Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Charles Muhangwa Kitwanga (12 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nianze kwa kumshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kuniteua kuwa Waziri wa Mambo ya ndani. Nawashukuru sana wananchi wa Misungwi kwa kuendelea kuniamini na kupata asilimia themanini na kitu, haikuwa jambo dogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, niende moja kwa moja kwenye hoja ambazo Waheshimiwa Wabunge wamezitoa. Naanza tu kwa kusema, upande mmoja una haki lakini upande mwingine lazima kuwe na wajibu. Ukidai haki, timiza wajibu wako. Ndugu zetu kwa mfano, kama jana walikuwa wakidai haki, lakini hawakutimiza wajibu wao kwa kufanya fujo na ndiyo sababu Wizara yangu iko pale kuhakikisha kwamba nchi yetu inaendelea kuwa tulivu na salama. Hilo tutalifanya kwa nguvu zetu zote kwa sababu hatuwezi kufanya biashara, wala shughuli zozote katika mazingira ya ambayo hayana utulivu na siyo salama. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie mambo machache tu ambayo Waheshimiwa Wabunge wameyazungumzia tukianzia na malalamiko mengi hasa oparetion ya bodaboda yaani ya pikipiki.
Waheshimiwa Wabunge, pamoja na wananchi wote, mtakumbuka kwamba hivi karibuni limejitokeza wimbi kubwa la uhalifu unaosababishwa na watu wanaoendesha pikipiki. Kwa hiyo, hapa hatuzungumzii bodaboda peke yake, tunazungumzia pikipiki zote.
Kwa hiyo, oparetion tunayoifanya sasa hivi ni ya kujaribu kuhakiki na kuona kama pikipiki zote zinamilikiwa kihalali na watu gani na kuhakikisha kwamba kila mmoja anayepita katika eneo linalotakiwa, anapita kwa kufuata Sheria za Usalama Barabarani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili ni jambo la usalama zaidi ili tuweze kuishi katika mazingira salama na wananchi wasiwe na wasiwasi, vilevile watu wote walio na pikipiki za kawaida au bodaboda wasiwe na wasiwasi, hili ni kwa nia njema na kuhakikisha kwamba nchi yetu inaendelea kuwa salama na tulivu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo limezungumziwa, ni la wakimbizi. Ni kweli wakimbizi kwa miaka ya nyuma walifikia kwenye 800,000, lakini walipungua sana na sasa hivi hali inaanza kurudia tena. Kwa sasa hivi tuna wakimbizi kwa mfano tuna Wakongo 63,000; tuna Warundi wapya ambao wameingia 124,000; tuna wakimbizi kama 199 wengine kutoka hata nchi kama Syria, lakini bado wanakuja kwetu, lakini tuna wakimbizi wengi tu, Warundi wapya ambao wamekuja tena sasa hivi ni 124,637.
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kinachotupa nia ya kujipanga upya sasa hivi ni kwamba baadhi ya wakimbizi wanaokuja wametoka katika maeneo ya majeshi. Wanapofika katika maeneo ya wakimbizi wanaanza kufanya recruitment ya askari. Hili tumeliona na tumejipanga na tunahakikisha kwamba halitaendelea. Nchi yetu haiwezi kuwa chanzo cha askari wanaokwenda kufanya vurugu katika nchi za majirani zetu. Nihakikishe tu kama alivyosema Mheshimiwa Rais katika hotuba yake kwamba, wale watakaokuwa wanahitaji Uraia, utaratibu utafuatwa kulingana na sheria zetu na tutaweza kuwapatia uraia.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo limezungumziwa na watu wengi, ni hili la maisha mazuri ya askari polisi wetu. Kitu cha kwanza wamezungumzia…
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa
muda wa Mzungumzaji)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Kitu cha kwanza ambacho wamezungumzia ni nyumba. Niseme tu kwa sababu ya muda, kwamba tuna mpango wa kujenga nyumba mpya 3,500 kila mwaka kwa ajili ya polisi wetu. Nakushukuru sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru tena kwa kunipa nafasi hii ili niweze kujibu hoja mbalimbali ambazo Waheshimiwa Wabunge 77 wamechangia. Kwa muda mfupi huu wa jioni, Wabunge 77 wameweza kuchangia hoja hii na kati yao 20 wamechangia kwa mdomo na wengine 57 wamechangia kwa maandishi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kabla sijaanza kujibu hoja, naomba niwataarifu Wabunge vitu vitatu. Cha kwanza, niko Serikalini sasa hivi kwa miaka 35. Nimeanza kazi mwaka 1984. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili, natambulika kwa jina la utani Mr. STK (Mzee wa STK) kwa maana ya sheria, taratibu na kanuni na la tatu ni kwamba nimewasilisha fomu yangu ya kwanza Tume ya Maadili mwaka 1998. Vitu vitatu hivyo vinatosha kuwapeni taarifa na mjue mimi ni mtu wa namna gani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho, huwa sipendi kusema sana, napenda kutenda. Kwa sababu hiyo basi nitajibu kwa kifupi sana lakini tutajitahidi kuwaleteeni majibu kwa maandishi kwa hoja zenu zote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya muda nitajibu hoja chache ambazo zimetolewa kwanza na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama halafu nitajibu kile ambacho Mheshimiwa Lema aliniomba nijibu na jibu langu ni fupi sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli baada ya kusoma ile bajeti mbadala nimesikitika sana, bila CCM nchi hii haina uongozi mwingine. Kwa sababu hotuba yote ina-refer magazeti na inapiga vijembe na hakuna bajeti mbadala. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hivyo ndivyo, bado tuna kazi kubwa sana ya kuandaa Kambi ya Upinzani maana iliyopo ni Kambi ya Upingaji. Kwa sababu kilichoandikwa ni kwamba kutokana na magazeti, tunasikia, huwezi kutueleza hapa yaliyoandikwa kwenye magazeti na uliyosikia, tuambie unayoyawaza wewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua wako wapiga kelele, natambua wako wajenga hoja wachache na hoja zao walizozisema Serikali itazichukua na itazifanyia kazi maana ni za maana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na Kamati ya Kudumu ya Bunge, mengi yaliyosemwa ni mapendekezo au ushauri mbalimbali na ushauri huo Serikali itauchukua na kuufanyia kazi maana Serikali hii ni sikivu na haipigi kelele, it doesn’t shout. Utawasikia tu wataanza ku-shout, we don’t work like that, we are professionals na ndiyo sababu nina miaka 35 Serikalini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwenyekiti wa Kamati au Kamati inapendekeza kwamba Serikali itoe fedha kwa ajili ya kulipa madeni ya watumishi, wazabuni na wakandarasi katika mafungu yaliyopo katika Wizara yetu. Nilifahamishe Bunge lako, sasa hivi Serikali imeamua kuweka madeni yote kwa pamoja. Kinachofanyika ni kwamba madeni yanahakikiwa na yakishahakikiwa kutoka Fungu Kuu (Treasury) yanalipwa na baadhi ya wafanyakazi pamoja na wakandarasi wa Wizara yangu tayari naadhi yao wameshalipwa na tunaendelea kuhakiki na wale ambao tunaona ni halali tutafanya hivyo kwa kuwalipa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliambiwa NIDA kuna wafanyakazi ambao wanaidai Serikali, tulipoita wale wafanyakazi 50 hawakuonekana kabisa na wengine ukiisoma mikataba yao huwezi kuelewa ndiyo sababu tunafanya uhakiki kwa kushirikiana na Treasury. Pale ambapo tutajiridhisha kwamba huyu kweli anaidai NIDA na ni mfanyakazi halali, watalipwa, pesa iko katika akaunti ya NIDA. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuendelea na hali ile ya zamani ya watu kufanya longolongo na msitusukume kuingia katika mambo ambayo hatuyapendi na ndiyo sababu tumeyafanyia kazi. Kwa taarifa yenu tu pale NIDA sasa hivi tuna vyombo vitatu vinahakiki yote yaliyotokea nyuma. Wa kwanza, Controller and Auditor General yuko pale, PCCB wako pale na PPRA wako pale. Hizi ni initiative ambazo Wizara yetu tumezifanya katika kuhakikisha kwamba maeneo yote tuliyokuwa tukiyatilia mashaka tunapeleka vyombo hivyo vitatu ikiwa ni pamoja na Uhamiaji. Tutafanya hivyo maeneo yote tutakayoona kwamba kuna wasiwasi. Mtuamini, sisi ni watu wa Hapa Kazi Tu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limezungumzwa ni lile la usimamizi wa sheria barabarani. Hili nalo tunalifanyia kazi kwa nguvu zetu zote. Tayari aidha, tumewaondoa baadhi ya askari katika Kitengo cha Usalama Barabarani au tumewafukuza, hakuna maneno. Tunatambua kwamba kuna Watanzania wengi ambao hawana kazi, mtu yeyote tutakayempa kazi na akaichezea atupishe tutapeleka watu wengine chuo chetu kule Moshi, watapata training waje waajiriwe Jeshi la Polisi. Hivyo ndivyo ilivyo na ndiyo sababu nikawapa kwanza yale maelezo ya mwanzo manne. Ni Jeshi la Polisi jipya, ni Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi mpya, tupitishieni bajeti tukafanye kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nije kwenye hoja mbalimbali zilizochangiwa na Wabunge. Uchakavu wa vituo vya polisi na nyumba na hili limezungumzwa na Mheshimiwa Kangi Lugola amesema atakuletea ile picha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli nilivyotembelea mimi mwenyewe nilisikitika na ndiyo sababu tukafanya juhudi kuhakikisha kwamba tunajenga nyumba za askari. Tunajenga nyumba za polisi 4,136 kwa mpangilio uliopo sasa hivi lakini vilevile tunajenga nyumba 9,500 za magereza. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili suala haliwezi kuchukua mwaka mmoja. Unapoanza kujenga nyumba labda sijui tuchukue wakandarasi wangapi, tunapopanga kuna kitu kinaitwa absorption capacity, tukisema kwamba mbona nyumba ni 4,136 tu, je, tukisema tujenge nyumba 10,000 tutazijenga mwaka mmoja na kwa utaratibu upi?
Kwa hiyo, hayo ya nyuma yameshatokea, kilichopo ni kuboresha tukienda mbele na tunasema tunaanza na nyumba 4,136 kwa polisi, nyumba 9,500 kwa magereza na hili halitafanyika katika kipindi cha mwaka mmoja tu. Tumeona mfano wa nyumba za polisi tulizozijenga Kurasini, zinazojengwa Mwanza, tumeona nyumba ambazo tumezijenga kwa Jeshi la Wananchi hazikuchukua mwaka mmoja, lakini tuna mpango huo na tutahakikisha kwamba tunaendelea kujenga kwa kadri uwezo utakavyokuwa unaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limejitokeza sehemu mbalimbali ni uhaba mkubwa wa mafuta na vipuri. Ni kweli katika magari yetu ya Polisi, Magereza, Uhamiaji na Zimamoto kuna uhaba wa mafuta na vipuri, hili na sisi tumeliona, tunashukuru kwa vile na ninyi mnaliona lakini tushirikiane kwa pamoja kupeana taarifa pale ambapo kunakuwa na ukosefu wa vifaa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo lililotolewa na baadhi ya wenzetu ni kwamba mafuta yaende moja kwa moja kwa OCDs yasipitie kwa RPCs, pendekezo hili tunalichukua, tukalifanyie kazi na tukiliona linawezekana kufanyika basi tutafanya hivyo lakini kwanza tulifanyie utafiti tuone kama linawezekana kufanyika. Kama haliwezi kufanyika basi tutaona namna ambavyo tunaweza ku-improve system iliyopo sasa hivi iweze kuwa ya haraka zaidi. (Makofi)
Mheshimiwa Mweneyekiti, eneo lingine ambalo limezungumziwa kwa hisia sana ni ulinzi binafsi kutokuwa na sheria. Hili na sisi katika Wizara tumeliona, tumewapa Jeshi la Polisi waweze kuangalia na kuona kama tunaweza kuwa na sheria ya haraka zaidi ambayo tunaweza tukaipitisha ili tuweze ku-regulate huu ulinzi binafsi. Nadhani ni wazo zuri na sisi tunalichukua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo limezungumzwa ni msongamano katika magereza yetu. Ni kweli, mimi nimetembelea magereza yote Dar es Salaam na mengine mikoani, msongamano kwa kweli ni mkubwa. Kama nilivyosema kwenye bajeti yetu kwa mwaka huu tutakarabati mabweni 49 na tutajenga mengine na tutaendelea kujenga magereza sehemu mbalimbali hasa hasa kwenye maeneo mapya ya utawala kama ambavyo imependekezwa lakini hii itategemea na upatikanaji wa fedha mwaka hadi mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuzungumzie suala la mikataba. Mikataba yote ina matatizo, Mheshimiwa Masoud ndivyo alivyokuwa anasema. Nadhani solution siyo kuleta mikataba hapa kwa sababu hadi leo hii kuna utaratibu maalum kama Mbunge au Kamati ingependa kuona mkataba, utaratibu upo wazi kabisa. Sidhani kama tutakuwa tunachukua mikataba halafu tunakuja tunaigawa humu yote kila mtu aone kwa sababu kila mtu ana nia yake. Lazima itambulike kwamba mkataba kati ya institution na supplier ni mikataba ya watu wawili, sidhani kama wewe ungependa mkataba wako na mtu fulani upelekwe mahali pengine au kwa mzazi wako lakini utaratibu upo hata mkitaka kuona mkataba wa Lugumi, tungeweza kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niwaonye na niwaambie ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge haya mambo ya security tunaiweka nchi katika hali ya utata. Tuyafanye kwa utaratibu ambao hauta-disclose information kujua kwamba kumbe polisi wana mkataba na mtu fulani kwa hiyo wana system fulani hao wahalifu watajua system uliyonayo na wataikwepa. Kinachotakiwa hapa, tutumie utaratibu wetu wa kawaida ambao upo hata mkitaka mikataba yote mtaiona, upo na upo very clear.
