazofungwa kwenye malori zina uharibifu mkubwa sana wa barabara zetu. Je, ni lini Serikali itatoa maamuzi kuhusu hizo tairi ambazo zinaharibu barabara zetu zinazo-cost hela nyingi sana za wananchi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, time frame ya kukamilisha barabara hii hivi sasa iko katika majadiliano kutokana na kuchelewa kwa Serikali kumlipa Mkandarasi kulikotokea katika kipindi kilichopita na hivyo, alivyorudi sasa tutapata muda kamili wa kukamilisha barabara hii kutokana na majadiliano yanayoendelea hivi sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa suala la matairi ya super single, Serikali hivi sasa inangalia uwezekano wa kubadilisha kanuni zinazotumika kwa sasa ama kupunguza kiwango cha uzito utakaotumika kwa super single badala ya kutumia kile kiwango cha matairi mawili, kipungue chini ya matairi mawili ama kupiga marufuku kabisa. Kwa hiyo, hilo tunalishughulikia na mara Kanuni hizo na baada ya kujadiliana na wadau kutakapokamilika, tutalijulisha Bunge lako maamuzi yatakayotokea.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri.
Swali langu la nyongeza namba moja, ni kwa nini sasa kwa kuwa, kila kitu kimekamilika na mchakato wa manunuzi umekamilika na barabara hii ni muhimu kwa usafirishaji wa korosho, ujenzi wa barabara hii usianze mara moja badala ya kusubiri mwaka wa fedha 2016/2017, hii maana yake tutaanza Julai na wakati wananchi wanasubiri ujenzi huu uanze mara moja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba Naibu Waziri atupe Kauli ya Serikali kuhusu kilometa 160 zilizobaki, kwa sababu barabara hii ina kilometa 210 na amesema ujenzi utaanza kwa kilometa 50. Naomba majibu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ilipangiwa bajeti yake kwa mwaka huu wa 2015/2016. Kwa hiyo, kuanza ujenzi kwa mwaka huu wa fedha, fedha zake hatuna. Fedha zimepangwa kwa mwaka wa fedha ujao na naamini Bunge lako Tukufu litaidhinisha bajeti hiyo na hivyo hatuna namna nyingine zaidi ya kuanza kujenga barabara hiyo kuanzia mwaka ujao wa fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili naomba nimhakikishie kwamba dhamira ya Awamu ya Tano ya Serikali ya Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni ya dhati na ndiyo maana tumeanza na kipande hiki cha kilometa 50. Mtakumbuka barabara nyingi tumekuwa tukianza na vipande vidogo vidogo sana, lakini katika Awamu hii ya Tano tutachagua miradi michache ili tupeleke rasilimali iweze kukamilika kwa haraka na baadaye tunaendelea kwenye miradi mingine, huo ndiyo mkakati wa jumla.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Katika Jiji la Mbeya tumekuwa na tatizo sugu sana la foleni katika barabara inayotoka Uyole hadi pale kwangu Mwanjelwa, ikifika saa 10 magari hayaendi kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Bunge lililopita, Bunge la Kumi hiki kilikuwa ni kilio changu cha muda mrefu kwamba kwa nini tusifanye bypass kutoka barabara ya Uyole hadi uwanja wa ndege wa Songwe, lakini mpaka leo hii hili jambo halijafanikiwa kwenye vikao vyetu vya Road Board nimekwenda mpaka kumwona Meneja wa TANROAD bila mafanikio. Namuomba Mheshimiwa Waziri husika hapa atoe tamko ni lini barabara hii ya bypass kutoka Uyole hadi Uwanja wa Ndege wa Songwe itakamilika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, taratibu za ujenzi wa barabara zote huwa tunaanzia kwenye vikao vya Road Board vya Mkoa ambavyo Waheshimiwa Wabunge ni wajumbe. Alichokizungumzia ni kwamba inaonekana Road Board ya Mkoa wa Mbeya bado haijaridhia ujenzi wa Bypass hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba nitawasiliana na Road Board Taifa pamoja na Road Board Mkoa wa Mbeya kujua sababu halisi, kwa nini bypass hii bado haijakubalika kitaalam. Siwezi kutoa commitment inayoombwa kabla sijajua sababu za kitaalamu za kutokubalika hiyo bypass.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nisikitike na samahani kwa kauli nitakayosema, ni aidha Manaibu Waziri wanapokuja kutujibu au Mawaziri hawako serious, wanatuchukulia for granted ama hawafanyi kazi yao ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, Naibu Waziri anasema majengo ni mali ya mkandarasi hayawezi kurejeshwa Serikalini. Anataka kutuambia mimi na Rais tarehe 14 Oktoba, 2015, tuliwadanganya wananchi wa Nzega tukijua kwamba majengo yale ni mali ya mkandarasi na hakutakuwa na chuo?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mji wa Nzega una sekondari inayoitwa Bulunde, majengo yalikuwa ya mkandarasi. Je, Serikali utaratibu ule ule iliyotumia kuyapata majengo yaliyotumika kwa ajili ya sekondari ya Bulunde, inakuwa na ugumu gani leo kuyapata majengo yanayotumiwa na mkandarasi anayejenga barabara ya Nzega - Puge ili kuanzisha Chuo cha VETA.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kilichosemwa tarehe hiyo anayoongelea, tarehe ya 14 Oktoba, 2015 ni sahihi na tulichokisema hapa kwenye jibu la msingi ni sahihi, ila tunaongelea vitu viwili tofauti. Tulichokisema hapa ni kwa mujibu wa mkataba na Mheshimiwa Naibu Spika wewe ni Mwanasheria unafahamu. Kama mkataba umesema hivyo na sisi leo tukasema tofauti, tutaiingiza Serikali kwenye hasara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilichosemwa tarehe 14 Oktoba, 2015 na Mheshimiwa Rais akiwa na Mheshimiwa Hussein Bashe kule Nzega nacho bado kilikuwa ni sahihi, mchakato wake ndiyo huo unaoendelea ambao tumeuongelea hapa. Ni kitu ambacho Serikali itakifanya, lakini siyo kwa kulazimisha na kukitoa hadharani.
MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ilivyokuwa kwa Nzega Mjini, Mheshimiwa Rais wetu alipokuwa kwenye kampeni katika Jimbo la Bagamoyo aliwaahidi wananchi kuikabidhi kambi ya mkandarasi iliyopo Daraja la Makofia kwa wananchi wa Bagamoyo ili waweze kuanzisha shule ya msingi. Naomba kujua kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri taratibu zimefikia wapi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nilimjibu Mheshimiwa Bashe, dhamira ya Serikali ya kuhakikisha majengo yanayojengwa na wakandarasi yanatumika baada ya mkandarasi kukamilisha kazi zake katika shughuli zingine za kijamii iko pale pale, lakini utaratibu wa kuyapata hayo majengo ndiyo tunaobishania. Namhakikishia Mheshimiwa Dkt. Kawambwa ombi lake maadam lilifika kwa utaratibu uliotakiwa, tutaendelea kulifanyia kazi kwa utaratibu huu ambao nimemweleza Mheshimiwa Bashe kwa lile eneo la Nzega na tutatumia njia ile ile tuliyotumia kwa shule ile ya Bulunde.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Vile vile naishukuru Serikali kwa majibu mazuri kuhusu daraja hilo na mwendelezo wa ujenzi wake lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Daraja hili la Kilombero unahusisha pia ujenzi wa barabara zinazoingia kwenye daraja hilo. Barabara hizo za maingilio ya daraja zinaunganishwa na barabara itokayo kwenye mto huo kwenda Lupilo – Malinyi - Kilosa - Mpepo - Londo - Lumecha hadi kwa Mheshimiwa Naibu Waziri Namtumbo. Barabara hii niliyoitaja hadi sasa haipitiki kabisa kutokana na uharibifu mkubwa uliofanywa na mvua na mkandarasi yupo site hawezi akamaliza ukarabati wa uharibifu ambao umefanyika. Je, Serikali ina mpango gani wa dharura kusaidia kunusuru hali mbaya ya usafiri katika barabara hiyo ambayo nimeizungumzia?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kivuko cha Mto Kilombero baada ya kukamilika daraja lile, tumekubaliana kupitia Mfuko wa…
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Baada ya kukamilika kivuko kile tulikubaliana kiende kwenye Kivuko cha Kikove, je, ni lini Serikali wataanza ujenzi wa gati hilo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni jirani yangu lazima akiri kwamba, katika mipango ya kunusuru maeneo ya dharura hatuwezi tukaanza sisi majirani kwa sababu maeneo yenye matatizo ni mengi sana. Hata hivyo, simaanishi nawakatisha tamaa wananchi wa Namtumbo ambao ndiyo wamenileta hapa pamoja na majirani zao wa Malinyi, sina maana hiyo, maana yangu kubwa ni kwamba tatizo hili la kukatika mawasiliano ni la Tanzania nzima. Maadam mvua imeanza kupungua, tunaamini sasa kazi ya kurejesha mawasiliano itafanyika kwa kasi kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli naomba nichukue nafasi hii kuwaelekeza TANROADS Mikoa yote sasa tuanze kuelekeza nguvu ya kurudisha mawasiliano katika maeneo yaliyokatika kwa sababu mvua sasa zimepungua. Fedha tutakazotumia hazitapotea bure kwa sababu mvua imepungua. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili, naomba Mheshimiwa Dkt. Mponda turudi kule tulipokubaliana ambapo ilikuwa katika kikao cha Mkoa na sisi tuliwakilishwa na watu wa TEMESA tuangalie kama mahitaji ya TEMESA Mkoa hayatoshi, wao watatuletea Kitaifa halafu tutaangalia utekelezaji wa hilo suala.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Kwa kuwa barabara hii ni sehemu ya Great North Road iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu na Watanzania; na kwa kuwa ni sehemu ya Tanzania tu ambayo haijakamilika mpaka sasa; na kwa kuwa baadhi ya Wakandarasi wanasuasua; kazi zimesimama kwa baadhi ya maeneo; je, Serikali inatuhakikishiaje Watanzania kwamba barabara hii itakamilika kwa wakati? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati akiwa Waziri wa Ujenzi katika Mkutano wa Wadau uliofanyika Saint Gaspar aliwaahidi Wanadodoma kwamba atajenga ring roads ili magari yanayotoka mikoa mbalimbali yaishie nje ya Mji kupunguza msongamano wa magari; je, ni lini upembuzi yakinifu utaanza kwa ajili ya kujenga barabara hizo za ring roads?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kuhusiana na kipande kilichobakia cha Msalato na vipande vichache vilivyobaki vya kukamilisha hii barabara ya North Great Road, kwa vyovyote vile muda si mrefu barabara hii itakuwa imekamilika na naomba kumhakikishia hilo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili la ring roads, aliyeahidi ambaye wakati huo alikuwa Waziri wa Ujenzi, hivi sasa ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, labda tu nimjulishe; hapa nina ramani nitamwonesha, labda kwa niaba ya wengine, hasa Waandishi wa Habari... (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, tayari tuna mpango mkubwa kabambe wa kujenga za ring roads ndani na nje ya Manispaa ya Dodoma katika kipindi cha miaka mia moja ijayo. Mpango huu utatekelezwa kwa kadiri mahitaji yanavyokuja. Barabara ambazo tunazo hapa za miaka mia moja ijayo, ziko barabara nane kubwa na jumla yake ni Kilometa 147.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa barabara hii ya kwenda Kondoa – Babati inafanana kabisa na ahadi iliyotolewa na Mheshimiwa Rais Mstaafu na Rais huyu wa sasa, Mheshimiwa Magufuli, kwamba barabara ya kutoka Mbande – Kongwa – Mpwapwa mpaka Kibakwe itajengwa kwa kiwango cha lami; na ahadi hii ni ya miaka nane: sasa namwuliza Mheshimiwa Waziri, je, katika bajeti ya mwaka huu barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa lubeleje pamoja na Wabunge wengine wa maeneo husika kwamba barabara inayoongelewa ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kwa kipindi cha mwaka 2015/2020, kwamba itakamilishwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Spika, naomba tusubiri tarehe 17, bajeti ya Mheshimiwa Waziri itasomwa ambayo itatoa majibu yote kwa undani zaidi na nisingependa kueleza sasa nikagusa hotuba yake.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Barabara hii ahadi yake ilikuwa ni kujengwa kwenye bajeti ya mwaka 2009/2010 na daraja lile ilikuwa ni 2009/2010, lakini mpaka leo daraja lile halijajengwa. Je, majibu ya msingi ya Mheshimiwa Waziri yataleta matumaini kwa wananchi wa Jimbo la Momba hasa eneo la bondeni kwamba itaanza kujengwa mapema mwaka 2016/2017?
Swali la pili, Momba ni Wilaya mpya ambayo inaunganisha Mji wa Tunduma na kutoka Tunduma kuelekea Makao Makuu ya Momba, eneo la Chitete ni Kilometa 120. Je, Serikali inasema nini kuhusiana na kutujengea daraja katika Mto Ikana katika Kijiji cha Chitete, Kata ya Msangano ili wananchi wa Tunduma waweze kufika kule wakiwa wanatumia barabara ile ambayo itakuwa na kilomita 68?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema na kama nilivyoelekezwa na Waziri wangu wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, ahadi yake kwa Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha, Mbunge wa Kwela, ambaye ndiye amekuwa akifuatilia ujenzi wa daraja hili pamoja na barabara kwa upande ule wa Mkoa wa Rukwa, utatekelezwa kama ulivyoahidiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali dogo la pili linalohusu Mto Ikana, namwomba Mheshimiwa Mbunge alilete swali hili rasmi Wizarani ili Watalaam walipitie kabla mimi Naibu Waziri sijatoa commitment ili commitment yangu izingatie ushauri wa Watalaam.
MHE. RIZIKI SHAHARI MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nina maswali mawili ya nyongeza na ukiniruhusu nina ombi pia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuondoa huduma za usafiri wa majini kwa wananchi wa Mafia kwa upande wa Serikali, lakini bado Serikali hiyo ikatoa huduma kwa Mashirika yake ya Umma kwenye sehemu nyingine za Maziwa Makuu. Serikali haioni kama inawabagua watu hawa wa Mafia?
Swali la pili; Waziri atakubaliana nami kwamba, kwa sababu katika swali langu la msingi niliulizia pia viwango vya boti. Huo utaratibu ambao wameruhusu SUMATRA wauendeshe ndiyo huo wa kutuwekea boti ambazo hazina viwango na pia hazina bima. Je, Serikali haioni kuna ulazima sasa wa kuwa na mipango ya muda mfupi, kuwa na usafiri wa kuaminika wa majini kwa Watu wa Mafia wakati wakiendelea kushawishi hao wawekezaji binafsi kuja kutoa huduma hiyo?
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nina ombi na hili ni kwa jumla siyo kwa Waziri wa Wizara hii tu, bali kwa Mawaziri wote kwamba tafadhalini sana, peaneni dose ya know your country, kwa sababu majibu mnayotoa ni standard namuomba Waziri husika aje Mafia aone kama hilo Gati analozungumzia lina viwango hivyo anavyovieleza hapa. Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana kwa karibu sana na Mbunge wa Jimbo la Mafia, Mheshimiwa Mbaraka Dau. Wameondoa tofauti ya Vyama, wameungana, wanawatumikia watu wa Mafia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbaraka Dau muda wote amekuwa akisisitiza kuhusu gati la Nyamisati ili kuweza kuunganisha kati ya Kilindoni na Nyamisati ili uwezekano wa kuongeza uvutiaji wa wawekezaji wa kutoa huduma katika eneo hilo. Nawashukuru sana kwa kuungana na mimi nawahakikishia Muungano huo tutahakikisha unazaa matunda haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ubaguzi kwa kutoa huduma kwenye Maziwa Makuu, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba uamuzi huu wa kuondoa shirika ambalo lilikuwa linatoa huduma za meli baharini upande wa Bahari ya Hindi ulifanyika ndani ya Bunge hili na kama mnaona kuna ulazima wa kurudia tena ili tulianzishe Shirika la Kutoa Huduma kwenye Bahari ya Hindi tutafanya uamuzi humu ndani, baada ya Serikali kulitafakari suala hilo kwa kina na kuangalia faida na hasara zake. Suala la ubaguzi halipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu SUMATRA kutoa vibali kwa boti ambazo hazina standard, nimemsikia na naomba kumhakikishia nitalishughulikia hilo kuona ukweli wake, undani wake na sababu zake ili tuweze kurekebisha huduma zinazostahili na boti zinazostahili kutoa huduma pale Mafia ziweze kufanya kazi.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Shahari nadhani ombi lako atakujibu Mheshimiwa Waziri baadaye baada ya kujiridhisha kama anaweza kuja huko.
MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
24
Kwa kuwa, katika jibu lake la msingi Mheshimiwa Waziri amesema sababu moja kubwa ya uwekezaji au kuvutia uwekezaji ni kukua kwa biashara, na kwa kuwa Mikoa ya Kusini, Ruvuma, Lindi, Mtwara ina karibu Watanzania milioni 5, na kwa sababu kwa Mikoa hii haijapata huduma ya uhakika ya usafiri wa meli kwa zaidi ya miaka 10 hivi sasa.
Je, Serikali haioni kuna haja sasa ya kuipa kipaumbele cha juu kabisa Mikoa hii kushawishi wawekezaji kuwekeza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia tumelisikia hilo tukalifanyie kazi, tutakuja na majibu pale Serikali itakapoona njia ya muafaka kulifanyia kuhusu wasafiri hao wa maeneo ya Kusini.
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu lakini nashukuru pia Serikali kwa msukumo wa kuimarisha mawasiliano. Nina swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa, iko minara ambayo imeshindikana kuihudumia muda wote kutokana na tatizo la barabara, katika Kata za Ulowa, Ushetu, Ubagwe, Bulumbwa, Ulewe, Nyankende wameshindwa kupeleka mafuta wakati wa mvua. Je, Serikali iko tayari kututengenezea madaraja ya katika maeneo ya Kasheshe na Karo ili mawasiliano yaweze kuimarika na huduma zingine kuendelea?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara ni wajibu wetu vilevile pamoja na mawasiliano. Ninachoomba ni kumhakikishia matatizo ya barabara na hasa madaraja hayo mawili, daraja ya Karo na daraja la Kasheshe yatafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo na kwa nafasi hii namtaka Meneja wa TANROADS Mkoa wa Shinyanga afuatilie madaraja hayo mawili ili wajibu wetu kama Wizara wakutoa huduma ya mawasiliano pamoja na barabara uweze kutekelezwa kikamilifu katika eneo hilo la Ushetu.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Kwa kuwa, tatizo hili la Ushetu la mawasilinao lipo pia katika Jimbo langu la Mkuranga katika vijiji kama vile vijiji vya Mkuruwiri, Nyanduturu, Kibesa, Msolwa, Kibewa na kwingineko. Je, Serikali ina mipango gani ya kuhakikisha kwamba wananchi hawa wa vijiji nilivyovitaja na vinginevyo viweze kupata mawasiliano ya simu na wao waweze kuwasiliana na ndugu zao na shughuli zao zingine za kijamii na kiuchumi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesikiliza, nimepokea maombi yake. Tutayafanyia kazi na tutawasiliana naye mara nitakapopata taarifa kamili kuhusu maeneo haya aliyoyaelezea.
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Upatikanaji wa gesi na mafuta katika nchi hii ulileta matumaini kwa Watanzania kwamba sasa watapata fursa ya kupata ajira katika shughuli hizo. Kwa kuwa Serikali inakiri kabisa kwamba ni muhimu hii kozi kuwa inatolewa hapa nchini ili Watanzania waweze kupata uwezo wa kuajirika au kupata ajira katika sekta ya mafuta na gesi na mpaka leo Serikali ndiyo bado iko kwenye mchakato wa kuanzisha kozi hii. Nataka kufahamu, Serikali kwa nini ilianzisha uchimbaji wa gesi na utafutaji wa mafuta hapa nchini wakati bado haijajenga uwezo kwa Watanzania kutumia fursa hizi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika sheria zinazosimamia shughuli za bandari inazitaka meli zikishaweka gati kwenye bandari zetu theluthi mbili ya wafanyakazi wanaoenda kutoa huduma kwenye zile meli wawe ni Watanzania. Kwa sasa meli zote zinazoingia zinakuja na wafanyakazi wake na hivyo kuwakosesha ajira Watanzania wanaotegemea ajira kwenye bandari zetu. Je, ni lini Wizara hii itaivunja hii Bodi ya SUMATRA na kuiunda tena upya ili iweze kusimamia majukumu yake?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Ally Mtolea, Mbunge wa Temeke kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mheshimiwa Abdallah Ally Mtolea na kwa kweli Watanzania wote wanafahamu kwamba Chuo cha Bandari tunachokiongelea pamoja na DMI ni hatua ya nyongeza. Mafunzo kwa ajili ya utaalam wa masuala ya mafuta na gesi yalishaanza kutolewa muda mrefu katika Chuo cha Dodoma pamoja na Chuo cha Madini na wahitimu wameshaanza kutoka. Kwa hiyo, nachomueleza Mheshimiwa Mbunge ni kwamba katika chuo hiki tunaongeza mafunzo. Kitu ambacho ni kipya katika chuo hiki ni yale mafunzo ya usalama ambayo yatafanyika katika Chuo cha DMI na wenzetu wa Norway wametuahidi kutuimarisha katika eneo hili ili tuwe nchi ya pili kwa Afrika kutoa mafunzo hayo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, hata sisi tumepata malalamiko kutoka kwa Mabaharia na kwa kweli tumehangaika nao sana na nadhani wanatuelewa kwamba tafsiri ya ile sheria unayoongelea haiko hivyo kama inavyotafsiriwa. Tunaomba tuipitie hiyo sheria upya pamoja na Sheria ya SUMATRA ili tukipate kile tunachokitaka yaani sisi, Mabaharia na Waheshimiwa Wabunge.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Waziri anaonaje akishirikiana na Wizara ya Elimu wanafunzi wote wanaosoma masomo ya sayansi kwa A level wapate somo la health and safety ili iwe ni general kwa public ikiwepo sisi Wabunge kupewa elimu kama moto ukitokea kwenye Bunge hili tahadhari inakuaje, milango ikoje na mambo mengine yakoje humu ndani?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Waziri wangu Kivuli wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa umakini kabisa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaongea na mtaalamu kati ya wataalamu wachache tulionao nchini. Tumechukua hoja yake na tutawasiliana na Wizara ya Elimu na namuomba ashiriki kama ambavyo amekuwa akitushirikisha katika mambo mengine ya elimu ili tuweze kufikia huko kwenye eneo ambalo yeye amebobea
MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri yenye kutia matumaini makubwa, naomba niulize kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara hizi zimeathirika kiasi kikubwa wakati huu wa mvua ambazo zimenyesha kwa wingi na kwa kuwa mpaka hivi sasa barabara hizo hazipitiki, je, Serikali iko tayari kutengeneza sehemu korofi ili usafiri uendelee kama ilivyokuwa zamani?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kusisitiza kwamba vijana wetu wa TANROADS pamoja na Mameneja wa TANROADS Mkoa hivi sasa waelekeze nguvu katika kufungua mawasiliano kwa sehemu zote zilizoathiriwa na mvua. Hii ikiwa ni pamoja na barabara hii ya Nyahua - Chaya ambayo imekatika kwa kipindi kirefu kidogo.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa kuna umuhimu wa kuunganisha barabara za mikoa na wilaya na kwa kuwa barabara inayounganisha barabara ya Iringa na Morogoro inapitia kwenye milima Kitonga na kwa kuwa linapotokea tatizo katika milima hiyo inakulazimu upite Dodoma, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutenga fedha kuunganisha barabara nyingine ambayo ni fupi inayoanzia Kidabaga – Idete – Itonya - Mhanga ambayo inaenda kutokea Mbingu kule Morogoro?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hili eneo la Kitonga likiwa na matatizo wasafiri wa upande wa barabara hii wanayoitumia kutoka Dar es Salaam – Mbeya na kwenda Tunduma wanapata matatizo sana na wakati mwingine wanalazimika kupitia njia ambazo ni ndefu zaidi. Ni kweli vilevile hii barabara iliyoongelewa na Mheshimiwa Mwamoto inayoanzia Kidabaga na kuingia Morogoro ni barabara fupi sana na sehemu ya kuunganisha ni kilometa zisizozidi 25.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutahakikisha eneo hili tunalifanyia kazi kwa haraka ili azma ya halmashauri zilizokuwa zinafungua barabara pande zote za kutoka upande wa Morogoro na upande ule wa Iringa iweze kukamilika kwa kumalizia hicho kipande kidogo kilichobakia cha kuunganisha mikoa hiyo miwili.
MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Spika ahsante sana. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini naomba niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa madaraja haya jinsi yalivyojengwa, kipindi cha mvua huwa ni kero kubwa kiasi kwamba mawasiliano yanakatika kabisa pamoja na kwamba madaraja yapo watu wanashindwa kuja mjini, wanashindwa kwenda vijijini; na kwa kuwa tunafahamu kwamba uchumi unategemea sana barabara na barabara zinaunganishwa na madaraja; na kwa kuwa maeneo hayo ya Jimbo ndiyo maeneo yenye uchumi mzuri kwa maana yanapata mvua za kutosha na mazao yake ni ya kuaminika.
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuyajenga madaraja haya katika kiwango cha kuyafanya yapitike hata wakati wa mvua ili Wilaya iweze kupata mapato na uchumi kipindi chote na watu kuondolewa kero za kusafiri wakati wa mvua?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Makanyaga kwa namna alivyoitikia wito wetu wa kuingia kwa umakini kuhusiana na matatizo haya ya madaraja mawili. Kwa taarifa tulizonazo kupitia TANROADS Mkoa, madaraja haya yanapitika isipokuwa kwa mwaka huu, mvua ilikuwa nyingi sana na siltation iliziba, maji yakawa yanapita juu ya daraja. Tunaamini hali ya mvua ya mwaka huu ambayo haikuwa ya kawaida pengine miaka ijayo hali haitakuwa hivyo.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, tutahakikisha TANROADS Mkoa wanaendelea kuyaangalia haya madaraja na wakiona kuna umuhimu wa kuyapandisha, kuyaondoa, kuyapanua na kuyageuza ili tulete daraja tofauti na zaidi ya hii vented drift kupitia Road Board ya Mkoa, mapendekezo hayo yatapitiwa na hatimaye Serikali itaangalia namna ya kuyashughulikia. Kwa taarifa ya Road Board Mkoa pamoja na TANROADS Mkoa, mazingira ya madaraja hayo ambayo tumeyatengeneza mwaka jana tu na mwaka juzi yanatosheleza kwa mazingira ya kiuchumi yalivyo sasa katika hilo eneo.
MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo lililojitokeza katika Jimbo la Chilonwa halitofautiani na hali iliyojitokeza katika Halmashauri ya Manispaa ya Moshi kutokana na mvua iliyonyesha ambayo imeharibu miundombinu sana na sababu kubwa ya uharibifu huo ni kutokana na mwelekeo wa namna ambavyo TANROADS wameelekeza maji kwenye Kata za Msaranga, Shirimatunda na Ng‟ambo, kiasi kwamba madaraja yameharibika sana. Je, Serikali inatoa ahadi gani kwa wananchi wa Moshi kwamba itatoa maelekezo kwa TANROADS kuhakikisha wanarekebisha miundombinu iliyoharibika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutawasiliana na TANROADS ili wakayaangalie hayo maeneo ili hatimaye wajue nini cha kufanya katika kurekebisha mawasiliano. Kwa kweli mawasiliano yamekatika sehemu nyingi za nchi yetu na kama ambayo nimekuwa nikijibu hapa mara nyingi, tulitoa maelekezo maalum kwa TANROADS Mkoa kwamba sasa baada ya mvua kwisha tuelekeze nguvu zetu katika kurekebisha mawasiliano pale ambapo yamekatika.
MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kutuona hasa sisi watu wa huku nyuma. Mimi nina swali moja tu. Kipande cha barabara cha kilometa nane kutoka Chuo cha Mipango hadi Msalato, huu ni mwaka wa tatu hakijakamilika na wakandarasi walishaondoka eneo hilo, tunavyozungumza hivi barabara ya kutoka njiapanda ya Usandawe pale Zamahero hadi Bonga karibu inakamilika, lakini kilometa nane hizi hakuna chochote kinachoendelea.
Mheshimiwa Waziri atuhakikishie hapa wananchi wa Dodoma na Wabunge wote hapa, lini kipande hicho kitakamilika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kipande hiki nimeshakijibu mara kama mbili na naomba niendelee kusisitiza na Waheshimiwa Wabunge mtuamini kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano inaposema kitu inamaanisha na inapoahidi itatekeleza.
Mheshimiwa Spika, nilisema kipande hiki cha kilometa nane nukta, Mkandarasi alikuwa ameondoka site kwa sababu Serikali hatukumlipa baadhi ya certificates ambazo alikuwa amezitoa na kwa sasa kutokana na makusanyo ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI aliendelea kufafanua, kwamba sasa hivi makusanyo ni mazuri na tunaelekeza katika miradi ambayo imekwama, tuondoe madeni ili wakandarasi warudi katika maeneo ambayo Wakandarasi waliondoka, moja kati ya maeneo hayo ni hilo eneo la Msalato, ili kuunganisha ile barabara ikamilike, maana yake hicho kipande cha kilometa nane nukta kidogo ndiyo kilichobakia.
Mheshimiwa Spika, naombeni sana Waheshimiwa Wabunge mtuamini na tutahakikisha huyu mkandarasi tunamfuatilia ili arudi kwa sababu yeye alikuwa na certificates nyingi ambazo hakulipwa na tumeshamlipa mpaka sasa lakini hatujamaliza zote, ni karibuni tu tunategemea kumaliza zote. Kwa kweli pamoja na kwamba hatujamaliza certificates zote, tunamtaka mkandarasi huyo arudi site, kabla hatujamalizia certificates za mwisho, akakamilishe hicho kipande kidogo kilichobakia ili tuhakikishe barabara hii inakamilika kama ilivyokusudiwa na wananchi waanze kutumia huduma kwa ustawi ule ambao ulikuwa unategemewa.

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kulikuwa na deni la mkandarasi huyo, lakini kwa ufupi mkandarasi tumeshamlipa na wakati wowote kuanzia sasa hivi mkandarasi huyo atarudi site aifanye kazi hiyo na tunaamini kazi hiyo itafanywa kwa viwango kama tulivyokubaliana.
MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, ni kweli sijaridhikia kwa sababu ukiangalia kwa miaka takribani kumi toka wameanza kujenga hivi vipande vidogo vidogo wamejenga kilometa 19 tu, ina maana hizi kilometa 96 labda zitatumia miaka mingine 30.
Swali, kwa kuwa barabara hii sasa ilianza kujengwa kwa vipande vya lami toka mwaka 2008 ambapo lami zile ziliziba kabisa makalavati hali inayopelekea wananchi wa Ndungu na Maore ama kufariki au mazao yao kuharibika kutokana na mvua au maji yale yanayotuama.
Je, ni lini sasa mtahakikisha kwamba makalavati yale yanajengwa ili watani zangu kule wasipate matatizo pamoja na vifo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naelekea kwangu sasa, kwa kuwa barabara ya Kawawa hadi Marangu Mtoni ilijengwa kwa lami mpaka kiasi cha nusu, lakini cha ajabu barabara hiyo imejengwa kiwango cha lami madaraja yote hayajajengwa hali ambayo inapelekea magari kuanguka na watu wameshafariki, ni lini madaraja katika barabara hiyo yatajengwa hasa ukizingatia land scape ya Kilimanjaro?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwa upande wa barabara hiyo ambayo umeisema haina lami na ni barabara pekee isiyo na lami..
SPIKA: Ni katika barabara za TANROADS za Mkoa.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ni kama tulivyosema katika jibu la msingi kwamba sasa tumedhamiria kuijenga barabara hiyo yote kwa lami na tutaanzia na upembuzi yakinifu pamoja na usanifu wa kina ambao unafanyika katika mwaka huu ujao wa 2016/2017 wa fedha na ninaamini Waheshimiwa Wabunge mtaipitisha bajeti yetu ili tuweze kuifanya hiyo kazi tuweze kutekeleza ahadi za viongozi wetu wawili waliopita kama ambavyo Waheshimiwa Wabunge wa maeneo hayo wanapenda.
Mheshimiwa Spika, kwa swali la pili nimejulishwa na CEO wa TANROADS kwamba amelisikia na tutakuja kulitolea jibu wakati wa bajeti ya Wizara.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.
Kwa kuwa ukikaa karibu na waridi unanukia basi na mimi naomba niombee barabara yangu ya kutoka Mkomazi kwenda Mnazi, Lunguza hadi Mng‟aro sasa ifikiriwe kujengwa kwa kiwango cha lami. Naomba Mheshimiwa Waziri atuambie ni lini barabara hii itaingia katika mchakato huo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumepokea ombi lake na tutaenda kulifanyia kazi, muda siyo mrefu tutamletea majibu yaliyo sahihi.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, nimeleta maombi yangu Wizarani kwa sababu Halmashauri ya Wilaya haina uwezo wa kukarabati barabara hii ya Gulwe - Berege - Chitemo - Mima - Sazima - Igoji Kaskazini - Fufu na Iwondo, sasa hivi haipitiki wananchi wanapata taabu hasa abiria kufika Makao Makuu ya Wilaya na ndiyo maana nimeleta. Tayari tulikuwa na kikao cha Bodi ya Barabara tarehe 29 mwezi wa Februari nilipeleka ombi hili. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri muifikirie barabara hii kuipandisha hadhi ili TANROADS waweze kuitengeneza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, barabara ya kutoka Mbande - Kongwa kwa Mheshimiwa Spika, Mpwapwa na Kibakwe kwa Mheshimiwa Simbachawene Waziri wa TAMISEMI, hii barabara imeahidiwa kutengenezwa kwa kiwango cha lami na ahadi hiyo ni ahadi ya Rais Mstaafu Mheshimiwa Kikwete mwaka juzi na mwaka jana wakati wa kampeni za CCM Mheshimiwa John Pombe Magufuli, Rais wetu aliahidi kuitengeneza barabara hii ya Mbande - Kongwa - Mpwapwa mpaka Kibakwe kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Waziri huoni kwamba kuna umuhimu wa kutengeneza barabara hii ambayo ni kiungo kikubwa cha Majimbo matatu Kongwa, Mpwapwa na Kibakwe?(
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, barabara hii kama ambavyo tumejibu hapo nyuma kwamba Serikali imedhamiria kuijenga na imeanza kuijenga na itaikamilisha mapema kwa kiwango cha lami kutokea Mbande - Kongwa - Mpwapwa hadi Kibakwe kama ambavyo Mheshimiwa Lubeleje, Mheshimiwa Job Ndugai pamoja na Mheshimiwa Simbachawene walivyokuwa wakitusukuma katika kuhakikisha hii barabara inakamilika kwa haraka.
Mheshimiwa Spika, ninawahakikishia mtapata majibu mazuri zaidi wakati wa bajeti kuhakikisha kwamba ninachokisema hapa na kwa kweli hatutarajii kitu ambacho Mheshimiwa Lubeleje mnamfahamu ni mtu wa siku nyingi sana na hatungependa aendelee kufika mara zote ofisini kwetu kufuatilia barabara hii mara kwa mara ni lazima tuifikishe mwisho.
Mheshimiwa Spika, kuhusu barabara ya Gulwe - Berege - Mima hadi Fufu pamoja na nilivyojibu katika jibu langu la msingi, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Lubeleje kwamba Mfuko wa Barabara utaangalia kwa makini na hasa kwa kuzingatia kwamba mwaka huu mvua imekuwa nyingi sana na zimeharibu barabara nyingi sana uwezo wa Halmashauri wa kuzirudisha hizi barabara ni mdogo.
Mheshimiwa Spika, tutaomba Mfuko wa Barabara na TANROADS wajaribu kusaidia maeneo mbalimbali katika kurudisha mawasiliano katika barabara zote zilizokatika nchini ikiwa ni pamoja na hii ya Gulwe - Berege - Mima hadi Fufu.
MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa wakandarasi hawa wakati wanaendelea kujenga barabara hizi katika maeneo yetu mbalimbali wamekuwa wakitumia bidhaa mbalimbali ikiwemo mawe, mchanga, maji, vibarua na vifusi; na kwa kuwa Serikali katika mikataba yao inakuwa kwenye BOQ imeweka bei maalum ambayo inawalipa wakandarasi hawa lakini wengi wakandarasi hawa wamekuwa wakichukua bidhaa hizo katika vijiji vyetu bure au kwa bei ndogo sana na hivyo kuwakosesha wananchi wa maeneo hayo kunufaika na bidhaa hizo. Je, ni lini Serikali sasa itatoa angalau bei elekezi kwa wakandarasi wote wanaofanya kazi za kujenga barabara waweze kununua mawe na bidhaa nyingine ili wananchi nao wafaidike kama watu wa madini na maeneo mengine?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Omary, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumkumbusha Mheshimiwa Mbunge kwamba wanaojenga hizo barabara ni sisi wenyewe, ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia kodi zetu. Kwa kweli masuala haya lazima tukubaliane tunaya-balance vipi kati ya upatikanaji wa material ya kujengea barabara pamoja na upatikanaji wa fedha za kujenga barabara yenyewe.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Omary kwamba Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambayo ndiyo yenye dhamana ya kutoa bei ya fidia kwa maeneo ambayo yanatwaliwa na Serikali italifanyia kazi suala hili lakini siyo rahisi kutoa bei elekezi kwa sababu nchi ni kubwa na kila mahali pana thamani yake tofauti sana. Vinginevyo itakuwa ni kitabu kikubwa sana ambacho kitaorodhesha kila mahali na thamani ilivyo kwa nchi nzima, itakuwa ni ngumu. Nadhani njia inayotumika ambayo kwa kawaida ni mazungumzo kati ya halmashauri na wale ambao wanahusika na eneo linalotwaliwa pamoja na mkandarasi ni nzuri zaidi kufikia muafaka wa bei ya kutumika katika kununua eneo linalotumika kwa ajili ya upatikanaji wa hayo material ya kujengea barabara.
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini naomba niongezee kwamba Serikali haiwezi ikaanza kununua udongo ama changarawe kwa sababu miradi hii tutashindwa kuijenga. Sasa hivi Serikali inatumia kila kilometa 1 kujenga barabara kwa takribani shilingi bilioni 1. Sasa kama tutaanza kununua udongo, changarawe tutashindwa kuwajengea wananchi wetu hawa barabara hizi. Serikali inalofanya tu ni kulipa fidia hasa kwenye structure kwa mfano majengo na maeneo mengine lakini hatuwezi kuanza kununua udongo, changarawe na vitu vingine tutatishindwa kujenga miundombinu kwa ajili ya Watanzania.
MHE. OSCAR R. MUKASA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ipo ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati akiomba kura kwa wananchi wa Biharamuro ya kujenga barabara kilometa 4 - 5 kwa kiwango cha lami kwenye Mji wa Biharamuro. Naomba kufahamu kutoka Serikalini kwamba utekelezaji wa ahadi hiyo umefikia wapi? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Biharamuro, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi anayoongelea ni kweli ilitolewa na Mheshimiwa Rais na kwa kweli ahadi hiyo ilianzia kutoka Serikali ya Awamu ya Nne na ni kwa ajili ya eneo hilo lakini vilevile eneo jirani ambalo Mheshimiwa Dkt. Kalemani anatoka, ahadi hizo zote tutazitekeleza. Lini, itategemea na upatikanaji wa fedha kwa sababu utekelezaji wa ahadi hizo unahitaji rasilimali fedha. Kwa hiyo, naomba nikuahidi ahadi hizo tutazitekeleza na nikuahidi miaka mitano hii ambayo ndiyo tumepewa hii dhamana ya kuwajengea Watanzania miundombinu na kutekeleza ahadi zote ambazo viongozi wetu walizitoa nikuhahikikishie tutazitekeleza.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Sera ya Serikali ni kuunganisha barabara za mikoa na za wilaya kwa lami lakini katika Mkoa wetu wa Iringa, Wilaya ya Kilolo ni wilaya ambayo toka mwaka 2002 imepata hadhi ya kuwa wilaya mpaka leo hii haijaweza kuunganishwa kwa lami kutoka yalipo makao makuu. Ni lini sasa Serikali itaunganisha wilaya hii na makao makuu kwa lami ili hii sera iweze kutimia?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wilaya ya Kilolo haijaunganishwa na barabara ya lami kama ambavyo Mbunge wa Kilolo na Mbunge wa Viti Maalum Mheshimiwa Ritta Kabati wamekuwa wakifuatilia suala hili ofisini kwetu na nyakati zote tumekuwa tukiwaahidi kwamba tutafuatilia. Kwanza Mheshimiwa Rais alipopita lile eneo hiyo pia ilikuwa ni sehemu ya ahadi yake licha ya kwamba hii ni ahadi ya kiujumla kwa wilaya zote.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie maadam dhamira yetu ni kuhakikisha miundombinu inajengwa na ahadi zote za viongozi wetu tunazitekeleza atupe muda ili tutakapopata ratiba kamili ya suala hili tutatekeleza. Mnafahamu tumeanza kwa kiwango fulani, ni kiwango ambacho hakitoshelezi nakubali kama ambavyo Mheshimiwa Mwamoto amekuwa akinisukuma kila wakati kuhusu hilo suala. Niwahakikishie wote Mheshimiwa Mwamoto na Mheshimiwa Ritta Kabati kwamba ahadi hiyo tutaitekeleza kama ambavyo tumeongea nao tukiwa maofisini.
MHE. MOHAMED O. MCHENGERWA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza Mheshimiwa Waziri atambue kwamba mimi siyo aina ya Wabunge ambao atawajibu rejareja nikamwachia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka Mheshimiwa Waziri atambue kwamba mwaka 1955 Mwalimu Nyerere aliahidi ujenzi wa barabara hii akiwa katika kikao cha Halmashauri Kuu ya TANU, Tarafa ya Mkongo. Pia tarehe 9/9/2015, Mama Samia Suluhu aliahidi ujenzi wa barabara hii kiwango cha lami alipokuwa katika harakati za kampeni pamoja na Rais, Mheshimiwa Magufuli. Vilevile Rais wa Awamu ya Nne na Awamu ya Tatu wote waliahidi ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Waziri ametudanganya hapa kwamba barabara hii inapitika kirahisi, naomba atuambie kwamba ahadi hizi za Marais hawa zilikuwa ni ahadi hewa? Hiyo ni moja. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, terehe 5 Juni, 2016, Rais Magufuli akiwa Ubungo aliahidi ujenzi wa barabara ya Ubungo kwa kiwango cha lami ambapo suala hili wananchi wa Jimbo la Rufiji waliliona kwamba ni neema kwa kuwa Mheshimiwa Rais atakuja pia kuweka ahadi za namna hiyo katika Jimbo la Rufiji hususani barabara hii ya Nyamwage - Utete ambayo inategemewa na wananchi hususani akina mama. Naomba kufahamu kwamba Wizara hii ipo tayari kukiuka Ibara ya 13 ya mgawanyo sawa wa pato la taifa kwa kuwasaidia na kuhakikisha kwamba inawatendea haki maskini na wanyonge wa Jimbo langu la Rufiji? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Omary Mchengerwa, Mbunge wa Rufiji kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, viongozi wanapotoa ahadi wanaonesha dhamira. Mimi nimhakikishie Serikali hii ya Awamu ya Tano ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli nayo ina dhamira ya dhati ya kuwajengea Watanzania miundombinu ikiwa ni pamoja na wananchi hawa wa Rufiji kwa barabara hii anayoiongelea. Naomba nimhakikishie kwamba hiki tulichokisema humu ni cha dhati na hatudanganyi na hakuna viongozi wanaodanganya. Dhamira huwa haidanganywi, dhamira ni dhamira, kinachofuatia baada ya dhamira ni uwezo wa kuikamilisha ile dhamira ambapo inategemea na upatikanaji wa fedha pamoja mipango mbalimbali ya taifa zima kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mchengerwa kwamba barabara hii tuna dhamira ya kuijenga na namhakikishia tutaijenga katika awamu hii ya miaka ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli 10. Mimi namhakikishia kwamba hii miaka 10 ya Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli tutaijenga mapema sana hii barabara kama ambavyo sasa tumeitaka TANROAD Mkoa wa Pwani ianze kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa kujenga kwa lami barabara hii kama ilivyoahidiwa na Marehemu Mwalimu Nyerere kama ambavyo yeye alisema.
MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na pia nashukuru kwa pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nitakuwa na maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, ni lini sasa hii kazi ya upembuzi yakinifu itakamilika ili ujenzi uanze?
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali la pili, wananchi wa Mbinga pamoja na Nyasa wanafurahi na wanaishukuru Serikali kwa kupata mradi wa ujenzi wa barabara wa Mbinga – Mbamba Bay chini ya mradi wa Mtwara Corridor. Je, Serikali haioni haja sasa kwa kutumia fursa hii kuunganisha kipande cha barabara inayotoka Unyoni mpaka Kijiji cha Mango Wilayani Nyasa kupitia Mapera, Maguu na Kipapa? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Martin Mtonda Msuha, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchukua fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Martin Mtondo Msuha pamoja na Mheshimiwa Stella Manyanya kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha Wilaya yao ya Mbinga inakuwa na miundombinu ya uhakika ili mazao wanayoyalima hasa kahawa inalifikia soko kwa urahisi na kwa bei nafuu. Mimi niwapongeze sana na nawahakikishieni kwamba nikiwa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano pamoja na Mheshimiwa Waziri wangu tutahakikisha dhamira yenu inakamilika katika kipindi hiki cha miaka mitano kwa kadri fedha zitakavyokuwa zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjulisha Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, kwanza naomba tuikamilishe na suala la tunaikamilisha lini kwa maana ya kutoa tarehe sio rahisi sana kwa sababu kwa sasa tupo katika hatua ya kumpata huyo mkandarasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba mtuamini kwamba tuna nia ya dhati, kazi hiyo tutaifanya na tutaisimamia na itakamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili, naomba niwajulishe Waheshimiwa Wabunge wote wa Wilaya ya Mbinga kuanzia Mheshimiwa Mtondo Msuha, Mheshimiwa Stella Manyanya na Mheshimiwa Sixtus Mapunda kwamba mwaka huu tunaanza kuijenga ile barabara ya kutoka Mbinga - Mbamba Bay.
Naomba mtupe fursa tuikamilishe barabara hii. Mtakumbuka ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kutembea kwa taxi kutoka Mtwara hadi Mbamba Bay na kutoka Bukoba hadi Mtwara itakuwa imekamilika kikamilifu kabisa. Baada ya hapo, nawahakikishia nguvu zetu zote tutakuwa tunaelekeza katika barabara hizo zingine ikiwa ni pamoja na hii barabara ya kutoka Unyoni hadi Mango kupitia vijiji ambavyo Mheshimiwa Mtondo Msuha amevitaja.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali nayo pia imeahidi ujenzi wa barabara ya Ifakara – Lupilo – Malinyi – Londo - Lumecha - Namtumbo Songea katika kiwango cha lami. Sasa ni muda barabara hiyo bado haijaanza kujengwa.
Swali langu, ni lini sasa hii kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itakamilika na barabara hii kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dokta Hadji Mponda, Mbunge wa Malinyi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie Wabunge wote wanaohusika na barabara hii ya kutoka Ifakara - Malinyi - Namtumbo - Songea kwamba Serikali ina nia ya dhati ya kuanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Labda nimhakikishie tu kwamba kazi iliyofanyika hadi sasa ni kubwa. Unafahamu kwamba kipande kile cha kutoka Lumecha - Londo kimeshakamilika kwa maana kufunguliwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini vilevile tumebakabiza kilometa 4 tu kukamilisha kuifungua hii barabara, wakati kazi ya feasibility study na detail design ikiendelea kufanyika. Nikuhakikishie kazi hii ya feasibility study na detail design pamoja na kipande hiki cha kilometa 4 kilichobaki cha kufunguliwa barabara hii itakamilika katika mwaka wa fedha wa 2016/2017 unaoanza Ijumaa.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujua tu ahadi ya ujenzi wa barabara ya kutoka Nyamwiswa – Bunda kwa kiwango cha lami ni ya muda mrefu toka mwaka 2000. Sasa napenda kujua ni lini Mkandarasi wa kujenga barabara hiyo ataanza kazi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kumbukumbu yangu, hii barabara imeshaanza kujengwa. Tatizo kiwango tunachokijenga ni kidogo, labda ndiyo anachokilalamikia Mheshimiwa Mbunge. Nimhakikishie kama kumbukumbu zangu zitakosea atanisamehe, lakini kuanza tumeshaanza. Namwahidi tu kwamba, tutaongeza kasi ili hatimaye barabara hii ikamilike kujengwa katika muda mfupi.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru kwa dhati kabisa Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa sababu wakati wa kampeni zake ilikuwa ni ahadi yake ya kujenga kivuko cha kutoka Lindi kwenda Kitunda na alisema baada ya wiki moja Mkurugenzi wa vivuko atakuja Lindi na kweli alikuja, akaja kuangalia eneo. Sasa baada ya kumaliza katika shughuli hiyo ya kwanza tulikuwa hatufahamu kinachoendelea ni kipi, lakini namshukuru Waziri kwa majibu yake mazuri yenye matumaini.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Mheshimiwa Rais alituahidi kwamba, katika maeneo yote kuanzia Tanga, Dar es Salaam kuja Lindi mpaka Mtwara kutakuwa na uwezekano wa kuwawezesha wananchi wa maeneo hayo kwa sababu wananchi hawa ni wavuvi wa samaki, kujenga kiwanda cha samaki ili kuongeza ajira kwa wananchi wa maeneo haya.
Je, Serikali imejipangaje katika kuhakikisha maeneo haya yanakuwa na kiwanda cha samaki?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, napokea shukurani kutoka kwa Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum. Namshukuru sana na kwa kweli nafurahia sana Wabunge wengi wanatambua juhudi za Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutekeleza ahadi, ana dhamira ya dhati na kila alipoahidi anajitahidi kutafuta fedha ili kuweza kuteleza ile ahadi yake. Sisi kwa kweli tulioko katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano tunajivunia kwa kupewa dhamana hii ya kuwajengea Watanzania miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu sehemu ya viwanda; maadam alitoa ahadi, nimhakikishie ahadi hiyo itatimia. Kama ambavyo amemsikia Mheshimiwa Mwijage, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji wakati akihitimisha hotuba yake ya bajeti, aliongelea kwa mapana kwamba, karibu kila mahali kuna aina ya viwanda ambavyo anavikusudia kuviboresha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa vyovyote vile, katika maeneo ya Pwani, wavuvi nao watafikiriwa katika kuhakikisha kwamba, tunapata viwanda na viwanda hivyo vinahamasishwa kutoka sekta binafsi waweze kuwekeza na sisi tutawawekea mazingira mazuri ili hatimaye watujengee viwanda na kuchangia katika kuibadilisha nchi hii kuwa nchi ya viwanda itakapofika mwaka 2025.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Kwa kuwa tatizo la kivuko cha Kitunda, Lindi linafanana sana na tatizo la kivuko baina ya Kilindoni na Nyamisati katika Wilaya ya Rufiji; na kwa kuwa, wananchi wa Mafia kupitia Mbunge wao, tuliiomba Wizara itupatie iliokuwa MV Dar es Salaam, ambayo kwa sasa imepaki pale Navy, Dar es Salaam ili ije itusaidie Mafia kuunganisha baina ya Kilindoni na Nyamisati. Je, ni lini Wizara itaridhia ombi hilo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kwanza niendelee kumhakikishia Mheshimiwa Dau kwamba, dhamira yetu ya kuhakikisha kivuko kinakuwepo kati ya Kilindoni na Nyamisati ni ya dhati na tutahakikisha inatekelezwa. Kikubwa nimwahidi kwamba hii meli anayoingolea MV Dar es Salaam, tumeshaeleza katika Bunge hili kwamba, meli hii bado hatujaipokea kutoka kwa supplier kutokana na hitilafu chache zilizokuwa zimeonekana na tumemtaka supplier arekebishe hizo hitilafu kabla haijatumika ilivyokusudiwa kutoka Dar es Salaam kwenda Bagamoyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Dau kwamba, kama wahusika wataona kwamba ni busara kwa sababu aina hii ya kivuko siyo ya kuipeleka mwendo mrefu sana. Kila kivuko kina design yake na kina capacity yake ya distance ya kutembea. Wataalam watakapotushauri kwamba, hili eneo nalo linaweza likatumika kwa MV Dar es Salaam, nimhakikishie hatutakuwa na sababu ya kusita kuhakikisha MV Dar es Salaam inahudumia kutoka Dar es Salaam hadi Bagamoyo na Dar es Salaam hadi Mafia.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na matatizo yaliyozungumzwa ya watu wa Kijiji cha Kitunda ambayo kwa karibu sana yanafanana na watu wa Jimbo la Busega, ambako kule Busega tuna Ziwa Victoria, hawa wana Bahari. Sasa hivi usafiri wa majini ni tatizo na Waziri mwenye dhamana wakati ule alitembelea Kijiji cha Nyamikoma katika Wilaya ya Busega na akaahidi ujenzi wa gati, lakini mpaka sasa hivi sijajua Serikali inamefikia wapi? Je, Mheshimiwa Waziri anaweza akawahakikishia wananchi wa Busega kwamba, lile gati la Nyamikoma litajengwa ili kusaidia usafiri kwa wananchi wa Jimbo la Busega na Majimbo mengine jirani kama Mwibara, Bunda na Ukerewe?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna maeneo mengi ambayo yameainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni anafahamu kwamba, katika aliyoyaeleza yamo. Nimhakikishie kile kilichoko katika Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi, ni wajibu wetu na ni lazima tukitekeleze katika kipindi hiki cha miaka mitano ambacho tumeahidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwombe Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni tulitafakari kwa undani kuchunguza katika kila kituo ambacho amekiorodhesha tuone. Hatimaye tumpe majibu kipi tunaanza lini na kipi kitafuata lini na hatimaye apate ratiba kamili ya utekelezaji wa ahadi hiyo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kwa kweli nimsifu sana kwa kazi kubwa anayofanya ya kufuatilia maslahi ya watu wako wa Jimbo la Busega. Ahsante sana.
MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii. Wilaya ya Pangani imepakana na Mji wa Zanzibar na wakazi wa Pangani wamekuwa wakijishugulisha na Mji wa Zanzibar kutokana shuguli za kijamii na kiuchumi. Je, ni lini Serikali itatupatia usafiri wa uhakika ili wakazi wa Pangani na wananchi wa jirani Muheza na maeneo ya Kilimanjaro na Arusha ili waweze kunufaika na usafirishaji huu kwa unafuu ili kuweza kufanya shughuli za kiuchumi na kijamii?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumewahi kutamka ndani ya Bunge lako Tukufu kwamba, iliyokuwa TACOSHIL tuliipaki kwa sababu tulikuwa tunatarajia sekta binasi ndiyo ijihusishe zaidi katika kutoa huduma za usafiri wa majini katika Bahari ya Hindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, inaonekana bado kuna kilio cha wengi na vile vile, hata jana nilikuwa na wateja wengine Dar es Salaam nao wanasisitiza kwamba, pengine tuangalie upya suala la TACOSHIL au tuseme huduma za meli kwenye upende wa Bahari kwamba na Serikali nayo ijihusishe kwa sababu kuna baadhi ya maeneo hayawezi kuendeshwa na sekta binafsi kwa faida.
Mheshimiwa Naibu Spika, tutaliangalia ndani ya Serikali, tuangalie kama kuna umuhimu wa kubadilisha sera hiyo na kama tutaona kwamba, hakuna umuhimu badala yake tuendelee kuhamasisha wawekezaji binafsi tutafanya hivyo. Kama tutaona kuna umuhimu tutaleta hapa tufanye maamuzi kwamba, labda turudishe ule uamuzi au yale masuala ambayo tulikuwa tunayafanya miaka ya nyuma chini ya TACOSHIL.
MHE. ZAYNAB M. VULLU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nami naomba niulize maswali mawili ambayo yanafanana na barabara ya Arusha - Simanjiro. Kwa kuwa barabara ya kutoka Mkuranga hadi Kisiju ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne na Awamu ya Tano, kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami na kwa kuwa hadi leo hii wananchi wa Wilaya ya Mkuranga na Wilaya ya Mafia wanaitegemea sana barabara hiyo: Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)
Swali la pili; kwa kuwa katika Kisiwa cha Mafia wananchi wake wanapata shida sana ya usafiri wa kutoka Mafia hadi kwenda nchi kavu ambayo ama ni Bandari ya Kisiju ama Bandari ya Nyamisati, lakini pia bado wana matatizo ya barabara za lami katika kisiwa hicho. Je, Serikali haioni sasa ni vyena ikatimiza ahadi yake ambayo ilitolewa na Rais ya kujenga barabara kuanzia Kilindoni hadi Rasinkumbi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba barabara ya Mkuranga hadi Kisiju ilitolewa ahadi na Viongozi wetu Wakuu wa Kitaifa kuanzia Rais wa Awamu ya Nne na sasa Rais wa Awamu ya Tano. Naomba nichukue fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Vulu, kama ambavyo tumekuwa tukiongelea hili suala mbele ya Waziri wangu, nami nampongeza sana kwa juhudi hizo za kufuatilia hizi barabara pamoja na mwenzake kwamba barabara hii kama ambavyo tumemwahidi tutaijenga kwa kiwango cha lami kama ilivyoahidiwa na Viongozi wetu Wakuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la lini tutaanza, naomba Mheshimiwa Zaynab Vulu utupe muda, maana yake tuna miaka mitano, ndiyo tumeanza tu, nikuhakikishie katika kipindi hicho ambacho kazi yetu kubwa itakuwa ni kuwajengea miundombinu Watanzania, tutahakikisha tunakupa jibu kamili la lini tutaanza kwa vitendo kwa maana ya kupitia bajeti zinazokuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili la kuhusiana na barabara inayoanzia Kilindoni ambayo ni sehemu muhimu sana ya kuunganisha mawasiliano kati ya wenzetu wa Mafia pamoja na Kisiju, naomba nayo nikuhakikishie kwamba tutaijenga kwa kiwango cha lami kama ambavyo imeahidiwa na unafahamu kwamba barabara hii kwa pale Mafia tumeashaanza sehemu kuijenga, tutahakikisha tunaikamilisha kujenga na hatimaye wananchi waweze kunufaika na matunda mazuri ya Serikali ya Awamu ya Tano aliyoiweka madarakani ikiongozwa na Jemedari, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mwenye nia ya dhati ya kuwasaidia watu wenye kipato cha chini ili waweze kuinuka na kupata maisha mazuri.
MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa maeneo yaliyotajwa kwenye swali la msingi, Naberera iko Simanjiro na Kibaya iko Wilaya ya Kiteto na ni maeneo yanayozalisha sana mahindi hapa nchini, kwa hiyo, ni maeneo muhimu sana kwa uchumi wa nchi yetu, lakini hakuna barabara hata moja inayounganisha hata na Makao Makuu ya Mkoa ambayo ni Babati na barabara zake ni za vumbi na hivyo zinaharibika sana kwa ajili ya kubeba mahindi nyakati za mvua.
Je, Serikali ina mikakati gani sasa kwa umuhimu nilioutaja kuhakikisha kwamba angalau kuna barabara hata moja inayounganisha maeneo hayo muhimu kwa uchumi na Makao Makuu ya Mkoa wa Babati?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, labda unipe fursa, katika swali lililopita nilisema barabara inayoanzia Kilindoni na wakati huo tunaongelea mawasiliano kati ya Mafia na Kisiju. Sikuongelea barabara kutoka Kilindoni kwenda Kisiju. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ukienda kwenye kumbukumbu, Hansard nadhani zitakuwa zimesema sahihi. Nilikuwa naunganisha usafiri kati ya Mafia na Bara, Kisiju wakati huo tunaongelea barabara ya Kilindoni inayoanzia Kilindoni, ambayo sasa amesema inaishia Rasinkumbi na hiyo barabara tumeanza kuijenga. Nilitaka tu niliweke sawa ili liweze kueleweka.
Mheshimiwa Naibu Spika, tuje kwenye barabara ya kutoka Naberela hadi Kiteto. Naomba kuchukuwa fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikai hii ya Awamu ya Tano tuna dhamira ya dhati ya kuhakikisha Mkoa wa Manyara nao unaingia katika ramani ya barabara za lami ukiacha ile Barabara Kuu ambayo inatoka Arusha kupitia Babati na kuja Singida. Nako huko tunaingiza katika ramani ya barabara za lami. Nimhakikishie kwamba hii barabara ambayo nilijibu katika swali langu la msingi kwamba, tunaanza kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, hii inayopita Kiteto kwenda Arusha na inayounganisha Mkoa wa Dodoma, hiyo nao ni sehemu ya kuhakikisha Mkoa wa Manyara tunaufungua katika kuuwekea barabara ya lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba katika miaka hii mitano tutafanya kazi ya uhakika kuhakikisha eneo hili tunaliweka sawa na tunajenga baadhi ya barabara ambazo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi tulishaainisha.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, barabara ya Mrugarama – Rulenge kwenda mpaka Mzani iko kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi kujengwa kwa kiwango cha lami, lakini kwa mwaka wa fedha 2016/2017 haiko kwenye bajeti, badala yake ni Kilometa tatu na nusu tu ambazo zimewekwa kwenye bajeti kwa ajili ya kiwango cha changarawe chini ya TANROAD; na barabara hii imekuwa mbaya sana kwa kipindi kilichopita cha mvua na mwaka mzima maana yake hakuna bajeti nyingine itakayotengeneza barabara hii:-
Je, Waziri haoni umuhimu wa kuongeza fungu ili kwa kipindi cha mwaka wa 2016/2017, barabara hii iweze kupitika kwa wepesi japo itakuwa imetengenezwa kwa kiwango cha changarawe?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gashaza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, uwezo wa kuongeza bajeti sina kwa sababu nina uhakika huu mwaka ndiyo tumemaliza, mmetupa kazi, mmepitisha bajeti yatu na tunawahakikishia sisi tutaisimamia kwa nguvu zetu zote. Kitu ambacho ninamhakikishia, tutahakikisha hii barabara aliyoiongelea, inapitika mwaka mzima. Kama itatokea mahitaji makubwa ya fedha kutokana labda na kuharibika kwa kiwango ambacho hakitegemewi, namhakikishia kwamba tutatafuta fungu la dharura ili kuweza kurudisha mawasilino kama yatakatika.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mawasiliano yatakuwepo katika kipindi chote cha mwaka wakati tukijiandaa na bajeti ya miaka inayokuja.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Tanzania nzima ili iwe barabara ni lazima kuwepo na madaraja. Katika Wilaya yangu ya Korogwe Vijijini wakati wa mvua barabara za Mkoa zote zimevunjika madaraja na hakuna magari yanayoweza kupita katika barabara ya Mkoa kutoka Korogwe kwenda Mnyuzi kwa kupitia Muheza; na barabara ya kutoka Korogwe kwenda Magoma kwa kupitia Maramba hadi Daruni.
Je, Serikali hamna mpango wa dharura kutusaidia madaraja haya ambayo wananchi wamepata taabu kwa muda mrefu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nilishasema huko nyuma kwamba baada ya mvua kwisha kipaumbele cha kwanza ni kufungua mawasiliano katika yale maeneo ambayo yalikuwa yamekatika na tulishawaelekeza viongozi wa TANROAD Mikoani kwamba wahakikishe tunafungua mawasiliano pale ambapo yalikatika. Naomba Mheshimiwa Stephen Nganyani tuwasiliane pamoja na TANROAD Mkoa ili tuone kitu gani kinaweza kufanyika kutekeleza kile ambacho nilikisema humu Bungeni.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali ilitumia pesa nyingi sana kwa ajili ya gati na kwa kuwa Serikali ilijenga majengo, mpaka sasa hivi yale majengo yamekuwa magofu na Wananchi wa Karema wamepoteza imani kabisa na Serikali kwa kwasababu walilia sana gati hili na wakalikosa mpaka sasa hivi:-
Je, ni lini sasa Serikali itaweka imani kwa wananchi wa Karema?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa, tulikuwa tuna mpango wa gati na tumetumia pesa nyingi, majengo yale yapo hayana kitu chochote, popo tu wanaingia na sasa tuna mpango wa bandari:-
Je, Serikali inaweka mikakati gani, kwa kuwa inatumia pesa nyingi na kupoteza kujenga bandari hii na wananchi wa Karema wawe na matumaini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kazi ambayo ilishaanza kufanyika wakati tulikuwa tunategemea kujenga gati, siyo kwamba imepotea, hapana. Tunapojenga bandari haina maana ile kazi yote iliyofanyika wakati tunajiandaa kukamilisha ujenzi wa gati inapotea. Hayo majengo bado yatatumika na kwa hiyo, fedha hazijapotea, ila tutakapoikamilisha hii kazi, majengo hayo na mengine ambayo yataongezeka, badala ya kuwa na gati peke yake tutakuwa sasa na bandari. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba hizo fedha hazijapotea.
Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, kama ambavyo ilielezwa katika bajeti yetu, kama utakumbuka katika kitabu chetu cha bajeti katika ukurasa wa 199 utaona kwamba Serikali imetenga shilingi bilioni 24.05 kupitia TPA kwa ajili ya ujenzi wa gati, bandari katika Maziwa Makuu.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika fedha hivi ambazo tayari zimetengwa, tutaangalia ni kiasi gani tukipeleke pale ambapo kilishapangwa toka mwanzo ili kuweka mazingira ya haraka ili wale wananchi waanze kupatumia pale mahali wakati wakisubiri ujenzi wa bandari ambayo ndiyo mambo makubwa na mazuri zaidi.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Kwa kuwa, Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2016/2017 mpaka 2020/2021 na katika mpango huo upo pia mpango wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo; na kwa kuwa katika ujenzi huo uliwekwa jiwe la msingi na kwa kuwa katika Mji wa Bagamoyo limetengwa eneo la viwanda ambapo kunahitaji uwepo wa bandari:-
Je, mpaka sasa Serikali imefikia hatua gani ya kuanza ujenzi huo ukuzingatia unategemea utaratibu wa Public Private Partnership? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tulieleza kwa kirefu dhamira na mpango ambao tayari Serikali imeshauweka wa kujenga Bandari ya Bagamoyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba mpango huo tunautekeleza kwa kupitia PPP. Kama ambavyo tulieleza katika bajeti, ni nchi tatu zinashirikiana katika hili kwa mpango wa PPP.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyosema, kikao cha karibuni kitakachofuata cha kufanya maamuzi ya kuingia katika hatua ya pili, kwa sababu kwa sasa kuna Joint Technical Committee imeundwa na inafanya kazi kila wakati kujaribu kupangilia, hatimaye utaratibu wa ujenzi wa hiyo bandari utakuwaje na hizo kazi zinapelekwa kwa hizi nchi tatu ambazo wanashiriki katika PPP hiyo; namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa itakapofika mwezi wa Kumi tutakuwa na jibu la uhakika la nini kitaanza na kitaanzia wapi.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa, Serikali ilitumia fedha nyingi sana kujenga gati la Karema, fedha hizo ambazo zilipotea na kilichojengwa pale ni nyumba moja ambayo haijakamilika na kuna choo ndicho ambacho kilikamilka; lakini fedha zilizotolewa na Serikali ni nyingi sana:-
Je, wale walioisababishia Serikali hasara kubwa sana ya fedha nyingi, mmewachukulia hatua gani ambazo ni za kisheria?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya Mheshimiwa Moshi Kakoso, naomba tuijadili kwa undani kama ambavyo tulianza na tuwashirikishe watu wengi zaidi ili hatimaye kama kweli kuna tatizo hili linaloongelewa tuanze kuwashughulikia wahusika kwa kutimia vyombo vyetu vya dola kuanza kufanya uchunguzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa ninachomwomba Mheshimiwa Mbunge, tupate taarifa kamili. Tunavyofahamu, bajeti ilitumika kama ilivyopangwa na kazi ilifanyika kama ilivyopangwa. Sasa kwa taarifa ya Mheshimiwa Moshi Kakoso, naye akiwa ni mmoja kati ya watu ambao tumedhamiria kwa pamoja kuwajengea miundombinu Watanzania, nina uhakika ana taarifa za ziada.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tuzipate hizo taarifa za ziada ili hatimaye tuzipeleke kwenye vyombo vya dola wazifanyie kazi na baadaye tuchukuwe maamuzi.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwanza naishukuru Serikali kwamba tukiwauliza maswali hapa kuwaomba waende kwenye maeneo, maeneo mengine wameshafika. Namshukuru sana Mheshimiwa Jafo kwani ametembelea barabara nilizokuwa nimeziomba za kule Msingi na Kinyangiri.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Ikungi ni moja kati ya Wilaya kubwa sana ambayo haina mtandao wa barabara na wananchi wamekuwa wakipata shida sana kufika kwenye Makao Makuu ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hususan Jimbo la Ikungi Magharibi ambao wamemwamini sana Mheshimiwa Magufuli na kumpa kura nyingi sana; ni lini sasa Serikali itaenda kule ikaangalie mzunguko wa barabara zile Puma, Ihanja, Iseke pamoja na Mwintiri hadi Igilasoni? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Martha Mlata kwamba, changamoto tunazozipata katika Wilaya ya Ikungi, nina uhakika baada ya wewe sasa kuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa CCM utatusaidia ili tuweze kuzitatua moja kwa moja ili wale wananchi wanapoambiwa nia ya Serikali ya Chama cha Mapinduzi kufanya maendeleo wasirudishwe nyuma kwa kukataa kushiriki katika masuala ya maendeleo kutokana na changamoto ambazo tunazo katika hiyo Wilaya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi watu wa miundombinu tutashirikiana naye kuhakikisha kwamba eneo hilo, changamoto zote za miundombinu tunazitatua ili Wilaya ya Ikungi iwe na hadhi kama Wilaya nyingine za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwanza naomba nishukuru majibu ambayo yametolewa na Naibu Waziri na naipongeza Serikali kwa utendaji mahiri wa kazi ambazo zinakuwa zinaletwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kwamba, kwa kuwa, umuhimu wa barabara kwa suala zima la kiuchumi halina mbadala; na kwa kuwa, Mkoa wa Rukwa ni miongoni mwa mikoa ambayo ilikuwa imeachwa nyuma kwa maana ya ukosefu wa barabara kwa kiwango cha lami, na kwa kuwa, umuhimu wa barabara kwa junction ya kuanzia Kangesa, kwenda Liapona, Kazila, unapita Mwaze pale anapotoka Muadhama Polycarp Pengo, hadi kwenda kufika Kijiji cha Mozi ambapo ndiyo customs, ni ya muhimu sana na iko chini ya TANROADS. Je, Serikali iko tayari kuiingiza katika mpango wa kuanza kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kwa kuwa katika bajeti ya 2016/2017 barabara hii haijaingizwa kwa ujenzi wa kiwango cha lami: Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari nimkabidhi barua ya maombi maalum ili iingizwe katika mpango wa kuanza usanifu kwa 2017/2018?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kandege Serikali yake ya Awamu ya Tano ina Ilani ya uchaguzi na ahadi ambazo zimetolewa na viongozi wa Kitaifa. Naomba atupe fursa kwanza tuanze kukamilisha zile barabara ambazo tumeanza kuzifanyia kazi ikiwa ni pamoja na hii barabara ambayo niliielezea kwa kirefu ambayo ipo katika Jimbo lake. Naomba sana hii sasa tuangalie huko mbele.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili, niko tayari, naomba niletewe hiyo barua maalum ili tukaijadili Wizarani na baadaye tuangalie kama tunaweza tukaiingiza katika miaka inayokaribia karibu tunaingia kipindi kingine, kama tunaweza kuikamilisha kufanya feasibility study na detailed design ili kuiandaa sasa ije ijengwe kwa kiwango cha lami katika kipindi hiki cha miaka 10 ya Mheshimiwa Dkt John Pombe Joseph Magufuli.
MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi nami kuweza kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la barabara katika Wilaya ya Kalambo linafanana na tatizo lililopo katika Wilaya ya Wanging‟ombe; naomba kujua ni lini Serikali itatengeneza barabara ya kutoka Njombe – Iyai inayopita Makao Makuu ya Igwachanya kutokea Mkoa wa Mbeya kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nina uhakika Mheshimiwa Mgaya anakumbuka, wakati mnaipitisha bajeti yetu; na kwa kweli tunashukuru sana mlipoipitisha; katika maeneo ambayo tumeyatengea fedha na tutahakikisha tunayasimamia katika mwaka huu wa fedha, ni pamoja na barabara hii ya Njombe – Iyai na kuendelea. Kuna kiwango cha fedha kimetengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mgaya, nafahamu kwamba unanikumbusha, pamoja na kwamba tuliahidi wakati wa bajeti lakini unaendelea tena kutukumbusha kila wakati ili kwa kutumia njia hiyo ya kurudia kutukumbusha kwamba tutatekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mgaya kwamba, sisi tuliopo Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasilaino tukiongozwa na Mheshimiwa Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, tukiahidi mara moja tunafuatilia utekelezaji. Nami namhakikishia kwamba ataona mwenyewe mwaka huu wa fedha utakapokwisha, ahadi hiyo ambayo ilishatolewa wakati wa kipindi cha bajeti itakuwa imetekelezwa.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja. Kwa kuwa tatizo la Barabara ya Kalambo linakwenda sambamba na tatizo la barabara iliyopo Jimbo la Busokelo Wilayani Rungwe inayotoka pale Tukuyu Mjini kuanzia Katumba – Suma – Mpombo – Isange – Ruangwa – Mbwambo hadi Tukuyu Mjini; na barabara hii imekuwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi zaidi ya miaka 10: Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami Kilometa 73 zilizobaki?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, utakumbuka tulikaa pamoja kati yako wewe, Mheshimiwa Mbunge pamoja na Waziri wangu kuhusu barabara hii. Nilikiri wakati ule na ninarudia kukiri hapa kwamba hatujaitendea haki, kwamba ni ahadi ya muda mrefu sana, lakini tumepanga kujenga Kilometa moja tu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuahidi na Mheshimiwa Mwakibete nilimwahidi kwamba mwaka ujao wa fedha mazingira hayo hayatajirudia. Naomba nirudie ahadi hii sasa hapa, maana yake pale hatukuwa hadharani, leo tuko hadharani.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwanza naishukuru Serikali kwa niaba ya wananchi wa Nzega, Mheshimiwa Profesa Muhongo na Mheshimiwa Kalemani wametekeleza ahadi ya kuturudishia machimbo ya Na. 7 na wiki hii wachimbaji wadogo watakabidhiwa maeneo yao. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza swali moja tu. Mwaka 2005 Rais wa Awamu ya Nne aliwaahidi wananchi wa Wilaya ya Nzega, hasa wa Jimbo la Bukene ujenzi wa kilometa 146 wa Barabara ya kutoka Tabora, kupita Mambali, kuja Bukene, kwenda Itobo, kwenda Kahama na Kilometa 11 kutoka Nzega Mjini kuunganisha mpaka Itobo kuweza kujengwa kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye bajeti ya mwaka 2014/2015 Serikali ilitenga fedha za upembuzi yakinifu na tenda ikatangazwa, Wakandarasi wote walioomba wakawa wame-bid zaidi. Je, Serikali iko tayari sasa kuongeza fedha ili barabara ile upembuzi yakinifu ukamilike na ujenzi uweze kuanza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Bashe kwa kunipa elimu ya kina utofauti kati ya hii barabara anayoongelea ya kutoka Tabora kupitia Mambali – Bukene hadi Kahama na ile ya kutoka Tabora kupitia Nzega Mjini hadi Kahama; ni barabara mbili tofauti na zote zina umuhimu mkubwa kiuchumi katika maendeleo ya eneo lile.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahadi za viongozi wa Kitaifa tumekabidhiwa tuliopo Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kuhakikisha kwamba tunazitekeleza. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika kipindi hiki cha miaka mitano, barabara hii kama ilivyoahidiwa, pamoja na hii nyingine ya kutoka Nzega hadi Itobo tunazishughulikia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa kwa suala lile la kukamilisha feasibility study na detailed design nimhakikishie Mheshimiwa Bashe kwamba tutawataka TANROADS waliangalie upya ili fedha ziongezwe na kazi ile ifanyike, kwa sababu lengo ni kukamilisha kazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kadri tunavyoendelea kuahirisha upatikanaji wa Mkandarasi kwa sababu ya bajeti kuwekwa kiwango cha chini, tutakuwa hatuwatendei haki wananchi wale wanaohitaji huduma ya ile barabara.
MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa barabara hii inatumiwa na magari mengi yanayotoka Meatu, Kwimba, Maswa, Bariadi na hivyo kufanyiwa matengenezo mara kwa mara na kuigharimu Serikali. Serikali haioni kuna haja sasa ya kuanza kuitengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami kwa awamu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa vile madaraja matatu aliyoyataja Mheshimiwa Naibu Waziri yote yako Wilaya ya Kwimba. Kuna daraja moja ukitoka tu Kijiji cha Malampaka na kuingia Wilaya ya Kwimba halijajengwa, je, ni lini sasa hilo daraja nalo litakarabatiwa lipanuliwe ili kuweza kusaidia barabara hii iweze kudumu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mashimba Mashauri Ndaki, Mbunge wa Maswa Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nimepokea ushauri wake na TANROADS wataangalia kama kutakuwa na uwezekano wa kupanua lile daraja pamoja na kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Watakapotoa ushauri wa kitaalam Serikali itazingatia mahitaji hayo.
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ni matarajio yangu makubwa kwamba, Serikali inakuwa na majibu ambayo hayabadiliki kutokana na muda. Swali kama hili nimeliuliza na Serikali ikakiri umuhimu wa barabara hii kwa sababu inaondoa takribani kilometa 100 na wakatutaka tutume ombi maalum. Je, ni lini Serikali itajenga kipande hiki ili barabara hii iendelee kutumika? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wakati aliyekuwa Waziri wa Ujenzi, ambaye ndiye Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alipofika Kalambo kuja kuomba kura tarehe 25/8 akiambatana na Mheshimiwa Lukuvi, alimtaka Mkurugenzi atangaze haraka kabisa ujenzi wa kivuko cha Mto Kalambo kwa sababu ya umuhimu wake. Je, ni lini kandarasi hii itatangazwa ili kivuko hicho kiweze kujengwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali huwa haibadilishi majibu yake na kwa jibu hili, tulimwambia awali kwamba alete ombi maalum, akileta swali jibu lake ambalo kwa kawaida linaletwa na wataalam wanaozingatia maombi na majadiliano yaliyoko mkoani na wilayani yatakuja kama yanavyokuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, hilo ombi likiletwa maalum na kuna utaratibu wa kuleta ombi maalum, linaanzia wilayani, mkoani hadi TANROAD Taifa na hatimaye Serikali ndiyo huwa inaamua. Tukileta maombi kwa kuuliza maswali, tutajibiwa na wataalam kutegemea na taratibu ambazo zimepitia katika mikoa na wilaya hadi wakati huo. Naomba sana Mheshimiwa Kandege kama ambavyo tulimjibu katika jibu letu la awali, alete ombi maalum na Serikali italifikiria kwa utaratibu ule unaotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, naomba tuonane na Mheshimiwa ofisini, tutakuwa na wataalam tuweze kulijadili na hatimaye tumpe majibu sahihi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumepata ahadi zote za Mheshimiwa Rais na tumeziratibu vizuri na sasa tunazifanyia kazi na tutazitekeleza awamu kwa awamu (phase by phase). Ahsante sana.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Anaitwa Mussa Mbarouk, Mbunge wa Tanga Mjini. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kutambua umuhimu wa barabara hii ambayo ina kivutio cha pakee ambacho imeunganika na mbuga pamoja na bahari. Je, Serikali kwa kuendelea kuchelewa kuitengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami, haioni kuwa inapoteza mapato mengi ya kiutalii kutokana na kivutio hiki? (Makofi)
Swali la pili, Wakazi wa Wilaya ya Pangani ambao wako pembezoni mwa barabara ile wamewekewa alama ya “X” nyumba zao, lakini bado wanaendelea kuishi na hawajui ni lini watalipwa fidia zao ili waendelee na maisha yao sehemu nyingine.
Je, Serikali ipo tayari kutoa ahadi kwamba ni lini itawalipa wakazi hawa fidia zao? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano inapotoa ahadi inatekeleza; barabara hii imeanza kufanyiwa usanifu na itakapokamilika maadam tumeshaona mtu anayetoa fedha tayari amepatikana kwa vyovyote vile ujenzi utafanyika kwa haraka itakavyowezekana ili mapato haya ya kitalii yaanze kuingia katika Mfuko wa Hazina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali la pili, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, hizo alama za “X” anazoziona ndiyo sehemu ya utaratibu wa kufanya fidia. Ni hatua ya kwanza, baada ya hapo wanamalizia hatua inayofuata na mara utaratibu wa kufanya uthamini utakapokamilika suala la ulipaji wa fidia litashughulikiwa.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, Mbulu ni Wilaya kongwe, imeanza 1905, sawa na Nairobi. Pamoja na ahadi zilizotolewa kwa muda mrefu na Marais waliyotangulia. Je, kwa kuchelewa kutengeneza barabara hii, huoni kwamba ni kuwadanganya wananchi wa Mbulu na kuwakatisha tamaa?
Swali la pili, kwa kuwa barabara hii ya kwenda Hydom, ipo Hospitali kubwa ya Rufaa ya Hydom ambayo ni Hospitali ya Kanda; na sasa hivi daraja la Enagao limevunjika na wananchi hawezi kwenda kwenye Hospitali hiyo: Je, Serikali haioni kwamba kwa kuendelea kutopitika barabara hii kunaweza kuendelea kupoteza maisha ya watu na wasipate huduma katika hospitali hiyo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kumhakikishia kwamba dhamira ya Serikali kujenga barabara ni kubwa na Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi. Tuna barabara nyingi ambazo kutokana na ufinyu wa fedha, hazijaisha. Namwomba awe na Subira na ninamhakikishia, katika kipindi hiki cha miaka mitano ahadi hii iliyotolewa itatekelezwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa matatizo yanayotokea ambayo yanatokana na hali ya hewa, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba TANROADS wataendelea kutumia fedha za dharura kuhakikisha barabara hizo zinapitika na zinaendelea kuwahudumia wananchi wa maeneo hayo.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, naomba Mheshimiwa Waziri aweze kunithibitishia juu ya kuanza ujenzi huo kwa mwaka 2016/2017, kwa kuwa kwenye vitabu vya bajeti sijaona bajeti iliyotengwa au fedha iliyotengwa kwa ajili ya barabara hiyo.
Swali la pili, barabara ya Lupembe kwa sasa hivi imefungwa, magari yote yanayoanzia tani kumi na kuendelea hayaruhusiwi kuingia, wakati wananchi wa Lupembe, hasa kata nane, wanategemea barabara hii kusafirisha mbao, wanategemea barabara hii kusafirisha nguzo na vifaa vya ujenzi kama mchanga na tofali, sasa hivi imefungwa hawawezi kusafirisha, hivyo kuathiri uchumi wa wananchi hawa. Naomba Serikali iniambie, ni utaratibu gani ambao itauweka kwa sasa hivi ambapo tunasubiri ujenzi wa barabara hii ili wananchi wasiendelee kuathirika kwa uchumi wao?
Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwa swali lake dogo la kwanza, naomba asubiri hotuba ya Waziri wangu wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ili apate tafsiri sahihi ya randama ambayo ameiangalia. Namhakikishia ujenzi huo unaanza mwaka 2016/2017 kama tulivyoeleza katika jibu la swali la msingi.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kuharibika na kukatika kwa barabara hiyo, naomba nichukue fursa hii kuwakumbusha tena TANROADS mikoani wote pamoja na Chief wao, kuhakikisha kwamba barabara zote ambazo zimekatika kutokana na mvua kubwa iliyopita zinafunguliwa, wasimamie suala hilo ili wananchi waendelee kupata huduma ya usafiri na maisha yaendelee kama kawaida.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa, Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliahidi kujenga barabara ya lami kilometa 1.5 katika Mji wa Mombo na Rais wa Awamu ya Tano ameahidi vilevile kujenga barabara hiyo kilometa moja, lakini cha kushangaza mpaka leo hii hela hazijaingia katika Mfuko wa Mkoa. Je, ile barabara ambayo imeahidiwa na Marais wawili itajengwa lini kwa kiwango cha lami kule Mombo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia kwamba ahadi za viongozi wetu, Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne na Rais wa Serikali ya Awamu ya Tano, tuliopewa dhamana tutaitekeleza.
MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Spika, kwanza kwa masikitiko makubwa nasikitishwa sana na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Spika, hii Serikali inajiita ni Serikali ya hapa kazi tu na kila siku imekuwa ikija na majibu mepesi kwa maswali mazito. Wamiliki wa mabasi ambao ni wananchi wa kawaida wenye uwezo wa kawaida wana uwezo wa kuwa na mawakala katika Wilaya mbalimbali nchini, Serikali ya Chama cha Mapinduzi inashindwaje kuwa na mawakala ili kusaidia wananchi waweze kuzipata tiketi hizi kwa urahisi? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa sababu mtu anatoka Kasulu, mtu anatoka Kibondo, mtu anatoka Ilagala anatumia sh. 10,000, sh. 8,000, sh. 7,000, anakwenda na kurudi, anakaa saa kumi usiku mpaka nne asubuhi, tiketi zinaanza kuuzwa na anakosa tiketi anarudi kijijini. Hizo gharama kwa mwananchi anaziona ni ndogo kuliko Serikali kuweka mawakala katika maeneo husika?
SPIKA: Sasa swali!
MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Spika, swali ni kwamba anaona gharama ya Serikali kuweka mawakala katika Wilaya husika ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa usafiri ni kubwa kuliko gharama wanazozipata wananchi kuamka saa kumi ya usiku na kukosa tiketi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, …
SPIKA: Hee! Bado!
MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Spika, bado, hilo ni swali la kwanza. Swali la pili, amekiri kwamba kuna ulanguzi wa tiketi. Tiketi ya daraja la tatu ambayo inauzwa sh. 24,000 katika soko la ulanguzi inauzwa sh. 35,000 mpaka sh. 40,000. Daraja la pili kwa bei ya sh. 56,000 inauzwa sh. 75,000 mpaka sh. 85,000 na daraja la kwanza kwa bei ya sh. 76,000 inauzwa sh. 100,000 mpaka sh. 110,000. Je, Serikali, ni lini sasa mtaondoa kero hii na kutoa ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ulanguzi wa tiketi ulikuwa kwa kiwango kikubwa sana kabla ya utaratibu huu ambao Serikali tumesema tumeubadilisha haujafanyika, baada ya utaratibu huu kufanyika tatizo hili la ulanguzi wa tiketi sasa halipo kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Spika, kuhusu gharama ambazo wananchi wanazipata tutaangalia uwezekano mwingine, badala ya kuanzisha wakala, tutaanzisha huduma ya wateja katika stesheni ile ile, upate uhakika wa tiketi kabla hujakwenda stesheni kulipa fedha na tunakokwenda TRL itaanzisha huduma ya kutoa tiketi ukiwa nyumbani huko kwa kutumia simu. Hatutaleta mawakala kwa
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
22
sababu kuleta mawakala kunaongeza gharama zaidi kwa TRL na vilevile ni gharama kwa uchumi.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu suala la…
SPIKA: Umesikia Mheshimiwa Sabreena, Serikali hii ya hapa kazi tu inaleta digital! Mheshimiwa Waziri endelea! (Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, namhakikishia kwamba tukishaanzisha utaratibu huo, hilo tatizo la pili ambalo analiongelea halitakuwepo tena.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri. Kwa kuwa barabara iliyotajwa ya kuunganisha Mbeya na Makete bado imechukua muda mrefu na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ana mpango wa kwenda Mkoa wa Njombe, haoni sasa kuna sababu kubwa ya kupita na kuangalia, kutokana na majibu aliyojibu kuona kama kweli itajengwa kwa wakati ambao ameahidi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa barabara hizi zipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, ikiwemo hii ya kuunganisha Wilaya ya Kilolo na Iringa Mjini. Je, haoni sasa ni muda muafaka wa kufika na kutembelea barabara ambayo inaanzia Ipogolo – Ndiwili - Kilolo ambayo kwa miaka saba imejengwa kilometa saba na kilometa zilizobaki ni 28, haoni kwamba itachukua miaka 28 pia kumalizia hicho kipande kilichobaki?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nitakagua kama ambavyo amependekeza ili kuthibitisha kwamba eneo hilo tunalokusudia kulijenga kweli litajengwa.
Pili, kuhusu barabara ya kutokea Kilolo hadi Iringa, ni barabara ambayo ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020 na hata hiyo barabara nyingine nayo ni sehemu ya Ilani. Namhakikishia, barabara zote zilizopo ndani ya kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi tutazishughulikia na kuzikamilisha kwa awamu kadri tutakavyokuwa tunapata uwezo mwaka hadi mwaka.
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, kwa kuwa matengenezo aliyosema Mheshimiwa Naibu Waziri yalihusu kukwangua tu na kusawazisha barabara, badala ya kuweka kifusi na kushindilia, hali ambayo imesababisha mvua kidogo tu iliyonyesha, tatizo la mashimo kurudi pale pale. Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hiyo, kwa kuweka kifusi na kushindilia ili iwe imara kabla hata ya lami? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye bajeti iliyosomwa jana, imepangiwa shilingi bilioni 120 kujengwa kwa lami kuanzia mwakani, ambayo ni asilimia 17 tu ya mahitaji yote ya fedha yanayohitajika. Pia Mheshimiwa Waziri hajajibu swali langu la mwisho sehemu (c); Je, ni lini barabara hiyo itakamilika kwa kiwango cha lami?
Naibu Spika, wakati mvua inanyesha, suala la kuweka kifusi nadhani lisingekuwa muafaka, kwa sababu ukiweka kifusi kitaharibu zaidi badala ya kujenga. Hivi sasa mvua kwa kuwa imekwisha suala sasa la kuimarisha kikamilifu hiyo barabara litafuatia.
Mheshimiwa Naibu Spika, utakumbuka kwamba nilishatoa maelekezo kwa Mameneja wote wa Mikoa sasa kuelekeza nguvu zao kufungua barabara zote nchini ambazo zilijifunga.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, namwomba Mheshimiwa Mbunge akiri kwamba hiki kiasi ambacho amepangiwa, kinatosha ukilinganisha na mahitaji makubwa ya Waheshimiwa Wabunge wengi humu ndani.

WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nami niongezee baada ya majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Barabara hii inafadhiliwa au inajengwa kutokana na pesa za Benki ya Afrika (ADB).
Kwa kawaida, barabara hii tutaigawa kwenye lots mbalimbali kwa sababu ni barabara ndefu sana. Kwa kawaida barabara hii kuanzia mwakani inaweza kuchukua baina ya miaka mitatu mpaka miaka minne, itakuwa imekamilika, itategemea hali ya hewa inavyokwenda.
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Spika, ahsante nimepokea majibu bahati nzuri naifahamu sana hii yote.
Kwa kuwa kwenye kikao cha RCC Mkoa tulipewa taarifa hiyo kwamba fedha hizo kweli za barabara ya Kidatu - Ifakara ina ufadhili wa USAID; nilitaka kujua sasa, mkandarasi huyu inachukua muda gani kwa sababu hela ipo tayari. Kwa hiyo, ili kumpata mkandarasi wa kuanza ujenzi barabara hiyo ningependa kupata majibu ya Serikali inachukua muda gani ili wananchi wa Kilombero wajue hii barabara inaanza kujengwa lini kwa kuwa hela ipo na upembuzi umeshafanyika? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, mbili; kwa kuwa ujenzi wa daraja la Kilombero ulianza tarehe 21 Januari, 2013 na mimi nilienda kwenye uzinduzi wa ujenzi wa daraja hilo na ahadi ya Waziri wakati huo kwa wananchi waliambiwa ujenzi wa daraja utamalizika mwaka 2015. Leo mnasema Disemba, 2016. Kwa kuwa wafanyakazi wanaofanya kazi katika lile daraja walitoa taarifa kwangu na kwa Peter Lijualikali kwamba kule chini kuna crack jamani, je, kwa taarifa hizi ambazo wafanyakazi wapo na unasema daraja linaendelea vizuri ingawa si kweli sio asilimia 50, je, Serikali iko tayari sasa kwenda kufanya utafiti lile daraja kabla halijaenda mbali zaidi tuangalie...
SPIKA: Mheshimiwa Susan Kiwanga swali!
MHE. SUSAN L. KIWANGA: Madhara yanayoweza kujitokeza katika daraja hilo kabla ya kuendelea?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, tulieleza tarehe 27 Januari, wakati Mheshimiwa Peter Lijualikali alipouliza swali la nyongeza kuhusiana na hilo hilo kwamba tulilazimika kubadilisha muda kutokana na upatikanaji wa fedha. Hatuna namna, fedha hazikupatikana, kwa hiyo, hilo suala tunalikamilisha kadri fedha zitakapokuwa zinapatikana. Kwa hiyo, kwa upande wa USAID ni kweli fedha zipo utaratibu wa kumpata mkandarasi ni lazima tuufuate kwa sababu tukiwaharakisha hata USAID wenyewe hawatatoa hizo fedha. Kwa hiyo, naomba tuvumiliane taratibu za ki-procurement zikamilike kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa suala la pili mimi naomba tu nimjulishe kwamba katika Wizara ambayo ina wataalam ni pamoja na sekta ya ujenzi. Naomba aamini suala hilo analoliongelea la crack ni la kitaalam, naomba tuwaachie wataalam na kwa mujibu wa wataalam wanaosimamia pale kazi ya ujenzi wa daraja hili itakamilika mwezi Disemba, 2016.
MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Spika, namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri. Lini sasa kauli ya Serikali hiyo barabara kipande cha kilometa 48 kitakamilika?
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la awali kwamba tunatafuta fedha ili kuanza kujenga barabara hii na mara tutakapopata fedha tutaanza kujenga barabara hii. Kutaka commitment ya Serikali kuhusu lini tutamaliza nadhani ni mapema mno. Naomba wananchi watuvumilie na Mheshimiwa Mbunge mtuvumilie tukipata fedha tutaanza kujenga na tutawajulisha wakati huo lini tutaweza kukamilisha.
MHE KHALIFA MOHAMMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na jawabu refu sana la Mheshimiwa Naibu Waziri, bado nina maswali mafupi mawili ya nyongeza. Swali la msingi lilikuwa ni risk, kuweka rehani roho za abiria. Hii haijalishi ukubwa wa ndege, ubebaji wa abiria wachache au wengi. Jawabu ilikuwa rubani kabla ya kurusha ndege, au vipindi kwa vipindi wanafanyiwa check-up.
Mheshimiwa Naibu Waziri, haoni binadamu katika maumbile yake unaweza kumfanyia check up sasa hivi lakini akifika pale hali yake ikawa na mgogoro. Je, haoni kwamba bado suala ni kuweka rehani roho za abiria?
Swali la pili, pamoja na treaties nyingi za Kimataifa na kuridhiwa na Bunge, je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kulisimamia hili na kukawa na ulazima maalum wa ndege yoyote ya abiria kuweza kuongozwa na rubani zaidi ya mmoja?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, risk inapimwa. Katika eneo hili sheria tulizo nazo za kimataifa ambazo nchi yetu imeziingiza katika sheria zetu na Bunge hili limeidhinisha, hiyo risk imepimwa kwa uzito wake na ndiyo maana ni aina fulani tu za ndege zinazobeba abiria kiwango fulani zinazoruhusiwa kuendeshwa na rubani mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, kuna marubani maalum wanaoruhusiwa kuendesha ndege usiku na wakati ambapo huwezi ukaona uwanja ulivyo, ni aina fulani tu ya marubani ambao wamepitia kozi maalum zinazozingatia leseni za IFR (Instruments Flights Rules). Ndege zile ambazo zinatumia CFR ambazo ni kwa marubani ambao hawaja-qualify sana hazihitaji masharti hayo na kwa kawaida hawaruhusiwi kuendesha usiku au kwenye kipindi ambacho mawingu ni mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa suala la afya, ambalo ndilo swali lake la msingi Mheshimiwa Mbunge, nadhani ukiweka hata marubani watatu, wanne, Mwenyezi Mungu kama afya hiyo hakubali nadhani siyo solution na ndiyo maana upimaji wa kila mwaka na kwa wale ambao wanarusha ndege za kimataifa za kibiashara upimaji wa kila baada ya miezi sita ni wa lazima. Ndugu zangu niwaambie, na niwaombe Wabunge wote tupime afya zatu. Tukiwa tunapima afya zetu kila wakati risk ya kupata labda pressure au nini ni ndogo sana. Wataalam wetu wanaotupima tuwaamini.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, hii barabara ni ya muhimu sana na ni ya miaka mingi sana na bahati nzuri sana hata Naibu Waziri wa Ujenzi mwaka 2015 alifika kule Mufindi na alifanya mikutano miwili na aliwaambia wananchi kwamba, baada ya kumaliza uchaguzi hii barabara itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kufuatana na umuhimu wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapoongelea viwanda, viwanda kule tayari viko, kuna kiwanda cha Kibwele pale, kuna kiwanda cha Kilima Factory, kuna kiwanda cha Lugoda factory, hivi ni Viwanda vya Chai na vinategemea hii barabara. Mheshimiwa Waziri aniambie kwa sababu upembuzi yakinifu walishamaliza na Serikali iliahidi na Chama cha Mapinduzi kimeahidi kwamba kitaweka kiwango cha lami. Ni lini hizi fedha zitapatikana na wataanza kujenga kwa kiwango cha lami?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi walishaambiwa tayari kuna nyumba zao zilishawekewa alama ya X na wanatarajia kuhama! Je, Serikali ni lini itaenda kutoa fidia kwa wale ambao walijenga nyumba jirani na barabara na Serikali ilisema itawalipa fidia kwa mfano, wananchi wa Kijiji cha Nzivi, Igowole, Kibao, Mtwango na pale Lufuna, kuna nyumba ziliwekewa X, Serikali itaenda kuwalipa lini ili waanze kuhama?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii. Tunapoongelea ujenzi ni pamoja na fedha za fidia pamoja na fedha za ujenzi wenyewe. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kama ambavyo barabara hii ipo katika ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015/2020, namhakikishia ahadi hiyo itatekelezwa, asiwe na wasiwasi!
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa tatizo la barabara lipo nchi nzima na katika Jimbo letu la Pangani pia tatizo hili la uharibifu wa barabara limekuwa ni sugu. Licha tu ya barabara inayounganisha Wilaya ya Pangani na mikoa mingine kuwa mbovu, lakini pia barabara zinazounganisha vijiji na vijiji zimekuwa mbovu kiasi ambacho kipindi cha mvua hazipitiki kabisa. Je, Serikali ina mpango gani sasa kuhakikisha barabara zile zinapitika kipindi chote cha mwaka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yangu itahakikisha ubora wa hizi barabara unaongezwa na unaimarishwa na tutaweka mipango maalum kuhakikisha magari makubwa ambayo mara nyingi ndiyo yanayoharibu barabara hizi hayataruhusiwa kupita katika barabara ambazo haziruhusu kupita magari yenye kiwango fulani cha tonnage.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sana nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara hii anayoiongelea iko katika Ilani yetu na tutaendelea kuiimarisha na nichukue fursa hii kuwaomba au kuwaelekeza TANROADS, Mkoa wa Tanga kuhakikisha kwamba, kama ambavyo tuliwapa maelekezo kufungua barabara zingine na hii wahakikishe inafunguliwa na maeneo hayo yote yaliyoharibika yatengenezwe.
MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu yenye kukatisha tamaa, naomba kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa mpango wa kujenga kwa lami inaonekana haupo kwa sasa na kwa kuwa barabara hizi mbili zinatengenezwa vipande vipande kila wakati na kuleta usumbufu kwa wananchi wetu: Je, sasa Serikali iko tayari kujenga kwa kiwango cha changarawe barabara nzima badala ya vipande vipande?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Kadutu kwa uamuzi huo ambao naweza kuuita wa kihistoria wa kurudi nyuma. Ila namwomba sana Mheshimiwa Kadutu, tunapojenga vipande vipande, hatimaye tutakamilisha.
Nami siamini kama wananchi wa Ulyankulu watapenda barabara hii ibakie katika kiwango cha changarawe.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, kwa namna anavyotusumbua ofisini, maana yake nimeambiwa na Waziri wangu jinsi alivyokuwa anapoteza muda wake pale Dar es Salaam kwa ajili ya kufuatilia ujenzi wa barabara hii. Namhakikishia kile ambacho tulimwambia ofisini tutakitekeleza. Atupe fursa ya kujenga vipande vipande hadi itakapokamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza hii barabara ipo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015/2020 na namhakikishia katika kipindi hicho tutatekeleza ahadi hiyo ya Chama cha Mapinduzi kama ilivyoahidiwa.
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara hii inaunganisha Mikoa ya Katavi - Tabora na Mkoa wa Shinyanga ikianzia Mpanda – Ugala – Kaliua - Ulyankulu katika Jimbo langu la Ushetu na hadi Kahama Mjini; na kwa kuwa ipo katika mpango na kwa mwaka wa fedha 2016/2017 imetengewa fedha kwa ajili ya feasibility study na detailed design; na kwa kuwa barabara hii katika hatua za awali…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa fupisha swali lako tafadhali.
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Kwa kuwa inasimamiwa na Meneja wa TANROAD, Mkoa wa Katavi; je, kwa nini Mameneja wa Mikoa mingine hawahusiki katika usimamizi na utaratibu huu ukatumika katika hatua za ujenzi wa lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba Mheshimiwa Kwandikwa tukutane ofisini tulijadili kwa undani ili majibu ambayo tutampa yawe na uhakika na yatakayotekelezeka.
MHE. MGENI JADI KADIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara ya Tanga daraja la Wami ni jembamba mno, magari mawili hayawezi yakapishana kwa wakati mmoja; hata juzi tu gari la maiti liliwahi kutumbukia: Je, Serikali ina mpango gani wa kulipanua daraja hilo?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani Mheshimiwa Mbunge atakumbuka, tulipokuwa tunaongelea bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kati ya miradi tuliyoongelea ni upanuzi wa daraja la Wami. Kwa hiyo, naomba kumhakikishia, kwa kuwa mmetupa fedha, tutatekeleza kile ambacho kipo katika bajeti yetu.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nimwulize Naibu Waziri maswali mawili ya nyongeza kutokana majibu yake kuwa marefu sana.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa bandari bubu zipo mipakani; vyombo vya ulinzi na usalama huwa vinakutana na changamoto kwenye bandari hizi. Je, Serikali mnatambua kama vyombo hivi vinakutana na changamoto kubwa kudhibiti silaha na hata magendo? Mna mpango gani kuongezea vyombo vya ulinzi na usalama, stahiki zao na hata vifaa vya utendaji kazi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa majahazi ndiyo yanayotumika kufanya sana uhalifu, kubeba madawa ya kulevya na hata kutorosha bidhaa haramu kama pembe za ndovu: Je, Serikali mna mikakati gani kukagua majahazi na kudhibiti vyombo hivi vya majahazi ndani ya bahari na ukaguzi wa mara kwa mara?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuna sheria na taratibu zinazotumika katika kulipa vyombo vya dola. Nimechukua wazo lake na tutawasiliana na Wizara mbalimbali ikiwa ni pamoja na Idara Kuu ya Utumishi pamoja na Wizara yenyewe ya Mambo ya Ndani ili tuangalie kwa pamoja uwezekano wa kuboresha kile ambacho sasa hivi kipo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, limefanana na hili la kwanza ingawa limeulizwa kwa namna nyingine. Namhakikishia kwamba vyombo hivi vya ulinzi na usalama vinatekeleza wajibu wake kwa umakini sana na namhakikishia kwamba tutaendelea kudhibiti kama ambavyo sasa hivi tumekamilisha kudhibiti katika eneo hili la mwambao wa Bahari ya Hindi na tumeamua bandari hizo ambazo nimezielezea katika swali la msingi zirasimishwe na tutahusisha halmashauri husika katika kuendelea kudhibiti na kukusanya mapato.


NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri ameyatoa, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, naomba kuongezea majibu hayo kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba vyombo vya usalama vinakabiliwa na changamoto nyingi wakati wa kukabiliana na wahalifu hawa wa magendo pamoja na uhalifu mbalimbali wa madawa ya kulevya, biashara haramu, wahamiaji haramu na kadhalika. Miongoni mwa changamoto hizo si tu kwamba vitendea kazi ni changamoto lakini pia hali ya hewa na masafa marefu ya kuelekea kwenye kina cha maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hatua ambazo tumechukua mpaka sasa hivi, kwanza kabisa tunajaribu kupata taarifa za kiintelijensia ili kazi ya kuweza kufanya operation iwe rahisi pale ambapo taarifa za uhakika tumezipa. Hii tunashirikiana vizuri sana na wananchi pamoja na jamii za maeneo husika. Lingine ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kuimarisha vitendea kazi hivi hasa speed boat kwa kadiri hali ya bajeti itakavyokuwa inaruhusu.
mimi nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kutoa majibu mazuri juu ya barabara hii ya Njombe - Makete, lakini pamoja na barabara hii ya Njombe - Makate ndani ya Mkoa wa Njombe tuna barabara nyingine zinazounganisha na Mkoa; iko barabara ya Itoni - Ludewa inayopitia kwenye kata za Uwemba, kata ya Luponde, kata ya Matola. Na sasa hivi kule Ludewa wanaanza kulipa fidia kwa ajili ya kuanza uchimbaji wa madini, barabara hii imekuwa ikiharibika sana haioneshi kwamba kuna fedha inayotosheleza kujenga hii barabara. Je, Mheshimiwa Waziri anatuambiaje sisi wana-Njombe juu ya barabara ya Ludewa - Njombe?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge, alishiriki katika kuipitisha bajeti ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, na anafahamu katika bajeti hiyo tuliongea kabla na tukahakikisha tunatenga kilometa 50 za kujenga katika mwaka huu wa fedha. Na kwa sababu, bajeti imeshapitia nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kazi yetu ni moja tu, kutekeleza eneo hilo ambalo bajeti imeipitisha.
MHE. AYSHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Barabara ya Njombe - Makete haina tofauti na barabara ya Manyoni - Itigi.
Swali, je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara kilometa mbili zilizobaki kutoka njia panda inayokwenda Tabora na ile inayokwenda katikati ya Halmashauri ya Mji Mpya wa Itigi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anakumbuka katika Bunge hili hili tumejibu maswali mbalimbali na maswali ya nyongeza kuhusiana na kile kipande kidogo cha kilomita 8.3 cha kutoka Njia Panda hadi Itigi, Makao Makuu ya Halmashauri mpya. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kile ambacho tulieleza wakati tunajibu swali hili hapa Bungeni; kwamba tutakapojenga ile barabara inayokwenda mpaka Rungwa, mpka Makongorosi kipande hiki kitajengwa, na unafahamu kwamba tumeshatenga fedha katika kutekeleza suala hili.
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya Makambako - Njombe - Songea, ilijengwa tangu mwaka 1984, na sasa ina hali mbaya sana kila siku inawekwa viraka lakini hali imekuwa ni mbaya sana.
Je, ni lini Serikali itajenga barabara ile upya ili kuwahudumia watu wa Mkoa wa Ruvuma na Njombe kwa ujumla?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Makambako hadi Songea na hususani Njombe hadi Songea imetengewa bajeti ya kufanyiwa ukarabati katika mwaka huu wa fedha. Na mimi nimhakikishie ukarabati huo utakaofanyika tutahakikisha ile kampuni itakayopewa kazi hiyo ya kufanya ukarabati inafanya kwa kiwango ambacho barabara hiyo inakuwa imara na kutumika kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mpakate na Wabunge wote wanahusika katika barabara hii, ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Leonidas Gama ambaye alinisumbua sana ofisini kuhakikisha kwamba hili eneo linakaa vizuri ili anapopita kule asipate matatizo anayoyapata sasa. Namhakikishia na wengine wote kwamba tutahakikisha mkandarasi atakayepata kazi hii ya ujenzi ambayo bajeti mmeshaipitisha anajenga kwa kiwango kinachotakiwa.
MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Mimi nilitaka kujua kuhusu kipande cha barabara kutoka Kibondo kwenda Mabamba kilometa 45 ambacho Mheshimiwa Waziri alizungumza kwamba kitajengwa kwa kiwango cha Lami. Lakini katika vitabu vyake vya bajeti imetengewa milioni 80, hiyo ni kwa ajili gani? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Kibondo hadi Mabamba ilitolewa ahadi na viongozi wetu, ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Na mimi naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi hii tutaitekeleza na wala asiwe na wasiwasi. Fedha tulizozitenga za shilingi milioni 80 anazoziongelea ni kwa ajili ya ukarabati mdogo mdogo si kuanza ujenzi. Ujenzi wa kipande hiki tutaufanya kadri uwezo wa kifedha tutakapokuwa tunajaliwa.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ameelezea kwamba katika hivi viwanja vya ndege kuna wheel chairs na stretchers, lakini swali langu la msingi lilihoji kwa habari ya ambu-lift. Ukisema wheel chair inamsaidia tu yule mhitaji kumpeleka mpaka eneo la ndege, lakini anapofika pale inabidi abebwe juu juu na wale staff wa airport kitu ambacho kinakuwa ni very risk!
Mheshimiwa Naibu Waziri, kutokana na umuhimu wa ambu- lift, ni nini commitment ya Serikali kuhusiana na uwepo wa huduma hii katika viwanja vyote vya ndege nchini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana naye kwamba ambu-lift ndiyo kifaa kinachohitajika zaidi na chenye usalama zaidi kuliko hivyo vingine. Kama nilivyojibu katika jibu langu la nyongeza, Wizara yangu itahakikisha wale wanaotoa huduma kwa maana ya uwanja wa ndege wa Mwalimu Nyerere, tunawaongelea Swissport, na ninawataka Tanzania Airport Authority nao wahakikishe wanaongeza huduma hiyo ya ambu-lift katika kiwanja cha Mwalimu Julius Nyerere International Airport pamoja na Kilimanjaro, Songwe na viwanja vingine.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WATU WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niseme natambua majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Ujenzi. Niongezee tu mambo machache kuhusu huduma kwa watu wenye ulemavu katika viwanja vya ndege na maeneo mengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Sheria Na. 9 ya mwaka 2010 ilifuta sheria za zamani zilizokuwa zinazungumzia masuala ya watu wenye ulemavu, na moja ya mambo ambayo yameelezwa wazi katika sheria mpya hii ni kutambua suala la kufikika kirahisi na kupata huduma mbalimbali kirahisi kwa watu wenye ulemavu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria hii ilianza kufanyakazi mwaka 2012 na ni wazi kwamba katika kipindi ambacho sheria hii imeanza kufanya kazi yapo, majengo na ipo miundombinu mingi sana ya Serikali ambayo kwa namna moja au kwa namna nyingine ilikuwa imejengwa kizamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, commitment ya Serikali kuyabadilisha ipo, lakini hili ni suala ambalo litachukuwa muda na Ofisi ya Waziri Mkuu itakuwa inawasiliana na Wizara nyingine kadri inavyowezekana kuhakikisha kwamba taasisi zote za Serikali katika nyanja mbalimbali, elimu, afya, miuondombinu na kadhalika, zinachukuwa hatua zinazofaa ili kuhakikisha kwamba watu wenye ulemavu wanapata huduma stahiki, kokote wanakokwenda.
MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa barabara inayozungumzwa hapa kujengwa kwa kiwango cha lami ni Bigwa - Kisaki na siyo Bigwa - Mvuha ambayo ni sehemu tu ya barabara hii; na kwa kuwa Serikali inazungumzia ufinyu wa bajeti pamoja na kupatikana kwa fedha ndipo ujenzi kamili wa barabara hiyo uanze:-
Je, Serikali ipo tayari kuruhusu ujumbe wa wananchi wa Morogoro Vijijini ukiongozwa na Wabunge wao wa Jimbo la Morogoro Kusini na Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki ili waweze kwenda kumwona Mkuu wa Nchi na kufikisha kilio chao na ikiwezekana waweze kujua kwa nini wafadhali wa MCC II ambao walipangiwa kuutekeleza mradi huu wameuacha na sasa unawaadhibu wananchi wa sehemu hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa madaraja yaliyotajwa hapo hususan daraja la Ruvu, Mvuha pamoja na Dutuni yanahatarisha sana maisha ya wananchi wanaopita humo barabarani kwa kutumia madaraja hayo:-
Je, Serikali itafanya mara moja matengenezo ya haraka ya kuwawezesha wananchi kupita kwa usalama? Naomba kauli ya Serikali, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Prosper Joseph Mbena, aliyekuwa Msaidizi wa Rais wa Awamu ya Nne, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kumwona Mheshimiwa Rais, nadhani anafahamu utaratibu kwamba anahitaji kuwasiliana na Viongozi wa Mkoa na kadiri Mkoa utakavyoona kutokana na hoja zitakazoongelewa hilo linaweza kufanyika. Kikubwa ninachomweleza, niliyomjibu hapa ni dhamira ya dhati za Serikali. Kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, barabara hii ya kutoka Bigwa hadi Kisaki, tutaijenga kwa kiwango cha lami kama tulivyoahidi katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi. Kama ambavyo Viongozi wetu Wakuu wakati wa kampeni na wakati wa misafara mbalimbali wameahidi, tutaitekeleza katika kipindi hiki cha miaka mitano na tunaanzia na nusu yake kutoka Bigwa -Mvuha. Tayari ma-consultant wanafanya kazi tarehe 30 Juni wanakamilisha na baada ya hapo tutaanza kutafuta fedha kujenga hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali lake la pili, ni kama nilivyojibu katika swali la msingi kwamba TANROADS Morogoro wataendelea kuyaimarisha madaraja hayo na kuyafanyia matengenezo ili yaweze kupitika kwa usalama wa wananchi wa maeneo hayo.
MHE.DKT. PUNDECIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali yetu ina lengo jema la kuunganisha barabara za mikoa ili kuharakisha maendeleo katika nchi yetu yote; na kwa kuwa ujenzi wa barabara nyingi umekuwa ukikumba nyumba nyingi zinazokuwa pembezoni mwa barabara ambazo zinawekewa „X’ kwa mfano, kutokea Ilalangulu kwangu kule mpaka Kasansa na fidia mara nyingi wanatathmini pale ambapo pesa zinakuwa hazijapatikana lakini pindi zinapopatikana wanakuja kuwalipa wananchi fidia ile ya mwanzo:-
Je, Serikali inasema nini kufikiria namna ya kutathimini upya fidia za wananchi mara ujenzi unapoanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria ya Fidia ile ya zamani na hata ya sasa ya mwaka 1999 imeeleza wazi kwamba baada ya kufanyiwa tathmini na kama fidia itachelewa kulipwa kuna penalty zimewekwa. Kwa hiyo, malipo yanalipwa zaidi na kuna utaratibu, malipo yanaongezeka kwa kadri muda unavyoongezeka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani hiyo sheria tuliiweka kwa makusudi kabisa tukijua wakati mwingine uwezo wa Serikali wa kulipa kwa pamoja ni mdogo, maana miradi mingi inaihusu Serikali. Kwa hiyo, katika kuwafidia wale ambao wanacheleweshwa kulipa, kuna utaratibu huo wa kufanya mahesabu mapya kwa kuzingatia kipindi ambacho amecheleweshwa kulipwa. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge hili litatekelezwa pindi tutakapoanza kupata nguvu ya kulipa fidia katika eneo husika.
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami naomba niulize swali la nyongeza ambalo linalingana kabisa na lile la Morogoro Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za kutoka Njombe – Mdandu - Iyayi na kutoka Njombe - Lupembe -Madeke, zilishafanyiwa upembuzi na usanifu miaka miwili, mitatu iliyopita:-
Je, ni lini sasa barabara hizi zitaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Sanga kama ilivyo kwa Mheshimiwa Prosper Mbena pamoja na Mheshimiwa Dkt. Kikwembe ni wafuatiliaji sana wa masuala haya ya barabara na fidia katika maeneo yao. Nawapongeza sana kwa hilo na nawaomba waendelee na juhudi hizo kwa sababu kwa kufanya hivyo wanatuunga mkono sisi tulio katika Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambayo dhamira yetu pekee ni kuwajengea wananchi miundombinu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambazo ameziongelea Mheshimiwa Sanga katika bajeti ambayo wameshaipitisha kuna mafungu ambayo yametengwa kwa ajili ya kuanza kujengwa kwa lami. Namhakikishia Mheshimiwa Sanga kwamba katika zile fedha zilizotengwa katika barabara hizo mbili, ikiwa na ile ya kwenda Madeke na hii ya kwenda Iyayi tutazisimamia kuhakikisha zinaanza kutumika kujenga barabara hizo kwa kiwango cha lami kama ambavyo viongozi wetu wa kitaifa waliahidi.
MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Manyoni kuna barabara ya kutoka Manyoni kwenda Sanza. Tatizo la Mto Sanza ni sawa kabisa na tatizo lililoko kule Morogoro Kusini. Daraja hili ni kubwa, linaunganisha Manyoni na Dodoma kwa jirani yangu Mheshimwa Badwel. Daraja hili lilijengwa mwaka 2014 na kukamilika lakini mwaka 2015 mvua iliponyesha likabomoka na sina mawasiliano na jirani yangu hasa wakati mvua zikinyesha:-
Je, ni lini Serikali itatujengea daraja hili?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge ambaye ni kati ya Wabunge wa Mkoa wa Singida walio…
MHE. DANIEL E. MTUKA: Manyoni Mashariki.
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Wa Mkoa wa Singida, Jimbo la Manyoni Mashariki ambaye ni makini kama walivyo Wabunge wengine katika kufuatilia masuala ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nami kwa kweli nichukue nafasi hii kumpongeza kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia mahitaji ya wananchi wa Manyoni Mashariki. Kwa kweli huwa anaenda mbali zaidi, anafika hata maeneo ya Bahi yale ambayo yanaungana na maeneo yake na Manyoni Magharibi, yeye pamoja na Mheshimiwa Mama Mlata. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana na kwa kweli nawapongeza sana kwa juhudi hizi zote wanazozifanya. Nawaombeni muendelee kutuunga mkono katika dhamira yetu ya kuwajengea Watanzania miundombinu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, hivi ninavyoongea CEO wa TANROADS Taifa, Ndugu Patrick Mfugale, ananisikia na atahakikisha anawasiliana na wasaidizi wake wa mikoa hii miwili; Dodoma na Singida ili waweze kuangalia hili eneo ambalo kwa taarifa ya Mheshimiwa Mbunge mawasiliano yamekatika. Nilisema kwamba baada ya mvua kukatika, mkazo wetu mkubwa kwa sasa ni kurudisha mawasiliano katika maeneo yale yaliyokatika. Kwa hiyo, eneo hili ni mojawapo kama ambavyo amelisema; hao viongozi wa TANROADS nawataka walishughulikie haraka sana ili warudishe mawasiliano na wananchi waendelee kupata huduma za usafiri.
MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika majibu ya msingi ya Mheshimiwa Waziri hayajaonyesha ni muda gani ambao pesa inayotafutwa na Serikali itapatikana. Naomba sasa atoe ufafanuzi wa kutosha ili wananchi wa Nachingwea waweze kujua pesa hii ambayo kimsingi inatakiwa ikae kwenye bajeti, ni wakati gani au ni muda gani ili iwe ni rahisi kwangu kufuatilia kujua barabara hii itajengwa lini ukizingatia upembuzi yakinifu ilishafanyika?
Swali la pili, Mheshimiwa Waziri, naomba nipate vigezo vinavyotumika vya ku-allocate pesa katika barabara zetu kwa kiwango cha lami na ukizingatia barabara ya Nachingwea ni barabara kongwe na ya muda mrefu lakini bado haijatengewa pesa kwa muda huu wote ambao tulitazamia tayari itakuwa imepata pesa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi fedha tunatafuta na tunaposema tunatafuta ni kweli tunatafuta. Kwa hiyo, kumjibu ni lini ujenzi utaanza au hizo fedha zitapatika, nafahamu juhudi zake, ameshakuja Wizarani kuhusu hiyo na kwa sababu ya juhudi zake, tumeshatenga shilingi bilioni moja fedha za ndani kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kujenga hiyo barabara kwa maana ya kuandaa documents. Natambua jinsi anavyokerwa na barabara hiyo, na mimi ninamhakikishia mara tutakapopata fedha tutamjulisha lini tutaanza kujenga.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu vigezo, ninamuomba Mheshimiwa Mbunge, atambue kwamba kitu cha kwanza kigezo chetu kikubwa ni Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi na katika kitabu kile cha Ilani, kuna barabara zote ambazo tumeahidi tutazijenga, tumeziweka mle ndani. Kwa hiyo, kigezo kikubwa ni hicho, lakini vilevile ahadi za viongozi wetu Wakuu kuanzia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyepita wa Serikali ya Awamu ya Nne na huyu wa Serikali ya Awamu ya Tano, pamoja na viongozi wengine akiwemo Makamu wa Rais. Hivyo ndivyo vigezo tunavyovitumia katika kupanga barabara ipi ishughulikiwe na kwa wakati gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, akitaka maelezo zaidi, namkaribisha Mheshimiwa Mbunge aje ofisini, akutane na watalaam ili tuweze kulichakata hilo na likafahamika kwa undani zaidi.
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala hili la Nachingwea linafanana sana na tatizo la Mikumi. Ningependa nipate majibu ya Serikali ni lini itatengeneza barabara ya lami ya kutoka Kilosa kwenda Mikumi yenye urefu wa kilometa 78, ambayo ni kichocheo kikubwa sana cha uchumi wa Kata za Mikumi, Muhenda, Ulaya, Zombo, Masanze pamoja na Magomeni?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, natambua juhudi za Mheshimiwa Haule na umekuja ofisini, tumeongelea kuhusu hii barabara na ninawashukuru mlipitisha bajeti yetu, katika bajeti ile unafahamu kwamba kuna bajeti ya kujenga hiyo barabara. Mimi nakuhakikishia, tutahakikisha tunasimamia vile fedha ambazo mmetutengea tutatekeleza ikiwa ni pamoja na kujenga eneo hili la barabara ya kutoka Kilosa hadi Mikumi.
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo ya Nachingwea yanafanana na matatizo yalioko kwenye Jimbo la Nyamagana, ningependa kujua kutoka kwa Mheshimiwa Waziri au Naibu Waziri, kauli ya Serikali juu ya barabara ya kutokea Kata ya Buhongwa kupita Kata ya Lwanima, Mitaa ya Sawa, Kanindo, Kishili, kutokea Igoma, lakini kutoka hiyo barabara inayokwenda Mkuyuni – Kanyerere – Tambuka Reli, kutokea Buzuruga kwa sabubu imekuwa ni ahadi ya muda mrefu na tunatambua namna ambavyo Jiji la Mwanza limekuwa likikua kwa kasi kila wakati. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya ujenzi wa barabara hizi zitakazopunguza msongamano kwa kiwango kikubwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mabula, kwa kweli ni Mheshimiwa Stanslaus Mabula na Mheshimiwa Angelina Mabula (wote wawili) wamekuja tumejadili kuhusu hizi barabara, tulikubliana kwamba, tutawasiliana na Meneja wa TANROADS Mkoa ili tuhakikishe kwamba, tunaweka mikakati ya kutekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mheshimiwa Naibu Spika, ninawahakikishia kwamba hiyo ahadi tuliyowapa tulipokutana ofisini ni ahadi ya dhati, inatoka katika sakafu ya mioyo yetu na tutahakikisha tunaitekeleza.
MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nilitaka nimuambie Mheshimiwa Naibu Waziri wa Miundombinu kwamba sasa hivi wakazi wanaodai fidia siyo 800 ni wakazi 1,600. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu yake mazuri aliyonipa, lakini nilitaka niongeze maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu tathmini iliyofanyika ilifanyika 1995 na wakati huo mfuko wa cement au vitu vyote ambavyo vinavyohusisha ujenzi vilikuwa viko bei ya chini, je, Serikali ina mpango gani wa kuwafanyia tathmini tena hawa wakazi 1,600 ili waweze kupata fidia yao kutokana na bei za vifaa vya ujenzi kupanda?
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili nalotaka kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba commitment ya Serikali, iseme itawalipa lini hawa wakazi wa Kipunguni, ambao wamebaki 1,600, kwa sababu mpaka sasa hivi Serikali haijasema itawalipa lini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILINO: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu concern ya Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kipunguni 742 ambao bado hawajalipwa fidia. Kwanza, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba itabidi tuwasiliane ili tuwe na takwimu sahihi. Kwa mujibu wa takwimu zetu waliobakia ni 742 na sio 1,600 aliowataja. Hata hivyo, kwa sababu yeye anafahamu ni 1,600 tutalisawazisha hilo. Naomba atuletee orodha ili tuweze kuangalia hatimaye tuone kuna tatizo gani katika hizo takwimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuwalipa hao 742 waliobakia, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi, Serikali itawalipa kama ilivyodhamiria. Kuhusu kwamba wafanyiwe tathmini upya, nadhani Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba hakuna sababu ya kufanya tathmini upya kwa sababu tathmini ile iliyofanyika na kwa kipindi ambacho kinachelewa tuna utaratibu wa kuhuisha viwango kwa maana ya kuongeza riba inayotakiwa kuongezeka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie kwamba suala la tathmini upya wala siyo la msingi sana. La msingi ni sisi kupata fedha na kuwalipa hawa waliobakia 742 na tutalifanya hilo mara tutakapopata fedha.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wangu wa Shabiby round about, Arusha Road walifanyiwa tathmini mwaka 2006 na waliambiwa wakati wowote Serikali itabomoa nyumba zao na kujenga barabara pale lakini mpaka leo wananchi hawa hawajalipwa na huu ni mwaka wa 10 hata choo kikibomoka hawajengi. Naomba Waziri aniambie, ni lini wale watu watalipwa fidia zao halali kwa maana zinazostahili kwa leo ili waondoke?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILANO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba umenizuia kusema yale yaliyopo ndani ya roho yangu lakini naomba uniruhusu, unafahamu fika Mheshimiwa Felister Bura…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, ni kwa sababu muda wetu ni mfupi ndiyo maana nimekusaidia kuwatangazia wote kwamba sifa zile zinamwendea kila Mbunge hapa ndani ili wewe uendelee tu kujibu maswali. (Kicheko/Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa juhudi za Mheshimiwa Felister Bura, hivi sasa tunaendelea kukamilisha kilomita nane za lami eneo la Msalato na kwa juhudi zake hizo hizo namhakikishia tutaendelea kuhakikisha tunawalipa fidia hawa watu ambao wanahusika katika hilo eneo. Kama ambavyo nilijibu awali, hakuna sababu ya kufanya tathmini upya badala yake ile formula ya kuongeza riba ndiyo inayotumika na hawa watu watalipwa haki yao bila matatizo yoyote mara fedha zitakapopatikana.
MHE. LUCY T. MAYENGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa suala hili la Kipunguni Dar es Salaam kutokana na jibu la msingi limekuwa likileta malalamiko mengi na limekuwa likizungumzwa kwa muda mrefu na kwa kuwa ofisi ya Wizara hii ipo Dar es Salaam:-
Je, kwa nini Serikali hasa Mheshimiwa Naibu Waziri asitoke yeye aende Kipunguni pamoja na wataalam ili aweze kupata majibu ya kujiridhisha badala ya kumsubiri Mheshimiwa Mbunge yeye ndiyo alete majibu hapa Bungeni.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi hawa wa Kipunguni walishafika ofisini kwetu, nikaondoka nao nikaenda kwa acting CEO wa Uwanja ule wa Ndege na baada ya kujadiliana kwa mpana ndiyo hayo majibu ninayoyatoa hapa yanatokana na vikao hivyo. Mimi mwenyewe nimekutana nao ofisini baada ya wao kuja na baadaye tulifanyia vikao Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam tukiangalia maeneo yote yale matatu ya Kipunguni, Kipawa na Kigilagila. Kwa hiyo, namhakikishia kwamba hicho nachokisema hapa ni kutokana na kile nilichokifanyia kazi. Ndiyo maana nasema huu utofauti kati yangu na Mheshimiwa Mbunge wa figure alizoleta hapa ningependa nipate ushahidi wa hicho anachokiongea.
Mheshimiwa Naibu Spika, nachokisema, waliobakia ni 742 na tutawalipa mara fedha zitakapopatikana, ni kutokana na kazi kubwa niliyoifanya katika eneo hilo. Hata hivyo, bado nitaendelea kuliangalia suala hilo nikishirikiana na hawa Waheshimiwa Wabunge ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Kaluwa kuhakikisha kwamba hicho tunachokisema ndicho sahihi.
MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Jambo lililotokea Segerea linafanana sana na lile linalotokea barabara ya Bwanga Ruzewe ambapo wananchi walivunjiwa nyumba kupisha ujenzi wa barabara hiyo miaka minne sasa na waliahidiwa kwamba watalipwa fidia na wameambiwa mara nyingi kuandika barua, wamekuwa wakifuatilia lakini hakuna jambo lolote linalofanyika. Naomba commitment ya Serikali, ni lini wananchi hawa watapewa malipo yao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nafurahi sana Mheshimiwa Doto Biteko amechukua nafasi ya kuwa Mbunge wa Bukombe kwa sababu Mbunge aliyemtangulia alileta kwetu pendekezo kwamba tutangulie kukamilisha ujenzi wa lami wa ile barabara baada ya hapo tushughulikie fidia. Mheshimiwa Doto Biteko anafuatilia sana ulipaji wa fidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia yote mawili tutayafanya lakini naomba sana tena sana tuanze kwanza kukamilisha ile lami. Kwa hiyo, kadiri tutakavyopata fedha kwanza tumalizie lami ambayo tumekusudia kuimaliza hivi karibuni, baada ya hapo, tutaendelea na hilo la fidia kama ambavyo Mbunge aliyemtangulia alikuwa anasisitiza sana na sisi tunapenda kufuata ile continuity.
MHE. MBONI M. MHITA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kutokana na changamoto za daraja la Wami kufanana sana na changamoto za madaraja ambayo yanaunganisha barabara inayotoka Handeni kwenda Turiani, je, ni lini Serikali itaanza mchakato wa ujenzi wa madaraja haya ili barabara inayounganisha Handeni na Mkoa wa Morogoro iweze kufanya kazi na kupitika? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoongelea Mheshimiwa Mboni Mhita pamoja na madaraja ambayo yamo katika barabara hiyo ni sehemu ya barabara iliyotolewa ahadi na viongozi wetu wa Kitaifa ijengwe kwa kiwango cha lami. Nami naomba nimhakikishie, tupo hapa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambapo kazi yetu kubwa ni moja tu kuwajengea miundombinu Watanzania kwa kuhakikisha kwamba ahadi zote za viongozi wetu wakuu zinatekelezwa. Pamoja na kwamba madaraja haya na barabara hii kama alivyoona katika bajeti tuliyoipitisha haikuwekewa fedha ya kutosha, nimhakikishie baada ya kukamilisha madaraja na barabara ambazo tayari wakandarasi walikuwa site kuanzia Awamu ya Nne, tutaanza kushambulia ahadi ambazo zilitolewa na viongozi wetu na ahadi zote zilizopo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuhakikisha kwamba tunazikamilisha katika miaka inayofuata.
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Umuhimu wa kimkakati wa daraja la Wami kwa maana ya usalama wa nchi yetu na uchumi wa Taifa letu unafanana sana na umuhimu wa kimkakati wa barabara ya Mabokweni - Maramba - Bombo Mtoni - Mlalo -Same kwa maana ni barabara inayopita kwenye maeneo ambayo ni mpakani, kwa hiyo, ina umuhimu wa kiusalama. Vilevile ni barabara ambayo inaunganisha mbuga za wanyama na inaunganisha Mkoa wa Tanga na Mkoa wa Kilimanjaro. Je, Serikali kwa umuhimu ule ule wa kimkakati, ipo tayari sasa kuijenga kwa kiwango cha lami barabara hii?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni bahati mbaya kwamba Mheshimiwa Mbunge alipofika ofisini kuleta tatizo la barabara hii au tuseme umuhimu, changamoto ya barabara hii, tuliongea lakini hatukumalizia kwa sababu kulikuwa na mambo mengine yalituvuruga. Mimi naomba sana tukae tena tumalizie ile kazi ya kuijadili hii barabara kwa undani tukiwashirikisha wataalamu wetu ili hatimaye tuwatendee haki wanaotumia hii barabara.
MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza naishukuru Serikali kwa kututengea fedha kwenye barabara ya Mbuyu wa Mjerumani Mbulu ambapo ina daraja la Magara ingawa fedha hiyo ni kidogo na imetengwa katika maeneo matatu au manne. Wabunge wa Babati na Mbulu tukishirikiana na Mheshimiwa Issaay na Mheshimiwa Flatei, tumekuwa tunaomba ile fedha yote iliyotengwa mwaka huu shilingi milioni 300 kama inawezekana na tumeshawasilisha kwa uongozi wa Mkoa, iende kujenga daraja la Magara ambapo itaonyesha mafanikio badala ya kuitumia katika maeneo mengine. Tunaomba Wizara itukubalie tupeleke fedha hiyo kwenye daraja na likikamilika basi hayo maeneo mengine yaendelee kufanyiwa kazi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Jitu, ingawa siyo sahihi ni Jitu Soni lakini kule wanasema Mbunge wetu ni Jitu lakini nadhani wana maana ya umakini unaotumia katika kufuatilia mahitaji yao. Nampongeza sana kwa hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu hili halimhusu yeye pake yake, linamhusu Mheshimiwa Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini na Waheshimiwa Wabunge wengine kama watatu hivi. Naomba kuwahakikishia kwamba ombi lenu tumelipokea, tutalitafakari na tutalifanyia kazi.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nianze kuipongeza sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa ujenzi wa daraja la Igumbilo ambalo leo hii wakimbiza mwenge wanalizindua pale katika Jimbo la Iringa Mjini.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu ni kuhusiana na ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Dodoma - Mtera - Iringa ambao umekamilika lakini sasa kuna malori makubwa sana yanakatiza katikati ya mji na kusababisha msongamano na barabara hii kuharibika katikati ya mji. Ni lini sasa ule mchepuko ambao ulikuwa umetengwa, ambao unatokea kwenye Chuo cha Tumaini kwenda kwenye barabara kuu utakamilika kwa sababu sasa hivi magari mengi sana yanapita kwenye ile barabara? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kutoka Mkoa mzito wa Iringa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, mchepuo wa Iringa upo katika mipango yetu. Naomba nimhakikishie kwamba kile ambacho wao kwa maana ya RCC walikileta kwetu na sisi tumekichukua, tutakifuatilia kuhakikisha kwamba tunakitekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini? Naomba tu Mheshimiwa Mbunge anipe nafasi kwa sababu siyo sahihi sana kutamka tarehe hapa, lakini naomba aangalie dhamira yetu kwamba ni ya dhati na tutatekeleza mradi huo wa ujenzi wa mchepuo wa barabara pale Mjini Iringa.
MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Juu ya suala la upembuzi yakinifu wa barabara hii limeshakuwa ni la muda mrefu sana. Bahati nzuri tayari hata Mkandarasi alishapatikana na tayari hilo tangazo lilishatolewa toka Desemba, 2015. Sasa leo hii mnapozungumza kwamba, process za kumpata mkandarasi zinaendelea ni mkandarasi gani tena mwingine huyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, imeshakuwa ni kawaida kwa Serikali kuwa inatoa utaratibu wa kwamba hiki kitu kitashughulikiwa muda fulani, lakini matokeo yake muda unapita na hicho kitu kinakuwa hakijafanyika. Sasa ningependa kujua kwa sababu 2016/2017 ni muda mrefu, ni muda ambao unachukua miezi 12, wananchi wa Ludewa wangependa wajue ni lini hasa itaanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa taarifa nilizonazo kama ambavyo nilisema katika jibu la msingi mkandarasi yupo katika hatua ya mwisho kupatikana. Vilevile ujenzi wa barabara hii atakumbuka kwamba, alisaidia sana Bunge limepitisha bajeti ya Wizara yetu na katika bajeti ile kuna fedha zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara hii, kwa hiyo, ujenzi utaanza katika mwaka ujao wa fedha unaoanza tarehe Mosi, Julai.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Huko nyuma takribani kama miaka sita sasa kumewahi kutolewa ahadi ya kujengwa baadhi ya barabara katika Mji wa Karatu kwa kiwango cha lami na ahadi hii imekuwa ni ya muda mrefu na mara nyingi tumeuliza hapa Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ituambie ahadi ile ilikuwa tu ni kuwahadaa wananchi ili watoe kura au mmeshindwa kutekeleza? Tunaomba jibu.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi zote za Serikali zinaonyesha dhamira ya dhati ya viongozi wote wanaotoa ahadi ya kutaka kujenga hizo barabara. Kinachotukwamisha zaidi ni uwezo wa kifedha na naomba nichukue fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, hicho kipande chake kitashughulikiwa kama ambavyo viongozi wetu waliahidi.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa muda mrefu sana Serikali iliahidi kujenga barabara inayokwenda kwenye hifadhi la Ruaha National Park na nakumbuka nilishawahi kuleta swali hapa Bungeni na Mheshimiwa ambaye sasa hivi ni Rais alikuwa Waziri alijibu kwamba, kuna pesa zinatoka Marekani kwa ajili ya ujenzi wa hiyo barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba Mheshimiwa anijibu ni kwa nini, kwa sababu barabara hii ni muhimu sana kwenye Mkoa wetu wa Iringa.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba anijibu kwa sababu katika tengeo la bajeti ya safari hii sijaielewa vizuri, sasa atuambie ni lini barabara ile itajengwa inayokwenda kwenye Ruaha National Park?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, barabara hiyo hatujaiweka katika mwaka huu wa fedha unaoanza Julai, lakini namhakikishia ahadi hii kama ambavyo ilitolewa na Mheshimiwa Rais na viongozi wengine itatekelezwa kama ilivyoahidiwa kabla ya kipindi hiki tulichopewa cha uongozi kwisha.
MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa, ahadi nyingi zinazotolewa na Mheshimiwa Rais, kuanzia Awamu ya Nne na mpaka sasa awamu ya Tano, tunavyotambua ahadi ya Mheshimiwa Rais ni kama amri.
Je, ni kwa nini ahadi zinazotolewa na Rais wetu hazitekelezeki mapema? (Makofi)
Swali la pili, kuna ahadi vilevile ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne katika Halmashauri ya Mji wa Maswa, ilisemekana kwamba zitajengwa kilometa tatu ilitolewa ahadi na Mheshimiwa Rais, Jakaya Mrisho Kikwete; je, ni lini ujenzi huu utaanza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, viongozi wetu wakuu wanapotoa ahadi huwa wanaonesha dhamira na baada ya hapo utaratibu wa kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza dhamira hiyo unafuata. Kuchelewa kujenga au kutekeleza ahadi ni kutokana na kukosekana kwa upatikanaji wa fedha na kwa kawaida mara fedha zinapopatikana ahadi huwa zinatekelezwa. Ninamhakikishia hata hiyo barabara analiyoongelea maadamu dhamira ilishaoneshwa ni wajibu wetu tuliopo katika sekta ya ujenzi kuhakikisha dhamira hiyo iliyooneshwa na viongozi wetu wakuu inatekelezwa.
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhahiri kwamba miundombinu ya kiwanja cha ndege ni pamoja na barabara inayoingia uwanjani na barabara hii sasa imechakaa. Sasa nataka kuuliza kwamba Serikali ina mpango gani wa ukarabati wa barabara inayoingia uwanja wa ndege wa Mtwara kutoka Magomeni Mjini Mtwara hadi uwanja wa ndege?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, amesema kwamba kuna master plan ambayo inaandaliwa; sasa nilitaka kuuliza kwamba kwa kuwa Serikali ina mpango gani wa kutwaa eneo la ardhi kwa sababu sehemu kubwa ya uwanja huo wa ndege imepakana na eneo la Jeshi; sasa kwa vyovyote vile watahitaji eneo la kijiji cha Naliendele; wamejiandaaje kutwaa eneo hili ili kuepusha migogoro ya wananchi wa Naliendele hapo baadaye?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu ukarabati wa barabara, ni sehemu ya mpango ambao nimeueleza katika swali langu la msingi. Tunapoongelea kukarabati uwanja huu ni kurekebisha njia za barabara za kurukia na kutua ndege pamoja na maingiliano na nyumba vilevile za abiria. Kwa hiyo, ni mpango wote, unaunganisha kila kitu ikiwa ni pamoja na barabara zinazoingilia uwanja huo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, namwomba Mheshimiwa Mbunge asubiri kwanza tupate taarifa kamili ya mpango kabambe huo ambao unakamilika mwezi Julai kama nilivyosema katika jibu langu la nyongeza, baada ya hapo ndiyo masuala ya kutwaa ardhi na mipango mingine ya kutekeleza mpango huo yatafuatia.
MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipati nafasi hii. Nami naomba niulize swali linalofanana na swali na msingi. Kwa jina naitwa Zaynabu Matitu Vulu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba na mimi niulize swali linalofanana na swali la msingi. Kwa kuwa Mafia ina uwanja wa ndege; na kwa kuwa Mafia ni eneo ambalo linapokea watalii wengi sana.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka taa ili wasafiri hao waweze kutumia ndege wakati wowote na kuweza kuunganisha na ndege zao kwa ajili ya safari zao za Kimataifa?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, uwekaji wa taa katika kiwanja cha ndege cha Mafia utafanyika pale mahitaji yatakapojitokeza. Kwa sasa hatuna ndege zinazotua usiku. Needs hiyo itakapojitokeza, wataalam watafanya mpango huo na taa hizo zitawekwa.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali na naomba niulize maswali mawili kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini swali langu la kwanza; kwa kuwa Serikali imeamua kuifanyia kazi barabara hiyo ya ulinzi; na kwakuwa kuna vijiji kumi vya ulinzi ambavyo vipo katika Jimbo la Lulindi na hakuna daraja pale, daraja lake la Mto Myesi Mbagala lilichukuliwa na maji wakati wa mafuriko 2012.
Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kuwaagiza watu wa TANROADS Mkoa wa Mtwara walifanyie tathmini daraja hilo ili liweze kujengwa wakati huu barabara hii ikitengenezwa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kwamba, kwa kuwa aliyekuwa Waziri wa Ujenzi ambaye sasa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa John Pombe Magufuli aliahidi kusaidia ujenzi wa madaraja matatu ambayo yalizolewa na maji katika mafuriko ya mwaka 2013 na 2014; madaraja ya Mto Mwiche katika kijiji cha Shaurimoyo, Nakalola na Nanjota na tayari lile la Nanjota limeanza kufanyiwa kazi; je, Mheshimiwa Waziri atalithibitisha vipi Bunge hili kwamba yale madaraja ya Shaurimoyo pamoja na Nakalola sasa litaingia kwenye mpango wa kujengwa?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikujulishe kwamba nilikuwepo katika hilo eneo. Nilikwenda na Mheshimiwa Mbunge, niliwaona wale watu jinsi wanavyopata shida kwa sababu zile kata zote zilikuwa zimekatwa kabisa, hakukuwa na mawasiliano; na kwa kweli tuliagiza angalau daraja moja liunganishwe kwa haraka ili watu waanze kupata sehemu ya mawasiliano waweze kwenda Masasi kujipatia huduma zao za kijamii.
Mheshimiwa Naibu Spika, madaraja hayo mengine mawili yametengewa bajeti na nawaagiza TANROADS watoe kipaumbele ili Kata zile zote ambazo zilikuwa zimetengwa ziweze kupata huduma kwa urahisi zaidi kama ilivyokuwa awali. Kwa kutegemea hilo daraja moja tu haitoshi.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu daraja la ulinzi, naomba nalo likafanyiwe tathmini kama ambavyo mwakilishi wa wananchi wa kule ameomba na ninafahamu kuna vijiji vingi ambavyo vipo katika ule mpaka, barabara ilikuwa ni ya Jeshi, lakini kwa sasa kuna makazi mengi na watu wanalima sana kule. Kwa hiyo, naomba vilevile pamoja na daraja hili katika barabara ile ya ulinzi walifanyie tathmini halafu waje na taarifa ambayo itatusaidia kufanya maamuzi ya nini kifanyike.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa swali la msingi lililoulizwa linafanana kabisa na matatizo yaliyopo kwenye Jimbo la Geita Vijijini ambapo mwaka 2013 Mheshimiwa Rais Mstaafu alipokuja kule tulimweleza kuhusiana na barabara mbadala ya kilometa 75 kuanzia Bugulula, Senga, Sungusila mpaka kwenda kuungana na Sengerema Mwamitiro kwamba ipande kutoka kwenye hadhi ya Halmshauri kwenda kwenye hadhi ya TANROADS na Mheshimiwa Rais Mstaafu alimwomba Mheshimiwa Rais wa sasa ambaye alikuwa Waziri kwamba atusaidie na akatuambia tufuate taratibu za Serikali na akatupa kuanzia shilingi milioni 400 tukaanza kukarabati ile barabara; na taratibu zote zimeshakamilika tumepeleka kuomba....

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Swali langu la msingi, Waziri wa Ujenzi anatoa kauli gani kuhusu kuipandisha barabara hii kuwa ya TANROAD angalau kwa kiasi cha changarawe?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema ahadi ilitolewa na viongozi wetu na kwa maana hiyo, viongozi wetu walionesha dhamira ya kuitengeza hii barabara. Na mimi namhakikishia, sisi ambao tumekabidhiwa dhamana ya kutekeleza dhamira za viongozi wetu, tutalishughulikia hili. Kuhusu matengenezo Regional Manager wa Geita afanyie tathmini, apeleke taarifa makao makuu ili maamuzi sahihi yaweze kufanyika kwa haraka.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lililoulizwa Na. 278, linafanana na barabara ya Mzani – Nyakahula – Mrusagamba – Mrugalama iliyopo Wilaya ya Ngara, Kagera. Pia kuna barabara ya Karagwe kupitia pori la Kimisi, Tubenako Ngara ambazo Mheshimiwa Rais aliahidi zitajengwa. Je, ni lini Serikali itakamilisha barabara hizo kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nilijibu awali, dhamira yetu ni kutekeleza ahadi zote ambazo viongozi wetu walizitoa katika nyakati mbalimbali, kuanzia awamu ya nne na awamu ya tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Oliva kwamba barabara hizo alizoziongelea, maadam zilitolewa ahadi, nasi tutazichukua ili tuweze kuzishughulikia kwa namna ambavyo uwezo wa kifedha utakavyokuwa unatujaalia.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nami naomba kuuliza maswali madogo mawili. Swali langu la kwanza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri…

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, nashukuru. Naomba kuuliza, ni kwa nini Wizara ya Ujenzi haijaweza kupitisha barabara mpya za Halmashauri ya Mji wa Mbulu na kwa kuwa mji wetu wa Mbulu ni mji mkongwe kuliko miji yote Tanzania? Naomba kauli ya Wizara kuhusu barabara hizi mpya kwa kuwa sasa magari yameongezeka sana katika Wilaya zetu. Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna barabara ambayo ni ya lami kwa pale Mbulu Mjini. Vilevile Mheshimiwa Mbunge atakuwa anafahamu kwamba katika bajeti ambayo tunashukuru sana mliipitisha hapa Bungeni, kuna bajeti ya kutekeleza baadhi ya barabara ambazo ziko ndani ya Wilaya ya Mbulu; na ninamhakikishia kwamba tutatoa kipaumbele ili fedha zile zilizotengwa kwa ajili ya kujenga barabara za Wilaya ya Mbulu na Wilaya nyingine tutazitekeleza kwa kadri Mwenyezi Mungu atakavyotujalia nguvu za kifedha.
MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la kuweka minara kwanza niipongeze sana Serikali kwamba imeendelea kupeleka minara katika Jimbo la Kalenga kwa kasi zaidi. Tatizo ninalolipata ni kwamba baada ya kusimikwa ile minara upatikanaji sasa au uanzaji wa kuanza kupata mawasiliano unatumia muda mrefu sana. Ningependa kujua Serikali ina mkakati gani ili mara baada ya kuwekwa ile minara mawasiliano yaanze kupatikana kwa muda unaostahili. (Makofi)
Swali langu la pili, narudi tu kwenye majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba amesema vijiji vilivyotamkwa hapa mwishoni vya Kaning‟ombe na Ikuvilo vitapita katika utaratibu wa kupitia UCSAF lakini katika tovuti ambayo nimekuwa nikiipitia ya UCSAF nitoe tu statistics kidogo inaonyesha kwamba kwa mwaka 2015 zilitangazwa zabuni175, Kata zilizopata wazabuni 116 hii kwa ni Tanzania nzima, idadi ya vijiji 156, miradi kuanza ilikuwa ni Mei, 2015. Lakini katika orodha hii yote hakuna vijiji ambavyo tayari vilishaanza kupatiwa mawasiliano ni zero, kupitia mradi ya UCSAF.
Ningependa kujua Serikali ina mikakati gani kuhakikisha kwamba inaipa pesa UCSAF ili kwamba miradi ambayo imeorodheshwa iweze kukamilika kwa wakati? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mgimwa naomba nikiri kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuwahangaikia watu wake, anafanya hivyo katika maeneo mengi ambayo Wizara yetu inaisimamia ikiwa ni pamoja na barabara, mawasiliano hayo ambayo leo ameyauliza na masuala mengine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba yale tunayomweleza anapofuatilia ofisini tunamthibitishia kwamba tutayatekeleza. Nimhakikishie kwamba Awamu hii ya Tano ya Serikali ya Dkt. John Pombe Magufuli inatenda inachoahidi. Mkakati wa kuhakikisha minara ambayo inajengwa inaanza kufanya kazi tutaifuatilia, kwa hili aliloliuliza nadhani ameuliza tu kuongezea utamu, tumemwambia kwamba mnara huo utaanza kufanya kazi mwishoni mwa mwezi Juni kama tulivyoongea, ni kweli na tutafuatilia. (Makofi)
Kuhusu mirafi ya UCSAF, naomba nimhakikishie kama nilivyosema hii Serikali inatenda inachoahidi, katika mwaka huu wa fedha hizo zilizotengwa miradi iliyotangazwa tutahakikisha inakamilika. Lakini usisahau kwamba miradi mingine tuliyoongelea hapa haitekelezwi na UCSAF peke yake mingine inatekelezwa na TTCL na Viettel ambayo katika tangazo hili miradi hiyo hutaiona.
MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali fupi kwa Naibu Waziri.
Ni lini sasa maeneo ya kata za Mwashiku, Ngulu, Uswaya na Igoweko yataweza kupata mawasiliano kama ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri ameweza kujibu swali la Mheshimiwa Mgimwa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Gulamali ni mfuatiliaji sana, siyo wa masuala ya mawasiliano peke yake, bali ni pamoja na barabara zake zile mbili ambazo viongozi wetu wakuu walitoa ahadi, na nyakati zote wakati akifuatilia hiyo miradi nimekuwa nikimhakikishia kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano inatenda inachoahidi. Mheshimiwa Gulamali nikuahidi katika yale uliyoyafuatilia vijiji hivi sikumbuki kama ulinitajia. Kwa hiyo, nitafuatilia ratiba ya utekelezaji wa makapuni yote yanayotuletea mawasiliano nchini kuona kama hivi vimeshaingizwa katika ratiba na kama vitakuwa havijaingizwa namhakikishia tutaviingiza.
MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru kwa kuniona, kwa kuwa tatizo la Jimbo la Kalenga linafanana kabisa na tatizo la Mkoa wa Kusini Unguja;
Je, ni lini Serikali itapeleka minara ya simu kwenye vijiji ambavyo bado havijafikiwa na huduma hii kwenye Mkoa wangu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Khadija Ali anafahamu kwamba tumefungua ofisi Unguja ambayo kazi yake kubwa ni kuhakikisha mawasiliano yanakamilishwa katika vijiji mbalimbali Unguja na Pemba. Naomba nimhakikishie akitembelea hii ofisi atapata uhakika wa eneo hilo analoliongelea ratiba yake ikoje.
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri, kwa kuwa suala hili linawagusa karibu Watanzania wote na mimi nitajitahidi kwenda polepole kama alivyoenda yeye polepole. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nyumba nyingi…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mwalongo naomba usiende polepole kwa sababu muda wetu unakimbia sana na watu wana maswali mengi. (Makofi/Kicheko)
MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa nyumba nyingi katika Mji wa Njombe zimewekewa alama ya kijani. Serikali haioni ipo haja ya sasa kufuta alama hizo ili kuwapa fursa wananchi wamiliki wa nyumba hizo kufanya ukarabati wa nyumba zao na kuzitumia nyumba zao kama dhamana katika taasisi za fedha? (Makofi)
Swali la pili, je, Serikali haioni sasa upo ulazima kuleta Sheria Namba 13 ya mwaka 2007 tuifanyie marekebisho ili ibainike bayana kwamba, maeneo ya mjini yawe na upana wa mita 42 badala ya 60 za sasa. Hii itasaidia kutunza historia za miji katika nchi yetu, lakini vilevile itaipunguzia gharama Serikali pamoja na wananchi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumeweka „X‟ ya kijani kama ishara kwamba hilo eneo haliruhusiwi kuendelezwa, haliruhusiwi kujengwa nyumba mpya kwa sababu ni eneo la hifadhi ya barabara kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2007. Kwa hiyo, kusema wafute na ianze kutumika kama dhamana siyo sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Watanzania wote wakati tunapitisha sheria hii tulikuwa na malengo ya kuiendeleza nchi yetu kimiundominu, tupate fursa ya kupanua barabara na hatimaye zitupeleke katika karne ya viwanda, tuwe na maendeleo makubwa na huko ndiyo tunakoenda hatuwezi kurudi nyuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, suala la kubadilisha sheria, kwanza mimi binafsi na niliongea na Mheshimiwa Waziri wangu naongea kwa niaba yake kwa kweli tulitaka tupanue zaidi kwa sababu sasa hivi tunaenda kwenye miundombinu, sehemu za mijini kuna flyovers na highways lazima tuwe nazo ambazo zinahitaji ardhi kubwa zaidi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naibu Spika kama ifuatavyo:- (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, alama ya kijani ama nyekundu, maana yake nyumba hiyo haitakiwi kuwepo hapo kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2007. Tunachotaka, wale ambao walijenga kabla ya mwaka 2007 haki yao inayoongelewa hapa ni ya kufidiwa, siyo kuendelea kukaa, ila hatuwaondoi mapema mpaka pale tutakapokuwa na mahitaji ndipo tutakapowafidia. Ila tutakachokifidia ni kile kilichofanyika kabla ya mwaka 2007. Chochote kitakachokuwa kimefanyika baada ya mwaka 2007 kitabomolewa bila fidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, hoja hiyo ya kubadilisha sheria mimi binafsi siiungi mkono lakini tumechukua ombi lako na tutaliwasilisha Serikalini likajadiliwe ili maamuzi ya Kiserikali yatolewe.

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri watu wengi wamesimama, lakini nadhani swali la msingi hapo ni kwamba hawa watu wenye kijani umesema mpaka mtakapohitaji barabara. Kama jibu ni hilo, hawa watu waendelee kusubiri? Kama utaihitaji barabara baada ya miaka kumi, wao inabidi waendelee kusubiri wasifanye chochote kwenye hayo maeneo yao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Naibu Spika kama ifuatavyo:- (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, alama ya kijani ama nyekundu, maana yake nyumba hiyo haitakiwi kuwepo hapo kwa mujibu wa Sheria ya mwaka 2007. Tunachotaka, wale ambao walijenga kabla ya mwaka 2007 haki yao inayoongelewa hapa ni ya kufidiwa, siyo kuendelea kukaa, ila hatuwaondoi mapema mpaka pale tutakapokuwa na mahitaji ndipo tutakapowafidia. Ila tutakachokifidia ni kile kilichofanyika kabla ya mwaka 2007. Chochote kitakachokuwa kimefanyika baada ya mwaka 2007 kitabomolewa bila fidia.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, kabla hujatoka, alama nyekundu ni kwamba wale watu wanatakiwa kubomoa wasiwepo; alama ya kijani maana yake sheria imewakuta. Sasa ndiyo anauliza Mheshimiwa Mwalongo wanatakiwa kusubiri muda gani hao wenye alama ya kijani ambao sheria imewakuta?
Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. (Makofi)
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hii alama ya kijani, hili tutalichukua na tutaliangalia tuone tutafanyaje.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu haya, ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi. Kama Serikali ilivyosema kwamba tunayo barabara ya lami ya kutuunganisha na Dar es Salaam. Sisi watu wa Mkuranga tunataka barabara itakayotuunganisha, Kisarawe mpaka Kibaha moja kwa moja, uwezekano wa kufanya hivyo upo, tunayo barabara ya kutoka Kimanzichana mpaka Mkamba, Mkamba mpaka Mkuluwili, Mkuluwili inapita katika Bonde la Saga, na kwenda kutokea Msanga, takapofika pale Msanga, itakwenda kuungana na barabara ya Manelomango inayotoka Mzenga, Mlandizi, inakwenda mpaka Mloka.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ambayo imeahidiwa katika ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Namuomba Waziri aichukue barabara hii, aziagize mamlaka zinazohusika ziweze kutuunganisha sisi watu wa Mkuranga, Kibiti, Rufiji kwa pamoja na Wilaya ya Kisarawe mpaka Kibaha.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI, NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimelisikia ombi lake amelisema kwa sauti kuu, ninafahamu barabara anayoielezea, ya kutokea Kimanzichana hadi Msanga. Ni barabara ambayo ipo, sana sana katika barabara hiyo, kuna tatizo dogo tu la bonde, hilo bonde linaloitwa Bonde la Saga, ambalo nadhani Halmashauri haina uwezo wa kulihudumia.
Mheshimiwa Naibu Spika, labda tu nimwambie kwamba kutokana na sauti hiyo kuu, Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, wajenge hoja ya kipande hiki kama cha kilometa mbili hadi cha kilometa tatu cha Bonde la Saga. Katika Mfuko wa Barabara kupitia Mkoa na hatimaye uje Taifa, tuangalie namna ya kufanya kama ombi maalum la kushughulikia hili bonde; nina uhakika bonde hili likishughulikiwa, uwezo wa Halmashauri kuishughulikia hiyo barabara upo.
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto za Jimbo la Mkuranga zinafanana na changamoto za Jimbo la Karagwe. Naishukuru Serikali kwa kutuunganisha Jimbo la Karagwe na Jimbo la Kyerwa kwa kuweka mpango wa kujenga kwa lami barabara ya Mugakolongo kwenda Mulongo. Nipende kumuomba Mheshimiwa Waziri akisaidie Kijiji cha Rwambaizi, barabara imekwepa kijiji na kama mnavyojua barabara huchochea maendeleo. Nipende kumuomba Mheshimiwa Waziri, atusaidie barabara ya Mgakolongo kwenda Mulongo, ipite kwenye kijiji cha Rwambaizi, ili wananchi wangu wa hicho kijiji waweze kupata maendeleo yatakayokuja na ujenzi wa barabara hiyo la lami, nashukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati nzuri barabara anayoitaja ni barabara ambayo ipo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi, na kwa mwaka 2016/2017 anafahamu kwamba imetengewa fedha. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Bashungwa, Wizara yetu dhamana yake ni kutekeleza ahadi za ilani ya Chama cha Mapinduzi, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha barabara hii katika miaka hii mitano, inakamilika kujengwa kwa lami.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa Mkoa wa Pwani ni Mkoa ambao umeelekezwa kupima maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda; na kwa kuwa Wilaya ya Kisarawe imetenga eneo la viwanda ambalo inapita barabara ya Kiluvya - Mpuyani.
Je, Naibu Waziri pamoja na jibu lake kwa swali la msingi, yupo tayari kutembelea barabara hiyo mara baada ya Bunge hili; ili kuona eneo la mkakati la ujenzi wa viwanda ambalo limetoa zaidi ya viwanja 111 na wawekezaji mbalimbali wameonesha fursa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana naye kwamba baada ya kumaliza Bunge hili, nitatembelea hii barabara inayoanzia Kiluvya, ili kuangalia changamoto zake
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Barabara inayounganisha Mkoa wa Singida, kwenda Wilaya ya Mkalama, ambayo inaunganisha pia Mkoa wa Simiyu, kupitia daraja la Sibiti kwa hali ya mshangao sana mkandarasi alifika site lakini akaondoka, sasa nilikuwa namuomba Naibu Waziri, yuko tayari kwenda kusaidiana na wananchi wale kushangaa ni kwa nini mkandarasi aliondoka site?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi na Mheshimiwa Waziri wangu, tutajigawa kuhakikisha kwamba maombi haya ikiwa ni pamoja na la kwake tunayatekeleza. Labda niombe hapo hapo Waziri wangu aniruhusu, kati ya Kiluvya na Daraja la Sibiti, mimi aniruhusu niende kwenye Daraja la Sibiti.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, matatizo ya Jimbo la Tarime Vijijini yanafanana na matatizo ya Jimbo la Mpwapwa. Kwa kuwa barabara ya kutoka Mbande - Kongwa - Mpwawa - Kibakwe tayari ilishafanyiwa upembuzi yanikifu na detailed design na ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2015 mpaka 2020 na ni ahadi ya Rais mstaafu pamoja na Rais wa sasa. Je, Mheshimiwa Waziri ni lini sasa mtaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali pili, unakumbuka Mheshimiwa Naibu Waziri wakati anajibu swali langu nilitoa ombi kwamba barabara ya kutoka Gulwe, kwenda Berege, Chitemo, Mima, Chazima, Igoji mpaka Ihondo na Fufu kwamba barabara hii iko chini ya Halmashauri ya Wilaya, lakini Halmashauri ya Wilaya haina uwezo wa kutengeneza kwa sababu haina fedha na imeharibika sana, mvua zimeharibu sana. Je, Mheshimiwa Waziri anawaambia nini wananchi wa kata hizo kwa sababu barabara hiyo inapitika kwa shida sana? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoiongelea ya kutoka Mbande, Kongwa, Mpwawa hadi Kibakwe kama alivyosema ni barabara ambayo imeahidiwa na viongozi wetu wa Kitaifa, lakini vilevile ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015/2020 ya Chama Tawala cha CCM. Naomba nimwahidi na nilishaongea naye pamoja na Mheshimiwa Job Ndugai, Mbunge wa Kongwa pamoja na Mheshimiwa George Simbachawene, Mbunge wa Kibakwe wote tuliongea kwa undani kuhusu barabara hii na bahati nzuri tuliwasiliana vilevile na viongozi wenzangu Wizarani ikiwa ni pamoja na Katibu Mkuu. Kwamba barabara hii pamoja na kwamba kwenye bajeti iliyopitisha hatujaitengea fedha nyingi lakini ni lazima ianze kujengwa kuanzia mwaka huu wa 2016/2017 kama tulivyoahidi. Namhakikishia nitalisimamia hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili kuhusu barabara ya kutoka Gulwe, Berege, Kitemo, Uhondo na kuendelea, naomba naye nimhakikishie kwamba barabara hii iko chini ya halmashauri, tutawasiliana na wenzetu wa TAMISEMI, tuone ni namna gani tunaweza tukaitendea haki hii barabara ili ipitike siyo kwa tabu kama ilivyo sasa bali ipitike kwa mwaka mzima bila matatizo yoyote.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa hii ya kuuliza swali la nyongeza, matatizo haya ya watu wa Tarime Vijijini ni sambamba na matatizo ya watu wa Jimbo la Mkuranga kuhusu barabara ya kutoka Mkuranga Mjini mpaka Kisiju kwani ni barabara inayounga wilaya mbili za Mafia, ni barabara inayobeba uchumi wa korosho, ni barabara inayobeba watu zaidi ya laki moja na ni barabara ambayo itakuwa ni tegemezi katika uchumi wa viwanda vitakapojengwa katika Kata ya Mbezi. Je, kwa kuwa hii pia ni barabara iliyoahidiwa na Mheshimiwa Rais wetu wa Awamu ya Tano, ni lini na yenyewe itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoiongelea naomba nikiri kwamba nimeisikia sasa, huyu Mheshimiwa tumekuwa tukiongea akifuatilia barabara zake za Mkuranga, lakini huko nyuma hii barabara hakuwahi kuitaja, ameitaja leo, nimeichukua na wataalam wangu tutamletea majibu sahihi kuhusu barabara hii.
MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mazingira ya Tarime yanafanana kabisa na mazingira ya barabara zilizopo katika Jimbo la Tunduru Kusini kutoka Mtwara Pachani, Msewa na Rasi mpaka Tunduru Mjini iliahidiwa na Makamu wa Rais wakati wa kampeni kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami. Je, ni lini mchakato wa ujenzi wa barabara hii utaanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni ngumu sana unapokaa hapa kujibu swali linalohusu barabara yako, kwa hiyo, naomba nijibu kwa niaba ya Waziri wangu wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Mtwara Pachani, Lusewa, Lingusenguse hadi Lalasi ni barabara ambayo iliahidiwa na Mheshimiwa Makamu wa Rais wakati wa uchaguzi, ndiyo kiongozi pekee aliyepita barabara hii. Kwa kweli baada ya kuiona na kuona idadi ya watu walivyo katika maeneo hayo akaahidi kwamba ataijenga kwa kiwango cha lami alipokuwa Lusewa na aliahidi vilevile barabara hiyo itajengwa kwa kiwango cha lami alipokuwa na Lalasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mpakate na wananchi wake wote wa Jimbo la Tunduru Kusini pamoja na wananchi wa Jimbo la Namtumbo na hasa Sasawala kwamba barabara hii kama ilivyoahidiwa tutaijenga, lakini naomba tu wananchi wetu waelewe kwamba ahadi tulizonazo za viongozi ni nyingi, zote tunazo tunazitekeleza kwa awamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka ujao wa fedha barabara hii imetengewa milioni 100 kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika nia ya kutekeleza ahadi ya Makamu wa Rais. Naomba nimhakikishie kazi hii itakapokamilika nitaweza kuwa na jibu sahihi lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi. Nataka kujua barabara ya kutoka Mpanda kwenda Mkoa wa Kigoma ni barabara ambayo imeahidiwa na Serikali kujengwa kwa kiwango cha lami na tayari kuna kilomita 30 kutoka Mpanda Mjini mpaka eneo la Usimbili Vikonge, limeshafanyiwa upembuzi yakinifu. Swali kwa Naibu Waziri, ni lini Serikali itaanza mchakato wa kuijenga barabara hii?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie barabara hii tumeanza kuijenga kama ambavyo yeye ameisema na tutaendelea kuijenga hadi ikamilike kama viongozi wetu wa Kitaifa walivyoahidi na ilishaanza kujengwa. Kwa hiyo, suala itaanza lini sio sahihi, imeshaanza kujengwa na mwenyewe amezitaja kilomita ambazo tayari tumezijenga. Tutaendelea kujenga na tutaikamilisha kabla ya kipindi hiki cha miaka mitano haikijakwisha.
MHE. DUSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri ningependa kujua tumeshuhudia vituo hivi vikijengwa lakini baada ya muda mfupi matumizi yake yanakuwa yamepitwa na wakati kwa sababu inahitajika kujenga eneo kubwa zaidi. Sasa swali kwa nini Serikali isiwe inafanya tathmini ya kina kujua mahitaji halisi ili kukwepa gharama ya kurudia ujenzi mara kwa mara?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, katika barabara hizi bado wananchi wamekuwa wana malalamiko kwamba fidia wanayopewa inachukua muda mrefu sana kukamilika kama ilivyo kwa barabara ya Tanga - Horohoro, ambayo mpaka leo bado kuna watu wanadai. Je, ni lini Serikali itahakikisha watu hawa wanalipwa stahili zao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kubadilika matumizi ya eneo la Mizani na kwamba ujenzi tunapoanza tunajenga eneo dogo na baadaye tunalazimika kubadilisha naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ombi lake tumelipokea na nitawataka watu wa TANROADs mikoa yote kuhakikisha kwamba wanapopanga matumizi ya vituo hivi wasiangalie muda mfupi waangalie muda mrefu ni afadhali kutumia gharama nyingi mara moja kuliko gharama kidogo, halafu tunaendelea kurekebisha kila mwaka. Kwa hiyo, tunamshukuru nimepokea ombi lake tutalifanyia kazi.
Kuhusu suala la stahili kwa watu ambao wanatakiwa kufidiwa katika maeneo haya, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni nia ya Serikali kuwalipa fidia watu wote wanaostahili katika maeneo yote. Lakini lazima tukiri kwamba ili tuweze kulipa fidia lazima tuwe na uwezo sasa kwa mfano unaweza ukalipa fidia, lakini ukachelewa kuanza kujenga, unaweza ukaanza kujenga watu wanaanza kutumia barabara na baadaye ukalipa fidia kadiri uwezo unapopata.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiria hii njia ambayo Serikali inaitumia, ni njia sahihi, kwanza tuwape huduma watu, baada ya hapo tuendelee kutafuta fedha za kuwalipa fidia na mara fedha zitakapopatikana nakuhakikishia watu hawa watalipwa fidia.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kuniona na napenda niulize swali moja la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa kikao cha Bodi ya Barabara katika Mkoa wa Geita kiliazimia kuipandisha barabara ya Geita, Mbogwe mpaka Ushirombo kuwa barabara ya TANROAD, ni lini sasa Serikali itakuwa tayari kuipandisha barabara hiyo ili iweze kuchochea maendeleo katika Wilaya ya Mbogwe na Mkoa mzima wa Geita?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa huyu ndiyo unatusukuma, unatufanya tusilale usingizi lakini nadhani unavyofanya ni
kwa manufaa ya wananchi wa Mbogwe. Nikupongeze sana kwa kazi hiyo kubwa unayofanya ya kufuatilia masuala ya watu wako wa Mbogwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ya Geita, Mbogwe, hadi Ushirombo, kama ambavyo amesema imeombwa na TANROAD Mkoa ichukuliwe na mkoa itoke katika halmashauri. Nadhani utakumbuka nimejibu mara nyingi maswali ya aina hii hapa kwamba maombi yote ya barabara sehemu zote nchini yako zaidi ya 3000 yatafanyiwa kazi kwa pamoja na tutaleta Muswada Bungeni ili tugawane sasa barabara zipi zipande hadhi na zipi zibakie katika halmashauri na tukifanya hivyo lazima tuangalie vilevile na resources; mgawanyo tuliopanga sasa ni kwamba, asilimia 30 iwe halmashauri na asilimia 70 iwe TANROAD.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa na hilo nalo tutatakiwa tulipitie ili kadri barabara nyingi tunapozipeleka TANROAD na fedha nyingi nazo tunatakiwa tuzipeleke TANROAD. Namhakikishia hilo litafanyika na Muswada utaletwa hapa Bungeni kwa ajili ya kuzigawanya hizo barabara.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mkiwa - Itigi, Rungwa - Makongorosi aliyoitaja Mheshimiwa Waziri ni barabara inayopita katikati ya Mji wa Itigi wenye vijiji vya Songambele, Majengo na Itigi Mjini na kwa majibu haya, maana yake barabara hii imeshushwa daraja. (Makofi)
Swali, wakati sheria inabadilika kutoka mita 45 kuja mita 60, wananchi hawa waliwekewa alama za “X” kwamba wasiendeleze maeneo yale. Sasa kwa majibu haya; je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kutamka kwamba wale wananchi waendelee na ujenzi? (Makofi)
Pili, Naibu Waziri anaweza kuthibitishia wananchi wa Itigi kwamba itakapoanza kujengwa kilometa 35 za kwanza na kipande kile kitakajengwa pamoja nacho? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimechanganyikiwa nimechanganyikiwa kidogo kwa sababu swali la pili linapingana au linakinzana na swali la kwanza; kwa sababu swali la kwanza tumemwambia tunajenga hiyo barabara wakati tunajenga hiyo ya kutoka Rungwa - Makongorosi hadi Mkiwa. Kwa maana nyingine, lile eneo ambalo limewekewa “X” ni lazima liendelee kubakiwa kuwekewa “X”. Sasa tumemaliza kufanya upembuzi yakinifu, hatua zinazofuata ni za kulipa fidia na kuanza ujenzi baada ya kutafuta hizi fedha na kupatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili sijui nijibu vipi kwa sababu nadhani la pili linajibu kwa hili la kwanza, kwa sababu tunajenga hili eneo na tutajenga. Tunachokifanya ni tunatafuta fedha.
Kwa hiyo, naomba sana asiwaambie watu wajenge hilo eneo. Maeneo ambayo yamewekewa “X” maana yake ni kwamba katika upembezi yakinifu imeonekana hapo ndiyo barabara itapita. Tafadhali sana, usiwahimize wakajenga, hilo eneo libakie ili tutakapopata fedha tuweze kujenga.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, siyo kwamba tutajenga na hiyo, tunajenga kupitia hapo.
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuniona na kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa ahadi aliyotoa Mheshimiwa Rais kwenye Mji wa Itigi inafanana kabisa na ahadi aliyotoa kwenye Mji mdogo wa Makongorosi ambapo alisema kwamba wakati inajengwa barabara ya kutoka Chunya kwenda Makangorosi na kuelekea Itigi na Mkiwa, Serikali itawajengea wananchi wa Makongolosi lami kilometa nne; je, ahadi hiyo itatekelezwa wakati barabara hiyo inajengwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni ahadi ya viongozi wetu, ni wajibu wetu na dhamana yetu kutekeleza ahadi za viongozi wetu pamoja na ahadi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namhakikishia kwamba ahadi hii itakamilika na hasa wakati ujenzi huu wa barabara ya kutoka Mkiwa hadi Makongorosi itakapofikia hilo eneo, kwa vyovyote na hizo kilometa nne ambazo zimeahidiwa, zitajengwa.
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Barabara ya Bigwa – Kisaki, Wilaya ya Morogoro Vijijini ni ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne na Awamu ya Tano kujengwa kwa lami. Mpaka sasa hivi hata kwenye bajeti iliyopita sikuona kitu chochote kinachoelezea kuwa itajengwa. Je, barabara hii kwa niaba ya wananchi wa Morogoro Vijijini itajegwa lini kwa kiwango cha lami? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumeongea na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo, ni kwamba hii barabara tutaijenga. Mheshimiwa Ishengoma anafahamu na tulishaongea kwamba hii barabara ambayo ni ahadi ya kiongozi wetu wa Kitaifa, tutaitekeleza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kwamba kiwango kilichowekwa katika bajeti ya mwaka huu ni ya matengenezo peke yake, ujenzi tumeshindwa kuuweka safari hii kwa sababu tumetoa vipaumbele kwa zile barabara ambazo makandarasi wako site na tunataka tuwamalizie hawa makandarasi wasiendelee kulipwa fedha bila kufanya kazi. Kwanza, tuwalipe fedha ili wakamilishe barabara ambazo zilishaanza muda mrefu. Tukishamaliza hiyo, sisi baaada ya hapo, sina uhakika kama ni lugha nzuri, lakini sisi ni mwendo mdundo kutekeleza ahadi zote za viongozi wetu na ahadi zote zilizomo katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuanzia mwaka wa pili wa Awamu hii ya Tano. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa naomba tupeni fursa ili tumalize kwanza hizi barabara ambazo zilikuwa zimeanza vipindi vya nyuma na wakandarasi wengi wako site wanapokea hela, interest na vitu vingine wakati hawafanyi kazi kwa sababu tulikuwa hatuna uwezo wa kuwalipa. Sasa tunafanya hilo, tukimaliza mwaka huu unaokuja hawa wote tutakuwa tumewamaliza na sasa tutaanza kutekeleza kwa kasi maeneo mengine yote ambayo viongozi wetu wakuu wameahidi na Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi imeongea
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, kipo! (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza kwa kuwa Mfuko wa Mawasiliano umenufaisha Kata chache sana katika Jimbo la Nanyamba; je, Serikali ipo tayari sasa kuingiza Kata ya Nyuundo na Kata nyingine ambazo hazina mawasiliano katika mwaka huu wa fedha 2016/2017 badala ya kutuambia siku za usoni ambazo hatujui itakuwa ni lini? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kuna Makampuni ya Simu yamefunga minara katika baadhi ya kata zetu lakini upatikanaji wa mitandao bado ni hafifu kama vile Kata ya Njengwa na Milangominne.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri yupo tayari sasa kuyaagiza sasa makampuni hayo kutuma wataalamu ili wakaangalie matatizo ya minara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu vijiji vya Kata vya Nyuundo ambavyo vimeainishwa katika awamu itakayofuata nimelichukua na tutaliangalia kama linaweza likatekelezeka kwa namna ambavyo ameeleza kwa sababu anafahamu kwamba bajeti imeshapita na tutaliangalia kwa namna itakavyowezekana. Naomba tu nimhakikishie kwamba Kata hii ya Nyuundo kwa vyovyote vile tutaishughulikia na mawasiliano tutayapeleka. Suala ni lini, itategemeana na fedha kama zitapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili la maeneo Njengwa na Milangominne, minara kutofanya kazi, nimelichukua tutalifanyia kazi. Nitawafuatilia wahusika nione hasa kuna tatizo gani.
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kule Wilaya ya Igunga Jimbo la Igunga kulikuwa na Kata za Kiningila, Sakamaliwa na Kinungu, zilikuwa zimewekwa kwenye Mpango wa Mawasiliano kwa Wote, lakini pia Jimbo la Manonga Kata ya Goweko na Kata ya Mwanshiku. Ni lini sasa mradi huu utatekelezwa kwa maana yake tulitegemea mwaka 2015 na mwaka 2014 yafanyike? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mila zetu, ukiulizwa swali na bosi wako huruhusiwi kujibu kwenye hadhara. Namuomba Mheshimiwa Dalaly Peter Kafumu tukutane ofisini ili tuweze kuwatendea haki wananchi wa Jimbo hili la Igunga pamoja na Jimbo jirani ambalo ameliulizia. Nakuomba sana tuonane ofisini ili tuweze kukutana na wataalam halafu tuliweke sawa, tuone ni namna gani ya kufanya.
MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kutupa kipaumbele sisi Kambi mbadala.
Kwa kuwa matatizo ya mawasiliano yaliyoko katika Jimbo la Nanyamba yanafanana na Jimbo la Ulanga, Kati ya Kata ya Ruaha, Chilombola, Ilagula, Ketaketa na Ilonga; je, ni lini Serikali itapeleka mawasiliano ya simu za mkononi katika Kata hizi ili na wananchi hawa wafaidi mawasiliano ya simu za mkononi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maswali yako tutayashughulikia, tumeyachukua.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nipate ufafanuzi zaidi wa hayo maeneo aliyoyaeleza ili tuweze kuyafanyia kazi na kuwatendea wananchi wake kwa namna inavyotakiwa. Naomba tukutane ofisini tuelezane kwa undani zaidi kuhusu hilo eneo ili hatimaye tutende kile ambacho wananchi wanakihitaji.
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Naomba kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo langu la Mtwara Vijijini, maeneo ya Moma na Dihimba kote, usikivu wa simu za mikononi siyo mzuri.
Je, ni lini atakwenda kufuatilia yale makampuni ambayo yalipewa kazi ya kuweka minara huko ambapo mpaka sasa hivi kwa kweli kwingine wamejenga, haisikiki na kwengine hawajafika kabisa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, CHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Hawa Ghasia kama Mwenyekiti wa Kamati, vilevile amemwona Waziri wangu kutetea maslahi ya watu wa Jimbo lake. Namshukuru sana kwa juhudi kubwa anazozifanya, kwanza kutusaidia sisi wote kama nchi kupitia Kamati ya Bajeti, lakini vilevile kuwatetea wananchi wa Wilaya ya Mtwara, Jimbo la Mtwara Vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia nitafika kukakagua hilo eneo na baada ya hapo tutampa majibu sahihi, siyo majibu tu, lakini vilevile kujibu kwa vitendo.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa wananchi wamezoea kabla ya barabara ya lami kujengwa huanza na upembuzi yakinifu: Mpaka sasa hivi hakuna hata dalili hizo: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anatuhakikishiaje wananchi wa Jimbo la Mtera kwamba upembuzi yakinifu utakaopelekea ujenzi wa lami ya barabara ile utaanza kufanyika?
Swali la pili, Naibu Waziri amejibu kwamba Serikali itaendelea kuitengeneza barabara ile kwa kiwango cha changarawe; barabara ile haijawahi kutengenezwa kwa kiwango hicho kwa muda mrefu. Je, kwa majibu hayo, Naibu Waziri anataka kutuhakikishia kwamba kwa maneno yake tu ya leo barabara ile imepandishwa hadhi na kuwa barabara ya Mkoa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikiri kwamba Mheshimiwa Livingstone Joseph Lusinde, ni mfuatiliaji mahiri. Nami namhakikishia kwamba kutokana na juhudi zake anazozifanya, hatimaye hilo analolitaka litatekelezwa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali lake la pili, naomba nimthibitishie kama nilivyosema kwenye swali langu la msingi kwamba hii barabara iko chini ya TAMISEMI na itaendelea kuhudumiwa chini ya TAMISEMI kwa maana ya Halmashauri. Haijapandishwa hadhi.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza kuhusu upembuzi yakinifu, kwa kuwa kuna ahadi ambayo viongozi wetu waliitoa, kazi hiyo ya upembuzi yakinifu itaanza ili kuweza kuitekeleza ahadi hiyo na hatutaanza mwaka ujao wa fedha kwa sababu bajeti imepeleka vipaumbele katika maeneo yale ambayo Serikali tayari ilikuwa na commitment, na tunataka kwanza tumalize hizi commitment, baada ya kumaliza tutarudi kuhakikisha ahadi zote za Viongozi wetu zinatekelezwa, ikiwa ni pamoja na ahadi hii ya kupeleka lami kwenye barabara inayokwenda katika Hospitali ya Mvumi Misheni.
MHE. KEMIREMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kumekuwa na uharibifu mkubwa sana wa barabara ya Mkoa wa Mwanza hususan barabara ya Mwaloni iendayo kwenye Soko la Kimataifa la samaki, Mkuyuni, Kiseke, Nyamongolo Bulale na Kishiri. Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kutengeneza barabara hizi, zenye umuhimu wa kiuchumi kwenye Jimbo la Ilemela na Nyamagana?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoiongelea ni barabara yetu sote; sisi Ujenzi na TAMISEMI; na kwa sasa iko chini ya TAMISEMI, lakini kazi tunaifanya kwa pamoja. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge, katika swali aliloliuliza kwamba tutafanya kazi kwa pamoja kati ya TANROAD Mkoa pamoja na wenzetu wa Halmashauri tuiangalie hii barabara ambayo inagusa eneo nyeti na muhimu la uvuvi ili tuweze kuiweka katika hali ambayo wavuvi wetu watapata fursa nzuri ya mawasiliano.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, tarehe 11/10/2014 ilikuwa siku ya Jumamosi saa 5.32; Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne wakiwa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano, walizindua daraja la Mto Simiyu kule Maligisu na kuahidi kwamba mita 50 kuingia kwenye daraja na mita 50 kutoka kwenye daraja itawekewa lami. sasa nataka kujua, je, ahadi hii ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa lini?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Richard Ndassa ni Mwalimu wangu. Naomba nimhakikishie kama ambavyo nimekuwa nikiongea naye kabla kwamba maungio haya ya daraja la Mto Simiyu kama ambavyo Viongozi wetu waliahidi, tutahakikisha tunayatekeleza. Naomba tu aendelee kutukumbusha, kwa kadri hapa ninavyoongea, wahusika wote kuanzia TANROAD Mkoa wa Simiyu, pamoja na Makao Makuu, wananisikia. Tuhakikishe hili daraja pamoja na barabara yake ambayo iliahidiwa, tuifanyie kazi kama ambavyo viongozi wetu waliahidi.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwanza nianze kwa kuipongeza Serikali kwa juhudi zake kubwa mnazofanya za kusambaza mawasiliano nchi nzima.
Kwa kuwa tatizo la mawasiliano katika Jimbo la Korogwe Vijijini ilikuwa ni Kata nyingi hazina mawasiliano; na kwa kuwa Serikali hii ni sikivu; kuna Kata ambazo hazina mawasiliano kabisa, kwa mfano, Kata ya Dindira katika Kijiji cha Kwefingo, Kata ya Chekelee katika Kijiji cha Bagai, Kata ya Mkalamo katika Vijiji vya Kweisewa na Toronto, Bungani na Kata ya Kerenge katika Kijiji cha Makumba:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini vijiji hivi navyo vitajengewa minara ili nao wanufaike na Serikali hii ya Awamu ya Tano?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumshukuru Mheshimiwa Stephen Hillary Ngonyani (Profesa Maji Marefu) kwa kunijulisha kwamba katika jibu langu la msingi la ujenzi wa mnara, ni kwamba kumbe tayari kazi imekamilika na umeme unawaka. Kilichobaki ni kutoa taarifa kwetu ili na sisi Wizara rekodi yetu tuweze kuirekebisha kuonesha kwamba umeme umewaka.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Profesa Maji Marefu na namhakikishia kwa kazi hii kubwa anayoifanya ya kufuatilia masuala haya na kutupa taarifa za uhakika katika maeneo mbalimbali ya eneo lake, kwa mfano: katika Kata ya Kerenge anafahamu mnara umejengwa katika Kijiji cha
Makumba, lakini vile vile Kata ya Dindira mnara umejengwa katika Kijiji cha Kwefingo ambacho ndiyo Makao Makuu ya Kata; anafahamu vile vile Kata ya Chekelei katika Kijiji cha Kwamkole nako mnara umejengwa; na mwisho Kata ya Mkalamo, Vijiji vya Kweisewa na Toronto Bungani, Minara imejengwa.
Hii yote hii ni kwa sababu ya juhudi zake za kufuatilia kwenye Makampuni yanayojenga minara; siyo Wizarani tu, bali na kwenye Makampuni yanayojenga minara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Ngonyani na naomba ajaribu kuambukiza hiki kitu anachokifanya katika eneo lake kwa Waheshimiwa Wabunge wengine na hasa mimi mwenyewe.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nami nakushukuru kwa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Matatizo haya ya mawasiliano yaliyopo katika Jimbo la Korogwe Vijijini, yako pia katika Jimbo langu la Wilaya ya Mkuranga katika Kata ya Panzuo, katika Vijiji vya Mkuruwili, Kibesa na Kibuyuni, Kisegese, Chamgoi; Kata ya Kitomondo katika Kijiji cha Mpera na Mitandara na katika Kata ya Bupu katika Kijiji cha Mamdi Mkongo, Mamdi Mpera na hata kule Tundu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sasa Mheshimiwa Waziri aniambie, ni lini wananchi hawa wa vijiji nilivyovitaja katika Wilaya ya Mkuranga watapata mawasiliano ili na wao waweze kuendeleza shughuli zao za kiuchumi na kijamii?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Ulega ameshaleta orodha ya hayo maeneo yote; kuanzia Kata ya Panzuo na hizo nyingine ambazo amezitaja katika Wizara yetu ili tuweze kuzifanyia kazi. Nami namhakikishia, orodha hiyo tumeipokea na tulishaiwasilisha kwenye Kampuni ya Viettel pamoja na UCSAF kwa maana ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote ili hatimaye watupe ratiba ya maeneo hayo yapangwe ratiba na bajeti kwa ajili ya kutekeleza kile ambacho Mheshimiwa Ulega anakipenda ili na wale wananchi wake waweze kunufaika na mawasiliano.
MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Wilaya ya Nachingwea tuna jumla ya Tarafa tano. Tarafa nne tayari zimeshafanikiwa kuwa na mitandao ya simu, lakini Tarafa moja ya Kilimarondo mpaka sasa hivi bado hamna mawasiliano ya uhakika na wako watu wa TTCL wameshafunga mitandao yao katika maeneo ya Kata ya Mbondo, Kegei pamoja na Kilimarondo.
Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka leo ninapozungumza ni mwaka wa tatu sasa, bado hawajawasha mitambo yao kwa ajili ya kutoa huduma. Naomba kuuliza swali. Nini mkakati wa Serikali juu ya kuhakikisha maeneo haya yanapata mawasiliano ya uhakika?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa namna anavyotupa moyo kuhusu uwekezaji uliofanywa na TTCL katika maeneo ya Jimbo lake. Namhakikishia kwamba kuanzia mwezi Septemba, TTCL itafanya mambo makubwa na nitahakikisha katika mambo haya makubwa yatakayofanywa kuanzia Septemba, 2016, eneo hili la Nachingwea ambapo tayari minara imeshajengwa litapewa kipaumbele.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Jimbo la Mheshimiwa Profesa Maji Marefu la Korogwe Vijijini ni pacha kabisa na Jimbo la Mbulu Vijijini kutokana na hali ya kukosa mawasiliano. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka mawasiliano kwenye Kata ya Ari, Tumati, Mung’ahai, Ng’orati, Masieda, Endagi, Chani kule Mbulu Vijijini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Massay alileta hiyo orodha na tuliongea na tena siyo na mimi tu, nilimpeleka na kwa Mheshimiwa Waziri. Naomba kumhakikishia tena, siyo pale ofisini tu, hata na hapa. Sina tatizo, yeye aendelee tu kufuatilia, maana amefuatilia mara nne kuhusu suala hilo hilo, nami nampongeza sana kwenye hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba tutatekeleza na tutafuatilia utekelezaji wa mawasiliano katika eneo hili la Mbulu Vijijini kama ambavyo tunafanya katika maeneo mengine na kwako nilikuahidi nitakuja. Siyo kwa
sababu hii tu, ni pamoja na ile barabara inayopitia Mbuyu wa Mjerumani mpaka lile eneo lako. Nilikuahidi na ninahakikisha nitalitekeleza.
MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza ambayo akinijibu vizuri basi nitaridhika zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Sheria hii ya Cyber Crime hasa ibara ya 39, inampa mamlaka Waziri ya kuamua kutoa au kuruhusu content gani iingie katika mitandao, lakini matusi, kejeli, picha za ngono zimeendelea kuwepo katika mitandao na Waziri hafanyi jambo lolote lile. Sasa naomba kuuliza, je, Waziri huyu anaangalia computer kama kazi yake inavyomtaka au naye amejikita katika makazi mengine ili tuweze kujua hapa kama sheria hii ina uzuri au ina upungufu wake?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Sheria ya Mtandao inampa nafasi pia Mkuu wa Kituo cha Polisi chochote kile kuweza kukamata computer, kukamata mali za mtu ambazo zinahusiana na hilo ambalo yeye analisema ni kosa. Je, Mheshimiwa Waziri, haoni kwamba hapa sasa ndipo tunapoanza kuharibikiwa baada ya kutumia njia halali ya kimahakama kupata ile order ya kukamata mali za watu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, mamlaka aliyopewa Waziri anayehusika na masuala ya mawasiliano si kama yalivyotafsiriwa na Mheshimiwa Kikwete. Isipokuwa pale
inapotokea malalamiko ndipo vifungu hivi vinapotokea. Pamoja na kwamba yeye anadhani masuala haya yanaendelea lakini nimempa taarifa kwamba masuala haya yamekuwa yakipungua sana. Kwa mfano, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, matukio yalikuwa 459 yaliyoripotiwa Polisi, maana yake kuna watu waliolalamika kuhusu matukio hayo wakaripoti Polisi; matukio 459, lakini baada ya sheria kuanza hakukuwa na tukio lolote lililoripotiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mambo yanaweza yakawa yanaendelea lakini kinachoangaliwa hapa ni yule anayetendewa; anapoona kwamba amekosewa anatakiwa atoe taarifa Polisi ili Polisi wachukue hatua. Hivyo vifungu vilivyotajwa vya Mheshimiwa Waziri na hicho cha Polisi ndivyo vinavyotumika. Si kazi ya Polisi kupita kwenye makompyuta na kutafuta makosa hayo, hapana! Kazi ya Polisi ni kupokea malalamiko na ndipo kuyafanyia kazi na kutafuta ushahidi kwa mujibu wa sheria ilivyotungwa.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na kwamba sheria hii ni nzuri lakini naamini kwamba bado elimu haijatolewa vizuri kwa wananchi hasa walioko pembezoni. Naibu Waziri, ningependa kujua, kwamba kumekuwa pia na tabia ya watu wahalifu ambao wanatumia namba za simu za watu wengine kwa kuwaibia watu wengine. Ukienda kwenye truecaller unakuta ni jina la Martha Mlata na namba ni ya kwake lakini aliyetumia ni mtu mwingine, je, hili nalo anatuambia nini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, sababu mojawapo kubwa ya kutaka kutekeleza kuondoa simu feki ni pamoja na hilo ambalo Mheshimiwa Martha Mlata amelieleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwamba ukiwa na simu feki, makosa haya yanapotendeka si rahisi Polisi ku-trace, inakuwa ngumu sana kufuatilia tukio hilo lilipotokea kwa sababu zile simu feki hazijawa registered na haziwezi kuwa registered kwa sababu utengenezaji ni tofauti na jinsi ilivyoandikwa na hakuna namba ya utambulisho katika zile simu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo ndugu zangu, ili tuweze kuhakikisha kazi hii tunaifanya kwa ukamilifu na kwa uzuri zaidi, nawaomba sana tuwahimize ndugu zetu wahakikishe simu zote zinasajiliwa na zile ambazo hazijatoka katika watengenezaji rasmi na hazina namba za utambulisho nafahamu kwamba kuanzia tarehe 16 saa sita usiku zitaondolewa katika matumizi. Lengo kubwa ni ku-improve katika utekelezaji wa haya ambayo Mheshimiwa Mlata ameeleza.
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza sijaridhika na majibu ambayo amenipa Mheshimiwa Naibu Waziri kwa sababu kusema hii barabara inapitika kila wakati si kweli! Barabara hii mwaka wa jana mzima ilikuwa ni barabara mbovu imejaa mashimo, magari yote yanayopita barabara ile yanaharibika sana. Kwa hiyo, kuna taarifa ambazo wamekuwa wakiletewa ambazo si sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri. Swali la kwanza; je, yuko tayari yeye mwenyewe binafsi kwenda kuitembelea barabara ile na kuiona ili aone umuhimu wake kwa sababu taarifa ambazo wamekuwa wanaletewa sio za kweli?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Rais akiwa pale Nkwenda kwenye kampeni aliiona barabara ile ikiwa na umuhimu kwa kuwa barabara hii inapita katikati ya Wilaya. Aliahidi kutupa kilometa 20 akiingia tu madarakani. Hizo kilometa 20 zinaanza kujengwa lini? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri kwamba miongoni mwa Wabunge ambao wanakuja ofisini kila wakati kufuatilia ni pamoja na Mheshimiwa Bilakwate. Mheshimiwa Bilakwate ameifuatilia barabara hii na tumekuwa tukijaribu kuangalia katika hizi barabara mbili zote zinaanzia karibu sehemu moja kuishia karibu sehemu moja. Suala ni ipi kati ya hizi mbili ni muhimu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi kilichopita kama ambavyo tumeongea ofisini, ni kwamba uongozi wa Mkoa pamoja na Mbunge aliyepita waliona kwamba hii barabara ya kupitia Kigarama ndiyo ipewe umuhimu wa kwanza na hii ya kupitia Omurushaka nayo wakati Mheshimiwa Rais alipokuwa kule aliipa kipaumbele. Kwa hiyo, barabara zote mbili sisi kama Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano tumezichukua kwa umuhimu wake. Tutaanza na hii ambayo tumeshaanza kufanya kazi, tukiimaliza hii tutakuja kukamilisha hii nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati tunasubiri kuanza hii ya pili ambayo ndiyo anayoifuatilia kwa umakini sana Mheshimiwa, tunamwomba sana akubali kwamba ile kazi tunayoifanya kwanza ya kuimarisha ule mlima maana tatizo kubwa liko pale mlimani hasa. Ombi lake la kwanza nalikubali, nitakuwepo naye huko, tukaongee na wananchi kuthibitisha ahadi ya kiongozi wetu mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini wakati huo huo afahamu mazingira tuliyonayo kutokana na hizi barabara mbili ambazo zote zinaonekana zina kipaumbele lakini viongozi wa Mkoa na Mbunge aliyepita inaonekana hiyo nyingine ndiyo waliitanguliza zaidi. Sasa ni suala la kutafuta namna gani zote mbili twende nazo kwa sababu zote zina umuhimu wa pekee na zinatoa huduma kubwa.
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Wakati wa kampeni, Mheshimiwa Rais aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Singida Mjini kwamba atajenga barabara kwa kiwango cha lami ya kuunganisha Kata zote za pembeni. Sasa, je, mchakato huu wa kujenga barabara utaanza lini? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumepewa ahadi zote ambazo viongozi wetu, Mheshimiwa Rais, Mheshimiwa Makamu wa Rais, walizitoa sehemu mbalimbali za nchi, ahadi zote tunazo. Tulichowekea fedha ili tuweze kuanza kutekeleza katika mwaka huu wa kwanza tunaoanza ni zile barabara ambazo zilishaanza kufanyiwa kazi toka zamani na wakandarasi wako site.
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani tutakubaliana kwamba ni vyema tukamaliza kwanza ile kazi iliyoanza siku nyingi za nyuma ili wakandarasi wasiendelee kupata fedha bila kufanyia kazi kwa kutopewa fedha za ujenzi na hivyo wanaendelea kukaa pale bila kufanya kazi na tunalazimika kuwalipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kipaumbele cha kwanza ni kukamilisha barabara ambazo zilianza. Nawahakikishieni Waheshimiwa Wabunge kwamba barabara zote ambazo Mheshimiwa Rais pamoja na Mheshimiwa Makamu wa Rais waliziahidi na bahati nzuri tumeshazipata, tutahakikisha tunazipangia ratiba ya utekelezaji katika kipindi kitakachofuata.
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Barabara ya kutoka Mbeya hadi Mkiwa inaunganisha Mikoa mitatu ya Mbeya, Tabora na Singida na iliamuliwa kujengwa miaka 10 iliyopita. Sasa kipande cha kutoka Chunya hadi Itigi kitakamilika lini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoingelea Mheshimiwa Mbunge imepangwa katika bajeti ya mwaka huu utakaoanza Julai. Kwa kweli nawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wameipitisha bajeti. Hivyo, ni wajibu wetu kuhakikisha bajeti hiyo tunaisimamia ili itekelezwe kama ilivyopangwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kusema ni lini barabara hii itakamilika, namwomba sana Mheshimiwa Mbunge atupe subira kwa sababu hivi vitu ni vya kitaalam, vinatakiwa vifuatane na mikataba ilivyo. Namhakikishia kwamba barabara hii itakamilika – hilo ndilo la msingi. Lini hasa; nadhani tusiende sana kwa undani kiasi hicho ili baadaye tukaja kushikana uongo hapa.
MHE. STELLA I. ALEX: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa suala la ujenzi wa barabara linaenda sambamba na uwekwaji wa alama za barabarani na kwa kuwa tayari Serikali imeshaanza kuweka alama hizi za barabarani kwa ajili ya watu wenye ulemavu kwa baadhi ya mikoa, kwa mfano Tanga, je, nini mpango wa Serikali kwa mikoa mingine?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba alama zote tunazoweka barabarani zinazingatia mahitaji maalum ya walemavu. Naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge na najua ameshakutana na Waziri wangu pamoja na wawakilishi wa walemavu ambao walikuja hapa Dodoma na wamelizungumzia hili suala kwa undani.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru kwa juhudi anazozifanya za kufuatilia mahitaji ya walemavu. Nina hakika kwa namna ambavyo ameanza tutafika mahali kila barabara ambayo walemavu wanaihitaji, tutaiwekea hayo mahitaji maalum kadri uwezo wa fedha utakavyokuwa unapatikana.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, majibu yenye matumani makubwa katika Mkoa wetu wa Lindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niipongeze Serikali kwa kuanzisha Mfuko huu wa UCSAF. Kwa utekelezaji wake katika Mkoa wetu wa Lindi ni kata 25 na vijiji 99 ambavyo tunavitarajia vianze kupata mawasiliano. Ningependa kujua ni kwa namna gani Serikali watapeleka msukumo kwa watoa huduma hii ya mawasiliano ili vijiji hivi 99 na kata 25 za Mkoa wa Lindi ziweze kupata mawasiliano?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi zake za kufuatilia suala hili. Alikuja ofisini na alikutana na Waziri wangu na kwa kweli pamoja na Wabunge wengine wa Mkoa wa Lindi wanalifuatilia sana suala hili ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuthibitisha kwamba tutayafuatilia haya makampuni yanayotoa huduma. Kwa wale ambao hawana huduma za kutosha tutahakikisha UCSAF inaingilia ili yapatikane mawasiliano kama ambavyo tumekusudia kutoa mawasiliano kwa vijiji vyote vya Tanzania.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri samahani kidogo. Mheshimiwa kule nyuma umesimama sijaelewa. Mheshimiwa Naibu Waziri naomba umalizie.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema kwamba tutazifuatilia hizi kampuni kuhakikisha kwamba zinatimiza wajibu wake wa kupeleka mawasiliano katika vijiji husika vya Mkoa wa Lindi vyote 99 katika kata 25 pamoja na vijiji vyote Tanzania nzima.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mlele, Kata ya Ilunde imesahaulika kabisa kwa mawasiliano. Je, Serikalini ni lini watapeleka mawasiliano Kata ya Ilunde?
NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, tunakusudia kupeleka mawasiliano vijiji vyote Tanzania nzima. Namhakikishia hicho Kijiji cha Ilunde kitapata mawasiliano. Kumwambia lini, naomba anipe muda zaidi niwasiliane na yule mtu anayehusika kupeleka mawasiliano tupate uhakika, nitakuja kujibu nikishapata majibu sahihi. Namhakikishia mawasiliano yatapatikana katika kata hiyo na nitafuatilia kwa makini. Nakushukuru sana kwa juhudi zako za kufuatilia suala hili.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Lindi yanafanana kabisa na yaliyopo katika Mkoa wa Morogoro kwenye Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki hasa kwenye Kata za Maturi, Mkulazi, Seregeti na Tununguo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka minara katika kata hizi na Vijiji vyake vile vya Usungura, Kidunda na vinginevyo ili kuimarisha mawasiliano katika vijiji hivyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tena kuchukua fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kama nilivyotoa maelezo katika jibu la swali la msingi kwamba tuna dhamira ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata mawasiliano. Kwa hiyo, naomba kuchukua fursa hii kumhakikishia kwamba tutafuatilia kuhakikisha katika Jimbo lake na hizo kata alizozitaja, mawasiliano ya simu yanapatikana kupitia Mic, Airtel, Tigo, Vodacom, Viettel pamoja na wengine ambao wanakuja karibuni tutakapotoa tenda ya masafa ya mawasiliano.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa ambayo iko pembezoni na viko vijiji ambavyo vimepakana na nchi jirani ya Burundi na vijiji hivyo havina mawasiliano. Je, Serikali iko tayari kushawishi makampuni kupeleka minara katika Vijiji vya Kitanga (Kasulu), Kilelema (Buhigwe) na Nyagwijima (Kibondo)?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tupo tayari na kwa kweli ndicho tunachokifanya siku zote hizi. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba katika suala la mawasiliano mipakani ni priority namba moja.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mlele, Kata ya Ilunde imesahaulika kabisa kwa mawasiliano. Je, Serikalini ni lini watapeleka mawasiliano Kata ya Ilunde?
NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, tunakusudia kupeleka mawasiliano vijiji vyote Tanzania nzima. Namhakikishia hicho Kijiji cha Ilunde kitapata mawasiliano. Kumwambia lini, naomba anipe muda zaidi niwasiliane na yule mtu anayehusika kupeleka mawasiliano tupate uhakika, nitakuja kujibu nikishapata majibu sahihi. Namhakikishia mawasiliano yatapatikana katika kata hiyo na nitafuatilia kwa makini. Nakushukuru sana kwa juhudi zako za kufuatilia suala hili.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Lindi yanafanana kabisa na yaliyopo katika Mkoa wa Morogoro kwenye Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki hasa kwenye Kata za Maturi, Mkulazi, Seregeti na Tununguo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka minara katika kata hizi na Vijiji vyake vile vya Usungura, Kidunda na vinginevyo ili kuimarisha mawasiliano katika vijiji hivyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tena kuchukua fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kama nilivyotoa maelezo katika jibu la swali la msingi kwamba tuna dhamira ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata mawasiliano. Kwa hiyo, naomba kuchukua fursa hii kumhakikishia kwamba tutafuatilia kuhakikisha katika Jimbo lake na hizo kata alizozitaja, mawasiliano ya simu yanapatikana kupitia Mic, Airtel, Tigo, Vodacom, Viettel pamoja na wengine ambao wanakuja karibuni tutakapotoa tenda ya masafa ya mawasiliano.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa ambayo iko pembezoni na viko vijiji ambavyo vimepakana na nchi jirani ya Burundi na vijiji hivyo havina mawasiliano. Je, Serikali iko tayari kushawishi makampuni kupeleka minara katika Vijiji vya Kitanga (Kasulu), Kilelema (Buhigwe) na Nyagwijima (Kibondo)?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tupo tayari na kwa kweli ndicho tunachokifanya siku zote hizi. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba katika suala la mawasiliano mipakani ni priority namba moja.
MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa majibu yaliyotolewa hapa na kwa niaba ya watu wa Ukerewe ambao Mbunge wao anaumwa ameniomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, barabara hii imeanza kujengwa mwaka 2013 mpaka leo ni zaidi ya miaka minne barabara iko asilimia 14 na Serikali inakiri hapa kwamba ujenzi unasuasua. Hii ni barabara inayounganisha Mkoa kwa Mkoa wala hata siyo Wilaya kwa Wilaya. Sasa ni lini au ni miaka mingapi, kwa sababu tukigawa hapa asilimia 85 iliyobaki ni miaka zaidi ya sita, ina maana mtoto azaliwe leo afikishe miaka sita aanze shule hamjamaliza barabara ambayo mmeanza kujenga miaka 13. Ni lini mnamaliza ujenzi wa barabara hii ambayo inaunganisha Mkoa kwa Mkoa msaidie watu wa Ukerewe? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili, mara nyingi tumeuliza hapa hilo swali Waziri, barabara ya kutoka Tarime Mjini - Nyamwaga - Nyamongo - Serengeti ambayo inapita kwenye Mgodi wa Nyamongo ambapo kila siku pale Serikali inapata pesa nyingi za wananchi wa Tarime. Ni lini mtaijenga barabara hii ili wale watu na wao wafurahie maisha kwamba ndiyo wanaotoa dhahabu inayochangia kwenye ujenzi wa miundombinu hii?
NAIBU WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, lini tunamaliza kujenga hiyo barabara siyo rahisi kumwambia lini, lakini anafahamu kwamba barabara hii ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 - 2020. Ni ahadi yetu na Mheshimiwa Mbunge anafahamu Serikali hii ya Awamu ya Tano ikiahidi inatekeleza.Kwa hiyo, mimi namhakikishia barabara hii itakamilika katika kipindi hiki cha miaka mitatu na anafahamu fedha hizi zinatokana na kodi ambazo tunakusanya. Mheshimiwa Mbunge ajitahidi tukusanye kodi nyingi barabara hii tuikamilishe kwa muda ambao yeye na mimi tutakubaliana.
Swali la pili kuhusu barabara ya Tarime - Nyamwaga - Nyamongo - Serengeti nayo anafahamu ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020. Vilevile anafahamu kwamba tumeshaanza kazi, naomba aiamini Serikali hii, kazi hii tutaifanya. Sisi tuliopata dhamana ya kusimamia ujenzi wa barabara hii tunamhakikishia tutaijenga kwa kadri fedha tutakavyozipata.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri na naishukuru Serikali kwa ujenzi wa kilometa moja lakini pamoja na majiibu hayo ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa kwa mujibu wa jibu la msingi kwamba kiwango cha kilometa 24 zilizobaki zinahitaji malipo ya fidia na kwa kuwa tarehe 7 Septemba, 2016 tulifanya kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa na taarifa ilitolewa kwamba takribani shilingi bilioni nane zitatakiwa kwa ajili ya fidia. Je, Serikali haioni kwa kuwa kiwango ni kikubwa kuongeza kama kilometa tano za ujenzi wa barabara hii kwenye eneo la viwanda kwenye maeneo hayo Kibaha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa ujenzi wa barabara hii ni ahadi ya Serikali ya Awamu ya Nne na kwa kuwa zipo ahadi mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ambazo hazikukamilika kwa Awamu ya Nne, je, Wizara haioni imefika wakati sasa iunde timu ya tathmini ya ahadi zote ambazo hazikutekelezwa ili ziweze kutekelezwa awamu hii na hususani kuanzia mwaka ujao wa fedha na kuendelea? Ahsante.
NAIBU WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Subira Mgalu kwa kufuatilia mambo mbalimbali ya Mkoa mzima wa Pwani, hongera sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hilo la viwanda la kilometa tano analoliongelea mimi namhakikishia ujenzi utaanza kama nilivyosema katika jibu langu la msingi mara tutakapopata zile fedha za fidia na kuwaondoa wale watu ambao wanatakiwa wafidiwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la tathmini ya ahadi ambazo hazijatekelezwa na viongozi wakuu, kwanza naomba nimhakikishie ahadi zote za viongozi wetu wakuu wa Serikali ya Awamu ya Nne na Serikali ya Awamu ya Tano orodha tunayo. Namhakikishia Serikali hii ya Awamu ya Tano kazi yake kubwa ni kuhakikisha kwamba ahadi zote za viongozi wakuu wa kuanzia Serikali za nyuma zinatekelezwa kikamilifu. Nitamshirikisha kumuonesha orodha kamili ya ahadi ambao zilitolewa na Awamu ya Tatu, Nne na Tano katika Mkoa wa Pwani
ili aelewe ninachokisema kwamba tuna dhamira ya dhati kuhakikisha ahadi za viongozi wetu zinatekelezwa.
MHE. MIZA BAKARI HAJI: Mheshimiwa Spika, asante na mimi nina swali moja la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani mbadala ya kuwaepuka Wakandarasi wa aina hii ambao wanaleta usumbufu mkubwa kwa wananchi na hasara kubwa kwa Taifa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Miza Bakari Haji kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuifuatilia kwa ukaribu sana sekta hii ya ujenzi, naomba nimhakikishie kwamba Serikali yetu iko makini kuhakikisha inafuatilia utekelezaji wa mikataba. Kwa sasa tunahakikisha mikataba yote inaziba mianya yote ya kumpa mtu unafuu wa kuja kuharibu baadaye na akaja akadai analindwa na mikataba. Kwa hiyo, tuna hakikisha mikataba tunaiweka sawasawa na tutakapogundua yeyote ambaye uwezo wake, tatizo siyo mikataba tatizo ni uwezo wake huwa tunamzuia hapati miradi tena mingine.
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Sambamba na majibu aliyotoa Mheshimiwa Naibu Waziri ninaomba awahakikishie wananchi wa Sikonge ambao wamekuwa hawaridhiki na matengenezo ya barabara ya Sikonge - Mibono hadi Kipili ambayo wakandarasi wamekuwa wakitengeneza kipande cha Sikonge hadi Mibono na kuacha kipande cha Mibono hadi Kipili bila matengenezoya aina yoyote kiasi ambacho haipitiki kila mwaka. Kwa sababu mwaka huu imepangiwa shilingi milioni 892 anawahakikishiaje wananchi wa Sikonge kwamba mwaka huu itatengenezwa kwa kiwango bora mpaka mwisho wa barabara ya Kipili?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge, pamoja na wananchi wa Sikonge kwamba fedha hizo zilizotengwa ni kwa ajili ya pamoja na kipande cha Mibono hadi Kipili na tutahakikisha tunasimamia ili barabara hiyo itengenezwe kwa kiwango kizuri kama ambavyo imetengenezwa eneo la Sikonge hadi Mibono.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa miongoni mwa sababu ambazo Mheshimiwa Naibu Waziri amezitaja, ambazo zinasababisha uharibifu wa barabara, magari na wakandarasi wasio waaminifu, sababu kubwa mwaka huu iliyosababisha barabara zetu kuharibika ni mvua za masika ambazo hazikutegemewa.
Mheshimiwa Spika, Serikali ilitoa kauli humu ndani katika Bunge la Bajeti kwamba TANROADS watoe fedha katika Halmashauri zetu kwa sababu ni dharura, wasaidie Halmashauri kujenga hizo barabara. Naomba nifahamu hii kauli ya Serikali imetekelezwa kwa kiwango gani, hususan katika Mkoa wangu wa Manyara na Jimbo la Babati Mjini maana hizo barabara hazijatengenezwa kabisa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwa uelewa wangu kauli ambazo tulikuwa tunazitoa kati ya mwezi wa nne na mwezi wa sita kuhusu kuwataka Regional Managers wote wa TANROADS kuhakikisha wanarudisha mawasiliano katika barabara zilizokatika yalitekelezwa. Kwa kuwa anahitaji takwimu, naomba anipe muda nichunguze katika eneo lake kama kulitokea tatizo lolote, ili tuweze kulirekebisha.
MHE. WILLIAM D. NKURUA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kupata nafasi tena ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa barabara hii ya kutoka Nangomba kwenda Nanyumbu imetolewa majibu ambayo yanatia moyo na sina mashaka kabisa na ahadi zinazotolewa na Serikali ya Awamu ya Tano; lakini kwa kuwa barabara hii inaunga barabara kubwa inayotoka Songea mpaka Mtwara, kwa jina maarufu inaitwa Mtwara Corridor. Barabara hii kutoka Songea mpaka pale ilipo mizani, Mnazi Mmoja ni zaidi ya kilometa 500.
Je, kwa kuwa Mangaka pana pacha ya kuelekea Msumbiji, Serikali haioni umuhimu wa kuweka pale mizani ili kuweza kudhibiti magari yote yaelekeayo Msumbiji na Mbamba Bay ili kulinda barabara zetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO Mheshimiwa Spika, nimepata taarifa hiyo kwamba kuna mchezo unafanywa na wasafirishaji wanaotumia magari makubwa kusafirisha bidhaa kutoka Songea kwenda Mtwara kwa sababu hakuna mizani kati ya Songea hadi Mangaka, hivyo wanabeba mizigo mikubwa, wanapofika Mangaka au kukaribia Masasi huwa wanapunguza mizigo kwa sababu mbele watakutana na mizani.
Mheshimiwa Spika, nimepata hiyo taarifa na ninaomba kuchukua nafasi hii kuwaagiza TANROADS wahakikishe wanaangalia mahali gani waanze kuweka mizani ya kutembea ili tuanze kudhibiti wakati kituo maalum cha kuweka mizani kitakapokamilika.
Mheshimiwa Spika, nafahamu kwa sasa sehemu mbalimbali za vipande hivi vya barabara kati ya Mtambaswala, Mangaka hadi Songea havijakamilika. Inawezekana kwamba mahitaji hayo ya kuweka mizani yatafanyika baada ya kukamilika kwa wakandarasi wote katika barabara hiyo ya Mtwara Corridor. Ninaomba kazi hiyo ya kuweka mizani inayotembea (mobile) ifanyike haraka ili kuweza kuhakikisha kwamba barabara zetu hazianzi kuharibika kabla kazi haijakamilika. (Makofi)
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa fursa niulize swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa shida ya Nanyumbu na maeneo yaliyotajwa ni sawa na shida iliyopo Jimbo la Ukonga Dar es Salaam, ningependa kujua kauli ya Serikali kwamba barabara ya kuoka Banana – Kitunda – Kivule – Msongola ambayo imeahidiwa takribani ni awamu ya tatu, kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami, pamoja na Majimbo yote Mkoa wa Dar es Salaam ikizingatiwa kwamba Wabunge wengi humu ndani wanakaa Dar es Salaam na Majimbo yao yana hali mbaya sana ya barabara hasa wakati wa mvua.
Ni lini barabara hiyo itakamilika? Nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, barabara ya Banana – Kitunda – Kivule na kuendelea ni kati ya barabara ambazo zipo katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 hadi 2020 kama ilivyo barabara ya Kongwa – Mbande ambayo Serikali imedhamiria kuijenga kwa kiwango cha lami katika kipindi hiki cha miaka mitano.
Mheshimiwa Spika, ninamhakikishia Mheshimiwa Mwita Waitara barabara hii kama sehemu ya ring roads za Dar es Salaam na kama ilivyoahidiwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi, tutaijenga kwa kiwango cha lami kama tulivyoahidi. Suala la lini, naomba sana katika masuala ya ujenzi wa barabara ni miradi mikubwa siyo rahisi sana kutoa tarehe.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Spika, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne alipofika Lushoto alituahidi kilometa nne za barabara ya lami.
Je, Serikali ina mpango gani wa kutekeleza ahadi hiyo iliyotolewa na Rais Mstaafu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, hicho kiwango cha kilometa nne ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne, na kama ambavyo nimekuwa nikisema kila wakati, dhamana tuliyopewa ni kuhakikisha tunatekeleza ahadi zote za viongozi wetu.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba kazi hii itafanyika katika kipindi hiki cha miaka mitano, kama ambavyo tumeongea huko nyuma na ninamsifu sana Mheshimiwa Shekilindi kwa kufuatilia, tutalitekeleza kama ambavyo nimekwambia huko nyuma.
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa fursa ya kumjibu Mheshimiwa Shekilindi. (Makofi)
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu na kwa kuwa mimi ni msema kweli daima napenda niseme sijaridhika na majibu hayo; na kwa kuwa, Serikali yetu hii ya Awamu ya Tano imejikita zaidi kuwaondolea dhiki wanyonge na wanyonge wa Zanzibar pamoja na Tanzania Bara bado wanapata dhiki katika suala hili, nipende kusema na kumwambia Waziri kwamba ni kwa kiasi gani Serikali itaongeza udhibiti wa mamlaka husika kwa kuhakikisha kwamba bei hizi zinapungua na wananchi wanapata nafuu.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa haiingii akilini Mhesimiwa Waziri anaposema kwamba mtu anayetaka kufanya safari afanye booking siku nne au siku ngapi hizo zote anazoziona yeye; kwa kuwa safari nyingine ni za dharura sana. Kwa mfano, watu wanapokuja huku Bara ni kwa ajili ya kupata tiba katika Hospitali ya Rufaa, pengine Muhimbili, pengine Kituo cha Cancer Ocean Road na mambo mengine ya dharura mtu anapoumwa unapomwambia akafanye booking ya siku nne ili apate nafuu ya ndege nafikiri hiyo siyo sahihi.
Mheshimiwa Spika, kwa hivyo, Mheshimiwa Waziri bado atilie mkazo katika mamlaka hizi pamoja na hivyo vyombo vya pwani, bado nauli hii bado ni kubwa sana kwa wanyonge…
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante, nataka majibu ya maswali yangu hayo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kukubaliana na maelezo yaliyotolewa na Mheshimiwa Asha Abdullah Juma na ninamhakikishia kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwamba tutafute muda twende wote Zanzibar tukakutane na Zanzibar Maritime Authority, ili tukalijadili hilo kwa undani, hatimaye mamlaka hizo mbili za Muungano, mamlaka iliyoko upande wa Zanzibar na mamlaka iliyoko upande wa Tanzania Bara ziweze kutekeleza majukumu yake kama ambavyo Mheshimiwa Asha Abdullah Juma amependekeza. (Makofi)
MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Naibu Waziri, bado hayajaridhisha. Nchini kwetu safari za ndani ni ghali kuliko safari za kwenda nje ya nchi. Hii imekuwa ni kero kubwa sana kwa wananchi wetu. Je, Serikali haioni umuhimu sasa wa kushirikiana na mamlaka hiyo ili kuweka kiwango maalum kisizidi hiyo bei kwa ajili ya kurahisisha usafiri kwa wananchi wetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, tuliamua na kupitia Bunge hili kwamba turuhusu ushindani na ndivyo tulivyofanya. Kupanga viwango kwa mamlaka zetu maana yake ni kutoka katika kile tulichoamua awali na mimi sina matatizo kama Bunge hili na Serikali kwa ujumla itaamua.
Kwa maoni yangu ni vema ngoja tuimarishe Shirika letu la Ndege la Air Tanzania na mnafahamu tumeanza kuliimarisha, litaingiza ushindani mkubwa na mimi nina uhakika hao sasa hivi ambao wamepanga viwango vya juu watalazimika kuvishusha ama kuondoka katika biashara hiyo na kuliacha shirika letu likitamba. (Makofi)
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nichukue nafasi hii kuuliza maswali madogo mawili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa kilio cha barabara ya Mbuyu wa Mjerumani – Magara – Mbulu ni ya muda mrefu na kwa kuwa barabara hii ndiyo inaunganisha Mji wa Babati na Mji wa Arusha kwa ajili ya wananchi wa Mbulu na kwa kuwa taarifa anayosoma Mheshimiwa Naibu Waziri ni taarifa aliyoandikiwa; wakati wa bajeti tulikubaliana fedha zote, karibu shilingi bilioni moja na milioni 200 zitumike kujenga daraja la Magara, na kwa sasa fedha zinazozungumzwa, shilingi milioni 300, ni hela ndogo sana.
Je, ni lini Naibu Waziri au Waziri mwenyewe mwenye dhamana ya Wizara hii atafanya ziara kujionea hali halisi ya mateso wanayopata wananchi wa Mji wa Mbulu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni katika uwanja wa Mbulu Mjini, aliahidi kuweka kilometa tano za lami katika Mji wa Mbulu kutokana na Mji wa Mbulu kuwa Mji mkongwe sana na kwa kuwa Rais aliahidi kwamba ahadi hii itatekelezwa katika bajeti ya mwaka 2015/2016.
