Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Mussa Azzan Zungu (2 total)

MHE. MUSSA AZZAN ZUNGU: Mheshimiwa Waziri Mkuu nakushukuru kwa jibu lako, lakini bado niko hapo hapo.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, nchi jirani moja hapa katika hizi za Afrika Mashariki, informal sector watu hawa wa madaladala, vinyozi, welders na kazi za kawaida ambazo siyo rasmi, wamewekwa katika viwango hivyo na wameweza kuchangia kwenye pato la Serikali trilioni nane mwaka 2009.
Hoja yangu ni kwamba, najua changamoto ambazo zipo kwenye Idara za TRA na zingine, basi Serikali ijaribu tu kulipitia na kutazama kwa sababu trilioni nane, kwa informal sector ni sawasawa na kiwango ambacho TRA ndiyo ilikuwa inakusanya miaka minne, mitano iliyopita.
Kwa hiyo, naomba tu Mheshimiwa Waziri Mkuu, mlitazame na mlifikirie kwa siku zinazokuja kama Serikali itaona upo umuhimu wa kuongeza mapato yake, informal sector nayo iweze kulipa VAT na Serikali ipate mapato yake. Nakushukuru.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Azzan Zungu Mbunge wa Ilala, kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa ametoa ombi na kwenye jibu langu la msingi nimesema, bado tunaendelea kukaa pamoja na wadau wetu; ambao ni wafanyabiashara wakiwemo na hao wa informal sector. Kwa hiyo, kadri tutakavyokuwa tunakutana, tunabadilishana mawazo, tunaweza pia kuboresha mfumo mzuri wa ukusanyaji wa mapato, tukitambua pia kwamba, sekta hiyo nayo ina mchango mkubwa sana kwenye pato la Serikali.
Mheshimiwa Waziri Mkuu nakushukuru kwa jibu lako, lakini bado niko hapo hapo.
Mheshimiwa Waziri Mkuu, nchi jirani moja hapa katika hizi za Afrika Mashariki, informal sector watu hawa wa madaladala, vinyozi, welders na kazi za kawaida ambazo siyo rasmi, wamewekwa katika viwango hivyo na wameweza kuchangia kwenye pato la Serikali trilioni nane mwaka 2009.
Hoja yangu ni kwamba, najua changamoto ambazo zipo kwenye Idara za TRA na zingine, basi Serikali ijaribu tu kulipitia na kutazama kwa sababu trilioni nane, kwa informal sector ni sawasawa na kiwango ambacho TRA ndiyo ilikuwa inakusanya miaka minne, mitano iliyopita.
Kwa hiyo, naomba tu Mheshimiwa Waziri Mkuu, mlitazame na mlifikirie kwa siku zinazokuja kama Serikali itaona upo umuhimu wa kuongeza mapato yake, informal sector nayo iweze kulipa VAT na Serikali ipate mapato yake. Nakushukuru.
WAZIRI MKUU: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Azzan Zungu Mbunge wa Ilala, kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa ametoa ombi na kwenye jibu langu la msingi nimesema, bado tunaendelea kukaa pamoja na wadau wetu; ambao ni wafanyabiashara wakiwemo na hao wa informal sector. Kwa hiyo, kadri tutakavyokuwa tunakutana, tunabadilishana mawazo, tunaweza pia kuboresha mfumo mzuri wa ukusanyaji wa mapato, tukitambua pia kwamba, sekta hiyo nayo ina mchango mkubwa sana kwenye pato la Serikali.