Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Susan Anselm Jerome Lyimo (1 total)

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Pamoja na kuvunja tume hiyo sasa Mheshimiwa Waziri Mkuu, kwa nini wakulima sasa wasipate wataalam bora kwa ajili ya kilimo hicho cha ili waendane sambamba na huu uvunjaji wa hii tume tupate kilimo chenye tija? Ahsante.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Susan Lyimo, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utaratibu ambao sasa tunaufanya ni kwamba mbali ya kwamba kuna Tume ya Umwagiliaji, ina maafisa wake lakini tumewashirikisha pia Maafisa Kilimo wa Wilaya, Maafisa Ugani walio kwenye ngazi za vijiji, wote hawa wafanye kazi kama timu moja. kwa hiyo, usimamizi wa kilimo utakuwa ni wa pamoja na kila palipo mradi iwe mradi upo kijijini, tutakuwa na Afisa Ugani wa Kilimo pale kijijini lakini yupo Afisa Ugani kwenye ngazi ya kata, yupo afisa kilimo ngazi ya Wilaya na Afisa Umwagiliaji ngazi ya Wilaya; hawa wote wakifanya kazi kwa pamoja na kwa maelekezo tuliyowapa na kwa sababu pia tulishasambaza maafisa kilimo kwa kuwaamisha kwenye Halmashauri ya Wilaya kuwapeleka vijiji, tuna amini kwa maelekezo yetu chini ya usimamizi makini wa Waziri wetu wa Kilimo na timu yake, tunaweza kufikia hatua nzuri na tuwahakikishie kwamba tutasimamia vizuri Sekta ya Kilimo na hasa kwenye Sekta ya Umwagiliaji. (Makofi)