Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Additional Questions to the Prime Minister from Hon. Hassan Selemani Kaunje (1 total)

MHE. HASSAN S. KAUNJE:
Mheshimiwa spika, ahsante sana. Mheshimiwa Waziri Mkuu, sababu zinazosababisha muda mwingine kutokupatikana maji ni pamoja na wakandarasi ambao wanakuwa wamelipwa lakini wanashindwa
kukamilisha miradi ya maji kwa wakati na sababu hizo ni pamoja na mradi wa Ng‟apa ambao uko Lindi. Je, ni hatua gani zinachukuliwa na Serikali dhidi ya wakandarasi wa aina hii ili maji yaweze kuwafikia wananchi?
WAZIRI MKUU:
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la
Mheshimiwa Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeeleza kwenye jibu langu la
msingi, suala la wakandarasi wetu kwa sababu malengo ya Serikali tunawapa hizi kazi ili waweze kuzimaliza katika kipindi kifupi sasa kama inatokea mkandarasi hawezi kamaliza kazi kwa kipindi kifupi, ziko sababu mbalimbali ambazo pia tumezizoea maeneo mengine, malipo kutoka kwa kuchelewa nako kutokana na tatizo la fedha inawezekana mkandarasi hajamaliza. Lakini malengo yetu kama mkandarasi analipwa vizuri na kwahiyo basi anatakiwa akamilishe mradi huo kwa wakati uliokubalika. Lakini ikitokea mkandarasi
hajamaliza kama kuna tatizo la fedha hilo ni juu ya Serikali kupitia Wizara ya Fedha kukamilisha kulipa madeni ili mradi ukamilike. Kama mkandarasi amelipwa fedha zote au zaidi ya asilimia 90 na hajakamilisha kwa kipindi kinachotakiwa, zipo taratibu za kisheria za kufanya kwa sababu ameingia zabuni kisheria na kwa hiyo, tunaweza tukatumia utaratibu wa kisheria pia kwa kuadhibu mkandarasi ambaye hajamaliza kazi lakini pia amelipwa fedha.
Sasa sina uhakika na mradi wa Lindi uko katika sura gani na kama
ingekuwa session hii inaweza kumpa Waziri Mkuu nafasi ya kupata majibu sahihi ningweza kukupa jibu sahihi la mradi huo wa Ng‟apa.