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunapiga kelele, tunaandika kwenye magezeti, we are putting our country at risk. Nichukulie tu mfano huu mkataba wa AFIS, sasa hivi kila mtu anajua kwamba Tanzania wanatumia mashine fulani za kutoa finger prints. Sasa ukishafanya hivyo mtu aliyekuwa anataka kutenda jambo bovu ataji-protect. Hivi sasa hao wanaotenda mabovu wakianza kuvaa gloves, don’t you see that you are putting your country at risk?
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nachowaomba jamani tukihitaji mikataba au tukihitaji kujua facts tufuate utaratibu wa Kibunge badala ya kwenda ku-shout na kupeleka haya mambo kwenye magazeti. Hakuna mtu anayeficha kitu, after all sisi wenyewe tunapenda sana kupata ushauri wa watu ambao ni the right channel, lakini tutumie utaratibu ulio sahihi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nashangaa sana, ndiyo sababu hamjaniona hata siku moja nimejibu chochote kwenye magazeti, lakini we shout a lot kwenye magazeti. Hilo nawashauri kama Wabunge wenzangu ninyi mna responsibility ya kulinda usalama wa nchi yetu. Kama Wabunge tumieni the right channel ku-request information mnayoihitaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo limezungumzwa na watu wengi sana ni maslahi ya askari mbalimbali. Kweli mimi nakubaliana nalo. Ukiangalia hotuba yangu kuna maeneo mbalimbali ambayo tunajaribu kuboresha maslahi ya askari na hili kwa kweli mimi nitalipigania kwa sababu wanafanya kazi katika mazingira mengine siyo mazuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu ambacho nataka nikiseme, kuna jambo limesemwa na upande huu kwamba askari wanatumiwa na Chama cha Mapinduzi. Jamani mtakapomaliza hapa si mtakwenda kwenye mikutano ya hadhara, niambie askari achana nao, ninyi hamuwatumii askari kwenye mikutano yenu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi unajua huwa ni mkweli kupita kiasi na nasimamia Wizara hii kwa kufuata STK, nitahakikisha kwamba sheria, taratibu na kanuni zinafuatwa, basi.
Sasa kama mimi ni mwaminifu au nini lakini ukweli unabaki pale pale, tufanyeni kazi kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni. Askari yeyote ambaye hatafuata sheria, taratibu hata kanuni nimesema consequence atakazozipata. Kama kuna askari ame-misbehave mwambie Mkuu wa Wilaya, RPC au OCD wake na kama unashindwa namba yangu iko wazi nipigieni, uwe Mbunge wa CCM, CHADEMA, CUF na hilo mnalitambua, Mheshimiwa Masoud unalitambua. Mheshimiwa Masoud anatambua kwamba mimi sibagui kwa sababu Jeshi letu la Polisi linalinda usalama wa raia na mali za Watanzania wote. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suggestion kwamba tuongeze boti za doria hasa baharini. Hilo na sisi tumeshaliona na siyo baharini tu, wale wenzetu wanaotoka Mkoa wa Kagera, Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa wana tatizo hilo. Kwa hiyo, tunaliangalia comprehensively tuone ambavyo tunaweza kutatua tatizo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Msigwa anasema alibambikwa kesi, kama kweli alibambikwa kesi njoo niambie. Wewe ni Mheshimiwa una-access ya kuniona wakati wowote tuone ni kwa namna gani tunaweza tukalirekebisha hili.
yaliyokwishazungumzwa na yameshajibiwa na mwenzangu, lakini moja ambalo amelisisitiza ni kwamba tuwe na vituo vya kutosha katika maeneo mbalimbali. Ni kweli kama nilivyosoma kwenye hotuba yangu tunakwenda polepole, lakini ni kwa kulingana na uwezo tuweze kujenga vituo katika maeneo mbalimbali hasa Wilaya mpya au maeneo mapya ya utawala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Lwakatare amezungumzia suala la kubambikwa kesi nimeshalijibu.
Mheshimiwa Khatib nadhani nimekusikia na tuna mpango wa pamoja wa kutembelea maeneo aliyoyasema, tumeshaongea, nitaenda hata kwako, usifikiri siendi upande wa CUF naenda tu, wote ni raia. Mbunge yeyote ambaye ana nia ya kwenda na mimi tujadiliane, tuone tukiwa na nafasi tutakwenda tu tuone kwa sababu nia ni kuhakikisha kwamba nchi nzima inakuwa salama na kuna usalama. Kwa sababu anapotoka Mheshimiwa Khatib pale siyo wote ni CUF, kuna wengine ambao ni CHADEMA, kuna wengine ambao ni CCM na Serikali yetu kama ambavyo Mheshimiwa Rais wetu anavyosema ni Serikali ya Watanzania wote na yeye ni Rais wa Watanzania wote na mimi ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ya Watanzania wote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani niishie hapo kwa kusema naomba kutoa hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2017/2018 - Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nianze kutoa shukrani kwa nafasi hii. Nianze tu kwanza kwa kutoa shukrani angalau safari hii nimeona hela katika kusaidia kupata maji katika Jimbo langu la Misungwi. Kwa masikitiko makubwa sana vilevile lile swali nililouliza la nyongeza kwamba, pale Ihelele ambapo ndipo chanzo cha maji hata leo hii pamesahaulika. Sasa safari hii patachimbika na mimi sitatoa shilingi, nitakachofanya nitakwenda ku-mobilize wananchi wa Misungwi kama 10,000 tukazime ule mtambo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tangu mwaka 2008 tunaendelea kusubiri, tunaendelea kusubiri na leo mmethubutu kuandika huku kijiji cha Nyanhomango kimepata maji wakati hakina. It’s so disgusting kwamba World Bank walikuja pale wakasema this is inhuman, halafu sisi tunaona ni human. World Bank wamefika pale wakaona kwamba hawa watu ambapo maji yanatoka hawana maji, wakasema this is inhuman, lakini wafanyakazi waliokuwa nao wameendelea kuona huo ni ubinadamu. Siwezi kukubali na sitakubali na hili lazima libadilike, kwa sababu hii nchi ni yetu wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia huku pesa nyingi zimepelekwa sehemu ambazo siwezi kuzitaja na maji labda yapo, ni vema tukatendeana haki. Inanipa shida zaidi kuona kwamba hata mahala ambapo Mheshimiwa Rais aliahidi maji pale Usagara hamna senti iliyowekwa humo, kama imo mnionyeshe. Ninachowaomba jamani tutendeane haki. Huwezi kuwa na mradi wa kwenda mpaka Tabora unatumia bilioni 600 unashindwa kuwapa hawa watu wa pale ambapo maji yanatoka hata bilioni kumi? Very unfair, ninazungumza hili likitoka moyoni mwangu kabisa. Nakipenda sana chama changu, naipenda sana Serikali yangu, nampenda sana Mheshimiwa Magufuli lakini ninyi watu wa Wizara lazima mtende haki. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, zaidi ya hapo hata ile barabara inapokwenda chanzo cha maji sasa hivi haipitiki kwa sababu ile ni ya tani 10, lakini yale malori yanayobeba yale madawa ni 28 tons, 40 tons, sasa Halmashauri kila ikijaribu kutengeneza inashindikana. Nashukuru Wizara ya Ujenzi angalau wameweza kui-upgrade ile barabara kuwa ya TANROADS. Niseme tu kwamba haki haijatendeka hapa na mimi sitatoa shilingi wala nini dawa yenu ni kwenda kuzima ule mtambo, eeh. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, dawa yenu ni kwenda kuzima ule mtambo wote tukose, eeh! Kwa sababu gani, kama tunasema na mmeniahidi hapa kwamba na mimi nimekwenda nimeongea na watu wa KASHWASA wakaniambia it is 4.2 billion, ziko wapi? nimeona hapa bilioni
3.9 najua ni za kutoka Mbalika kuja Misasi. Halafu sasa tutakuwa tunapoteza hata hela, kwa sababu kutoka Mbalika kuja mpaka Misasi tayari mabomba yamewekwa, kutoka kwenye chanzo cha maji kuja hapa Mbalika, hamjaweka, hata common sense jamani hatuna? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingine inanishangaza sana, yaani mnishukuru tu nilikuwa Waziri zamani nilikuwa siwezi kusema, sasa nimetoka tutapambana. Ninachosema ni lazima tuwe good planner, lazima tuwe na mipango mizuri, tuwe na mikakati mizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mbona kwenye REA tume- perform vizuri tu, kwa nini tusi-perform vizuri hata kwenye maji vijijini, tuna matatizo hapo kidogo. Sasa mpaka nashangaa wakati mwingine, niliomba mradi kwa rafiki zangu kutoka Austria nikawa nimepewa, baadae nikapigwa figisu figisu eti kwamba wewe una-interest, ndiyo nina interest! Kwa sababu watu wangu wa Kolomije wanahitaji maji! (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, watu wangu wa Bukumbi wanahitaji na tulipokuwa Bukumbi na Mheshimiwa Rais akawambia wananchi huyu ana marafiki zake wengi nchi za nje. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, nikawa nimetafuta kule mara ya kwanza wakasema kwanza Tanzania ichangie 20 percent kwenye design hela kidogo, sasa hivi wamesema hivi hata hiyo 20 percent tunawasamehe kamilisheni hiyo miradi awamu ya kwanza ili nami Bukumbi wapate maji, Kolomije wapate maji, Ibongoya wapate maji. Kwa sababu waliishaniahidi kwamba tukiishamaliza tu hiyo awamu ya kwanza na wewe utapata. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa namuuliza mmojawapo ya wakubwa hapo kwamba hebu vipi huu mradi wa Austria ananiambia achana na huo mradi wa Austria. Sasa hatuwezi kutajana majina, I was a little bit disappointed. Niombe tu huo mradi na wenyewe tuupe, kwa sababu sasa hivi wameshakubali, kinachotakiwa ni sisi ku- respond kwa Serikali ya Austria kusema kwamba go ahead, halafu wakishamaliza hapo wanachosema pelekeni ombi lingine sasa la hivyo vijiji vyangu ambavyo nimevitaja. Hamia huko kama unataka, ni pazuri sana. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo ndugu zangu wapendwa sitajihangaisha kutoa shilingi, lakini mjue mtajua sasa maharage ni mboga au ni zao la biashara. (Makofi/ Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa uliokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia katika ajenda hii iliyoko mbele yetu. Tuanze kwanza kwa kutazama uchumi wetu na jinsi tulivyojipanga. Sisi sote tunatambua kwamba tuna vision 2025 na hii vision tukakubaliana kwamba tutai-cascade in five years plans. Plan ya pili tulionayo leo hii ni plan ya kuipeleka nchi yetu kwenye uchumi wa viwanda. Sasa tunafikaje pale kwenye uchumi wa viwanda Mheshimiwa Mpango pamoja na timu yake wameweka vizuri katika hotuba yao na katika maelezo ambayo tumeyapata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sisi tunaitafsiri vipi na kuielewa na kuhakikisha kwamba ina-add value na kumwezesha kila Mtanzania aweze kusema kwamba yuko kwenye uchumi wa viwanda na anaishi maisha bora kuliko alivyokuwa zamani. Tuangalie kwanza nchi yetu imeajiri au watu wetu wanashughulika na kitu gani kwanza, asilimia kubwa. Tukiangalia tunakuta kwamba wananchi wengi wanashughulika na kilimo. Sasa viwanda vyetu vingi vielekezwe wapi na tutambue kwamba kuna viwanda angalau vya three categories; kuna viwanda vikubwa, mahitaji yake ni tofauti; kuna viwanda vya kati, mahitaji yake ni tofauti; na kuna viwanda vidogo ambavyo vitaweza kuajiri au kuwafanya wananchi wa kawaida washiriki wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vyote hivi vinahitaji mazingira yanayoeleweka. Nirudie tena nilishawahi kusema katika eneo letu la kwanza kabisa ambalo tuli-invest heavily lilikuwa ni eneo la madini, mwekezaji anapokuja kwenye madini anachukua madini anahama nayo, tukawapa incentives za kutosha wakaendelea wakawekeza kwenye madini. Sasa hivi tuko kwenye viwanda, viwanda hivi vinatakiwa vipewe incentives.