Je, ni kitu gani kilipelekea ahadi ile isitekelezwe mpaka leo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi mwenyewe nitakuwa nimefika katika hiyo barabara na nitakujulisha lini, lakini kwa vyovyote itakuwa ni kabla ya mwezi Januari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili, ni suala la ukosefu wa fedha ndilo lililosababisha kipindi kilichopita kilometa tano za barabara hiyo zilizoahidiwa zisijengwe.
Naomba tu nikuhakikishie kwamba tunachukua kwa umuhimu mkubwa na tutaitekeleza hii ahadi ambayo Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne pamoja na wakati huo alikuwa Waziri wa Ujenzi walizitoa, nikuhakikishie kwamba tutazitekeleza.
MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa katika barabara hii korofi kipindi chake cha kuharibika sasa kimekaribia, kipindi cha mvua ambacho katika maeneo ya Lulanga, Itagata, Ukimbu, Mitundu, Kiombo, Mwamaluku, Mwamagembe, Kintanula hadi Rungwa udongo huo aliousema ni mbaya na ukarabati uliofanyika kipindi cha nyuma ulikuwa haukidhi kiwango. Je, sasa Serikali iko tayari kufanya marekebisho ya kutosha katika kipindi hiki kabla mvua hazijaanza?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; katika ujenzi wa kipande hiki cha kilometa 57 ambacho Meshimiwa Naibu Waziri amekisemea hapa, watakapoanza wanatarajia ni muda gani utachukua kukamilika? Maana yake wananchi wanahamu kubwa ya kuona barabara ya lami katika kipande hiki nikiwemo mimi Mbunge wao.
Mhesshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba, baada ya Bunge hili nitakuwa na safari ya kuipitia barabara hii. Nitamjulisha Mheshimiwa Mbunge tarehe kamili nitakapokuwa katika eneo lake ili tusaidiane kutambua kwa karibu zaidi na kwa macho siyo kuandikiwa tu, hatimaye tuhakikishe tunaposimamia hatua za marekebisho ambazo Mheshimiwa Mbunge anazihitaji tuweze kuzisimamia vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu lini tutakamilisha, nimwombe Mheshimiwa Mbunge ajue dhamira ya Serikali hii ya kuikamilisha hii barabara, aone kama ambavyo tumejibu katika swali la msingi maeneo ambayo tayari tumeyakamilisha na tupo katika kuendelea kukamilisha maeneo yaliyobaki. Naomba atuamini, kusema ni lini huwa naogopa sana kwa kazi hizi za ujenzi ambazo zina process, lazima upate hela na hatimaye ujihakikishie kipande gani kinakamilika kwa wakati gani. Naomba aniwie radhi kwamba hiyo kazi ya kusema lini hasa siyo rahisi sana. Kikubwa tuna dhamira ya dhati na tutakamilisha kujenga hii barabara kama ambavyo kwenye Ilani imeeleza. Ahsante.
MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza nakubaliana na Mheshimiwa Naibu Waziri kuwa kutokana na mchango mkubwa wa maendeleo wa Taifa wa Baba Hayati Mwalimu Nyerere ni mkubwa nikiri hivyo, lakini nataka kuweka Hansard sawa. Rais Marehemu Aboud Jumbe ni Rais aliyefungua demokrasia mwanzo Zanzibar ikiwemo Baraza la Wawakilishi la Katiba ya Zanzibar. Lakini kumbukumbu nyingi zinaonyesha Baba Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere anazo ikiwemo Ukumbi wa Mkutano wa Kimataifa, Dar es Salaam, Uwanja wa Ndege wa Kimataifa kuitwa jina lake, Mfuko wa Taasisi ya Fedha, kuna barabara hata Zanzibar zipo zinaitwa Baba Nyerere. Leo kweli tunamtendea haki Hayati Aboud Jumbe Mwinyi mtu aliyeishi karibu miaka 32 na kila mmoja Mtanzania anajua aliishi kule Kigamboni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuteleza siyo kuanguka, kutokuwa na meno siyo uzee, je, Serikali imesema ipo tayari kuchukua mapendekezo yangu na kubadilisha jina hilo? Hilo la kwanza.
Pili, je, kwa nini Serikali haikutafakari mapema na badala yake Serikali inasubiri mapendekezo kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge. Lini Serikali ya Jamhuri ya Muungano itawaenzi viongozi wetu kwa kuweka historia katika kumbukumbu ili vizazi vijavyo vikaja kuwa na historia hiyo.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hakuna ambaye hatambui michango ya viongozi wetu wa Kitaifa wote, nimwombe tu, bahati nzuri yeye ni Mbunge wa Baraza la Wawakilishi na nina hakika anafahamu kwamba tuna forum kati ya Serikali hizi mbili, tuombe tuzitumie zile forum kama kuna kitu anadhani kina tatizo, tuweze kukijadili na kukirekebisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, namwomba sana kama kuna daraja lingine, kama kuna barabara nyingine, tafadhali wewe tuambie ili tuweze kuangalia uwezekano wa kutumia hilo jina kwa hilo eneo ambalo hata ninyi watu wa Baraza la Wawakilishi mtaridhika nalo.
MHE. PETER A. P. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu haya mazuri ya Mheshimiwa Waziri na kwa namna ambavyo wafadhili wetu wameonesha nia ya kuweza kusaidia, lakini kwenye majibu ya Waziri ameonesha mradi utaanza kwenye robo ya tatu, lakini sijaona mradi unakamilika lini? Kimsingi, kwa Kilombero hii imekuwa ni kero. Tumechoka kuzika ndugu zetu, tumechoka kuharibu magari yetu, mazao yanakuwa na bei kubwa kwa sababu ya usafirishaji; kwa kweli imekuwa ni kero kubwa sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri sasa aniambie kwamba huu mradi unaisha lini ili hii kero iweze kwisha nasi tujione ni sehemu ya Tanzania? Kwa sababu imefika hatua sasa ukiwa unakwenda Ifakara unasema sasa naingia Tanganyika, maana kule ni vumbi! Hii imekuwa ni kero, kwa hiyo, naomba atuambie sasa huu mradi unakamilika lini? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lingine tunaomba atusaidie kwa sababu pale Ifakara na hii Wizara kwa sababu ni ya Uchukuzi na Mawasiliano, pale kuna daraja la Mto Lumemo, kutokana na mafuriko linakwenda katika muda wowote. Kwa hiyo, atuambie kama wako tayari kwenda kuangalia lile daraja na athari za mafuriko waweze kusaidia ili haya mafuriko yatoweke na daraja lipone. Nashukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba wananchi wa Ifakara, Mlimba na maeneo yote mpaka kule Mahenge ambapo daraja la Kilombero linawahusu; kazi ambayo Serikali imeifanya ni kubwa na kama ambavyo nimejibu katika swali la msingi, ujenzi utaanza kipindi cha robo ya tatu. Utakwisha lini? Nadhani kwa sasa ni mapema mno kwa sababu kuna baadhi ya makubaliano katika hawa wafadhili yanatarajia kukamilika hivi karibuni. Tutakapokamilisha na mazungumzo yakikamilika na Mkandarasi tutaweza kuwa na majibu sahihi. Kwa sasa naomba Mheshimiwa Mbunge akubali na wananchi waelewe kwamba Serikali imeji-commit kujenga hiyo barabara na itakapofika robo ya tatu ya mwaka huu wa fedha kazi hiyo itaanza na baada ya hapo, tutajua kadri tutakavyoendelea, lini kazi hiyo itakamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili, nikubaliane naye na bahati nzuri nina ratiba ya kwenda huko, nitamjulisha siku ambayo nitakuwa huko ili nitakapokuwa huko akanionyeshe hilo daraja tuangalie nini kinaweza kufanyika.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Tatizo la barabara ya Kidatu na Ifakara linafanana na barabara ya junction ya kuelekea Rusumo almaarufu kama zero-zero kupitia barabara ya Nyakahula - Rusahunga mpaka Nyakanazi. Hiyo barabara imekuwa ikifanyiwa ukarabati mara kwa mara lakini bado inaharibika kwa muda mfupi sana. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya matengenezo makubwa katika barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hiyo anayoongelea hivi sasa tunavyoongea ina mkandarasi anayefanya matengenezo. Ni kweli hoja anayoongelea kwamba, kunakuwa na matengenezo ya mara kwa mara na hii inatokana na matumizi makubwa sana ya malori makubwa yanayopita katika barabara hiyo na naamini matengenezo ya sasa yamezingatia ukubwa wa matumizi ya barabara hiyo na hivyo matengenezo yake sasa yatakuwa ya muda mrefu tofauti na huko nyuma.
MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi. Nataka kufahamu kwa uhakika ni lini Serikali itasema waziwazi siku ambayo kazi ya ujenzi wa barabara ya Masasi, Nachingwea utaanza? Kwa sababu upembuzi yakinifu ulifanyika pale muda mrefu, wananchi wanakosa amani katika eneo lile kwa sababu nyumba zao nyingi zilichorwa „X‟ na hawajui lini zitavunjwa au waendelee na ujenzi katika eneo lile. Tuliona tija ya Serikali imetoa nguvu kubwa sana na sasa hivi wanakaribia kuanza ujenzi wa barabara inayokwenda Ruangwa kuanzia Nanganga. Tunataka tuone pia na upande wa Masasi Nachingwea na wenyewe ujenzi unaanza mara moja.
Kwa hiyo, tunaomba commitment ya Serikali watueleze, ni lini ujenzi wa hii barabara utaanza au kama siyo hivyo, basi wananchi wale waambiwe waendelee kuendeleza yale makazi yao kwa sababu wanaishi katika maisha duni, hawajui ni lini nyumba zao zitavunjwa kwa sababu ya uendelezaji wa barabara katika eneo hilo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Mwambe awaelimishe wananchi waliopo katika barabara hiyo kwamba wasijenge, kwa sababu Serikali ina dhamira ya dhati ya kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba katika mwaka huu wa fedha kuna fedha zimetengwa kwa ajili hiyo. Suala la lini, naogopa sana kusema kwa sababu kuna process ya kufikia hiyo hatua. Naomba tukamilishe hiyo process, itakapokamilika tutamjulisha lini tunaanza.
MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Tatizo la barabara hii ya Kilombero linafanana na tatizo la barabara yetu ya Tabora - Itigi. Kipande cha Chaya - Nyahua kilomita 89 ambacho kinaifanya barabara hii mpaka sasa isiweze kupitika na tunaelekea katika kipindi cha mvua.
Barabara hii ni muhimu sana kwa sisi wakazi wa Tabora, Katavi na Kigoma. Tunaomba Serikali ituambie ni lini barabara hii itatengenezwa ili kufungua barabara hii na kusaidia wakazi wa mikoa hiyo? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Musa Ntimizi anafahamu kwamba mwezi wa Kumi na Moja ndiyo tutakuwa na kikao na Kuwait Fund kuhusu hii barabara. Labda kwa maana ya taarifa kwa wananchi wa kule nao wajue ni kwamba tunatarajia kupata fedha kutoka Kuwait Fund kwa ajili ya kukamilisha hiki kipande ambacho kimebakia kati ya Chaya na Nyahua; na kikao cha kupata hiyo commitment kitafanyika mwezi ujao mwezi Novemba.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali mawili kama ifuatavyo:-
Swali langu la kwanza; Mheshimiwa Waziri atakiri kwamba wananchi wa Kata ya Mkundi, Kata ya Mpindimbi na Kata ya Singano wanapata tatizo kubwa sana kutokana na kutokuwepo kwa madaraja haya. Aliyekuwa Waziri wa Ujenzi katika Serikali ya Awamu ya Nne na Rais wa Jamhuri ya Muungano, aliahidi kwamba atasaidia jambo hili ili madaraja yale yajengwe. Je, nini kauli yake leo; kwa sababu hata usanifu katika madaraja hayo haujafanyika? Nini maelekezo yake kwa Watendaji? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa barabara ya Ulinzi ambayo inaunganisha kati ya Tanzania na Msumbiji ni barabara muhimu sana ya kiuchumi kwa wananchi katika maeneo yetu: Je, ni hatua gani zimeshafikia sasa katika maandalizi ya ujenzi wa barabara hiyo katika awamu hii ambayo ameisema kwamba shilingi milioni 140 zimeshapatikana?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli ahadi hii ya kuifungua hii barabara na pamoja na kuwawezesha wananchi wa Kata hizi za Mkundi, Mpindimbi na Singano zimetolewa na viongozi wetu. Naomba kumhakikishia kwamba haya niliyoyasema katika jibu langu la msingi ndiyo hatua madhubuti za kufikia utekelezaji wa ahadi hizi za viongozi walizozitoa katika nyakati mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa maeneo hayo ambao wanaathirika, kwamba Serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha madaraja yale yanarudishwa, lakini vilevile barabara ile ya Ulinzi inafunguliwa. Nini tunakifanya katika hiyo Shilingi milioni 140?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utangazaji wa tenda kwa ajili ya kazi hii utafanyika hivi karibuni na vilevile kazi hii ya upembuzi yakinifu nayo itafanywa na Mtendaji wa TANROADS Mkoa wa Mtwara. Labda kwa taarifa hii naye nimkumbushe kama alikuwa amejisahau kwamba kazi ya kuhakikisha hayo madaraja yanafanyiwa usanifu ili yaweze kukamilika kama viongozi wetu walivyoahidi, ifanywe haraka ili kazi ile itekelezwe kama viongozi walivyoahidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa hali ya barabara za Lulindi ni nafuu kuliko Mbulu Vijijini; na kuna barabara imeahidiwa ya Karatu - Mbulu; Mbulu – Hydom; Hydom – Sibiti na Mheshimiwa Rais, kwa kujengwa kwa lami; na majibu ya MheshimiwaWaziri yalikuwa yanasema mwanzoni uchambuzi yakinifu umeshaanza. Je, barabara hii inajengwa lini sasa ili wananchi wa Mbulu na maeneo mengine wapate nafuu ya kiuchumi na kupita hasa kuelekea kwenye Hospitali ya Hydom?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano inapoahidi ina dhamira ya dhati ya kutekeleza ahadi zake zote ikiwa ni pamoja na barabara hii. Tumeongea mara nyingi ofisini kuhusu hili suala na tumemwambia mara nyingi kwamba tuna dhamira ya dhati, tunatafuta fedha. Hatuwezi kuanza ujenzi kabla hatujapata fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juhudi za kutafuta fedha zinaendelea kwa kasi na mara zitakapokamilika tutamjulisha Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa maeneo ya Mbulu mpaka wanavyoungana na Hanang wajue kwamba lini barabara yao sasa itakuwa vizuri na sasa wataenda kwenye ile hospitali wakiwa na barabara nzuri.
MHE. MARIA N. KANGOYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na kazi nzuri ya Serikali, napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; je, ni lini barabara ya kutoka Kilombero - Kivukoni mpaka Mwaya - Ulanga itakamilika kwa ujenzi wa kiwango cha lami? (Makofi)
Swali la pili; je, ni lini ujenzi wa barabara ya kutoka Bigwa mpaka Kisaki itakamilika kwa ujenzi wa kiwango cha lami pamoja na madaraja yake?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kwamba barabara hizi ni muhimu na zinahitaji kujengwa kwa kiwango cha lami kama ambavyo Ilani ya Chama cha Mapinduzi imefafanua. Katika barabara zote mbili; moja, hii ya upande huu wa Ulanga Kusini na hii ya upande wa kwa Mheshimiwa Mbena, niwahakikishie kwamba dhamira ya Serikali ni ya dhati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo tumekuwa tukiwaeleza katika vipindi vilivyopita, dhamira yetu ya kujenga barabara hizi iko pale pale na tutahakikisha tunatafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo na kazi hiyo ya kutafuta fedha ya kujenga barabara hizi inaendelea.
MHE. FREDY A. MWAKIBETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kwa masikitiko makubwa sana na nisononeke moyoni mwangu kwamba Mheshimiwa Waziri majibu aliyoleta hapa sio niliyouliza kwenye swali langu la msingi. Nimeuliza, barabara itajengwa lini ya Mkoa wa Mbeya na Njombe yeye amenitajia barabara za Katumba – Lusanje – Kandete. Nilikuwa namaanisha barabara inayotoka Mwakaleli kwenda mpaka Makete halafu iunganishwe na Njombe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini zaidi swali la pili nimeuliza Jimbo la Busokelo litaunganishwa na Jimbo la Rungwe. Lakini Waziri anasema Serikali haifikirii kufungua barabara kuunganisha maeneo hayo kutokana na milima mikali, hivyo barabara ziendelee kutumika zilizopo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nisikitike kwa sababu wananchi wa Jimbo la Busokelo katika Vijiji nilivyovitamka Suma pamoja na Kilimansanga ni zaidi 5,000. Akisema kwamba waendelee kutumia barabara hizo hizo wakati tayari hakuna muunganisho wa hizo barabara nashindwa kuelewa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili swali ningeomba liweze kujibiwa kwa mara nyingine tena kwa sababu majibu aliyojibu hapa sio, hayaniridhishi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimsihi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kumaliza Bunge hili mimi nitakuwa na ziara eneo hilo. Kwa sababu katika jibu la msingi barabara anayoongelea ya Mkoa wa Mbeya kuunganisha na Njombe tumesema inapitia Mwakaleli, Kata ya Kandete na Luteba; na tumesema inapitia Katumba - Lusanje - Kandete - Ikubo hadi Luteba. Maadam anasema narudia yale yale, sasa kama nilichokisema anasema sio sahihi, naomba tukakutane site ili tuweze kupata uhakika wa kile ambacho yeye anakiamini wakati sisi hiyo ndio tunavyofahamu.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa tatizo la Busokelo linalingana kabisa na Korogwe Vijijini. Kwanza nianze kuipongeza Serikali kwa kazi nzuri wanayonifanyia kule Korogwe kwa kujenga daraja la Magoma. Barabara ya kutoka Old Korogwe kwenda Maguzoni ni barabara ya Mkoa, lakini daraja lake lilibomoka toka mwanzo wa mwaka huu.
Je, Serikali ina mpango gani wa dharura wa kujenga daraja hili ili wananchi waliokuwa wapo kwenye kisiwa waitumie barabara yao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa daraja hilo tutalishughulikia na kwa nafasi hii nawataka TANROADS Mkoa wa Tanga walete taarifa kamili ya lini wamepanga kukifanya ili tuweze kutekeleza kile ambacho Mheshimiwa Mbunge na ambacho wananchi wa Korogwe wanakitaka.
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Mheshimiwa Waziri naomba nikuulize swali; barabara ya Mgakolongo kwenda Kigarama mpaka Mlongo upembuzi ulishafanyika muda mrefu na wananchi wameshindwa kuendeleza maeneo yao kwasababu walishawekewa “X”. Barabara hii ni lini itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Bilakwate kwa namna anavyofuatilia ujenzi wa barabara zote mbili zinazopita katika Jimbo lake; moja upande wa Kaskazini na nyingine Kusini n nikubaliane na yeye kwamba hii ya Kusini inapita katika maeneo makubwa, ingawa hapa hajayasema lakini ameyaongea katika Ofisi yangu. Naomba nimhakikishie kwamba fedha zimetengwa kwenye mwaka huu wa fedha wa mwaka 2016/2017; nimuhakikishie tutajenga kabla ya tarehe 30 Juni, 2017.
MHE. CAPT. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kushukuru majibu mazuri ya Serikali, lakini pia napenda nishukuru ushirikiano tulioupata kwa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege; kama walivyosema, walifika Newala na wameelekeza kiwanja kikaeje na wametueleza ukubwa wa eneo linalohitajika. Nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza, kwa kuwa taratibu za Kimataifa zinataka kabla hatujahamisha uwanja ule wa ndege, ule uwanja wa mwanzo ufutwe; na kwa kuwa Halmashauri imeandikiana sana na Wizara na viwanja vya ndege kutaka kufuta ule uwanja wa zamani, jambo ambalo halijafanyika mpaka sasa. Je, Serikali inaweza kutuhakikishia kwamba kazi ya kufuta ule uwanja itafanyika mara moja?
Swali la pili, kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa Waziri ametupa majukumu Halmashauri ya Mji kufanya tathmini ili eneo lile liweze kutwaliwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, kazi ambayo tutakwenda kuisimamia mara baada ya kutoka hapo. Je, Halmashauri ya Mji ikishamaliza suala la tathmini na kwa kuwa viwanja vya ndege ni mali ya Serikali Kuu, siyo mali ya Halmashauri, Serikali itakuwa tayari kuwafidia wale wananchi wachache ambao walikuwa wanalima pale kwa kuzingatia kwamba gharama hazitakuwa kubwa kwa sababu pale hakuna mazao ya kudumu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu Mheshimiwa Huruma kwa jina lake ni mtu wa huruma…
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa George Huruma Mkuchika, ana kaka yake anaitwa Uchicheme Wala Uchimumunye; Ukimumunya Nchale Ukitema Nchale.” (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mkuchika kwamba uwanja huu ukishakamilisha suala la process ya kulitwaa tutafanya kama anavyopenda na kama wenzetu wa Halmashauri ya Newala wanavyopenda.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba, tena naomba sana masuala ya kuvamia viwanja vya ndege, ndugu zangu, vinginevyo tutakuwa tunaipa hasara Serikali. Naombeni sana viongozi wenzetu wa Halmashauri mbalimbali watunze viwanja vyetu vya ndege ili viweze kutusaidia katika shughuli za kitalii na usafiri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kwanza namhakikishia kwamba tutachukua hizo hatua na pengine nichukue fursa hii kuwaagiza Bodi ya TAA ichukue hatua za haraka kuhakikisha kwamba uwanja huu unafutwa kwa mujibu wa taratibu tulizojiwekea.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa katika Kata ya Mnazi, Tarafa ya Umba, kuna tatizo linalofanana na huku Newala Mjini; kuna kiwanja cha ndege (air stripe) ambayo ni ya muda mrefu sana haitumiki na sisi tupo karibu na hifadhi ya Mkomazi: Je, Serikali haioni kwamba ni wakati muafaka sasa kukifufua kiwanja hiki ili kiweze kuchochea utalii katika hifadhi ya Mkomazi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimepokea ombi la Mheshimiwa Shangazi na nitawasiliana na Waziri wa Maliasili na Utalii ambao kiwanja hiki ilikuwa ni mali yao na ni kwa ajili ya shughuli za utalii ili tuone namna gani kiwanja hicho kitafufuliwa na kama kuna shughuli za kiuchumi zitakazowezesha kiwanja hiki kujilipa.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Sekta ya Utalii ni sekta ambayo inachangia kwa kiasi kikubwa pato la Taifa na sekta hii ili iweze kuwa endelevu ni lazima pawepo na uhakika wa usafiri ikiwemo viwanja vya ndege. Kuna Kiwanja cha Ndege kilichopo Karatu kwa maana ya Kiwanja cha Ndege cha Manyara; kimetelekezwa na hakiendelezwi. Je, ni lini Serikali itahakikisha inaendeleza kiwanja hicho?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nitawasiliana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) na Bodi yao tuone nini kinaweza kufanyika katika kiwanja hiki na mipango yao ikoje katika kuvifufua viwanja mbalimbali ikiwa ni pamoja na hiki.
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Spika, kwa masikitiko makubwa sana nimemshangaa kidogo Naibu Waziri. Kwanza inaonekana historia ya barabara hii haifahamu. Nitaomba kabla sijauliza maswali mawili madogo, niseme kilichotokea.
Mheshimiwa Spika, wakati ujenzi wa barabara hii ya Mwandiga - Manyovu unaanza, kuna watu waliambiwa na Serikali wabomoe wakafuata sheria wakabomoa, wale waliogoma kubomoa wote walilipwa na Serikali hii. Hapa naulizia wale waliotii sheria.
Mheshimiwa Spika, sasa niulize masawli mawili ya nyongeza.
Je, Rais Magufuli ambaye alikuwa Waziri wa Ujenzi, Sheria ya Babaraba hii anaijua vizuri sana, na Waziri Magufuli alipokuja pale kuomba kura eneo la Kalinzi, tarehe 19, mwezi wa Septemba alisema yafuatayo wakati akisema tungependa vitu gani atusaidie atakapokuwa Rais. Moja ya mambo makubwa manne aliyoambiwa mojawapo ilikuwa ni suala la fidia ya wale watu ambao walitii sheria walipwe. Rais Magufuli alisema maneno yafuatayo, alisema; “Ninajua mgogoro wa barabara hii, wale ambao hawakulipwa wameenda mahakamani, ninawaomba mfute kesi tukimaliza uchaguzi na ninyi mtalipwa.” Wale wote wamefuta kesi. Sasa nimuulize Naibu Waziri, kesi imefutwa, Rais aliahidi, sasa tujiulize, Rais alitudanganya au wewe ndiye unayetudanganya hapa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba niwahakikishie wananchi wale walioathirika wa kati ya Mwandiga na Manyovu, wakati wanaahidiwa na Mheshimiwa Rais kwamba atawalipa fedha kama wahanga wa ile barabara alikuwa hadanganyi, alikuwa anasema kutoka katika sakafu ya moyo wake.
Pili, tunapolijibu swali hili, kwa sababu swali hili eneo lililopewa nguvu ni eneo la fidia, sasa ukitoa nguvu katika swali kwenye eneo la fidia wakati huku unajua kwamba hawa watu hawastahili fidia inakuwa ni tatizo. Kwa sababu hatuwezi tuka-create precedent, maeneo mengi sana tumewataka watu wa mita 30 toka hifadhi ya barabara wabomoe nyumba zao bila fidia, kwa sababu ndivyo sheria inavyosema, lakini tunapoongelea kuwalipa wahanga ni kitu kingine na ahadi ya Rais ni kitu kingine.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wale wahanga kwamba Mheshimiwa Rais atatekeleza ahadi yake ya kuwalipa, anawalipa kama wahanga, hatuwalipi fidia. Fidia hatulipi ndani ya eneo la mita 30 au mita 22.5 kwa kipindi kile cha chini ya mwaka 2007, na kwa sasa hatulipi ndani ya mita 30 kila upande.
Ninaomba tukileta precedent hapa tutaleta matatizo katika nchi hii, kama ahadi ya Rais kwa specific case ya eneo la Mwandiga mpaka Manyovu, itatekelezwa kwa asilimia 100 kama ambavyo ahadi nyingine zote za Rais tutahakikisha zinatekelezwa katika kipindi hiki cha miaka mitano.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Suala la fidia katika kupisha ujenzi wa barabara kule Mwandiga linafanana kabisa na barabara ya lami inayojengwa kutoka Nyamswa - Bunda - Kisolya - Nansio ambayo na yenyewe wananchi kule wanastahili kufidiwa. Mheshimiwa Naibu Waziri atakumbuka nimemsumbua sana juu ya jambo hili, nimemsumbua sana Mheshimiwa Waziri, lakini wananchi kule wanadhani mimi sifanyi kazi wanadhani siwasilishi matatizo yao.
Naomba kupitia kinywa chake ndani ya Bunge hili, Wanamwibara wanamsikia, atuambie ni lini fidia ya Wanamwibara hawa watafidiwa kwa sababu wamepisha ujenzi wa barabara? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Kangi Lugola kwa namna anavyofuatilia haki za wananchi wake. Namuomba sana kwamba wale ambao wanastahili kulipwa fidia tulimuahidi kwamba Serikali itahakikisha watu hawa wanalipwa fidia mara tutakapopata fedha. Hapa hatuongelei watu ambao hawastahili kulipwa fidia kwa maana ya wale ambao majengo yao yalikuwa ndani ya eneo la hifadhi.
MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, swali la Kigoma Kaskazini linafanana kabisa na swali la wananchi wa Segerea na Ukonga. Wananchi wa Kipunguni A, Kipunguni Mashariki, Kipawa na Kigilagila waliambiwa wapishe maeneo yao kwa ajili ya ujenzi au upanuzi wa uwanja wa ndege. Wanachi hawa wamefanyiwa tathmini tangu mwaka 2007, imekuwa ni danadana, sasa Waziri atuambie ni lini wannachi hawa watalipwa fidia baada ya kuwa wanapewa pesa kidogo wanaambiwa watalipwa na siku zinakwenda na wanashindwa kuendeleza maeneo yao.
Je, ni lini, fidia hizo zitalipwa na hawa wananchi waweze kupata maeneo mengine ya kujisitiri? Wananchi hao wanamsikia. Nakushukuru sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, Mbunge wa Segerea anafahamu kwamba tulikaa kikao…

Naomba nipewe fursa ya kujibu swali.
Mheshimiwa Mbunge wa Segerea alishafanya kikao na mimi mwenyewe kuniita, katika kikao hicho nilikutana na wahusika wote wanaotakiwa kulipwa fidia katika eneo la Kipunguni. Kwa hiyo, namshukuru sana, kwanza Mheshimiwa Anatropia kwa kumuunga mkono Mbunge mhusika katika eneo hili na Mbunge mhusika katika eneo hili anafahamu kwamba nimeshatoa ahadi ya kuhakikisha suala la kulipa fidia eneo la Kipunguni kwa ajili ya kupisha ujenzi wa uwanja wa ndege nitalishughulikia na litafikia mwisho katika kipindi hiki cha miaka mitano na anafahamu sababu yake.
Mheshimiwa Spika, sababu yake ni kwamba kuna fedha ilishatolewa, lakini kuna uwezekano fedha zilizotolewa zote hazikuwafikia walengwa. Kwa hiyo, tumeunda Tume inafanya uchunguzi wa suala hili kuhakikisha zile fedha zilizotakiwa kuwafikia walengwa tujue zimeenda wapi na tutafunua kila palipofunikwa kuhakikisha fedha zile zilizokusudia kulipa wahanga wale zinapatikana na hatimaye wahanga walipwe. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nilimhakikishia Mbunge mhusika wa hilo eneo na sasa naomba nimhakikishie Mheshimiwa Anatropia, suala hili tumelichukua kwa nguvu na tutalishughulikia, tutafukua kila aina ya kaburi kuhakikisha kwamba wahusika wanalipwa fidia iliyostahili. Nilitoa katika mkutano ule wa wadau kwamba ni katika kipindi hiki cha miaka mitano.
MHE. CONCHESTA L. RWAMLAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba kuna umuhimu wa kuwa na sheria hii na pia imesema imetunga sheria kwa ajili ya mazao yale yanayosimamiwa na bodi ya mazao: Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuweza kufanya marekebisho katika sheria hiyo ili hata mazao mengine mchanganyiko yaweze kulindwa ili wakulima waweze kufanikiwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; ni wazi kwamba bado ulanguzi wa mazao unaendelea, walanguzi wanafuata wakulima mashambani na siyo sahihi kusema kwamba magulio ni sehemu ya ushindani wa bei na Halmashauri zenyewe hazijawa na mkakati maalum wa kuweza kuunda sehemu za kuuzia mazao na kuweza kuzisimamia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali inachukua hatua zipi kuhakikisha kwamba vituo hivi vinakuwepo na vinakuwa na usimamizi ili wakulima waweze kunufaika kwa kupata bei nzuri kuweza kubadilisha maisha yao?
Mwenyekiti, ni kama ambavyo nimeeeleza katika jibu la swali la msingi kwamba Serikali inaona umuhimu wa kuanzisha sheria.
Kwa hiyo, ombi lake tumelipokea na Serikali imeshaonesha nia kwamba hilo inalishughulikia na imeshaanza kufanya kwa mazao hayo mengine. Kwa maana nyingine tutaendelea kushughulikia na mazao mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kule kwetu Namtumbo magulio kwa kweli huwa yanaleta ushindani. Kwa hiyo, naungana kabisa na jibu la msingi kwamba Halmashauri waimarishe magulio na sehemu za minada kwa kweli maeneo hayo yanaleta ushindani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama kuna njia nyingine kutokana na mazao mbalimbali mengine, tuwasiliane na Halmashauri hizo na sisi ni wajumbe wa Halmashauri, tuweze kuboresha kanuni zetu, bylaws zetu, ili tuhakikishe mkulima anapata haki yake kwa jasho analolitoa.
MHE. MGENI J. KADIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya nyongeza, ninayo maswali mawili. Kwa kuwa Serikali inaitisha zabuni mwezi wa Februari kama ilivyosema na imetenga shilingi bilioni tatu kwa mwaka wa fedha 2016/2017: Je, Serikali haioni kuwa ni muda mfupi unaobakia mpaka kumalizika bajeti? Je, daraja hilo kweli litajengwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili: Je, Serikali haioni kuchelewesha kujenga daraja hilo ni kuzorotesha maendeleo na kuongezeka kwa ajali na hicho ndiyo kilio cha watu wa Tanga?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kumhakikishia Mheshimiwa Jadi Kadika kwamba huo muda unatosha sana. Taratibu ni lazima zifuatwe kabla ujenzi haujaanza. Kwa hiyo, hatua za kwanza zilikuwa ni kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na hatimaye kuandaa nyaraka za zabuni, kazi hiyo tumeikamilisha. Sasa mwezi wa Pili, tunaitisha tenda na mambo yakikamilika tukampata mkandarasi, hiyo shilingi bilioni tatu itatoka na kazi ya ujenzi itaanza.
MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Wananchi wa Kata ya Tangini na Pangani ambapo ndiko barabara hii inapita, wamekuwa wakipata adha kubwa sana. Takriban zaidi ya miaka mitano iliyopita upembuzi yakinifu, usanifu pamoja na tathmini kwa maana ya evaluation ilishafanyika na wananchi hawa wanadai kiasi cha fidia ya shilingi
8,552,777,000/= na hadi leo hawajapata fidia hiyo na hawajui wataipata lini. Mbali na hili jitihada za…
MHE. SILVESTRY F. KOKA: Yah. Jitihada za RCC kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya kujenga barabara hii zimekwama kwa sababu ya fidia hii haijalipwa. Je, Serikali italipa lini fidia hii kupisha maendeleo ya barabara hii kwa wananchi hawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa sasa barabara hii imezuiwa kupitisha magari zaidi ya tani 10: Je, TANROADS ina mpango gani wa kurekebisha barabara hii ili shughuli za kiuchumi za wananchi hawa ziweze kufanyika kwa kupitisha magari ambayo ni zaidi ya tani 10?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Koka kwamba mara tutakapopata hizo shilingi bilioni 8.65 tutazitoa na kuanza kulipa fidia. Lini? Kama nilivyosema katika jibu la msingi, tunazitafuta hizo fedha na mara tutakapopata tutazilipa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kitu kimoja; anafahamu kwamba barabara hii ipo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 – 2020, nimhakikishie, tuliahidi na tutatekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa kuiwezesha barabara hii ibebe magari ya zaidi ya tani 10, nimelipokea, nitawasiliana na Meneja wa TANROADS Mkoa tuone nini kifanyike ili ombi la Mheshimiwa Mbunge, ambapo ni mahitaji ya wananchi wake hasa wa Kata za Tangini na Pangani waweze nao kupata unafuu kiuchumi. Namwomba tu, kama anaweza kuharakisha, kama hawa wananchi wanaweza wakasamehe hiyo shilingi bilioni nane, nimhakikishie mwezi ujao tutaanza kujenga.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya wakazi wa Wilaya ya Malinyi, Wilaya ya Ulanga na Kilombero, tunaishukuru Serikali na tunawapa pongezi kutekeleza ahadi ambayo wametuahidi ya ujenzi wa daraja la Kilombero ambayo imekuwa jawabu kubwa la kero ya miundombinu katika Wilaya hizo tatu. Hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, ujenzi huo wa daraja la Kilombero unahusisha pia na barabara za maingilio na barabara hiyo ya maingilio inaunganisha barabara inayotoka Ifakara, Lupilo, Malinyi, Kilosa Mpepo, Londo, Lumecha, Namtumbo mpaka Songea. Barabara hii kipindi cha masika inachafuka sana kutegemea na mazingira ya mvua maeneo yale na inakuwa inapitika kwa tabu sana. Sasa, je, Serikali inajipangaje na ukarabati wa kudumu wa maeneo korofi katika barabara hiyo niliyotaja?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili; barabara hii niliyotaja inajulikana kwa T16, barabara hiyo iko katika upembuzi yakinifu unaosanifu kwa kina ambao umekamilika. Barabara inatakiwa ijengwe kwa kiwango cha lami. Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara hiyo inayotoka Ifakara, inatobokea mpaka Songea ambayo itakuwa sio kwa ajili ya mkaazi wa Morogoro itasaidia pia na ndugu zetu majirani wa Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Njombe?
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, napokea kwa niaba ya Serikali pongezi alizotupa na kwa kweli ni wajibu wetu kutekeleza ahadi zote ambazo tumezitoa katika Ilani ya Uchaguzi ya 2015/2020.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara anayoongelea nayo iko katika Ilani ya Uchaguzi ya 2015 hadi 2020 ya kujengwa kwa kiwango cha lami. Upembuzi na usanifu wa kina haujakamilika – physically umekamilika lakini taarifa bado haijakamilika na tunatarajia hiyo kazi itakamilika mwezi Mei, 2017. Kwa sasa taarifa ya rasimu imeshawasilishwa TANROADS wanaipitia kwa kina ili hatimaye wamrudishie maoni yule Mhandisi Mshauri ambaye ni kampuni ya Kyong Dong na baada ya hapo ndio atakuja kukamilisha kuandika taarifa ya mwisho. Kwa ratiba ilivyo ataiwasilisha taarifa ya mwisho mwezi Mei, 2017. Baada ya hapo Serikali itaanza kujipanga kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa suala la ukarabati wa maeneo korofi kwa sasa ili iweze kupitika muda wote; nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Hadji Mponda Mbunge wa Malinyi na wananchi wote wa Malinyi hadi Kilosa kwa Mpepo kwamba Serikali ina mkakati kabambe na kila mwaka tunatenga fedha na nafahamu mwaka huu kuna wakandarasi wawili wako site katika maeneo korofi wanafanyia ukarabati wa hali ya juu ili kuhakikisha barabara hiyo inapitika mwaka mzima bila matatizo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kukamilika kwa daraja la Mto Kilombero ni wazi kwamba sasa Mkoa wa Morogoro unafunguliwa kibiashara. Nini mipango ya Serikali kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Lindi kwa barabara inayopitia kutoka Liwale kuelekea Morogoro? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kiongozi wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa ni moja kati ya ahadi yake ya kuhakikisha barabara kutoka Ilonga hadi Liwale inashughulikiwa. Ahadi hiyo tumepewa na nimhakikishie kwamba tutaishughulikia hadi tuikamilishe katika kipindi hiki cha miaka mitano.
MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali juu ya ujenzi wa daraja la Kilombero lakini ahadi ya Serikali ya kukamilisha ujenzi wa barabara kupitia daraja la Kilombero kwenda Songea kupitia Namtumbo ni ya muda mrefu sana na hivi sasa wananchi wa Songea ukitaka kusafiri kwa kawaida ni masaa 15 kutoka Dar es Salaam mpaka Songea. Hii barabara kutoka Kilombero kukatiza Namtumbo kwenda Songea ingerahisisha sana na usafiri ungekuwa mwepesi sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ni vizuri Serikali itupe majibu ni lini tunatazamia tuanze ujenzi wa barabara hii ya kuelekea Songea kupitia Kilombero? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli hoja ya kujenga barabara hii ilianza toka mwaka 1996, tunafahamu. Tatizo lililokuwepo katika kipindi kirefu sana tulikosa fedha lakini hatimaye katika kipindi hiki na Serikali hii ya Awamu ya Tano naomba nimhakikishie kwamba kazi hii itafanyika muda si mrefu na kwa vyovyote ni ndani ya kipindi cha miaka mitano ambayo ahadi imetolewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu, akiangalia kitabu chetu cha Ilani atakuta hii barabara imeandikwa itajengwa kwa kiwango cha lami na hatua za mwanzo ndio hivyo tunazikamilisha mwezi Mei na baada ya hapo tunaanza utaratibu wa kutafuta fedha za kujenga hiyo barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, lingine vile vile mimi mwenyewe natoka Namtumbo na nimetoa ahadi kwamba barabara hii mwaka huu lazima itoboke, isipotoboka TANROADS watatoboka! Kwa hiyo, nimhakikishie suala la kutoboa barabara hii, itatoboka mwaka huu, lakini kuanza ujenzi ni baada ya miaka ijayo ya fedha.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Baada ya MV Butiama kusita kufanya shughuli zake pale kulikuwa na meli ya MV Clarius ambayo nayo imesimama kufanya kazi na kuna taarifa kwamba itatengenezwa na watu wa MSCL ili iendelee kufanya shughuli zake lakini meli hii imekuwa chakavu, inahitaji matengenezo makubwa. Sasa kwa kuwa wenye jukumu la kutengeneza ni MSCL wenyewe lakini wanatatizo kubwa sana la fedha. Je, Serikali sasa haioni kwamba kuna haja ya kuwasaidia hawa MSCL kwa kuwapa fedha za kutosha ikiwepo pamoja na pesa za OC ili waweze sasa kutengeneza meli hii iweze kufanya kazi katika mazingira mazuri ikizingatiwa ni ya muda mrefu na katika hali halisi ya sasa kumsafirisha abiria kwa saa tatu majini akiwa amekalia viti vya mbao si kitu kizuri sana?
Swali la pili; ratiba za meli kutoka Mwanza kwenda Ukerewe zina mahusiano ya moja kwa moja na ratiba za vivuko vingine. Kwa mfano, Kivuko cha MV Nyerere kutoka Mgolola kwenda Ukala sasa kumekuwa na matatizo ya kutowiana kwa ratiba kiasi kwamba wasafiri wanakaa muda mrefu. Kwa mfano, akifika Nansio anakaa kwa saa tano ili apate usafiri mwingine wa kumpeleka kisiwa cha Ukala. Je, Serikali haioni sababu za msingi za kuainisha ratiba ya vivuko hivi ili kuondoa gharama kubwa ambazo wasafiri wanazipata wanapokuwa safarini? Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la kwanza, nakubaliana naye kwamba kuna haja ya kuwaongezea uwezo wa kifedha ikiwa ni pamoja na fedha za OC ili MSCL waweze kutekeleza wajibu wao na hasa katika kuikarabati meli hii ya MV Clarius.
Kwa upande wa pili, ratiba nimepokea ombi lake, nitawasiliana na taasisi hizi mbili zinazohusika, TEMESA pamoja na MSCL waangalie kama kuna uwezekano wa kurekebisha ratiba zao, lakini kwa mazingira ninayoyafahamu, tukirekebisha kutakuwa na tatizo vilevile la kuwasumbua wale wa Ukala wakakaa muda mrefu sana kusubiri MV Clarius ifike, ilete abiria. Tutaangalia kama kutakuwa na uwezekano wa kutafuta njia nyingine kuweza hili kuliweka sawa ili wananchi waweze kunufaika na huduma hizo mbili za kivuko pamoja na Meli.
MHE. DUA W. NKURUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nashukuru
kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Miundombinu, lakini nataka
nifanye marekebisho kidogo siyo Kata ya Mnauje ni Kata ya Mnanje.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya majibu yake mazuri, nina swali dogo
la nyongeza. Katika Kijiji cha Marumba, Kata ya Mkonona kulijengwa mnara wa
TTCL na mnara ule uliwashwa, lakini utendaji kazi wa mnara huu siyo mzuri. Kijiji
hiki kipo mpakani kabisa mwa Tanzania na Msumbiji na sote tunafahamu
umuhimu wa mawasiliano mipakani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, kijiji hiki kinahudumia mpakani na
mnara huu haufanyi kazi vizuri. Je, Serikali itafanya nini kuhakikisha kwamba,
mnara huu unafanya kazi haraka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, nimepokea taarifa yake na nitatafuta muda nizungukie huo mpaka
ili tuone vijiji vyote vya mpakani hali ikoje, ikiwa ni pamoja na hiyo Kata ya
Mkonona.
MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Tatizo la
mawasiliano ni kubwa sana kwenye Visiwa vya Ukerewe, hususan kwenye
maeneo ya Bwasa, Kata ya Igala na maeneo ya Bukiko, Kata ya Bukiko. Sasa je,
Serikali iko tayari kutumia wataalam wake kufanya utafiti na kusaidia upatikanaji
wa mawasiliano kwenye maeneo haya ya visiwa vya Ukerewe?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko
tayari. Naomba tu nitoe kauli kwamba Mfuko wetu wa Mawasiliano kwa wote
(UCSAF) waifanye kazi hiyo haraka iwezekanavyo.
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niipongeze
Wizara hii imekuwa ni sikivu sana. Katika Jimbo la Mlalo karibu Kata zote sasa
mawasiliano yapo, isipokuwa katika Kata ya Rangwi na Kata ya Malindi hasa
eneo la Makose. Je, ni lini sasa katika hii Kata ya Rangwi na Malindi mawasiliano
ya simu za mkononi yatapatikana?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Rashid
Shangazi kwa namna anavyofuatilia mambo mbalimbali, hususan barabara
pamoja na mawasiliano katika Jimbo lake. Nimhakikishie, kama ambavyo
nimekuwa nikimweleza wakati anakuja ofisini kufuatilia shughuli za wananchi
wake kwamba, haya maeneo machache ya hizi Kata mbili za Malindi, Rangwi,
Serikali itaangalia uwezekano wa kuyafikia na hasa kwa kushirikiana na wadau
wetu kwa maana ya makampuni ya mawasiliano ya simu.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana
kwa kuniona. Matatizo yaliyopo ya usikivu wa simu Jimbo la Nanyumbu ni sawa
na yaliyopo Wilaya ya Ngara katika Kata ya Mganza, Nyakisasa, Keza, Kabanga
na Rusumo, ambayo yanaingiliana na nchi jirani za Rwanda na Burundi. Je,
Serikali ina mpango gani wa kuboresha usikivu wa simu katika Kata hizi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, nimemsikia na vilevile nilimsikia Mbunge wa Jimbo ameeleza kwa
muda mrefu sana matatizo ya Jimbo hilo. Namwona pale nimhakikishie na
nimhakikishie Mheshimiwa Semuguruka kwamba, upacha wao ni lazima uzae matunda katika miaka hii mitano na tutafuatilia maeneo hayo ili hatimaye
mawasiliano yapatikane ya uhakika.
MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja
na majibu mazuri ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali
la kwanza; kwa kuwa, wananchi wale walifanyiwa tathmini ya nyumba zao
muda mrefu na kwa kuwa, pesa inapanda thamani kila kukicha. Je, Serikali ipo
tayari kuwafanyia tathmini upya na kuwalipa kwa wakati?
Swali la pili; kwa kuwa, wananchi hawa wamepoteza imani na matumaini
ya kulipwa fidia zao kwa wakati na kwa kuwa, jitihada za Mbunge wa Jimbo
Mheshimiwa Aeshi Hilaly, amekuwa akifanya juhudi muda mrefu. Je, Mheshimiwa
Waizri yupo tayari kuongozana nami mpaka kwa wananchi ili akajionee
mwenyewe nyumba zinavyobomoka? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, kama ambavyo nilieleza katika jibu la swali la msingi kwamba hivi
tunavyoongea suala la uhakiki wa mali za wananchi ambao wataathirika na
mradi huu lipo katika hatua za mwisho. Kwa maana hiyo, taarifa kamili ya nani
na nini watalipwa inatarajiwa kupatikana hivi karibuni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kwenda kujionea madhara ambayo
wananchi wale waliosimamishwa muda mrefu kuendeleza nyumba zao,
naomba sana uwasiliane na Mheshimiwa Aeshi ili Mheshimiwa Aeshi aniruhusu
niongozane naye. Kwa sababu, nina uhakika Mheshimiwa Bupe Mwakang‟ata
na Mheshimiwa Aeshi wanafanya kazi moja ya kuwatetea wana Sumbawanga,
nimhakikishie tu kwamba nitakuwa tayari kuongozana na yeye akiwa na
Mheshimiwa Aeshi.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa,
tathmini imefanyika toka mwaka 2009 mpaka leo hakuna kitu kinachoendelea.
Wananchi wa Sumbawanga wanataka majibu ya uhakika ni lini watalipwa pesa
zao, kwa sababu ahadi zimekuwa za kila siku?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa
Naibu Spika, nimhakikishie kwamba mara baada ya uhakiki unaofanyika
kukamilika, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kuwalipa wananchi hao fidia zao.
MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nachukua nafasi hii kuishukuru kampuni ya Azam kwa kuleta usafiri huu kati ya Pemba na Tanga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu ni hili kwamba meli hii ya Sealink ni meli kubwa na uwezo wa abiria wa Pemba na Tanga siyo mkubwa sana. Viko vyombo vilivyojaribu kufanya safari za pale lakini vikashindwa kulingana na runningcost zilivyo kubwa sana. Je, ikitokea meli hii imekatisha safari kama zilizotangulia, Serikali itakuwa tayari kukubaliana na mimi kuipeleka meli ya MV Dar es Salaam, ambayo kwa sasa imekaa haifanyi kazi na ni ya Serikali, ikatoe huduma kati ya Pemba na Tanga? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa ajali nyingi zinazotokana na vyombo vya baharini, moja ya sababu ni uzito unaopitiliza katika vyombo hivyo: Ni utaratibu gani unaotumika kujua uzito unaostahiki ili kuepusha ajali zinazotokea mara kwa mara katika vyombo vya baharini? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, Sealink 2 ya Azam Marine imefanya utafiti wa muda mrefu, ndio maana imeanza na safari moja kwa wiki na kama wateja wataongezeka wataongeza safari. Kama itatokea kwamba hiyo ikasimamisha, ina maana abiria hakuna wa kutosha.
Mheshimiwa Spika, kuipeleka MV Dar es Salaam kufanya kazi hiyo, tatizo litakuwa lile lile, kwamba abiria hakuna wa kutosha. Sidhani kama nimemaanisha kwamba Serikali iendeshe meli hiyo ya MV Dar es Salaam kwa hasara, lakini kubwa ni kwamba MV Dar es Salaam haijakabidhiwa rasmi kwa TEMESA. Nadhani tumekuwa tukijibu maswali mengi kuhusu MV Dar es Salaam na hivi tunavyoongea sasa hivi kuna kampuni ya South Africa imekuwa contracted na ile kampuni ya Holland kufanya marekebisho ya ile speed. Ni mpaka pale watakapolikamilisha hilo, ndiyo tutakabidhiwa.
Mheshimiwa Spika, tutakapokabidhiwa tutajua nini cha kufanya, kwa sababu maombi yako mengi. Sasa tunaongelea Tanga, wenzetu wa Mafya wameomba, kwa hiyo, tutaangalia nini muafaka wa kufanya kwa MV Dar es Salaam itakapokabidhiwa rasmi Serikalini.
Mheshimiwa Spika, kuhusu uzito, tuna taasisi yetu ya SUMATRA ndiyo inayosajili vyombo vyote vya majini na vitu vinavyotumia criteria ya kusajili ni pamoja na uzito wa mizigo, kiwango cha abiria, hivi vyote vinaangaliwa.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, chombo chetu au taasisi yetu ya SUMATRA ndiyo yenye wajibu wa kuhakikisha kila chombo kinachoingia majini kinachukua kiwango cha abiria na uzito unaostahiki. Ndiyo maana kila mahali ambapo meli au boti imesajili, tuna wataalam wa SUMATRA katika maeneo hayo.
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Nami naishukuru Kampuni ya Azam Marine kwa kurahisisha usafiri kutoka Tanga kwenda Pemba. Swali langu ni moja dogo lifuatalo:-
Kwa kuwa kuna malalamiko ya muda mrefu ya kutokupatikana kwa usafiri wa uhakika kutoka Dar es Salaam kuelekea Bandari ya Mtwara; na Serikali imekuwa ikiahidi mara kadhaa kwamba wako katika mkakati kabambe wa kuhakikisha kwamba usafiri kwa njia ya baharini kutoka Dar es Salaam kwenda Mtwara utapatikana kwa haraka; Serikali ituambie, ahadi hii ya muda wa miaka saba iliyopita, ni lini Serikali itaandaa mikakati ya kurahisisha usafiri huu? Naomba majibu.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ni hivi karibuni tu humu Bungeni nilisema kwamba Serikali inaangalia uwezekano wa kutatua tatizo la usafiri kwenye Bahari ya Hindi, kwa sababu maamuzi yetu ya nyuma yalilenga kutoa fursa hii kwa wawekezaji binafsi. Ndiyo maana tulipotoa hizo fursa, wawekezaji kama Azam Marine walijitokeza na wengineo kuwekeza. Ni kwenye Maziwa Makuu tu ndiyo Serikali tuliendelea kutoa huduma.
Mheshimiwa Spika, tutaendelea kuhamasisha wawekezaji binafsi lakini pale itakapoonekana kwamba wawekezaji binafsi, hawawezi kabisa kutoa huduma hiyo, Serikali itaangalia uwezekano wa kurudisha TACOSHILI ya zamani ili iweze kutoa huduma katika Bahari ya Hindi. Nimhakikishie tu kwa sasa hivi watu wa Mtwara wanasafiri kwa raha sana kwa njia ya barabara.
MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:- Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, uwanja wa ndege wa Moshi umeharibika sana na ni uwanja wa muda mrefu sana tangu wakati wa Muingereza; na ni uwanja muhimu sana na wenye faida sana kiuchumi hasa utalii, kama ilivyoonekena hapa. Na unawezekana kujiendesha wenyewe na ukaleta faida wala hautategemea viwanja vingine kujiendesha. Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, nilikuwa naomba time frame, je, ni lini Serikali sasa itapeleka hata hizi milioni 350 angalao basi kufanya huo ukarabati ili uwanja huo uweze kutumika? Kwa sababu hii inaonekana inaweza ikawa ni ahadi ya kibajeti, lakini fedha hii isiende kwa wakati; na labda bajeti iishe ikiwa haijapatikana. Naomba nipate uhakika ni lini fedha hii itaenda ili uwanja huo uweze kutumika na uweze kujengewa uzio wake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kulikuwa na mpango wa Serikali wa kuwa na chuo cha mambo ya anga (school of aviation). Naomba kujua kutoka Serikalini, ni lini chuo hicho kitaanza ili kuweza kusaidia watu wetu kupata utaalam wa mambo ya anga katika nchi hii? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, hizo shilingi milioni 350 naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Kilimanjaro kwamba zitatumika katika mwaka huu wa fedha; na taratibu za kumpata mkandarasi wa kufanya hiyo kazi zimeshaanza. Kusema lini, kwa maana ya tarehe naomba unipe subira, wakati hiizi taratibu zitakapokamilika ndipo tutakapojua. Lakini kikubwa ni kwamba fedha hizi kwa vyovyote vile lazima zitatumika katika mwaka huu wa fedha kabla haujaisha. Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu shule ya aviation, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna mipango hiyo katika viwanja vingi na hizi zote zinaunganika. Kwa sababu katika masuala ya kufundisha, kwa mfano wenzetu marubani wanahitaji kutumia viwanja vingi na kimoja kati ya viwanja hivi ni hiki cha Moshi. Tuna shule, NIT wameanzisha kwa ajili ya kufundisha marubani na ndege zitakuwa zinatumia viwanja hivyo vyote ambavyo viliainishwa toka mwanzo kama sehemu ya aviation school. MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa vile muda umekwenda itabidi sasa tuchukue swali moja la msingi na muuliza swali tu. Tunaendelea na Mheshimiwa Omary Ahmed Badwel ambaye atauliziwa kwa niaba na Mheshimiwa Daniel Mtuka.
MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuunganisha mikoa miwili ni jambo kubwa sana; na kwa kuwa barabara ya Manyoni - Sanza pamoja na ile ya Chali - Igongo zote zina hadhi ya TANROADS, na tatizo kubwa ni Daraja la Mto Sanza; daraja hili muda mrefu limekuwa ni wimbo. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa daraja hili ili sasa kuunganisha mikoa miwili?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa anayoifanya kufuatilia suala hili, kwa sababu sio mara ya kwanza kulisema hapa. Amemuona Waziri wangu kwa ajili ya utekelezaji wa suala hili. Utakumbuka tulikuambia na ninaomba kupitia nafasi hii wananchi wako wajue kwamba daraja hili ni kipaumbele katika Wizara yetu katika bajeti itakayofuata, labda kama vyanzo vya fedha mtavipunguza, lakini kama hamtavipunguza tuna uhakika tutapata fedha za kutosha kwenye bajeti ya Wizara kuhakikisha na Daraja hili la Mto Sanza tunaliingiza kwenye bajeti.
MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba barabara hii inasimamiwa na Halmashauri ya Moshi, lakini kwa kuzingatia kwamba ilikuwa ni ahadi ya Mheshimiwa Rais Mstaafu na aliyekuwa Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Magufuli, ambaye ni Rais kwa sasa, katika bajeti ya mwaka 2015 waliahidi kutoa shilingi milioni 810 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, lakini mpaka sasa hivi wananchi wa Old Moshi na wa Kilimanjaro kwa ujumla wake hawajaona chochote kinachoendelea zaidi ya ahadi ya pesa ambazo ziko kwenye makaratasi tu.
Sasa tunataka kujua, watupe time frame, ni lini barabara hii itaanza na ni lini hii zabuni itapitishwa ili barabara ile iweze kujengwa kwa kiwango cha lami, ukizingatia barabara ile kule Tsuduni kuna vivutio vya utalii, kuna vipepeo, kuna waterfalls na kadhalika? Sasa Mheshimiwa Waziri atueleze ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami una hatua. Tunaanza na upembuzi yakinifu, baada ya hapo tunafuata usanifu wa kina na baadaye ndipo tunaingia kwenye ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Fidelis Owenya kwamba barabara hii kutokana na ahadi ambayo Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne aliiitoa tayari imeingizwa katika mchakato. Tumemaliza hatua ya kwanza ya upembuzi yakinifu, sasa hivi tunakaribia kumaliza hatua ya pili ya usanifu wa kina ambapo kilichobakia sasa ni kupata tu taarifa ya mwisho ya msanifu na baada ya hapo barabara hii itaanza kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, isitoshe, kama ambavyo nilivyosema katika jibu langu la nyongeza, Mheshimiwa Owenya barabara hii imeshatengewa fedha kwa mwaka huu wa fedha na bahati nzuri sasa hatua zile za mwanzo ambazo zilikuwa ni za lazima zikamilike kabla ya ujenzi kuanza sasa zinakaribia kukamilika. Nimhakikishie ahadi tutaitekeleza kama ilivyoahidiwa na viongozi wetu wakuu.
MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza na swali langu napenda kulielekeza kwa Waziri, Wizara ya ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Swali langu linafanana sana na swali lililoulizwa hivi punde; ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Ziba kwenda Ikinga, Simbo mpaka Tabora na Ziba, Choma mpaka Shinyanga hasa ukizingatia hizi ni ahadi za Mheshimiwa Rais na huu ni mwaka wa 2017? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Seif Gulamali na wananchi wote wa Manonga na Wilaya ya Igunga kwa ujumla, kwamba ahadi zote ambazo viongozi wetu wamezitoa katika kipindi hiki cha miaka mitano tutazitekeleza. Lazima twende hatua kwa hatua, hatuwezi kutekeleza ahadi zote kwa mwaka mmoja wa fedha. Na nimhakikishie tu kwamba kabla ya kipindi hiki cha miaka mitano barabara hii tutakuwa tumeitendea haki kama ambavyo viongozi wetu wakubwa wa kitaifa walitolea ahadi.
MHE. PASCHAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Barabara ya kutoka Mji Mdogo wa Mlowo Wilaya ya Mbozi kuelekea Kamsamba ni barabara muhimu sana kwa kuwa inaunganisha Halmashauri ya Mbozi lakini pia na Halmashauri ya Momba. Pia barabara hii inaunganisha Mkoa mpya wa Songwe na Mkoa wa Rukwa na Katavi. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nadhani amewahisha swali hili kwa sababu anajua kuna swali lingine zuri kabisa la Mheshimiwa Silinde linakuja; lakini nimhakikishie tu kwamba kila ambapo Serikali hii imeahidi itatekeleza.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru sana. Kwa kuwa barabara inayokwenda katika mbuga za wanyama katika Mkoa wetu wa Iringa ni barabara ya kiuchumi pia na Serikali kwa mara ya mwisho nilipouliza swali hilo iliniambia kwamba inafanya upembuzi yakinifu.
Je, ni lini sasa Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara hiyo kwa sababu hii barabara tunategemea kwamba kama itakuwa imemalizika, uchumi wa Iringa kutumia utalii utaongezeka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Ritta Kabati pamoja na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi, walimchukua Waziri wangu wakaenda kuikagua barabara hii na nafahamu aliyowaahidi alipokuwa kule site.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nikuhakikishie, yale ambayo Waziri wangu aliwaelezeni kule site ni lazima tutayatekeleza.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Hili swali la ujenzi wa daraja ninaliuliza leo ni mwaka wa saba mfululizo nikiwa ndani ya Bunge hili Tukufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na jitihada ambazo nimeanza kuziona ambazo zinaweza kuzaa matunda hivi karibuni, ni kwamba wametangaza tender tarehe 11.01.2017; sasa ninachotaka kujua ni kwamba, ili tupunguze maneno maneno mengi, je, Serikali itakamilisha lini utaratibu wa tenda ili ujenzi huo uanze? Wananchi wangu kule wameshachoka story hizi wanataka waone daraja likiwa limejengwa kwahiyo hicho ndiyo kitu cha kwanza, commitment ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili; ni kwamba palipokuwa na ahadi ya ujenzi wa daraja ilikuwa inaambatana na muendelezo wa ujenzi wa barabara ambayo Mheshimiwa Haonga alikuwa ameuliza katika swali la nyongeza kutokea pale Kamsamba mpaka Mlowo kilometa 166.
Sasa ninachohitaji kujua ni kwamba wakati wa awamu ya nne Waziri Mkuu alipokuwa analijibu hili swali alisema umeingizwa katika mradi wa MCC 3 lakini bahati mbaya wale watu wa Marekani wa MCC 3 walishajitoa katika kuhudumia miradi ya ndani ya nchi yetu. Sasa, je, Serikali ile miradi ambayo iliondolewa na MCC katika Serikali hii ya Awamu ya Tano itatekelezwa vipi ili kuhakikisha kwamba daraja linakamilika na liendane na ujenzi wa lami? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi Mheshimiwa Mbunge na ninaamini ni kwa niaba ya wananchi wake, wanahoji udogo udogo au utaratibu unaotumika, kwamba kasi yake kama ya konokono. Mimi nikuhakikishie, hii ni Serikali ya Awamu ya Tano, Serikali hii iko tofauti, Serikali hii imewaahidi wananchi sehemu mbalimbali na umeshaanza kuona sehemu mbalimbali magoli yanaanza kufungwa. Ninakuhakikishia na goli lako litafungwa, daraja na hizo barabara ninazoongelea kabla ya miaka hii mitano haijakwisha. Tuache utaratibu huu wa kitaalam ukamilike na nina uhakika kwa kuwa wameshaanza haitachukua muda kuikamilisha hii kazi ya usanifu na mimi mara baada ya hapo, kwa kuwa fedha tayari tunazo nitahakikisha nalisimamia hili eneo likamilike na hasa kwa sababu mwenzako, jirani yako; na mimi nawasifu sana ninyi Wabunge wawili, wewe na Mheshimiwa Ignas Aloyce Malocha. Ninawasifu sana kwa ushirikiano mnaotumia katika kuhakikisha Daraja la Momba linajengwa.Ni daraja linalohudumia watu, halina Silinde wala halina Ignas Malocha. Mheshimiwa Ignas Malocha anakuja ofisini, Silinde anauliza hapa, wote wanawalenga wananchi wa Momba pamoja na watu wa Kwela.
Mimi niwahakikishie, kazi hii tutaifanya kwa umakini na kama ambavyo tumekuwa tukiwaahidi tutaikamilisha kwa wakati muafaka kabla hiki kipindi chetu hakijaisha.
MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa hali ya Momba ni sawa sawa na Moshi Vijijini, kwa sababu Rais wa Awamu ya Nne Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliahidi kujenga barabara ya Kibosho kwa Raphael kupitia central mpaka International School; na kazi hiyo ilianza lakini mkandarasi ameondoka site. Vilevile Rais wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Pombe Magufuli aliahidi kujenga barabara ya Mamboleo mpaka Uru Shimbwe kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba nijue ni lini ahadi hizi zitatekelezwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Komu tuonane ili anipe taarifa za zaidi hasa ya huyo mkandarasi ambaye anasema ameondoka site. Njoo ili tuhakikishe huyo mkandarasi anarudi kwa sababu tulishatoa maelekezo wakandarasi wote ambao walikuwa wamesimama kwa sababu ya kutolipwa warudi site, sasa nashangaa leo naambiwa kuna mkandarasi huku tena kwenye barabara muhimu sana ya ndugu zangu kule wa Kilimanjaro. Hebu njoo ofisini tuongee kwa undani tulifanyie kazi na wataalam wetu wa Mikoa wa TANROADS au wa Halmashauri.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti nikushukuru kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa Daraja la Magala na barabara yetu ya Karatu - Mbulu - Haydom - Sibiti Mheshimiwa Waziri aliahidi kwamba itaanza upembuzi yakinifu, sasa swali, je, barabara hii iko kwenye hatua gani, upembuzi yakinifu na lini anafikiri kwamba itaanza ujenzi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Massay, tulikubaliana kwamba twende site kwa sababu kuna mambo kama matatu ya msingi katika eneo lake. Mimi nimuombe, tutakapofika site tukaifanya kazi inayokusudiwa kuifanya baada ya hapo kama kutakuwa na maswali zaidi ndipo aulize, lakini kwa sasa nimhakikishie kwamba ahadi yangu ya kwenda site iko pale pale na tumekubaliana kipindi gani twende. Mimi naomba tuitumie fursa hiyo kushughulikia mambo makubwa yote matatu ikiwa ni pamoja na Daraja la Mto Ugala, barabara hiyo aliyoitaja Karatu - Mbulu - Haydom vilevile pamoja na wale watu wa Yaeda Chini ambao hawana mawasiliano ya simu.
MHE. LIVINGSTONE J. LUSINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake. Hata hivyo napenda niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, punde wakati akijibu maswali leo asubuhi, amesema barabara ili ijengwe kwa kiwango cha lami inapitia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina; na kwa muda aliouonyesha ni kama vile kila kitendo kinachukua zaidi ya miaka miwili.
Je, kwa miaka iliyobaki kabla hata ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina haujaanza kufanyika, Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Jimbo la Mtera kwamba barabara hiyo itakamilika mwaka 2020?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema barabara hiyo itaendelea kujengwa kwa kiwango cha changarawe na sasa hivi barabara hiyo bahati nzuri inajengwa. Je, Naibu Waziri yuko tayari kuongozana na mimi ili akaone hicho kiwango cha changarawe anachokisema kwamba kinajengwa badala ya kiwango cha changarawe naona wanajenga kwa kiwango cha tope, yuko tayari twende tukaone site? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitumie fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Lusinde kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwatetea wananchi wa Mtera.
Mimi nimhakikishie, Serikali hii iko pamoja naye na hicho anachokidhania kwamba inachukua zaidi ya miaka minne kufanya hizi kazi mbili, kwanza hii barabara siyo ndefu sana kwa hiyo, haitaweza kuchukua miaka minne. Ni barabara fupi na tunaweza tukaingia kwenye hatua ya design and build, kwa maana ya unafanya yote kwa wakati mmoja. Nikuhakikishie tu ahadi yetu kwenye hilo tutaitekeleza kwanza hii barabara ni ndogo sana. Siamini kama wewe unafahamu ni barabara fupi inayohitaji gharama siyo kubwa sana kwa hiyo, tutaikamilisha kwa wakati kabla ya kipindi hiki cha miaka mitano hakijaisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, kwa kweli naomba kwa heshima kabisa ikiwezekana hata leo jioni hebu twende tukalione hili ili tuweze kulishughulikia kwa haraka. Kama ni kweli ni tope siyo sahihi kabisa.
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nichukue nafasi hii kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri hayakugusa ahadi ya Mheshimiwa Rais aliyoitoa katika barabara ya Mji wa Mbulu na ahadi hiyo iliwagusa wananchi wa Mji wa Mbulu wakati wa uchaguzi. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anatuambia nini kuhusu utekelezaji wa ahadi hii ambayo imesahaulika, hadi sasa mwaka mmoja umeisha baada ya uchaguzi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii hatujaisahau. Tulichokifanya katika mwaka wa kwanza ni kutekeleza barabara zile ambazo wakandarasi walikuwa wameondoka site kwa kutolipwa madeni yao, na unaona kwamba sasa hivi tumefanya kazi kubwa sana na barabara nyingi zinaanza kukamilika baada ya kulipa madeni ambayo walikuwa wanayadai. Nimhakikishie, kuanzia bajeti ijayo, tunaanza sasa, kwanza kukamilisha zile barabara zilizobakia za nyuma ili tusiwe tunadaiwa daiwa riba pamoja na usumbufu, lakini vilevile tuanze sasa kwa kiwango chochote tutakachoweza kwa mwaka ujao wa fedha barabara zile mpya tulizoziahidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie katika safari yangu ambayo Mheshimiwa Massay tumekubaliana tutafika mpaka Mbulu na ninadhani nitalala Mbulu Mjini ili tuliangalie hilo kwa undani pamoja na hayo matatizo matatu makubwa ambayo nimeyaongea kabla.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, shida ya barabara ya Jimbo la Mtera inafanana sana na shida ya barabara ya Jimbo la Ukonga. Barabara ya kutoka Banana - Kitunda - Kivule - Msongora ni barabara ambayo imeahidiwa kwa miaka ishiri ambapo Mheshimiwa Rais wa sasa alikuwa Waziri kwenye eneo hilo aliahidi na haikutekelezwa, miaka kumi ya Mheshimiwa Kikwete iliahidiwa haikutekelezwa. Kwenye bajeti ya mwaka jana ilionyesha kuwa TANROADS wanasaida kujenga angalau kilometa 3.2.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapozungumza hapa walishaenda wakafanya survey wakapata na mkandarasi yupo anasubiri. Shida iliyopo ni kwamba fedha hazipo na ieleweke tu kwamba barabara hii ndiyo inayohudumia Kata ya Kitunda, Kata ya Mzinga, Kata ya Kivule, Kata ya Msongora na mojawapo ya shida ya barabara hii imeleta madhara makubwa kwa sababu shule zilizoongoza kwa kufanya vibaya, shule ya msingi Kitonga ipo eneo hili na shida mojawapo ya watoto wale kufeli ni kwamba wanatoka mjini kati, wanaenda kule hakuna usafiri wanatembea kwa miguu, kwa hiyo wanatega shule na wamefeli ndiyo maana wakaomba walimu wasiadhibiwe kwa sababu hii.
Sasa naomba nimuulize Mhesimiwa Naibu Waziri ni lini baabara hii itaweza kutengenezwa kwa kiwango cha lami au hata changarawe ili magari yatoke Banana mpaka Msongora – Kitonga, walimu na watumishi wengine, wanafunzi waende shuleni kwa uhakika kupunguza shida iliyopo sasa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waitara anafahamu kwamba tatizo hili aliliwasilisha kwangu vilevile kupitia kwa Afisa Elimu Sekondari ambaye naye alilalamika sana kuhusiana na kufeli shule zake, kuwa za mwisho katika Mkoa wa Dar es Salaam; na alisema kwamba mchango mmojawapo ni matatizo ya hii barabara na wanafunzi wanapangiwa kule mbali kwa sababu shule za karibu huwa zinajaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimuhakikishie, Serikali imelichukua hili, tutalishughulikia ili turekebishe haya. Naomba unipe fursa niwasiliane na TANROADS Mkoa wa Pwani nipate taarifa zao za karibuni maana yake nilishawaambia kuhusu hili tatizo baada ya kupata hiyo taarifa kutoka kwa Afisa Elimu wa Sekondari wa Wilaya ya Ilala, na baada ya kujua sasa alifanya nini baada ya malalamiko yale nitakuja nikuambie hatua ipi tunaichukua.
MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa kunipa nafasi nilulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya kutoka Mtwara hadi Newala – Masasi kipande cha kutoka Mtwara hadi Nnivata tender ilishatangazwa, na kwa mujibu wa maelezo ya Meneja TANROADS Mtwara ni kwamba mkataba ulisainiwa tarehe 16 Januari, lakini ukimuuliza Waziri anasema hajui, Naibu Waziri hajui na wengine wanakwambia mara mkataba uko kwa Ofisi ya Mwanasheria wa Serikali. Sasa nilitaka kujua mkataba umesainiwa au haujasainiwa na inachukua muda gani kujua ndani ya ofisi hiyo hiyo inamchukua Waziri muda gani kupata taarifa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ghasia na kupitia kwake na wananchi wake wa Mtwara Vijijini kwamba Serikali kama ambavyo imepanga kwenye bajeti ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami katika mwaka huu wa fedha itatekeleza ahadi hiyo na tofauti ambayo ameieleza kati ya tunachokifahamu sisi na anachoambiwa na TANROADS Mkoa kule kimetokana na sintofahamu iliyotokea kwa mkandarasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kila kitu kukamilika na document kuwa tayari kusainiwa kuna kipengele ambacho ilibidi Mwanasheria Mkuu wa Serikali akikamilishe kukiangalia na kukiweka sawa kabla mkataba haujasainiwa.
Kwa hiyo, ninavyofahamu mimi na kwa namna Mheshimiwa Waziri wangu alivyonieleza na namna nilivyoambiwa na TANROADS pamoja na Katibu Mkuu mkataba huu utasainiwa muda wowote katika wiki hii kwa sababu Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu namshukuru ametusaida kulitatua lile tatizo ambalo lilikuwa linatusumbua, kwa hiyo mkataba utasainiwa muda wowote kati ya wiki hii na wiki ijayo. Kikubwa na cha msingi fedha tumetenga, tuko tayari kuanza ujenzi, process za kumpata mkandarasi wa kujenga tayari sasa zimefikia mwisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba Mheshimiwa Ghasia pamoja na mengi anayotushauri kwenye hili atuvumilie kidogo, lakini kubwa ni kwamba zile fedha tulizozitenga shilingi bilioni 21 zitatumika katika mwaka wa fedha kuanza ujenzi.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nisikitike kwa majibu yaliyotolewa na Wizara juu ya swali hili, haya siyo majibu sahihi kwa swali hili. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Mji wa Kakonko nyumba zinazozungumziwa zilikuwepo kabla ya mwaka 1967 kwa sheria iliyotungwa. Haiwezekani survey inayofanyika ikafanyika na kukuta hakuna nyumba hata moja inayokidhi
vigezo vya kulipwa. Kwa maelezo hayo, Serikali ya Chama cha Mapinduzi imepanga kuwatia umaskini wananchi katika Mji wa Kakonko. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, survey ile inaonesha tangu miaka tisa iliyopita hakuna aliyekuja kuzungumzia kwamba nyumba zile hazitalipwa. Wananchi wamekuwa wakipigwa picha wanapewa matumaini ya kulipwa leo taarifa inakuja hawawezi kulipwa. Sasa nauliza, je, ana uhakika kwamba
hakuna nyumba iliyokuwepo kwa sheria iliyokuwepo kabla ya mwaka 1967?
