Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Kiswaga Boniventura Destery (34 total)

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali imekiri kuwa kuna upungufu wa nyumba 1,183 za kuishi walimu na sasa tayari wananchi wa Wilaya ya Magu wameshajenga maboma 27 yapo tayari kukamilishwa; je, Serikali inaweza kutusadia fedha za kukamilisha ili walimu waingie kwenye nyumba hizo kupunguza uhaba wa nyumba za walimu?
Swali la pili, kwa kuwa nyumba hazitoshi, je, Serikali inaonaje kuwasaidia walimu ambao wanapanga nje mitaani kuwaongeza mishahara kidogo ili waweze kumudu upangaji wa nyumba mitaani? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA) Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi hii kubwa anayoifanya katika Jimbo lake na kwa sababu wamejenga maboma 27, hii inaonyesha ni commitment, jinsi gani watu wa Magu wameendelea kujitahidi kuhakikisha kwamba Walimu wanapata fursa ya kuishi katika nyumba bora.
Mheshimiwa Spika, kwa sababu request imesema ni jinsi gani Serikali itaweza ku-top up hiyo amount? Nasema, ni lazima tuangalie, tufanye ile resource mobilization kutoka katika pande zote.
Mheshimiwa Spika, napenda kumshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba katika allocation ya own sources katika Halmashauri zetu, tuangalie ni jinsi gani tutafanya kupitia vyanzo mbalimbali katika Halmashauri; na bahati nzuri sasa hivi tumefanya uboreshaji mkubwa sana katika ukusanyaji wa mapato katika Halmashauri zetu. Nakiri kwamba Halmashauri zimefanya kazi kubwa sana baada ya kuwapa commitment wahakikishe wanakusanya own source kwa kutumia electronic devices na hili wamelifanya.
Mheshimiwa Spika, nina mategemeo makubwa sana kwamba Halmashauri ya Magu hivi sasa, maana yake mapato yake yataongezeka kwa kasi. Naomba nimwambie kwamba Serikali kupitia TAMISEMI, itashirikiana na Halmashauri ya Magu kuona jinsi gani tutayafanya mpaka maboma hayo yaweze kukamlika. Lengo ni kwamba walimu wetu waishi katika mazingira salama na wapate motisha ya kufundisha.
Mheshimiwa Spika, katika sehemu (b) ya swali lake linasema, jinsi gani kama kutakuwa na topping allowance ilimradi walimu waweze kupata jinsi gani watakapokuwa mitaani waweze kulipia lile suala la pango.
Mheshimiwa Spika, naomba nikiri kwamba ni kweli tuna wafanyakazi mbalimbali ambao wanaishi katika mazingira magumu; acha walimu, acha sekta ya afya, acha mabwana shamba, wote wapo katika mazingira mbalimbali. Hili Serikali imeliona, ndiyo maana katika jibu langu la msingi mwanzo nilisema kwamba lazima tuhakikishe kwamba mishahara inaboreshwa ili mwisho wa siku hata mwalimu akikaa mtaani aweze kuwa na ile purchasing power ya kulipia nyumba. Ahsante.
SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na swali linalofuata. Tuko Wizara hiyo hiyo ya TAMISEMI; swali la Mheshimiwa Omary Tebweta Mgumba, Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na ninashukuru majibu ya Serikali. Naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
(a) Kwa kuwa Serikali imekiri kwamba kuna upungufu wa vitendea kazi, kwa maana ya magari na mafuta; je, ikiongeza kununua magari, italipatia Jeshi la Polisi Wilaya ya Magu hasa Kituo cha Kabila gari lingine?
(b) Kwa kuwa Jeshi la Polisi ni walinzi wa mali na raia lakini maisha yao ni magumu sana, hata wanapostaafu, wanaendelea kuwa na maisha magumu.
Je, Serikali kwa sababu askari katika Wilaya ya Magu wako 135 na nyumba wanazoishi askari kumi ziko tano tu; Serikali ina mpango gani wa kujenga nyumba Wilaya ya Magu? Nipatiwe majibu ni nyumba ngapi zitakazojengwa. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Magu kuongezewa gari moja, ni kwamba sasa hivi, Kituo cha Magu kina gari tatu tayari, lakini nadhani zitakapokuwa tayari hizi gari nyingine ambazo nimesema kwamba kuna gari jumla 777 zinatarajiwa kukamilika, ukiacha zile ambazo zimeshatolewa, hilo jambo tutalichukua na tutalifanyia kazi. Ni jambo ambalo linawezekana, tutalizingatia.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kuhusiana na nyumba. Kwanza nirekebishe tu, Magu kuna askari 147 siyio 135 kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema. Kwa hiyo, suala la nyumba kama ambavyo nimezungumza kwamba kuna mpango wa kujenga nyumba 4,136 na katika Mikoa ambayo nyumba hizo zitajengwa, Mwanza ni mojawapo. Labda baadaye tuangalie katika orodha ya nyumba zitakazojengwa Mwanza kama Magu ipo. Kama haipo vilevile ni jambo ambalo tunaweza kuliangalia kwa pamoja baadaye.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pia nashukuru majibu ya Serikali na kuwapongeza Wizara hii kwa jinsi wanavyoshughulikia masuala haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Wizara inatambua kwamba Magu bado vijiji 85 na 34 vitaingizwa kwenye mpango wa REA III, je, Wizara inaonaje kuviingiza vijiji vyote vilivyobaki kwenye mpango huu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa REA II inaendelea na miradi kule Magu na kwa sababu baadhi ya vijiiji mkandarasi ameondoa nguzo ambazo zilikuwa zinategemewa na wananchi na wananchi wengine hawajawekewa, je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuambatana nami kwenda Jimboni kwangu kutembelea vijiji hivyo pamoja na Vijiji vya Mahaha, Nobola, Bungilya, Mwamabanza na Matale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakubaliana na Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine na naamini kila Mbunge angependa sana vijiji vyake vyote viingie kwenye REA III. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunaendelea kufanya tathmini kama itaonekana ipo haja ya vijiji vyote kuingia basi vitaingia lakini kutegemeana na bajeti. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la pili la kuondoa nguzo kwenye maeneo mengine na kupeleka maeneo mengine, hili nimelichukua. Sambamba na hilo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi tuko tayari kutembelea maeneo yote yenye kero za umeme na kuhakikisha kwamba zinatoweka. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ridhaa yako niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge, usambazaji na upatikanaji wa umeme nchini ulianza mwaka 1908 enzi za ukoloni wa Mjerumani. Kwa hiyo, miundombinu mingi sana imeharibika kama transfoma na mingine, kwa hiyo, tunaendelea na ukarabati. Kwa hiyo, maeneo mengine ambayo Waheshimiwa Wabunge mtapenda tutembelee, tutaendelea kutembelea na tutaendelea kuboresha lengo ni kuhakikisha wananchi wote wanapata umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba lengo letu ni wananchi wote wapate umeme. Nimwombe sana Mheshimiwa Lukuvi kwa sababu anaimarisha nyumba za wananchi, sisi hatutajali kumwekea mtu umeme eti mpaka awe na nyumba nzuri, tutamtundikia umeme hata kwenye mkaratusi karibu na nyumba yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Kwa kuwa Mwanza tuna Kiwanda cha Tanneries ambacho sasa kimegeuzwa kuwa chuo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukirudisha hicho kiwanda ili kiweze kufanya kazi iliyokusudiwa?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Mwanza kuhusu kiwanda cha Mwanza TANNERIES, ambacho kimegeuzwa kuwa chuo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Katibu Mkuu anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji Profesa Mkenda, alikuwa Mwanza wiki iliyopita, kile kiwanda kitaendelea kuwa Chuo na tunalenga kuwafundisha wananchi namna ya kutengeneza nguo, ni Technical School ni VETA ambayo itasaidia watu wa nguo, lakini kando na eneo hilo, kuna Kiwanda cha Ngozi, hicho ndicho tatizo mtu aliyepewa amekigeuza hifadhi ya makatapila na matrekta tunataka kifanyekazi. Kwa hiyo, chuo kitaendelea kufanyakazi tunawafundisha vijana, wanakwenda kwenye viwanda vyao vidogo vidogo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo ni huyo mtu ambaye kiwanda cha Ngozi cha Mwanza amekigeuza hifadhi na kuja Mwanza tarehe 30 na nitakwenda kushughulikia, tarehe 30 mwezi huu.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza msitu unaozungumzwa haupo, hata athari zinazozungumzwa kwamba vijiji vinavyozunguka watapata athari ya upepo siyo kweli, kwa sababu hata wewe ukisimama mle mita mia tatu unaonekana huo ni msitu?