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kitu kimoja tu. Mtu yeyote atakayekuja hapa atakuta ardhi, atakuta wananchi ambao watashiriki, atakuja na expertise na capital. Baada ya kujanavyo hivyo vitu, atajenga kiwanda. Sijawahi kuona hata mtu mmoja amejenga kiwanda akakibeba. Tuseme kwa mfano ametoka London, akakibeba akaendanacho London. Tuwape incentives hawa watu wajenge viwanda, hawatavibeba kutoka hapa kwendanavyo London. Madini tuliwapa incentives, wakabeba wakaendanayo leo tuna mashimo baadhi ya sehemu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nisisitize sasa hili la kilimo. Kwanza naipongeza Serikali, inaweka miundombinu kwa ajili ya kupata umeme. Je, huu umeme mkubwa tunaoujenga kama hatuuwezeshi kuwa na viwanda vya ku-consume huu umeme, si tutaanza kuu-export huu umeme badala ya ku- add value ndani na kusababisha watu wakapata ajira; watakapopata ajira watalipa Pay As You Earn na zile pesa zitazunguka mifukoni mwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunapokuwa na kilimo, nichukulie mfano mzuri tu wa pamba; enzi ya Mwalimu pamba ilikuwa inanunuliwa na Vyama vya Ushirika na Vyama vya Ushirika vilikuwa heavily subsidized. Tulikuwa na viwanda (generies) vya kati na tulikuwa na viwanda vikubwa vya nguo. Vyote hivi vilikufa kwa nini? Hebu angalieni leo China; wengi tunavaa nguo kutoka China, wengi tunavaa nguo kutoka India. Policy yao kuhusu viwanda vya nguo ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, huwezi kuwa na kiwanda cha nguo bila Serikali kuwa involved in one way or another. Kwanza kumbuka kwamba unahitaji a minimum ya kama dola milioni 50 ili uweze kununua raw materials ambayo ni pamba uweze ku-run mwaka mzima. Pamba ile utaihifadhi kwa mwaka mzima, kwa sababu, utakapokuwa unanunua pamba, ni msimu na sana sana ni miezi mitatu, baada ya miezi mitatu msimu umefungwa. Je, hiyo pamba utakayostahili kuwanayo kwa mwaka mzima, si lazima uwe na capital ya kutosha? Sasa kama una hela zako nyingi, na huwezi kuwa na cash money, itabidi ukakope. Kama unataka kukopa, hiyo interest rate ikoje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu tufikirie, leo hii kama kila Mtanzania anaevaa nguo kutoka China, asivae nguo kwa ku-save dola 10 tu, Watanzania wote, tuko milioni ngapi? Tuko milioni 55, lakini dola 10 tu kila mtu a-save anunue nguo ya hapa ili hiyo dola 10 izunguke kwenye uchumi wetu, tutakuwa tumezungusha hela kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hela hizo zitakapokuwa zimezunguka, si zitanunua vitu vingine ambavyo vimelipiwa ushuru? Ushuru huo utaupata kutokana na hiyo dola 10 kuwa imezunguka kwenye uchumi wako ukaweza kuuwezesha uchumi wako kukua. Kwa nini hawa watu wenye viwanda vya nguo wasipewe tax holiday au incentive kubwa hata ya ku-save dola 10 tu kwa kila nguo? Hilo ni jambo la kutazama. Tutazame: Je, watu wangapi watakuwa wameajiriwa kwenye viwanda vya nguo? Angalia MWATEX, MUTEX, KILTEX na kila mahali ambapo kulikuwa kuna viwanda kama hivi, vilikuwa vinaajiri watu wangapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka MWATEX wakati ule kilikuwa kinaajiri zaidi ya watu 1,000. Wacha hapo, wako wale wa kutengeneza zile nyuzi. Viwanda vile vya kati vya kuchambua pamba; kulikuwepo sijui Bukumbi, Buchosa, sijui wapi, kulikuwa na genery karibu 20; katika hiyo ilikuwa inaitwa Victoria Federation kwanza halafu ikawa Nyanza, ikaja SHIRECU na sehemu zote zile. Zote hizo leo hazipo. Maana yake wale wafanyakazi hawapo na kwa sababu hiyo sasa hakuna Pay As You Earn na kwa sababu wale wafanyakazi hawapo, hawana hela ambayo itawawezesha kusaidia kiwanda cha chumvi Uvinza kwa sababu wangeweza kununua chumvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie ile trickledown na jinsi ambavyo tunaweza tuka-affect. Kwa hivyo, mipango yetu iangalie wapi tu-invest, wapi tutoe msamaha ili tuwezeshe viwanda vyetu na watu wetu waweze kupata faida kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nawaomba ndugu zangu, najua rafiki yangu Mheshimiwa Dkt. Mpango una akili sana na Naibu wako, hebu panueni zaidi tuione hivyo na muishawishi Serikali yote kwa pamoja, tuweze kuangalia ni kwa namna gani sasa tutatoka tulipo tuweze kweli kuwa nchi ya viwanda? Hatuwezi kuwa tunaimba tu bila kuangalia watu wengi ambao wanaguswa na eneo gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie labda tena eneo la service au transport. Tunajenga SGR; very good plan na very long looking kama ambavyo Wajerumani walikuwa wanajenga reli kutoka Dar es Salaam mpaka Mwanza na kote walikuwa wanakwenda kuchukua raw materials. Sasa uchumi umebadilika, tunahitaji kujenga reli hii ili ituletee faida. Hatuwezi kujenga reli kwa ajili ya abiria wa kibinadamu tu, tujenge hii reli tukiwa na thinking kwamba, reli itakapofika Mwanza iweze kutusaidia kubeba mizigo yetu tuweze kui- export au tuweze kupeleka raw materials kwenye viwanda vidogovidogo ambavyo vimeajiri watu wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna daraja zuri sana, natumaini litaanza kujengwa hivi karibuni pale Kigongo – Busisi. Very good decision again. Watu sasa hivi kwa sababu ya usafiri kutoka Kigongo kwenda Busisi, wakati mwingine malori yanajipanga kuanzia saa sita mchana linakuja linavuka saa sita usiku. Hayo ni masaa 12, lakini kama tutakuwa na lile daraja, litatumia dakika nne tu kutoka Kigongo kwenda Busisi na kuendelea na safari zake. Tutakuwa tume-save time na tutakuwa tumemwezesha huyo mtu kufanya business haraka zaidi. Sasa tu--add value kwa sababu vilevile pale Fela kutakuwa na dry port. Hatuwezi tu tukawa tunaleta mizigo inayotoka nje tukaiweka pale Fela halafu wananchi kutoka DRC, Burundi, Rwanda na Uganda wanachukua mizigo kutoka bandarini na kupitisha pale kwenye daraja. Lazima tuwe na mpango mkakati wa kujenga maeneo ya biashara kubwa, business centres.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikiwezekana pale kuwe na business centre kubwa, vifaa badala ya watu kwenda kununua Guanzhou watu walete au tuwashawishi wale wanye maviwanda kule Guanzhou walete pale Mwanza au eneo lolote karibu hapo. Sasa nguo au vifaa vyote vinavyoletwa pale vipewe tax free. Vikiwa tax free, Mtanzania unapokwenda kununua pale unalipia ushuru, unachukua vile vifaa vyako unaweza kuvitumia. Mtu anayetoka Rwanda, Kongo, Burundi nakadhalika akinunua pale, anapeleka Rwanda bila tax.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa ambacho mimi nakiona tuna shida kubwa ya uwoga na vilevile tuna shida kubwa ya kuona kama tutaibiwa. Tupige brain, tuweke control, tuweke system ambazo zitatuwezesha leo hii vifaa vinapokuwa hapa, unakuwa unaviona kwamba, huyu ameleta mizigo ya dola 1,000,000. Katika mizigo ya dola 1,000,000 labda 500,000 ameziuza localy, 500,000 amezi-re- export baada ya kuwa ame-import, lakini kwa sababu tuna wasiwasi inakuwa ni tatizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano tu, tulikuwa na wasiwasi kweli kutumia hata hii. Tuliyapenda sana makaratasi, lakini leo hii you could see hapa kwenye meza zetu. Meza zetu ni safi, hazina matatizo and you will save a lot of money, tume-dare. Rais wetu ni very daring, let all of us be daring. Tu-dare kufanya, tukifanya makosa, tumwambie hapa nimekosea, nipe nafasi. Kama anaona hawezi kukupa nafasi, akutumbue, halafu tuendelee mbele, mwingine atakuja. Naye kama ni daring, mwishoni ataona hawa wamefanya hivi kwa nia njema. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie tourism. Tourism again nimeiona hata humu kwamba tunanunua ndege tunaimarisha Air Tanzania, very good, briliant na matokeo yake tunayaona na trickledown again nimeshaizugumza. Ndege zetu sasa zinaruka kwenda Mumbai na Watanzania wanaleta mizigo, zinakuja na watalii, watalii wanakwenda kwenye mbuga. Watu kwenda kwenye mbuga hawaendi na ndege, wanaenda na Landrover ambazo zinaendeshwa na Watanzania. Wakifika Mlima Kilimanjaro kwa rafiki yangu Mheshimiwa Selasini, wale wanaozunguka ule mlima wanakuwa wapagazi, wame-gain wanapanda kwenda Mlima Kilimanjaro. Hiyo ndio trickledown ya uchumi na ndege zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tusiishie hapo. Wenzetu wa ATC wana mpango wa mpaka 2021, let us look beyond that. Tumeleta Dreamliner 8 mbili, let us think of having Dreamliner 9 mbili nyingine za market ya kwenda Israel na Ufaransa. Watu wengi wanaokuja hapa; sasa hivi ukiangalia, nilikuwa naangalia kwenye TV naona jinsi Waisrael wanavyokuja wengi na wanalalamika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bahati nzuri nina rafiki zangu wawili watatu kule, walikuwa naniambia, hivi nchi yenu inashindwaje kuwa na flight angalau mara tatu kwa wiki kuja Israel ili zitupunguzie gharama? Kwa sababu tunapokuja Tanzania, ndege tunazokujanazo tuna-charter mandege makubwa, it becomes very expensive kwa sababu anaenda mara moja, akirudisha, basi anaendelea kule, anaanza kutafuta market nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama tutakuwa na three times per week labda kutoka Tel Aviv na pale Israel kuja hapa, tutapata watalii wengi zaidi. Kwa hiyo, we should not be afraid, let us dare again to bring Dreamliner 9 mwaka 2023 mwaka 2024. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa biashara ya ndege, ndege hainunuliwi hivi hivi. You buy a slot; Unapo-buy a slot wanaweka kwenye kiwanda jinsi ndege zinazvyokwenda kama inafikia time yako ndiyo ndege inatoka. Kwenye kiwanda kama umeweka, wana-plan vizuri kwamba, itakapofika wakati wa kuweka engine, engine itakuwa imetolewa Rollsroyce imefika kwenye kiwanda inafungwa pale. Pale itakapofika, wewe ndio unahangaikahangaika, inafika wakati wa kuwekewa engine, engine hazipo, huwa hawasubiri. Inapita, engine itakwenda ifungwe huku pembeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo sababu ndugu zangu hapa wakati fulani wakati tunaleta ile Dreamliner 8 ya kwanza kwa sababu tuliinunua haraka haraka time ya kuiwekea engine ilikuwa imeshapita, slot yake ikawa imepita, engine zikafungwa nje watu wakaanza kusema aah, mmenunua ndege ambazo zina engine siyo za Rollsroyce, kumbe ile tumenunua slot ilikuwa ni too short, muda ukawa umepita wa kufunga zile engine zikafungwa badaye. Hivi, hamkuona aibu siku zinafika hapa na zina Rollsroyce? Hao ninaowasema wanajijua. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie umeme. Umeme tulionao sasa hivi we are looking at 2,150 Megawatt, very shortly, lakini kwa nchi kama ya kwetu kama kweli tutafuata mipango tuka-plan kama ninavyoshauri, huo hautatosha. Lazima tuwe na mixture. Maji yakikauka kama inatokea, siombei hilo, lazima tuwe na alternative. We should be thinking again kwenye mipango yetu ya viwanda hii, tuwe na umeme mwingine mkubwa wa level ya at least three thousand, five thousand Megawatt za makaa ya mawe. Leo hii tukianza kutengeneza, kufua vyuma hapa, umeme unaohitajika siyo huu mnaozungumzia. Kiwanda kimoja kinaweza kikahitaji 200 Megawatt na ndivyo hivyo viwanda vikubwa tunavyovizungumzia. Hapa mliokaa mbele, kaeni kwa pamoja, chakateni, tusitoe nafasi kwa watu ambao hawana environment nzuri kama sisi kupata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina mfano mmoja, kuna kiwanda hapo nchi jirani sitaki kuitaja, nyuma yake kimeandikwa his excellence something her, halafu mwisho kuna e; wamejenga kiwanda na kilikuwa kijengwe hapa. Kinachoniuma zaidi, sasa hivi wanatengeneza magari ya kutumia umeme nchi hiyo na hao watu I brought them here. The bureaucracy we have in our system is so bad, mwishowe wakaenda Rwanda. Volkswagen sasa hivi zinatengenezwa Rwanda, ilikuwa kiwanda kijengwe hapa. Hebu tupunguze hiyo bureaucracy. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie kwa kumalizia, anayejenga kiwanda hapa, hatakinyanyua kwendanacho. Hebu punguzeni hizo bureaucracy. Kama ataleta figisufigisu na kutaka kutuibia, hatakibeba, mwondoeni, wekeni watalaam wengine, Watanzania watakuwa wamejifunza, wataendeleza hicho kiwanda. It should not take six months ku-discuss issue ya kiwanda. Anaambiwa nenda hapa, nenda hapa, nenda hapa. Hivi kwa nini wenzetu wana-discuss mara moja mara mbili?