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa majibu
hayajakidhi vigezo vya nyumba zilizopo katika eneo hilo ambazo zitabomolewa na zote hazina vigezo, Serikali iko tayari kwenda kufanya survey upya katika Mji wa Kakonko na kujiridhisha kwamba zipo nyumba ambazo zinakidhi vigezo na hivyo wananchi wake waweze kulipwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, hizi sheria tunatunga wenyewe humu ndani ya Bunge. Sheria ya siku za nyuma toka mwaka 1932 mpaka ilipokuja kurekebishwa mwaka 1967 na
sasa tunayo ya mwaka 2007 zote zilitungwa ndani ya Bunge. Naomba sana ndugu zangu tuheshimu kile ambacho tulikubaliana wote ndani ya Bunge hili.
Mheshimiwa Spika, naomba kurudia jibu langu la
msingi kwamba katika barabara hiyo survey imefanyika na hakuna nyumba ambayo ipo nje ya mita 22.5 kwa sheria ya 1967 na nje ya mita 7.5 ya nyongeza kwa sheria ya mwaka 2007. Kwa hiyo, kurudia survey wakati mwingine tunapoteza
fedha lakini kama kutakuwa na tatizo mahsusi, naomba Mheshimiwa Bilago awasiliane na meneja TANROAD Mkoa halafu tutaanzia hapo.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa utaratibu wa kuweka ‘X’ kwenye nyumba au shughuli ambazo zinafanywa na wananchi kwenye maeneo ambayo Serikali inataka kuweka miundombinu ni utaratibu ambao sasa umezagaa nchi nzima. Kwa kweli unaathiri sana maendeleo ya wananchi wetu kwa kuwa utaratibu huu unazuia wananchi kuendeleza
maeneo yao na inachukua muda mrefu kwa Serikali kuanza kutekeleza mipango yake. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, sasa, je, Serikali haioni kwamba umefika wakati wa kuubadilisha utaratibu huu wawe wanapanga mipango yao wakikamilisha ndiyo waende kuzungumza na wananchi kwenye maeneo husika? Mfano mzuri ni kwenye maeneo ya Jimbo langu la Mtama ambako inasemekana utapita mradi wa reli, zimewekwa ‘X’ kwa muda mrefu. Kama Serikali itakubaliana na utaratibu huu wa kubadilisha sasa utaratibu watoe tamko hapa niwaambie wananchi wangu wapige chokaa waendeleze maeneo yao. Makofi/Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama mtagundua sasa hivi kila barabara inayojengwa tunaweka mawe mita 30 kila upande ili tusisubiri wakati wa kupanua barabara. Watu wajue toka mwanzo kwamba barabara hifadhi yake ni mita
30 kila upande. Tatizo lililojitokeza siku za nyuma hizo alama zilikuwa haziwekwi kwa hiyo watu walikuwa wanavamia hifadhi ya barabara wengine kwa kujua na wengine kwa kutokujua.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa sasa ni kweli baada ya kupitishwa hii sheria mwaka 2007 tumeamua kuweka alama mita 30 kila upande na yeyote aliye katika eneo hilo tunamwekea ‘X’ ajue kwamba yupo ndani ya hifadhi ya barabara na hivyo anatakiwa aondoke. Sio suala la kufidia,
wale wenye haki ya kufidiwa, wanakuja kufidia wakati kutakuwa na mradi maalum utakaopita mahali hapo na hatimaye fedha zinapopatikana. Hiyo ndiyo dhana ya kuweka alama hizi za mita 30 na tumefanya hivyo nchi nzima.
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Majibu ya Waziri hayajaniridhisha. Barabara hii ina umuhimu mkubwa kwani hutumiwa na watalii wengi wanaotoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta kuja Serengeti National Park. Je, hamuoni kwamba tunapoteza watalii wengi kutokana na ubovu wa barabara hii?
Mheshimiwa Spika, kwa taarifa niliyoipata ni kwamba barabara hii ilikuwa iishe 2017, lakini nashangaa kwa majibu ya Waziri kwamba barabara hii inaisha 2018. Sasa nataka
nijue barabara hii inaisha 2017 au 2018? Je, upembuzi yakinifu unaisha 2017 au 2018? Je, kwenye bajeti 2017 barabara hii imetengewa bajeti?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii unaisha mwaka 2018 kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi. Nimhakikishie Mheshimiwa Sokombi kwamba hicho tunachokisema ndicho tutakachokitekeleza na umuhimu wa barabara hii
umetokana na hao watalii wengi ambao wameanza kuonekana. Tunataka barabara hii pamoja na hiyo nyingine, kama unavyofahamu tunajenga barabara nyingine ya kutoka Sanzatu, zote hizi tutazijenga kwa ajili ya kufungua utalii. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge hawa watalii mara baada ya kukamilisha kujenga barabara hizi wataongezeka.
MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru. Kwa kweli niendelee kusikitika kwamba Serikali inashindwa kuona barabara ambazo zinaweza zikaongeza chachu ya ukuaji wa uchumi kwenye nchi yetu kupitia utalii.
Mheshimiwa Spika, ningependa kujua ni lini Barabara ya Tarime – Nata kwa maana ya kwenda Mugumu itakamilika kwa kiwango cha lami? Mheshimiwa Naibu Waziri anatueleza
kwamba upembuzi yakinifu unakamilika 2018, watalii wengi wanaotoka Kenya wanapita Tarime wanaenda Serengeti, tukiboresha ile barabara kwa kiwango cha lami tutakwenda kukuza uchumi wetu kwa sababu watalii wengi watapita
kwa sababu barabara inapitika. Ni lini sasa Serikali itajicommit, isiseme leo itamaliza upembuzi yakinifu 2018, ione kuna uhitaji wa haraka sana wa kujenga barabara ya Tarime – Mugumu na iweze kumalizika ndani ya mwaka mmoja kama ikiwezekana tuweze kukuza uchumi wa nchi yetu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, katika ujenzi wa barabara tuna hatua tatu muhimu na hatua hizi ni lazima zikamilike. Hatua ya kwanza ni upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Baada ya Serikali kuiona barabara hii kwamba ina umuhimu na inaongeza mapato yetu katika utalii imeamua kuianza hiyo kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kazi hiyo itakamilika mwaka 2018.
Mheshimiwa Spika, baada ya kazi hiyo kukamilika,
hatua ya pili itakayofuata ni kutafuta fedha za ujenzi wa barabara hiyo. Huwezi ukajenga barabara bila fedha. Kwa hiyo, Serikali itatafuta fedha ili tuanze kujenga barabara hiyo.
Tukishapata fedha tutatangaza tumpate mkandarasi wa kuanza kujenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, ningeomba tu Mawaziri na Naibu Mawaziri wakafanye utafiti kwanza wa kina kabla ya kujibu maswali.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu aliyojibu Naibu Waziri, haoni wakati umefika sasa ukiona kuwa mizigo iliyokuwa inapimwa kwa tani hapo mwanzo na hivi sasa kuchanganywa na CBM haoni ipo haja kwa hivi sasa mzigo wote ule ukapimwa kwa tani badala ya CBM ukizingatia
Wazanzibari wanategemea chakula sana kutoka Tanzania Bara kwa ndugu zetu wa damu na vilevile biashara kubwa iliyopo kati ya Zanzibar na Tanzania Bara ndiyo uchumi mkubwa wa Zanzibar ukiacha zao la Karafuu kuzaa mwaka hadi mwaka?
Swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri utakuwa tayari kufuatana na mimi mguu kwa mguu na tarehe unipe ili Hansard zikae sawa kwenda kuona kama alivyofanya Waziri aliyepita Mheshimiwa George Harrison Mwakyembe na
akaona matatizo yaliyopo pale na mengine akayapatia ufumbuzi lakini kwa bahati mbaya akaondoka Wizara ile, ikiwemo umeme uliopo pale ni hatari chini, mabonde ya mpunga yaliyopo pale hivi sasa bila kukusudia baada ya bandari na wakati wenye meli wanalipa gharama zile.
Je, ni lini tutafuatana mimi na wewe ili kwenda kuona kadhia zilizopo pale ikiwemo na Kampuni ya Hisab kushindwa kufanya majukumu yake?
Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, hivi vyote viwili ni vipimo vinavyotumika kutegemeana na aina ya mzigo ulivyopakiwa, ni lazima vyote hivi viwili vitumike the Cubic Bank Metres pamoja na tonnage. Kutaka itume tonnage peke yake kuna
aina ya mizigo itatoa hali siyo nzuri kwa TPA namna ya kuihandle kutokana na namna ilivyopakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kutokana na
swali lake la pili na ukijua wazi kwamba Waziri wangu ni mdau mkubwa wa bandari zote za kule Zanzibar nitaomba niwasiliane nae tukubaliane yeye au mimi na tukishakubaliana nitakupangia tarehe, tutakupigia siku ya kwenda huko Zanzibar kulishughulikia hili.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Watanzania wengi
wanategemea bandari na kumekuwa na ukiritimba wa kutozwa kodi mara kwa mara wafanyabiashara sasa hivi wanakwepa bandari zetu, je, Serikali ina mikakati gani kuweka utaratibu mzuri wa utozaji kodi katika mizigo ya wafanyabiashara ili biashara zipate kupita katika bandari zetu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali langu la msingi kwamba upangaji wa bei na hiki kitabu ambacho kinatumika na watu wa TPA wakati kinaandaliwa
kabla hakijapitishwa huwa kinashirikisha wadau wa bandari. Labda tu nimhakikishie kwamba tutakapofika muda wa kureview hizi rates tutahakikisha wadau tunawashirikisha tena,
inawezekana dynamics zimebadilika kwamba mazingira ya wakati bei hizi zinapangwa ni tofauti na mazingira ya sasa. Tutamshirikisha na nitaomba sana comments zako na wadau
waziweke ili tupate kitabu kipya ambacho kitazingatia hayo ambayo wewe umeyasema na Mheshimiwa aliyeuliza swali la msingi ameyasema.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika kijiji cha Kirando mwambao wa Ziwa Tanganyika, TPA wameweka mtu wao kutoza ushuru mzigo wowote unaotoka pale katika kijiji cha Kirando wakati TPA hawajaweka huduma yoyote. Hamna kibanda, hamna hata
choo, hamna chochote walichoweka lakini kila mwananchi anayesafirisha mzigo kwenda Kabwe, kwenda Mwandakerenge, kwenda Mvuna anatozwa ushuru na watu wa TPA.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kuna huduma nyingi za bandari na mojawapo ni kuwa na vyoo, sehemu ya kupumzikia lakini kuna huduma zile za kutoa mzigo kutoka kwenye maji na kuupeleka kwenye nchi kavu. Ile huduma ina gharama, inahitaji kulipiwa. Kwa hiyo, wale ambao wanapata hiyo huduma hata kama hizi huduma zingine hazijakamilika kwa vyovyote vile watatakiwa walipie ili kurecover zile gharama wanazotumia watu wa bandari.
Mheshimiwa Spika, labda tu hoja yake ni kwamba
tuboreshe hii bandari ya Kirando ili huduma zote za bandari ikiwa ni pamoja na uwepo wa vyoo na huduma zingine eneo la kupumzikia abiria tuzijenge. Hilo nimelipokea, tutalifanyia kazi.
MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti,
nishukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa Singida Mjini ni mji ambao unakua kwa kasi sana kwa sababu Serikali imehamia Dodoma, Serikali haioni haja
sasa ya kutenga fedha kwenye bajeti ya mwaka huu ili uweze kuwalipa fidia wananchi wa kwenye hilo eneo la Manga na Uhamaka ilitoe hilo eneo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa
Serikali imeanza ukarabati kwenye uwanja wa ndege wa sasa, je, Serikali itamaliza ukarabati huo lini ili na sisi tuweze kuutumia uwanja huo kwa kupanda ndege? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Sima na wananchi wa Mji wa Singida wawe na subira, tupate taarifa ya mwisho ya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili hatua ya pili ifuate. Si rahisi tukaanza
kutenga fedha kwa mwaka huu na hasa vipaumbele ambavyo tulipitisha mwaka huu, mtakumbuka ambavyo tulipitisha katika mpango wa mwaka huu wa fedha, vinahitaji rasilimali fedha nyingi na hivyo hii kazi tutaifanya mara badaa
ya kazi hii ya upembuzi yakinifu kukamilika. Itakuwa sio rahisi kwa mwaka huu, mnafahamu kwamba bajeti ya mwaka huu tumeshaipitisha katika ngazi ya Kamati na hivi sasa tunaanza kuingiza katika hatua za Bunge Zima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu ukarabati;
nimhakikishie Mheshimiwa Sima kwamba kazi hii ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina itakapokamilika suala la ukarabati litafuata.
MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nishukuru kwamba uwanja wa ndege wa Lindi upo kwenye mapendekezo ya Serikali ya kutaka kuufanyia
ukarabati lakini kwa sasa wananchi wa Lindi tunakosa huduma ya ndege mpaka twende Mtwara kwa kuwa uwanja ule sasa hivi umekuwa ni chakavu sana. Nataka commitment ya Serikali, ni lini itakamilisha ukarabati wa uwanja wa ndege
wa Lindi ili ndege zianze kutua kama kawaida?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli uwanja wa Lindi ni kati ya viwanja 11 vinavyofanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kutumia fedha za mkopo kutoka Benki ya Dunia. Kimsingi kazi hii itakapokamilika ndipo
tutapata ratiba kamili ya tuanze wapi na tumalizie wapi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu nimkakishie
Mheshimiwa Bobali, kwamba kutokana na umuhimu wa kuhakikisha wananchi wa Lindi nao wanakuwa na kiwanja cha ndege, tutahakikisha katika kuangalia priority, na lindi tutaiangalia kwa macho matatu.
MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaishukuru sana Serikali kwa kupanua uwanja wa ndege wa Dodoma, lakini upanuzi huo umeathiri sana barabara ya Area D round about ya Shabiby, na wananchi wanaotoka Area D na Majengo Mapya
hurudi mpaka Kisasa kuja mjini kilometa nyingi.
Je, Serikali iko tayari kujenga barabara nyingine ya
lami kuwapunguzia safari ndefu wananchi wanaokaa maeneo ya Area D na Majengo Mapya?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunahitaji kuangalia upya namna Area C na Area D inavyoweza kufikika ukitokea Dar es Salaam bila mzunguko huo mkubwa kwa kuhakikisha tutapata barabara nyingine badala ya ile ambayo sasa hivi imefungwa kwa ajili ya kiwanja cha ndege. Kwa hiyo, namhakikishia Serikali nayo inalifikiria na tutalifanyia kazi kwa haraka hilo.
MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa sababu pia uwanja wa Musoma upo kwenye ajenda hiyo na kwamba upembuzi yakinifu umeshafanywa. Kwa sababu kutengwa fedha ni kitu kingine na ujenzi ni kitu kingine, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi katika uwanja wa Musoma?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Sokombi na wananchi wote wa Mji wa Musoma na viunga vyake ambao kwa kawaida wamezoea kutumia uwanja wa ndege wa Musoma kwa safari zao kwamba Serikali iko makini na katika muda wa
hivi karibuni kama mtakumbuka tuliwaambia katika viwanja vitatu vya mwanzo tutakavyohakikisha kwamba ujenzi wake unaanza haraka ni pamoja na Musoma, Nduli na Mtwara.
Naomba nimhakikishie Serikali ipo mbioni kuhakikisha viwanja hivi vitatu vinapata fedha na uzuri wake fedha za viwanja hivi vitatu vinatarajia ataketupa fedha maana sio mfadhili ni mkopehsaji hivi karibuni.
MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa fursa niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mheshimiwa
Naibu Waziri katika majibu yake ya msingi ametamka neno fidia, kuhusiana na kuwafidia wale watakaoathirika na ujenzi wa kiwanja cha ndege Singida. Kwa kuwa neno hilo fidia
amewatonesha na kuwakumbusha wananchi wa Mwibara ambao barabara ya Bunda, Kisoria na Nasio kwa miaka mingi hawajafidiwa. Je, wananchi hao wanataka kumsikia Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini watafidiwa au kwenye mwelekeo wa bajeti fidia ya Mwibara ipo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lugola amekuwa akifatilia sana suala la fidia katika eneo lake, na naomba nitumie fursa hii kumdhihirishia yale ambayo tumekuwa tukimwambia ofisini na maeneo mengine ambako amekuwa akituuliza swali hili ni sahihi, kwamba tunatafuta fedha kwa ajili ya kulipa fidia na kwa kweli nimhakikishie mara tutakapopata hizo fedha suala la fidia hilo tutalishughulikia kwa kazi sana.
MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Manispaa ya Iringa na kiwanja cha ndege cha Nduli kimekaa kimkakati, ukizingatia kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii inaboresha Southen Sackett kwa ajili ya kuimarisha utalii Kusini mwa Tanzania. Ni lini sasa Serikali ilikuwa imeahidi kwamba kiwanja hiki kitaboreshwa kama ambavyo Waziri amesema kwamba ni miongoni mwa viwanja 11 ili Manispaa ya Iringa iweze kukua kiuchumi na kimkakati kwa ajili ya ku-boost uchumi wa Taifa ambao kimsingi uchumi unaenda chini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nilijibu swali la Mheshimiwa Sokombi, kwamba katika viwanja ambavyo tunatarajia kupata mkopo hivi karibuni ni kiwanja cha Musoma, Nduli na Mtwara. Kwa hiyo, naomba
nimhakikishie Mheshimiwa Msigwa kwamba kiwanja cha Nduli nacho kipo katika mtazamo wa mbele sana ili kuhakikisha kwamba utalii unaongezeka katika mbuga yetu ile ya Ruaha na kuleta mapato makubwa kwa Serikali.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti,
ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niko kwenye Kamati ya Miundombinu; kwa kuwa uwanja huo huo wa Nduli tayari kuna pesa zimetengwa kwa ajili ya ukarabati huo lakini pia mradi huu umeshakubaliwa na wananchi kwa sababu
Serikali tayari ilishakaa na wananchi waliopo katika eneo lile. Sasa naomba jibu kutoka kwa Serikali, kwa sababu kuna wananchi ambao wamekuwa wakiendeleza maeneo ambayo yataguswa sasa ni lini itaweka alama na ili
wasiyaendeleze maeneo yale ili wakati wa kulipa fidia pesa iwe kidogo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ritta Kabati amekuwa akihoji haya masuala ndani ya Kamati ya Miundombimu na mimi niendelee kumpongeza kwa namna anavyochukua hatua kuwatetea wananchi na kuhakikisha kwamba maslahi yao yanazingatiwa na Serikali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu kama
ambavyo nimekuwa nikimhakikishia mara nyingi katika Vikao vya Kamati, kwamba kazi hii ya kuweka alama tutaifanya hivi karibuni. Naongelea si zaidi ya miezi mitatu, minne ijayo kazi hii itakuwa imekamilika ili kuhakikisha kwamba wananchi wa pale wanajua mipaka ya maeneo tutakayotumia katika kukarabati na kupanua ule uwanja wa Nduli.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Tunaunga mkono juhudi ambayo inafanyika ya kuboresha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dar es Salaam. Lakini kuna malalamiko ya muda mrefu ya wananchi wa Kata ya Kipawa, Ukonga - Kipunguni, Kigiragira kule Buyuni, wanadai fidia Serikali mpaka leo na
wameshindwa kufanya shughuli za kimaendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua ni lini
mgogoro huo utamalizwa na Serikali ili uwanja ukamilike na wananchi wakaendelea kuwa na amani na kuishi maisha ambayo na wenyewe wanapaswa kuishi kama binadamu wa kawaida hapa Tanzania? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tena kumthibitishia Mheshimiwa Waitara pamoja na jirani yake Mheshimiwa Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea kwamba kazi mlioifanya, mtakumbuka mimi ndio Mbunge wa Segerea alinileta kukutana na wale wananchi wa Kipunguni, kuhusiana na suala hili. Niwaombe kwamba tulidhamiria suala hili tutalimaliza katika miaka hii mitano. Mnafahamu baadhi ya maeneo tumeshaanza kulipa fidia, Mheshimiwa Bonnah
Kaluwa unalifahamu hilo na umelifuatilia kwa kasi sana na ninakuhakikishia pamoja na Mheshimiwa Waitara kwamba wananchi wale watalipwa fidia katika miaka hii mitano. Kuna matatizo ambayo yapo katika suala hili la fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tunashughulikia matatizo yaliyoingiliwa katika suala hili la fidia, kuna wajanja wachache walitumia fursa wakatumia fedha vibaya na tumepelekea PCCB wanafanya kazi, tutakapopata taarifa PCCB tutakuja kulimaliza hili suala la fidia katika wale ambao wamebakia kulipa.
MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili limerudi mara ya pili, lililetwa mwaka 2016 na majibu yalikuwa tofauti. Mwaka 2016 waliniambia fedha ziko tayari kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya Uyole ya TANZAM, lakini leo wananiambia upanuzi utaanza pale upembuzi yakinifu na usanifu utakapopatikana na kuonesha viwango vya upanuzi vinavyohitajika na Serikali itakapopata fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 waliniambia fedha tayari ipo. Sasa hili ni tatizo, mara wanahama kutoka
project hii ambayo tulikuwa tumeshaizungumzia, wanarukia project nyingine wakati wameshasema fedha hakuna. Kwa nini upembuzi unafanywa na TAMISEMI badala ya TANROADS?
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwape ushauri kwamba efforts ziwekwe kwenye kupanua barabara kuu inayopita
Mwanjelwa ya TANZAM iwe ya four lanes kwa sababu mchakato wake umeshaanza, nyumba za wananchi zimeshavunjwa, wengine wamevunja kwa hiyari na wengine wanasubiri fidia huu ukiwa mwaka wa pili sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, mtachukua ushauri wangu kurudisha efforts kwenye barabara kuu ya
TANZAM kwa sababu tayari mchakato wake ni kama umeshaanza na ule mchakato mwingine ni kama kuanza
upya?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Mheshimiwa Naibu Waziri kila anapokuja kujibu swali lililoulizwa na Mbunge wa
Upinzani hasa CHADEMA huwa anapenda kusema hata Mbunge fulani wa Viti Maalum wa CCM aliuliza hilo swali?
Mfano, akiuliza Msigwa utamtaja Mheshimiwa Ritta Kabati, nikiuliza mimi utamtaja Mheshimiwa Mary Mwanjelwa? Kwa nini unapenda ku-undermine shughuli za Wabunge wa Upinzani ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri
wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambaye yupo katika sherehe ya uzinduzi wa ujenzi wa reli ya standard gauge,
naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Mbilinyi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie kwamba Wizara hii inachapa kazi na Serikali hii kila inachoamua kutekeleza na inachokisema inamaanisha hicho. Naomba nirudie kwenye jibu langu la msingi kwamba
kazi ya usanifu pamoja na upembuzi itakapokamilika, suala la fedha litashughulikiwa na kazi hiyo itaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, naomba nimhakikishie kwamba ushauri wake umefika, tutawasilisha kwa wataalam
wakaufanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nyongeza tu, mimi bahati mbaya huwa nasema ukweli. Sasa kama Mbunge wa
Viti Maalum amelishughulikia hilo hilo, nadhani ni sahihi naye kusema kwa sababu ninachokisema ni ukweli.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali
moja dogo la nyongeza.
Ni kweli kabisa hili suala nimekuwa nikilifuatilia na kuliulizia kwa miaka mingi. Nakumbuka hata Mheshimiwa
Rais alipokuwa Waziri wa Ujenzi, hili suala nimekuwa nikilizungumza hususan katika barabara ya mchepuko wa
Uyole hadi Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni kama ifuatavyo; pamoja na maswali mazuri ya Mheshimiwa Mbilinyi,
nilitaka kujua ni lini barabara ya mchepuko kutoka Uyole hadi Uwanja wa Ndege itakamalika pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri? Kwa sababu kwenye kikao chetu cha Road Board tulikubaliana kwa pamoja kwamba barabara ya mchepuko lazima itiliwe mkazo, vinginevyo nitakamata shilingi kwenye bajeti yake. Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali Mheshimiwa Mary Machuche Mwanjelwa, Mbunge wa Viti Maalum, swali ambalo huwa linafuatiliwa sana na
Mheshimiwa Mbilinyi, Mbunge wa Mbeya Mjini kama ifuatavyo:- (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mwanjelwa kwamba kazi hii inayofanyika sasa
ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina inafanyika kwa umakini na watu makini. Nikuhakikishie, mara itakapokamilika mchepuko huu tutaujenga.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwanza Naibu Waziri anakiri kwamba barabara ile imejengwa chini ya kiwango;
lakini Naibu Waziri atakubaliana na mimi, alipotembelea Mafia tuliikagua barabara hii mimi na yeye. Barabara hii si ya kufanyiwa matengenezo makubwa, ni ya kurudiwa upya.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, ng’ombe akikatisha kwenye barabara anaacha mashimo, barabara ya lami! Gari likipata
puncture ukipiga jeki, jeki inakwenda chini kama unapiga jeki kwenye tope, kule Mafia wanaiita barabara ya big G
(chewing gum).
Mheshimiwa Spika, sasa nina maswali mawili. Swali la kwanza; kwa kuwa Serikali inakiri kwamba mkandarasi
huyu ameijenga chini ya kiwango, ni hatua gani za kimkataba na za kisheria zimechukuliwa dhidi ya huyu
mkandarasi aliyeisababishia Serikali hasara? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, wananchi wa maeneo ya Kilindoni, Kiegeyani na Utende ambao wahanga wa kubomolewa nyumba zao, wengine walikuwa ni wahanga wa kubomolewa nyumba zao, wengine wamekatiwa minazi yao na mikorosho yao na mazao yao mbalimbali, mpaka leo wengi wao hawajalipwa fidia kutokana na ujenzi wa barabara ile, ningependa nisikie kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri, nini hatma ya waathirika hawa wa fidia? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza nikiri kwamba
nilikuwa Mafia na Mheshimiwa Dau na tuliikagua hiyo barabara. Lakini namuomba tu asiongeze utani sana ndani
ya Bunge, maeneo machafu ni machache ambayo yameshaainishwa na kwa mujibu wa mkataba tumeshachukua hatua ya kumlazimisha mkandarasi kurudia maeneo hayo kwa gharama zake.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu fidia; nimuombe Mheshimiwa Kitwana Dau, kwamba yale tuliyoongea Mafia
ayazingatie. Nikuhakikishie yeyote mwenye haki ya kulipwa fidia atalipwa. Sehemu ya wengi tunaowaongelea pale ni
wale ambao waliifuata barabara.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, lakini vilevile niipongeze sana
Wizara hii.
Katika Serikali ya Awamu ya Nne kupitia Ilani yetu ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi iliweka ahadi kwamba
itaweka lami barabara ya kutoka Korogwe - Kwa Shemshi - Dindila - Bumbuli hadi Soni, lakini mpaka leo hii hakuna ufafanuzi wowote wa kujengwa kwa lami. Nataka Serikali iwahakikishie wananchi kule kwamba barabara ile ni lini sasa itajengwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, hii barabara anayoizungumzia ya kuanzia Korogwe kuelekea Bumbuli – Dindila mpaka kule mwisho ni barabara ambayo amekuwa akiiongelea mara nyingi kuanzia kipindi cha bajeti ya mwaka jana. Nimhakikishie tu yale ambayo tulimueleza, kwamba barabara hii kwanza itaanza kujengwa kutokea Korogwe, kama ambavyo usanifu ulionesha.
Mheshimiwa Spika, lakini la pili, nimhakikishie kwamba haya anayoyasikia kuhusu hii barabara sio kweli. Serikali ina dhamira ya dhati ya kutekeleza ahadi yake ya kuijenga hii barabara kwa lami. Kama nilivyomueleza mara nyingi tu ofisini na maeneo mengine na hata alipomuona Waziri wangu, nikupongeze sana kwa namna unavyofuatilia kwamba barabara hii tutaijenga baada ya kukamilisha hizi barabara ambazo sasa hivi zinatuletea madeni mengi, tunataka tuziondoe kwanza hizo ili tuzianze hizi nyingine, lakini kimsingi katika miaka hii mitano ahadi hiyo tutaitekeleza.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na wakandarasi kujenga barabara chini ya kiwango au kukarabati barabara
chini ya kiwango si jambo geni na Mheshimiwa Spika, na wewe ni shahidi barabara ya kutoka Morogoro kuja hapa
Dodoma sasa hivi tayari imeshavimba, Wabunge wote mnajua. Lakini hiyo barabara ninayoitaja pia inapita Jimboni
kwako, nadhani shahidi tayari sasahivi imeshaanza kuvimba, nimeona tu nikuulizie bosi wangu.
Mheshimiwa Spika, Waheshimiwa Wabunge pia mashahidi, ukarabati unaofanywa hata kwenye barabara
za hapa Dodoma, Area D, Area C pia uko chini ya kiwango, unaigharimu sana Serikali kuwa tunakarabati barabara mara kwa mara pindi Waheshimiwa Wabunge wanapokuja Dodoma.
Mheshimiwa Spika, kingine, barabara ya kutoka Musoma – Bunda na yenyewe pia, ilishaharibika kabla hata
ya kukabidhiwa.
Swali langu, je, mna mkakati gani katika barabara mpya ya kutoka Kisorya - Bunda Mjini - Nyamswa, ambayo
bado haijajengwa, inajengwa kwa kiwango cha lami, ili barabara hiyo isiigharimu Serikali fedha za kutosha na iwe ya kiwango? Naomba jibu zuri na ujue unamjibu Waziri Kivuli na Mjumbe wa Kamati Kuu.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nimechanganyikiwa kwa sababu swali ninalotakiwa nilijibu ni moja, sijui ni jibu lile la Mbande, niache lile la Kisorya au nijibu la Kisorya niache haya ya Mbande?
SPIKA: Nimekuachia kama Engineer nikajua tu utapata moja la kujibu hapo.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka
Morogoro hadi Dodoma na viunga vya Dodoma huwa zinajengwa kwa kufuata mikataba. Katika ile mikataba kuna
viwango ambavyo vinawekwa kwa mkataba na kutokana na kiwango cha fedha. Kwa hiyo, mimi nimhakikishie
Mheshimiwa Ester Bulaya kwamba barabara hizi za kutoka Morogoro hadi Dodoma, pamoja na Dodoma Mjini,
tunahakikisha kwamba kile kiwango cha mkataba kinafikiwa. Nichukue nafasi hiyo kuwapongeza watu wa
TANROADS kwa kuhakikisha kwamba wanasimamia kwa kiwango kikubwa na pale inapotokea mkandarasi
aliyetengeneza hajafikia kiwango, hatua bhuwa zinachukuliwa.
MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Spika,
nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, hii barabara ambayo Mheshimiwa Dau ameisema, wenzenu ndiyo ilikuwa lami ya kwanza
tumeiona katika miaka 50 ya uhuru, kwa hiyo, ilipoharibika baada ya siku chache kwa kweli tumeumia. Sasa hii barabara ukitoka pale round about ya Kilindoni kwenda Utende ni kwamba zaidi ya theluthi mbili ya barabara ni mbovu. Sasa
nashangaa Mheshimiwa Naibu Waziri anavyotwambia
kwamba ni sehemu chache.
Sasa swali langu, je, Mheshimiwa Waziri
atatuhakikishia ushirikishwaji uliokamili wa wadau wote wa
Mafia na watumiaji wa barabara ile kabla ya hiyo kazi ya
kuanza ukarabati ili na sisi tujue hilo andiko mlilosema ninyi
mapungufu machache na kazi itafanyika kwa kiasi gani?
Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nakubali, tutashirikisha wadau na kwa taarifa hii TANROADS Mkoa wa Pwani wawashirikishe wadau wa Mafia kabla CHICO hajaanza kurekebisha yale maeneo ambayo yamegundulika yana matatizo.
MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali hata hivyo nina maswali
mawili kama ifuatavyo:-
(a) Serikali kupitia kwa Naibu Waziri imekiri kwamba ni asilimia 23 tu ya zoezi zima la ujenzi wa nyumba za Wakuu
wa Wilaya na Mikoa ndizo zilizokuwa zimetekelezwa. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kuhakikisha kwamba hizi nyumba zinakamilika kwa wakati katika mwaka wa fedha ujao?
(b) Je, Serikali imepanga kiasi gani cha fedha kwa Wilaya ya Mbogwe katika mwaka ujao wa fedha? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika
jibu la swali la msingi kwamba kuna kiwango cha fedha ambazo TBA wanahitaji kuzipata ili waweze kukamilisha zoezi hili la ujenzi. Naomba tu kama nilivyosema kwamba fedha zimetengwa katika mwaka huu wa 2017/2018 na niombe radhi sina kile kiwango kamili kilichotengwa chini ya TAMISEMI tutaweza kukupa hizo taarifa baadaye baada ya kuwasiliana na watu wa TAMISEMI kujua kiasi gani kimetengwa. Lakini nina uhakika na nimepata taarifa kutoka TBA kwamba mwaka huu wa fedha unaokuja wanaanza kujenga nyumba hizo hadi kuzikamilisha kwa sababu wameahidiwa kupata fedha zilizobakia zote.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa tatizo linaloikabili Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe linafanana na linaloikabili
Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, lakini tofauti iliyoko kati ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe na ile ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga imekwishakujengwa takribani zaidi ya miaka mitano iliyopita, imekwisha kuezekwa, isipokuwa mpaka sasa haijamalizika kwa kutopakwa rangi, haijawekwa madirisha, haijawekwa mfumo wa wiring pamoja na milango na madirisha ambapo thamani ya umaliziaji huo inakadiriwa kuwa 300,000,000. Waziri anawahakikishiaje wananchi wa Wilaya ya Mbinga kwamba mwaka huu hautaisha mpaka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbinga inakamilika? Kwa sababu inapozidi kukaa zaidi ya miaka mitano inazidi kupoteza ubora, inakuwa ni nyumba ya popo, bundi na kadhalika ambayo siyo malengo ya ujenzi wa ile ofisi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilijibu swali la msingi, na bahati nzuri nyumba anayoongelea ina uhusiano wa moja kwa moja na swali la msingi, kwamba
mwaka ujao wa fedha 2017/2018 TBA imeahidiwa kupata fedha kutosha na itakamilisha majengo ambayo imeyaanza.
Aidha, nikupongeze, maana sikutengemea utarudia tena kuliuliza hapa wakati ulishakuja ofisini na tukaongea kwa
kirefu.
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, hivi karibuni TBA walikabidhiwa maeneo ambayo yalikuwa ya National Housing ambayo
yalikuwa katika Halmashauri zetu ili waweze kufanya ujenzi mbalimbali. Lakini kwa bahati mbaya maeneo haya ambayo TBA wamekabidhiwa yaliyokuwa tayari yanatumika na Halmashauri zetu, mfano ni eneo la National Housing lililoko pale Mji wa Babati ambalo linatumika na vijana wetu wa Machinga. Ombi hilo tulishapeleka Waziri ya Ardhi, lakini sasa maeneo yale yamekabidhiwa TBA ambayo iko Wizara ya Ujenzi.
Naomba nifahamu Serikali au Wizara ya Ujenzi iko tayari na TBA kupokesa maombi yetu tena ili eneo hilo la
National Housing libaki kwa vijana wetu wa Machinga wasisumbuliwe kama ambavyo kauli ya Rais imesema?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, Wizara yangu iko tayari
kupokea hayo maombi kama ambavyo umesema na tutayaangalia kwa maslahi mapana ya nchi.
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, nakushuku sana. Kwanza naishukuru Serikali kusema kweli kutenga pesa za daraja kiungo muhimu sana kuhusu barabara. Hii barabara ni muhimu inaunganisha mikoa mitatu; Katavi, Rukwa na Songwe, ni muhimu kwa ajili ya wakulima wetu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nataka jibu sahihi, ni lini Serikali itakuwa tayari kujenga barabara ya lami katika mwambao wa Ziwa la Rukwa ili wananchi wafaidike? Atoe tarehe maalum, ni lini na mwaka gani? Maana hili daraja litajengwa, barabara inaweza ikaendelea hivyo hivyo kuwa tope wananchi wakateseka. Mwambao kule wanalima sana mazao muhimu sana. Kwa kuwa hii nchi ina njaa kila sehemu, tutakuwa tunakomboa sana wananchi wengine kutokana na mwambao wa Ziwa Rukwa kuwa na ardhi nzuri sana…
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Spika, hii
barabara inaanzia Mkoa wa Katavi, Kibaoni inakwenda mpaka Songwe kupitia Mwambao wa Ziwa Rukwa.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Ally Keissy ameuliza kwa sauti nzuri. Nikupongeze sana kwa hilo kwa sababu imenitia moyo.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Ally Keissy kwamba kama ambavyo nimejibu katika jibu la swali la msingi barabara hizi zote tunazitafutia fedha. Nimhakikishie kwamba procurement ya kupata mjenzi wa daraja la Kamsamba ambalo ndilo tunaanza nalo ni katika muda wa wiki mbili, tatu zijazo tutakuwa tumeshakamilisha. Ile hela ambayo ilitengwa mwaka huu itatumika na hatimaye mwaka unaofuata kwa hela hizi ambazo tumezitenga ambazo nilieleza toka mwanzo nazo tutakuwa tumekamilisha hii kazi itakuwa imekwisha.
Mheshimiwa Spika, baada ya hapo, sasa tunaenda kwenye barabara hizo.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, natambua jitihada ambazo zimefanyika kwenye hii barabara ikiwemo ujenzi wa daraja la Momba.
Mheshimiwa Spika, nataka tu niulize swali dogo, barabara hii imekuwa katika ahadi, Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete mwaka 2009 alipokwenda kwenye Halmashauri ya Momba aliweka ahadi ya kujenga hii barabara. Mheshimiwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokwenda kule vilevile alitoa ahadi ya kuhakikisha hii barabara inakamilika kwa sababu hili bonde linaunganisha Mikoa mitatu na ni muhimu kwa mazao yetu.
Mheshimiwa Spika, Rais wa Awamu ya Tano Mheshimiwa John Pombe Magufuli alisema katika Serikali yake hataki kusikia mambo ya michakato, ahadi, tunatafuta fedha, alisema mwenyewe. Watu wa Mikoa wa Songwe, Rukwa pamoja na Katavi tumekuwa tukilia kila mwaka ni kwa nini sasa mwaka huu msiweke commitment katika barabara zote mkatenga tu fedha kuelekeza katika Mkoa huu wa Rukwa, hususan hii barabara kutoka Mlowo mpaka Kamsamba na Kilyamatundu kwa kiwango cha lami ili tuache
kuwasumbua tena katika kipindi cha miaka mitano. Mheshimiwa Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nikuhakikishie barabara ya Mbande – Kongwa tunaijenga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia
Mheshimiwa Silinde kwamba daraja la Kamsamba nadhani maswali yake yote ya nyuma yalikuwa yanaelekea hapo. Umeona kwamba sasa hii siyo ahadi tena tunatekeleza, siyo michakato, tunatekeleza. Kabla hujatekeleza taratibu za usanifu, upembuzi lazima zifanyike vinginevyo huwezi ukatekeleza. Kwa hiyo, hatua ya kwanza ya kufanya usanifu wa kina na upembuzi yakinifu tunaianza kwa kutafuta fedha na mara tutakapopata fedha, kazi hii tutaanza. Suala siyo
michakato hapa tutatekeleza kama tulivyoahidi.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa jibu zuri lenye kuleta matumaini kidogo kwamba mwaka huu wa fedha wamependekeza kutenga kiasi cha shilingi bilioni tatu. Kwa kuwa kiwango hiki ni kidogo na kwa kuwa barabara hii imeahidiwa tangu Ilani ya 2005.
Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kutafuta chanzo kingine, mfano mikopo yenye masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia, Benki ya Maendeleo ya Afrika ili kuweza kuikamilisha kwa kuwa eneo hili linataka kuwa la viwanda?
Swali la pili, kwa kuwa wakazi wa maeneo hayo yanayopita barabara hii ya Kisarawe - Mpuyani -
Manerumango, maeneo ya Kazimzumbwi, Masaki, Kibuta pamoja na Marumbo na Manerumango yenyewe, wakazi hawa walizuiwa maeneo yao wasiyaendeleze wala kukarabati nyumba zao lakini mpaka sasa wakazi hawa
hawajui fidia gani watakayolipwa. Kwa kuwa katika jibu la msingi amesema upembuzi yakinifu umekamilika.
Je, ni lini wakazi wa maeneo haya watalipwa fidia
yao wale wanaostahili? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimepokea ushauri wake wa kutafuta vyanzo vingine ili kuhakikisha barabara hii tunaikamilisha, tutakwenda kuufanyia kazi ushauri wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu fidia kwa wananchi wa Kazimzumbwi, Mabuta na maeneo mengine, hadi Maneromango, kwanza ningeomba hii dhana ya fidia ieleweke wazi na Waheshimiwa Wabunge wote na mtusaidie kwa wananchi. Tukiwa na kauli moja wananchi hawatahangaika, kwa sababu kauli yetu kupitia sheria tuliyoipitisha ndiyo ilikuwa kwa umoja wetu, sasa ni vizuri
tunapolishughulikia hili suala la fidia katika maeneo ambayo barabara zinapita au miradi mingine ya miundombinu inapita, tuwe na kauli inayofanana na sheria tulizopitisha ili tusiwachanganye wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuwekewa alama ya ‘X’
iwe ya kijani au iwe nyekundu maana yake ni kwamba nyumba hiyo au jengo hilo au shamba hilo au miti hiyo iko ndani ya hifadhi ya barabara. Waliowekewa kijani maana yake ni kwamba watakuja kufidiwa, lakini haina maana kwamba wanafidiwa wakati huo huo au waendeleze nyumba zao, maana yake ukiendeleza unaongeza gharama tena za kufidia, unaipa gharama zaidi Serikali na lengo la Serikali ni kupeleka miundombinu katika maeneo hayo, prime objective siyo kufidia, prime objective ni kujenga
miundombinu, lakini ni lazima tuwafidie wale ambao wana haki ya kufidiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, niwaombe wananchi wote ambao wamewekewa ‘X’ wajue kwamba wako ndani ya eneo la mradi, watafute maeneo mengine, tena ni vizuri wakatafuta taratibu kwa muda wa kutosha badala ya kuja kuhangaika dakika za mwisho, mara nyingi kwa mfano wale ambao wana ‘X’ nyekundu watakuja kubomolewa bila fidia na wale wa kijani kwa vyovyote kabla barabara haijajengwa au kupanuliwa tutawafidia mara tunapopata fedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninaomba sana Mheshimiwa Subira Mgalu, kupitia kwako natambua mchango mkubwa unaotolewa na pacha wako, Mheshimiwa Selemani Jafo katika suala hili…
Ninawapongeza sana kwa kazi kubwa mnayoifanya kwa pamoja…
Kwa ushirikiano huo tutahakikisha barabara hii inajengwa.
MHE. WILLIAM M. NGELEJA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuongezea maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Moja, kwa kuwa eneo la Nyamikoma kihistoria lilikuwa na gati, gati hilo lilikuwa linatumika kusafirisha marobota ya pamba kuyapeleka Kisumu nchini Kenya, enzi zile wakati kilimo cha pamba kipo juu. Napenda kusikia kauli ya Serikali kama katika mazingira hayo bado kunahitajika utafiti wa kijiografia ambao Mheshimiwa Naibu Waziri ameuzungumza ukilinganisha na maeneo mengine ambako hakuna gati? Pili, eneo la Nyamikoma linafanana na maeneo mengi ya mwambao wa Kanda ya Ziwa au Maziwa Makuu kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa mfano, Magu Ginnery, Nasa Ginnery, Mwabagole Ginnery pale Misungwi, Sengerema Buyagu Ginnery ambako ndiko ninakotoka pamoja na Buchosa – Nyakarilo. Napenda kujua kama katika mpango huo ambao Mheshimiwa Naibu Waziri amesema Oktoba watakamilisha ramani zinazohitajika.
Je, anatoa kauli gani za matumaini kwa wananchi
wa maeneo haya ambako pia wanatarajia magati yajengwe ili kuboresha zao la pamba ambapo kwa sasa hivi Serikali imewekeza nguvu nyingi katika kufufua viwanda na hasa viwanda ambavyo vinategemea rasilimali ya hapa nchini? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nakubaliana nae kwamba Gati la Nyamikoma lilikuwepo toka zamani, lakini taarifa tunazozikusanya sasa hivi tunataka tupate picha kamili kwa sasa ya maeneo ya magati yote na bandari zote ili hatimae tujue tupange vipi vipaumbele vyetu katika uendelezaji wa magati na bandari hizo. Kwa hiyo, pamoja na kwamba ilikuwepo na unafahamu kwamba matumizi yake yamepungua sana itaingia katika mpango huo na bahati nzuri kama nilivyosema katika jibu langu la msingi kwamba kazi hiyo tunatarajia kuikamilisha mwishoni mwa Oktoba, 2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili; maeneo yote aliyoyataja yapo katika mpango kabambe wa kupitiwa kuandaa hizo taarifa za GIS na baadaye kuja kuamua maeneo gani tuanze, maeneo gani tufuatie katika gati zote na bandari zote kwenye Maziwa yote Makuu; Ziwa Victoria, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa, nimhakikishie kwamba wananchi wa maeneo yake na maeneo mengine aliyoyataja tutahakikisha kwamba tunayapitia na tunapata taarifa kamili zitakazotuwezesha kuamua wapi tuanze na wapi tufuatie.
MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini sambamba na hayo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ya Masasi – Nachingwea – Nanganga inahudumia Wilaya tatu, hivyo umuhimu wake katika mkoa na Taifa unafahamika sana kiuchumi. Majibu aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri, naomba niyapokee kwa sababu kwanza wameonesha utashi wa kutenga shilingi bilioni tatu, lakini nilikuwa nataka nijue, kwa urefu wa barabara ile ambao tayari umeshafanyiwa upembuzi yakinifu kilometa 97, kwa kutenga shilingi bilioni tatu ambazo haziwezi kujenga hata kilometa zisizozidi 10, ni nini nia ya Wizara juu ya ujenzi wa barabara hii ambayo imekuwa kero kubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi na Wilaya ya Nachingwea kwa ujumla?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba kujua pia kupitia Naibu Waziri, upembuzi yakinifu ambao ulifanyika toka mwaka 2016 uwe umekamilika, umehusisha nyumba za wakazi ambao wamesimamisha shughuli zao. Nilikuwa nataka nijue, katika kiasi hiki cha fedha shilingi bilioni tatu, kinahusisha pia fidia kwa wale wananchi ambao wanapaswa kulipwa ili waweze kupisha ujenzi wa hii barabara? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ina nia ya dhati ya kutaka kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami na ndiyo maana imeshatekeleza hatua ya kwanza muhimu sana ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa nini tumetenga fedha kidogo; kwanza hatujatenga; tunaomba tutengewe fedha kidogo siyo kwa sababu ya kutokuwa na dhamira ya dhati, bali ni kwa sababu ya fedha ambazo Wizara nzima inatarajia kuomba kutengewa imepungua sana ukilinganisha na mwaka uliopita. Kwa hiyo, tutagawana haka kasungura kadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaanza mwaka huo ujao na miaka inayofuata tutaendelea kukamilisha na hatimaye tutakamilisha hiyo barabara kuijenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili, naomba nimhakikishie kwamba tunapoanza kujenga na tunapotenga fedha kwa ajili ya ujenzi, inahusisha vilevile na fidia ya maeneo yale ambayo tutajenga katika mwaka huo wa fedha.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa Jimbo la Geita Vijijini miaka 56 ya uhuru hawajawahi kuona lami. Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni aliwaahidi lami kwenye barabara ya kutoka Geita – Bugurula – Nzela mpaka Nkome. Sasa namuuliza Mheshimiwa Waziri, je, ni lini Serikali imejipanga kuanza kufanya upembuzi yakinifu na kuanza kutengeneza kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo kawaida ya kutaja terehe kamili ya lini barabara itaanza kujengwa katika Wizara yetu kwa sababu taratibu zake za kufikia hadi ujenzi ni nyingi na zinahusisha taasisi mbalimbali ambazo huwezi ukazipangia muda wa kukamilisha hatua yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ni ahadi ya Serikali ya Awamu ya Tano kwamba suala hili tutalitekeleza kama ambavyo Mheshimiwa Rais aliahidi wakati wa kampeni katika kipindi hiki cha miaka mitano.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Barabara ya Nangurukulu – Liwale, Nachingwea – Liwale, ni barabara ambazo zimo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini mara nyingi nimekuwa nikiuliza barabara hizi, naambiwa itajengwa, itajengwa; sasa wana-Liwale wanataka kusikia ni lini barabara hizi zitaingia kwenye upembuzi yakinifu na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua tunayoifanya sasa ni kutafuta fedha. Nimhakikishie Mheshimiwa Kuchauka, mara tutakapopata fedha, suala la upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii ambayo imeahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tutaitekeleza.
MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Ngorongoro, Mkoani Arusha, wamekuwa wakipata shida sana ya usafiri kutokana na ubovu wa barabara.
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ambayo ilikuwa kwenye bajeti ya 2016/2017 ya kujenga barabara ya lami inayoanzia Loliondo hadi Mto wa Mbu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu kumhakikishia Mheshimiwa Magige na Mheshimiwa Olenasha kwamba mkandarasi tunatarajia kumpata muda siyo mrefu kwa sababu taratibu za kumpata mkandarasi zipo katika hatua za mwisho na mara tutakapompata mkandarasi barabara hii itaanza kujengwa.
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya wananchi wa Mji wa Tunduma, napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu wananchi wa Mji wa Tunduma wamekubali ushauri wa viongozi wao na kuondoa nyumba katika maeneo mbalimbali na kuhakisha kwamba barabara 42 zimepatikana kwenye Mji wa Tunduma, Serikali ina mpango gani wa kuwaunga mkono ili kuhakikisha kwamba barabara zile zinakuwa kwa kiwango cha lami kwenye Mji wa Tunduma, ukizingatia mji unaendelea kukua?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukulie kwamba taarifa hii ni ombi na kule wakati tunapita kwenye kampeni tulitoa ahadi zinazofanana na hayo ambayo ameyasema. Nimhakikishie tu kwamba ombi hili tutalipeleka katika timu ya wataalam ambayo ndiyo huwa inaandaa vipaumbele kulingana na ahadi za viongozi wakuu, ahadi za Wabunge, na kadhalika, waweze kuliangalia ili tuweze kulitekeleza kama ambavyo tuliahidi wakati wa uchaguzi.
MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza niipongeze Wizara kwa majibu mazuri, baada ya hapo nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii ya Manyovu - Kasulu imekuwa ni kero kubwa sana hasa wakati huu wa mvua na sasa hivi nauli ya kutoka Manyovu - Kasulu imefikia mpaka shilingi 10,000; na tunayo barabara nyingi ya lami ya kutoka Kigoma mpaka Manyovu yenye urefu wa kilometa 60 ambayo nauli yake ni shilingi 3,000. Kwa hiyo, umuhimu wa kujenga barabara hii na kuianza mapema inajionyesha kwa vigezo hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kujua, Wizara imekiri kwamba inafanya upembuzi yakifu, wananchi wa Buhigwe wanataka kujua upembuzi yakinifu unaisha lini na ujenzi unaanza lini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mheshimiwa Rais alipokuwa akijinadi tuliita vijiji vya Mlela, Buhigwe, Kavomo, Nyankoloko, Bwelanka na akaahidi kwamba atajenga barabara ya kilometa tano katika Wilaya ya Buhigwe, je, ni lini ahadi hiyo itatimizwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kumpongeza sana Mheshimiwa Ntabaliba kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia miradi mbalimbali ya Miundombinu katika Wilaya yake na Jimbo lake, nikupongeze sana. Mimi ninakuhakikishia kama ambavyo tumekuwa tukiwahikishia katika ofisi zetu mimi na Waziri wangu, kwamba tutashirikiana na wewe kuhakikisha mambo yote ambayo tuliyaahidi katika Wilaya yako yanatekelezwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu la msingi, ujenzi utaanza baada ya kukamilika upembuzi na usanifu wa kina, kwa maana unaofanywa na kufuatiliwa na wenzetu wa AfDB. Nikuombe tu kwa kuwa anayefanya si Serikali, kazi hii inafanya na AfDB chini ya Afrika Mashariki suala la lini ni gumu kukueleza isije ikaonekana tunasema uongo hapa Bungeni. Nikuhakikishie suala hili litakamilika katika kipindi kifupi kijacho na baada ya hapo shughuli za ujenzi zitaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili, nimuhakikishie, kama ambavyo tulimuhakikishia ofisini, kwamba kilometa zake tano ambazo Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano aliahidi zitatekelezwa mara baada ya masuala haya ya miradi ambayo ni kiporo yatakapokamilika; na uzuri wake sehemu kubwa za viporo zinakamilika mwaka huu ujao wa fedha baada ya hapo tutakamilisha ahadi zingine zote ambazo Mheshimiwa Rais aliziahidi hasa za kilometa tano, kilometa sita katika sehemu mbalimbali za Miji ya Tanzania hii.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Wananchi wa Jimbo la Geita Vijijini hususan Jimbo la Geita Vijijini ndilo Jimbo pekee linaloongoza kwa kupata chakula kingi kila mwaka kwenye Kanda ya Ziwa; wamekuwa na kilio cha barabara yao kutoka Senga - Sungusila - Lubanga mpaka Iseni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge watatu walionitangulia wote wamekuwa wakiomba Serikali barabara hii ichukuliwe angalau tu kwa kiwango changalawe sio lami na Serikali imekuwa ikitoa ahadi kila siku tunafanya tunafanya, na mipango yote sisi kwenye RCC tumeshabariki. Sasa nataka kujua Waziri ni lini barabara hii unaichukua na kuiweka kwenye angalau kiwango cha molami tu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru sana Mheshimiwa Musukuma kwanza kwa kutukumbusha kuhusu barabara hii. Aliiongelea muda mrefu, kuanzia miaka ya nyuma na sasa tunamuhakikishi kwamba hii barabara itachukuliwa na TANROADS, kwa maana ya kukasimiwa. Barabara hii haijakidhi vigezo vya kupandishwa hadhi, lakini Waziri ameshakubali na ameshaikasimu barabara hii ili iweze kutekelezwa na TANROADS Mkoa wa Geita.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sera ya masuala ya ujenzi ni kuunganisha barabara ya mkoa mmoja na mwingine kwa kiwango cha lami, na kumekuwa na ahadi ya muda mrefu ya ujenzi kwa kiwango cha lami barabara ya Njiapanda - Karatu - Mang’ola mpaka Lalago, ambayo inaunganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu, je, ni lini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Mheshimiwa Paresso asubiri, ni keshokutwa tu bajeti yetu inakuja, na ramani yote ya shughuli za ujenzi wa barabara zote itakuwa imeanikwa wazi. Nisinge penda kwenda kwa undani kwa sababu ni sehemu ambayo Waziri wangu ataishughulikia keshokutwa.
MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ila nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, kwa kuwa nyendo zimekuwa nyingi, watu wanakwenda sana kutoka sehemu moja kwenda nyingine kwa ajili ya kiuchumi na mengineyo, kwa hiyo ajali za majini, baharini na kwenye maziwa yawezekana zikatokea. Serikali imejipanga hivi ilivyojipanga; Je, Serikali inaonesha vipi shughuli zinazofanywa na SUMATRA na kule Zanzibar, kwa sababu bado ajali zitakuwa zinatokea tunafanyaje?
Swali la pili; Serikali ina mpango gani kwa wale waliopatwa na msiba na kupoteza ndugu zao wakati ilipopata tatizo MV Bukoba, MV Spice Islander iliyozama kule Nungwi na ajali nyingine. Je, watu wote hawa wameshalipwa fidia zao?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mahusiano ya MRCC na upande wa Zanzibar, naomba nimhakikishie kwamba MRCC ni ya masuala ya Muungano na yanasimamiwa na SUMATRA, kwa hiyo Zanzibar Maritime Authority watashirikiana na taasisi yetu katika kusimamia hii MRCC iweze kuhudumia pande zote za Muungano mara ajali inapotekea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili nimuombe tu Mheshimiwa Asha Juma kwamba ajali ya MV Bukoba na ajali nyingine zote zimeshughulikiwa na Serikali kwa kiwango kikubwa sana, maadam sina takwimu hapa nisingeweza kumpa undani wa nini kilifanyika, lakini ni masula ambayo yalishughulikiwa na Idara yetu ya maafa iliyo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa ukamilifu kabisa.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ziwa Victoria kumekuwa na meli nyingi ambazo zimekuwa zikisaidia wananchi kubeba mizigo na abiria kwenda Ukerewe na nchi za jirani. Hivi sasa ni meli moja tu inayotembea MV Umoja imepaki, MV Serengeti imepaki, inayotembea ni MV Clarias peke yake. Wananchi wanaoenda visiwani hasa Ukerewe wanatumia feri za mizigo, sasa za kwetu zimeharibika, sina hakika kama Wizara imeshindwa kukarabati zile feri ama watumishi walioko kule wanafanya mipango na wale watu wenye maferi. Nataka kujua kwa Waziri ni lini feri hizi zitaanza ku-operate kwa muda muafaka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba tunazo meli ambazo zimesimama kwa sababu ya kuharibika ikiwa ni pamoja na MV Umoja na MV Serengeti na hata hii MV Clarias siyo muda mrefu sana imekarabatiwa ni karibuni tu imeanza kutoa hiyo huduma, nayo ilikuwa imeharibika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti iliyopita ya 2016/2017, tulitenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa meli za Ziwa Victoria, nimhakikishie pamoja na kwamba taratibu za kumpata mtu wa kuweza kufanya hiyo kazi zimeshakamilika, muda siyo mrefu kazi hiyo itaanza na kazi hiyo itakapokamilika meli hizo zitarudi majini. Aidha, tuna mpango wa muda mrefu wa kujenga meli mpya itakayohudumia Ziwa Victoria na maziwa mengine Tanganyika na Nyasa, kwa Nyasa tumeshakamilisha ili kuhakikisha kwamba meli hizo ambazo zimefanya kazi muda mrefu sana katika maziwa hayo zinapunguziwa uzito na meli mpya zitakazokuwa zimejengwa. Utaratibu wa kujenga meli hiyo bado tunaendelea nao na muda si mrefu tunatarajia kupata mkandarasi wa kujenga meli hiyo.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Swali langu ni dogo tu, majanga ya moto katika Jiji la Mbeya yamekuwa yanajitokeza mara kwa mara hususan Soko la SIDO Mwanjelwa, Uhindini na sababu kubwa ni uchakavu na ubovu wa miundombinu. Naomba Serikali iniambie ina mkakati gani katika kuondoa tatizo hili kwa kushirikiana na Halmashauri?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, emphasis ya swali lake ipo katika miundombinu na ndiyo maana nilikuwa nadhani nilijibu na kama kutahitajika maelezo ya ziada yataweza kutolewa, emphasis yake ameitoa kwenye miundombinu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie muda si mrefu hapa tutasoma bajeti yetu ataona ni kwa namna gani Wizara yetu imezingatia haya ambayo ameyauliza, vilevile wakati tunapitisha Bajeti ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI unafahamu kuna baadhi ya fedha zimetengwa kwa ajili ya kushughulikia miundombinu katika Jiji la Mbeya.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ambayo Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ameyatoa kuhusiana na vifaa vya Zimamoto siyo tu kwa Mkoa wa Mbeya lakini nchi yetu kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa Mbeya binafsi nilifanya ziara katika Mkoa wa Mbeya na nataka nipongeze sana uongozi wa Jeshi la Zimamoto, Mkoa wa Mbeya kwamba umefanya ubunifu wa hali ya juu kwa kuhakikisha kwamba unapanua huduma za zimamoto katika Wilaya nyingine za Mkoa wa Mbeya.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika kuwaunga mkono tuliweza kuhakikisha kwamba tunafanya mambo makubwa matatu. Moja, tumewapatia gari ambayo itakuwepo katika Wilaya ya Rungwe, pili kulikuwa kuna changamoto ya gari ya zimamoto ya Mkoa wa Mbeya ambayo tumefanya jitihada ya kukamilisha matengenezo yake na sasa inaendelea kutoa huduma katika Mkoa wa Mbeya, pamoja na mambo mengine ambayo zaidi yanalenga katika kuongeza utoaji wa elimu ya uokoaji katika Mkoa mzima wa Mbeya na Wilaya nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba katika bajeti inayofuata na katika bajeti zilizopita tumetoa kipaumbele sana katika kuhakikisha kwamba tunatenga fedha kwa ajili ya ununuzi wa magari ya ziada ya zimamoto. Hizo ni kati ya jitihada ambazo tunachukua ukiachilia mbali mchakato ambao unaendelea sasa hivi wa mazungumzo na kampuni ya Ubelgiji pamoja na Austria kuweza kupata mkopo wa vifaa vya zimamoto na uokoaji kwa Tanzania nzima.
MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa kazi nzuri anayoifanya kupeleka mawasiliano katika Jimbo langu.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, swali hili nimeuliza mwaka 2014 nikajibiwa kwamba 2015 nitapata majibu ya uhakika, sikupata majibu. 2015 nikapata nafasi ya kuuliza nikaambiwa 2016, leo hii ni 2017 naambiwa ni 2018. Naomba niweze kupata majibu ya uhakika leo kwamba ni lini sasa vijiji hivi vilivyoorodheshwa vitapata minara ya simu na wananchi wangu waweze kupata mawasiliano hayo ya simu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; katika minara ya simu ambayo inajengwa katika maeneo mbalimbali katika Jimbo langu la Kalenga service levy hailipwi moja kwa moja kwenye Halmashauri, inaenda kulipwa kwenye makampuni yenyewe ambayo mengi yapo Dar es Salaam. Wananchi katika Jimbo langu wanakosa mapato ya ndani kutokana na minara hiyo ya simu. Ningependa kujua kutoka Wizarani, je, ni namna gani sasa wanaweza kuwapelekea fedha hizi wananchi ambao nao wanatakiwa kwa namna moja au nyingine waweze kupata faida kutokana na minara hii ya simu, kwa sababu inayotumika pale ni ardhi?
Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba fedha ambazo yanapata makampuni haya au faida ambazo zinapata kampuni hizi zinakwenda pia kuwasaidia wananchi katika maeneo husika? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tunapojibu maswali hapa huwa tuna dhamira ya dhati ya kutekeleza kile tunachokijibu na kwa kawaida Wizara huwa tunajiandaa kujipanga kutekeleza kile ambacho tunakijibu hapa. Inapofika wakati wa bajeti inaweza ikatokea kama ilivyotokea kwa eneo hili kwamba Mfuko wetu wa Mawasiliano kwa Wote huwa unakosa fedha, unapokosa fedha tunatarajia tuifanye hiyo kazi mwaka unaofuata, hiyo inabakia dhamira yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba dhamira yetu ni kuhakikisha vijiji hivi kama tulivyosema katika jibu la msingi, tunavitekeleza katika mwaka huu wa 2017/ 2018 na fedha tunatarajia kuziomba na tunaamini mtazipitisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ile minara ya simu pale inapojengwa kwa kawaida yale makampuni yanaingia mikataba na ama vijiji au mwenye ardhi husika, kwa kawaida Wizara hatuingilii sana katika mikataba hii ya kulipa gharama za ardhi inayotumika na wawekezaji katika minara ya simu. Hata hivyo, nalichukua wazo lake au pendekezo lake ili tuangalie namna gani Wizara inaweza kusaidia katika kuhakikisha minara hii ambayo imewekwa katika Jimbo hili la Kalenga inatumika na inawanufaisha wananchi kupitia mikataba yao ambayo wameweka.
MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Kwa kuwa, katika Mkoa wa Njombe kuna matatizo makubwa sana ya mawasiliano hasa maeneo ya mwambao katika Wilaya ya Ludewa kama Rupingu, Ibumi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea minara watu wa maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyoshirikiana na Mbunge wa Jimbo la Ludewa katika kuhakikisha kwamba eneo la Mwambao linashughulikiwa kikamilifu. Kwa sababu swali hilo limeulizwa muda siyo mrefu na tumelijibu hapa likiulizwa na Mheshimiwa Deo Ngalawa na leo linaulizwa na Mheshimiwa Lucia Mlowe nawashukuruni sana kwa ushirikiano wenu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimekuwa nikilijibu kupitia Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo kwamba eneo hilo tutahakikisha tunajenga minara katika kipindi hiki na itakapofika mwaka 2020 tatizo hilo tutakuwa tumelitatua. Siyo hilo tu na lile lingine la kutoboa barabara katika ukanda ule wa Ziwa, tutakuwa tumeshashughulikia hayo matatizo.
MHE. SIXTUS R. MAPUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nami nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo linalolikabili Jimbo la Kalenga linafanana vilevile na Kijiji cha Ruvuma chini, Kijiji cha Kihungu, Kijiji cha Mpepai, hao nao wanapata shida kubwa ya mawasiliano. Je, ni lini Serikali itahakikisha vijiji hivi navyo vinawekwa katika mpango na mwaka huu usipite wapate mawasiliano kama wanavyopata Watanzania wengine?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji hivyo alivyovitaja vya Ruvuma chini, Mpepai na eneo lote lile la ukanda wa Ziwa Nyasa pamoja na Mto Ruvuma, maeneo hayo yameingizwa katika mpango wa UCSAF, tunachohitaji ni kupata fedha ili tuweze kuyatekeleza hayo maeneo na nimhakikishie tutaendelea kufuatilia kama ambavyo Waziri wangu alimuahidi ofisini wakati alipokuwa akifuatilia hili suala.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba tutalifuatilia hadi tunakamilisha mawasiliano katika maeneo hayo ili watu wetu wasiwe wanapata matatizo na mawasiliano ya nchi jirani na wakashindwa kuwasiliana kwa upande wa Tanzania.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda kwamba Serikali za Vijiji chini ya TAMISEMI zinasimamiwa vizuri na sasa wenzetu TAMISEMI wanataka kuweka mpango wa kuhakikisha kwamba mikataba yote inayoingiwa kati ya vijiji na wawekezaji tunakuwa na wataalam wa sheria kutoka Halmashauri wanaohakikisha kwamba maslahi ya wanavijiji yanalindwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge masuala haya na sisi tunayafuatilia kwa sababu yanatuletea picha siyo nzuri sana kwa wawekezaji wetu tunaowapeleka maeneo mbalimbali ya vijiji wanakojenga minara. Tutayafuatilia na baadaye tutakuja kukuletea mrejesho kupitia wenzetu wa TAMISEMI.
MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa swali hili la mawasiliano linafanana sana na matatizo katika Jimbo la Kilindi katika Kata za Saunyi, Kwekivu na Tunguli. Napenda kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri ni lini kampuni za mawasiliano zitaweza kuweka minara katika Jimbo langu la Wilaya ya Kilindi? Ahsante.
MHE. DOTO M. BITEKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi hii. Kwa kuwa, Serikali imesema kwamba imeshaweka utaratibu wa namna gani itatekeleza ahadi za viongozi, ikiwemo ahadi ya Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni ya ujenzi wa kilometa tano za lami kwenye Mji wa Ushirombo; wananchi wa Bukombe wanataka kujua tu sasa kwamba ni lini? Kwa sababu amesema ndani ya miaka mitano, basi waambiwe ni lini itaanza kutekelezwa katika kipindi cha miaka hii mitano, maana huu ni mwaka wa pili tayari tumeingia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hicho ndicho wananchi wanataka kusikia. Nakushukuru.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba kumpongeza sana Mheshimiwa Biteko kwa kazi kubwa anayoifanya kufuatilia masuala ya miundombinu katika maeneo yake. Namwomba tu, yale ambayo tuliongea ofisini na yale ambayo tuliongea mbele ya Mheshimiwa Waziri wangu ni kweli tutayatekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utaratibu tuliopewa, kitu cha kwanza ni kuhakikisha tunatekeleza ahadi zote, lakini wakati huo huo zina Wakandarasi site ili kuondoa matatizo ya kulipa interest pamoja na idle time. Hicho ndicho kipaumbele cha kwanza ili tuweze kupata hela nyingi zaidi za kuwekeza kwenye miundombinu badala ya kuwalipa watu ambao wanakaa tu hawafanyi kazi. Kwa hiyo, hicho ni kipaumbele cha kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kipaumbele cha pili ni kuhakikisha ahadi zote za Mheshimiwa Rais na zilizoandikwa katika Ilani ya Uchaguzi tunazipangia ratiba. Sasa tunakwenda miaka kwa miaka; mwaka wa kwanza tumemaliza, mwaka huu mmeona kwamba mambo mengi tumeyaingiza ambayo ni mapya siyo yale ambayo tulikuwa tunategemea wakati ule kwa sababu tumeshapunguza kwa kiwango kikubwa yale madeni ambayo tulikuwa nayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Ushirombo kwamba ahadi zote katika miaka hii mitatu iliyobakia tutatekeleza ahadi hii tuliyoitoa wakati wa uchaguzi.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutoka Masasi mpaka Nachingwea ni kama kilometa 42 na kutoka Masasi mpaka Ndanda ni kama kilometa 40; na kwenye bajeti iliyokuwa imeitengwa ambayo imeombwa mwaka 2017/2018 kama shilingi bilioni tatu, ni fedha ndogo ambayo haiwezi kukidhi kumaliza barabara hiyo. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kukamilisha barabara hiyo kwa kiwango cha lami kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge alikuwa ameomba, kwa sababu fedha iliyotengwa ni ndogo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali dogo la pili la nyongeza ni kwamba, matatizo ya Jimbo la Ndanda yanafanana kabisa na Jimbo la Momba kule; sasa naomba niulize kwamba barabara ya kutoka Kakozi kwenda Kapele mpaka Namchinka kilometa 50.1 imepandishwa hadhi na Wizara yako, lakini mpaka sasa haijawahi kuhudumiwa na hiyo barabara ni mbovu. Ni kwa nini barabara hizi mnazipandisha hadhi na hamzihudumii kwa wakati? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu udogo wa fedha, kitu ninachojaribu kumweleza ni kwamba katika ule mpangilio wa kutekeleza ahadi sasa tumefikia kuanza utekelezaji wa ahadi ya barabara hii na tumeanzia na hizi fedha ndogo kutokana na bajeti tuliyopata mwaka unaokuja wa 2017/2018. Nimhakikishie, katika miaka yote inayofuata, barabara hii itakuwa inaendelea kupewa fedha za kutosha ili hatimaye katika kipindi chetu tulichoahidi, barabara hii itakuwa imekamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya Kakozi – Kapele na kuendelea ambayo imechukuliwa na TANROAD, nimhakikishie tu kwamba tutahakikisha TANROAD inapanga fedha za kutosha kwa ajili ya utekelezaji wa barabara hii kama ilivyokusudiwa kwa kupandishwa hadhi.
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba barabara ya Sikonge – Mibono – Kipili ilipandishwa hadhi tangu mwaka 2009 na hadi leo imetobolewa kwa kiwango cha kilometa 42 tu kati ya 282 ambayo ni kama kilometa tano kwa mwaka; ina maana kwamba hadi itakapokamilika barabara hiyo tunahitaji miaka 44. Je, Serikali iko tayari kuwaambia wananchi wa Sikonge kwamba itajenga barabara hiyo kwa kipindi cha miaka 44 ijayo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu wa fedha za Mfuko wa Barabara zinazogawiwa mikoani kwa ajili ya matengenezo, haturuhusiwi kutumia fedha nyingi sana kwa ajili ya kutoboa barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ombi lake tunalichukua na tutatafuta namna ya kuhakikisha barabara hii kipande hiki kipya cha kukitoboa tunakitoboa kwa haraka zaidi na naomba wananchi wote wa Sikonge wachukue hiyo ndiyo kama commitment ya Serikali.
MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Barabara ya kutoka Mlowo - Mbozi kwenda Kamsamba - Momba haipitiki wakati wa mvua, je, ni lini Serikali itatengeneza barabara hii kwa kiwango cha lami ili kuweza kusaidia uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Songwe na Mkoa wa Katavi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, yale ambayo tumeshayasema kabla ni ya kweli na tutayatekeleza. Tulichokiahidi, kitu cha kwanza ni kukamilisha daraja, tukishamaliza kukamilisha daraja tutashughulikia hii barabara katika kiwango cha lami. Tupeni fursa, hizo pesa ambazo tumezitenga kwa ajili ya daraja kwanza tukamilishe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina uhakika, maadam tunatenga fedha za utengenezaji wa hii barabara kuhakikisha inapitika karibu muda wote, naomba tupeni fursa tutekeleze kwa namna tulivyopanga.
MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kweli nasikitika sana kuona majibu ambayo ametoa Mheshimiwa Waziri. Hii ni mara yangu ya pili namwuliza hili swali. Mara ya kwanza alinijibu hapahapa Bungeni, akasema kabla ya mwezi wa Sita barabara hii itakuwa imeanza ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Waziri, anapotujibu siyo kuwajibu Wabunge kuwafurahisha, haya ni majibu ambayo tunakuja kuuliza kwa ajili ya wananchi wetu. Naomba Mheshimiwa Waziri atupe majibu ambayo ni ya uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza; ni lini barabara hii ujenzi utaanza? Kwa sababu hii barabara ni ya muda mrefu tangu kipindi cha Mheshimiwa Rais Mkapa amestaafu; amekuja Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, sasa anakuja Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwenye bajeti ya mwaka 2017/2018, je, imetengwa pesa kwa ajili ya ujenzi huu kuanza na wananchi wapewe fidia?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie, tunapojibu hapa kwanza tunaonesha dhamira lakini pili, tunaonesha mipango ambayo ipo mbioni. Hatuwezi kuanza ujenzi wa barabara hii kabla ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika. Hakuna aina hiyo ya ujenzi ya barabara kuu na muhimu kama hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge atupe fursa tukamilishe upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa mwaka huu tunakamilisha kazi hizo mbili. Kwa hiyo, hatujatenga fedha za kuweza kujenga, tumetenga fedha kwa ajili ya kukamilisha kazi hizo mbili. Nimhakikishie kwamba mara baada ya kazi hizo mbili kukamilika, ujenzi utaanza, Serikali hii ya Awamu ya Tano inachosema inakusudia kukitekeleza na huwa inakitekeleza.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Dar es Salaam – Isaka – Rusumo, inayojulikana kama central corridor ni barabara inayohudumia nchi takriban nne ambazo zipo kwenye Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, lakini kipo kipande cha kilometa 150 kutoka Lusahunga kutoka Rusumo; Nyakasanza kwenda Kobelo mpaka Bujumbura. Kipande hiki kimekuwa ni kero kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana ambao ndiyo
huu tunamalizia 2016/2017 barabara hii ilitengewa shilingi bilioni tano, lakini mpaka sasa hivi ukarabati unaofanyika ni mdogo na kwa bajeti hii ya 2017/2018 tumetengewa shilingi bilioni 1.19 tu kiasi kwamba haiwezi kufanya ukarabati unaoridhisha. Je, ni lini Serikali sasa itaweza kutenga fedha za kutosha ili kukarabati kipande hiki ambacho ni kero kwa Watanzania wanaotumia barabara hii na wageni wanaotoka kwenye nchi za Burudi na Rwanda, Kongo na Uganda ili barabara hii iweze kukidhi viwango na kukidhi mahitaji?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Gashaza kwa sababu anapita hii barabara, anafahamu kazi kubwa inayofanywa kuirekebisha hiyo barabara kuanzia Isaka na kuendelea. Tunakwenda kwa hatua; mimi mwenyewe nimeona ukarabati ulioanzia Rusahunga kuelekea Rusumo. Nimeiona, nimepita hiyo barabara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namwomba Mheshimiwa Mbunge, aridhike na hiki kinachofanyika na kwa vyovyote vile, baada ya kukamilisha hii, tutakwenda kukamilisha kipande kilichobakia. Suala siyo rahisi kupata fedha zote za kutosha kuikamilisha barabara yote kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kuikarabati barabara hii mpaka ikamilike. Tutafika Rusumo, tutafika hii njia inayokwenda Burundi.
MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa ahadi za barabara ya Karagwe kwenda mpaka Benako kutoka Nyakaanga zimekuwa kero kwa muda mrefu; nimeingia Bungeni mwaka 2005 barabara ya kwenda mpaka Mlongwe nimeiongea barabara ya kutoka Nyakaanga kwenda Benako nimeiongea:-
Ni lini Serikali itachagua moja; kutengeneza upande
na mmoja kuumaliza na kuingia wa pili? Mnatafuta ma-engineer na Wakandarasi ambao hawana viwango. Barabara unatengeneza siku mbili, tatu, barabara inaharibika. Lini mtatafuta ma-engineer wa uhakika wa kutengeneza barabara zikawa za viwango?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Mbunge kwa makini anachokiongelea. Huwa naamini kwamba tunachagua Wakandarasi makini, ila kwa kauli yake inaonekana tunatakiwa tuongeze nguvu zaidi na macho yaangalie zaidi ili kuhakikisha kweli tunapata Wakandarasi wanaoweza kusaidia kufanya kazi bila kurudia rudia mara nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa ushauri wake.
MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Barabara hii ambayo sasa hivi iko chini ya plan ya kujengwa kwa kiwango cha lami imekuwa na matatizo sehemu zile za Kizengi ambako madaraja yake ni mabovu na ikitokea dharura yoyote gari moja likazimikia barabarani magari mengine hayapiti. Je, katika kipindi hiki cha kungojea Serikali ina mpango gani wa kupanua Daraja lile la Kizengi?
Mheshimiwa Spika, pili, barabara hii inaunganisha Mikoa ya Dodoma, Singida na Tabora lakini hatuoni uharaka wa kujenga barabara hii. Je, Serikali sasa inaweza kutuambia ni lini hasa ujenzi huu utaanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Almas Maige kwamba tulichokisema, ile sentensi ya mwisho, kwamba TANROADS itaendelea kuifanyia matengenezo barabara hii ili iweze kupitika majira yote hii ni pamoja na madaraja. Kwa hiyo, asiwe na wasiwasi, matengenezo haya yanahusisha na madaraja.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili, nimhakikishie kwamba taratibu tumezianza na tutaanza kujenga hii barabara mara baada ya kukamilika evaluation na tukampata mkandarasi.
MHE. BONNAH M. KALUWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nimkumbushe Mheshimiwa Waziri kwamba nimekuwa nikiuliza hili swali na leo hili ni swali la tatu; lakini pia Naibu Waziri alikuja kuongea na wananchi wa Kata ya Kipawa, Mtaa wa Kipunguni kuhusiana na mambo ya fidia na akawaahidi atarudi. Mpaka sasa hivi ni mwaka mmoja Mheshimiwa Waziri hajawahi kurudi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri; kwa kuwa wananchi hawa walifanyiwa tathmini mwaka 1995, leo ni miaka 22: Je, atawalipa kwa kutumia tathmini gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, namwuliza Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa hawa wananchi…
Mheshimiwa Mwenyekiti, basi nabadilisha la kuja…
Mheshimiwa Spika, nataka nimuulize Mheshimiwa Waziri kwamba, hawa wananchi wamesimamisha maendeleo kwa muda mrefu; aseme hapa leo katika Bunge hili kwamba: Je, waendelee na maendeleo yao mpaka watakapopata hizo pesa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli niliahidi nitarudi, lakini nilimwambia nitarudi nikiwa na majibu sahihi. Sikusema mwaka mmoja, niliwaambia ni katika kipindi cha miaka mitatu tatizo hilo tutalitatua. Naona umeshaona tofauti, toka pale nilipofika, mwaka huu tumeshatenga shilingi bilioni tano na mwaka ujao tumeshatenga shilingi bilioni 30. Unaona kabisa kwamba nitakaporudi kule, nitarudi kwa kishindo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili kwamba tunalipa kwa tathmini gani? Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunalipa kwa tathmini ile iliyofanyika pamoja na interest ya miaka yote hiyo. Ndivyo sheria za fidia zinavyotuongoza, kwamba kuanzia mwaka uliofanya tathmini ukizidisha miezi sita hujalipa, kuna interest inaingia na kadri utavyoendelea kuchelewa ndivyo interest inavyoingia. Ndiyo maana kama umeona gharama inayodaiwa iliyopo katika kitabu kile cha tathmini ni shilingi bilioni 19, lakini fedha tutakazolipa ni zaidi ya shilingi bilioni 35, ina maana ni kwa sababu ya kuongeza interest ambayo ni kwa mujibu wa sheria. (Makofi)
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, umuhimu wa ujenzi wa reli hii ya Tanga ambao utahusisha mpaka Mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Mara una umuhimu ambao utaongeza mizigo sana kwenye reli hii. Tunahitaji iwe reli ya kisasa kutokana na viwanda ambavyo vinategemewa kujengwa kwenye ukanda huo ukitilia maanani kwamba Mkoa wa Tanga sasa hivi tuna viwanda vingi vya simenti na kuna kiwanda kikubwa sana ambacho kitaanza kujengwa karibuni kwa ajili ya simenti na ukitilia maanani kwamba kuna bomba la mafuta ambalo linatoka Hoima kule Uganda mpaka Bandari ya Tanga. Bandari ya Tanga imeshaanza kuboreshwa. Sasa nataka kumwuliza Mheshimiwa Waziri maswali mawili kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la Mheshimiwa Waziri linaonekana ni lepesi na halina uzito, nataka kujua kuna mikakati gani ambayo imeshafanyika na Serikali kuweza kutafuta hizo fedha za kuanza ujenzi wa reli hiyo? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, sasa hivi kuna changamoto kubwa katika Bandari ya Tanga ukitilia maanani kwamba Bandari ya Mombasa wameshajenga reli ya standard gauge ambayo inatoka Mombasa inakwenda Nairobi mpaka Kisumu na Tororo mpaka Kampala. Sasa sisi bado hatujaanza hiyo kazi; Mheshimiwa Waziri anaonaje suala la kuhusisha sekta binafsi katika utaratibu wa PPP ili tuweze kupata mwekezaji wa kujenga reli hii kwa haraka?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Balozi, Mheshimiwa Mbunge kwamba reli hii ya Tanga –Arusha – Musoma ni muhimu sana na ni lazima tuifanye kazi hii kwa haraka. Anafahamu na nampongeza tu kwa kazi kubwa ya kufuatilia shughuli hii pamoja na Wabunge wengine wa Mkoa wa Tanga, kwamba reli hii imeshaanza kufanyiwa kazi na hatua ya kwanza kuifanyia kazi ni kufanya hiyo feasibility study na detailed design. Nashukuru kazi hii imekamilika na tunatarajia tumlipe Mkandarasi tupate taarifa ili tukishapata hiyo taarifa yake tuweze kuanza sasa hatua za kutafuta fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na ushauri wake kwamba katika hatua hizi za kutafuta fedha ni pamoja na kutumia mfumo wa PPP. Tunakubali ushauri wenu, mmetushauri hilo na sisi tumekubali kwamba tutahakikisha tukishapata ile taarifa tutaanza hatua madhubuti za kufuata Sheria ya PPP ili ujenzi huo uanze haraka kwa sababu tukisema tujenge kwa hela zetu, reli zote hizi ambazo tunaenda nazo kwa sasa hatutaweza kwa muda mfupi. Kwa hiyo, nadhani ni wazo sahihi na tunashukuru sana kwa ushauri wenu, tutatumia njia hiyo ya PPP.
MHE. LATHIFAH H. CHANDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kutokana na kwamba Serikali inanunua ndege na kuikodisha ATCL, hata hivyo umiliki huu wa ndege uko kwa Wakala wa Ndege za Serikali. Kwa maana hiyo basi, ATCL inakodisha hizi ndege. Sasa je, ATCL inatoa malipo yoyote kwa Serikali kwa ajili ya kukodisha ndege hizi? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni kwamba mpaka sasa hivi Serikali inaisimamia management pamoja na Bodi ya ATCL, kwa maana hiyo ATCL haina mamlaka huru ya kutekeleza shughuli zake za utawala. Sasa swali langu ni kwamba, Serikali ina mpango gani wa kuiachia management na Bodi ya ATCL ili iweze kufanya mamlaka yake kwa uhuru na kuweza kufanya shughuli za kibiashara kwa ajili ya kuipatia Serikali mapato ambayo itakuwa ni faida endelevu? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna malipo yanayolipwa na ATCL kwa mmiliki wa ndege, lakini nadhani Mheshimiwa Lathifah anafahamu, mmiliki wa ndege, TDFA, inamilikiwa kwa asilimia 100 na Serikali na kwa upande mwingine mwendesha ndege au mkodishaji wa ndege hizo ni ATCL ambaye naye anamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100. Hiyo haifanyi ATCL apunguze nguvu katika kuhakikisha kwamba anafuata shughuli za biashara na hatimaye analipa gharama za kukodisha ndege hizo. Kwa hiyo, zinalipwa na takwimu tu bahati mbaya sina, ukizitaka nitakuletea uone hadi sasa ATCL wameshalipa kiasi gani kwa TDFA ambao ndege zao wamezikodisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uhuru wa bodi na management, nimhakikishie Mheshimiwa Lathifah, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ni moja kati ya Wizara zinazohakikisha taasisi zake zinazofanya shughuli za kibiashara zinafanya shughuli kibiashara na haziingiliwi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Taasisi hizo zikiwa ni pamoja ATCL, haiingiliwi, bodi ina mamlaka kamili ingawa tu wanalalamika kuna vikao vingi sana vya taasisi za Kiserikali na taasisi za Bunge, lakini hizi zote ni kwa mujibu wa sheria. Sheria za Bunge zinawataka wao wawajibike Bungeni kila wanapotakiwa kuwajibika na Sheria za Msajili wa Hazina zinawataka wao wawajibike kwa Msajili wa Hazina kila wanapoona kwamba wanahitaji kuwajibika, lakini huko siyo kuingilia uhuru wao. Taasisi hizi zinatekeleza wajibu wao kwao, wao wanaendelea kuwa huru katika kufanya maamuzi yao.
MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali tu madogo ya nyongeza. Kwa kuwa tumekuwa tukikaa katika vikao vya Bodi za Barabara mara nyingi sana hasa katika Mkoa wetu wa Iringa, barabara nyingi sana za Halmashauri zetu tunakuwa tukipeleka lakini hazipandishwi daraja. Je, ni vigezo gani sasa vinatumika maana utakuta sehemu nyingine barabara zinapandishwa lakini sehemu nyingine barabara nyingi hazipandishwi madaraja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza pesa kwenye Halmashauri kwa sababu Halmashauri nyingi barabara zake ni mbovu sana ili Halmashauri hizi ziweze kutengeneza barabara zake kwa kiwango?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, vigezo vya kupandisha hadhi barabara vimeainishwa katika Sheria ya Barabara pamoja na Kanuni zake kama ambavyo nilisema katika jibu langu la swali la msingi. Vigezo hivyo havijabadilika na kama tutataka kubadilisha tutakuja Bungeni kuvibadilisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuongeza fedha; fedha nazo tumekubaliana kwamba Mfuko wa Barabara unagawa asilimia thelathini zinaenda kwenye Halmashauri na asilimia 70 zinaenda kuhudumia barabara za trunk road za mikoa. Sasa kama tunadhani kwamba formular hii kwa sasa labda haitufai bado ni suala la kuamua sisi Waheshimiwa Wabunge ndani ya Bunge hili Tukufu ili tuweze kubadilisha zile sheria ambazo tulikubaliana wenyewe.
MHE. ELIAS J. KWANDIKWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona ili nami niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa hitaji la Mufindi Kaskazini linafanana na Ushetu na kwa kuwa Mheshimiwa Rais wetu Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliahidi kupandisha hadhi barabara hii inayounganisha mikoa mitatu; Mkoa wa Geita, Shinyanga na Tabora kwa kupitia maeneo ya Mbogwe, Mwabomba, Nyankende, Ubagwe, Uloa hadi Kaliua. Je, Serikali itaipandisha hadhi lini barabara hii? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hizo ni barabara tatu tofauti lakini zinazoungana na kwa hiyo nadhani tufuate tu utaratibu. Kwa hapa itabidi mikoa yote mitatu kwa vipande vyake ifuate taratibu za kuomba kupandisha hadhi hizo barabara. Kama tayari zimefuata taratibu hizo basi nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba maombi yake yatashughulikiwa kama ambavyo tumeongelea kwa barabara ambayo inaanzia Mtili – Ifwagi – Mdaburo na kuendelea. Utaratibu huo tutaufuata na maombi hayo tutayapitia kwa pamoja na zile zitakazotangazwa tutakuja kuwajulisha rasmi baada ya kutokea kwenye Gazeti la Serikali.
MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa swali la msingi linaulizia ahadi ya Serikali na Mheshimiwa Dkt. Magufuli alivyokuwa Waziri wa Ujenzi aliahidi kukamilisha barabara ya Kawawa – Nduoni –Bakula – Marangu Mtoni ambayo ni barabara muhimu sana kwa ajili ya utalii, inajulikana kama utalii road. Alipokuwa anafanya kampeni wakati wa uchaguzi aliahidi pia kwamba itakamilika na imeshajengwa nusu tu kwa lami. Sasa ni lini Serikali itakamilisha barabara hii kwa maendeleo ya utalii na Serikali iweze kupata mapato. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Waziri kivuli wa Wizara hii nadhani anafahamu na tumejadili, ingawa katika kipindi kifupi kidogo hakuwepo lakini nadhani anafahamu kwamba tumekuwa tukijadili utekelezaji wa ujenzi wa barabara mbalimbali na tumesema kwamba kwanza tuzikazanie zile ambazo zina madeni ili tuondokane na madeni na baada ya hapo tutaendelea na hizi zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hizi zingine kipaumbele cha uhamasishaji wa utalii nacho tulikiweka. Kwa hiyo, nimshukuru alitusaidia kuweka hiki kipaumbele na hivyo mara tutakapomaliza barabara hizi ambazo zina mikataba ya muda mrefu zitafuata hizi barabara zinazohamasisha utalii na vile vile zinazohamasisha viwanda.
MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nami niulize swali dogo tu la nyongeza. Kwa kuwa tatizo ambalo lipo kule Mufindi linafanana kabisa na kule Kilolo; barabara nyingi za Kilolo zimekuwa zikiahidiwa na hasa na Mheshimiwa Waziri. Sasa je, ni hatua gani ambazo inapaswa tuchukue endapo Mheshimiwa Waziri ameahidi kwa upande wa Serikali lakini utekelezaji haujafanyika?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ni dhamira, kwa hiyo tunapotoa ahadi tunaonesha dhamira ya kutaka kutekeleza hicho kitu. Hatua inayofuata baada ya kuwa na hiyo dhamira ni kutafuta fedha na mara fedha zitakapopatikana hii ahadi yetu tutaitekeleza.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Barabara hii nimekuwa nikiulizia mara kwa mara na hii ni kutokana na umuhimu wake. Katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015 ukurasa wa 62 inaeleza kuwa itafanyiwa upembuzi yakinifu na hivi sasa ni miaka miwili sioni dalili ya kutenga pesa kwa ajili ya kufanya usanifu katika barabara hiyo. Je, ni lini sasa Serikali itatenga pesa kwa kuanza kazi hiyo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Mawaziri wote wawili ni wapya, yawezekana hawajatambua vyema umuhimu wa barabara hii. Naomba Mheshimiwa Waziri afanye ziara ya kutembelea barabara hii toka Mlowo hadi Kibaoni ili ajionee fursa zilizopo katika barabara hiyo.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu sana umuhimu wa barabara hii na pengine hukupata fursa ya kufahamu Waziri wangu alishapita katika sehemu ya kipande cha hiyo barabara; nami nilikusudia kupita lakini kwa bahati mbaya kulikuwa na dharura. Nimhakikishie sasa hivi baada ya Bunge nitapita katika barabara hiyo na nitaanzia Tunduma. Kwanza kuanzia Makao Makuu ya Mkoa wa Songwe kuanzia Vwawa, Tunduma na nitafuata hii barabara mpaka inakoishia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namuahidi nitafuata hiyo na tumempa commitment na fedha zimetengwa, tunaanza na ujenzi wa Daraja la Momba na mara tutakapomaliza Daraja la Momba tutatenga fedha ya kuanza upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kama ambavyo nilijibu katika swali la msingi. (Makofi)
MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Kama ilivyo kwa Jimbo la Kwela, kuna barabara mbili ambazo ziliahidiwa na Mheshimiwa Rais; Barabara ya Mbalizi kwenda Makongorosi ambayo inaunganisha Mbeya na Mkoa mpya wa Songwe. Pia kuna barabara ya Isyonje – Kikondo – Makete mpaka Njombe ambayo vile vile inaunganisha Mikoa ya Mbeya na Njombe ziliahidiwa na Rais kwamba zitajengwa kwa kiwango cha lami. Je, ni lini hizi barabara zitajengwa kwa kiwango cha lami pamoja na kulipa fidia wale wote ambao ni waathirika.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba serikali imeshaanza kuchukua hatua za dhati kabisa za kujenga barabara ya kutoka Isyonje – Makete na hiyo barabara yote tumeshaanza hatua na kwamba wakandarasi wameshatafutwa na nadhani anafahamu Mheshimiwa Mbunge na hasa nikijua amemuulizia vile vile Mwenyekiti wangu wa Kamati ya Miundombinu ambaye naye yupo katika barabara hiyo. Nimhakikishie Serikali itatekeleza kile ambacho imekusudia na imeanza kukitekeleza.
MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.Kwa kuwa matatizo yanayowakabili watu wa Kwera yanafanana kabisa na matatizo yanayotukabili watu wa Morogoro Kusini Mashariki na Morogoro Vijijini kwa ujumla, kuna Barabara ya Bingwa – Mkuyuni – Kisaki mpaka kuelekea Rufiji kule Mloka kuelekea Mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara na pia kuelekea katika Mbuga ya Selous.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii iliahidiwa kuwekwa kiwango cha lami tangu Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne na Waziri wa Ujenzi aliyekuwa katika Serikali ya Awamu ya Nne ambaye sasa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli; na kwa kuwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umeshamalizika, je, Mheshimiwa Waziri, ni lini barabara hii itaanza kutengenezwa kwa kiwango cha lami ili kuinua hali ya kiuchumi ya wananchi hawa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba hii barabara baada ya kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, anafahamu kwamba tumeanza kujenga. Hata hivyo, nakubaliana naye kwamba kipande ambacho tumeanza kujenga mpaka sasa ni kifupi. Nimhakikishie, tutaendelea kuongeza kasi ili hatimaye barabara hii ifike Kisaki kama ilivyokusudiwa.
MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Matatizo yaliyopo Kwera yako sawasawa kabisa na matatizo ambayo yapo kwenye Manispaa ya Tabora kwenye barabara ile ya Mambali ambayo inapita Misha, Kata ya Kabila, Kata ya Ikomwa mpaka kutokea Bukene. Barabara hii kwa kiwango kikubwa eneo kubwa lipo eneo la halmashauri na haijapandishwa daraja pamoja na maombi ya muda mrefu. Hata hivyo, kwa kuwa Halmashauri ya Tabora uwezo wa kuitengeneza barabara hii kwa lami unaonekana haupo kabisa, Serikali ina mpango gani kuhakikisha barabara hii inawekwa kiwango cha lami ili iweze kuwa endelevu katika uchumi wa Mkoa wa Tabora? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwakasaka ni mjumbe wa Kamati yangu ya Miundombinu. Tumeliongea sana hili katika Kamati na naomba tu nirudie kumhakikishia, kama ambavyo tulikuwa tumeongea katika Kamati, kwamba Serikali muda si mrefu itakamilisha kupitia maombi yote ya barabara ambazo zimeombwa kupandishwa hadhi na matokeo ya maombi hayo yatatangazwa kwenye Gazeti la Serikali hivi karibuni.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nimekuwa nikisimama hapa mara nyingi naongelea Barabara ya Nangurukuru – Liwale na Barabara ya Nachingwea – Liwale. Majibu ninayoyapata ni kwamba barabara hizi zitajengwa katika kipindi hiki cha miaka mitano, lakini barabara hizo sasa hivi hazipitikia kutokana na mvua za masika zilizokatika sasa hivi. Je, nini commitment ya Serikali kwa kuwaokoa hawa Wanaliwale ili waweze kupata barabara inayopitika masika na kiangazi? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kuchauka ni Mjumbe wa Kamati yangu ya Miundombinu na kwa kweli michango yake tunaithamini sana katika Makati hiyo; na amekuwa akiongelea mara nyingi barabara hizi zote pamoja na ile ya kwenda Nangurukuru. Nimhakikishie Mheshimiwa Kuchauka, yale ambayo tumekuwa tukiyajadili katika Kamati ya Miundombinu, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuyatekeleza. Hata hivyo, nimwombe, wala sio dhambi, pitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ataona nini Serikali iliahidi kwa ajili ya barabara hizi na nimhakikishie tutatekeleza kile ambacho tumeahidi.
MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Napenda kujua, kuna barabara ya Nyamswa –Bunda ambayo mwezi wa 12 mwaka jana alifika Mheshimiwa Profesa Mbarawa, Waziri na kuitembelea barabara hii na kuahidi kwamba ikifika Februari mwaka huu mkandarasi atakuwa site. Kwa bajeti inayoendelea sasa hivi, hiyo barabara ilitengewa bilioni nane. Sasa napenda kujua; ni lini mkandarasi atakuwa site kwa ahadi ya Waziri, kwa maana ya kwamba hii barabara ni ya muda mrefu kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi toka mwaka 2000?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara anazoziongelea ni kweli zipo katika mpango na fedha zimetengwa na tenda zimetangazwa. Nimwombe tu Mheshimiwa Getere kama ambavyo nimekuwa nikimwomba ofisini, maana amefuatilia sana ofisini, naomba tu yale masuala ya kutaka kupigana ayapunguze, lakini nimhakikishie kwamba kile ambacho nilimuahidi ndani ya ofisi tukiwa pamoja na Katibu Mkuu, tutayatekeleza.
MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mimi nauliza kwa kifupi tu. Barabara hii aliyouliza Mheshimiwa Malocha, mimi na yeye tumekuwa tukiiuliza kila mwaka na huu ni mwaka wetu wa saba hapa Bungeni na ni commitment ya Mheshimiwa Rais Dkt. Jakaya Kikwete aliyepita na Rais wa sasa aliyeko madarakani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kwamba Serikali imekuwa ikitenga fedha kwenye barabara hii, lakini zimekuwa hazitoki na mwaka huu tumeona pamoja na lile daraja. Sasa nataka commitment yake, endapo na mwaka huu stori zitakuwa zilezile za miaka saba iliyopita, ni hatua gani atachukua kama Waziri ili hii barabara ikamilike?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Silinde amekuwa akiuliza mara nyingi na jibu letu muda wote limekuwa hilo hilo, kwamba tutajenga daraja hilo, lakini ameona mwaka huu tumetenga fedha na mwaka ujao na ameshiriki kuzipitisha, nikupongeze pamoja na Wabunge wote. Namuahidi kwamba katika kipindi hiki cha miaka mitano daraja hili litajengwa, lisipojengwa kwa kweli nitamruhusu anikate kichwa.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, ninaomba sasa kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amekiri kwamba, TTCL walishalipwa fedha za sola za Kimarekani 94,000 na ilikuwa ni mwaka 2015. Je, Serikali kwa nini haijawasisitiza TTCL kukamilisha kazi hii ambayo imechukua muda mrefu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, miongoni mwa kata ambazo Kampuni ya Viettel ilikuwa imeshinda zabuni mwaka 2015 ni pamoja na kata ya Sindano, lakini hadi sasa kazi hiyo haijafanyika. Je, Mheshimiwa Waziri atalithibitishia Bunge hili kwamba Viettel watakwenda kufanya hiyo kazi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeisisitiza sana TTCL ikamilishe kazi iliyoianza. Na kama utarudia tena sehemu ambayo nilijibu swali la msingi ni kwamba, kazi hii waliikamilisha, lakini waliikamilisha kwa kutumia teknolojia ya CDMA na sasa wanaondoka katika teknolojia hii ya CDMA kwa sababu teknolojia hii haiwawezeshi wao kuongeza hizi huduma za nyongeza za mobile money na banking kwa hiyo, wanabadilisha mtandao na mtakumbuka kuna wakati hapa Dodoma walizindua ile ya 4G LTE kwa hiyo, sasa wapo katika mpango huo wa kuzindua huo mtandao mpya na hivyo kazi hiyo tutahakikisha inakamilika mapema kama ambavyo wao wameahidi by June, 2017 watakuwa wamefika kule Lupaso na Lipumbiru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu Viettel, ninafahamu Viettel wamekuwa na matatizo kidogo kwa sababu ya mikataba na tunarekebisha kwa sababu, kuna baadhi ya kodi walikuwa wanatarajia wasilipe. Kwa hiyo, wameingiza vifaa vyao vya kuweza kutuletea mawasiliano, lakini vimekwama kidogo kwa sababu ya malipo ya kodi na tutahakikisha hilo linasuluhishwa haraka, wanalipa kodi inayotakiwa, ili hatimaye vifaa hivyo viende vikafanye kazi, vikasimikwe kule kulikokusudiwa.
MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuwa, ni Wizara hiyohiyo ya Uchukuzi, ingawa niliomba swali namba 70.
Kwa kuwa mawasiliano ni haki ya kila Mtanzania, lakini
toka nchi imepata uhuru kuna maeneoa ambayo hayajapata mawasiliano, ikiweko kata ya Kala na Ninde. Ni lini Serikali itatimiza wajibu wake wa kupeleka mawasiliano katika hizo kata, ikizingatia ziko pembezoni? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuhakikishie Serikali ina nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata mawasiliano na ndio sababu kubwa ya kuanzisha huu Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Kwa hiyo, mara tutakapopata fedha tutakuja huko ambako Mheshimiwa Aida umekueleza.
MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yanayowakumba wakazi wa Lulindi, Masasi, yanafanana kabisa na wakazi wa Wilaya ya Malinyi katika kata za Sufi, Kilosa Mpepo; swali langu, kata hizo ninazozitaja ni kwamba kama alivyosema jibu la msingi Mheshimiwa Waziri, kwamba, kupitia Mfuko wa Fursa ya Mawasiliano kwa Wote (UCAF), wamejenga minara miwili katika Kata ya Ngoeranga na kata ya Sufi, lakini minara hiyo ambayo imejengwa chini ya Tigo haifanyi kazi kabisa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali nangu. Je, ni lini Serikali watarekebisha minara hiyo na vilevile kumalizia Kata zile mbili ambazo hazina mawasiliano kabisa, kata ya Sufi na kata nyingine?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niwakikishie kwamba kata hizo mbili alizozieleza ambazo hazina mawasiliano kabisa ikiwa ni pamoja na kata ya Kilosa Mpepo, tutahakikisha kwamba tunazifikishia mawasiliano kwa kadri tutakapopata fedha na maadamu ulishawasilisha hilo mapema Mheshimiwa Mponda nadhani utakumbuka Mheshimiwa Waziri wangu alivyokujibu na nikuthibitishie lie jibu alilokupa Waziri wangu na mimi nitalifuatilia utekelezaji wake.
Mheshimiwa Mponda kuhusiana na kata mbili ambazo…
Alitaja kata nne na nimeongelea kata mbili, kata hizo mbili ambazo Tigo wamejenga minara nitazifuatilia kuhakikisha kwamba minara hiyo inafanya kazi.
MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa suala la Lulindi linafanana kabisa na tatizo lililoko katika jimbo la Makambako. Makambako kuelekea usawa wa kwenda Mbeya ni kilometa mbili eneo moja linaitwa Majengo hakuna mawasiliano. Kilometa tano kuelekea usawa wa kwenda Njombe kijiji chenye eneo la Kyankena Kiumba hakuna mawasiiano; Kitandililo Mawandea hakuna mawasiliano. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka minara hii ilimawasiliano yaweze kupatikana katika maeneo hayo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongea na Mheshimiwa Deo Sanga kutokana na matatizo hayo na matatizo hayo yanatokanana maeneo yenye mteremko kwa hiyo mawasiliano yaliyopo katika eneo hili kuna maeneo ambayo hayana mawasiliano kwa sababu yako chini. Kwa hiyo, tutahakikisha kwamba kwanza kama nilivyokuambia nitapenda nipite hayo maeneo barabara hiyo nikajionee halafu baada ya hapo tuwatake watu wa Mawasiliano kwa Wote wajaribu kurekebisha hayo maeneo ambayo ni ya mteremko tunawezaje kuyapelekea mawasiliano.
MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali ya nyongeza.
Tatizo la mawasiliano lililopo Lulindi linafanana na
tatizo lililopo katika jimbo la Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe. Katika Halmashauri tuna kata nne ambazo hazina mawasiliano kata za Ninga, Ikondo, Ukalawa na Mfiriga hakuna minara na hakuna mawasiliano, je, ni lini Serikali itajenga minara katika kata hizi ili wananchi waweze kupata mawasiliano kwa kuwa inawaathiri kiuchumi kutokana na kutokuwepo mawasiliano? Naomba majibu ya Serikali. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kila kijiji Tanzania kinafikishiwa mawasiliano. Na ndio dhamira ya kuanzisha Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Kwa hiyo, nikuhakikishe Mheshimiwa Mbunge tutayafikisha mawasiliano katika maeneo hayo uliyoyataja mara tutakapopata fedha za kutuwezesha kufikisha mawasiliano maeneo haya.
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, mawasiliano sasa hivi kwa wananchi ni uchumi. Kwa sababu wananchi sasa hivi wanafanya mawasiliano kwa mambo mengi ya kibiashara ya mawasiliano ya magonjwa na kila kitu na vilevile mawasiliano ninafikiri kama hakuna sehemu hakuna mawasiliano hakuna maendeleo. Katika kata za Sibwesa na Kasekese wameweka minara tayari toka Mei na pesa zimashatumika sasa ni lini Serikali itawasha kwa sababu wananchi wanaona ile minara lakini haina faida katika muono wao?
Swali la pili, wananchi wa Ilunde wameahidiwa kwa muda mrefu sana kuhusu mawasiliano. Na ukiangalia kata ya Ilunde iko katikati ya pori ina maana wananchi wale maisha yao yako hatarishi na wengine wanakwenda kupanda kwenye miti, wengine wanadondoka wanavunjika mikono na miguu kwa ajili ya kutafuta mawasiliano. Ninaomba kauli ya Serikali, ni lini sasa Serikali itawajengea mnara kata ya Ilunde? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana kabisa na Mheshimwa Mbunge kwamba mawasiliano ni biashara na nakubaliana naye kwamba ni muhimu sana kuwe na mawasiliano maeneo yote na kama nilivyosema katika majibu yangu ya swali la msingi kwamba Serikali nia ya dhati ya kuhakikisha tunapeleka mawasiliano kila sehemu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini naomba nikiri kwamba mikoa mitatu hii ya Songwe, Rukwa na Katavi sijaizungukia sawa sawa ili nijue hasa matatizo yake katika sekta zote tatu. Nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya kikao hiki cha Bunge la Bajeti nitafika katika mikoa hii mitatu hususan katika kijini hiki cha Ilunde nione na nipate hali halisi. Na mimi nijisikie hali…na hatimaye tupange mipango ya kuondoa matatizo haya.
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa rufsa hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo haya yaliyopo kwenye Mkoa wa Katavi yako pia katika imo jimbo langu la Mkururanga kilometa 60 tu kutoka katika Mkoa wa Dar-es salaam ambapo kata za Kwanzuo Kisegese, Mkamba na kwingineko ikiwa ni pamoja na kijiji ambacho wewe unalima kijiji cha Koragwa Tundani na pale Mkuranga maeneo ya Kiguza. Yote yana shida ya mawasiliano.
Je, Mheshimiwa Naibu yuko tayari yeye na hao viongozi wa huo Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote kushirikiana name kuhakikisha maeneo haya yanapata mawasiliano? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli kwa dhati kabisa niko tayari.
MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona niulize swali ndogo la nyongeza. Matatizo ya usikivu wa simu yaliyopo Mpanda vijijini ni sawa na yaliyopo Wilaya ya Ngara kata Muganza, Nyakisasa Keza, Kabanga na Rusumo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha usikivu wa simu katika kata hizo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema Serikali ina nia ya dhati kabisa yakufikisha mawasiliano kila sehemu na hasa, eneo hili analoliongelea ni maeneo ya mpakani na maeneo ya mpakani tuna utaratibu maalum wa kuhakikisha kwamba mawasiliano yanafika haraka katika maeneo hayo. Kwa hiyo Serikali itahakikisha inafikisha mawasiliano mara fedha zitakapozipata.
MHE. ANNA J. GIDARYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Matatizo yaliyoko Katavi yanafanana sana na matatizo yaliyoko katika Jimbo la Babati Vijijini kata ya Duru vijiji vya Endagwe, Hoshan, Ameyu, Eroton na Wikanzi maeneo haya hayana mawasiliano ya simu. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri ni lini maeneo haya yatapewa vipaumbele ukizingatia uwanja wa ndege wa Manyara unapelekwa Mwikanzi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mara tutakapopata fedha tutahakikisha tunapeleka mawasiliano katika maeneo haya ya Mkoa wa Manyara na hasa maeneo hayo ambayo tuna kusudia kujenga uwanja wa ndege kama ambavyo Mheshimiwa Anna umeyaeleza.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa taratibu zote za kuipandisha hadhi barabara hii zilishafanyika ikiwemo kupitia vikao halali vya Wilaya na Mkoa na kikao cha Road Board mimi mwenyewe nilishiriki tukaipitisha hii barabara. Nilikuwa nataka kuuliza ni sababu ipi inayokwamisha kutokupandishwa hadhi kwa barabara hii?
Pili, kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati anaanza safari ya ushindi ya kuomba ridhaa ya wananchi, ziara yake ya kwanza aliifanya Mkoa wa Katavi na kituo cha kwanza alianzia maeneo ya Mishamo aliwaahidi wananchi wa Mishamo kuwaboreshea barabara hiyo ya kutoka Mishamo mpaka Ziwa Tanganyika kwenye jimbo la Mheshimiwa Hasna Mwilima.
Je, hawaoni sasa ni wakati muafaka wa kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais, ambayo aliwaahidi wananchi wa Mishamo ili kutekeleza ahadi iliyokuwa ameiahidi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukurusana Mheshimiwa Moshi Kakoso kwa sababu itabidi nikapate ukweli ama mkoa haujawasilisha Wizarani ama pale Wizarani pana uzembe. Kwa hiyo, nitakwenda niangalie na nifuatilie hili suala kama kikao halali kilishakaa kwa nini Wizarani hatujapata hayo maombi.
Kwa hiyo, baada ya hapo nikishajua wether kuna tatizo Mkoani inawezekana walikaa lakini hawakuwasilisha au pengine pale Wizarani kuna tatizo.Nitakapopata jibu mtaona matokeo yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya Mishamo kwenda mpaka Baharini ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, wakati wa kampeni tumeipata tunayo katika orodha ya ahadi tulizonazo, nikuhakikishie kwamba tunakwenda awamu kwa awamu katika kutekeleza ahadi zote ambazo tuliziahidi katika kipindi hiki cha miaka mitano. Tutahakikisha ahadi hiyo nayo tutaitekeleza.
MHE.GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Sasa hivi ninavyoongea barabara ya Ifakara - Mahenge haipitiki kabisa, wananchi wanakosa huduma za muhimu kama petroli, dizeli na dawa kwa ujumla. Je, wananchi wa Ulanga wanataka kusikia kauli ya Serikali nini kitafanyika sasa hivi ili watu hawa wa waweze kusafiri kwenda Mahenge? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue fursa hii kuitaka TANROADS Taifa na TANROADS Mkoa wa Mogororo washughulikie ufunguzi wa barabara hii iliyokatika.(Makofi)
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Barabara ya kutoka Kitunda - Kivule -Msongola ninapozungumza sasa hivi haipitiki kabisa nauli imepanda kutoka shilingi 500/= mpaka shilingi 1,000/=; walimu na wanafunzi ambao wanasoma shule ya Mvuti, Mbondole, Kitonga wanatembea kwa miguu kwa umbali wa zaidi ya kilometa 11.
Ningeomba kujua ni hatua gani kwasasa Mheshimiwa Waziri unaweza akachukua kuwasaidia wananchi wale na hasa watumishi wa umma ili waweze kuendelea kupata huduma muhimu katika eneo hilo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nafurahi sana hawa Wabunge wawili wanafanyakazi pamoja ikiwa ni pamoja na Mbunge Bonnah Kaluwa, Mbunge wa Segerea. Alishalileta hilo na kwa taarifa yako TANROADS Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na TANROADS Taifa hivi tunavyoongea wanalishughulikia hilo kwa namna ambayo lililetwa kwetu na Mheshimiwa Bonnah Kaluwa. (Makofi)
MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali ya nyongeza kwamba barabara ya kutoka Igurubi mpaka Igunga kwenda Loya tuliiombea na tulishapeleka maombi kwamba ipandishwe hadhi. Leo mwaka wa tano kuna shida gani?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, maombi ya kupandisha hadhi barabara tunayoyashughulikia sasa ni ya muda mrefu ya kuanzia mwaka 2011/2012 mpaka sasa. Kwa hiyo, nikuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara yako nayo tutakuja kutoa majibu ipi imekubalika kupandishwa hadhi, ipi imekubalika kukasimiwa na ipi tutapendekeza ibakie kwenye Halmashauri, muda sio mrefu maadamu Waziri wangu tayari ameshaanza kulifanyia kazi kwa kasi inayotakiwa kwa sasa...
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize kwali la nyongeza. Kuna barabara ya kutoka Nyororo – Igohole mpaka Mtwango ina kilometa 40 na upembuzi yakinifu ulishafanyika miaka miwili iliyopita. Je, Serikali ni lini itaanza ujenzi wa kiwango cha lami ile barabara? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane tupate takwimu sahihi ya barabara unayoongelea inaanzia wapi, inafikia wapi, ina kilometa kiasi gani na kama imeshajadiliwa kwenye Road Board ya Mkoa ili hatimaye tutende haki ya kile kinachotakiwa katika barabara hiyo.
MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize swali kwamba kwa kuwa ahadi za Rais wakati anaomba kura zimekuwa nyingi na Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kuzitekeleza ikiwepo barabara ya Monduli Juu kule kwa Sokoine. Ni kwa nini Serikali sasa isilete programu maalum inayoonyesha ni lini ahadi hizo zitatekelezwa na fedha zake katika nchi nzima? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi zote ambazo Mheshimiwa Rais alizitoa wakati wa kampeni tunazitekeleza awamu kwa awamu, hatuwezi kuzitekeleza zote katika kipindi cha mwaka mmoja. Kuna kipindi cha miaka mitano na tutahakikisha…
… ahadi zote tunazitekeleza.
MHE. ANTONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Kwa hali ilivyo sasa hivi Moshi Vijijini barabara nyingi hazipitiki na hali ni mbaya sana katika kata ya Mabogini barabara inayoanzia Bogini kwenda Chekereri mpaka kule Kahe na kule Uru Mashariki kata ya Uru Madukani, Mamboleo, Kishumundu mpaka kule Materuri. Hizi barabara zote zimeshaombewa kupandishwa daraja lakini hakuna kinachoeleweka. Sasa ninataka kufahamu kutoka kwa Waziri atakuwa tayari kutoa agizo kwa ajili ya kufanyika tathmini maalum ili hizi barabara tujue tatizo liko wapi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninaamini Halmashauri iendelee kurekebisha hii barabara iweze kupitika muda wote, lakini wakati huo huo majibu ya barabara zipi tutapandisha hadhi yatakuja muda sio mrefu ujao.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka nimpe taarifa kwamba katika Kata ya Hayderer kuna mnara wa Airtel umeanzishwa, una miaka miwili, haujamalizika kabisa, uko kwenye foundation. Sasa kwa kuwa Kata za Yaeda Ampa na Tumati zinakaribiana. Je, Wizara iko tayari sasa kujenga mnara katikati ya kata hizi ili angalau katika mnara huu uliotangazwa tender, kata hizi mbili zikapata mawasiliano?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa maeneo mengi mitandao haifiki, maeneo ya Endagichan, Endamasak, Enargatag, Runguamono, Munguhai, Gembak na Gidamba. Serikali sasa ituambie, ina mpango gani tena wa kuingiza vijiji hivi na kata hizi ili angalau basi Jimbo langu lipate mawasiliano? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tutafuatilia mnara wa Airtel ambao amesema umekaa kwa muda mrefu katika kiwango cha msingi. Tutafuatilia tuone tatizo ni nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuhusu ombi la kujenga katikati ya zile kata mbili; tumelipokea na tutalifuatilia na vilevile vijiji vyote ambavyo amevitaja tumepokea ombi hili, tutaangalia namna ya kuyashughulikia ili hatimaye vijiji hivyo vyote vipate mawasiliano. (Makofi)
MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Matatizo ya mawasiliano ya Mbulu Vijijini yanafanana sana na matatizo ambayo yapo kule katika Tarafa ya Amani Jimbo la Muheza hususan kwenye Kata za Misarai, Kwezitu, Mbomole na kwingineko. Sasa Serikali ina mpango gani kupeleka minara kwenye sehemu hizo na Tarafa hiyo ambayo kwa kweli mawasiliano ni tabu sana?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali ni kupeleka mawasiliano ya uhakika katika Tarafa ya Amani tukiunganisha kata zote ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja. Namwomba Mheshimiwa Balozi Adadi Rajab tuwasiliane ofisini ili tupitie kwa pamoja, tuone kata gani imesahaulika katika zile ambazo Serikali tayari imeziingiza katika mipango yake ya kutekeleza mawasiliano kwa wote.
MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa tatizo la mawasiliano ya simu katika Jimbo la Mtama ni baya kuliko ilivyo katika Jimbo la Mbulu Vijijini, kwa sababu katika Tarafa tano; Tarafa tatu mawasiliano ya simu ni tabu sana, wakati mwingine inabidi upande juu ya mnazi au juu ya kichuguu ili uweze kuwasiliana. Tulianza kupata matumaini baada ya Kampuni ya Viettel kuanza kusambaza minara, tukadhani hali itarekebishika, lakini inaonekana kama kazi ile kama imesimama hivi.
Sasa ni lini kazi ile itakamilika ili wananchi wangu waweze kufaidi matunda ya kazi nzuri ya mawasiliano ya simu katika Jimbo la Mtama?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, haikubaliki kati ya tarafa tano, tarafa mbili tu ndiyo zipate mawasiliano ya uhakika, hiyo haikubaliki. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tutalifuatilia hili, nini hasa kimesababisha ujenzi wa minara katika maeneo hayo kusimama na baada ya hapo tutaangalia namna ya kushughulikia.
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Tatizo lililopo Mbulu Vijijini linafanana kabisa na tatizo lililopo Wilaya ya Kakonko. Wilaya ya Kakonko Kata za Nyamtukuza, Nyabibuye, Warama, Muhange, Kasuga na mwambao wote wa Burundi, simu zinaingiliana na mitambo ya Burundi na hivyo wananchi wa Wilaya ya Kakonko maeneo hayo yanayopakana na Burundi wanapata hasara kubwa sana kwa kuongeza vocha ambazo zinaliwa na mitandao ya Burundi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba commitment ya Serikali hapa; Serikali inafanya jitihada gani kuhakikisha kwamba wananchi hawa hawapati hasara katika matumizi yao ya simu? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo aliyoyataja, kama alivyosema, yako mpakani na tuna mipango maalum ya kushughulikia maeneo ya mipakani. Nitakwenda kuangalia ni kwa nini hasa eneo lake bado halijaboreshwa kwa namna ambavyo ameeleza?
MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, naishukuru Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais, Mheshimiwa John Pombe Magufuli, kwa mara ya kwanza wananchi wa Kazovu, Isaba, Chongo na Katete wataona hata bajaji na gari. Nilipoingia Bungeni mwaka 2010 kilio changu cha kwanza ilikuwa ni barabara lakini awamu ya sasa ni awamu ya chapakazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali dogo, Mheshimiwa Naibu Waziri juzi umetuma wakandarasi wako kuangalia kipande kilichosalia cha kutoka Kazovu kwenda Korongwe, lini sasa Serikali yako itasaidia kipande hicho kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi haina fedha?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Keissy kwa kazi kubwa anayoifanya ya kutafuta barabara hii ijengwe na hatimaye sasa amepata majibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa na mimi napokea salamu hizo za pongezi kwa niaba ya Serikali kwamba tumedhamiria barabara hii ikamilike. Ndiyo maana nimepeleka wataalam wangu kwenda kuiangalia kazi hiyo ili hatimaye tuangalie namna gani tunafanya na kama tulivyojibu katika swali la msingi kwamba sasa tunatafuta fedha kwa ajili ya kuishughulikia barabara hii tukianzia na feasibility study and detail design.
MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa ujenzi wa miundombinu na hasa barabara ni kichocheo kikubwa cha maendeleo; je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kuongeza kasi ya ujenzi wa barabara hii kutoka Ilongero Mudida, Kungi Kidarafa hadi Haydom kutoka kilomita 1.6 ambazo zinajengwa kwa sasa kwa mwaka hadi kufikia kilomita tano ili kuharakisha ujenzi huo na kufungua fursa za kiuchumi kwa mikoa ya Manyara, Arusha na Singida?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa ni viongozi wa chama changu ndiyo walitoa ahadi hii nina imani kubwa na Serikali ya chama changu chini ya Jemedari Dkt.John Pombe Magufuli. Je, Waziri yuko tayari sasa kufanya ziara ili kujionea hali halisi ya barabara hii na kuona sehemu iliyofikia ili kuwajengea upya imani wananchi wa Wilaya ya Singida Vijijini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hii barabara ni muhimu sana na kama tulivyoeleza inaunganisha mikoa miwili ya Singida na Manyara; na pale Haydom pana mambo mazito sana ukitoka Haydom unaenda kwenye ile hospitali kubwa ambayo tunategemea sana watu wa maeneo yale kuanzia Singida mpaka Manyara yote. Kwa hiyo, umuhimu wake tunaufahamu na kwa sababu hiyo tutaangalia kuongeza kasi ya kujenga barabara hii kadri tutakavyokuwa tunawezeshwa kifedha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, nimjulishe tu Mheshimiwa Mbunge mimi barabara ile nilipita lakini bahati mbaya katika ziara zangu huwa naangalia kazi tu; lakini kwa sababu ni vizuri vile vile kwenda kufanya ziara pamoja na Wabunge, nitaangalia muda mwingine nitakapokwenda katika barabara hiyo nimhusishe na Mbunge ili na yeye ajue kwamba huwa napita katika barabara hiyo. (Makofi)
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru pia ninamshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii sio ahadi tu ya Rais Mstaafu na kwenye Ilani ya Uchaguzi bali pia ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipotembelea Wilaya ya Mafia mwezi Septemba, 2016. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Mafia kwa kuwa ni kisiwa, hali ya upatikanaji wa udongo ni ndogo sana. Udongo unapatikana katika kijiji kimoja cha Bweni na wataalam wanasema baada ya miaka miwili udongo huo utakuwa umekwisha kabisa. Kwa hiyo, mtakapokuwa tayari kuja kujenga barabara ya lami, udongo Mafia utakuwa umekwisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, sasa kwa kuwa Ilani ya CCM inasema mwaka huu mtaanza na usanifu na katika majibu yako hujasema hata kama usanifu utafanyika, swali la kwanza; kwa nini usanifu usifanyike mwaka huu ili ujenzi ufanyike mwakani?
La pili; ni kwanini sasaSerikali isitilie maanani hili suala la ukosefu wa udongo na kuharakisha ujenzi huu ifikapo mwakani? Ahsante.(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbaraka Kitwana Dau kwa namna anavyofuatilia masuala ya miundombinu katika Kisiwa cha Mafia na kwa kweli aliponipeleka Mafia mimi nimebadilika kabisa. Naomba nimhakikishie yale ambayo tuliyaongea tutayafuatilia ili kuhakikisha ahadi hii ambayo kama alivyosema sio ya Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne peke yake bali ipo katika Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2015; lakini vilevile Waziri Mkuu alipokwenda pale ambapo yeye alitangulia kabla yangu naye alirudia kuahidi kutokana na mazingira yalivyo pale Mafia.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba nikuhakikishie kwamba tutawasiliana ndani ya Wizara kama ambavyo tulikwambia awali ili tuone uwezekano wa kuanza feasibility study and detailed design ya barabara ile mwaka huu kwa kadri ambavyo Mwenyezi Mungu atatujaalia na mimi naamini Mwenyezi Mungu yupo upande wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dau kwa swali lako la pili naomba tukutane na Mheshimiwa Waziri wangu na kwa sababu leo ni siku ya mwisho ya Bunge na Waziri wangu yupo jana ulikutana nae lakini naomba tukutane nae tena ili tulikamilishe hili kama ambavyo uliambiwa na Waziri wangu jana.
MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Niipongeze pia Serikali ni kweli majuzi tumepokea ugeni na shughuli hiyo imeanza mara moja. Hiyo ndiyo Serikali ya Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kuna nyumba zinatakiwa kubomolewa maeneo ya Kintinku, Chikuyu, Maweni barabara kuu zimewekewa alama ya kijani tangu 2013 na kijani maana yake ni kwamba kuna malipo ya fidia, lakini hawajalipwa fidia, Serikali inasema nini? Ni lini wananchi hawa watalipwa?
Samahani Mwenyekiti, swali la pili. Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu 2013 tuliomba barabara inayoanzia Chikuyu – Chibumagwa - Mpandagani - Ikasi ambayo ina urefu wa kilomita 84 ipandishwe daraja lakini tangu kipindi hicho naona ni kimya Serikali haijaleta majibu. Hata hivyo, tarehe 17/3/2015 wataalam kutoka Wizara husika walikuja kukagua barabara hii. Tulitegemea majibu yatoke lakini mpaka sasa hivi ni kimya. Ni lini sasa Serikali itapandisha hadhi barabara hii?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ya Kintinku - Chikuyu na Maweni ambayo yapo katika barabara kuu yamewekewa alama ya ‘X’ ya kijani kama ambavyo tumeweka alama za ‘X’ za kijani na nyekundu katika barabara nyingi sana humu Tanzania tokea Sheria ile ya 2007 ilipopitishwa na Kanuni ya 2013 ilipopitishwa. Maana ya zile ‘X’ ni kwamba tunakujulisha eneo hilo liko ndani ya hifadhi ya barabara kwa mujibu wa Sheria mpya ya mwaka 2007 lakini eneo lako liko kati ya mita 22.5 ambayo ni hifadhi ya barabara kwa sheria ya zamani na mita 30 kwa sheria ya sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu upanuzi huu umefanyika wakati wewe tayari ulishajenga unastahili kulipwa fidia lakini unachotakiwa kufanya ni kuhakikisha kwamba huongezi maendeleo yoyote katika eneo hilo, hiyo ndiyo maana yake. Sasa fidia inakuja wakati eneo hilo linapohitajika. Eneo hilo linapohitajika kupanua barabara tunawalipa fidia kabla hatujaanza kazi ya upanuzi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kama ambavyo yeye alisimama na mimi nikasimama, barabara inayoanzia Chikuyu - Chibumagwa na kuendelea ombi la kwamba ipandishwe hadhi nimwombe tu avute subira majibu yatolewa. Tuna maombi mengi tu yamekuja na mara yatakapokamilika tutatoa taarifa barabara zipi zimepandishwa hadhi na zipi hazikupandishwa hadhi kutokana na vigezo ambavyo tumejiwekea wenyewe kwa mujibu wa sheria.
MHE. MPAKATE D. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba niulize swali la nyongeza, kama ifuatavyo. Tatizo la Manyoni linafanana kabisa na mazingira ya tatizo la barabara ya Mtwaro - Pachani - Lusewa - Mchoteka - Nalasi - Mbesa - Tunduru Mjini ambayo iliwekewa alama za ‘X’ zaidi ya miaka saba iliyopita. Je, ni lini ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami utaanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naona Mheshimiwa Mbunge ameanza kutaja maeneo ambayo yako katika Jimbo langu katika kuongeza umuhimu wa swali lake. Naomba tu niseme masuala ya fidia ni ya Kitaifa na wakati ambapo tutaanza kujenga na sasa hivi siwezi kusema tunaanza lini kwa sababu fedha zilizotengwa kwa sasa ni za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa sababu kazi hiyo bado haijakamilika. Naomba kwanza tuikamilishe kazi upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kabla hatujaanza kutafuta fedha za kujenga hiyo barabara.
MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na bandari iliyokuwepo Serikali ilipata uwezekezaji wa ujenzi wa bandari mpya ya Mwambani na kama sikosei ilikuwa ni Serikali ya Uganda na Serikali ya Kuwait. Swali la kwanza, kwa kuwa feasibility study pia ilikwishafanyika, je, ujenzi huu wa bandari mpya wa Mwambani nao umefikia hatua gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, zipo systems za
FIFO na LIFO method, First In First Out na Last In First Out, kwa nini naambiwa kwamba itaanza kujengwa bandari ya Bagamoyo katika siku za karibuni isianze kujengwa ile bandari ya Tanga? Nataka kujua hilo.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, bandari ya Mwambani kama ilivyo bandari ya Bagamoyo tulikuwa tunatarajia ijengwe kwa njia ya PPP. Unapokwenda kwenye masuala ya PPP inategemea na yule aliyeonesha nia ya kujenga. Wapo watu wameonesha nia Bagamoyo na Tanga pia lakini tatizo lililotokea kwa Mwambani ni kwamba upembuzi yakinifu na usanifu wa kina uliofanyika ulionesha kwamba bandari ile haina faida. Sababu yake hawakufikiria mizigo ambayo italetwa na reli inatokea Musoma hadi Tanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sasa tumeanza kazi upya ya kuipitia hiyo taarifa ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili waunganishe na uwekezaji mpya uliojitokeza pale Tanga ili hatimaye bandari ile ya Mwambani ionekane ina faida kuijenga. Kwa hiyo, ni kweli kuna huo utaratibu wa FIFO na kadhalika lakini hatimaye kwa sababu unatumia PPP ni lazima ufuate wale wateja wako wanaotaka kuwekeza pale unaendana nao vipi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali la pili, nalo nadhani nimelijibu wakati najibu hili kwa kirefu kwa sababu hoja ni ileile. Nakushuruku sana.
MH. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Pangani kama zilivyo wilaya nyingine zilizoko pembezoni mwa bahari ina bandari bubu nyingi. Bandari hizi zinatumika kuingiza mizigo ambayo ni halali na ambayo pia siyo halali kama vile madawa ya kulevya, wahamiaji haramu hata na bangi kitu ambacho kinasababisha bandari hizi zinakuwa ni chanzo kikubwa cha rushwa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuzitambua bandari hizi ili zile zenye vigezo ziweze kurasimishwa na kutambulika rasmi ikiwa ni pamoja na kuzikarabati na zile ambazo hazifai zifungwe kwa maslahi ya Taifa na watu Pangani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, anayoyasema ni sahihi na nadhani anafahamu kwamba ndicho tunachotekeleza ndani ya Serikali kwa sababu tuna timu ya Wakuu wa Mikoa yote iliyoko kwenye mwambao na upande wa Zanzibar wanakutana kila wakati kuhakikisha wanapitia zile bandari bubu kuona zipi zinaweza zikaendelezwa na kurasimishwa na zipi ambazo zinatakiwa kufungwa inasimamiwa kufungwa. Nadhani ni kitu ambacho anafahamu tunakitekeleza na nimushukuru sana kwa sababu kwa kuuuliza hivyo maana yake anaunga mkono hatua tunayoichukua.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali ndogo la nyongeza. Serikali iliazimia kufanya marekebisho ya kuziboresha bandari za Maziwa Makuu kwa maana ya Ziwa Victoria, Nyasa na Lake Tanganyika. Serikali iliazimia kujenga bandari ya Kalema ili iweze kuunganisha na nchi jirani ya DRC. Ni lini bandari ya Kalema itakamilika kama Serikali ilivyokuwa imetoa hoja ya kujenga bandari hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Kakos, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Miundombinu, kwa namna anavyofuatilia maendeleo ya bandari za Mwambao wa Ziwa Tanganyika. Amekuwa mstari wa mbele sana katika kulihangaikia hilo na sisi tunamuunga mkono katika hilo, tutahakikisha dhamira yake ya kuwatumikia watu wa Mwambao wa Ziwa Tanganyika inatimia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu kwamba kazi inayofanyika sasa ni kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa reli na bandari, reli kutoka Kaliua mpaka Kalema pamoja na bandari yake ili hatimaye tujenge reli na bandari tuweze kuhudumia mizigo mingi kutoka Kalemie upande wenzetu wa DRC Kongo. Nimwombe akubali kwamba yale ambayo tunakubaliana katika Kamati ndiyo Serikali itakayoyatekeleza. Ahsanteni sana.
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ujenzi, nina swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa baadhi ya makampuni haya kwa muda mrefu sana yamekuwa yakifanya udanganyifu na hasa katika miamala ya simu pamoja na muda wa maongezi kwa wateja na kwa kuwa Serikali tayari imeshaanza kudhibiti suala hili. Je, Serikali haioni kwamba ni busara na ni vyema kuendelea kudhibiti makampuni yote haya ya simu yaweze kulipa kipato sahihi na kutokuwanyonya wananchi katika suala la miamala ya simu pamoja na muda wa maongezi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana naye na ndivyo tunavyotaka kufanya na tunavyoEndelea kufanya kwa kutumia huu mtambo wa TTMS na makampuni yote hatutaacha hata moja tutayaingiza katika mfumo huu na kuhakikisha mapato yao yote yanayopatikana tunayafahamu na tunapata haki yetu.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujua kama mfumo anaosema Mheshimiwa Naibu Waziri unasaidia pia kukusanya data za malipo ya nyimbo za wasanii ambazo zinatumika kama miito kwa sababu ni mara nyingi wamekuwa wakidhulumiwa na kutokujua ni kiasi gani wameuza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, hatujaanza kulifuatilia eneo hilo, lakini tukishakamilisha mfumo huu wa Total Revenue Assurance, nina uhakika tutaingia huko. Kikubwa hapa ni mikataba kati ya wasanii na hawa watoa huduma. Ni kazi ya sisi kupitia huu mtambo kuhakikisha tunasimamia mikataba yao na hatimaye tunawanufaisha wasanii. Hilo nadhani litaweza kufanyika, ngoja tusubiri mtambo huu ukamilike katika mfumo wake wa Total Revenue Assurance.
MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na wizi unaofanywa na baadhi ya makampuni ya simu, yanakata fedha za wateja yakidai kwamba tumekuunganisha na huduma fulani ambayo mteja hakuomba. Je, Serikali imejipanga vipi kudhibiti hali hii ya wizi unaofanywa na makampuni haya? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo ni namna tunavyotumia simu hizi. Mara nyingi sana huwa tunaulizwa maswali fulani na tunapojibu tunahalalisha makato bila wenyewe kujijua au unapobonyeza baadhi ya button unajikuta unakubali ukatwe bila mwenyewe kujua. Kwa hiyo, tumewataka watu wa TCRA wahakikishe wanatoa elimu ya kutosha ili wananchi wasifike mahali fedha zao zinakwenda bila ridhaa yao wakati wao wana utaalam wa kuwajulisha wananchi na wakatuelewesha ni namna gani tuzitumie hizi gadgets hasa hizi za android za siku hizi…
MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nauliza swali hili nadhani ni mara ya saba tangu nimekuwa hapa Bungeni. Makampuni ya simu ya nchi jirani kwa mfano MTN ya Zambia na Safaricom ya Kenya yana nguvu kiasi kwamba ukiwa Tunduma huwezi kupata mitandao kutoka kwenye makampuni ya hapa kwetu na ukiwa kule Rombo karibu nusu ya eneo la Rombo Safaricom ndiyo inayosikika na mbaya zaidi hata Redio yetu ya Taifa haisikiki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa inaonekana kama wananchi wa mipakani tumetengwa fulani hivi na huduma hizi za simu pamoja na Redio ya Taifa. Naomba hii iwe mara ya mwisho, ni lini Serikali itarekebisha tatizo hili ili kutoingiza wananchi wanaokaa mipakani kwenye roaming facility na hivyo kuibiwa muda wao wa maongezi bila wao wenyewe kutaka? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani wakati tunapitisha bajeti ya Wizara ya Habari mtakumbuka kwamba tuliongelea sana uimarishaji wa TBC. Tatizo ni kwamba mitambo yetu hatujaifikisha katika maeneo ya mipakani kwa kiwango cha kutosha. Tukishaifikisha mitambo yetu katika maeneo ya mipakani frequency haziwezi kuingiliana, uki-tune TBC utapata TBC, ingawa bado ukitaka ku-tune ya upande wa pili nayo utaisikia kwa sababu wenyewe watakuwa wapo kwenye frequency tofauti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tutahakikisha tunaimarisha ile miundombinu ya TBC ili isikike vizuri maeneo yote ya mipakani. Vilevile wenzetu wanaotoa huduma za mawasiliano ya simu na internet nao wakiimarisha huduma zao tatizo hili litakwisha. Kwa hiyo, tupo katika mazingira hayo ya kuimarisha na nadhani atakumbuka tulichokubaliana au tulichopitisha kwenye bajeti ile ya Wizara ya Habari. Ahsanteni sana. (Makofi)
MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini zipo taarifa ambazo si rasmi sana kwamba zabuni ile ya kumpata mkandarasi wa kujenga daraja la Mto Momba zilisitishwa hivi karibuni na kuleta wasiwasi mkubwa sana kwa wananchi wa mikoa ya Songwe, Katavi na Rukwa kwamba daraja lao inawezekana lisijengwe. Leo Waziri anawathibitishia nini wananchi wa mikoa hiyo kwamba daraja hilo litaanza kujengwa lini?(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Wilaya ya Momba ina kanda mbili, kuna ukanda wa juu na kuna ukanda wa chini na katika Ukanda wa Chini kuna Kata za Msangano, Chitete, Chilulumo, Mkulwe, Kamsamba pamoja na Ivuna. Ukanda wa Juu kuna Kata za Kapele, Miunga Nzoka, Ikana pamoja na Ndalambo na Halmashauri ya Mji wa Tunduma. Barabara za kuingia katika Makao Makuu ya Wilaya mpya hazipitiki kabisa. Ni lini Serikali itahakikisha kwamba inatenga fedha za kujenga barabara ya kutoka Ikana mpaka Chitete na Tunduma kuelekea Chitete?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mwaka huu wa fedha wa 2016/2017 tumetenga shilingi milioni 2,935 na taratibu za kumpata mkandarasi zinazofanywa na TANROADS ziko katika hatua za mwisho. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba taratibu hizo mara zitakapokamilika, mkandarasi akipatikana atalipwa fedha hizo kama advance payment. Mwaka unaofuata ambao ujenzi utaendelea zimetengwa tena shilingi bilioni tatu kwa ajili ya kuendeleza ujenzi huo, naomba nimhakikishie hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu maeneo ya barabara aliyoyataja, hayo majina kwangu ni mageni kidogo lakini kama ana maana ya ile barabara inayounganisha hii mikoa mitatu ambapo sehemu kubwa inapita eneo la Mkoa wako wa Songwe, nadhani anafahamu na mara nyingi tumekuwa tukijibu hapa kwamba mara tutakapomaliza kujenga hili daraja la Momba tutaingia sasa kwenye suala la ujenzi wa barabara. Kama ana maana ya barabara nyingine, naomba nimkaribishe ofisini tukutane na wataalam tupate ratiba ya nini hasa kitafanyika katika mwaka huu wa fedha na mwaka ujao wa fedha na hatimaye tupate majibu ya suala lake na tuweze kuwaridhisha wananchi anaowawakilisha.
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la kutokuwa na mawasiliano katika jimbo hilo la Momba linafanana kabisa na barabara ya ulinzi ambayo inaanzia Mtwara Mjini na kuzunguka Mikoa yote ya Kusini kwamba mvua zilizonyeesha hivi sasa barabara hii haipitiki na hasa katika maeneo ya kijiji cha Kivava na Mahurunga mvua imeweza kukata madaraja na barabara hii hivi sasa haipitiki. Je, Serikali hivi sasa ipo tayari kuharakisha ujenzi wa barabara hii ya ulinzi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba sasa hivi mkandarasi yuko site kwa ajili ya ujenzi wa kipande cha kutoka Mtwara hadi Mnivata na baada ya hapo tunaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kuendelea kujenga barabara hiyo mpaka Newala na baadaye tunaendelea na ile barabara inayoambaa kwenye Mto Ruvuma ambayo tunasema ni barabara ya ulinzi, nadhani hilo analifahamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madaraja yaliyobomoko, bahati nzuri Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mtwara ni kati ya Mamaneja ambao ni wepesi sana na alishatujulisha hayo na tumempa maelekezo ya kufanya huku akiwasiliana na Road Board kwa ajili ya kutumia fedha za emergency kurekebisha zile barabara zilizokatika.
MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri ameeleza katika swali la msingi umuhimu wa ujenzi wa daraja la Mto Momba kwamba ni kiungo muhimu katika kuunganisha mikoa mitatu. Kwa kuwa Sera ya Serikali katika ujenzi wa barabara za lami inazingatia barabara zinazounganisha mikoa. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii muhimu kwa kiwango cha lami inayounganisha mikoa mitatu ya Katavi, Rukwa na Songwe?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Ignas Malocha kwa kazi kubwa anayoifanya ya kufuatilia ujenzi wa barabara hii.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Malocha amekuja ofisini kwetu mara nyingi na tumeongea sana kuhusu barabara hii na tumemwambia mara tutakapokamilisha ujenzi wa daraja la Momba hatua itakayofuata ni kuhakikisha tunaanza na kazi ya feasibility study and detail design kwa ajili ya kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Tumeongea hayo ofisini na mimi nimwombe yale ambayo tulikubaliana ofisi tutayatekeleza kwa manufaa ya wananchi wa mikoa hii mitatu.
MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nchi nyingi duniani stesheni za reli ni vituo vya biashara tofauti kabisa na nchini kwetu Tanzania. Serikali inaweza kueleza ni kwa nini stesheni kubwa kama Morogoro, Dodoma, Tabora na Mwanza huduma huwa zimedumaa na hakuna huduma za biashara? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, TRL ipo tayali kushirikiana na sekta binafsi kuendesha stesheni za reli kwa kuziboresha ikiwemo kuweka hoteli, huduma za maduka na kadhalika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Halima Abdallah Bulembo kuuliza kitu ambacho Serikali nayo imekuwa ikijiuliza ni kwa nini wafanyabiashara hawachangamkii fursa za kufanya biashara katika maeneo ya stesheni za reli. Kwa sababu ametupa nguvu zaidi leo, suala hili tutaendelea kulisukuma, TRL waangalie uwezekano wa kuwahamasisha wafanyabiashara washirikiane nao kama wataona hili linafaa katika mazingira ambayo wanafanyia biashara hiyo ya reli.
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa fursa na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sisi wadau wa reli tuna imani kubwa na Wizara lakini tuna imani kubwa na Mkurugunzi wa TRL, Bwana Masanja lakini tumekuwa na kero kubwa ya kutokukata tiketi bila kuwa na kitambulisho huku tukijua mazingira ya stesheni za vijiji zilivyo, tukijua watu wetu wanaoishi vijijini walivyo. Mtu akiwa mgonjwa mahuhuti hana kitambulisho anataka kwenda stesheni yenye zahanati anakataliwa kupewa tiketi. Je, Wizara pamoja na Shirika inakubaliana na mimi kufuta hilo sharti la vitambulisho ili mtu aweze kupata tiketi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimia Naibu Spika, ni kweli kuna adha katika suala la uhitaji wa tiketi na tumeliona hilo, lakini kuna ukweli vilevile wapo watu wengi wamekuwa wakitumia fursa hiyo ya kutotumia kitambulisho kurusha tiketi, wanakusanya tiketi nyingi wanakuja kuwauzia watu wengine. Kwa upande wa pili vilevile suala la kiusalama, watu wengi sana ambao siyo Watanzania wamekuwa wakitumia safari zetu za reli na hivyo kuonekana kwamba TRL inashiriki katika kusafirisha wasafiri haramu. Kwa hiyo, tutaangalia katika hasara na faida ya suala hilo, kwa sasa naomba atuvumilie tutaendelea kufuata huo utaratibu hadi hapo tutakapoona kwamba changamoto hizi mbili kubwa zitafutiwe namna nyingine ya kuzishughulikia.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa fursa hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, matatizo ya vituo vya reli yanafanana sana na matatizo ya vituo vya boti vinavyomilikiwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari - TPA. Kituo cha boti cha Nyamisati hakina vyoo, maji na migahawa. Je, ni lini Naibu Waziri ataielekeza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari - TPA wakajenge vyoo, maji, umeme pamoja na masuala mengine ya kijamii? Ahsante sana.(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nachukulia aliyoyasema ni mapendekezo, tumepokea mapendekezo yake na kwa sababu anajua kile kituo cha Nyamisati hivi sasa ndiyo kinaanza kufanyiwa kazi ya kujengwa basi watakapokuja katika hatua za ujenzi watu wa TPA wafikirie vilevile mapendekezo ambayo Mheshimiwa Dau ameyatoa ili yaweze kushughulikiwa.
MHE. JOSEPH K. MHAGAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa vile barabara hii ya Makambako - Songea uharibifu wake umechangiwa kwa kiwango kikubwa na usafirishaji wa magari na mizigo mizito kutoka na kuelekea Songea. Ni lini sasa Serikali itajenga reli kutoka Makambako kuelekea Songea kupitia Madaba? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile mizigo mingi pia inatoka Mbeya kuelekea Songea mpaka Mbinga, ni lini sasa Serikali itakamilisha meli ya kutoka Kyela kwenda Mbamba Bay ili mizigo mingi inayopita barabara ya Mbeya kuelekea Songea ipite kwa kutumia meli na kuokoa barabara zetu?(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali haijafikiria kujenga reli kutoka Makambako kwenda Songea, badala yake inafikiria na kwa sasa inatekeleza upembezi yakinifu na usanifu wa kina wa reli kutoka Mtwara - Songea hadi Mbamba Bay. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu meli, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mhagama, hivi karibuni tu TPA wamekamilisha ujenzi wa meli mbili aina ya tishali zinazojiendesha ambazo zitafanya safari za kubeba mizigo kati ya Itungi pamoja na Mbinga. Kwa hiyo, meli hizo zitasaidia sana kupunguza mizigo inayopita katika barabara ya Makambako hadi Songea. Meli hizo zitazinduliwa hivi karibuni zinaitwa Self Propelled Barges, ni meli aina ya tishali.
MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ya Makambako - Songea imefanana sana na barabara ya Manyovu - Kasulu - Kibondo hadi Kabingo na bahati nzuri barabara hiyo Naibu Waziri ameitembelea. Ni kwa nini sasa barabara hiyo wasiingie kwenye ule mtindo wa kusanifu na kujenga (design and build) wakati usanifu unachukua muda mrefu kufika mpaka Kabingo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara anayoongelea ni karibu unakamilika, kwa hiyo, nadhani kubadilisha mfumo kwa sasa haina sababu sana. Mfumo wa jenga sanifu tunapenda kuutumia lakini tunajua gharama yake ni kubwa kidogo ukilinganisha na tukifanya usanifu wenyewe na baadaye tunatoa tender.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi nimuombe tu, tuhakikishe tunakamilisha kazi hii inayokamilika sasa hivi na baada ya hapo tuanze kutenga fedha za kujenga barabara hiyo. Kwa sababu lengo lako ni kuhakikisha barabara hii inajengwa kwa kiwango cha lami na inajengwa haraka iwezekanavyo.
MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la barabara la Makambako - Songea yanafanana na matatizo ya barabara inayotoka Mwatasi -Kimara – Idete - Idegenda ambako uzalishaji wa mbao pamoja na matunda aina ya pears ni wa kiwango kikubwa sana lakini hali ya barabara hii siyo nzuri. Ni lini Serikali sasa itafanya mpango mkakati kuhakikisha hizi barabara zinatengenezwa kwa kiwango cha lami ili kupelekea usafirishaji wa mbao uwe salama na safi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Songea - Makambako ni trunk road wakati barabara anayoongelea ni ya district. Ni kweli zinafanana kwa sababu zote ni barabara lakini zina hadhi mbili tofauti na district road zinashughulikiwa na Halmashauri chini ya TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na hoja yake lakini naomba Watanzania wote tuungane kama watu wamoja, tuweke vipaumbele vya hizi barabara na vile ambavyo tunakubaliana tuanze navyo, tuanze navyo, kwa sababu hatimaye fedha zinahitajika na hatuwezi kujenga barabara zote kwa wakati mmoja, ni lazima tuanze hizi, baadaye tunafuata hizi, hatua kwa hatua. Kwa hiyo, nimuombe avute subira itafika wakati baada ya kukamilisha zile ambazo tumekubaliana ni vipaumbele chini ya Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya 2015 - 2020 tutakuja huku ambako Mheshimiwa Mgonokulima anakuongelea.
MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Makambako - Songea halina tofauti na tatizo la barabara ya Kimanzichana – Mkamba, Mkamba – Mkuruwili, Mkuruwili – Msanga hiyo ni kwa Wilaya ya Mkuranga na tatizo la Mpuyani - Mwanarumango, Mwanarumango – Msanga -Vikumbulu na hiyo inatokana na tatizo kubwa la mvua iliyonyesha na kupelekea barabara kukatika hadi kufanya wafanyabiashara ya kusafirisha abiria na magari ya mizigo yanayobeba malighafi kupeleka viwandani kushindwa kufanya safari zake.
Je, Serikali kwa kuwa haina pesa na lengo lake ni kuweka lami kwa barabara hizo, ni lini Serikali itakuwa tayari kuweka changarawe na kukarabati yale maeneo korofi ili kuweza kusaidia jamii ya maeneo hayo waweze kupita kwa usalama? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli lazima nitambue juhudi za Mheshimiwa Zaynabu Vulu katika kufuatilia barabara hizi na hasa hiyo barabara aliyoitaja ambayo inaharibiwa na magari makubwa yanayobeba malighafi zinazokwenda viwandani. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Vulu, kama ambavyo tumekuwa tukimhakikishia mimi na Waziri wangu wakati anafuatilia masuala hayo Ofisini kwetu mbele ya wataalam vilevile, aendelee kufanya kwa namna anavyofanya ili hatimaye yeye na sisi tufike hapo tunapotaka kufika. Tunajua katika barabara hii moja aliyoitaja ni ile barabara niliyosema ni kipaumbele namba mbili cha kuhamasisha viwanda au cha kuwezesha viwanda. Nikumhakikishie tuna nia thabiti na wakati wowote tutakapopata fedha tutahakikisha barabara hizi zinajengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama alivyosema kwa sasa tumeshatoa maelekezo kwa Mameneja wote wa Mikoa wa TANROADS, barabara zote zilizokatika zirudishiwe kwa kutumia fedha za emergence. Washirikiane TANROADS pamoja na Mfuko wa Barabara kuhakikisha wanarudisha mawasiliono katika maeneo yote ambayo mawasiliano yamekatika. Maelezo hayo tumeyatoa na nina hakika Meneja wetu wa Mkoa wa Pwani atahakikisha maeneo hayo anayoyataja Mheshimiwa Mbunge ambayo barabara zimekatika mawasiliano yanarudi. (Makofi)
MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo lililopo kwenye barabara ya Makambako – Songea linafanana kabisa na tatizo lililopo Mombo – Soni - Lushoto kilometa 36 na juzi baada ya zile mvua kubwa imesababisha uharibifu mkubwa wa barabara ile. Je, ni lini sasa Serikali itaifanyia ukarabati mkubwa barabara hii ya Mombo – Soni - Lushoto kilometa 36?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rashid Shangazi kwa sababu yeye alikuwa wa kwanza kunijulisha matatizo yaliyotokea katika barabara hii anayoongelea kabla hata ya wataalam wangu hawajaniambia. Nadhani sasa anafahamu kwamba barabara hiyo imeanza kupitika kwa sababu kazi imefanyika ya kurudisha mawasiliano na kutengeneza pale ambapo mawe yaliteremka na kuziba barabara. Tunashukuru barabara hiyo sasa inaanza kupitika baada ya matengenezo kukamilika na tutaendelea kuifanyia marekebisho pale ambapo tutaona panahitajika. Nakushukuru sana Mheshimiwa Shangazi. (Makofi)
MHE. ABDALLAH H. ULEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu hayo ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi hawa ni wa muda mrefu sasa, wao wenyewe wameridhi kutoka kwa wazazi wao ambao wameshafariki, na wao wenyewe miongoni mwao wanaelekea kuwa watu wazima sasa, ni lini Serikali itawalipa haki zao wananchi hawa, ilimradi wale warithi wao wasisumbuke kama ambavyo wao sasa hivi wanavyoishi, wakiwa hawaelewi ni lini watalipwa pesa zao? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu la swali la msingi, ni kwamba wananchi hao waliowekewa alama ‘X’ hawatakiwa kufanya maendelezo, lakini hawatakiwi kubomoa nyumba zao, wataendelea kuzitumia mpaka pale Serikali itakapokuja kuyatwaa maeneo hayo kwa ajili ya upanuzi au ujenzi wa barabara.
Kwa sasa kwa wale ambao wako ndani ya mita 22.5 wanatakiwa wabomoe na waondoke wakajenge sehemu nyingine. Wale ambao wako kati ya mita 22.5 na mita 30 wanaendelea kuyatumia maeneo yao mpaka pale Serikali itakapolitaka hilo eneo, na ndipo uthamini utafanyika na fidia watalipwa. Tumetoa hizo alama ‘X’ barabara zote Tanzania nzima, sidhani kama ni sahihi kwamba wewe uliyewekewa alama ya kijani ya ‘X’ ulipwe fidia nchi nzima hata bajeti yote tukiitumia kulipa fidia haitatosha. Kwa hiyo, tutakuwa tunalipa pale tu ambapo sasa tunataka kuanza kulitumia hilo eneo. (Makofi)
MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwa wananchi wa Mkuranga na Kisiju pale Songea Mjini na sisi tuna tatizo hilo hilo la ‘X’. Barabara ya Mtwara Corridor ambayo inapita Songea Mjini inafanya mchepuko katika eneo la Ruhilaseko kuelekea Masigira, Msamala, Mkuzo na Luhuwiko. Eneo hili wananchi wamewekewa ‘X’ kwa muda mrefu lakini hawajalipwa fidia yao na wala barabara haijaanza kujengwa. Sasa naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je wananchi hawa ambao wana alama za ‘X’ za muda mrefu ni lini watalipwa fidia zao ili barabara ianze kujengwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa jibu la haraka kwa swali lake ni kwamba tutalipa fidia mara pale barabara hiyo au barabara ile ya mchepuko tutakapoanza kuijenga. Katika fedha tutakazozitenga kwa ajili ya kujenga barabara ile ya mchepuko zitahusisha vilevile na fedha za fidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu niongeze kidogo kuhusu eneo analoliongelea, kwa bahati nzuri ule mchepuko ni lazima ujengwe haraka kutokana na mazingira ya mji wa Songea yalivyo, na hivyo nimhakikishie tu kwamba malipo haya hayatachelewa sana kwa sababu ujenzi wa barabara ile ya mchepuko hautachelewa sana kushughulikiwa.
MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, shukrani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, katika majibu yake ya msingi amesema kwamba watalipwa pale maeneo watakapoyahitaji, lakini tukiangalia kuna maendeleo yanayoenda kufanywa sasa hivi, kwa mfano katika barabara yangu ya Kibaoni, Usevya, Mbede, Majimoto, Mamba, Kasansa mpaka Mfinga ambako tutatekeleza REA III. Ni lini wananchi hawa wenye alama za ‘X’ za kijani mtawalipa pesa zao ili waweze kufaya marekebisho ya nyumba zao waweze kuweka umeme wa REA?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu katika swali la msingi la Mheshimiwa Ulega, ni kwamba kila tunapotaka kuanza kujenga barabara fedha zinazotengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara zinaunganishwa vile vile na fedha za kulipa fidia katika maeneo ambayo tunatarajia kuyajenga.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Pudenciana Kikwembe na wananchi wa Kavuu kwamba tutawalipa fidia wale wanaostahili kulipwa fidia mara tutakapopata fedha za kuanza kujenga barabara husika.
MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kulifanywa swali langu na mimi kuwa swali la Kibunge.
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa kwa mujibu wa jibu lake la nmsingi ameeleza kwamba kwa mwaka huu 2016/2017 zimetengwa shilingi 3,000,000,000 kwa ajili ya ukarabati wa kipande hiki cha barabara ya Mlandizi – Chalinze kwa kuwa tupo mwezi huu wa sita umebaki wa mmoja tu, je mpaka sasa ni kiasi gani wamekipeleka kwenye mamlaka yetu ya barabara TANROADS Pwani?
Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa kuwa kwa mujibu wa Sheria za Fedha inapofika mwisho wa mwaka wa fedha 30 Juni, 2017 pesa zote zilizosalia zinarudishwa kwenye Mfuko Mkuu wa Hazina. Na kwa kuwa barabara hii haijakarabatiwa mpaka sasa, je, Mheshimiwa Waziri anatuthibitishiaje kwamba barabara hii itakarabatiwa kwa kuwa mwaka wa fedha umekaribia kukamilika? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Subira Mgalu kwamba fedha hizi zilizotengwa ni za ukarabati, fedha zinazorudishwa ni zile za maendeleo, fedha za ukarabati huwa hazirudishwi. Kwa hiyo, nikuhakikishie fedha hizi zilizotengwa zipo na zitafanya hiyo kazi iliyokusudiwa mara taratibu za kusaini mikataba itakapokamilika. Nikuhakikishie Mheshimiwa Subira Mgalu huo ndio ukweli wenyewe, fedha hizi hazitarudishwa.
MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi, unapokuwa katika eneo la huyu mwekezaji Loliondo, unaambiwa welcome to etisalat Arabic network kwa maana kwamba unatumia mtandao wa huko Arabuni na tunafahamu nchi yetu kwa hapa Tanzania kuna mitandao mitano ikiwepo Halotel, Zantel, Tigo pamoja na Airtel na Vodacom.
Je, ningependa kufahamu sheria zinasemaje kwa sababu hawa waliopo wanatambulika na kuna kiasi kinachopatikana kwa Serikali kutokana na mapato ya mitandao hii, sasa je, kwa huyu ambaye anakuambia welcome to etisalat Arabic network naomba ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, mtandao huu anaousema umesajiliwa na TCRA na unasimamiwa na TCRA na unalipa ada zote zinazotakiwa zilipwe chini ya TCRA, tofauti yake tu ni kwamba wao hawajapanua mtandao wao ukaenda na maeneo mengine. Kwa hiyo, wao wamechukua masafa na masafa hayo yanafanya kazi katika lile eneo na inaruhusiwa kisheria, ni mtandao ambao unasimamiwa na nchi yetu.
MHE. JOEL M. MAKANYAGA: Mheshimiwa Spika, asante nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza ni ombi namuomba sasa Mheshimiwa Waziri tuondoke naye mguu kwa mguu twende katika eneo hili la daraja ili tukalione kwa pamoja tuwe na uelewa wa pamoja wa namna gani nzuri zaidi ya kulishughulikia daraja lile, kwa sababu majibu haya maeneo fulani hayako sawa.
Swali la pili kwa kuwa daraja hili ni moja kati ya ahadi zilizotolewa na Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan wakati wa kampeni za mwaka 2015 pia lipo daraja kati ya Msanga na Kawawa. Je, Serikali haioni kwamba kunaumuhimu sasa wa kuendelea kutekeleza ahadi za viongozi wakati ule wa kampeni mwaka 2015 walishughulikie daraja hilo pia? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama hutajali Jumatatu baada ya Bunge saa saba mchana twende manaake hapa ni karibu, twende tukalione ili tuwe na uelewa wa pamoja kama ulivyopendekeza. (Makofi)
Katika swali la pili ni kweli kwamba dhamira yetu ni kuhakikisha ahadi zote za viongozi wetu wote kuanzia Awamu ya Nne na Awamu ya Tano tunazitekeleza kwa asilimia mia moja. Kwa hiyo nimuhakikishie kwamba ahadi hii ya daraja hili alilolitaja tutalishughulikia kwa kadri tutakavyopata uwezo kifedha.
MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, barabara ya Kaliua - Ulambo ambayo inakilometa 34 ilishafanyiwa upembuzi yakinifu, ishapata fedha, tender ilishafunguliwa na ilitakiwa ianze ujenzi mwezi wa pili mwaka huu. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri ni nini kinachozuia ujenzi wa barabara hii kuanza wakati sasa hivi ni mbovu sana na wananchi wa Kaliua wanateseka sana kwenda Urambo na maeneo mengine? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Magdalena Sakaya ni matatizo tu ya procurement ni kweli process zilianza mapema lakini bado hazijakamilika na nikuhakikishie kwamba barabara hii itajengwa muda sio mrefu kwa sababu tayari tumepata idhini ya kuanza ujenzi wa hiyo barabara.
MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa majibu haya yenye matumaini kwetu wananchi wa Mikoa hii ya Kusini, kwa sababu sasa tunaona Serikali inafanya jitihada kubwa sana katika kuharakisha maendeleo kwa Mikoa hii ya Kusini. Kwa hiyo, naishukuru sana Serikali yetu ya Chama cha Mapinduzi kwa kazi nzuri ambayo tunaisubiri kwa hamu kubwa sana.
Mheshimiwa Spika, napenda sasa kujua, baada ya ujenzi huu wa reli hii ya Mbamba Bay kukamilika, halafu itakapokuja katika eneo hili la Mtwara – Lindi.
Je, ujenzi huu wa reli ya Mtwara - Lindi utaishia Lindi tu au itakuwa Mtwara – Lindi – Dar es Salaam? Napenda kujua hilo, ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdallah kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuendeleza Mikoa ya Kusini katika masuala ya miundombinu.
Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kutupongeza na nimwahidi kwamba reli ambayo tunaiongelea hapa ni ile ambayo ilikuwepo zamani ambapo ilikuwa inatoka Mtwara – Lindi inapita Mnazi Mmoja na ilikuwa inaishia Liwale. Hoja ya kujenga reli kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam hatujawahi kufikiria. Tumesikia na tutaendelea kulitafakari hilo suala.
MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya kitaalam ambayo kwa namna moja au nyingine akina mama zangu wa Mkoa wa Rukwa na hususan wa Bonde la Tanganyika, bado hawajatendewa haki. Tunasema ya kwamba tunazuia magonjwa na vifo vya wamama na watoto, katika maeneo haya hatutakuwa tumezuia vifo vya akina mama na watoto, bali tutaendeleza vifo hivyo.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa Mheshimiwa Waziri anahusika vilevile na suala zima la mawasiliano, afahamu ya kwamba kata ya Kara haina mawasiliano ya barabara na wala haina mawasiliano ya simu. Huu utaalam wa TARURA watakuwa wamewapa umuhimu upi wa kuweza kuyafanyia kazi katika hizi barabara zetu za Ziwa Tanganyika na vilevile zinazoelekea kwenye barabaa za Ziwa Rukwa ziko katika hali hiyo hiyo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, napenda kupata majibu yaliyokuwa sahihi hasa kuhusu akina mama zangu wa Bonde la Tanganyika na Bonde la Rukwa, wanasaidiwa vipi juu ya hizi barabara na hao ndugu wa TARURA?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Silafu Jumbe Maufi kwa namna anavyoshirikiana na Wabunge wenzake katika kufuatilia masuala mbalimbali ya maendeleo ya watu wa Mkoa wa Rukwa na vilevile Mkoa wa Katavi. Sina uhakika kwa nini wanashirikiana wakati ni watu wa mikoa miwili tofauti, lakini nadhani ni kwa sababu maeneo yao yanafanana. Mara nyingi barabara anazoziongelea nyingine zinaunganisha mikoa yote hii miwili, kwa mfano, barabara zinazoenda kwenye Ziwa Rukwa zinapita katika mikoa hii yote miwili.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie, kama ambavyo tumeweka katika bajeti, barabara hizo tutazishughulikia kwa kadiri bajeti ilivyopangwa. Kwa mfano, barabara inayounganisha mikoa hiyo miwili, lakini vilevile na Mkoa wa Songwe anafahamu kwamba tumeanza kujenga daraja linalounganisha mikoa hiyo na tukishamaliza kujenga daraja, tutaanza sasa kuiangalia barabara yenyewe.
Mheshimiwa Spika, kubwa nimhakikishie kwamba Serikali inafahamu sana na wala haina nia hiyo anayoiongelea. Barabara hizo zitashughulikiwa na TARURA kwa kiwango na kwa kasi ile ile ambavyo angetegemea kwa kuzipandisha hadhi. Kwa sababu TARURA na TANROADS kwa sasa wana hadhi sawa na uwezo sawa.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, hata kwenye upande wa rasilimali fedha nako huko tunakuangalia, ili kuhakikisha taasisi hizo mbili zinatekeleza ahadi zetu na ahadi za viongozi katika maeneo hayo ambayo yameulizwa kwa kasi na kiwango kinachotakiwa.
MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza.
Kwanza napenda niipongeze sana Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi kwa kuanza kujenga barabara ya lami kuanzia Mbande kwenda Kongwa - Mpwapwa mpaka Kibakwe. Sasa swali langu ni hivi, je, hii barabara ikishafika Njia Panda ya Kongwa inaendelea moja kwa moja mpaka Mpwapwa? Hilo ndiyo swali langu. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, barabara ya Mbande –Kongwa – Mpwapwa mpaka Kibakwe ni barabara moja. Tumeianza na tutahakikisha tunaikamilisha kama ambavyo imeandikwa katika Kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015 hadi 2020.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba hatuishii Kongwa, tutaendelea na ujenzi wa hiyo barabara kama ambavyo kwenye Ilani tumeahidi.(Makofi)
Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii nisema kwamba wakati nikitembelea barabara hii, wananchi wa Kongwa walikusifu sana. Na mimi niombe nichukue fursa hii, pamoja na kwamba pengine siyo sahihi, lakini ni muhimu nizifikishe zile sifa za wananchi wa Kongwa ambao walikuwa hawategemei kama hiyo barabara tutaijenga. Na mimi niliwahakikishia hii barabara iko katika ilani na ahadi zote tulizoweka katika ilani tutazikamilisha pamoja na barabara hii ya kutoka Mbande – Kongwa – Mpwapwa hadi Kibakwe kwa Mheshimiwa Simbachawene.
MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri wa Ujenzi, napenda kuuliza swali moja la ziada kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni ukweli usiopingika kwamba barabara hii ni muhimu sana kiuchumi na ukizingatia kutoka Makao Makuu ya Wilaya ya Kilindi kwa maana ya Songe hadi Gairo ni kilometa hizo alizotaja. Barabara hii nyakati za mvua ina changamoto kubwa sana na ni juzi tu Mheshimiwa Naibu Waziri wa Afya alipokuwa anakuja Makao Makuu ya Wilaya, alikwama maeneo ya Chanungu pale kwa takribani saa mbili.
Swali langu linakuja, je, ni lini sasa Mheshimiwa Naibu Waziri atahakikisha kwamba watu wa TANROADS Mkoa wa Tanga wanasimamia kwa dhati matengenezo maeneo yafuatayo, kwa maana katika Bonde la Chanungu, Kijiji cha Mafulila pamoja na eneo la Kikunde, karibu kabisa na Kijiji cha Gairo hapa kuhakikisha kwamba barabara hii inapitika kwa msimu mzima wa mwaka? Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilieleza katika jibu la swali la msingi, barabara hii ni muhimu sana na Serikali inalifahamu hilo.
Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nilisema, tunatenga bajeti ya fedha na mwaka huu zimetengwa kuhakikisha kwamba barabara hii inapitika majira yote. Kwa sababu hiyo, nawaelekeza TANROADS Mkoa wa Tanga na TANROADS Mkoa wa Morogoro kuhakikisha barabara hii inapitika majira yote. (Makofi)
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa barabara hii ni muhimu kwa wananchi wa Majimbo ya Mtama, Newala Vijijini na Newala Mjini kwa ajili ya usafirishaji wa korosho, choroko na mihogo. Je, ni lini sasa Serikali itaanza maandalizi haya ya ujenzi kwa kiwango cha lami, yaani kwa kufanya feasibility study? Watuambie ni lini wataanza sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; naipongeza Serikali kwa kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami Barabara ya Mtwara – Nanyamba – Tandahimba – Newala na Masasi. Hata hivyo, barabara hii ni kilometa 210, lakini ujenzi ambao umeanza ni kilometa 50 tu, wananchi wa Nanyamba, Tandahimba na Mtwara wanataka kusikia Serikali ina kauli gani kuhusu kilometa 160 zilizobaki?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema, kwamba Serikali imeiwekea umuhimu sana barabara hii kwa sababu ya mazingira ya korosho na jinsi wanavyopata shida katika kusafirisha katika yale maeneo kutoka Newala mpaka kuja kuunga Mtama. Kwa hiyo nimhakikishie tu kwamba mara fedha zitakapopatikana suala la feasibility study and detailed design tutaanza kulishughulikia.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuendeleza ujenzi Barabara ya Mtwara – Newala hadi Masasi nimhakikishie tu, tumeanza na hizo kilometa 50 hatutasimama, tutaendelea mpaka barabara hii itakapokamilika. Alikuja ofisini Mheshimiwa Chikota tulimwambia kuhusu hilo. Nimpongeze sana kwa jinsi anavyoendelea kufuatiliam nilitegemea kwa kuwa tulishamaliza ofisini asingerudia kuuliza, lakini kwa sababu anajua umuhimu wa barabara hii bado amerudia kuuliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana na jibu ni hilo, kwamba tutaendelea kuijenga barabara hiyo, hatutasimama. Tutamaliza hizi kilometa 50, baada ya hapo tutaendelea na kilometa zilizobaki mpaka tumalize kilometa zote 200.
MHE. KAPT. MST. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa huruma yako kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Kwanza nataka niipongeze Serikali kwa kazi nzuri waliyofanya ya kujenga kwa kiwango cha lami katika maeneo korofi kama Mlima Kinombedo na Kitangari.
Mheshimiwa Naibu Spika, Lakini swali langu ni hili; kwa sababu ni sera ya Serikali kwamba mikoa iunganishwe kwa barabara za lami, barabara hii inaunganisha Mikoa ya Mtwara na Lindi, barabara hii inategemewa sana na wananchi wa Tandahimba, Newala na nchi ya Msumbiji wale wanaovuka. Nini kauli ya Serikali, tunajua kwamba sasa hivi inatafutwa fedha. Je, Serikali inaweza kutoa kauli hapa kwamba sasa kuanzia bajeti ijayo wataanza kutenga pesa za kufanya upembuzi yakinifu wakati fedha zinatafutwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa barabara hii inaunganisha Mikoa ya Mtwara na Lindi, kama ambavyo tuna barabara ya lami imeunganisha Mikoa ya Mtwara na Lindi kutokea Masasi na vilevile tumeunganisha barabara ya kutoka Mtwara yenyewe mpaka Lindi zote kwa barabara ya lami. Hii tunayoongelea ni kama barabara ya tatu na ina umuhimu wa pekee kutokana na mazingira, kama nilivyosema ya korosho.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba nia ya Serikali ya kuunganisha mikoa, iko katika maeneo ambayo hatuna barabara kabisa, lakini katika eneo hili kwa barabara hii nimhakikishie kwamba tutaendelea kuhakikisha inajengwa na mara tutakapopata fedha tutalishughulikia hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ingawa haipo katika ile sera yetu ya kuunganisha mikoa kwa sababu tunazo barabara mbili zinazounganisha mikoa hiyo miwili hii ni ya tatu, lakini nayo tutaitekeleza, sio kwamba hatutaitekeleza. Kubwa hasa linalovuta ni mazingira ya kiuchumi yaliyopo Newala, ndiyo yanayotuvuta, lazima hii barabara nayo ijengwe kwa lami. Kwa hiyo, mara tutakapopata fedha nikuhakikishie barabara tutaijenga.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri ambayo amenipatia kutokana na swali langu ambalo nimeliuliza.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu yake mazuri ambayo umenipatia, amesema hakuna taarifa zozote za kitabibu ambazo zimekuja kwake kuhusiana na madhara yanayotokana na utumiaji wa hizo simu kwa kusikiliza masikioni. Mimi ninao ushahidi wa kutosha, je, yuko tayari nimletee mtu au watu kuhusiana na suala hilo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kuna baadhi ya madereva wa vyombo vya moto, nikisema vyombo vya moto mnajua ni nini, wanapoendesha huwa wanasikiliza simu na kutokana na kusikiliza huko wengi wao wameweza kupata madhara na hatimaye wengi wanapoteza maisha na hasa vijana ambao ndio nguvukazi kubwa. Je, Serikali itaanza lini, kwa sababu mmesema mtatoa elimu, Serikali itaanza lini kutoa elimu hiyo ili kunusuru maisha ya vijana hawa? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa mimi sio Daktari nakubaliana na Mheshimiwa Mama yangu ampeleke huyo mtu kwa wenye dhamana na afya ili wakamchunguze na taarifa ya kitabibu itakapotufikia tutachukua hatua.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la Madereva naomba nianze sasa kwa kuchukua fursa hii kuwaasa Madereva wote wanaoendesha vyombo vya moto kutosikiliza simu wakiwa katika mwendo. Kama ni lazima asikilize simu asimamishe chombo cha moto halafu ndipo asikilize simu. Kusikiliza simu huku unaendesha ni kuhatarisha maisha yake lakini vilevile ni kuhatarisha maisha ya abiria ambao wakati mwingine wamewabeba. Tutaendelea kutoa elimu hii na kuendelea kutoa makatazo haya mara kwa mara kila tunapopata fursa ili kuhakikisha tunaokoa maisha ya watu wetu. (Makofi)
MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru. Napozungumzia ujenzi wa barabara ya Tanga – Pangani – Saadani, nazungumzia uchumi na maisha ya wananchi wangu wa Jimbo la Pangani.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa barabara hii ni ahadi ya muda mrefu na ujenzi wake umekuwa wa kusuasua yaani ahadi hii tangu mimi sijazaliwa mpaka sasa hivi nimekuwa Mbunge. Kwa kuwa Serikali imesahatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii ya Tanga – Pangani – Saadani, nini kinachokwamisha kuanza kwa ujenzi wa barabara hii na wananchi wangu kulipwa fidia? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, pamoja na nia njema ya Serikali kuhakikisha kwamba inajenga barabara ya Tanga – Pangani – Saadani, yapo maeneo korofi ambayo yanasababisha matatizo na usumbufu kwa wananchi wangu, mfano ni eneo la kutoka Mkwaja kwenda Mkaramo, Tundaua kwenda Kirare.
Je, Serikali ina mkakati gani wa muda mfupi na wa haraka ili kuhakikisha kwamba maeneo haya yanarekebishwa ili wananchi wangu wasipate tabu kwa muda huu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza katika swali la msingi, barabara hii imetengewa fedha shilingi milioni 4,435. Nimhakikishie tu hiyo ndiyo dalili njema, huo ndiyo ushahidi kwamba sasa Serikali imedhamiria kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa barabara hii ni pamoja na kuwalipa fidia wale wote wanaostahili fidia namna barabara hii itakavyopita.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Pangani na wengine ambao wanaguswa na barabara hii, dhamira ya Serikali ya kuijenga barabara hii iko palepale na tumeshaanza na tunatarajia muda si mrefu washirika wa maendeleo pamoja na African Development Bank kwa namna mazungumzo yanavyoendelea tutakuja kuongezewa fedha ili tukamilishe kazi hiyo kwa umakini unaotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kipande cha Mkaramo hadi Mkwaja, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Meneja wetu wa TANROADS Mkoa wa Tanga ataliangalia hili alete taarifa yake, gharama ya kurekebisha hiki kipande kidogo ili mawasiliano yawepo katika muda wote wa mwaka.
MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Rais wa Awamu ya Nne alifanya ziara yake katika Wilaya ya Nyang’hwale na kuahidi ujenzi wa barabara kutoka Kahama –Nyang’holongo – Bikwimba – Karumwa – Nyijundu – Busolwa – Ngoma - Busisi (Sengerema) kwa kiwango cha lami. Pia 2010 Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano na yeye alifanya ziara katika Wilaya hiyo ya Nyang’hwale na kuahidi ahadi hiyo hiyo ya ujenzi wa barabara hiyo hiyo. Je, kauli ya Serikali ni lini upembuzi yakinifu utaanza kwa ujenzi wa barabara hiyo ya lami kutoka Kahama - Karumwa - Busisi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia sana kuhusu ujenzi wa barabara hii na kwa sababu hiyo anafahamu mimi niliamua kupita barabara hii wakati nikitoka Mwanza na Geita na kweli nimeona umuhimu wa barabara hii walau sasa wataalam watakachokuwa wanaeleza nitakuwa nafahamu wanachosema ni nini. Nikuhakikishie, mara fedha zitakapopatikana kwa shughuli hii kazi hii itafanyika.
MHE. JEROME D. BWANAUSI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya Mtwara – Tandahimba – Newala – Masasi imeshaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kuanzia Mtwara. Je, Mheshimiwa Waziri anawathibitishia nini wananchi ambao walipaswa kulipwa fidia zao wanalipwa fidia haraka ili kupisha ujenzi huo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Mbunge, tulishajadiliana kuhusu suala hili na tulikubaliana kwamba tuangalie namna zile fedha zilizotengwa ni kiasi gani kitumike kwa ajili ya fidia na kiasi gani kiendelee kukamilisha ujenzi wa barabara ile. Nimuombe tu tuwasiliane ili hatimaye tukubaliane yeye na sisi. Ninachomhakikishia wote wanaostahili kulipwa fidia katika barabara ile watalipwa fidia, hakuna ambaye hatalipwa fidia. Hilo ndilo ninalokuhakikishia na nilikwambia hivyo kabla, nakushukuru sana.
MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nilitaka nipate ufafanuzi kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, kuna ujenzi wa barabara ambao unaendelea ya kutoka Sumbawanga – Stalike – Kigoma. Barabara ile kuna maeneo ambayo tayari ujenzi umeshapita na wananchi wanaoishi pembezoni mwa barabara ya kwenda Kigoma wameshahamishwa na baadhi ya wananchi tayari walishalipwa fidia lakini kuna wengine wamerukwa. Sasa Serikali inatumia utaratibu gani kuendelea kuwabagua kuwalipa baadhi ya wananchi fidia na wengine kuwaruka?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ujenzi wa barabara hii ya kutoka Sumbawanga - Stalike - Kigoma unaendelea na unafahamu kwamba kwa sasa tunajenga vile vipande viwili ambavyo wakandarasi wako kwenye eneo na lingine lile la kutoka Mpanda - Tanganyika unafahamu kwamba tuna fedha lakini napo tunatarajia mkandarasi hivi karibuni atakuwepo site na tunaendelea kutafuta fedha kukamilisha kabisa hadi Kigoma. Nikuombe tu kwa kawaida ulipaji wa fidia ni kutegemea na makadirio yaliyofanywa na valuers waliopita katika maeneo hayo. Mara nyingi inatokea maeneo mengine kuna watu ama wanarukwa na wakati mwingine wanarukwa kwa sababu wakati ule valuation inafanyika pengine yule mtu hakuwepo. Kwa hiyo, nikuombe tu suala hili tutaendelea kulishughulikia na tushirikiane kuhakikisha kwamba wale waliosahaulika na kama kweli wana haki wapate haki yao. Sisi muda wote tunasema mwenye haki ya kulipwa fidia ni lazima alipwe fidia na kwa vyovyote kama kuna watu ambao hawana haki ya kulipwa fidia hatutawalipa fidia.
MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri amesema kila kitu karibia kimeshakamilika, wananchi wa Handeni, Kiberashi, Kijungu, Kiteto na Nchemba wao wanataka kujua ni lini huu mradi utaanza? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, niombe tu kuwahakikishia wananchi wa maeneo hayo yote aliyoyataja kuanzia Handeni – Kiberashi – Kijungu – Kiteto – Nchemba - Kwamtoro hadi Singida ambako barabara hii itapita, Serikali imedhamiria kwa dhati kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Mwaka huu wa fedha ndiyo tunaanza kufanya maandalizi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami na tumetenga shilingi milioni 500 kama nilivyosema kwenye jibu langu la msingi. (Makofi)
MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niishukuru Serikali kwa ujenzi wa barabara ya lami inayotoka Nela kuelekea Kiwanja cha Ndege. Niulize swali dogo, kwa kiwango hicho hicho ni lini Serikali sasa itaanza mpango wa kuboresha barabara kwa kiwango cha njia nne kutoka mjini katikati kwa maana ya barabara ya Kenyatta kwenda Shinyanga kupitia Kata za Mkuyuni, Igogo, Mkolani, Nyegezi pamoja na Buhongwa ili na yenyewe iweze kufanana na yale mazingira yaliyopo? Nakushukuru. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Stanslaus Mabula na wananchi wa Mkoa wa Mwanza, ni kweli Jiji lile sasa lina hadhi kubwa na kwa kweli barabara zake nazo lazima tuhakikishe zinakuwa katika hadhi inayostahili Jiji lile. Nimepokea maombi yake, mimi nimechukulia hayo kama ni maombi, nitakwenda niyawasilishe kwa wataalam waanze kuangalia uwezekano wa kufikiria hilo ombi ambalo Mheshimiwa Stanslaus Mabula amelieleza.
MHE. MUSSA B. MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza niseme nashukuru kwa Serikali kutenga takribani shilingi bilioni nne kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Pangani. Je, ni lini kazi rasmi ya ujenzi wa barabara hiyo itaanza?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba kumpongeza sana huyu Mheshimiwa Mbarouk kwa sababu anashirikiana vizuri na Wabunge wenzake wa Tanga katika kuhakikisha maendeleo katika maeneo yao yanafanikiwa bila kujali itikadi. Nikupongeze sana kwa sababu hatimaye ni wananchi wanaotuleta humu ndani na hatimaye ni wananchi watakaotuondoa tusipoangalia interest za wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nikuhakikishie kama ambavyo nilijibu kwenye swali la msingi la Mheshimiwa Aweso ni kwamba mwaka huu wa fedha tumetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kuijenga barabara hii kwa kiwango cha lami. Ujenzi wa barabara una hatua, hii ndio hatua ya kwanza tunaianza mwaka huu wa fedha.
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba mwaka 2010 wananchi wa Jimbo la Nzega waliahidiwa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete kilometa 10 za lami ndani ya Mji wa Nzega. Mwaka 2014, Waziri wa Ujenzi ambaye ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania sasa aliwaahidi tena mbele ya Rais Kikwete ahadi hiyo hiyo. Mwaka 2015 Rais wa sasa, Rais John Pombe Magufuli aliwaahidi wananchi wa Jimbo la Nzega ujenzi wa Daraja la Nhobola na kilometa kumi za lami ndani ya Mji wa Nzega. Waziri wa TAMISEMI ndani ya Bunge hili mwaka 2016 akijibu swali langu la msingi alisema Serikali inashughulikia ujenzi wa Daraja la Nhobola katika bajeti ya 2016/2017 na Naibu Waziri Ngonyani katika Bunge lililopita aliahidi daraja hili litajengwa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka Naibu Waziri anijibu ni lini ahadi ya daraja hili itatimizwa katika Halmashauri ya Mji wa Nzega? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Hussein Bashe na wananchi wa Nzega kwamba ahadi zilizotolewa na viongozi mbalimbali ama ndani ya Bunge kwa kujibu maswali, wakati wa ziara ama wakati wa kampeni kuhusu ujenzi wa hayo maeneo mawili aliyoyasema, ujenzi wa kilometa kumi pamoja na daraja la Nhobola maana yake hii siyo mara kwanza kuliuliza hili suala, nikuahikikishie kama ambavyo tumekuhakikishia siku za nyuma kwamba ahadi hii itatekelezwa katika Serikali hii ya Awamu ya Tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilimhakikishia Mheshimiwa Mbunge hilo, na ni kweli tulisema kwamba tungeweka kwenye bajeti ya 2016/2017 na unafahamu kwamba bajeti ni mchakato, kikubwa nachokwambia ni kwamba Serikali itatekeleza ahadi hii ya viongozi mbalimbali pamoja na sisi ambao tumekuwa tukijibu maswali hapa kwa niaba ya Serikali.
MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri, lakini hii barabara ina miaka minne sasa tangu upembuzi yakinifu kukamilika. Naibu Waziri wa Ujenzi aliyepita aliwahi kuja kule akaongea na wananchi akasema kwamba ujenzi wa kiwango cha lami utaanza mara moja. Naibu Waziri naomba awaambie wananchi ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu upembuzi yakinifu ulishakamilika? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa kijiji cha Nyololo, Nziwi, Igowole, Mninga, Kibao, Lufuna na Mtwango waliwekewa alama ya ‘X’ kwenye nyumba zao na Serikali iliahidi kwamba alama ya ‘X’ ambayo ni ya kijani watapewa fidia. Wananchi wameshindwa kuendeleza nyumba za biashara kwa sababu zimewekewa alama ya ‘X’. Ni lini Serikali italipa fidia wananchi wale ambao wanasubiria mpaka leo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA
MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi barabara hii tutaanza kuijenga mara tutakapoanza kupata fedha. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Kigola kwamba Serikali itatumia kila aina ya nguvu zake kuhakikisha kwamba inapata fedha na kutekeleza ahadi au dhamira ambayo Naibu Waziri aliyepita aliionyesha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kwamba ni kweli wote waliowekewa alama ya ‘X’ za kijani watalipwa fidia na zitalipwa tutakapopata hizi fedha za ujenzi. Ulipaji wa fidia unaenda sambasamba na ujenzi wa barabara husika. Kwa hiyo, fedha hizi tunazozitafuta tunazitafuta zote, za ujenzi na za kulipa fidia.
MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naiomba Serikali itoe tamko hapa kuwaeleza wananchi wa Ilongelo, Mdida, Singa, Mtinko, Nkungi hadi Haydom kwa ahadi yao waliyoahidiwa na Rais wa Awamu ya Nne kwamba barabara ya lami itajengwa kutoka Singida kupita maeneo hayo hadi Haydom lakini sasa hivi hakuna kinachoendelea. Naomba Serikali iwaambie wananchi hao. Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Martha Mlata, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Singida na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa huo, kama ifuatavyo:- (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba juhudi zake za kufuatilia ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami hatimaye zitazaa matunda kwa sababu ahadi ambayo ilitolewa na Rais wa Awamu ya Nne tunayo na nimhakikishie kwamba ahadi hiyo tutaitekeleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaenda kutekeleza ahadi hizi awamu kwa awamu kama ambavyo nimekuwa nikimueleza yeye pamoja na Wabunge wenzake wanaofuatilia sana barabara hii, barabara hii inaunganisha Wabunge wengi sana.
MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Spika, huu ni mgogoro wa eneo ambalo limetathminiwa tangu mwaka 1997, huu ni mwaka 2017 miaka ishirini baadae.
Swali la kwanza, ni kwa nini Serikali inakataa kufanya tathmini upya katika maeneo haya hasa ukizingatia hali ya maisha ya sasa, kwamba hawa watu hata wakilipwa fidia leo hawawezi kufanya chochote kulingana na ugumu wa maisha ulivyo, kwa nini Serikali haipo tayari kufanya tathmini ya fidia ili walipwe kulingana na hali halisi ya maisha ya sasa?
Swali la pili, mgogoro huu pia umeathiri wananchi waliohamishwa kutoka Kipunguni ‘A’ kwenda Kipunguni ‘B’ Jimbo la Ukonga, Kipawa wakapelekwa Kata ya Buyuni Ukonga. Tunapozungumza hawa watu hawajalipwa fedha na walihamishwa kutoka Kipawa Kipunguni wakapelekwa Mbuyuni ambako hawakupewa tena maeneo. Sasa kuna mgogoro kati ya wananchi waliotoka Kipawa Kipunguni na wakazi wenyeji wa kule Buyuni.
Mheshimiwa Waziri yupo tayari baada ya Bunge hili au hata weekend yoyote tuambatane twende akawasikilize wananchi wenyewe awaone wanavyolalamika na kulia aone kama kuna sababu ya msingi sana ya kuchukua hatua mapema kwa kulipa fidia na kuondoa mgogoro uliopo katika eneo hilo. Nakushukuru sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, sasa tumedhamiria kulipa fidia yote katika mwaka huu wa fedha unaoanza mwezi Julai, kwa sababu tumedhamiria tukisema tuanze kufanya uthamini upya itatuchelewesha kwa sababu kazi ya fidia nayo ni kazi ya muda mrefu.
Mheshimiwa Spika, ninawaomba sana ndugu zangu tulimalize hili suala na kwa kweli kwa namna fidia tulivyolipa ni kama tumekuja kulipa mara tatu zaidi ya ile thamani iliyokadiriwa mwanzo kwa sababu ya hiyo interest na interest ni kwa mujibu wa sheria, sehemu zote mbili kulipa kwa kufuata interest ya kila mwaka ama kuamua kufanya fidia upya zote ni njia sahihi na zote zinafuata sheria za nchi yetu.
Ninakuomba tulipe fidia kwa kufuata interest ambayo imekadiriwa kuanzia mwaka huo walipofanyiwa tathmini, najua Serikali tutaingia hasara kwa sababu tutalipa zaidi kuliko kama tungeweza kufanya evaluation upya, lakini Serikali imekubali ili tusipoteze muda tena tulimalize hilo once and for all.
Pili, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge niko tayari baada ya kumaliza Bunge hili tupange twende tukalishughulikie suala hilo huko. (Makofi)
MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu aliyotoa kwa swali hili, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wavuvi wa Ziwa Tanganyika katika Manispaa ya Kigoma Ujiji maisha yao yote yanategemea uvuvi na vyombo vile kama mitumbwi inatumika kwa ajili ya uvuvi siyo kusafirisha abiria. Sasa ni lini Serikali itaondoa tozo hii ili kuondoa manyanyaso kwa wavuvi wa Kigoma Ujiji?
Swali la pili, sambamba na vyombo vya majini, bodaboda walioko Wilaya ya Kakonko na Wilaya zingine hapa nchini nao wanatozwa SUMATRA. SUMATRA ya bodaboda ni shilingi 22,000 sawa na kiti kimoja mwenye basi angelipa kwa kiti basi lenye abiria...
Mheshimiwa Mwenyekiti ndio nakuja. Basi lenye abiria 60 lingelipa shilingi 1,320,000. Ni lini sasa Serikali itaondoa tozo ya SUMATRA kwa bodaboda katika Wilaya ya Kakonko na Wilaya zingine nchini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali yote mawili kwa pamoja kwamba kimsingi hatutozi tozo kama ambavyo nilisema katika jibu la msingi, kinachotozwa na SUMATRA ni ada ya ukaguzi. SUMATRA wanahitajika kukagua iwe hizo meli au hizo boti zinazotumika kwenye uvuvi au pikipiki zote hizi zinatakiwa zikaguliwe ili tuwe na uhakika zinapotoa huduma au zinapofanya shughuli za uvuvi zipo salama. Sasa kazi hiyo inayofanywa na SUMATRA inahitaji kulipiwa ada kidogo.
MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika Ziwa Tanganyika kumekuwa na tatizo la wavuvi wengi kuvamiwa hasa kutoka nchi za jirani kama Congo, wale wavuvi wamekuwa wakipata shida sana. Je, Serikali imejipangaje kuhakikisha hawa wavuvi wanaotoka upande wa Kigoma nao angalau wanaridhika na rasilimali zao na kutokunyanyaswa na raia ambao wanatoka Congo na nchi jirani za Burundi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu mojawapo ya kufanya ukaguzi ni pamoja na kuvisajili vyombo hivyo ili vipate uraia kwa sababu mara nyingi vyombo hivi vinapotumika kwenye maji siyo rahisi kujua hapa umevuka mpaka au hapa uko ndani ya nchi yako. Kwa hiyo, usajili wa vyombo hivi ni muhimu sana na vikishasajiliwa vinatambulika kwamba hiki ni chombo cha Tanzania, hiki chombo cha Burundi, hiki chombo cha DRC tunapokutana katika maeneo yale ya Ziwa Tanganyika. Hiyo ndiyo silaha pekee ya kuiwezesha nchi yetu, kwanza wale maadui kutambua kwamba wanamgusa raia wa Tanzania na hivyo Serikali ya Tanzania inaweza kuwa tayari kumtetea mtu huyo. Kwa hiyo, njia mojawapo ya utetezi ni hiyo ya kuvisajili vyombo hivyo na tukiishavisajili tunafanya shughuli za doria mara kwa mara katika ziwa lile na nadhani Mheshimiwa Mbunge atakuwa amewahi kuona matokeo mazuri ya doria zinazofanywa katika Ziwa Tangayika katika kuhakikisha kwamba wavuvi wa Tanzania wanakuwa salama.
MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Tunayo sera katika nchi hii inayotoa kipaumbele kwa ujenzi wa kiwango cha lami kwa barabara zinazounganisha mikoa. Barabara hii tunayoongelea inaunganisha Mkoa wa Arusha na Simiyu. Kutokana na jiografia ya maeneo hayo, barabara hii ni muhimu sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri katika jibu lake anasema barabara hii itajengwa fedha zitakapopatikana. Sasa naomba swali, kutokana na sababu hizo za kisera na kijiografia, je, utafutaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii umefikia hatua gani? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutokana na mvua nyingi zilizonyesha katika maeneo ya barabara hii na hata ile inayounga Mji wa Karatu na Mbulu, zimeharibika sana na usafiri umekuwa wa shida na maeneo mengine barabara zimekatika. Kwa kuwa mvua sasa zinaelekea mwisho, ukarabati na ujenzi wa barabara hii utaanza lini?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu katika swali langu la msingi, suala la upembuzi yakinifu na usanifu wa kina haujakamilika, ndiyo kazi inayoendelea. Hatuwezi kuanza kutafuta fedha kabla hatujajua tunahitaji fedha kiasi gani katika ujenzi wa barabara hii. Tunaposema mara baada ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kukamilika ni wazi hatua inayofuata ni ya kujenga kwa kiwango cha lami na hapo ndiyo fedha tunaziongelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili itakumbukwa kwamba nilipojibu swali la nyongeza wiki iliyopita, nilitoa maelekezo kwa TANROADS pamoja na Mameneja wote wa Mikoa Tanzania nzima, kwamba sasa mvua zimekatika sehemu nyingi, tuelekeze nguvu katika kurudisha mawasiliano kwa barabara zile ambazo ziliathiriwa sana na mvua na kuleta changamoto ya mawasiliano. Hii ni pamoja na hii barabara anayoongelea Mheshimiwa Qambalo.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo la Karatu linalingana kabisa na tatizo la Korogwe Vijijini hasa kwenye barabara inayotokea Korogwe - Kwashemshi - Bumbuli - Soni imekatika na barabara hii iliamuliwa na Serikali kwamba itajengwa kwa kiwango cha lami na sasa hivi mawasiliano hakuna. Je, Serikali haioni kuna umuhimu wa kuitengeneza barabara hii haraka haraka ikarudisha mawasiliano ya dharura ambayo yalikuwa yameshakatika kwa muda mrefu?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyojibu awali, barabara zote ambazo zimekatika hivi sasa TANROADS pamoja na Mameneja wa Mikoa wa TANROADS wote Tanzania nzima waanze kuelekeza nguvu katika kurudisha mawasiliano kwa barabara zile zilizokatika ikiwa ni pamoja na barabara hii ya ndani ya Jimbo la Korogwe Vijijini kwa Mheshimiwa Ngonyani.
MHE. CECILIA. D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba niulize swali dogo la nyongeza. Katika Awamu ya Nne Mheshimiwa Rais aliyepita aliwahi kutoa ahadi ya kujenga kiasi cha kilometa takriban mbili hadi nne za lami katika Mji wa Karatu na hasa ukizingatia Mji wa Karatu ni mji wa kiutalii kwa sababu ni lango la kuelekea Ngorongoro. Je, ni lini ahadi hii itatekelezwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nisingependa sana kumaliza utamu wa hotuba ya Waziri wangu ambayo inakuja Jumanne wiki ijayo. Ningeomba Mheshimiwa Mbunge asubiri hotuba ya Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano ambayo itakuwa inajibu kiu yake hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu pekee ambacho naweza kumhakikishia ni kwamba ahadi zote zilizoko katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ambayo ndiyo Serikali hii inaitekeleza, ahadi zote zilizotolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati akiomba kura sehemu mbalimbali za nchi, ahadi zote zilizotolewa na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais na ahadi zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge, tutaziangalia na kuhakikisha kwamba zinatekelezwa kwa sababu zote kwa pamoja ni ahadi za Chama cha Mapinduzi.
MHE. JUMAA H. AWESO: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi hii nami nipate fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunapozungumzia barabara ya Tanga –Pangani - Saadani ndipo tunapozungumzia uchumi na siasa ya Pangani. Kwa kuwa katika majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri imeeleza kwamba African Bank wameonesha nia ya kutoa fedha kwa ajili ya barabara hii, je, Serikali imefikia wapi katika ufuatiliaji kuhakikisha kwamba African Bank wanatoa fedha hizi ili wananchi wa vijiji vya Choba, Pangani Mjini, Bweni, Mwela pamoja na Makorola na Sakura wanalipwa fidia ili wajue hatma ya maisha yao? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa malengo ya Serikali ni kuhakikisha kwamba inakusanya mapato na Wilaya ya Pangani ni miongoni mwa Wilaya ambazo zimejaliwa na Mwenyezi Mungu kuwa na Mbunga ya Saadani ambayo ni pekee Afrika mbuga ambayo imepakana na bahari. Kwa nini sasa Serikali isitenge fedha zake za ndani kuhakikisha kwamba inajenga barabara hii kwa haraka ili kukusanya mapato kupitia Mbuga hii ya Saadani?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jumaa Hamidu Aweso, Mbunge wa Pangani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Aweso anafahamu kwamba katika maeneo ya kwanza niliyotembelea ni Pangani na ilikuwa ni ziara ya kuifuatilia barabara hii pamoja na ile gati. Anafahamu baada ya hapo Waziri wangu naye alikwenda kwa ajili ya kufuatilia barabara hii pamoja na gati. Kwa hiyo, kwa namna wananchi wa Pangani walivyotupokea tukiwa na yeye, nina uhakika wanafahamu nia yetu ya kuhakikisha barabara hii inajengwa ni ya dhati na tutahakikisha fedha hizi ambazo wenzetu wa African Development Bank wanataka kutoa tutazifuatilia. Hivi ninavyoongea, kuna kikao Zambia kuhusiana na miradi ya African Development Bank. Kwa hiyo, namhakikishia tunafuatilia na tuna uhakika hatimaye tutazipata fedha hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika mradi huu hatuwaachii African Development Bank peke yake na sisi kama Serikali tutatenga fedha, moja kwa ajili ya masuala ya fidia lakini vilevile na masuala ya ujenzi. Kuna kiwango ambacho sisi kama nchi ni lazima tutenge. Kwa hiyo, hata Tanzania kama Serikali inawajibika katika kuhakikisha barabara hii inajengwa. Namhakikishia kama ambavyo tumemwonesha na wananchi wake wameona tutalifuatilia hili mpaka lifikie mwisho.
MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Tunajua kuna Halmashauri nyingi mpya na kutangaza Halmashauri mpya ina maana kama Halmashauri ilikuwa moja kuna mgawanyo wa vyanzo vya mapato na kadhalika. Hizi Halmashauri mpya nyingi vyanzo vyake vya mapato ni vidogo ikiwepo Halmashauri ya Mji wa Bunda na huko ambako wewe pia una interest nako barabara nyingi hazipitiki.
Nataka kujua Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha wanapeleka fedha za kutosha kwenye Halmashauri hizi mpya kupitia TANROADS Mikoa ili waweze kuhakikisha barabara zinapitika ikiweko na barabara yangu kutoka Rwahabu – Kinyabwiga na barabara ya kutoka Tairo – Gushingwamara? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Bunda Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimeeleza huko nyuma kwamba TANROADS Mkoa siyo wa TANROARD Taifa na wale Wahandisi wa Halmashauri wote sasa nchi nzima, wakae na kuhakikisha zile barabara ambazo zimekatika sasa tunazirudishia, hii ni pamoja na Mfuko wa Barabara ambako fedha zinatoka. Tunajua hizi barabara zingine ni za Halmashauri, zingine za Mkoa na zingine za Kitaifa lakini hii ni dharura, kwa hiyo wote tunashirikiana kwa pamoja ili tuweze kufungua mawasiliano pale ambapo yamekatika.
MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa ahadi za Rais, zimekuwa zikitolewa na moja ya Mji wetu wa Haydom, Mbulu na Dongobesh tumeahidiwa kujengwa barabara ya lami kwa kilometa tano. Je, lini Serikali inatekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge anafahamu na nimeshajibu hoja hiyo huko nyuma kama mara mbili hivi. Najua kwa nini anarudia, ni kutokana na umuhimu wa barabara hiyo, lile eneo halina lami kabisa kama ilivyo kwa Mbunge wa Loliondo. Niliwaambia kwamba ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano na Awamu ya Nne, ni lazima tutazitekeleza kwa sababu ndiyo wajibu tuliopewa katika Wizara yetu. Lini hasa? Naomba atuachie kwani siyo rahisi kutoa tarehe hapa Bungeni.
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja dongo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kilio changu cha zaidi ya miaka minne katika Bunge hili ni kuhusu barabara ya mchepuko kutoka Uyole - Songwe Airport kupitia Mbalizi kimekuwa kirefu na nimekuwa nikielezea ni kwa nini. Naishukuru Serikali kwenye bajeti yake Mheshimiwa Waziri amesema kwa kilometa 40 hizi upembuzi yakinifu utaanza. Nilitaka Mheshimiwa Waziri atoe tamko hapa upembuzi yakinifu huu utaanza lini kutokana na adha hii ya Wanambeya ambayo tumekuwa tukiipata kwa muda mrefu? Ahsante.
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa anafahamu kwamba hilo eneo analoliongelea ndilo eneo ambalo na mimi kila wakati napita nikienda kuwatembelea wakwe zangu. Nakuomba sana Mheshimiwa Dkt. Mwanjelwa, utuamini siyo kwa sababu hiyo, utuamini kwa sababu tumedhamiria na ndiyo dhamana yetu ya kutekeleza ahadi zote za Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne ambaye aliitolea ahadi barabara hii na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano ambaye naye aliitolea ahadi. Mimi nakuomba utuamini mwaka huu wa fedha unaokuja kuanzia Julai, 2016 mpaka Juni, 2017 kama huo upembuzi yakinifu hautafanyika, ninakuhakikishia dada yako atarudi.
MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Kwenye majibu ya Waziri anasema uandaaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya kumpata mkandarasi umekamilika. Labda tu nimpe taarifa Mheshimiwa Naibu Waziri hizi barabara kwa miaka ya fedha miwili mfululizo, 2014/2015, 2015/2016 zilitengewa fedha, zikatangazwa, tatizo ilikuwa fedha zilizotolewa na wakandarasi walichokuwa wakihitaji zilikuwa ni ndogo hivyo licha ya matangazo mara tatu hakuna kilichofanyika. Ukiangalia bajeti ya ujenzi zimetengwa kiasi kilekile cha fedha, barabara ya Mlimani City - Goba imetengewa shilingi bilioni 2.5, fedha ambazo mwaka jana ilishindikana, halikadhalika Tegeta Kibaoni - Goba. Nataka tu Naibu Waziri aniambie kiukweli tu kabisa, anawahakikishia vitu wananchi wa Jimbo la Kawe kwamba kwa bajeti hii iliyotengwa ujenzi utaanza kufanyika kwa mwaka huu wa fedha? Hilo ni la kwanza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili barabara muhimu sana ya New Bagamoyo Road, tunafahamu kwamba kwa miaka miwili iliyopita pia zilitengwa shilingi bilioni 88, zilitolewa na Wajapan through JICA. Madhumuni yalikuwa ni kujenga barabara ya Mwenge - Tegeta (double road), kujenga barabara ya Mwenge - Morocco (double roads), 88 billion akiwa Waziri wa Ujenzi ni Magufuli. Sasa leo kile kipande cha Mwenge - Morocco inaonekana kama kimekufa kuna ukarabati wa kienyeji unaendelea pale. Nilitaka Naibu Waziri aniambie zile shilingi bilioni 88 zimekwenda wapi na kile kinachoendelea pale Mwenge - Morocco ndiyo permanent ama ni temporary kukidhi mahitaji ya sasa ya barabara?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Halima Mdee, Mbunge wa Kawe kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Kawe na wananchi wake wote wa Kawe kwamba nilichokieleza katika jibu langu la msingi kuhusu kuanza kwa ujenzi wa hizi barabara mbili alizozitaja ni sahihi na tutajenga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili kwamba shilingi bilioni 88 zilikwenda wapi, nadhani anafahamu kwamba hiyo double road anayoongelea kuna sehemu yake imeshajengwa, kilichobaki ni kama anavyosema ni hiki kipande cha kati ya Mwenge - Morocco, upande ule mwingine umeshajengwa na hizo hela ndiko zilikoenda. Zimekwenda huko, zimetumika kujenga barabara hiyo na namhakikishia kazi inayoendelea sasa hivi pale, inaendelea kwa kiwango.
MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Tunashukuru sana kwa kazi ya barabara inayoendelea kutoka Dodoma - Kondoa - Babati ingawa inakwenda kwa kasi ya kusuasua. Tatizo moja kubwa wakati wa ujenzi kuna alama na maelekezo mbalimbali yanayotakiwa yawepo wakati wa ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Barabara hii hizi alama zinapungua maeneo mengine hakuna kabisa, kwa hiyo, unakuta watu wanapotea kilomita kadhaa halafu ndiyo urudi tena. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha wanawasimamia wakandarasi hawa waweke hizi alama ili kuondoa ajali na upotevu wa muda wa namna hii? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wote wa maeneo yote ya wakandarasi watatu wa kuanzia hapa Dodoma mpaka mwisho kabisa, wa CHICO, namuelekeza Regional Manager wa Dodoma asimamie kuhakikisha kwamba alama za barabarani zinazowaongoza wananchi wanaopita na magari yao ziwe zinawekwa na kusimamiwa muda wote zisiwe zinaondolewa ili wananchi wale wanaopita na magari yao wasipate shida ya kupoteapotea au kutumbukia kwenye mitaro. Namuelekeza atekeleze hilo na mimi mwenyewe nitafuatilia.
MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Swali la Mheshimiwa Mdee linafanana kabisa na suala ambalo liko katika Jimbo la Ndanda hasa katika maeneo ya Lukuledi - Chikunja - Nachingwea. Barabara ile siku za karibuni itajengwa kwa kiwango cha lami lakini tunaomba kufahamu fidia ya watu wale itafanyika kwa njia gani na ni umbali gani toka katikati ya barabara mpaka mwisho wa hifadhi ya barabara? Watu wale wanahitaji kufahamu jambo hili, ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumjibu Mheshimiwa Mbunge swali la nyongeza la kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema hiyo barabara hatujaanza kuijenga na tumeiwekea bajeti mwaka huu unaokuja wa 2016/2017. Nadhani unafahamu kwamba tunafuata ile Sheria ya 1967 ya Road Reserve ambayo sasa hivi tunaongelea kila upande kutokea katikati ya barabara wale wote ambao wako ndani ya mita 60 na wale ambao wako nje ya mita 60 wana haki tofauti. Wale ambao wako nje ya road reserve wana haki ya kulipwa fidia na wale ambao waliifuata barabara, nadhani kama sheria inavyosema na kama tulivyopitisha humu Bungeni hawana haki ya kulipwa fidia. Kwa hiyo, huo ndiyo umbali ambao umwekwa kisheria na ni sisi wenyewe tulipitisha humu ndani. Sisi kazi yetu ni kuisimamia tu, hapa kazi tu.
MHE. PHILIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na mimi niweze kuuliza swali lanyongeza. Kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Songwe naomba niiulize Serikali. Rais Awamu ya Nne, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alipokuja Songwe ambapo sasa ni Wilaya mpya aliahidi ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mbalizi - Mkwajuni - Makongorosi na tayari Serikali 2013 imeshafanya upembuzi yakinifu lakini baada ya hapo hakuna kinachoendelea. Je, Serikali ni lini itaanza sasa ujenzi wa lami wa barabara hiyo?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mulugo, Mbunge wa Songwe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, tuliwasiliana na Mheshimiwa Mulugo kuhusu barabara hii. Najua unaifuatilia sana, ni haki yako kuifuatilia na ni wajibu wako na sisi ni wajibu wetu kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kwa sababu barabara hii iko katika Ilani. Naomba tu kumhakikishia kwamba kama ambavyo tumeitaja katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi na kama ambavyo wewe unafuatilia utekelezwaji wa Ilani hiyo, tutatekeleza katika kipindi hiki cha miaka mitano.
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa katika umiliki wa Benki Kuu ya Tanzania, Zanzibar imeainishwa wazi kwamba inamiliki asilimia 12, ni vipi leo Waziri anatuambia Shirika hili la Jamhuri ya Muungano kati ya Zanzibar na Tanzania Bara au Tanganyika, haikuainishwa asilimia za umiliki wa Shirika hili. Je, siyo njia ile ile ya kuendelea kuinyonya Zanzibar na kuinyang‟anya haki zake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili…
SPIKA: Mheshimiwa kabla maswali yako hayajaendelea, una chanzo cha hizo asilimia zinazonyonywa, una reference yoyote au ni mawazo yako wewe?
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, amesema Naibu Waziri hapa kwamba Shirika linamilikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa asilimia 100, Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano, lazima tujue asilimia zinazomilikiwa na Serikali ya Zanzibar, tujue Wazanzibari haki zetu zi zipi, kama ilivyoainishwa katika Benki Kuu kwamba Zanzibar inamiliki Benki Kuu kwa asilimia 12.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo swali langu namwomba Waziri asikwepe hili suala, atuainishie hisa za Zanzibar ni kiasi gani katika ATCL kwa sababu hapo mwanzo Shirika hili lilikuwa ni ATC na wamiliki walikuwa ni hao hao Serikali, kwa hiyo imetoka Serikali halafu ikajibinafsishia Serikali… (Makofi)
SPIKA: Swali la pili!
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Mheshimiwa Spika, swali la pili, Naibu Waziri amesema kwamba deni la kutua kwa ndege ya ATCL, kwa muktadha ule ule wa kuinyang‟anya Zanzibar haki zake, ndege hii inatua katika viwanja vya ndege vya Zanzibar na hailipi kodi na hapa Mheshimiwa Naibu Waziri ametaja deni ambalo lipo, lakini bado anatuambia kwamba mpaka CAG alihakiki wakati wanajua kwamba walikuwa wanatua Zanzibar na hawalipi kodi…
SPIKA: Swali ni nini?
MHE. ALI SALIM KHAMIS: Ni lini deni hili litalipwa kwa Serikali ya Zanzibar haraka iwezekanavyo, kwa sababu deni hili ni la siku nyingi? Ahsante
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, siyo Serikali ya Tanganyika. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina uwezo wa kumiliki na ndiyo maana inamiliki hisa asilimia 100 za ATCL ambayo tuliibinafsisha huko nyuma na sasa tumeirudisha na tunataka kuirekebisha zaidi.
Mheshimiwa Spika, kuhusu deni, tumelitaja, haya madeni ni ya siku nyingi, ni ya Shirika ambalo lilishakufa, ATC, sasa tuko kwenye kampuni ATCL, lakini tunasema deni hili likishahakikiwa, litalipwa na ndege za ATCL zitakapoendelea kutua landing fee ya kila kiwanja italipwa.
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Tanzania tunayo makampuni binafsi mawili yanayotoa huduma za ndege kwa wasafiri hapa nchini, FastJet pamoja na Precision.
Mheshimiwa Spika, lakini ningependa kujua ni utaratibu gani wa gharama za nauli wanazotumia kupanga. Kwa sababu gharama ya kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza na kurudi inakaribia shilingi 800,000 vivyo hivyo gharama ya kutoka Dar es Salaam kwenda Mbeya inakaribia shilingi 800,000 sawasawa na nauli ya kutoka Dar es Salaam kwenda Dubai kwa ndege za Emirates. Nataka kujua, ni utaratibu gani unaotumika kupanga gharama za nauli kwa wasafiri hasa kwa Dar es Salaam, Mwanza pamoja na Mbeya, routes za ndani hizi ni nani anayepanga nauli hizi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, nauli za ndege kwa sasa zinapangwa na soko.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kinachotokea taasisi yetu ya SUMATRA huwa inafanya kazi ya kuangalia kama hizo nauli ambazo hupangwa na soko na pengine soko haliko sawasawa inafanya utaratibu wa kurekebisha.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kikubwa ambacho Serikali imeamua ni kufufua Shirika letu la ATCL liwe na ndege za kutosha ili tuweze kuondoa ukiritimba wa kampuni chache zinazotoa huduma za ndege kwa sasa, hatimaye bei ya soko iwe kweli bei ya soko. (Makofi)


SPIKA: Majibu ya nyongeza Mheshimiwa Waziri Profesa Mbarawa.
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri zinapangwa na soko lakini Mamlaka ya TCA (Tanzania Civil Aviation) ndiyo inasimamia jambo hili. Kwa kulijua hili, Serikali inafanya kila linalowezekana tuweze kufufua Shirika la Air Tanzania na ambapo sasa tuna utaratibu wa kununua ndege mbili, Q400, wakati wowote zitaweza kufika hapa Tanzania kuhakikisha kwamba bei hiyo sasa tunaisimamia ipasavyo.
MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Ndani ya Wilaya ya Serengeti hatujawahi kushuhudia mvua kubwa kama hizi zinazoendelea kunyesha. Barabara za halmashauri hususan madaraja yamesombwa na maji na ruzuku tunayopata kutoka Road Fund, haitoshi. Je, Wizara iko tayari kutusaidia kujenga madaraja yale ya halmashauri?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tumepokea ombi lake na kwa kweli kabla hatujaiandaa bajeti itakayokuja kusomwa na Waziri wangu hapa, bajeti hiyo imezingatia matatizo makubwa ya uharibifu wa madaraja na barabara sehemu mbalimbali nchini na hasa kwa kuzingatia viwango tulivyojiwekea vya mgawanyo wa fedha za Road Fund za 30% kwa 70%, siyo rahisi sana kwa upande wa Serikali za Vijiji kuhakikisha kwamba madaraja yote yaliyobomoka pamoja na barabara zote zilizokatika znarudishwa katika hali yake ya kawaida. Tusubiri majibu atakayoleta Mheshimiwa Waziri wakati bajeti itakaposomwa.
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya kuanzia Mombo - Soni – Lushoto ni nyembamba hata mvua zikinyesha magari hayapiti, kuna maporomoko ya mawe na magari ambayo yana mizigo mikubwa na upana mkubwa hayawezi kupita. Je, ni lini sasa Serikali itafanya upanuzi wa barabara ile?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa barabara ndiyo kichocheo cha uchumi wa nchi yetu, je, ni lini sasa barabara ya kuanzia Nyasa - Gale Magamba - Mlola itajengwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu upanuzi wa barabara ya Mombo pamoja na ujenzi kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Nyasa - Mlola, naomba Mheshimiwa Mbunge suala hili tukalitafakari ndani ya Wizara, tuwahusishe wataalam ili tuweze kuleta majibu ya kitaalam. Kwa sababu hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge alilete swali lake rasmi kama swali la msingi ili liweze kushughulikiwa kikamilifu.
MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mehshimiwa Naibu Spika, asante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Nashukuru kwa jibu la Mheshimiwa Waziri japokuwa majibu aliyonipa inaonesha kwamba ni mipango ya baadaye sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Gati la Bukondo kwa sasa hivi ninavyosema liko katika hali mbaya sana kiasi kwamba watu kuvuka kwenda kupanda meli inabidi waogelee kwanza ndipo waikute meli, kwa hiyo hali ni mbaya sana. Sasa ningependa kujua Mheshimiwa Waziri kwamba ni lini watakwenda kufanya ukarabati kwa sababu katika swali langu la msingi nimeuliza ukarabati wa hilo gati?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Ziwa Victoria katika Halmashauri ya Ziwa Victoria pamoja na Chato tunategemea sana usafiri wa majini hasa kwa MV Chato ambayo inatoka Chato - Bukundo kwenda mpaka Nkome. Na Nkome pia gati lake liko katika hali mbaya sana, ningependa kujua nini mkakati wa Serikali kuhakikisha ya kwamba inakarabati magati yote hayo ili wananchi waweze kupata usafiri wa kutosha?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba kwa namna anavyofuatilia maendeleo ya wananchi wake wa Bukwimba na wa Geita kwa ujumla. Amefika ofisini Dar es salaam na amefika vilevile Dodoma kumfuata Waziri wangu. Tumejadiliana hilo kwa kirefu na tulimuahidi kwamba tutawasiliana na wataalam wanaohusika na masuala haya ya gati ili hatimaye tuweke msukumo ili hili hitaji lake liweze kutekelezwa na wananchi wapate huduma wanayokusudia.
Mheshimiwa Naibu Spika, mimi naomba kurudia kile ambacho Waziri wangu alimuahidi, na mimi nilikuepo wakati anaahidiwa, na sisemi asije tena, aendelee kufuatilia, najua mambo mengi sana anafuatilia. Naomba uendelee kufuatilia, lakini kwa hili suburi tutakapokamilisha yale mawasiliano kati yetu na taasisi zinazohusika ili upate majibu sahihi na sisi tutafanya msukumo unaohitajika ili hatimaye kile kinachokusudiwa katika swali lako kiweze kukamilika.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa fursa. Kwa kuwa gati ya Bukondo linafanana sana na kesi iliyopo kwenye gati la Nyamisati na la Kilindoni kule Mafia.
Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Gati la Nyamisati, na lini Serikali itakamilisha ujenzi wa jengo la abiria kwa Gati la Kilindoni?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa taarifa yako, mimi naitwa Bwana Nyamisati. Kila ninapokutana na Mheshimiwa Dau, ndivyo anavyoniita Mr. Nyamisati, kwa sababu ameniambia nisipokamilisha hili ana namna, mimi sijui ana namna gani ya kuhakikisha sirudi hapa Bungeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia tena Mheshimiwa Dau na Waheshimiwa Wabunge wengine waliokuwa wanafuatilia masuala hayo mawili pamoja na ile meli ya kutoa huduma kati Mafia na Dar es Salaam, naomba kuwahakikishieni wote, kwamba kile ambacho tumewaambia tuliwaambia tukiwa na dhamira njema. Tutahakikisha Nyamisati ambayo tayari imeshapangiwa bajeti kwa mwaka huu na mmeshaipitisha inatekelezwa. Na vilevile Kilindoni, kwa sababu tunajua Kilindoni na Nyamisati ndiyo tunakamilisha mawasiliano kati ya Mafia na upande huu wa Bara. Naomba nikuhakikishie nisingependa kuahidi kwamba tutaanza dakika hii au tutamaliza dakika hii, mimi nikuhakikishie kazi hii tutaisimamia mpaka ikamilike.
MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la gati lililopo katika Wilaya ya Geita linafanana kabisa na tatizo la gati lililoko katika Wilaya ya Nyasa. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Gati ya Ngumbi katika Ziwa Nyasa?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, samahani nadhani ni Ndumbi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:Mheshimiwa Naibu Spika, gati linaloongelewa kama ambavyo mmeona linamuhusu sana Naibu Waziri anayehusika na masuala ya Elimu; na kwa kweli nilishuhudia mwenyewe wakati nilipoenda kukagua ile gati ambayo inatumika kupakia mkaa wa kutoka Ngaka kwamba tunahitaji kufanya mambo mazito pale ili ile biashara ambayo tayari imeshapanuka iweze kufanyika kikamilifu.
Mheshimiwa Naibu Spika, anafahamu Mheshimiwa Naibu Waziri na Mheshimiwa Jacqueline Msongozi kwamba katika bajeti hii ambayo nawashukuruni sana Waheshimiwa Wabunge; na mnisamehe jana nilipa matatizo kidogo kuona kwamba mmeniwezesha kuanza kujenga reli na miundombinu mingine nikatoa kwa sauti kubwa sana kuunga mkono bajeti, nanyi mkapitisha; pamoja na hii gati ambayo ipo ina bajeti tutaisimamia kuhakikisha inakamilika na kile tunachokusudia kitendeke pale Ndumbi kiweze kukamilika.
MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi naomba pia niulize swali; kwa kuwa Jimbo la Kigoma Kusini kwenye Ukanda wa Ziwa Tanganyika tunatumia meli ya Liemba, lakini kwa bahati mbaya gati karibu tano kwa muda mrefu sasa hazijajengwa na wala hazijakamilika.