(a) Je, Serikali kwa sababu inasema ni chujio haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa kulipunguza eneo hilo ikawapa wananchi upande mwingine, na upande mwingine ili wakaendelea na shughuli za kijamii na eneo linalobaki wakaliboresha kwa kupanda wenyewe misitu endelevu.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu majibu haya ni ya kudanganywa, je, Naibu Waziri yupo tayari kuambatana nami kwenda kuliona eneo ambalo linasemwa ni hifadhi?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la kwanza, nataka hapa kwa ufupi kabisa tuelewane kwamba, dhana hii ni kwa Watanzania wote kwa nchi nzima. Dhana ya kwamba changamoto za mahitaji ya ardhi kwa ajili ya matumizi mengine ya kibinadamu zitamalizwa kwa kuendelea kumega au kwa kuchukua maeneo yaliyohifadhiwa ni dhana ambayo siyo ya maslahi kwa Taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukiendelea kufikiria kwamba ardhi iliyohifadhiwa ambayo ipo hivyo ilivyo leo kwa sababu imehifadhiwa kwa muda wote ambao imehifadhiwa, dhana hiyo itatufikisha mahali ambapo uhifadhi huo utapotea na ukipotea athari zake ni pana na kubwa na zinatugusa wote nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli inawezekana ukifika katika msitu huo huoni miti juu, lakini msitu unahifadhiwa kwa ajili ya tafsiri ya misitu ya miti unayoiona ipo juu, lakini pia ni kwa sifa za ardhi pale chini, ndiyo maana tumesema chujio, unaweza usione miti lakini, viumbe vilivyopo pale chini kwenye udongo sifa za ardhi ile iliyopo pale na yenyewe pia ni sehemu ya uhifadhi na ni muhimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika sehemu ya pili ya swali lake, kwanza siyo kweli kwamba majibu ni ya kudanganywa, lakini hakuna mwisho wa kufanya vizuri, kila unapodhani umefanya vizuri bado kuna kufanya vizuri zaidi. Nipo tayari kuambatana naye kwenda kuboresha uelewa nilionao tayari, kwenda kupata majibu ya pamoja mimi naye wakati tutakapoweza kupanga wote kwa pamoja, ili tuweze kupata hayo majibu sahihi na kuweza kutatua matatizo haya kwa maslahi ya Taifa letu.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nazidi kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kadri anavyochapa kazi kuhakikisha kwamba anatoa majibu yanayoridhisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, wa kuwa zahanati hizi wananchi walizijenga, Nyang‟hanga, Salongwe, Bundilya, Nsola, Nyamahanga, Nyashigwe, Chabula, Ikengele, Isangijo, Langi na Lutale; na ziko hatua za kukamilisha ili waweze kupata huduma; na kwa kuwa bajeti ya mwaka 2015/2016 inaelekea mwisho; je, Serikali inaweza kutupatia fedha hizi kwa haraka ili tuweze kukamilisha miradi hii na wanachi wapate huduma?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi inasema kila kijiji kiwe na zahanati, na wananchi wetu wamekuwa wakiwahi kutimiza wajibu wao kwa maana ya kujenga maboma haya.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha utekelezaji wa ilani hii ili wananchi waweze kupata huduma hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuweka kumbukumbu sawa, miongoni mwa maswali mengi niliyoyapata yalikuwa ni maswali kutoka Jimbo la Magu na miongoni mwa ziara yangu ya kwanza katika nafasi yangu Mheshimiwa Rais aliyonipa nilianza Jimbo la Magu kwa Mheshimiwa Kiswaga. Kwa hiyo. nimpongeze sana kwa kazi kubwa anayofanya na katika ziara hiyo niliona miradi mbalimbali ukiwemo mradi wa ujenzi huu wa zahanati. Naomba nikiri wazi, ni kweli fedha hazijaenda. Lakini Serikali kama tulivyosema, kwamba tumejipanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, watu wate mnafahamu kwamba mara baada ya uchaguzi miradi mingi ilikuwa imesimama, lakini mchakato mkubwa uliofanyika kuanzia mwezi Januari mpaka tunapozungumza hivi, angalau fedha nyingi zimeenda katika miradi mbalimbali. Wakati napita kwa Mheshimiwa Kiswaga miradi mingi ilikuwa imesimama. Katika kipindi hichi Jimbo la Magu limepatiwa karibuni shilingi bilioni 4.9 baada ya msukumo mkubwa wa Serikali katika miradi mingine ya maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo najua Serikali itaendelea ku-push kuhakikisha kwamba mambo yanakwenda. Najua katika zahanati fedha hazijaenda, lakini hata zile fedha za maji mlizokuwa mmeomba Serikali imeweza kuzipeleka kule. Hii inamaana kwamba Serikali inawajali watu wa Magu. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kufanya juhudi zilezile.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la mpango mpana wa jinsi gani maboma haya yatamaliziwa nimesema hapa mara kadhaa. Ni kwamba ni kweli jukumu letu ni kumalizia maboma. Lakini katika ajenda ya sera ya Serikali na Ilani ya Uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi tumejielekeza kwenye vituo vya afya katika kila kata na zahanati katika kila kijiji.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana Waziri wangu mwenye dhamna hapa hata jana alisema mpango wetu mpana sasa hivi ni kuhakikisha angalau kila mwaka katika Halmashauri zote tujenge kituo kimoja cha afya, lakini halikadhalika ujenzi wa zahanati na kumalizia yale maboma. Imani yangu kubwa ni kwamba kwa sababu tuna Halmashauri 181 tukijenga kituo kimoja cha afya, maana yake tulikuwa tumejenga kwa mwaka mmoja vituo vya afya 181, ni mapinduzi makubwa kwa mwaka mmoja peke yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, imani yangu ndani ya miaka mitano tutafanya mabadiliko makubwa, na mwisho wa siku ni kwamba Sera na Ilani ya Chama cha Mapinduzi itatekelezeka kwa mipango hii tunaifanya pamoja baina ya TAMISEMI, Wizara ya Afya na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Kamati ya Bajeti.