Mheshimiwa Mwenyekiti, I have so many bad experiencies ya kuleta wataalam au viwanda hapa halafu mambo yanakuwa hivyo hivyo, tubadilike. We should be business minded halafu wote tutumie coconut; wote humu ndani. Nilikuwa namsikiliza Waziri mmoja kwenye Baraza la Obasanjo, Mnaigeria, anazungumzia jinsi ambavyo tunasitasita na jinsi ambavyo hatuwezi kutoa maamuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumbukeni, dakika moja ikipita, ukitaka kuirudisha nenda kaburini. Utaikuta kaburini umeshakufa, kwa sababu ikishapita unasogea kaburini, ikishapita dakika nyingine unasogea na wote jinsi tunavyosherehekea mwaka mpya, yaani sherehe za kuzaliwa, kumbuka unasogea kaburini. Ahsante sana. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Kicheko/ Makofi)





















Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii. Vilevile nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa jinsi ambavyo amekuwa mwema pamoja na matatizo niliyopa sasa ni mzima kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu wa Spika, nianze kwanza kwa kuipongeza sana Serikali kwa uamuzi wake wa kuhakikisha kwamba inajenga miundombinu itakayowezesha uchumi wetu kupaa. Serikali imejikita katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na reli, tunakuwa na viwanja vya ndege, tunakuwa na barabara na tunakuwa na mashirika ambayo yanaweza kweli kweli kuonekana kwamba ni mashirika ambayo yana nia ya kuonesha kwamba tunajenga uchumi wa viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kikubwa ambacho nikiseme ni jinsi ambavyo Serikali imeweka kipaumbele kuhakikisha kwamba inatumia fedha zake za ndani. Hili nilisisitize kwa sababu kuna watu hapa wanasema kwamba kukopa si fedha za ndani. Hicho ni chanzo kingine katika kuhakikisha kwamba unajipatia pesa katika Serikali yako. Aidha, unaweza ukakusanya ushuru, unakusanya pesa na kupata revenue. Vilevile unaweza ukakopa ukapata hizo pesa na baadaye utalipa kwa kutumia pesa zako za ndani. Kwa hivyo kukopa ni pesa zako za ndani.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, pamoja na pongezi hizo niangalie tu namna ambavyo tunaweza tukahakikisha kwamba uchumi wetu unapaa kwa haraka sana. La kwanza ni linkages. Tunapojenga reli, tunapopanua bandari ni lazima tuangalie ni kwa namna gani hiyo bandari itaweza kuharakisha uchumi wetu. Huwezi kuwa na bandari iliyo nzuri halafu mizigo inafika huna mahala pa kuiweka. Kwa hiyo, dry ports ziwekewe umuhimu unaolingana na jinsi ambavyo tunapanua bandari zetu, ikiwemo dry port ya pale Fela katika Jimbo la Misungwi.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, vilevile niipongeze Serikali kwa kuweka umuhimu wa pekee katika kuhakikisha kwamba Shirika letu la Simu la TTCL linaimarishwa. Nizungumzie umuhimu uliopo kwa Shirika la TTCL na tuangalie ni kwa namna gani Serikali iliangalie shirika hili kwa umuhimu wa kipekee.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo hii tukiingia vitani Airtel wakaondoka, Vodacom wakaondoka na mashirika ya binafsi yakaondoka tutawasiliana vipi? Ni vyema tukaona huu umuhimu na tukaweka nguvu sahihi ya kuhakikisha kwamba Shirika letu la Simu la TTCL linapewa kila msaada na isiwe msaada tu wa pesa au vifaa kwa sababu matatizo mengine yanatokana na namna ya uendeshaji, na hili nitajaribu kulizungumzia na nitoa ushauri kwa Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu wa Spika, ushauri wa kwanza ni kuhusu usimamizi na katika kusimamia niombe Serikali iangalie uwezekano wa kuwa na mfumo wa eyes on hands off. Serikali isiingilie ingilie haya mashirika hasa hasa yale ambayo Serikali imeya-own kwa asilimia kikubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sioni kwa nini kama Serikali imejenga ikaweka bodi imara na bodi yenyewe ikaajiri Mkurugenzi au Mtendaji Mkuu imara, na kukawa na mfumo mzuri wa mawasiliano kila siku Katibu Mkuu au Waziri aende kuweka mkono wake kwenye shirika hilo. Yeye Waziri, Katibu Mkuu na Wizara mama ihangaike na kuhakikisha kwamba tuna sera zilizo sahihi na hizo sera zinajengewa mfumo wa utekelezaji na hao wajumbe wa Bodi pamoja na menejimenti yake kuweza kutekeleza ile sera ambayo Serikali ingependa itekelezwe.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, vilevile kujengwe mahusiano mazuri ya mawasiliano. Sioni kwa nini kama menejimenti wanakaa kila wiki kwa vyovyote vile wataitaarifu bodi kinachoendelea labda kila quarter, lakini Bodi nayo iwajibike kumweleza Waziri na Katibu Mkuu nini kinachoendelea kwenye shirika hilo angalau kwa muda ambao watakuwa wamejipangia. Hapo kila mtu atakuwa ametekeleza wajibu wake yake bila kumwingilia mwingine. Tunaangalie vilevile nilikuwa nakizungumzi issue ya linkage, hii ni kitu muhimu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa unakuta tunahangaika kutengeneza reli, reli inapokuwa inajengwa kutoka Dar es salaam kuja Morogoro unaweka reli ya umeme. Ukishafika Morogoro kuja Dodoma kwanza tofauti ile standard gauge na ile reli iliyopo zinatofautiana. Sijui unaanza kupakua hiyo mizigo uweke kwenye ile reli nyingine ile ya zamani na vichwa vile vya … Mimi nadhani kuwe na mpango ambao unakuwa ni wa jumla utachukua muda, lakini mnakuwa na umuhimu wa kusema kwamba tutajenga reli kutoka Dar es Salaam mpaka Kigoma, tutajenga reli kutoka Dar es Salaan mpaka Mwanza.

