Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Mbaraka Salim Bawazir (1 total)

MHE. MBARAK S. BAWAZIR: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Nataka nimwulize Mheshimiwa Waziri, ni lini atamalizia mradi wa maji wa Kilosa, hasa akizingatia kwamba hivi sasa Kilosa kuna kipindupindu? Imebakia pesa kidogo ili wamalizie mradi huo wa maji endelevu.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwenye maji, kwa kweli maji yako mengi sana Kilosa na kuna mabwawa yanahitajika yachimbwe kama Kilimagai, Godegode na Kidete. Haya mabwawa yatasaidia hata kuleta mafuriko ndani Kilosa yangu na vile vile katika…
Duh, ahsante
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nirejee pia kwa Waheshimiwa Wabunge wote. Hii miradi ya maji katika mwaka wa fedha 2016/2017 tumeainisha kila Wilaya ni miradi ipi ambayo ni vipaumbele inakwenda kufanywa na fedha zimetengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba sana Mheshimiwa Mbunge aseme specifically ni mradi upi anaoulizia? Kwa sababu ndani ya Kilosa ipo miradi mingi, ili tuweze kujua hasa ni upi na ni hatua gani ambazo tunaweza kuzichukua. Kwa hiyo, naomba tuwasiliane na Mheshimiwa Mbunge, tukae ili tuweze kubadilishana mawazo tuone ni namna gani huo mradi ambao anauulizia, nimpe majibu ambayo ni sahihi.