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iliongeza mipaka yake ikawafuata wananchi katika vijiji vinane vya Mwamumtani, Mwalali, Ndung‟wa, Ndinho, Ntantulu, Kiliju, Longalombogo na Shishani na haikuwashirikisha wananchi, je, ni lini sasa eneo hili litarudi kwa wananchi kwa kuwashirikisha wananchi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa amesema umegaji wa eneo hili haujaleta tija na haujamaliza changamoto ya wananchi na kwa kuwa Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni akiwa kwenye Kijiji cha Nanga katika Kata ya Kinameli aliliona hili na alitaja Sheria ya Ardhi, Na.4 akasema kwamba akiwa Rais eneo hili atalirudisha kwa wananchi. Je, kwa nini Mheshimiwa Naibu Waziri anapingana na ahadi ya Rais?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, nazingatia kujibu kwa kifupi, moja kwamba zoezi lililofanyika huko nyuma la upanuzi wa mipaka halikushirikisha wananchi na ni lini Serikali itashirikisha wananchi? Kwanza si kweli kwamba Serikali inaweza kupanua mipaka ya eneo lolote lile hasa mipaka ya wananchi wanaopakana na hifadhi bila kushirikisha wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, bado Serikali ina nia njema ya kufanya zoezi la kupitia mipaka kwa namna bora zaidi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma. Ndiyo maana nimesema kwenye jibu la msingi kwamba tunakwenda sasa kushirikisha Wizara nyingi zaidi na tunakwenda kufanya ushirikishwaji zaidi katika hatua hii lakini mara hii tunakwenda kuweka vizuri kumbukumbu ili hata vizazi vijavyo vije kuona kwamba zoezi hilo lilifanyikaje kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili la ahadi ya Mheshimiwa Rais ikihusisha Sheria Namba 4, napenda kujibu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza haiwezekani kabisa tukafika mahali tukaweza kupingana na maelekezo ya Mheshimiwa Rais. Hilo ni jambo ambalo haliwezekani kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kama alikuwa anataka kujua utekelezaji sasa wa hiyo ahadi ya Mheshimiwa Rais ambayo aliitoa, Rais akishatoa ahadi maana yake tayari ni amri kwetu sisi watekelezaji. Nimekwishamwambia kwenye jibu la msingi na jibu lake litakuwa ni hilo na hapa nitoe tu wito kwa ufupi hata kwa maswali ya nyongeza mengine kama inawezekana basi jibu litakuwa ni hilihili tu kwamba Waheshimiwa Wabunge wote wavute subira, wasubiri utaratibu huu ambao Serikali inaenda kufanya kwa kushirikisha Wizara nilizozisema ili twende tukatafute suluhu sasa ya matatizo haya kama nilivyokwishayasema.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na kadri ambavyo imeanza kushughulikia jambo hili hasa kwa kuamini kwamba katika Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi tulifanya ahadi na wananchi, lakini ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa wazee hawa wengi ni wakulima ambao wakati wote Serikali inapokuwa na hali mbaya ya chakula huzuia mazao yao kuuzwa mahali popote ili kukidhi mahitaji ya nchi, kwa hiyo, hawa wazee wamechangia sana katika Taifa hili.
Je, ni lini sasa Serikali pamoja na hatua nyingine ambazo imezichukua itakamilisha mpango huu ili wazee hawa waweze kulipwa? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa sisi sote tuliopo humu ni wazee watarajiwa, je, Serikali inaweza kutuambia hapa itaanza kwa kutoa kiasi gani kila mwenzi na kwa kila mzee?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la kwanza la mpango huu utakamilika lini, kwenye majibu yangu ya msingi nimesema kwamba hatua ambayo tumefikia hivi sasa ni zile za kuainisha idadi ya wazee wote nchini, kuainisha viwango vya pensheni, lakini baadaye tutakapojiridhisha taratibu zote hizi zimekamilika, Serikali itatoa taarifa ni lini sasa tutaanza kufanya kazi hii ya malipo. Nimuondoe shaka Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua umuhimu wa wazee katika nchi hii hasa kwa mchango wao mkubwa walioutoa katika ustawi wa Taifa letu. Kwa hiyo, pindi taratibu hizi zitakapokamilika basi tutakuwa tayari kutoa taarifa na kusema ni lini mchakato huu wa kuwalipa pensheni wazee utaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili la nyongeza ameuliza ni kiasi gani kitakacholipwa. Tumefanya tafiti mbalimbali katika nchi tofauti na tumejiridhisha na mapendekezo yaliyopo sasa katika kiwango cha kwanza cha kuanzia itakuwa ni shilingi 20,000 kwa kila mzee. Utaratibu uliowekwa ni kuanza na wazee wa kuanzia umri wa miaka 70 ambao wako takribani 1,570,000 na baadaye tutaendelea kuona jinsi ya kuongeza umri chini ya hapo kadri uwezo utakavyokuwa unaruhusu.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, je, Serikali ina mpango gani wa kuzielekeza Halmashauri kutumia force account ili miradi midogo midogo kama hii iweze kutengenezwa kwa fedha ndogo na iweze kuleta impact?
Swali la pili, kwa kuwa jambo hili linafanana kabisa
na vituo vya afya vilivyoko Jimbo la Magu katika kituo cha afya Lugeye pamoja na Nyanguge. Serikali ina mpango gani wa kuvijengea majengo ya upasuaji ili wananchi waweze kupata huduma karibu? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa Serikali hivi sasa si kutoa maelekezo, tayari tumeshatoa maelekezo hivi sasa na Halmashauri mbalimbali zinaendelea kutumia force account na tumepata mafanikio makubwa sana, kwa sababu maeneo mbalimbali unapopita hivi sasa mradi ambao zamani ulikuwa saa nyingine ulikuwa unagharimu shilingi milioni 150 utakuta sasa hivi milioni 70 mradi umekamilika tena upo katika ubora unaokusudiwa.