Mheshimiwa Naibu wa Spika, kitakachokuwepo pale ni kwamba kutoka Dar es Salaam kwenda Morogoro itachukua muda huu; na kutoka Morogoro kwenda Dodoma itachukua muda huu na Dodoma kwenda Mwanza au kwenda Kigoma itachukua muda huu. Na katika muda huo lazima kuwe na mipango thabiti ambayo tunasema kwamba hiyo ni transition period ambayo itakuwa inaeleweka kwa wafanyabiashara na watu wenye viwanda nchini ambapo watakuwa na matarajio yanayoeleweka, na mipango hii ifuatwe.

Mheshimiwa Naibu Spika, maana kwanza nimeipongeza Serikali kwa namna ya kutafuta revenue.

Hakuna sababu ya kuanza kujenga nusu nusu wakati hujui kinachofuatia na huna mpango wa kupata hela. Ni vyema ukawa umejipanga kwamba nikitoka Dar es Salaam kufika Morogoro nitakuwa nimepata hela za kutoka Morogoro kwenda Dodoma na nikianza kujenga kutoka Morogoro kwenda Dodoma nitakuwa nimepata hela za kutoka Dodoma kwenda Tabora. Tusiwe na mipango ya zima moto. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nisisitize hili la usimamizi wa taasisi na ili watu wengi hatuliwekei umuhimu na hatujui madhara yake. Sielewi kwa nini kwa mfano TCRA ambayo ni shirika ambalo kwa vyovyote vile kulingana na sources za funding yake lazima litajitegemea. Kwa hiyo, pale kinachotakiwa ni kuwa na bodi ambayo ni imara yenye watu wenye kuwaza mawazo mapana. Yale yaliyoko kwenye utaratibu au kwenye sheria TCRA hayo ni ya kawaida, mtu yeyote anaweza akayafanya.

Mheshimiwa Naibu Spika, these people should think beyond that na tunahitaji watu wanaoweza ku-think beyond that, na hicho ndicho kinatupa tatizo. Watanzania wengi tunajaribu kuwaza leo nitakula nini na jioni nitakula nini. Tukitaka kuendelea ni lazima tuwaze leo tutakula nini, kesho kuna nini, kesho kutwa chakula kitapatikana wapi na wiki ijayo nini tufanye. Haya mawazo ya kuwaza leo hii, halafu kesho hujui, kesho inapofika ndipo unaanza kuwaza, tuondokane nayo.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia hotuba hii ya Mheshimiwa Waziri Mkuu. Nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa uhai na kuifanya afya yangu iwe njema mpaka sasa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwanza kwa kutoa pongezi kwa Serikali ya Awamu ya Tano. Juzi nilikuwa namsikiliza Profesa Patrick Lumumba wa Kenya anampongeza Rais wetu kama Rais na ametoa term mpya ya kiingereza, The Magufulification of Africa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile nimpongeze Waziri Mkuu kwa hotuba yake na usimamizi mzuri, lakini niipongeze Serikali kwa ujumla wake kwa jinsi ambavyo inatekekeleza the vision 2025, hasa hii awamu ya pili ya miaka mitano – mitano na utekelezaji wake unaonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Waheshimiwa Wabunge elimu tunaona sasa hivi inavyokwenda vizuri. Tunaona jinsi ambavyo barabara zinajengwa, tunaona ujenzi wa reli, tunaona upanuzi wa bandari, tunaona jinsi tunavyoendeleza afya hospitali nyingi au dispensary nyingi katika vijiji vyetu. Vilevile tumeona ndege zinavyonunuliwa kuhakikisha kwamba tunainua uchumi wetu. Ndege siyo tu kwa ajili ya usafiri, lakini wale wenzetu walioko katika sekta ya utalii watakubaliana na mimi jinsi tunavyopata ndege ndivyo tutakavyokuwa na watalii wengi na watakaokuwa wanaleta pesa katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tufanye nini, ili tuweze kuongeza kasi yetu hii ya uchumi. Kwanza kabisa Serikali iangalie upatikanaji wa resource. Resource siyo pesa tu ni pamoja na human resource na time factor. Nilikuwa nikisikiliza mazungumzo yalivyokuwa yanaendelea hapa, I think we are wasting a lot of resource inayoitwa time. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo la kusikitisha tunabishana vitu ambavyo viko obvious ni kwamba wote ni Watanzania na Watanzania wote tushirikiane na tulikubali kuungana. Tuendelee na hilo kwa msimamo huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa zaidi ambacho niweze kukizungumzia ni usimamizi wa resources hizi na shughuli tunazozifanya. Tunaweza tukaona tunafanya vizuri sana katika Serikali Kuu, kwa sababu tuna Wakuu wa Mikoa, tuna Wakuu wa Wilaya, lakini tukienda kwa wenzetu wa TAMISEMI ambao wanaenda chini ambako tunataka tuone maendeleo ya mtu mmoja mmoja hadi vijijini hali yetu siyo nzuri sana. TAMISEMI ukienda pale Wizarani kwa kweli, wanafanya vizuri sana. Nimpongeze sana Katibu Mkuu pamoja na Mawaziri wanafanya kazi nzuri, reaction yao ukipeleka tatizo lako ni instant, lakini ni vipi huku chini tume- fail?
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie tu namna ambavyo tunaweza tuka-improve. Wenzetu katika baadhi ya nchi wanasema ili uwe Diwani lazima uwe na elimu ya kiwango fulani, ili uwe Mbunge lazima uwe na elimu ya kiwango fulani, lakini sisi tukifanya hilo tutakuwa tunavunja Katiba yetu, lakini kuna upande mwingine kwa sababu kuna wanasiasa na kuna watendaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hawa watendaji katika Halmashauri zetu, hawa Wakurugenzi tunawapataje? Wenzetu hawa walioko katika Wizara husika Wakurugenzi hawa wanapatikanaje? Au ni hawa wanaotuita sisi kuwa msiwasikilize wanasiasa, wakati Wakurugenzi wengi walikuwa wagombea wakashindwa kupata nafasi, kwa hiyo ni wanasiasa waliokosa nafasi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa sheria hii mpya iliyokuja, ukitoka kwenye utendaji ukaenda kwenye siasa, you will never go back kwenye utendaji, baki huko huko. Umeshindwa umeshindwa, umepata, umepata na ndivyo wenzetu wanavyofanya na lazima hili liwekewe mkazo, ili tuweze kuhakikisha kwamba, tunakuwa na Serikali inayosimamiwa vizuri. Tunakuwa na sera nzuri, lakini usimamizi wake unakuwa na mapungufu. Hilo nadhani tutaliangalia zaidi na wenzetu wakiliangalia vizuri katika area ya monitoring and evaluation. Sasa monitoring and evaluation kwa kiswahili chake kizuri sina uhakika kwa sababu kiswahili kilianzia huko Pwani, kikapita Morogoro wakachakachua, hapa Dodoma wakachakua, kilipofika Mwanza mimi sikumbuki. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie zaidi katika eneo la Watendaji na Madiwani. Madiwani wetu ni watu ambao wamepata Udiwani kwa sababu wana uhuru wa kuweza kutafuta udiwani na wakachaguliwa katika maeneo yao katika Kata zao au kwa kupitia Viti Maalum. Lakini Watendaji hapa kuna issue, na hapa Serikali yetu kupitia kwa Waziri Mkuu lazima tujipange vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kichwa changu na kichwa cha Jenista Mhagama ni vichwa viwili tofauti kabisa na uwezo wetu wa kufikiri uko tofauti kabisa, kwa hiyo ni vema tukapima, tukahakikisha kwamba pale anapofaa Jenista Mhagama aende Jenista Mhagama, pale anapofaa Kitwanga aende Kitwanga, lakini hii ya kubeba jumla jumla na wakati mwingine ndugu zetu ife, siwezi kukubaliana na hilo na bahati nzuri ukiwa msema kweli hata ukikaa pazuri watakuondoa tu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiwa unatenda haki kwa kila mtu hata ukikaa Koromije watakuondoa wakupeleke Mtwara. Kwa hiyo, niweze kusema ukweli na iweze kueleweka na ijulikane kabisa hawa wanasiasa katika Halmashauri zetu tuwaacheni wako pale kihalali. Lakini watendaji wetu let us choose the people who are right to every post. Tujipime, tujiangalie, tujitazame. If you are doing the right thing everybody will clap for you. Kama unafanya ubabaishaji wako, watasema huyu naye. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu yetu izungumzwe as a system, isizungumze kama chunk of shule ya msingi, shule ya sekondari, izungumzwe as a system, mfumo mzima and let us produce real na tusijali, wenye akili wapewe resource waweze kuitumikia nchi hii. Wanaozembea zembea wasipewe, after all nchi haiendelezwi na kila mmoja, watu watano wanaweza wakaendeleza nchi. They think, they deliver, they influence others and the country move. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naku-address wewe nilinde tu hawa wasinisumbue. (Kicheko)

Labda niende kwenye Wilaya yangu kwenye Jimbo langu. Kwanza kabisa nianze kwa kuwapongeza TARURA. TARURA wameanza vizuri sana. Wakati tuna Idara ya Ujenzi tu katika Halmashauri zetu tulikuwa na matatizo kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Looh! nilikuwa na mambo mengi lakini sasa sijui nitasemaje. Nizungumzie maji katika maeneo ya Kanyerere, Koromije, Mamae. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakuomba tu nitaomba tena nafasi katika Wizara zinazohusika niweze kuchangia. Tuongeze tena, turudishe tena ziwe dakika kumi na tano jamani. Ahsante sana.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Nishati
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze tu kwa kusema kwamba unapozungumzia Serikali ya viwanda halafu huna umeme ni sawasawa na binadamu anayeishi halafu hakuna hewa. Hilo ni wazi, kwa hivyo niipongeze sana Serikali ya Mheshimiwa Rais John Joseph Pombe Magufuli kwa juhudi wanazozifanya za kuhakikisha kwamba tunajenga Serikali ya viwanda na umeme upo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kikubwa ambacho nitakizungumzia na nitatoa ushauri, kwanza ni namna gani tuwe na umeme wa kutosha. Huu mlolongo wa kusema megawatt 20, megawatt 40 forget about it, zungumzia megawatt 2,000 za Stiegler’s Gorge, sasa hivi tuanze mpango mkakati wa kuweka umeme wa makaa ya mawe megawatt 5,000. Haya mambo tunayoambiwa eti tukienda kwenye makaa ya mawe tutachafua hewa, nenda Marekani, Uingereza umeme wanaotumia percentage kubwa ni upi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, teknolojia imebadilika, tuwe na mpango mkakati wa ku-generate umeme mkubwa wa makaa ya mawe na tutajenga teknolojia inayoweza ku- absorb zile fusion ili zichukue zile fumes zote kusiwe na matatizo. Faida kubwa tutakayopata, wananchi wengi watapata kazi katika maeneo hayo, miji iliyopo karibu na pale itakuwa imeendelea na umeme tutakaokuwa tuna- generate ni wa bei nafuu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, duniani umeme wa bei nafuu ni maji na mkaa. Halafu hao Wazungu wanao-generate umeme wa mkaa wanatudanganyadanganya hapa, danganyweni ninyi siyo Kitwanga. Ni lazima tufikirie, tuwe na uwezo wa kujua teknolojia hii tutaipataje lakini kila siku tunalalamika hapa, ninyi mmekuwa watalaam sana kuliko Wazungu ambao wana umeme wa makaa ya mawe miaka nenda rudi na bado wanaishi tu na wana afya nzuri hata wakati mwingine kuliko hata sisi? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani lazima mje hapa na mpango mkakati, hatutaki hizi megawatt 200 ama 300, tunataka big. Tumepanda kutoka megawatt 1,450 mpaka 1,517, hilo Mheshimiwa Waziri mdogo wangu usilitaje, hilo siwezi kukusifia nalo. Come with big kama ulivyo big, you are a good person and you are doing wonderful job na hii miradi midogo mingi, it is costing us a lot kui-manage. Yaani una-manage mradi wa megawatt 20, una Afisa Utumishi, Engineer na mambo mengine mengi.