Swali langu kwa Mheshimiwa Naibu Waziri; je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kuwapunguzia adha wananchi wanaotumia meli ya Liemba kwa kujenga Gati ya Kirando, Mgambo, Sibwesa na Gati ya Kalia? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hizi gati anazoziongelea katika mwambao wa Ziwa Tanganyika ni gati muhimu sana kwa sababu tuna vilevile tatizo la barabara. Kwa hiyo, usafiri wa ile meli ni muhimu sana kabla hatujafungua usafiri wa barabara.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulishawaagiza Tanzania Ports Authority kwamba katika mwaka huu wa fedha lazima ahadi ambazo viongozi wetu walizitoa kuanzia Serikali ya Awamu Nne na hii Serikali ya Awamu ya Tano, ni lazima tulitekeleze katika eneo hili kwa sababu mateso yaliyoko katika eneo hilo kwa kweli ni makubwa.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kuanzia mwaka huu wa fedha na katika miaka hii mitano ikikamilika ahadi zile tutakuwa tumezikamilisha, ikiwa ni pamoja na kuimarisha gati ya Kirado, Simbwesa na hizo zingine ambazo Mheshimiwa Mbungu amezitaja.
MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na ninamshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri sana, nina maswali mawili ya nyongeza:-
Kwa kuwa wananchi wa Mwanza na Ukelewe wamepata usumbufu zaidi ya miaka mitano kwa kukosa usafiri; na kwa kuwa ni sehemu muhimu sana kwa wavuvi; ni lini sasa Serikali itawapa usafiri wa dharura wananchi wale ili waone umuhimu wa Serikali yao inavyowasaidia?
Swali la pili, kwa kuwa tatizo la Ukerewe linalingana kabisa na Tanga, wananchi wa Tanga, Pemba, Unguja pamoja na Bagamoyo wanahitaji meli kama hiyo ili iwasaidie; je, Serikali ina mpango gani wa kuwahakikishia wananchi wa Ziwa, umetaja Ziwa Nyasa, umetaja Ziwa Victoria, umetaja Ziwa Tanganyika; lakini je, katika Bahari ya Hindi wananchi wa Tanga, Pemba, Unguja na Bagamoyo ni lini na wao watapata meli ili na wao waepukane na kile kimbunga cha kila siku kufariki kwenye meli? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru Mheshimiwa Stephen Ngonyani, Mbunge wa Korogwe Vijijini kwa namna ambavyo ameniamsha namna ya kufuatilia masuala ya wananchi wa Korogwe Vijijini na mimi vilevile Namtumbo, kwa kweli ninaomba Wabunge wengine wafuate nyayo zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu dharura nadhani Mheshimiwa anafahamu kwamba tuna usafiri ambao sasa hivi upo, isipokuwa hautoshelezi. Kwa masuala ya dharura usafiri unapatikana, nia yetu kubwa ni kuondokana na meli hizi chakavu, tuzitengeneze na tulete mpya. Kwa hiyo, masuala ya dharura siyo tatizo yamekuwa taken care off.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa upande wa swali la pili niliwahi kujibu swali kama hilo katika Bunge hili kwamba katika miaka ya 1980 - 1990 tuliamua kuingiza sekta binafsi katika shughuli za usafiri na kwa upande wa meli tulianzia na upande wa Bahari ya Hindi unafahamu kwamba kuna wasafirishaji binafsi wengi wanafanya shughuli hizo za usafiri. Kama ombi lako maana yake unataka Serikali iondoe hiyo sera ilete sera nyingine tutaliwasilisha Serikalini likajadiliwe tuone hasara na faida yake, kwa sasa naomba tuendelee kupata huduma za meli kutoka kwa wasafirishaji binafsi, TACOSHILI tulishaisimamisha miaka ya 1990.

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ngonyani hasa sehemu (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi tunavyoongea upo usafiri wa kudumu baina ya Dar es Salaam, Unguja na Pemba. Ipo meli ambayo inaitwa MV Mapinduzi II ambayo ni meli ya kisasa inayosafiri baina ya Unguja na Pemba na tutaongea na Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano huko Zanzibar kuhakikisha kwamba meli hii inasafiri kutoka Pemba kwenda Tanga kama ilivyokuwa hivyo zamani.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.
Kwa kuwa kulikuwa na ahadi ya Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kununua meli katika maziwa makuu matatu kwa maana ya Ziwa Tanganyika, Ziwa Victoria na Ziwa Nyasa, na katika bajeti hii ya Mawasiliano na Uchukuzi kuna ununuzi wa meli moja ya Ziwa Victoria, lakini hivi karibuni Waziri wa Katiba na Sheria alisikika akipongeza uundwaji wa meli mpya ya mizigo na abiria katika Ziwa Nyasa. Je, ni lini sasa meli mpya itapelekwa katika Ziwa Tanganyika ili tuachane na meli ya MV Liemba?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kiongozi wetu wa Serikali ya Awamu ya Nne alitoa ahadi ya kuleta meli mpya katika maziwa yote makuu matatu na ahadi hiyo ilirudiwa na Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pombe Joseph Magufuli kwamba atatekeleza ahadi hiyo ambayo mwanzo ilitolewa na Mheshimiwa Kikwete.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie hili tuliloliongelea katika jibu langu la swali la msingi ndiyo kuanza kutekeleza ahadi ya viongozi hawa wakuu, tunaanza na meli ya MV Victoria na unafahamu kwamba wakati kuna meli ndogo inatengenezwa kule Nyasa baada ya hapo tutafuatia na meli katika
Ziwa Tanganyika na hatimaye ahadi hizo za viongozi wakuu zitatekelezwa katika kipindi hiki cha miaka mitano tulichoahidi. Tuanze na hatua moja halafu tutasonga mbele.
MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza niishukuru Serikali kwa jitihada ambazo zimefanywa, barabara ile imeanza kujengwa, lakini Serikali iliahidi barabara hiyo inapojengwa ingejengwa sambamba na kilometa 60 za kutoka Uvinza kuja eneo la Mishamo ili ziweze kuendana na kasi ya Mheshimiwa Rais na vile vile Ilani ya Chama cha mapinduzi. Je, ni lini eneo hilo la kipande cha kilometa 60 kutoka Uvinza kuja Mishamo kitaanza kujengwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa ujenzi wa barabara ulishaanza, tayari Serikali imetathmini wale ambao wamefuatwa na barabara. Ni lini wale ambao walioathirika kwa kufuatwa na barabara wataanza kulipwa?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ni kweli tuliahidi kwamba tungejenga kuanzia Uvinza na vile vile kuanzia huku ambako tumeanzia na nimuahidi tu kwamba, madam tumeanza kupata hizi fedha kwa ajili ya upande mmoja, tumeona tuanze hii wakati tunaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ule upande wa pili. Nimhakikishie mara tu tutakapozipata fedha tutatekeleza ahadi tuliyoitoa.
Mheshimiwa Spika, kuhusu watu ambao wameifuata barabara; nimhakikishie tu Mheshimiwa Selemani Kakoso na wananchi husika kwamba watu wote walioifuata barabara hawatalipwa fidia na wale wote ambao barabara imewafuata watalipwa fidia; na taratibu za kuwatambua zilishafanyika na nimhakikishie kwamba hilo tutalitekeleza.
MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Spika ahsante kwa kunipa nafasi. Tatizo la ujenzi wa barabara lililopo Mpanda hadi Uvinza halina tofauti na tatizo la ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami lililopo Mbinga hadi Nyasa. Barabara ile iliahidiwa na Serikali kwamba itajengwa, napenda kujua ni lini sasa ujenzi ule utaanza? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Chikambo, kama ambavyo nilimweleza alipofika ofisini mbele ya Waziri wangu akifuatilia utekelezaji wa barabara hii akiongozana na Mheshimiwa Stella Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kwamba barabara hii inaanza kujengwa mwaka huu wa fedha.
Mheshimiwa Spika, nimhakikishie tu kwamba tumechelewa katika taratibu za Procurement kwa sababu nafahamu fedha zinazotarajiwa kujengea barabara hii zinatoka African Development Bank na kwamba wao wana utaratibu wao wa Procurement, ni lazima tuufuate. Tumechelewa lakini tutahakikisha mara tutakapokamilisha taratibu za Procurement barabara hiyo itaanza kujengwa.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu marefu ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati ambayo Naibu Waziri ameielezea inaonyesha kabisa nia ya muda mrefu na bado iko ndani, lakini tatizo hili huku nje bado linaendelea kuwa kubwa yaani watu bado wanaendelea kuathirika sana na bandari hizi bubu.
Swali la kwanza, je, Serikali haioni kwamba kwa kuendelea kuweka mikakati hiyo mirefu ndani wananchi wanaathirika na pengine sasa ingefika wakati ikachukua mkakati wa kudhibiti angalau wakati ile mikakati ya muda mrefu ikiwa inaendelea?
Swali la pili, bandari bubu hizi ziko katika vijiji vinavyozunguka mwambao wote wa pwani. Kwa kufanya mikutano na Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Bandari na watu wengine haoni kama anawatenga wale wanakijiji au wale ambao wanazitumia zile bandari na ambao wanaishi karibu na zile bandari na sasa pengine ingekuwa ni vizuri Serikali ikaenda kwa wahusika moja kwa moja kuzungumza nao ikaangalia? Kuna athari pia za mazingira uchafuzi wa mazingira ni mkubwa sana katika bandari hizi bubu. Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hii mikakati siyo mirefu sana nimejaribu tu kuisoma kwa kirefu lakini siyo mirefu sana. Ni mikakati mitatu tu maalum isipokuwa nimeileza kwa undani ndiyo maana inaonekana kama ni mikakati mirefu au ya muda mrefu.
Hata hivyo nadhani kitu cha kufahamu hapa ni kwamba bandari bubu inaanzishwa katika maeneo ambayo maeneo ya karibu tu kuna bandari ambayo ni rasmi. Kwa hiyo ni tabia ya watu kukimbia bandari rasmi na kujianzishia bandari bubu pembeni.
Kwa hiyo suala la kuahusisha walioanzisha bandari bubu tutalifanya katika maana ya kudhibiti, lakini siyo kwa maana ya kumshirika wakati yeye aliyeanzisha hiyo bandari bubu huku akijua kwamba anafanya makosa na anatafuta fedha kwa njia ambayo siyo sahihi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali la pili, ni kweli wanaohudumia hizo bandari bubu kama nilivyosema ni watu ambao wamejianzishia uratatibu wao nje ya utaratibu wa Serikali na tutafanya kila njia kuhakikisha kwamba tunawashirikisha katika kudhibiti lakini wakati wa kurasimisha hata vile vijiji tunavyowapa mamlaka wanawatumia wale ambao wana uzoefu wa kuendesha hizi bandari na hivyo tukifanya hivyo masuala ya usafi na mazingira wa bandari hizo yatashughulikiwa kikamilifu.
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kuwa matatizo yaliyopo kwenye mwambao wa Pwani hayana tofauti sana na matatizo yaliyoko kule Geita. Mkoa wa Geita unayo bandari bubu inaitwa Nungwe ambayo inatumiwa na Mgodi wa GGM kushusha shehena kubwa.
Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari baada ya kumaliza shughuli za Bunge afuatane na Wabunge wa Geita akalione lile eneo ili Serikali iweze kuipitisha kuwa bandari halali na watumiaji wengine waweze kupita pale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru kwa hiyo taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Musukuma kuhusu hiyo bandari bubu ya Nungwe na niko tayari kufuatana nae pamoja na Wabunge wengine wa Geita ili tukaiangalie hiyo kwa undani na tuone kama ipo katika orodha ambayo inashughulikiwa na viongozi wa Mikoa wa Ziwa Victoria katika kushughulikia suala la kudhibiti bandari bubu. (Makofi)
MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru taarifa ya Serikali inaeleza kwamba kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo kuna bandari bubu 32. Serikali muda wote imekuwa ikisema kwamba iko katika mikakati ya kuhakikisha kwamba bandari bubu hizi zinaweza kudhibitiwa, lakini tatizo linaloendelea la kuingia kwenye nyaya za umeme, matairi ya magari fake pamoja na maziwa ya watoto fake yanaendelea kuadhiri afya za binadamu na matukio mengine ya hapa na pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri anaweza akawaambia nini Watanzania juu ya mkakati wa ziada kuhakikisha kwamba matairi ya magari fake, nyaya za umeme, maziwa ya watoto fake yanadhibitiwa katika bandari bubu kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo? Naomba majibu ya haraka. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZINA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli katika bandari bubu zilizoko katika mwambao wa Pwani kuanzia Tanga hadi Bagamoyo na Kunduchi tuna kazi kubwa sana tunaifanya pale ya intelijensia pamoja na kazi ya kuhakikisha kwamba chochote kinachotoka pale hakingii katika soko kabla hakijakamatwa na Serikali. Nadhani unakumbuka ni mara nyingi tu tumeshika bidhaa mbalimbali zinazotoka upande wa pili kuingia upande huu mwingine wa nchi kwa maana inatoka Zanzibar kuingia huku kupitia hizi bandari bubu tumefanyakazi kubwa sana ya kuhakikisha kwamba zinasimamiwa haziathiri soko la nchi yetu na pili, hawaleti bidhaa ambazo ni fake kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafanya kazi hiyo na kwa kweli nichukue nafasi hii kuwapongeza sana vyombo vya ulinzi na usalama vya maeneo hayo kwa kazi kubwa wanayofanya.
MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo yanayoikumba Tanga pamoja na Bagamoyo ya bandari bubu yanafanana sana na mpaka kati ya Newala na Msumbiji ambapo wananchi wa Msumbiji wanakuja kutibiwa pale Newala. Ni lini sasa Wizara ya Ujenzi itakuja kufanya iwe rasmi badala ya kuwaachia polisi wale wananchi wanaokuja kutoka Msumbiji wanakimbizana nao. Kwa nini sasa Wizara ikaja na ikarasimisha na ikawa ni rasmi? Naomba jibu lako Mheshimiwa Waziri.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge ambaye ametoa taarifa hii. Alitupa taarifa mapema na nimpe tu taarifa kwamba suala hili tumeanza kulifanyia kazi kwa nguvu zote na matokeo yatakapokuwa tayari tutakuja tumfahamishe.
MHE. YOSEPHER F. KOMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, tatizo la ongezeko la bandari bubu katika Mkoa wa Tanga ni kutokana na uwezo mdogo wa Bandari ya Mkoa wa Tanga. Je, Waziri anatuambia nini kuhusu kuboresha Bandari ya Tanga kwa maana ya kina na miundombinu ili ongezeko hili la bandari bubu liweze kupungua? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna mradi ambao sasa hivi unaendelea, unatarajiwa kukamilika karibuni wa kuongeza kina katika lile eneo ambalo sasa hivi tunalitumia. Vilevile unafahamu kwamba tuna nia pia ya kuanzisha bandari kubwa zaidi ya Mwambani na kama sehemu ya mradi ule mkubwa wa kuhakikisha mizigo ya kutoka Uganda inapita katika reli ile ya kutoka Tanga – Musoma na Bandari ya Mwambani. Mipango hii ya Serikali ni thabiti na tumeanza kuitekeleza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hilo la kuongeza kina ni karibuni tu mwezi ujao kazi hiyo itakuwa imekamilika.
MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na ukweli kwamba wakandarasi 13,000 ni kidogo sana ukilinganisha na idadi ya Watanzania, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kigezo kimoja wapo kinachotumika kutoa kazi wanaangalia uzoefu wa kufanya kazi hiyo hiyo kwa yule anayeomba na kwa kuwa tumekuwa tukisisitiza kutoa ajira kwa vijana wetu, graduates wanapo-graduate tunawaambia waanzishe makampuni.
Swali la kwanza, je, vijana hawa wanapo-graduate kwenye vyuo vikuu wakaanzisha kampuni, wakiomba kazi wataweza kupata kazi kwa utaratibu huu? (Makofi)
Swali la pili, ukiangalia sifa mojawapo inayotumika kazi ni kwamba uwezo wa kifedha wa Mkandarasi lakini uzoefu unaonyesha uwezo wa kifedha wa wakandarasi wetu ni mdogo, wengine wanafutiwa hata kwa kushindwa kulipa ada na wengine wanashindwa hata ku-access mabenki kwa sababu ya utaratibu mbovu wa mabenki tulionao.
Je, Serikali haioni wakati umefika wa kuanzisha Benki ya Wakandarasi na kuboresha taratibu ili kuwezesha Wakandarasi wetu waweze kujikomboa na kupambana na umaskini. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa tunawahamasisha graduates wa fani ya uhandisi pamoja na ubunifu wa majenzi waanzishe kampuni na Serikali ina window maalum. Tumeweka window maalum ya kuhakikisha hawa watu tunawapa training, nadhani mfano utagundua pale Daraja la Mbutu tulifanya hivyo, hatukuzingatia uzoefu bali tulifanya pale ya majaribio, vilevile barabara ya kule Bunda kwenda Serengeti nayo vilevile kuna kilometa 50 tuliziweka kwa hawa Mbutu Joint Venture, tunaona kwamba kumbe hilo linawezekana na ndani yao ameshajitokeza mkandarasi mmoja sasa amepata uwezo mkubwa zaidi, Kampuni ya Mayanga ambayo sasa inajenga uwanja wa ndege wa Geita.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tutalifanya hilo na tutaendelea kulifanya lakini lazima tuzingatie sheria kwa sababu tukienda kinyume cha sheria tutakwenda kinyume na kile ambacho tulikubaliana humu Bungeni. Tutatafuta kila aina ya mwanya kujaribu suala hili za uzoefu lisitukwamishe sana kuhamasisha wakandarasi wa kizalendo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la uwezo wa kifedha ni suala la wakandarasi wenyewe na nadhani Mheshimiwa Balozi Buberwa Kamala unafahamu kwamba wakandarasi wana mpango huo wa kuanzisha benki yao na Serikali tutaendelea kuhamasisha mpango huo ukamilike.
MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa ni ukweli kwamba wakandarasi hapa nchini pamoja na wazabuni mbalimbali ambao wamekuwa wakitoa huduma kwa Serikali, wamekuwa wakiidai Serikali fedha nyingi na Serikali imekuwa hailipi kwa wakati.
Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba wakandarasi hao wakimaliza kazi na wazabuni wakimaliza huduma wanazotoa waweze kulipwa kwa wakati bila kuhatarisha kazi ambazo wanafanya?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wakati tunaingia tulirithi deni la shilingi trilioni 1.215 la makandarasi. Nichukue fursa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Rais pamoja na Wizara ya Fedha wametuwezesha kati ya hizo tumeshalipa shilingi bilioni zaidi ya 790, sasa hivi tumebakiza deni dogo sana katika yale madeni ya nyuma makubwa. Ingawa kwa kulipa madeni hayo, makandarasi wameendeleza kuongeza nguvu ya kuongeza kazi na wameongeza tena madeni mengine, lakini hayo madeni mengine walau sasa hivi yanashughulikiwa kwa namna ambayo hayazalishi tena idle time ambayo ni fedha ambazo tunalazimika kuzilipa wakati kazi haifanyiki kwa sababu tu ya kuchelewa kulipa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunashukuru kwamba sasa suala hilo halipo tena na kwa kweli tunaishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kazi hii, naomba mtupongeze na tutaendelea kukamilisha deni lililobakia ili hatimaye wakandarasi hawa wasiwe tena na madeni.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine miradi yote ya wakandarasi wazalendo tumekuwa tukilipa kikamilifu kabisa, huwa haichelewi kwa sababu tunajua uwezo wao ni mdogo na kwa kulipa mara deni linapo-accrue lengo ni kuwawezesha hawa wakandarasi wa kizalendo waweze kukua zaidi.
MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na tatizo kubwa sana katika nchi hii hasa katika utekelezaji wa miradi mikubwa, mkandarasi kupewa Mikoa zaidi ya miwili ama mitatu. Jambo hili limekuwa likiifanya miradi kuchukua muda mrefu, kwa mfano miradi ya REA.
Je, hatuna wakandarasi wa kutosha kwa mfano katika miradi ya REA ili kila mkoa uwe na mkandarasi mmoja kuokoa muda? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa miradi ya REA kuna sababu maalum ya kufanya hivyo na imetokana na uzoefu wa nyuma. Lakini kimsingi katika miradi ya masuala ya ujenzi iwe majengo, barabara au reli tunafuata qualificatio/sifa ambazo huyu mkandarasi amefuata na kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi inavyotuongoza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lazima tufuate hivyo, inawezekana kabisa mkandarasi wa Mkoa mwingine akapata kazi mkoa mwingine ni kitu cha kawaida kabisa kama ilivyo mkandarasi wa nje ya nchi anapopata ndani ya nchi yetu ni kitu cha kawaida kinachoangaliwa ni sifa ya mkandarasi aliyeomba hiyo kazi na kwa mujibu wa taratibu za zabuni.
MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa swali la msingi limeongelea vigezo na kwa kuwa Rais aliyepo madarakani wakati akiwa Waziri wa Ujenzi, aliweka kigezo kwamba kazi zinapotangazwa walau kampuni moja ya mwanamke ipate kazi ili kuwainua wanawake na jambo hilo kwa sasa linafifia.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kutuambia ana mkakati gani wa kutoa walau waraka TANROADS na Halmashauri kwamba wanawake wanapopata kazi wame- qualify wapewe kazi hizo ili kuwainua wanawake? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninamshukuru sana Mheshimiwa Munde kwa swali hili la nyongeza kwa sababu ananipa fursa ya kuelezea nini Wizara yangu inafanya katika kuwainua wakandarasi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu tuna mradi maalum wa kuhakikisha kwamba wakandarasi wanawake kwanza wanapatikana kwa sababu ili wapatikane kwanza lazima wajisajili na Bodi ya Usajili wa Wahandisi. Ndani ya Bodi ya Usajili wa Wahandisi tuna programu maalum kwa ajili ya wanawake tu na nashukuru wenzetu wa NORAD wanatusaidia fedha kwa ajili ya kuhakikisha hawa wahandisi wanawake wanasajiliwa, wakishasajiliwa wanaanzisha kampuni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kawaida kampuni hizo zinazoanzishwa na akina mama tunazilea kama nilivyosema, kila wanapopata kazi na wamekuwa wakipata kazi mbalimbali ingawa kwa sasa bado ni kampuni chache zilizoanzishwa kupitia njia hiyo na tutaendelea kuzihamasisha nyingi zaidi zianzishwe. Kila wanapopata kazi wanalipwa malipo yao yote wanayostahili ili waweze kuendelea kukua, huwa hatuwaachii deni la aina yoyote katika wakandarasi hawa wazalendo na hasa hawa wakandarasi akina mama. (Makofi)
MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Napenda kuikumbusha Serikali kwamba kwa barabara hii kama sehemu ya trunk road ya Tabora- Mbeya michakato ya upembuzi, upembuzi yakinifu, usanifu, usanifu wa kina ilianza mwaka 1974 sasa ni miaka 43 haijakamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba nipate majibu kwenye maswali mawili, la kwanza, je, Serikali iko tayari sasa kujibu swali langu la msingi lini itaijenga barabara hii kwa kiwango cha lami? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, Serikali kama haitaji muda maalumu, je, haiashirii kwamba haiko tayari kuiweka kwenye mpango maalum barabara hii kuijenga kwa kiwango cha lami? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Joseph George Kakunda kwamba Serikali mara itakapokamilisha upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na uandaaji wa makabrasha ya zabuni zoezi la kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii litafanyika kwa sababu wakati huo tutakuwa tumejua gharama za ujenzi wa barabara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mheshimiwa George Kakunda tuwe wakweli na tuitendee haki sekta yetu ya ujenzi. Barabara hii ni sehemu ya barabara kuanzia Mbeya hadi Singida na tumekuwa tukifanya kipande baada ya kipande. Hivi tunavyoongea unafahamu kwamba sehemu kubwa imeshajengwa sasa tumebakiza kilometa hizi 172 tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie kwamba Serikali iko makini inafuatilia ujenzi wa barabara hii na siyo kwamba hatuko tayari kama alivyosema kwenye swali lake la pili. Kama tungekosa kuwa tayari hatungekuwa tumeanza ujenzi katika maeneo hayo ambayo tumeshayajenga.
MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Swali langu la nyongeza linaendana na swali la msingi namba 347.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara ya Kiguza kupitia Hoyoyo hadi Mvuti inaunganisha Mkoa wa Dar es Salaam na Mkoa wa Pwani na katika kipindi kilichopita mvua nyingi sana zimenyeesha na hatimaye kusababisha kukatika kwa daraja na kukata mawasiliano baina ya mikoa hii miwili.
Sasa Serikali inatusaidiaje juu ya barabara hii tukiamini kwamba ujenzi wa barabara hii utasaidia sana kupeleka malighafi au rasilimali nyingi tukiamini kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ni Serikali ya viwanda na kutakuwa na vigae vitakavyosafirishwa kupitia barabara hii. Naiomba Serikali itupe majibu kwamba inatusaidiaje juu ya suala hili kuhakikisha ile barabara inakamilika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete kwa kulikumbusha hili kwa sababu lilishaletwa kupitia Mkoa wa Pwani kupitia Mbunge wa Mkuranga pamoja na Wabunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Pwani na sasa kwa sababu mama naye ameshindilia hapa, mimi naomba tu nichukue fursa hii kuiagiza TANROADS kwanza ikaangalie hali ya hii barabara kwa sasa hasa pale ambapo pamekatika. Halafu tujadiliane na wenye barabara ambao ni Halmashauri juu ya tufanye nini kwa pamoja kati ya Serikali Kuu na Halmashauri kurekebisha barabara hii kwa sababu kwanza barabara hii ni muhimu sana kwani ni kiungo muhimu kati ya malighafi inayotoka nje ya Pwani na inayoingia Mkuranga. Kwa hiyo, ni barabara mojawapo ya kuwezesha viwanda kukua.
MHE. HALIMA ALI MOHAMMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, je, atakubali kwamba moja ya sababu zinazopelekea vifo vya mama wajawazito na watoto wachanga wanapokwenda hospitali ni barabara na miundombinu mibovu.
Je, Naibu Waziri anasema nini katika suala hili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa miundombinu ya barabara na mingineyo ili kuhakikisha kwamba watu wetu wanakuwa na ustawi unaotakiwa ikiwa ni pamoja na hayo ambayo Mheshimiwa Mbunge Halima ameyaeleza na ndiyo maana miaka yote tumekuwa tukitenga bajeti kubwa zaidi katika eneo la miundombinu na hasa miundombinu ya barabara pamoja na miundombinu ya barabara vijijini na tukaunda kabisa TANROADS ishughulikie miundombinu ya barabara ili kuhakikisha kwamba changamoto ambazo wananchi wetu wanazipata za kiafya na changamoto zingine za kusafirisha mazao zinatatulika.
MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Kwa kuwa umuhimu wa barabara ya kutoka Matai kwenda Kasesha ni sawa sawa kabisa na umuhimu wa barabara iliyouliziwa katika swali la msingi, na kwa kuwa Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana alipata nafasi ya kwenda kutembelea barabara hii na akaahidi kwamba mkandarasi angetafutwa ili ujenzi ufanyike, na kwa kuwa pesa ilitengwa katika bajeti iliyopita, jumla ya shilingi bilioni 11 na ujenzi huo haukufanyika, je, Serikali iko tayari kuwahakikishia wananchi wa Kalambo kwamba ujenzi wa barabara hii utafanyika hivi karibuni?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mheshimiwa Waziri wangu Profesa Makame Mnyaa Mbarawa alitembelea katika eneo hili, na kwa namna alivyoona mazingira ya barabara hii ya Matai hadi Kasesha alitoa ahadi kwamba hii barabara ataishughulikia. Nimhakikishie Mheshimiwa Kandege na wananchi wa Kalambo hasa wale wanaoguswa na barabara hii ya Matai hadi Kasesha, kwamba Wizara yetu tumeshapokea maelekezo ya Mheshimiwa Waziri na kazi inafanyika ili kuhakikisha ahadi au dhamira ya Mheshimiwa Waziri inakamilika kwa kuhakikisha kwamba tunafuata taratibu za kupata fedha za kujengea barabara hii ili ipitike vizuri zaidi.
MHE. LEONIDAS T. GAMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niulize swali moja la nyongeza kwa vile barabara inayounganisha Tanzania na Msumbiji iliyopo Mkoani Ruvuma, inatokea katika Jimbo la Songea Mjini katika Kijiji cha Likofusi kuelekea Mkenda katika Jimbo la Peramiho, barabara hii ni muhimu sana kwa uchumi wa Mkoa wa Ruvuma na kwa uchumi wa nchi kwa ujumla. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, ni lini Serikali itafanya utaratibu wa upembuzi yakinifu wa barabara ile na kuijenga kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Likofusi hadi Mkenda ambayo inatuunganisha na wenzetu wa Msumbiji tumeishaifanyia kazi kuanzia siku nyingi. Kwanza tumeishajenga daraja ambalo tayari limekamilika, lakini vilevile wenzetu wa viwanda na biashara wamejenga soko, nalo limekamilika, halafu na sisi vilevile tumefanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii na umekamilika; hivi tunavyoongea tupo katika hatua ya kutafuta fedha kuhakikisha barabara hii inajengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa umuhimu wa barabara hii na hasa tukifahamu kwamba barabara hii inaunganisha Jimbo la Songea Mjini na Jimbo la Peramiho ambalo Mheshimiwa Jenista Mhagama ndiye anayeliongoza, na tunaona jinsi Mheshimiwa Jenista Mhagama anavyotuhangaikia humu ndani kitaifa, Mheshimiwa Waziri wangu alitoa ahadi kwamba atahakikisha barabara hii inatekelezwa kwa maana ya hatua hii ya ujenzi mapema iwezekanavyo, na si zaidi ya miaka miwili kuanzia sasa tutakuwa tumeanza kujenga.
MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Serikali kwa ujumla kwa hatua hii ambayo imefikiwa; na nikiri kwamba ni kweli fedha hizo zimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi. Hata hivyo nilikuwa na maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa fedha zilizotengwa bilioni kumi na mbili ni kidogo sana ukichukulia wastani wa ujenzi wa kilomita moja haipungua bilioni moja, kwa hiyo fedha zinazotakiwa ni karibu bilioni
140. Kwa kuwa fedha zilizotengwa bilioni kumi na mbili ni kidogo sana na kwa maana hiyo inaweza ikachukua muda mrefu sana barabara hii kuanza kujengwa, je, Serikali haioni kwamba kwa mazingira tuliyonayo hivi sasa, ambapo tayari tuna makontena 277 yenye zaidi ya thamani ya bilioni 600 ambayo ni dhahiri kwamba kuna ukwepaji kodi mkubwa; je, Serikali haiwezi ikaona namna ya kutumia kiasi cha fedha kitakachopatikana kutokana na kodi hiyo iliyokwepwa ili kuweza kupata fedha za kujenga mara moja barabara hii kwa mwaka huu wa fedha tunaouanza? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali pili; wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, pamoja na wenzao wa Wilaya ya Nyang’hwale walishiriki kwenye mkutano wa kampeni wa Mheshimiwa Makamu wa Rais pale Kalumwa, na Mheshimiwa Makamu wa Rais aliahidi kwamba barabara ya kutoka Kalumwa kwenda Mwanza iko kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami na Serikali iko katika mpango wa kuangalia uwezekano wa kuunganisha kutoka Kalumwa kuja hadi Kahama. Je, Serikali imefikia wapi, katika utaratibu huo au mpango huo, au utekelezaji wa hiyo ahadi ya Makamu wa Rais wa kujenga barabara ya kutoka Kahama kupita Busangi, Chela, Nyang’holongo, Kalumwa hadi Mwanza kwa kiwango cha lami? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninaomba Mheshimiwa Ezekiel Magolyo Maige akumbuke kwamba suala la ukwepaji halina uhusiano sana na ukiangalia jibu la msingi nililolitoa. Maadam Kampuni ya Acacia Mining imeonesha nia ya kushirikiana na Serikali tuna uhakika tutaendelea kuwafuatilia ili tuongeze fedha za ujenzi wa barabara hii ili iweze kukamilika kwa haraka zaidi. Suala hili la kitaifa la ukwepaji naomba tumuachie Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli alikamilishe kwa namna alivyolianzisha baada ya hapo ndipo tuweze kuliongelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa swali la pili ni kweli Mheshimiwa Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan alitoa hiyo ahadi na mimi naomba tu nikuhakikishie kwamba ahadi hii aliyoitoa mbele yako Mheshimiwa Mbunge ukiwawakilisha watu wako wa Msalala sisi Serikali tumeambiwa na tunaanza kuingiza katika mchakato wa kuitekeleza ahadi hiyo kama ambavyo tunapanga kutekeleza ahadi zote ambazo viongozi wetu wakuu wamekuwa wakizitoa sehemu mbalimbali za nchi. (Makofi)
MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mwaka 2010 na mwaka 2015 kwa maana ya uchaguzi wa mwisho wa kumchagua Rais Jakaya Mrisho Kikwete, wananchi wa Jimbo la Nzega waliahidiwa na Mheshimiwa Rais Kikwete, vilevile ahadi hiyo imekuja kutolewa na Mheshimiwa Rais Magufuli, ya ujenzi wa daraja la Nhobola. Mwaka wa jana Desemba Mheshimiwa Rais aliwahakikishia wananchi wa Jimbo la Nzega kuwa daraja hilo linajengwa kwa commitment iliyotolewa na Wiziri wa Ujenzi. Je, ni lini daraja hilo litajengwa. Nashukuru.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa anayoyaongelea Mheshimiwa Hussein Bashe kuhusu Daraja hili Nhobola na amekuwa akiliulizia mara kwa mara, na sisi tumekuwa tukimjibu mara kwa mara kwamba tunashughulikia kutekeleza ahadi hii ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, lakini ni ahadi ambayo ilirudiwa na Mheshimiwa Rais wa sasa, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Pamoja nisingependa kusema lini, lakini nimhakikishie kabla ya miaka hii haijaisha daraja hili tutakuwa tumelitekeleza kama ambavyo viongozi wetu waliahidi. (Makofi)
MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nilikuwa naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri wa Ujenzi, barabara ya Isandula iliyoko Magu kwenda Jojilo mpaka Hungumalwa iko kwenye mpango wa kujengwa kwa lami na usanifu ulishafanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, ziko barabara mbili, barabara ya Kamanga kwenda Sengerema kwa Mheshimiwa Ngeleja, Mkoani Mwanza; tungependa kujua barabara hizi ambazo ni ahadi ya muda mrefu, ni lini hasa ujenzi wa lami katika barabara hizo utafanyika? Ningependa Mheshimiwa Waziri anipe majibu kwa sababu tumekuwa tukiuliza barabara hizi mara nyingi humu Bungeni, ni lini, ni lini barabara hizi zitajengwa kwa kiwango cha lami?(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa heshima niliyonayo kwa Mheshimiwa Ndassa sikutarajia aulize swali, hasa maswali haya ambayo amekuwa akiyarudia na muda wote nimekuwa nikimwambia kwamba mzee wangu ambaye umekaa humu kwa muda mrefu, usihangaike kuendelea kuuliza maswali haya.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali hii iko makini, na nikuhakikishie tumeanza mipango na wataalam wamesikia uliyouliza hapa, kama ambavyo walisikia kule nyuma ulipouliza, wanaendelea kulifanyia kazi, na tutakapopata jibu sahihi tutakuletea. Kikubwa tunachokuahidi ni kwamba barabara hizi ni ahadi za viongozi wetu, na ni lazima ahadi hizi zikamilike kama zilivyo ahadi zingine zote za barabara sehemu mbalimbali za nchi. (Makofi)
MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa barabara kuu ya kuingia Wilayani Lushoto ni moja tu, na hizi mvua zinazoendelea kunyesha mawe na vifusi vinaziba barabara.
Je, Serikali haioni sasa imefikia wakati wa kutujengea barabara mbadala ya kutoka Dochi-Ngulwi hadi Mombo ambayo ni kilomita 16 tu ili kunusuru maisha na mali za wananchi wa Wilaya ya Lushoto? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shekilindi, Mbunge wa Lushoto, swali ambalo nikiri kwamba ni mara ya pili kuniuliza, ingawa ni mara ya kwanza kuniuliza ndani ya Bunge. Naomba nikiri kwamba analifuatilia sana suala hili na niwapongeze sana wananchi wa Lushoto kwa kumpa dhamana hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nafasi hii niliyopewa ninamuelekeza Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tanga, naye alete maoni yake kuhusu ombi hili, kama ambavyo nilimuelekeza awali ili hatimaye tulifanyie maamuzi na tuone namna ya kulitekeleza.
MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Barabara ya Tanga – Mabukweni – Malamba – Bombo Mtoni – Mlalo mpaka Same ni barabara inayounganisha Mkoa wa Tanga na Mkoa wa Kilimanjaro; na kwa mara kadhaa barabara hii imeahidiwa kujengwa kwa kiwango cha lami. Ni lini sasa barabara hii itajengwa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuombe Mheshimiwa Dunstan Kitandula tukutane ofisini na wataalam ili tuweze kujadili kwa kina suala hili ili huu usumbufu usiendelee, tuwe na lugha moja kati yetu sisi wataalam katika kuhakikisha kwamba wananchi na hasa wa Jimbo la Mkinga wanaotumia barabara hii waondokane na adha ambazo wanazipata kwa sasa. Nikuombe tukutane na wataalam, Katibu Mkuu pamoja na watu wa TANROADS tulijadili kwa kina na hatimaye tupate majibu sahihi na majibu ambayo wote tutakuwa tunaelewa kwa pamoja na hatimaye tuchukue hatua.
MHE. DKT. FAUSTINE E. NGUGULILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na mimi kunipa fursa ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika dhana ya kupunguza matumizi ya fedha na kubana matumizi katika Serikali, Serikali imekuwa inanunua magari kutoka kwa ma-dealers, magari haya huwa yanakuja na warrants ya kilometa laki moja au miaka mitatu matengenezo yanakuwa bure, lakini warrant hii Serikali imekuwa haitumii na badala yake imepeleka magari kwenye garage za watu binafsi na kutumia gharama kubwa sana.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwanza inasimamia hizi warrant, ikiwa ni pamoja na kuwa na mpango wa kununua magari kutoka kwa manufactures?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumepokea ushauri wake tutaenda kuufanyia kazi na baadae tutamletea majibu stahiki.
MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ambayo hayako makini, majibu ambayo hayaendi sambamba na swali langu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mantiki ya swali langu lililenga usalama wa wasafiri pale na mali zao. Kwa kipindi kirefu sasa wananchi wanaotumia bandari mbili hizi, kila bahari inapopata michafuko kidogo wamekuwa wakifa kwa wingi sana pale.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha inathibiti vifo vya watanzania katika bandari mbili hizi ambao mara kwa mara wanapotea wao na mali zao?
Swali langu la pili la nyongeza, inaoneka Serikali haikufanya utafiti wa kutosha. Swali langu halilengi ubora wa bandari, linalenga usalama wa raia wetu pale kati ya bandari mbili hizi.
Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari kufuatana na mimi kuona mazingira halisi ya usafiri pale katika bandari ya Mkokotoni kwa sababu TRA wako pale wanakusanya kodi?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama amenisikiliza vizuri katika jibu langu la msingi hatua ambazo tunazichukua ya kwanza ilikuwa inajibu swali lake kikamilifu. Hatua zilizofuata tumeongeza mipango mingine tunayoifanya, kwamba SUMATRA hufanya ukaguzi kila mwaka, vilevile hufanya kaguzi za kushtukiza kuhakikisha kwamba vyombo hivi vinavyoelea majini vinakuwa na usalama wa abiria na mizigo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili niko tayari, tutapanga tukubaliane siku ya kwenda na tukaelee majini kati ya Bandari ya Tanga na Mkokotoni ili tukubaliane haya ambayo Serikali inayasema na Mheshimiwa Mbunge anadhani kwamba hatuyajibu kikamilifu. (Makofi)
MHE. ALLY SALEH ALLY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nakubaliana na Waziri kwamba suala la kwanza ni ukaguzi, lakini kwa kweli suala la ujuzi na utaalam ndio muhimu sana katika uokozi.
Je, Serikali imejiandaa vipi katika suala hili la kutayarisha umma na wataalam wa kuweza kufanya uokozi kuliko kungojea kutibu badala ya kuzuia?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tumeongelea umuhimu wa shughuli za SUMATRA na hapa tuliongelea masuala ya ukaguzi, lakini unafahamu kwamba SUMATRA wana kituo kikubwa Dar es Salaam ambacho kinashughulika na masuala ya uokozi katika bahari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo hiki vilevile kina vituo vidogo Mwanza na wanawasiliana na vituo vingine vya sehemu mbalimbali katika Bahari ya Hindi ili kuhakikisha kwamba kama kunatokea tatizo lolote vyombo hivi ambavyo vinashirikiana hata na wenzetu wa Marine Service kuhakikisha kwamba usalama wa baharini unakamilika. Mheshimiwa Ally Saleh unafahamu kuna tower kubwa sana kwenye Bandari ya Dar es Salaam kazi yake kubwa ni kuhakikisha kwamba ina-coordinate shughuli zote za uokozi na wataalam tunao.
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo ya usafiri wa baharini ya Bumbwini yanafanana sana na matatizo ya usafiri baina ya Bandari ya Kilindoni, Mafia na Bandari ya Nyamisati, Kibiti. Wananchi wa Mafia wamekuwa wakisafiri katika maboti ya mbao ambayo si salama na hayana bima.
Je, ni lini Serikali itainunulia Wilaya ya Mafia boti ya kisasa kuondokana na tatizo la usafiri baina ya Bandari ya Nyamisati na Kilindoni ili kuepusha maafa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbaraka Dau anafahamu kwamba Serikali ina mikakati maalum ya kuhakikisha inatatua tatizo la usafiri Mafia. Tukianzia kuhakikisha kwamba magati yanayotumika ni ya kisasa na yako salama. Kwa vyovyote vile magati haya yakishakaa salama tutavutia wawekezaji wa kuleta meli na kama ikitokea kwamba hakutakuwa na meli zitakazofika, pamoja na kuimarisha gati kwa maana ya gati iliyoko tayari pale Mafia, lakini vilevile hili linalopokea upande wa Bara, tukishakamilisha hizo kama hatutakuwa na wawekezaji binafsi watakaovutika kutoa huduma za usafiri nikuhakikishie Mheshimiwa Dau tutakaa pamoja tuangalie tufanyeje pamoja na Serikali tuone namna ya kutatua usafiri wa eneo hili la Mafia. (Makofi
MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na napenda kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu, vilevile napenda kuipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa azma yake ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Vilevile kwenye issue ya magari naipongeza Serikali kwa kuamua kununua kwa wingi (bulk procurement) ambayo inapunguza bei, na vilevile kununua kwa mtengenezaji badala ya kununua kwa mtu wa katakati ambayo nayo inapunguza bei, nawapongeza.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza.
Sasa hivi Serikali pamoja na kwamba haina sera ya magari, magari mengi yanayotumika ya Serikali ni Toyota, bei ya Toyota Land Cruiser VX bila ushuru ni shilingi milioni 220. Bei ya Toyota Land Cruiser Prado ambazo kwa sifa zote zinafanana ni shilingi milioni 120 bila kodi. Kwa hiyo, Serikali ikiamua kununua magari 20 ya VX na ikaacha ikanunua Prado ita-save karibu shilingi bilioni mbili ambayo inaweza ikatatua matatizo ya maji katika Mji wa Chunya, Mji wa Makongorosi hata Mkwajuni kwa Wilaya mpya ya Songwe. Je, Serikali inasemaje kuhusu kuachana na VX na kutumia Prado kwama inavyotumia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar?(Makofi)
Swali la pili, kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Serikali inafuata Sheria ya Udhibiti na Ununuzi wa Mali ya Umma Sura ya 410. Sheria hiyo inasisisitiza ununuzi wa mali ya umma ni kwa tender na disposal ya mali ya umma ni kwa tender. Zamani ilikuwa magari ya Serikali yale yanayochakaa yanakusanywa...

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa. Magari yanakusanywa MT Depot na yanauzwa kwa tender. Siku hizi hawafanyi isipokuwa Idara ya Usalama wa Taifa ndio inauza kwa tender.
Serikali inasemaje kuhusu Viongozi wa Serikali ambao wanajiuzia magari yaliyochakaa badala ya kuuza kwa tender? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema masuala ya ununuzi wa magari ni masuala yanayosimamiwa na sheria vilevile Wizara ya Fedha ndio inayosimamia GPSA. Kwa maana hiyo, nachukua maoni yake tutaenda tukayafanyie kazi kwa kushirikisha GPSA pamoja na Wizara ya Fedha pamoja na Idara Kuu ya Utumishi ili hatimaye tupate majibu sahihi na hatimae nitakueletea hayo majibu sahihi Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa. (Makofi)

WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nataka kuongezea kidogo hasa kuhusu magari baina ya Toyota Prado na Landcruiser VX.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati unanunua kitu unaagalia mahitaji yako, kwanza unangalia bei, unaangalia safety, unaangalia mantainance cost, vitu vyote hivi unaviangalia baada ya hapo ndio unaweza kupima. Ukinunua gari baina ya Zanzibar na Bara ni mazingira tofauti, magari yanayotumika Zanzibar yanatumika kwa siku pengine kilometa 30, hapa mtu anasafiri takribani kilometa 200, 300 mpaka 500 mpaka 1,000 kwa siku, 1,200 naambiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa vile ukinunua gari inabidi vitu vyote hivi uviangalie, sio uangalie price tu. Uangalie comfort, uangalie safety, uangalie mainatainance cost na vitu vingine vyote. Ahsante. (Makofi)
MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninasimama kwa niaba ya Mheshimiwa Oran ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Mbeya Vijijini. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Mbeya kijiografia imekaa vibaya sana, vituo vingi zaidi hasa katika Kata ya Igoma Tarafa ya Tembela pamoja na kule Isangati hakuna vituo vya polisi kabisa na jiografia yake kama nilivyosema ni mbaya. Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne alikuwa ameahidi kabisa kwamba vituo hivi vijengwe, lakini mpaka leo hakuna. Nataka kujua majibu ya Serikali ni lini itajenga Vituo vya Polisi huko Igoma pamoja na Ilembo katika Tarafa ya Isangati?
Swali la pili, Wabunge wa Mkoa wa Mbeya wote kwa pamoja tunachanga kwa juhudi zetu na wananchi kujenga Kituo cha Polisi cha Mbalizi. Ninataka kujua ni nini mkakati wa Serikali katika kuongeza nguvu katika kituo hiki cha Polisi Mbalizi? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Mary Mwanjelwa, Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo hili na Wabunge wa Mkoa wa Mbeya ambao wameshirikiana katika kujenga kituo hiki. Binafsi nilikwenda pale kuzindua ujenzi huo na sisi vilevile tulichangia, lakini niwapongeze pia, wananchi wa Mbeya kwa kuweza kujitolea kukijenga kituo hiki katika hatua ambayo sehemu iliyofikia ni karibu asilimia 50 ya ujenzi imekamilika na huu ni mfano wa kuigwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, changamoto ambayo ameizungumza katika maeneo mengine ya Isangati, nitoe changamoto kwamba wakiendelea na jitihada kama hizi itasaidia kuharakisha ukamilishaji wa ujenzi wa vituo katika maeneo mengine kwa haraka ili kusaidia kukamilisha dhamira njema ya Serikali ya kukamilisha ujenzi wa vituo 65 nchi nzima vyenye mapungufu katika maeneo mbalimbali nchini.
MHE. PETER J. SERUKAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri, Mfuko wa Mawasiliano Vijijini haujapewa pesa za kutosha lakini Waziri anasema vijiji hivi vimeingia kwenye Mfuko wa Mawasiliano Vijijini. Je, nataka kujua kama kweli umeingia kazi hii inaaza lini?
Swali la pili, nilidhani Serikali ingekuja na jibu la kusema badala ya kutegemea bajeti ya Serikali, waongee na makampuni ya simu kama Halotel, Airtel, Vodacom na Tigo ili waweze kupeleka mawasiliano kwenye vijiji hivyo kwasababu mbele ya Kazinga kuna Mwamgongo ambayo Mwamgongo tayari kuna mawasiliano na huwezi kufika Mwamgongo lazima uanzie Kazinga. Kwa hiyo, nilitarajia Serikali badala ya kutegemea bajeti peke yake, nikuombe uende ukaongee na makampuni ya simu ili yaweze kupeleka huduma hiyo kwenye vijiji hivyo.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kama nilivyoeleza katika jibu la swali la msingi kwamba ujenzi wa Miundombinu kwa ajili ya mawasiliano utafanyika mara baada ya fedha za mradi zitakapopatikana na vijiji hivi vyote tulivyovitaja tayari vimo katika mpango, vimeingia katika mpango vinasubiri upatikanaji wa fedha. Lini? Ni mara fedha zitakapopatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ombi lake la pili, labda tu nimfahamishe kwamba, mfuko wa mawasiliano kwa wote unatekeleza miradi mbalimbali kupitia Kampuni hizo hizo za Halotel, Tigo, Airtel na Vodacom, wao hawatekelezi wenyewe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, makampuni haya yanapata ugumu wa kupeleka mawasiliano katika vijiji kwa sababu wanasema havina faida na hivyo Serikali inatoa ruzuku kupitia mfuko huu wa mawasiliano kwa wote na fedha zinapopatikana tunatangaza tender na makampuni hayo ndiyo yanayoomba hizo zabuni kupeleka mawasiliano hayo katika maeneo hayo.
Kwa hiyo, nadhani ni kweli Halotel, Airtel, Voda hata kama tutakwenda kuwashawishi siyo rahisi wao kukubali kwasababu wanajua hakuna faida katika maeneo hayo na hivyo inahitajika ruzuku ya Serikali na ruzuku ya Serikali tunaitoa kupitia mfuko huu wa Mawasiliano kwa Wote.
MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pia nashukuru kwa majibu sahihi ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri kazungumza hapa kwamba Bandari hiyo ya Mtwara ndiyo itakuwa chanzo cha ufunguzi wa kitu tunachoita Mtwara Corridor, maendeleo ya Kusini mwa Tanzania na Afrika kwa ujumla. Naomba kujua kwamba hili gati linajengwa hivi sasa ni gati moja tu. Mkakati wa Serikali ukoje kuhakikisha kwamba wanamaliza ujenzi wa magati matatu yaliyobaki ili yaweze kukamilika magati manne?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba kujua kwa kuwa Bandari ya Dar es Salaam hivi sasa ina msongamano mkubwa sana na Mtwara sasa hivi hii bandari inajengwa. Je, Serikali ipo tayari hivi sasa kuhakikisha kwamba inapunguza cargo on transit kutoka Bandari ya Dar es Salaam waweze kuruhusu Bandari ya Mtwara ili kuweza kuondoa msongamano hivi sasa? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, magati matatu yaliyobakia mpango wake wa kujengwa kwanza tunataka kushirikisha Sekta Binafsi lakini vile vile kwanza tunataka tuhakikishe kwamba gati hili moja na kwa namna mizigo ilivyo kwa sasa tunadhani kwamba linatosha kwa muda mfupi na wa kati. Baada ya hapo ikishafunguliwa ile reli ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay kwa vyovyote vile gati hizi nne lazima ziongezeke. Kwa hiyo, nimshukuru kwa swali hilo, nimepata fursa ya kutoa ufafanuzi zaidi.
Mheshimiwa Spika, kuhusu Bandari ya Mtwara kutumika kama mbadala wa Bandari ya Dar es Salaam; sababu mojawapo ya kupanua hii gati kama tulivyosema hili gati ni la urefu wa mita 350, ni kubwa sana ili liweze kuruhusu meli kubwa sana ziweze kutia nanga Mtwara. Moja kati ya sababu ni hiyo, kwamba meli zingine kubwa ziweze kutua Mtwara badala ya muda wote kufikiria kuingia Dar es Salaam.
MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniruhusu kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, je, baada ya majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ni lini hasa Mkandarasi ataanza kujenga minara hiyo ya mawasiliano ya simu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, baada ya majibu hayo mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, je, wananchi waishio Tarafa ya Mwambao mpakani mwa nchi ya Malawi, ni lini wataanza kupata mawasiliano hayo.(Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo tumeongea naye siku za nyuma, taratibu za manunuzi siyo rahisi sana mimi kama Waziri kuja hapa kutamka, kwa sababu siwezi kuziingilia taratibu za manunuzi. Taarifa niliyopewa kutoka kwenye Bodi imeniambia kwamba Mkandarasi amepatikana kwa ajili ya hayo maeneo manne lakini hawawezi kunitajia mpaka taratibu zile zingine zikamilike za kum-engage huyo Mkandarasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Mbunge, asubiri taratibu hizo za manunuzi zitakapokamilika ambazo nina uhakika hazitachukua muda mrefu kabla ya mwezi huu kuisha tutamjulisha lini kwa sababu inakuwa ndani ya mkataba wa yule Mkandarasi, anatakiwa aanze lini na akamilishe lini, tutakapokamilisha hilo tutamjulisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile suala la lini mawasiliano yataanza kupatikana nalo litajibiwa vizuri zaidi baada ya ule mkataba kati ya UCSAF na Mkandarasi kukamilika. (Makofi)
MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Katika Jimbo la Babati Mjini, vijiji vya Himiti, Chemchem na Imbilili havina mawasiliano na hili nililiandikia kwa Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii akanijibu kwamba, anafanya maongezi na watu wa Halotel mwezi wa Tatu mwaka huu minara ya Halotel ingeweza kusimikwa katika vijiji hivyo, lakini hadi sasa hakuna kazi yoyote inayoendelea. Naomba nipate kauli ya Serikali, ni lini mazungumzo yao na watu wa Halotel yatakamilika ili wananchi wa Jimbo la Babati Mjini katika vijiji nilivyovitaja vipate mawasiliano?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mazungumzo yanaendelea na eneo ambalo tuna tatizo nalo ni eneo la kodi ya vifaa ambavyo vinatakiwa vitumike katika kukamilisha haya mawasiliano. Namwomba tu maadam bajeti wameipitisha jana na kuna baadhi ya kodi tumeziondoa, nina uhakika mazungumzo haya yatakamilika karibuni na yakishakamilika tutakuja kumwambia watu wa Halotel watakamilisha lini.
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali moja, Mkoa wa Kigoma Wilaya Tano zinapakana na nchi jirani ya Burundi na kati ya Wilaya hizo zina vijiji ambavyo vimepakana kabisa na nchi ya Burundi na wakati mwingine zinapata mawasiliano kutoka Burundi. Je, ni lini Serikali itakaa na makampuni ili kuweza kupeleka minara katika vijiji vya Kalalangabo, Mtanga na Kiziga? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Vijiji hivyo vya Kalalangabo namshukuru amenitajia hapa nimhakikishie tu kwamba katika zabuni itakayofuata ambayo mkazo mkubwa ni katika maeneo ya mpakani na zabuni inayofuata ni ya mwezi wa 10, vijiji hivyo tutavifikiria. (Makofi)
MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mawasiliano mbali na simu, mawasiliano ni pamoja na barabara, wananchi wa Jimbo la Geita Vijijini Sengerema na Buchosa kumekuwa na kero kubwa sana ya TANROAD Mkoa wa Mwanza kuweka mzani kwenye barabara ya vumbi, kitendo ambacho hatukioni kwenye mikoa mingine yoyote Tanzania. Je, Waziri yuko tayari kutoa kauli ili mizani inayowekwa kwenye barabara ya vumbi ambayo ni mbaya iondolewe mara moja?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Mbunge na ninachoweza kumwahidi ni kwamba nitalifanyia kazi suala hilo, nikalione hilo eneo, nijue kwa nini wameweka mizani katika barabara ya aina hiyo, baada ya hapo tutachukua hatua. (Makofi)
MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Katika Jimbo la Nanyamba kuna kata saba ambazo hakuna mawasiliano ya uhakika ya simu, Kata ya Hinju, Nitekela, Nyundo, Mnima, Kitaya, Kilomba na Kianga. Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea mawasiliano ya simu wananchi wa maeneo hayo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianzia na Kijiji cha mwisho hicho cha Kianga, Kitaya, Nitekela na kadhalika nimhakikishie kwamba majina haya tumeyapata na bahati nzuri hayo maeneo anayoyaongelea nayo yapo katika maeneo ya mpakani ni maeneo ambayo yanatakiwa yapewe kipaumbele. Kwa hiyo, nimwahidi katika kwamba katika Zabuni inayofuata ya kuhakikisha vijiji vyote Tanzania tunapeleka mawasiliano, zabuni ya mwezi wa Kumi vijiji hivyo navyo tutavifikiria. (Makofi)
MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Matatizo yaliyopo katika Jimbo la Ludewa yanafanana sana na matatizo ambayo yapo katika Jimbo la Mikumi. Matatizo ya mtandao wa mawasiliano ya simu, hasa kwenye Kata za Vidunda, Muhenda, Uleling’ombe pamoja na Tindiga lakini pia Kata ya Masanze hasa kwenye vijiji vya Munisagala na Chabima. Je, ni lini Serikali italeta mawasiliano haya ya simu katika kata hizi za Jimbo la Mikumi. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilidhani jibu alilolitoa jana la kuikataa bajeti ni kwamba labda mwaka huu wote tusiangalie katika eneo la Mikumi. Nitaomba tukutane, pengine ile aliikataa siyo kutoka rohoni.
MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali. Nipende tu kumuuliza swali Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Igunga Kata ya Mwashiku, Vijiji vya Matinje, Buchenjegele, Ngulu na maeneo ya karibu pale, ni maeneo ambayo wanachimba dhahabu na wafanyabiashara wadogo wadogo wanapata tabu sana katika kufanya transactions za fedha kupitia hii mitandao ya simu, biashara hii za dhahabu wanaifanya kwa muda mrefu sasa. Je, ni lini sasa Serikali itawapelekea mawasiliano ya simu kama mitandao ya Vodacom, Airtel, na mitandao mingineyo ili kuwarahisishia wananchi kutokutoka maeneo yale ya Vijiji vile vya Matinje kwenda mpaka Nzega au Igunga? Ahsante. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo aliyoyataja kwa uelewa wangu ni kwamba yana mawasiliano. Sasa nitapenda tukutane tujadiliane kwa kirefu, labda anaongelea mitandao ya ziada. Kama kuna eneo ambalo halina mtandao tuwasiliane, tukubaliane cha kufanya.
MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Jimbo la Tabora Mjini, Kata ya Ikomwa maeneo ya Kapunze; Kata ya Kabila, maeneo ya Igosha; Kata ya Ndevelwa, maeneo ya Ibasa; na mengine ambayo kwa muda mrefu hayana mawasilino, Halotel inaonekana inasuasua hata kwenda kufanya survey tu maeneo yale. Sijui Serikali ina mkakati gani kuhakikisha hawa Mameneja wa Mikoa wa Halotel wanafanya kazi ipasavyo ili maeneo hayo yapatiwe huduma ya mawasiliano? Serikali ina mkakati gani kwa kuwa hiyo pesa inalipwa na Serikali kuhakikisha hawa Mameneja wa Mikoa wa Halotel wanafanya kazi yao kwa ufanisi.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mheshimiwa Mbunge kwa taarifa hiyo, lakin nataka tu niweke record sawa, Kampuni ya Halotel haijengi kwenye vijiji kwa kutumia fedha za Serikali ni fedha zao ila tumekubaliana na Serikali kwamba tuwape unafuu fulani wa kupata wayleave bila kulipa fidia ili waweze kufikisha mawasiliano katika vijiji vingi zaidi Tanzania, tuliwapa vijiji 4,000. Kwa hiyo ni fedha zao siyo hela za Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu nimhakikishie kwamba tutaliangalia na hilo eneo, tuone kama Halotel wataweza kufikisha mawasiliano mapema au tuviingize hivi vijiji katika mpango wa Mawasiliano kwa Wote, ambapo hapo ndiyo tunatoa fedha za Serikali kwa makampuni ambayo yanashinda tenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana kwa juhudi zake za kufuatilia masuala ya wananchi wake na mkutano wetu uliotukutanisha mimi na Waziri wangu kuyaongelea haya masuala, nimhakikishie kwamba tutatekeleza yale ambayo tulikubaliana kwenye kikao pamoja na kwamba leo amerudia kuliuliza hilo, labda kwa sababu ni muda mzuri wananchi wasikie. Hata hivyo, tunatambua juhudi zake na kwa namna ambavyo amelifuatilia sana suala hilo ofisini kwetu. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
MHE. PROSPER J. MBENA: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pia nifanye marekebisho kidogo Mheshimiwa Waziri alipozungumzia Jimbo langu mimi ni Mbunge wa Morogoro Kusini siyo Morogoro Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Serikali imekubali kufanya matengenezo ya mara kwa mara katika barabara ya Bigwa mpaka Kisaki ili iweze kupitika wakati wote; na kwa kuwa hivi sasa kuna tatizo kubwa katika sehemu ya Milengwelengwe katika Kata ya Mngazi, usafiri umekuwa mgumu barabara imeharibika. Je, Waziri yuko tayari kuagiza Mkandarasi pamoja na Meneja wa TANROAD Morogoro kwenda haraka eneo hilo na kufanya matengenezo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa nini Serikali isirahisishe matengenezo ya mara kwa mara katika barabara hii kwa kuruhusu kutengeneza vitengo vya matengenezo ya barabara katika Tarafa tatu ndani ya barabara hii ya Bigwa hadi Kisaki ili kurahisisha matengenezo ya barabara? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbena kwamba Meneja wa TANROADS Mkoa wa Morogoro anatakiwa aende haraka eneo la Ilengwelengwe kuhakikisha kwamba mawasiliano kati ya Kisaki na Morogoro Mjini yanapitika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili nimepokea ushauri wake, ngoja tupeleke kwa wataalam waangalie, wakachakate waone uwezekano wa kulitekeleza hilo. Nadhani anakumbuka kwamba zamani tulikuwa na vikosi vya PWD au tulikuwa tunajulikana zaidi PWD na baadaye tulivyoondoa na TANROADS ikaunda hiyo ofisi za Mikoa na ofisi za Mikoa zinafanya kazi zile zile ambazo PWD ilikuwa inafanya kazi zamani. Hata hivyo, kama nilivyosema ngoja nilichukue hilo wazo likachakatwe halafu tuone tutasonga mbele vipi.
MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika nakushukuru kunipa nafasi na mimi kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali inakiri kabisa kwamba kuna mialo ambayo haijasajiliwa na inasafirisha abiria na mizigo kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. Nataka kujua Serikali kupitia SUMATRA na TPA wanatumia utaratibu gani kuhakikisha kwamba vipimo vya kuhakikisha kwamba mizigo na abiria wanaoingia kwenye vyombo vya usafiri vinakwenda sambamba na uwezo wa chombo?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, bado kuna vyombo vingi vibovu na visivyokuwa na life jacket vinafanya safari za kubeba abiria kutoka Pwani ya Tanga kwenda Pemba; kutoka Pwani ya Dar es Salaam kwenda Unguja na kutoka Pwani ya Mkoa wa Pwani kwenda Mafia na sehemu zingine za jirani kama visiwa vya Comoro. Vyombo hivi vinafanya safari usiku vingine vinapotea na hata kumbukumbu hatuna. Serikali ina mpango gani wa kudhibiti safari za usiku za vyombo vibovu vinavyosafirisha abiria ili visiweze kufanya hivyo kunusuru maisha ya Watanzania?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi kwamba vyombo vyote vya majini kuanzia wakati vinatengenezwa kuna loading mark huwa inawekwa yaani chombo kikielea majini hakitakiwi ile loading mark izame chini, hicho ndicho kitu cha kwanza ambacho vijana wa SUMATRA wanakitumia katika kuhakikisha kwamba chombo hiki kinachokwenda kuelea majini na kusafirisha abiria na mizigo hakijazidisha abiria wala mizigo, kwa kukagua ile loading mark.
Mheshimiwa Spika, pili kuhusu suala la ni namna gani tunaweza kudhibiti, na vile vile vyombo hivi vinavyosafirisha abiria kati ya Tanga, Dar es Salaam na Zanzibar tunavidhibiti vipi. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vijana wetu wa SUMATRA wapo katika mialo, mialo ile iliyosajiliwa. Labda tu nichukue fursa hii kukiri na mara nyingi nakiri kwamba kuna mialo ambayo haijasajiliwa, na mingine hatuijui.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu hiyo ndiyo maana tumeweka usimamizi kwa kutumia viongozi wetu kamati za ulinzi na usalama za Mikoa yote ya Pwani na Zanzibar wanakutana kila baada ya miezi, na wakati mwingine miezi sita wanakutana na mikoa mbalimbali katika hii mikoa ya ukanda wa Pwani pamoja na Zanzibar ili kujadili na kuhakikisha kwamba wanaitambua ile mialo yote ambayo haitambuliki. Mialo hiyo ndiyo inayotumika mara nyingi kusafirisha mizigo usiku bila kufuata utaratibu.
Mheshimiwa Spika, niwaombe tu nanyi Waheshimiwa Wabunge tuhamasishe watu wetu wasitumie hii mialo ambayo haijasijiliwa, kwa sababu kwanza ni hatali lakini pili inapoteza mapato yetu kwa sababu hii mialo tunaitumia vilevile kukusanya kodi zinazotusaidia kuleta huduma mbalimbali za jamii na kufanya shughuli mbalimbali za kijamii.
Mheshimiwa Spika, niwaombe sana tusaidiane ili kuhakikisha mialo hii ambayo inaoparate illegally tuidhibiti kwa pamoja tukishirikirikiana na nyinyi Waheshimiwa Wabunge, muwaelimishe watu wenu. Kwa sababu hatimaye hawa watu wanatoka katika maeneo yetu. (Makofi)
MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, hali ya usalama wa abiria na mizigo katika bandari ya Kilindoni kwa zaidi ya miezi mitatu sasa iko mashakani kufuatia kukatika kwa ngazi katika gati la Kilindoni. Abiria wanalazimika kupanda kwa kutumia mitumbwi na viboti vidogo vidogo kwenda kupanda boti kubwa hali ambayo ni hatari sana kwa usalama wao.
Sasa je, Mheshimiwa Waziri anaweza akatuhakikishia Wananchi Mafia kwamba atawaelekeza watu wa Mamlaka ya Bandari waje watengeneze warekebishe gati lile ili lianze kutumika? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, ninafahamu umuhimu wa usafiri wa majini kwa ndugu zetu wa Mafia, ni njia kuu kwa wale ambao hawana uwezo wa kutumia ndege na kwa sababu hiyo nawaagiza TPA wafanye haraka sana kwenda Mafia pale Kilindoni ili lile daraja ambalo limekatika liweze kurekebishika na hatimaye ile gati iweze kuanza kutumika kwa kutoa usafiri kwa ndugu zetu wa Mafia.
MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, suala la ukaguzi katika vyombo vya majini kwa kweli bado halifanywi kwa asilimia 100, hasa nikizungumzia katika bandari ambazo ziko katika Wilaya zetuSUMATRA hawana ofisi katika kila Wilya ambazo ziko Pwani.
Nikizungumzia Pangani hakuna ofisi ya SUMATRA na badala yake SUMATRA wamekabidhi madaraka yale kwa watua wa TRA ili waweze kuwakagulia vyombo ambavyo vinasafiri. Pamoja na hayo TRA hawana wafanyakazi wa kutosha jambo ambalo wakati mwingine wakati chombo kinasafiri, iwe ni usiku au ni mchana, unakuta TRA hayuko pale kwa ajili ya kukagua kile chombo. Kwa hiyo chombo unakuta kinajaza kuliko uwezo wake na ndivyo hivyo vyombo ambavyo vinapoteza muelekeo Baharini vinapata ajali watu wanakufa na hatujui idadi ya watu waliokufa wala mizigo inayopotea.
Mheshimiwa Spika, nizungumzia Bandari ya Pangani mizigo mingi sana inapotea kutokana na hiyo hali na watu wengi wanakufa kutokana na hiyo hali na hawatangazwi. Sio hilo tu kuna zile bandari ambazo ni bubu, bado hazina kabisa usimamizi na watu wamekuwa wakipoteza maisha pamoja na mizigo. Sasa ni lini Serikali itachukulia kwa umuhimu wake suala hili la usafiri wa majini ambao umekuwa ukipoteza maisha ya watu bila kugundulika ili ajali hizi ziweze kupungua? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la swali la msingi kwamba SUMATRA wamepewa mamlaka ya kusimamia bandari zetu zote na bandari zote ambazo zimesajiliwa. Nakiri kwamba kuna bandari zingine ni bandari bubu na huwa zinazuka kila wakati, ni bandari ambazo zinatumika na wahalifu, kwa sababu kila ukiwadhibiti hapa wanaenda kutafuta sehemu nyingine. Ni wahalifu kwa sababu wanakiuka sheria za shughuli za bandari zinazosimamiwa na SUMATRA na kila tukijaribu kuwaelimisha, kwamba jamani acheni kutumia bandari bubu mtumie bandari ambazo zimesajiliwa rasmi, bado tunakuwa na matatizo.
Mheshimiwa Spika, mimi niwaombe Waheshimiwa Wabunge, wakati mwingine kama tutataka SUMATRA iwe katika kila aina ya bandari inayozuka kila wakati uwezo huo tutakuwa hatuna. Niwaombe sana Waheshimwa Wabunge tusaidiane, tuhakikishe mizigo yetu ipite katika zile bandari ambazo ni rasmi, tuache kupitisha katika bandari bubu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusu kukabidhi kazi za SUMATRA kwa upande wa TRA au hata taasisi nyingine, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba pale ambapo TRA inaona kwamba zile kazi zimewazidi huwa wanarudi kwetu, kwa maana na SUMATRA na kuwaambia kwamba hapa tunahitajika tuwe na permanent station ya watu wa SUMATRA na hatimaye huwa tunafanya hivyo.
Mheshimiwa Spika, katika maeneo yale ambayo traffic si kubwa sana tunawatumia wenzetu wa TRA na sehemu zingine TPA wanatumika kutegemeana na jinsi ya kutumia resources za Serikali tulizonazo. Sidhani kama tutaweza kwa SUMATRA peke yake kusimamia kila bandari tulizonazo, kuweka idadi ya staff inayotakiwa. Tunatumia taasisi zingine kufanya kazi hizo kwa kushirikiana na tasisi hizo zinawasiliana muda wote kuhakikisha kwamba pale ambapo panapolamika kuweka permanent station ya SUMATRA hatimaye tunafanya hivyo.
Mheshimiwa Spika, lakini naomba nirudie tena. niwaombe sana ndugu zangu, na hasa ninyi wenzetu mnaotoka katika maeneo ya ukanda wa Pwani mtusaidie ili watu wetu wafuate sheria na Sheria za SUMATRA na Sheria za TPA ni sheria mama kama zilivyo Sheria zingine, si kwamba zile Sheria ziko kiwango cha chini.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo kila mmoja ana uwezo wa kuzivunja kwa kadri anavyoona inafaa. Niwaombeni sana tusaidiane ili tuhakikishe kwamba maisha ya wananchi wetu na mizigo yao haiathiriwi katika safari za baharini na kwenye maziwa.
MHE. SEIF K. GULAMALI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; nina maswali (a) na (b).
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Serikali imekiri kuwa kati ya kata 19 zilizoko ndani ya jimbo la Manonga kata tisa hazina mawasiliano, kwa maana ya vijiji vyote vilivyoko ndani ya zile kata tisa, je, Serikali haioni kuwa katika maeneo hayo wananchi hawatendewi haki kwa sababu wanakosa mawasiliano? Na je, Serikali kutokana na majibu yake inatuhakikishiaje kuwa mpaka Novemba itakuwa tayari maeneo hayo yamepata minara ya simu katika maeneo yaliyotajwa?
Mheshimiwa Spika, swali b je Waziri atakuwa tayari tuongozane naye ili awezekwenda kujionea hizo kata ambazo hazina mawasiliano ya simu? Kama yuko tayari ni lini ili aweze kuona adha ambazo wananchi wanazipata? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema awali kwenye jibu la msingi Serikali inakiri kuwa kati ya kata 19, kata 10 zinamawasiliano na kata tisa hazina mawasiliano. Kwetu sisi hayo ni mafanikio makubwa na tutahakikisha kata tisa zilizobaki ambazo ni chini ya asilimia 50 tunazifikishia mawasiliano katika kipindi hiki cha miaka mitano itakapofika mwaka 2020 hilo litakamilika na tutalikamilisha kwa kutumia mkataba tulionao na kampuni ya Viettel kwa kuwa tuna mkataba nao, lakini vilevile Mfuko wetu wa Mawasiliano kwa Wote.
Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge umefika ofisini tumekutana na wataalam, bahati nzuri hivi vyote tuliviorodhesha na sasa unafahamu, labda ni vizuri tu na wananchi wako wakafahamu kwamba kata hizo zote tisa tumeshazichukua na tutazifanyia kazi katika kipindi kifupi kijacho.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba niko tayari kufika katika eneo lake na kuzipitia hizo kata.
Mheshimiwa Spika, kama utakumbuka ndani ya Bunge lako Tukufu alipouliza swali lake la nyongeza nilimjibu kwamba mimi siamini kijiji kama Machinja hakina mawasiliano kwa sababu watu ni wengi sana. na nitumie nafasi hii kuyafahamisha makampuni ya simu tunamaeneo mengi yenye watu wengi sana, mahala ambapo pana biashara kubwa. Maeneo hayo hatuhitaji fedha ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote yaende katika maeneo hayo. Kwa sababu maeneo hayo ni yakibiashara, yana watu wengi na mkipeleka mawasiliano mtapata fedha za kutosha. Its economically viable.
Kwa hiyo karibuni sana Waheshmiwa Wabunge tupeane taarifa maeneo ambayo yana watu wengi sana center kubwa sana makampuni yenyewe yaende tusitumie hela zetu za Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote. Hela hizi za mfuko wa mawasiliano kwa wote tuzitumie katika maeneo ambayo hayavutii kiuchumi.
Mheshimiwa Spika, nitakuja katika lengo hilo hilo la kuhamasisha makampuni kwanza yaje, lakini pili tuone UCSAF itafanyaje kazi kama ambavyo tulikuahidi ulipofika ofisini na tukakutana na wataalam. Hongera sana Mheshimiwa kwa kufuatilia suala hili kwa umakini sana.