Kwahiyo Mheshimiwa Kiswaga ni kwamba sasa hivi jambo hilo linaendelea na linaendelea kwa ufanisi mkubwa, na nipende kuwashukuru sana Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi ambao wanasimamia jambo hili kwa uzuri zaidi
na hasa Waheshimiwa Wabunge katika Majimbo yenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, katika suala zima la Jimbo la Magu ambalo Mheshimiwa Mbunge umesema na ni kweli, katika harakati za Serikali tuna mpango ambao si muda mrefu sana tutakuja kuuanza katika kituo chako kimoja cha afya tutakuja kujenga jengo la upasuaji na kuweka vifaa tiba vyote. Kwa hiyo, naomba nikushauri
Mheshimiwa Mbunge kwamba usiwe na wasiwasi Serikali yako kama kila siku inavyopiga kelele hapa Bungeni itaendelea kushirikiana nanyi na ujenzi huo Mungu akijaalia utaanza hata kabla ya mwezi wa sita.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali pamoja na mikakati mizuri ambayo Serikali inaiweka lakini ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa nina imani kwamba Waziri na Maprofesa wote mlioko ndani humu mmesoma bure A-Level na kwa sababu watoto hawa wanachaguliwa, wengine wanashindwa kuendelea na masomo haya kwa kukosa fedha, kwa sababu bado ni watoto wa maskini na wengine wamefaulu vizuri masomo ya sayansi pamoja na hesabu, je, Serikali haioni kwamba inapoteza vijana wazuri ambao wanaweza kusaidia Taifa?(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa hawa watoto wanaochaguliwa kuendelea na A-level ni wachache kuliko wale ambao wanahudumiwa na Serikali kwa maana ya O-Level, je, Serikali haioni kwamba ni wakati muafaka sasa wa kuleta bajeti ili tuweze kuwasaidia watoto hawa wa maskini ili waweze nao kusoma bure wafaidi matunda ya Serikali hii? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi Serikali ingependa kusomesha wanafunzi katika ngazi zote za elimu bure endapo uwezo ungekuwa wa aina hiyo. Kama nilivyosema ni kwamba awamu ya mwanzo tuliongeza shule za msingi lakini tukaja tukaongeza shule za sekondari kila kata na sasa hivi tunaendelea kuongeza shule za kidato cha tano na sita (A-level) kwa sababu ni chache ukilinganisha na wanafunzi wanaofaulu na hasa baada ya Serikali kuchukua jitihada za makusudi za kuongeza ubora wa elimu, imekuwa sasa wanafunzi wanaofaulu ni wengi na hivyo hatuwezi kuwaacha bila kupata elimu hiyo. Kwa hiyo, kabla hatujaweza kutoa fedha kwa kuwalipia hiyo ada, ina maana kama hawana sehemu ya kusomea itakuwa bado hatujafanya jambo la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili la kuongeza bajeti, hilo ni suala letu sote kama Wabunge. Tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais lakini pia Mheshimiwa Waziri Mkuu ambaye tukonaye humu, Wizara yetu ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ni kati ya Wizara ambazo zinapewa kipaumbele cha hali ya juu kwa kupewa bajeti kubwa kuliko Wizara nyingine. Kwa hiyo, naamini Serikali itaendelea kufanya hivyo.
MHE. DESTERY B. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na hasa niendelee kuanidka Kiswaga. Kwa kuwa swali langu linafanana kabisa na suala hili la Kigamboni, Wilaya ya Magu ambayo ni Jimbo lina vijiji 82, ni vijiji 29 tu vina umeme. Je, vijiji 53 ni lini vitapatiwa umeme ambavyo hata Mheshimiwa Dkt. Kalemani anavifahamu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nimsahihishe kidogo Mheshimiwa Kiswaga, vijiji ambavyo havijapata umeme katika Jimbo la Magu siyo 53 vipo 56. Kwa hiyo, Mheshimiwa Kiswaga tutakupelekea umeme.
Mheshimiwa Spika, niseme tu utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu umeshaanza na katika Wilaya yake, maeneo yote yameshafanyiwa survey na Mheshimiwa Mbunge tumeenda naye na tumetembelea maeneo hayo na nimhakikishie vile Vijiji vya Mahala, Igombe, Shishani, Nyasato, Kayera mpaka Mahala vitapatiwa umeme na utekelezaji huo umeshaanza. Nikupe tu uhakika kwamba survey itakamilika tarehe 10 mwezi huu na wakandarasi wataanza kazi rasmi. Kama nilivyosema tuliboresha kwa sababu vile vijiji vyako vitatu vimepelekewa nguzo moja moja kwa hiyo sisi tunahesabu kama vijiji vyote havijapata umeme, kwa hiyo, ni 56 katika Jimbo la Magu.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali.
Kwa kuwa Serikali imekiri kufuta leseni 423 yenye eneo la hekta 69,652.88; je, Serikali iko tayari kuwapatia wachimbaji wadogo wadogo eneo hili ambalo limefanyiwa utafiti ili waweze kujiajiri na kujipatia ajira na waweze kulipa kodi stahiki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, je, Serikali iko tayari kuwanunulia vifaa vinavyohusiana na wachimbaji wadogo wadogo ili waweze kukodisha kuliko ilivyo sasa wanachimba bila utaalam na vifaa vinavyostahili?
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ni kwamba Serikali iko tayari kuwasaidia wachimbaji wadogo. Imekwisha kutenga maeneo 11 ambayo yana jumla ya hekari 38.9 kwa ajili ya wachimbaji wadogo wadogo. Kwa hiyo, kwa maeneo haya ambayo yamesharudishwa Serikalini, Serikali itaendelea kufanya mpango wa kuweza kuwapatia wachimbaji wadogo wadogo ili waweze kuchimba na wao waweze kupata faida na waweze kunufaika na madini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wachimbaji wadogo kupitia ruzuku iliyokuwa inapitia SMMRP ambayo ilikuwa inatoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo na wadau wengine wa uchimbaji iliweza kutoa fedha ili kuweza kuwasaidia wadau waweze kununua vifaa kwa ajili ya uchorongaji, kufanya utafiti na kuweza kusaidia wale wachimbaji wengine wadogo wadogo kwa kukodisha. Lakini vilevile STAMICO ambayo iko chini ya Wizara ya Madini pamoja na GST na yenyewe ina juhudi za dhati kabisa kununua vifaa ambavyo wachimbaji wadogo watakuwa wanakodisha ili waweze kujua mashapu yaliyopo ni mashapu ambayo yana faida ambayo wanaweza wakachimba na wakapata uchimbaji wa tija ili kujiondoa katika ule uchimbaji ambao wanachimba kwa kubahatisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo Serikali iko pamoja na wachimbaji wadogo. Ahsante sana.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa, mkandarasi anaendelea na mkataba mpaka kuezeka. Je, Serikali ina mpango gani wa ku-lease fedha ambazo zitahitajika, ili halmashauri isikiuke mkataba?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa, hatua ya kuezeka inakwenda kukamilika na jengo hili limechukua muda mrefu. Je, Serikali iko tayari kutenga fedha kwa mwaka ujao wa fedha, fedha za kutosha ili kukamilisha jengo hilo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kwanza ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba kandarasi zote ambazo zimeanzishwa hatuishii njiani. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie na nimwombe mkandarasi aliyepo hapo aendelee na kazi ili pesa ambayo imeahidiwa na Serikali ikifika asilazimike kwamba awe ametoka site na kulazimika kurudi kwa mara nyingine. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, naomba kwa kushirikiana na Mbunge na nia njema ya Serikali kuhakikisha kwamba katika bajeti 2018/2019, ujenzi huu unaendelea, kwa hiyo tuweke kwenye bajeti.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa Kituo hiki cha Afya kinahudumia maeneo makubwa katika eneo la Ilemela, Usagara Wilaya ya Misungwi, pamoja na Jimbo la Sumve na ni Kituo cha Afya ambacho kiko highway, wakati wowote watu wanapata matatizo wanaposafiri wanahitaji huduma hii kubwa. Kwa kuwa sera ya mwaka 2007 ni kama imepitwa na wakati ukilinganisha na mazingira:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kubadilisha ili angalau kulingana na mazingira ya Kituo hiki cha Afya cha Kisesa, kiweze kupandishwa hadhi na kuwa hospitali ya wilaya ili kiweze kuhudumia maeneo makubwa?