Ninaongea na Mwenyekiti, tatizo kubwa la watu wa huku wanapenda kusifia vinavyofanywa na CCM wao wamelala tu. (Kicheko/ Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi REA kila mtu anasifia lakini nazungumza with this feeling because I love my country. I am ready to die for it and there is nobody can change me on that. Kama ulikuwa hujui kwamba najua Kizungu njoo nikufundishe Kisukuma. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala ambalo lipo hapa kila mtu analisema, ukosefu wa pesa, hivi kwa nini unakosa pesa? Wewe kama ni Waziri wa Fedha halafu unasema hatuna pesa, ondoka hapo. Wewe kama ni Mbunge wa Jimbo fulani wananchi wako wanasema unajua kuna matatizo, ondoka hapo. You are been a human being and you are given that opportunity to save that place, because people trust you and you must think. No thinking, get out of that place. (Makofi/Kicheko/ Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, niwaombe ndugu zangu Wabunge jambo la kwanza ambalo litatufanya tuisaidie nchi yetu ni ku-think and implement. Work hard, be ready to die for what you requested for.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, niwaombe ndugu zangu wa REA, we are here and we have brain. Mkiwa na upungufu wa mawazo tupo. Watanzania lazima tuweze kusaidia mahali popote, tuache kulalamika. Unalalamika kwa nini, hujala? Kula, shiba, fanya kazi. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata mimi asubuhi sikuwa na hela, nimekwenda kufanya kazi nimepata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami niweze kuchangia bajeti hii. Kwanza nianze tu kwa kusema, kwa kweli bajeti hii ni bajeti iliyotengenezwa, ikapikwa, ikawekwa, ikachujwa na ikatoka kuwa bajeti ya uchumi wa viwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kabla sijaendelea naipongeza Serikali kwa kile inachofanya na Mheshimiwa Mpango pamoja na Naibu wake na wafanyakazi wote katika Wizara nawapongeza sana, bajeti yao ni nzuri kwa Taifa letu. Nianze kwa kutaja tabia za pesa. Tabia za pesa ziko hivi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa complement hiyo.

Mheshimiwa Spika, tabia ya pesa ziko mbili ya kwanza pesa huwa hazitoshi, pili pesa huwa haiishi utamu. Kwa hivyo, ndugu zangu wa mkono wangu huku wa kulia kila siku wanapokuwa wanalalamika kwamba tuna madeni ni kwa sababu pesa siku zote haitoshi na utamu hauishi. Ni jambo ambalo lazima tujivunie kwamba bajeti hii imelenga katika ule mpango wa 2025, tuwe uchumi wa kati vilevile tuwe na viwanda.

Mheshimiwa Spika, ukiangalia mapunguzo katika elimu hii ni katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na resource inayoitwa human capital. Hawa watu tutakaokuwa tunawahitaji kwenye viwanda vyetu wasiwe ma-expert tuwajenge kutoka hapa, kwa hivyo tunapopunguza katika daftari, tunapopunguza katika vifaa vya elimu tunataka tuwe na wataalam wa kwetu, Watanzania watakaoweza ku-serve katika viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa tufanye nini cha ziada, kwanza tuache hizi biashara ndogondogo, naipongeza sana Serikali kwa kile ilichokifanya hasa kwa upande wa simu. Nakumbuka nilipokuwa Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia mwaka 2011 nili- suggest kwamba tuweke mitambo TCRA itakayo- monitor matumizi ya simu ili tuweze kujua kila senti inayotumika je, inalipiwa kodi, tumechukua miaka mingi kidogo.

Mheshimiwa Spika, nikiwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini mwaka 2013 nilipendekeza kufunga flow meter kwenye upakuaji wa mafuta, nikapendekeza vilevile tukawa tumeunda timu ya kuweza kusaidia tuwe na single off-loading point, najua ndani yetu humu ndani wako Wabunge wengine ambao wanafanya biashara za mafuta na wanaipinga sana hiyo single point off-loading, naomba hili tulitilie mkazo sana.

Mheshimiwa Spika, flow meter zifungwe na iwe ni sehemu ya off-loading kwenda kwa wale matenki ya watu siyo pale wanapopokea, kwa sababu wanasema na wanadanganya kwamba kuna evaporation, kuna asilimia kubwa inatokea kwamba mafuta yanapotea, tuhakikishe kwamba tunachukua pesa zetu pale tunapowapelekea hawa wauzaji. Kwa hivyo, mafuta yatakapokuwa yanapakuliwa kutoka kwenye meli yaende sehemu moja, halafu kutoka kwenye sehemu hiyo sasa tunawapelekea hawa sijui OILCOM, MOIL sijui PUMA ndipo wapelekewe na tunapowapelekea tayari tumeshachukua pesa zetu. Nadhani hili litatusaidia sana kuweza kuongeza mapato katika Serikali yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, vilevile niiombe Serikali kwa ujumla to work as a team, naomba ndugu zangu wa viwanda na biashara, ndugu zangu wa ardhi na ndugu zangu wengine tuwe na ushirikiano. Mwekezaji anapokuja isichukue siku 40, miezi miwili mpaka anapata kibali cha kuanzisha kiwanda. Inashangaza pale ambapo mwekezaji anataka kutengeneza magari anaacha kuwekeza Tanzania anakwenda anawekeza Rwanda! Wakati ukitaka kupeleka vitendea kazi pamoja na raw material Rwanda ita-incur cost nyingine kuvisafirisha kwenda kule.

Mheshimiwa Spika, nadhani tuliweke incentive sana kwenye madini, incentive hizo tuziweke kwenye viwanda. Halafu niwaambieni kitu kimoja madini resources kubwa iko ardhini kwetu, akishachimba akaitoa haiwezi kurudi, lakini resources kubwa kwenye viwanda ni capital yake atakayoileta na akishajenga kiwanda hawezi kukibeba akakitoa akaenda nacho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hivyo lazima tuwe na mipango na sera ambazo ni za kuvutia zaidi kwa sababu after all hatuko stationary lazima kuwe na mabadiliko, tukimrahisishia akaleta kiwanda hapa, pale ambapo tutaona kwamba upande wetu labda hatukuwa tumefanya vizuri sana, bado we can negotiate, we are negotiating now kwenye madini, lakini tutaendelea kuwa mtu akiwa ameleta kiwanda atakuwa ame-employ watu wetu, atakuwa amelipa tax, hawa watu walikuwa employed na wenyewe watakuwa wamelipa tax kupitia kwenye pay as you earn.

Mheshimiwa Spika, tutumie uzoefu wa sehemu zingine kuweza kuona kwa nini sisi ukiangalia Kenya, ukiangalia Tanzania, Kenya bajeti yao ni 30 billion USD, Tanzania ni 14 billion USD why? Nasi tu wengi na vilevile ni nchi kubwa! Kwa hivyo ni lazima tuhakikishe tunaweka miundombinu inayopendeza au inayovutia ili tuweze kuwashinda wenzetu.(Makofi)

Mheshimiwa Spika, PPP imezungumziwa sitaki kuirudia, kwa mfano tumezungumzia reli ya kutoka Mtwara kwenda Mbamba Bay sijui muda gani.

Mheshimiwa Spika, labda niseme tu kwamba, tuhakikishe kwamba hiyo reli inavutia, uzoefu aliousema Spika umenikutanisha na watu wengi sana. Pale ambapo tutahitaji kusaidiana maana yake Mtanzania lazima ui-serve nchi yako kutokea mahali popote. Mimi nina watu wa kutosha zile contacts zangu nikiwa Bank of Tanzania bado ninazo na naweza nikawapa watu wapo wengi tu wanaotaka kuwekeza hasa kwenye reli hiyo na maeneo mengine mengi.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Mheshimiwa Spika, lakini sijasema kitu kimoja tu, naunga mkono hoja asilimia 108. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nikushukuru sana kwa nafasi. Kwanza nianze kabisa kwa kuipongeza Serikali kwa mpango huu ambao kwa kweli umeendana na Vision yetu 2020-2025 ambayo tumeikatakata katika vipingili vya miaka mitano-mitano. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na hili suala tunalosema kwamba pesa zimepungua. Kwa kweli, nilichukua muda kuzungumza na wataalam wa Benki Kuu walichoniambia money in circulation zinaendana na uchumi na hakuna hata siku moja tumeweza kupungua bali siku zote pesa zinaongezeka. Ikabidi nipige kichwa niweze kufikiria ni kwa nini watu wanasema pesa zimepungua? Tofauti iliyopo sasa hivi na zamani ni kwamba kila hela unayoipata ni lazima uwe umeifanyia kazi. Siku za nyuma wakati mwingine hii magumashi zilikuwa nyingi tunapatapata hela ambazo tulikuwa hatuzifanyii kazi, tufanyeni kazi pesa tutapata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuunge mkono huu mpango kwa sababu wote tuliupitisha kama Mpango wa Miaka sasa umekuja katika mpango wa mwaka mmoja ili tuweze kufanya utekelezaji wake. Nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu kwa jinsi anavyotekeleza maana tukianza kufikiria wengine kabla hatujazaliwa reli iliyokuwepo ilijengwa na Mjerumani lakini kwa sasa hivi tunajenga reli hii wenyewe na tunaijenga sisi Watanzania kwa pesa zetu, hata kama tumekopa. Unaweza ukawa una hela zako kwa kukusanya kodi au unaweza ukawa na hela zako kwa kukopa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kuangalia nini nikishauri Serikali ili tuweze kuweka tija zaidi katika uchumi wetu. La kwanza ni katika utekelezaji, je, ni namna gani tutaongeza money in circulation ndani yetu? Ni kweli tuna miradi mikubwa, kwa mfano, tuna ujenzi wa reli yetu, makampuni yanayojenga pale ni ya nje, malipo yatakayofanyika pesa zile zinaweza zikaenda nje, tulenge nini sasa? Kwa sababu Serikali ni moja, Wizara ya Ujenzi, Wizara ya Ardhi na watu wote, pale tunapokuwa tunamuajiri mkandarasi wa nje tuhakikishe kazi ambazo zinaweza zikafanywa na wakandarasi wa ndani, wapewe wakandarasi wa ndani ili wakilipwa hizo pesa zibaki hapa na ziende kwenye mzunguko. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuangalie katika upande wa madini. Ukiangalia akina nani hasahasa wanaweza ku-contribute, ukiangalia mwenye mradi wa madini, asset kubwa aliyonayo ni madini yaliyopo chini, kinachofuatia ni ile pesa, kinachofuatia ni ule utaalam aliokuwanao. Sasa madini kama yana-contribute sehemu kubwa basi wenzetu wa Wizara ya Madini wawaangalie wachimbaji wadogowadogo na wachimbaji wa kati ambao ni Watanzania tuwawezeshe waweze kuchimba na hela nyingi zibaki katika maeneo yetu. Hicho ndicho ninachoweza kuishauri Serikali katika mpango wetu huu kwa ajili ya ku-make sure kwamba hizi pesa tunazozipata na huu uchumi mzuri ambao tunao sisi Watanzania leo hii unawafaidisha Watanzania hata kule Koromije. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuangalie sekta ya utalii. Niiombe Serikali iweke nguvu sana katika Shirika letu la Ndege la Tanzania. Watu wanazungumzia Shirika la Ndege la Tanzania lakini contribution yake huwezi ukajua itakuwaje pale litakapokuwa na nguvu. Kwa mfano, chukua jirani zetu wa Kenya, wanaruka moja kwa moja mpaka New York, wanaleta watalii moja kwa moja wao wenyewe. Nchi yetu kama itakuwa na Shirika la Ndege lenye uwezo na lenye nguvu watakaporuka mpaka pale Julius Nyerere International Airport kutakuwa na ndege nyingine itakayoruka kuwachukua watalii kuwapeleka Mwanza ambapo ni karibu na Serengeti. Watakapowafikisha pale Mwanza kutakuwa na mtu kutoka Koromije mwenye Pick-up yake, mwenye Landrover yake, atakayewabeba watalii na kuwapeleka Serengeti. Uchumi utakuwa umeshuka mpaka kwa mtu wa Koromije kule chini. Wasiojua ni wale wa upande huu, eleweni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nitoe mfano mzuri mmoja tu ambao watu wataweza kuona jinsi ambavyo pesa zitazidi kubaki hapa Tanzania. Kuna Kampuni ya ESTIM inayojenga barabara kutoka Ubungo mpaka nadhani Kibaha, ile ni kampuni ya Kitanzania na pesa zitakazopatikana pale nyingi zitabaki, lakini ukipita pale utafikiria ni kampuni ya nje, hamna tofauti. Kwa hivyo, niwaombe ndugu zangu waliokaa huku mbele, mliokaa huku mbele kidogo mlitambue hilo na mshirikiane na mimi nilikuwa nikikaa zamani, bado nyie ni wenzangu. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudie tena kusema Mtanzania anayependa nchi yake ataitumikia nchi yake mahali popote. Let me say this thing once and for all, I have never been in this House drunk, I will never do that and it will never happen. Mnaoendelea kusema hivyo, endeleeni na mtaendelea mpaka Yesu atakapokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa complement. Niendelee kuzungumzia kitu kingine ambacho ni cha muhimu sana kwa Taifa letu, ni hili tunalolizungumzia la Stieglers’ Gorge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naunga mkono hoja.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Maji na Umwagiliaji
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniweka hai. Kwa sababu leo ndiyo nasimama kwa mara ya kwanza kuzungumza Bungeni hapa baada ya kupata matatizo ya kuugua, naomba nitoe shukrani zangu za dhati kabisa kwa Wanamisungwi ambao waliacha kufanya kazi zao wakaamua kuwaomba Mapadre na Wachungaji kwa siku mbalimbali kuweza kuniombea niweze kupona. Siyo Wanamisungwi tu, nimshukuru sana Mheshimwa Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kwa support na kwa jinsi walivyoweza kufika kuniona wakati nikiwa naumwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimshukuru sana Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Zanzibar, Mheshimiwa Karume aliyefika kuniona. Namshukuru sana Makamu wa Rais wa Zanzibar, wao wanamuita Makamu wa Pili, mimi sitambui hilo kwa sababu hakuna wa kwanza, kuna Makamu wa Rais tu Zanzibar. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana wewe pamoja na Bunge lako Tukufu kwa kuniombea. Wewe mwenyewe ulifika zaidi ya mara moja kuja kuniona, nakushukuru sana pamoja na timu yako. Nawashukuru sana Wabunge wote kwa jinsi ambavyo mlifika na mliniombea na leo hii nazungumza nikiwa najidai. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwashukuru sana Watanzania wote kwa sala na maombi yao. Jamani niseme hivi, kabla hujafa hujaumbika na hapa ulipo kwa sababu unatembea mshukuru Mwenyezi Mungu na utumie dini yako uendelee kumuomba. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya shukrani hizo, niseme tu kwamba ni watu wengi sana walifika kuniona na kunitakia kheri, siwezi kuwataja wote lakini kwa sababu ya muda mfupi na nadhani huu hutauweka kwenye zile dakika zangu kumi. (Kicheko)

Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kujikita kwenye hoja, leo sitaondoka hapa kwenda Ihelele kuwashawishi wananchi wa Misungwi kwenda kufunga ule mtambo unaotoa maji sehemu mbalimbali kwa sababu leo nitatoa shukrani kwamba ombi langu lilisikilizwa na wananchi wa pale Ihelele ambapo mradi mkubwa wa maji unatoka, sasa hivi kuna mradi lakini nitazungumzia matatizo yanayojitokeza. Hilo litakuwa zaidi katika kutoa ushauri wangu kwa Serikali yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatizo kubwa katika miradi hii ni muundo. Ukiangalia muundo wa namna miradi inavyoendeshwa ni finance based, pesa zikipatikana wanaanza kusema tutapeleka kijiji hiki, wilaya hii na wilaya hii, kitu ambacho kinasababisha sasa utekelezaji wa muda mrefu unakuwa tatizo. Nitatoa mfano mdogo tu katika Mkoa wa Mwanza na particularly katika Wilaya yangu ya Misungwi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna miradi mingi ambayo utakuta meneja wa mradi, engineer wa mradi na vitu kama hivyo, yote haya yapo katika utawala wakati ambapo miradi hii ingekuwa consolidated halafu kukawa na individuals ambao wanasimamia miradi in particular, mambo ya Afisa Utumishi na Meneja wa Mradi yote yasingekuwepo. Kungekuwa na Meneja wa Mradi ambaye ni mkubwa kiwilaya au kimkoa lakini waone namna ambavyo kutakuwa na muundo mzuri.

Mheshimiwa Spika, nichukulie mfano wa Mkoa wa Mwanza. Kuna mradi wa Ukerewe, kuna mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda Kwimba kupitia kwa ndugu yangu Mheshimiwa Ndassa na kuna mradi wa maji wa Misungwi; Misungwi tuna miradi minne na kila mradi una meneja, hii yote ni gharama matokeo yake sasa wakishaondoka pale uendeshaji unakuwa ni tatizo.

Mheshimiwa Spika, nichukulie mfano pale Wilayani Misungwi kuna mashine nzuri sana zinazopeleka maji Ukiliguru lakini customer base ya Ukiliguru ni watu wachache. Waki- pump maji kwa wiki mbili, bili ya umeme kwa mwezi inakuja shilingi milioni 10, shilingi milioni 10 zitalipwa na watu 200 wanaokaa Ukiliguru?

Mheshimiwa Spika, halafu siyo tu hapo katika Wilaya yangu, kuna mradi sasa wa Wilaya unaotoa maji Nyahiti kupeleka Misungwi, huo nao ni mradi. Kuna mradi huu ambao sasa hivi unaitwa mradi wa kupiga kelele Kitwanga Bungeni unaotoa maji Ihelele kuja Mbalika mpaka kufika Misasi, huo nao ni mradi unajitegemea. Sasa hivi mradi huo una matatizo, baadhi ya wakandarasi hawajalipwa na naomba tukishatoka hapa tuweze kuzungumza na wenzangu wa Wizara waweze kuniambia wamefikia wapi kuwalipa wakandarasi. Mheshimiwa Waziri nakushukuru ulifika katika Wilaya yetu ukaweza kuahidi kwamba pesa zitatolewa lakini mpaka sasa hivi hazijafika.

Mheshimiwa Spika, ushauri wangu, tujaribu kuona katika Wilaya tuweke mfumo unaoeleweka, mfumo wa Dar es Salaam na maeneo yanayoizunguka ulivyowekwa, huo ndio the best. Sijui ni DAWASA sijui nini ile ya Dar es Salaam inahudumia Dar es Salaam, Bagamoyo na sehemu kubwa zinazoeleweka na kuna mpangilio. Je, kuna tatizo gani kwa Mkoa wa Mwanza kuwa na institution moja na hizi zingine zilizopo kwenye Wilaya zikawa subsidiary za institution hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tunamsifia sana Mheshimiwa Eng. Sanga kwa Mkoa wetu wa Mwanza kweli anafanya kazi sana. Ukienda pale Misungwi ukiuliza hamna jibu, ukienda Ukiliguru hamna jibu, unakwenda kwa Sanga ndiyo anaanza kukuelezea, aah, mimi pale sina mamlaka jaribu kumuomba Waziri kama naweza kupewa nguvu, kwa nini asiwe na nguvu siku zote? Kwa sababu kama tungekuwa na institution moja kwa Mkoa wa Mwanza zile za Misungwi, Sengerema na Ukerewe zikawa subsidiary ya hiyo MWAUWASA tungeweza kuwa na sehemu moja inayosimamia miradi yote na hii mipangilio yote ingekuwa mizuri zaidi. Sasa nyie mkipata pesa mnaanzisha mradi na unakuwa unajitegemea, mkishaondoka kwenye mradi hamna mwendeshaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa imefikia mpaka kwenye kata, Kata ya Fera wana mashine pale wana-pump maji lakini customer base ya Kata ya Fera ni wanakijiji. Sasa wanakijiji wataweza kweli kulipia bili ya umeme waweze ku-pump maji kila siku? Mimi nadhani hapa kidogo tuna tatizo, miradi hii isiwe finance based, iwe na organization zinazojitegemea na pesa zinazofika mnasema kwamba leo hii tunaweka pesa eneo hili na inasimamiwa vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

SPIKA: Ahsante sana Mheshimiwa.

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Muda umeisha?

SPIKA: Ndiyo, umeisha.

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Eeeh, naunga mkono hoja. (Makofi/Kicheko)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 – Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze moja kwa moja kuchangia ajenda hii muhimu sana, lakini nitaiangalia kwa mapana yake zaidi ya badala ya ufinyu unaoangaliwa na baadhi ya watu wengi na nitaiangalia katika upande wa uchumi nikizingatia zaidi balance of payment. Nataka nizungumzie ATC na SGR na kama nitapata muda nitakwenda zaidi katika maeneo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukianza na ATC, nizungumzie kimapana katika uchumi hasa tukiangalia tourism. Kwa mwaka 2017 tourism iliingiza shilingi bilioni 2.25 sawa sawa na asilimia 27 ya total export zote katika goods and service kwa nchi yetu. Kwa mwaka 2018 iliingiza Dola bilioni 2.45 sawa sawa na asilimia 29. Sasa tukiangalia ATC, nini mchango wake na utakuwa mchango wake katika tourism?

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiangalia sasa hivi, Kenya Airways inafanya safari tano kila siku kutoka Nairobi kuja Dar es Salaam na safari tatu kila siku kutoka Kenya kuja Zanzibar. Kwa nini wanafanya hivyo? Kwanini ATC isifanye hilo? Ni kwa sababu sisi tuliicha ATC. Sasa tuone umuhimu wa ATC katika kuchangia tourism katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tunapoangalia ATC kwa kusema kwamba watu wa Misungwi watapanda ndege, yaani nashindwa kuelewa, ni kufikiri kidogo sana. Tufikiri kiupana. Tukiangalia ATC pale itakapoanza kwenda katika far East kwamba iende India au China italeta watalii. Watalii watafika Dar es Salaam watachukuliwa watakwenda KIA, watakapofika KIA wale ndugu zangu wenye Land Rover, wale wenye Pick-up watawachukua watalii kufika karibu na Mlima Kilimanjaro.