NAKALA YA MTANDAO (ONLINE DOCUMENT)
6
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali iko hatua za mwisho, mkataba wa kujenga jengo la X-ray, jengo la upasuaji, limeanza mwaka 2013. Kama ni hatua za mwisho, leo ni miaka mitatu. Serikali haioni kwamba hii ni aibu, miaka mitatu inajenga majengo haya bila kukamilika na yanasubiri tu shilingi milioni 77 ili yaweze kukamilika? Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuniambia hizi shilingi milioni 77 zikipatikana hata kesho ili huduma hizi zianze kutolewa, yuko tayari kunipa fedha hizi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikiri wazi, kituo cha Kisesa, junction yake ukiiangalia na ukubwa wake sasa hivi wa population ya pale, kweli ni eneo ambalo lina-capture watu wengi sana. Ukiangalia hata Kata jirani wanategemea sana Kituo cha Afya cha Kisesa. Kubwa zaidi, kwa mujibu wa sera siwezi kusema hapa kwamba tutabadilisha sera hii, kwa sababu nyie mnafahamu, lengo letu ni kuzifikia kila Halmashauri kupata hospitali za wilaya. Hivi sasa mnaona tuna deficit na tunaenda kwa kasi ili mradi angalau sasa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tuna wilaya zipatazo 139 na Halmashauri 181. Lengo letu ni kwamba kila Wilaya angalau ipate hospitali ya wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo letu kubwa ni kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi, tutafanya juhudi kituo hiki kiweze kukamilika na suala la upasuaji liweze kuendelea na huduma nyingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la pili ni kwamba, X-ray kwa muda mrefu imesuasua katika kituo hiki. Kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa sababu yeye alikuwa ni Mwenyekiti wa Halmashauri hii ya Magu ambayo naizungumza hivi leo. Kwa hiyo, hata mambo yanayoendelea huko, naye alichangia kwa kiwango kikubwa mpaka kufanikisha ujenzi huo unaendelea, naye anajua wazi tunaendaje. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati iliyofanyika katika hicho kituo, sasa hivi tuko katika hali ya mwisho. Kwa sababu najua juhudi ya Mheshimiwa Mbunge aliyokuwa anaifanya hata nilipokuwa Jimboni kwake kule mwezi wa Kwanza katika harakati kubwa za kuboresha huduma ya afya hiyo na hata alikuwa anaomba hata ingewezekana watu walioasisi mifumo mizuri ya afya, Dkt. Pembe arudi Magu kwa ajili ya kuhakikisha afya inakwenda vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo kubwa ni kuhakikisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kama tulivyofanya mawasiliano na Mkurugenzi kule, tutaweka nguvu ili ikifika mwezi wa Sita jengo lile liweze kukamilika na wa Kisesa waweze kupata huduma kama ilivyokusudiwa.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa matatizo ya Magu yanafanana sana na matatizo ya Nyamagana, Barabara ya Ngudu – Magu – Ngumarwa, usanifu umeshakwisha kukamilika, sambamba na Barabara ya Airport – Igombe – Kayenze – Kongolo – Nyanguge ili kupunguza msongamano wa kuingia Jiji la Mwanza na kwa sababu ni ahadi ya Mheshimiwa Rais, je, barabara hizi zitaanza kujengwa lini kwa kiwango cha lami? (Makofi)
WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana yanayotolewa na Naibu wangu, Mheshimiwa Jafo, napenda kujibu maswali ya nyongeza yaliyoulizwa yanayofanana sana na Waheshimiwa Wabunge juu ya ahadi za Mheshimiwa Rais ya barabara zilizoko chini ya Ofisi ya Rais TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumezihakiki, tunazifahamu lakini pamoja na mipango ya halmashauri, Wizara yangu itakuja na mpango mkakati wa namna ya kuzitekeleza barabara hizo zote kabla ya mwaka 2020. Serikali hii ni Serikali ya vitendo, tuliahidi, ni lazima tutatekeleza na ahadi za Rais ni kipaumbele chetu.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Kwanza naishukuru Serikali kwa kutupa mradi wa maji pale Magu Mjini, mkandarasi yuko site; lakini pia nipongeze Kampuni ya Alliance Ginnery, mwekezaji amechimba kisima kirefu pale salama na kinatoa lita 9,000 kwa saa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa suala hili la Nyamagana linafanana kabisa na Jimbo la Magu, kijiografia na kwa fursa zilizopo. Katika Tarafa ya Sanyo kwa maana ya Kisesa yote na vijiji vyake pamoja na Tarafa ya Ndagalu kuna hali mbaya sana ya maji katika Vijiji vya Ng’aya, Salama, Ndagalu, Nyabole, Kabila na Mahala...

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, je, kwa sababu Halmashauri tumeomba dharura, ni lini Serikali sasa itatupatia fedha kwa ajili ya kuchimba visima virefu ili tuweze kusaidia wananchi hao?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kabisa kwamba tumesaini mradi mkubwa ili kupata maji Wilaya ya Magu Mjini, lakini nikiri kwamba kuna kata ambazo ziko pembezoni na huo Mji ambazo bado hazijapewa huduma ya maji, lakini nichukue ombi lako, tuhakikishe kwamba tunapeleka visima, nikuombe Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane. Sio wewe tu katika tarafa zako, zipo tarafa nyingi, wengine ni majirani zako, pale Kasoli hakuna maji. Kwa hiyo, niombe tuwasiliane ili tuweze kuangalia tufanyeje kupitia kwenye bajeti zako au maeneo mengine yoyote utakayoona yanawezekana tuhakikishe kwamba hayo maeneo yaliyobaki ya vijiji nayo pia yanapata walau dharura kwa kuchimbiwa visima kama maji yatakuwepo chini ya ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lengo la Wizara ya Maji na Umwagiliaji kuhakikisha kwamba wananchi wote wa Tanzania popote pale walipo, tunawapatia maji safi na salama. (Makofi)
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kwamba uchumi ukiwa nzuri tutaongeza, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa majibu yanaonesha kwamba kila baada ya miaka miwili Serikali ilikuwa ikiongeza posho za Waheshimiwa Madiwani mpaka 2015 na leo tuko 2017 tayari miaka miwili. Je, Serikali haioni kwamba kulingana na mazingira wanayofanyia kazi Waheshimiwa Madiwani pamoja na kupanda kwa maisha, sasa ni muda muafaka wa kuongeza posho angalau kidogo ili waweze kumudu maisha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mikopo hii wanayokopa kwenye mabenki ni kutokana na posho yao, Serikali haioni kwamba hizi fedha ni ndogo zaidi, hawawezi hata kupeleka kwenye usafiri. Je, Serikali kwa nini isiweke ruzuku kama inavyotoa kwa Waheshimiwa Wabunge nusu ili Waheshimiwa Madiwani waweze kumudu usafiri? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba kwa wastani wa miaka miwili posho ya Madiwani inaongezeka; naomba nikiri kwamba Madiwani wetu wanafanya kazi kubwa sana. Mheshimiwa Kiswaga na Waheshimiwa Wabunge naomba niwaambie kwamba kwa bahati nzuri nilipata fursa ya kukaa na Madiwani katika vikao vya ALAT kule Musoma na hapa Dodoma na hii imekuwa ni concern yao kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni kweli na sasa hivi limewasilishwa katika mamlaka husika na kwamba sasa linafanyiwa kazi na linachambuliwa vizuri. Mambo yakikamilika vizuri basi watapata mrejesho kwamba Serikali imeamua vipi katika jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ruzuku kwa vyombo vya usafiri nadhani ni wazo zuri naomba tulichukue, na Serikali itaangalia ni jinsi gani itafanya kwa sababu Madiwani wanafanya kazi kubwa, lakini siwezi kutoa commitment kutoka hapa kwamba nini kinafanyika kwa sasa.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Swali la kwanza; kwa kuwa, Serikali imekiri upungufu wa Walimu katika Wilaya ya Magu, je, itakapoajiri itanipangia Walimu wa kutosha?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa bado tuna upungufu hasa wa Walimu wa sayansi. Serikali ina mkakati gani wa kuziba pengo hilo la Walimu wa sayansi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la kwanza kuhusu upungufu wa Walimu napenda nimhakikishie kwanza kwamba angalau Wilaya yake ya Magu ina nafuu kidogo. Kuna baadhi ya Halmashauri zina upungufu wa Walimu kwa chini ya asilimia 60 ya mahitaji. Angalau wilaya yake ina asilimia zaidi ya 70. Kwa hiyo tutakapoajiri tutapanga Walimu kulingana na uwiano wa upungufu uliopo nchi nzima. Kwa hiyo, asiwe na wasiwasi wowote.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili, kuhusu upungufu wa Walimu wa sayansi; tulikuwa na upungufu wa Walimu wa sayansi kama 19,000. Sasa tumejizatiti, tunaandaa utaratibu wa kuajiri Walimu wa sayansi kama Walimu 6,000 mpaka mwishoni mwa mwezi wa Sita. Tunaamini upungufu wa Walimu wa sayansi mpaka 2020/2021 hatutakuwa nao tena.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge zima kwamba tumejindaa vya kutosha kuhakikisha kwamba tunapunguza upungufu wa Walimu wote wa sayansi na wa shule za msingi.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa Serikali imeanza kujenga barabara ya Bariadi na barabara ya Magu Ndagalu tumejenga vipande viwili, hapa katikakati barabara ya Magu – Ndagalu - Bariadi ni lini itakamilishwa kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hili la Bariadi, Magu tuna miradi mingi ambayo inaendelea kujengwa na Mheshimiwa Mbunge anatambua pia tunajenga daraja la Sukuma kwa nia ya kuboresha eneo hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge kwa sababu network ya barabara katika eneo hili ni kubwa, tuonane ili angalau nimpe hatua ambayo tumefikia, lakini ni dhamira ya Serikali kuhakikisha maeneo haya yanaunganishwa vizuri ili wananchi waweze kujiimarisha kuchumi.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hata sisi viongozi wa Bunge mojawapo ya sifa ni kuwa na kazi halali zinazotuingizia kipato kama hawa Wenyeviti wa Vitongoji ambao sisi tunalipwa, wao hawalipwi. Je, Serikali iko tayari kuleta sheria ili waweze kulipwa mishahara? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa viongozi hawa ndiyo wanaohamasisha maendeleo kama ujenzi wa zahanati, shule za msingi, sensa na kusimamia amani, je, Serikali iko tayari iko tayari kuendelea kuwalipa posho? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la kwanza, napenda nimhakikishie kwamba wakati wowote Serikali inapopata mapendekezo huwa inayafanyia kazi. Kwa hiyo, mara tutakapopata mapendekezo kutoka kwenye vikao halali vinavyohusika tunaweza wakati wowote tukafanya marekebisho ya sheria kutokana na muktadha wa muda utakavyokuwa na mapendekezo yatakavyokuwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu kulipa posho, Serikali ilishatoa Mwongozo tangu mwaka 2003 kwamba yatumike mapato ya ndani kulipa posho kwa viongozi hawa na posho zile zimeainishwa. Kwa hiyo, ni jukumu la Wakurugenzi wa Halmashauri na Mheshimiwa Mbunge namwomba sana asimamie kwenye jimbo lake na watumie Mwongozo huo kuhakikisha kwamba viongozi wetu hawa wanalipwa posho.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi. Tatizo la Pwani linafanana kabisa na tatizo lilipo Wilaya ya Magu katika miradi inayoendelea Sola, Kisamba, Bubinza, Matelamuda, pamoja na Kabila Ndagalu na Kitongo Sima, miradi hii imesimama sasa kwa sababu wakandarasi wamesha-raise certificate na Wizara tayari inazo taarifa hizo. Je, ni lini Wizara italipa fedha kwa wakandarasi ili miradi hiyo iweze kuendelea?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Kiswaga kwa kazi nzuri sana anayoifanya katika Jimbo lake la Magu. Tunatambua kwamba utekelezaji wa miradi ya maji inategemeana na fedha. Sasa sisi kama viongozi wa Wizara hatutakuwa kikwazo katika kuwapatia wakandarasi wake fedha. Nimwombe baada ya Bunge tukutane ili tupate zile certificate tuangalie namna bora ya kuwapatia fedha ili wakandarasi waendelee na kazi.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru. Kwa kuwa Mji wa Kisesa kulikuwa na mpango wa kuwekwa maji ya bomba pamoja na Vijiji vya Mahaha, Kabila, Dagalu huko. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwafikishia maji wananchi hawa ili waweze kupata huduma hiyo inayostahili? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri anayoifanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa na jitihada kubwa sana katika Mkoa wa Mwanza katika kutatua tatizo la maji. Kuna utekelezaji wa miradi mikubwa sana Magu, Lamadi pamoja na maeneo mengine. Nataka nimhakikishie; nami kama Naibu Waziri, baada ya Bunge nataka nifike katika Jimbo lake ili twende tuka-push miradi ile iweze kukamilika na wananchi wake waweze kupata maji.
MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Nini sasa commitment ya Serikali? Financing agreement ni lini itasainiwa ili miji hii midogo iweze kupata maji?

Swali la pili, kwa kuwa kuna mradi ambao ulikuwa umeanza upembuzi yakinifu na umeshakamilika katika Ziwa Victoria ambao utanufaisha Wilaya ya Kwimba Jimbo la Sungwe na Wilaya ya Maswa Jimbo la Malampaka na Vijiji vya Magu takribani 40, ni lini mradi huo utaanza kutekelezwa?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Magu kwa kazi nzuri sana na kuweza kuwapigania wananchi wake mpaka ule mradi wa Euro milioni 104 kuweza kuanza katika Jimbo lake. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba safari moja huanzisha nyingine. Tunatekeleza mradi huu, lakini kwa kuwa ile ni kazi ya nyongeza, sisi kama Wizara ya Maji hatutakuwa kikwazo, tutafanya mawasiliano haraka, pamoja na wenzetu wa Wizara ya Fedha ambao wamekuwa na mchango mkubwa katika Wizara yetu; tutashirikiana kwa haraka ili mradi huu uweze kusainiwa na uweze kupeleka maji katika eneo lake.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala zima la eneo lake kwa vijiji alivyovitaja pamoja na suala la upatikanaji wa maji, maeneo mengi ya Magu pamoja na Sumve yamekuwa karibu sana na Ziwa Victoria. Siyo busara sana kuona tuna rasilimali hizi za kutosha halafu maji yale yasinufaishe wananchi. Sisi kama Wizara ya Maji, tuna Mhandisi Mshauri sasa hivi anayefanya kazi ya upembuzi katika kuhakikisha rasilimali ile ya Ziwa Victoria, maeneo ya miji yaliyoko karibu waweze kupata maji safi na salama yenye kutosheleza.