Mheshimiwa Naibu Spika, watakapofika Mlima Kilimanjaro wale wananchi wa kawaida kabisa kule Kilimanjaro watakuwa wapagazi, watabeba ile mizigo ya watalii kwenda kupanda Mlima Kilimanjaro. Umemgusa raia wa mwisho kabisa na pale hujazungumzia ATC. Uone umuhimu ATC itakaosaidia katika uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuiangalie sasa ATC katika umuhimu wake regionally, halafu tutaangalia intercontinental inachangia vipi? Tutakapokuwa na ATC inaenda India ambayo ni shirika letu, maana yake sasa zile fedha ambazo zinachuliwa na mashirika ya nje kuleta watalii Tanzania zitakuwa zimeingia kwa ATC ambayo ni mali ya Watanzania na zitaongeza hilo pato kwenye tourism katika uchumi wetu. Watu hilo hatuwezi kuliangalia. (Makofi)

Mheshimiwa naibu Spika, siyo hivyo tu, tutakapokuwa tumetoka pale kwenye ATC, wale watalii watakapokuwa ni wengi zaidi wanakuja kwetu, pato la Taifa litakuwa limeongezeka zaidi. (Makofi)

Nawaomba ndugu zangu, badala ya kushambulia kununua ndege, tumpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu mwenye mawazo mapana. Anaona mbali zaidi, anaangalia kiupana zaidi lakini sisi tunaangalia kiufinyu kwa kuangalia ndege itabeba watu wa Misungwi. Hiyo siyo nia njema ya Rais wetu kuweza kuisaidia nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba Watanzania wote tumuunge mkono Mheshimiwa Rais wetu kwa kufanya kazi na kufikiri zaidi katika maeneo yetu. Tusianze kufikiri kidogo kidogo. Watanzania na ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, niwaombe sasa tuone ni kwa namna gani tunaweza kuisaidia ATC badala ya kuibeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi itaanza intercontinental flights, kwa maana itakwenda India na China kuleta watu zaidi, lakini biashara tunayoiangalia, tusiangalie utalii tu, tuangalie je, watu watakaotoka uwanja wa ndege watakuwa wametoka wapi? Sasa hivi kuna watu wanakuja pale Kariakoo kutoka Malawi, Zambia, Congo kufanya biashara. Sasa kama tutakuwa na ndege yetu ambayo itaifanya Kariakoo iwe ni Guangzhou ya Afrika, Guangzhou ya Afrika, maana yake ni nini? Maana yake utalii ambao unasababishwa na ATC utakuwa umeleta uchumi kukua zaidi katika nchi yetu. Kwa hiyo, tuangalie kwa mapana, tuache kuiangalia ATC kiufinyu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nishauri kwamba badala ya kuwa na hizi ndege chache ATC waangalia regionally, wa-focus zaidi sasa hivi, ndege hizi Air Bus ziwe ni za regional; ziende South Africa, Burundi, Rwanda, lakini wanunue tena ndege nyingine ambazo zitatusaidia sasa; hao watu wanaokuja kutoka kule watasambaaje katika nchi yetu? Kwa hiyo, waangalie uwezekano wa kununua ndege nyingine za aina hiyo kwa ajili ya local. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, International au intercontinental sasa hivi wameanza ku-focus kule Far East baadaye kwa mipango yao ya kati au ya jinsi wanavyoona waweze ku-focus Europe. Kwa hiyo, wanunue ndege nyingine kubwa zaidi ambazo ni sawa sawa na hizi Dream Liner ziweze kwenda Europe na sehemu nyingine. Vile vile, kwa baadaye zaidi tuweze ku-focus market ya Marekani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nisiishie hapo tu, kwa sababu ya muda niweze kuzungumzia umuhimu vilevile wa reli yetu katika transit trade. Again hii ni mawazo mapana ya Mheshimiwa Rais wetu. Mimi nampenda kwa sababu he think big na watu wengi tuna-think low halafu tuna-think very narrow hatumwelewi. Sasa niwaombeni, mimi nina-think big and I think wide, ndiyo sababu leo naamua kutoa shule hii muweze kuelewa. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, transit trade tukiiangalia tuone ni kwa namna gani ita-contribute kwenye uchumi wetu. Tunaposema transit trade tunaangalia nchi zinazopakana nazo. Mimi nashangaa wakati mwingine hatuwazi namna gani tunaweza kuzitumia hizi nchi tunazopakana nazo kukuza uchumi wetu zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiwa na reli ambayo itatoka Dar es Salaam kwenda Kigoma, Mwanza na pale Fela tukatengeneza Economic Zone, maana yake sasa mizigo itatoka moja kwa moja kwa haraka Dar es Salaam kwenda Mwanza. Ikisafika Mwanza pale, ndugu zetu wa Rwanda na Burundi watachukua ile mizigo kutoka pale Fela na kuweza kuisafirisha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama tutakuwa na Economic Zones, kwa mfano, tuwe na Economic Zone katikati ya Dar es Salaam na Dodoma ambapo tutakuwa na maeneo maalum ambayo biashara mbalimbali zitafanyika na tutaitumia hiyo reli sasa kusafirisha products zetu kwenda kuziuza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tutakuwa na Economic Zone nyingine, yaani business centers pale katika kwa mfano kati ya Dodoma na Tabora, maana maeneo yale sasa wakiwemo wafugaji, wakulima na wafanyabiashara wengi wakiwa na productions ambazo zinakwenda kwenye centre ambapo kuna businesses wanazozifanya, wasiwe na matatizo ya kuweza kusafirisha vifaa vyao au vitu vyao kwa ajili ya raw material kuja kufanya production. Waweze kupata usafiri wa rahisi na kitu kitakachoweza kutusaidia ni reli yetu hii. Kwa hiyo, Watanzania tuwaze na tuweze kufikiria namna gani hii SGR itatusaidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakumbuka reli… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kitwanga, muda wako umekwisha. Ahsante sana.

MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Nina uhakika wale wanaojua upande gani nausema wamepata shule yangu. (Makofi/ Kicheko)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2018 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020
MHE. CHARLES M. KITWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Kwa sababu mimi naongea pole pole, nimeomba wakubwa zangu waniongezee dakika kidogo. Naomba nizungumzie bajeti hii ambayo ni nzuri sana inayoendana hasa na ile vision yetu ya 2025. Vision 2025 ndiyo the plan. That is the plan, lakini hii vision imekuwa cascaded into strategic plan za miaka mitano. Tumeanza na kujenga misingi. Sasa hivi tunajenga uchumi wa viwanda ili tuende kwenye uchumi wa kati. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunapojenga uchumi wa kati we must sacrifices, kwa sababu hapo unachukua decision nzito na kubwa zinazokuwezesha kumlisha ng’ombe ili baadaye uanze kumkamua. Watu tunaanza kulalamika kwa sababu tulikuwa tumezoea ule uchumi tunaotaka kuondokana nao.

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu, ana long vision and wide. Nawaomba sisi ambao tumepewa nafasi za kumsaidia tuelewe anachofanya, nasi tuwe na long vision and wide ili tumsaidie sasa kuhakikisha kwamba tunafika kwenye huu uchumi wa kati. Hizi strategic plans za miaka mitano zinakuwa again cascaded into yearly operation plan. Hizi operation plans ndizo plans tunazoletewa sisi hapa kuziangalia. Hizi yearly operation plans ndiyo zinatuwezesha kutengeneza bajeti. Hii bajeti ina-support sasa kuweza kutekeleza hii miradi tuliyo nayo. Nafurahi sana kuona jinsi ambavyo tunakuwa na big project. Hizi big projects zimelenga kuhakikisha kwamba huu ndiyo ulishaji wa ng’ombe ili anenepe tuweze kupata maziwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mafanikio makubwa ambayo tumeyapata na hii sasa nianze kutoa ushauri kwa Serikali yangu. Cha kwanza, naishauri Serikali yangu iendelee kutoa elimu bure na kuwalipia wanafunzi wanaosoma Chuo Kikuu ambao wanapata sasa hivi mikopo yao bila matatizo. That is how you think big na unatekeleza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, haya mafanikio hatuyaoni, tunapiga kelele tu, lakini mafanikio ni makubwa sana kwa sababu hii ni mojawapo ya pillar ambayo inatuwezesha kwenye education tuwe na wanafunzi, tuwe na watendaji watakaokuwa ni wa kwetu tuliowajenga kwenye vyuo vyetu. Tumetoa hela zetu kwa ajili ya watakaokuja sasa kufanya kazi kwenye viwanda vyetu. Nampongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Elimu, anasimamia vizuri na hapo kwa kweli siwezi kusema sana pale. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuko kwenye umeme; niseme ukweli, hata kama wasio na macho wanaona, mabadiliko ni makubwa sana. Maendeleo ambayo yamepatikana kwa kuweka umeme vijijini yanaonekana, watu wote wanaona. Watu ambao sasa hivi wamekuwa active na wamekuwa knowledgeable kwa kutazama hata TV tu hizi ndogo, wanachomelea, wanaendelea kujipatia kipato kutokana na umeme kufika vijijini, lakini wengi wetu ambao tumekuwa na narrow mind na short vision hatuyaoni hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye health. Wananchi wetu wakiwa na afya kwanza watafanya kazi lakini zitakuwa ni resources za kununua product zetu ambazo sisi tunazizalisha. Ukiwa na wananchi wenye afya njema, wanafanya kazi, wanajipatia kipato, utaweza kuzalisha katika viwanda vyako na wananchi wataweza kuwa na vipato hivyo waweze kununua hizo mali na uchumi utakua.

Mheshimiwa Naibu Spika, nawaomba ndugu zangu ushauri tu wa health pamoja na vituo vya afya vizuri tunavyovijenga, dispensaries, hospitali zetu za Wilaya ambazo zinaonekana, Hospitali za Rufaa katika mikoa yetu ambazo zinaonekana, sasa tujikite kuwa na wataalam waliobobea na kuweka mfumo mzuri hao wataalam waliobobea waungane na utafiti wa wagonjwa. Pale mgonjwa anapoingia hospitalini isichukue muda mrefu kupimwa na kujua afya yake na kumwezesha aweze kutibiwa ili atoke haraka hospitalini aende kuendelea kuchapa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika na Watanzania wenzangu, niliseme hili linalotusumbua sana. Huko nyuma tulizoea sana kupata hela za magumashi, sasa hivi fanya kazi ndipo upate hela, bila kazi huwezi kupata hela. Ndiyo sababu imeandikwa hata kwenye vitabu vyetu vya dini, asiyefanya kazi na asifanye nini? Asile. Tufanyeni kazi, mambo ni mazuri, yanaendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nije la mwisho sasa katika ushauri wangu, good governance. Hili ni eneo ambalo kwa kweli tunahitaji kuongeza nguvu, ndilo linalotusababisha tusi- perform katika baadhi ya sekta. Tunahitaji tuhakikishe kwamba kila usimamizi, kila senti inayopatikana, ni senti ambayo inaenda kuzalisha au kutumika kama ilivyokuwa imepangwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika upatikanaji wa resources hizi za pesa, ziko za aina mbili; pesa zetu na pesa za misaada. Pesa zetu zipo za aina mbili; zile tunazokusanya kodi na zile tunazokopa. Tunapokopa pesa ni za kwetu, maana mbeleni tutazilipa kwa kutumia zile tulizokusanya. Kwa hiyo, tunapopata mkopo tuhakikishe ule mkopo tunautumia vizuri, tusiwe na hali ya kwamba tunawekewa masharti, unajikuta zile pesa nyingi zinarudi tena kwa yule aliyetukopesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitoe mfano mzuri tu kwa ndugu zangu wa Wizara ya Maji. Pale Wizara ya Maji kuna matatizo, maana kutokea Awamu ya Nne kulikuwa na mradi wa kutoa maji Ruvu kwenda Kimara. Kulikuwa na mradi wa Ukerewe, sasa hivi tuna mradi wa kutoa maji Shinyanga kwenda Nzega, Igunga na Tabora; na sasa hivi tuna mradi huu unaoitwa wa Wilaya 29, una matatizo. Kwa sababu pale kuna Mhandisi Mshauri ambaye kwa miradi yote niliyoisema ameshiriki na kushiriki kwake hakina tija sana kwenye nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba, nitakuletea makaratasi ambayo yanazidi kiasi hiki uipelekee Serikali ijue kwamba Watanzania wanajua, wanaelewa; na nini kinachoendelea. Maana mimi nilifikia hatua maana mimi nilifikia hatua nikaenda nikatafuta, huyu Mhandisi Mshauri, ofisi zake ziko wapi?

Ukiona mahali ofisi zake zilipo ndipo hapo itabidi ofisi yake iwasiliane na Serikali, hatutakuwa na muda tena wa kuona tunafanya yale yaliyotokea wakati wa Symbion, wakati wa Lugumi, wakati wa IPTL, haya yatakuwa mabaya zaidi kwa jinsi nilivyoona na nilivyosoma. Nitakuletea hayo makaratasi uyasome pamoja na Serikali itayarishie kwamba hapo mambo siyo mazuri maana tuna umeme, tuna nguvu kazi, tutawezaje kuwa na viwanda vinavyofanya kazi kama havipatiwi maji? Maji ni resource kubwa sana katika uendeshaji wa viwanda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunivumilia, naunga hoja hii mkono asilimia 100. (Makofi)