Mheshimiwa Spika, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Sumve pamoja na Mheshimiwa wa Magu, sisi kama Wizara ya Maji, tumejipanga katika kuhakikisha mradi ule utakapokuwa umeshasanifiwa, utaanza kwa haraka ili wananchi waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Kwa kuwa bajeti inayoendelea sasa tuko robo ya tatu na Serikali ilitenga shilingi milioni 750, ni lini Serikali itazileta hizi fedha za bajeti ya mwaka huu unaoendelea ili tuweze kuendelea na ujenzi wa jengo hilo la Halmashauri? (Makofi)

Swali la pili, kwa kuwa jengo hili ni la muda mrefu na Serikali imewekeza fedha nyingi za kutosha na ili ufanisi wa shughuli za Halmashauri uweze kwenda vizuri, je, mwaka huu wa fedha Serikali itatenga fedha za utoshelevu ili kuhakikisha kwamba jengo hili linakamilika na majengo mengine ambayo yako kwenye nchi hii? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Magu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimetangulia kujibu kwenye swali la msingi kwamba Serikali kwa mwaka huu wa fedha 2020/2021 imekwishatenga shilingi milioni 750 kwa ajili ya kufanya shughuli za umaliziaji wa jengo la utawala katika Halmashauri ya Magu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Magu kwamba fedha hizo ziko katika hatua za mwisho za kutolewa ili ziweze kufikishwa katika Halmashauri hiyo kwa ajili ya kutekeleza shughuli hizo zilizokadiriwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na jengo hili kuwa la muda mrefu ni kweli na Serikali inatambua kwamba jengo hili lina muda mrefu tangu limeanza kujengwa, na dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kwamba linakamilika mapema iwezekanavyo na ndiyo maana katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha Serikali itatenga kiasi cha shilingi bilioni moja na milioni mia moja kwa ajili ya jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itatenga fedha hizo na zitafikishwa ili ziweze kukamilisha jengo hilo kwa ajili ya kuboresha huduma kwa wananchi.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa suala hili linafanana kabisa na Vituo vyangu vya Kisesa na Nyanguge, ni vituo vya siku nyingi ambavyo havitoi huduma inayostahili kwa wananchi.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha hasa kufanya ukarabati na kuvipatia vifaa vya kutolea tiba katika Vituo vya Nyanguge na Kisesa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifutavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kusema kwamba sisi sote Waheshimiwa Wabunge tunafahamu kazi kubwa sana ambayo imefanywa na ambayo inaendelea kufanywa na Serikali yetu katika kuhakikisha kwanza tunajenga vituo vya afya lakini tunakarabati vituo vya afya. Sisi sote ni mashahidi kwa kipindi hiki cha miaka mitano jumla vituo vya afya vipatavyo 487 vimeendelea kujengwa na kukarabatiwa na vimeanza kutoa huduma za afya.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba hatua moja inatupelekea kuendelea na hatua nyingine. Naomba nimhakikishe Mheshimiwa Kiswaga, kwanza kuhusiana na Kituo cha Afya cha Kisesa na Nyanguge kwamba vinahitaji ukarabati, ni kweli na suala ambalo tunakwenda kulifanya ni kuanza kuweka taratibu za ukarabati na upanuzi wa vituo hivi kadri ya upatikanaji wa fedha. Tuna kata nyingi, tutakwenda kwa awamu, si rahisi kumaliza vituo vyote kwa pamoja lakini vituo hivi vyote ni kipaumbele.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na vifaatiba, naomba niwakumbushe watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa, maelekezo yalikwishatolewa Serikali imekuwa ikigharamia ujenzi wa vituo hivyo, kuanzia hospitali za halmashauri, vituo vya afya na zahanati. Katika hospitali za Halmshauri tumetenga bajeti kwa ajili ya vifaa tiba lakini katika vituo vya afya, tumewaelekeza Wakurugenzi katika mamlaka za Serikali za Mitaa kutenga fedha ili tuweze kununua vifaatiba.

Kwa hiyo, ni muhimu sana Mamlaka ya Halmashauri ya Magu wahakikishe wanatenga fedha katika mapato ya ndani na fedha zipatikanazo na malipo ya cost sharing ili kununua vifaatiba. Kwa ujumla, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuboresha miundombinu hii kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa tatizo lililoko Busega linafanana kabisa na tatizo lililoko katika Jimbo la Magu. Jimbo la Magu lina vijiji 82, vijiji 40 vina zahanati, vijiji 42 havina zahanati. Tunavyo vijiji 21 ambavyo vimekamilisha maboma ya zahanati. Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia maboma hayo 21 ambayo yanahitaji bilioni moja na milioni 50 ili wananchi waweze kupata huduma kama inavyosema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwamba kila kijiji kiwe na zahanati?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Serikali inaendelea kujenga vituo vya afya na zahanati katika vijiji na kazi kubwa imekwishafanyika nchini kote ikiwepo katika Jimbo la Magu. Hata hivyo, ni kweli kwamba bado kazi ni kubwa, bado kuna vijiji vingi na kata nyingi ambazo bado zinahitaji kujenga vituo vya afya na zahanati. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kiswaga kwamba Serikali itaendelea kutenga fedha kila mwaka wa fedha kuhakikisha tunaendelea kujenga vituo vya afya na zahanati nchini kote, lakini pia katika Jimbo hili la Magu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitambue kwamba katika mwaka huu wa fedha, tayari Jimbo la Magu limeshapelekewa milioni 150 kwa ajili ya kuchangia nguvu za wananchi kujenga na kukamilisha maboma matatu na katika mwaka ujao wa fedha pia imekwishatengewa shilingi milioni 150 kwa ajili ya kukamilisha maboma matatu ya zahanati. Kwa hiyo maboma haya yote yaliyobakia pamoja na nguvu za mapato ya ndani ya halmashauri, Serikali itaendelea kutenga fedha kuhakikisha maboma haya yanakamilika na kusogeza huduma za afya karibu zaidi na wananchi.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Napenda kuuliza swali la nyongeza moja. Rais aliyepita, Mheshimiwa Magufuli alituahidi kutujengea daraja kutoka Kata ya Ifunda kwenda Kata ya Lumuli sasa napenda kujua, je, tumefikia hatua gani kutekeleza hiyo ahadi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie kwamba Serikali ya Awamu ya Sita, moja ya mpango wetu ni kwamba ahadi zote za Viongozi Wakuu na Viongozi wetu Wastaafu na ile ambayo ilitolewa na Hayati Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, zote zipo katika mipango ya utekelezaji wa Serikali. Kwa hiyo, aondoe shaka zipo pale na Serikali inachosuburi tu ni namna ya kuzitekeleza. Ahsante sana.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pia naomba niipongeze Serikali kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuanzisha mamlaka mapya ya utawala ni kusogeza huduma kwa wananchi, na suala hili limeletwa leo lina mwaka mzima uchambuzi unaendelea. Je, ni lini sasa wananchi hawa watapata jibu sahihi kwamba wilaya yao ianze mara moja?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuanzisha mamlaka mpya ni kweli kunasogeza huduma karibu zaidi na wananchi, lakini pia kuna gharama mbalimbali ambazo zinaendana na kuanzisha makao mapya ya halmashauri. Na ndiyo maana halmashauri nyingi ambazo zimeanzishwa na maeneo mengine ya utawala bado Serikali inawekeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu, ujenzi wa majengo ya utawala halmashauri, ujenzi wa ofisi mbalimbali za maeneo hayo ili kuwezesha wananchi kupata huduma bora kupitia ofisi hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunakwenda kwa hatua, tuko hatua hii, tunakamilisha maeneo hayo na baadaye tutakwenda kwenye halmashauri nyingine na sisi tutashauri mamlaka kadri itakavyoona inafaa kwa ajili ya kuona uwezekano wa kuanzisha mamlaka hizi. Ahsante.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kule Magu Lutale, Wamanga na Igogo, kuna uhitaji mkubwa sana wa vituo vya afya: Je, Serikali ina mpango gani kuyaangalia maeneo yale ambayo yako mbali na huduma? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Jimbo la Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kata ambazo amezitaja Mheshimiwa Mbunge ikiwepo ya Mtalia na hizo nyingine mbili kwa kadri ya uhitaji wa vituo vya afya, Serikali ilishatoa maelekezo kwamba Halmashauri ziainishe kata za kimkakati kwa ajili ya kujenga vituo vya afya, kwa kuwa hatujengi kituo cha afya kila kata wala hatujengi zahanati kila Kijiji, bali tunajenga vituo vya afya kwenye kata za kimkakati ambazo zina vigezo ambavyo vinaelezea na pia zahanati.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge kwamba twende tukaainishe haya maeneo kama ni maeneo ya kimkakati na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Magu alete Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kwenda hatua inayofuata.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Barabara ya Kisesa, Bujola kwenye Makumbusho ya Machief wa Kisukuma imebaki kilometa 1.3.

Je, ni lini itakamilishwa na Serikali kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya ambayo ameianisha ni kwamba mpaka sasa Serikali imeshafanya kazi sehemu kubwa. Kwa hiyo, sehemu ndogo ya kilomita 1.3 iliyobakia na yenyewe ipo katika mpango ili iweze kukamilika. Ahsante sana.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata ya Kisesa Bujorwa Bukandwe Bujashi ambazo zina matatizo ya maji?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo yote ambayo bado miradi haijaanza ama miradi imeanza lakini ipo kwenye utekelezaji tutakavyopata fedha, ndani ya mwaka huu wa fedha na mwaka ujao tutakuja kuendelea na kazi ya usambazaji wa maji.
MHE. BONIVENTURE D. KISWAGA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ni miezi miwili sasa tangu fedha hizi zitumwe kule Buchosa. Je, Serikali inaweza kuwaambia wananchi ni lini mkandarasi ataanza kazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa milioni 45 ni awamu ya kwanza, je, fedha zilizobaki zitatumwa lini ili kuendelea kutekeleza mradi huo?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiswaga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tulipeleka milioni 45 kwa ajili shughuli za awali ambazo zilikuwa kwa ajili ya due technical survey, topographical pamoja na ile ESIAM na tayari shughuli hizi zimekwisha fanyika. Mchakato uliokuwa unaendelea ni kwa ajili ya kutafuta mafundi pamoja na wazabuni wa vifaa mbalimbali kwa sababu utaratibu tutakaotumia katika ujenzi ni ule utaratibu wa force account.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tulikuwa tunaendelea na mchakato huo na hivi sasa mchakato umekamilika, tumekwisha pata mafundi wote kwa ajili ya ujenzi. Lakini vilevile tumepata wazabuni wa kupeleka vifaa eneo hilo. Kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, fedha zote kwa ajili ya ujenzi tayari ziko wizarani na kwa awamu ya kwanza tunapeleka jumla ya milioni 300 kwa ajili ya kuandaa misingi ili baadae tuweze kupeleka fedha nyingine kwa ajili ya sehemu ya juu ya majengo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie tu nimuondoe wasiwasi hatutatumia mkandarasi na badala yake tutatumia mafundi kwa sababu tunatumia force account na fedha sasa hivi tunavyozungumza milioni 300 tayari iko Buchosa ili kuendelea na ujenzi wa misingi ya majengo yote tisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa, wananchi wa Kata ya Mwamanga Kijiji cha Mwamanga, Inolelo na Kisasa B, wanapata shida sana wakati wa mvua kwenda kwenye huduma hasa wanafunzi wa sekondari. Je, Serikali ina mpango gani wa kutupa fedha kwa ajili ya kujenga barabara na daraja hili kuunganisha hasa bottleneck ili wananchi wapate huduma hiyo?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nitakaa na Mheshimiwa Kiswaga tuone katika bajeti ya 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya kuanza ujenzi huu wa daraja katika Kata ya Mwamanga kule Wilayani Magu na kama haijatengewa fedha katika mwaka wa fedha 2023/2024 basi tutaangalia kutenga fedha kwenye mwaka wa fedha 2024/2025.
MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Wilaya ya Nyamagana ina tarafa moja tu, na idadi ya wananchi ni kubwa. Ukigawa kulingana na tarafa mbalimbali maana yake unawanyima fursa wananchi wa Nyamagana kupata huduma stahiki hasa walio pembezoni kule Ngwanyima na Kishiri;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuangalia, hasa idadi ya wananchi na umbali wa kupata huduma kwenye maeneo hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa hali ileile ya Nyamagana inalingana kabisa na hali ya Jimbo la Magu, hasa Kata ya Mwamanga na Kata ya Lutale;

Je, Serikali ina mpango gani wa kuziona kata hizi ambazo ziko mbali na huduma katika vituo vya afya kwenye wilaya zao? (Makofi)

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mabula; la kwanza kuhusu Jimbo la Nyamagana kuwa na tarafa moja tu.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye majibu yangu ya msingi, Serikali iliangalia maeneo ambayo ni pembezoni na yako mbali na huduma za afya kabisa na kuyapa kipaumbe na kuwa ni kata za kimkakati. Hili la Nyamagana tunalipokea kama Serikali na kuweza kuangalia ni namna gani tutapeleka timu ya kufanya tathmini na kuona vituo vya afya vya Serikali vilivyopo katika jimbo hili na kuona uwezekano wa kutenga bajeti ya kuwaongezea vituo vya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Nyamagana.

Mheshimiwa Spika, nikienda kwenye swali lake la pili la kata hizi alizozitaja ikiwemo Kata ya Mwamanga katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa kata hizi za kimkakati kote nchini, ikiwemo katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Tutaangalia katika bajeti ya mwaka 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Magu, ili tuweze kuanza na ujenzi wa kata hizi za Mwamanga na nyingine ambayo aliitaja Mheshimiwa Kiswaga.