Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions from Hon. Zuberi Mohamedi Kuchauka (119 total)

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona. Migogoro ya ardhi kati ya hifadhi zetu na wananchi wanaozunguka hifadhi imekuwa ni migogoro ya muda mrefu na imeenea katika nchi nzima. Katika Jimbo langu la Liwale sisi ni miongoni mwa tuliozungukwa na Hifadhi ya Selous.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunao mgogoro mkubwa sana kati ya hifadhi ya Selous pamoja na Kijiji cha Kikulyungu wakigombea bwawa la Kihurumila. Mgogoro huu umeshapoteza maisha ya watu kwa muda mrefu na hata Mbunge aliyepita wa Jimbo la Liwale mgogoro huu umemfanya asirudi tena Bungeni pale alipotamka Bungeni kwamba anasikia watu wamefariki katika bwawa hilo, badala ya yeye kwenda kujiridhisha na kuangalia hali halisi ya mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini basi Mheshimiwa Waziri atashiriki katika kutatua mgogoro huu ili maisha ya watu wa Liwale yasiendelee kupotea wakigombea bwawa la Kihurumila? Naomba majibu.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo amemaliza kuuliza Mheshimiwa Mbunge hivi punde. Waheshimiwa Wabunge karibu wote wanaopakana na hifadhi wakisimama hapa watazungumza matatizo yanayofanana kuhusiana na suala la mipaka baina ya hifadhi na wananchi wanaoishi jirani nazo.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa niseme tu kwa jibu la ujumla ili kila mmoja ajiandae kupokea matokeo katika hili. Ni kwamba Serikali ya Awamu ya Tano ambayo inatekeleza Ilani ya CCM ya Uchaguzi ya mwaka 2015 - 2020, imejipanga vizuri kwa kuweka suala hili baada ya kuliona kuwa ni tatizo kubwa sana; imejipanga vizuri kwa kuliweka waziwazi kwenye Ilani yake na imesema hivi:
“Katika kutatua migogoro hii, Chama kitaendelea kusimamia Serikali yake kuhakikisha kwamba, kinaendelea kujenga mahusiano mema baina ya Hifadhi za Taifa na wananchi wanaoishi karibu na hifadhi hizo kwa namna ambayo wananchi hao watanufaika na uwepo wa hifadhi hizo.”
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia, Ilani hiyo hiyo ukurasa wa 23 mpaka 25 inasema:
“Tutasimamia zaidi katika kutatua migogoro ya mipaka kati ya wananchi na maeneo ya jirani na hifadhi kwa kushirikisha wadau katika kuhakiki mipaka ya maeneo ya hifadhi kwa kuweka alama za kudumu, kuandaa mipango ya matumizi bora ya ardhi na kuzingatia utawala wa sheria katika kusimamia rasilimali za maliasili.”
Sasa hata wale wanaoingilia katikati ninavyozungumza, pengine wanataka kusema kwamba, hilo ndilo lililoandikwa, lakini wanasubiri utekelezaji. Sasa nataka niseme kwamba, Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga sasa kutekeleza kwa vitendo haya ambayo nimeyasema, kama ambavyo yamekuwa yakisemwa siku zote, lakini sasa hivi tumejipanga vizuri zaidi katika utekelezaji.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nasikitika sana kwa majibu ya kukatisha tamaa yaliyotolewa na Mheshimiwa Naibu Waziri. Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 41 leo, Serikali ya Chama cha Mapinduzi inasema haina mpango wowote wa kujenga Kituo cha Polisi pale, anaposema kwamba ni zaidi ya Wilaya 65, sidhani kama hizi Wilaya nyingine ambazo anazi-include yeye zina umri wa miaka 40. Wilaya ya Liwale ina jumla ya kilometa 66,000 na hizi tarafa anazozisema zipo umbali wa kilometa zaidi ya 60 kutoka Liwale Mjini… (Makofi)
SPIKA: Mheshimiwa Kuchauka, swali sasa!
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, najenga hoja. Wilaya ya Liwale mpaka leo, nimetembelea kile kituo, mafaili yale wanafunika na maturubai, lile jengo walilopanga la mtu binafsi linavuja. Sasa ninachoomba, nipewe time frame, ni lini Kituo cha Polisi Liwale kitajengwa. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, vilevile katika Tarafa ya Kibutuka, ndiyo tarafa inayoongoza kwa ufuta na wafanyabiashara wakubwa wako pale na Kata ya Lilombe sasa hivi kuna machimbo na wafanyabiashara wengi wako pale, ni lini Kata hizi zitajengewa vituo vya Polisi?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba nichukue concern ya Mheshimiwa Mbunge Kuchauka kuhusiana na unyeti na umuhimu wa kujenga kituo pale Liwale, lakini kama nilivyomwambia kwamba vituo hivi pamoja na vingine ambavyo tumepanga kuvijenga, tutavijenga kadri ya fedha zitakavyoruhusu.
Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kwa kuwa Mheshimiwa Mbunge amezungumzia kwa uchungu kuhusiana na matatizo makubwa yaliyopo katika Wilaya yake, basi niseme tu kwamba pale ambapo tutapata fedha tutatoa kipaumbele kwenye kituo cha Liwale.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na swali lake la pili, anauliza kwamba, katika Tarafa ya Kibutuka, ninachoweza kusema ni kwamba kama nilivyojibu katika jibu la msingi, kwamba tumejaribu kupeleka Askari katika Tarafa ile ili waweze kusaidia ulinzi kwa wakati huu, wakati tunajiandaa na ujenzi wa kituo pale ambapo fedha zitapatikana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, natoa shukrani zangu kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu ya kutia matumaini. Lakini nataka ieleweke kwamba Wilaya ile ya Liwale ipo mbali sana na makao makuu ya Mkoa, Wilaya ya Liwale haina usafiri, haina barabara za kutosha yaani za kuaminika, Wilaya ya Liwale haina mtandao wa simu unaoaminika, Wilaya ya Liwale haina usikivu wa redio. Sasa muone jinsi Wilaya hii ilivyo kisiwani, hawa ni miongoni mwa walipa kodi wa nchi hii, sijui kama kodi zao watanufaika nazo vipi? Nashukuru kwa jibu la kwanza nimepata timeframe na mimi nitafuatilia kuhakikisha hii timeframe inafikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa swali la pili napata wasiwasi, nimepata tu majibu ya moja kwa moja. Nahitaji kujua ni lini Redio Tanzania itasikika Liwale? Hapa nimepewa tu majibu ya jumla jumla. Mwisho kabisa hapa amesema kwamba mpango wa muda mrefu sasa hata huo mpango wa muda mfupi nao haujatajwa, huo ni wa lini? Naomba nipatiwe majibu.
vipi? Nashukuru kwa jibu la kwanza nimepata timeframe na mimi nitafuatilia kuhakikisha hii timeframe inafikiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwa swali la pili napata wasiwasi, nimepata tu majibu ya moja kwa moja. Nahitaji kujua ni lini Redio Tanzania itasikika Liwale? Hapa nimepewa tu majibu ya jumla jumla. Mwisho kabisa hapa amesema kwamba mpango wa muda mrefu sasa hata huo mpango wa muda mfupi nao haujatajwa, huo ni wa lini? Naomba nipatiwe majibu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Matatizo yaliyopo kwenye hii Wilaya ya Busanda yanafanana kabisa na yale yaliyoko katika Wilaya ya Liwale. Wilaya ya Liwale hatuna Chuo cha Ufundi, je, ni lini Serikali itatujengea Chuo cha Ufundi Wilayani Liwale?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba Liwale wanahitaji chuo, lakini kwa bajeti ya mwaka huu Liwale haimo katika vyuo vitakavyojengwa. Ninachoshauri kwa sasa ,wale wanafunzi wote wanaohitaji kupata mafunzo haya ya ufundi waende pale katika vyuo vyetu ambavyo viko tayari na chuo ambacho kina uwezo wa kuchukua wanafunzi wengi pale Mtwara na watapata mafunzo yanayostahili.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kukamilika kwa daraja la Mto Kilombero ni wazi kwamba sasa Mkoa wa Morogoro unafunguliwa kibiashara. Nini mipango ya Serikali kuunganisha Mkoa wa Morogoro na Mkoa wa Lindi kwa barabara inayopitia kutoka Liwale kuelekea Morogoro? Ahsante.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kiongozi wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilikuwa ni moja kati ya ahadi yake ya kuhakikisha barabara kutoka Ilonga hadi Liwale inashughulikiwa. Ahadi hiyo tumepewa na nimhakikishie kwamba tutaishughulikia hadi tuikamilishe katika kipindi hiki cha miaka mitano.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa swali la nyongeza. Kwa kuwa, tatizo kubwa la miradi hii ya umwagiliaji ni ule upembuzi yakinifu sijui na usanifu. Kwa sababu, katika Jimbo langu la Liwale kuna Mradi wa Umwagiliaji wa Ngongowele umetumia zaidi ya shilingi bilioni nne na mradi ule sasa hivi uko grounded, hautegemei tena kufufuka. Je, ni nini kauli ya Serikali juu ya pesa zile zilizopotea pale na hatima ya mradi ule?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kuhusu ujenzi wa Mradi wa Ngongowele ni kweli Mheshimiwa Mbunge tumeshaongea naye. Mradi huu umeshakamilika na tulikuwa tunatarajia kwamba sasa wananchi wagawane na kuanza kuutumia.
Mheshimiwa Spika, kama alivyoongea Mheshimiwa Waziri muda mfupi uliopita, miradi mingi hii ya umwagiliaji ilisanifiwa. Nimejaribu kuzungukia miradi ya umwagiliaji, unakuta mradi umekamilika, lakini umekumbwa na tatizo la chanzo cha maji; kimekauka. Sasa hivi tulikuwa tunafikiria kurudia usanifu kuhakikisha miradi yote ambayo imekamilika, basi tunajengea mabwawa ili muda wote iwe inafanya kazi.
Mheshimiwa Spika, miradi mingine imekamilika, lakini unakuta inafanya kazi kipindi cha mvua tu. Baada ya mvua kunakuwa hakuna maji, miradi haifanyi kazi, jambo ambalo siyo lengo. Ni miradi michache tu kama miwili katika mzunguko niliozunguka ndiyo nimekuta kwamba ina vyanzo vya maji vya kudumu ambavyo vinafanya kazi muda wote, watu wanalima mara mbili mpaka mara tatu. Kwa hiyo, alichokizungumza Mheshimiwa Mbunge ni kweli kwamba, huu mradi ulikamilika na umetumia fedha nyingi, lakini una shida kwamba haufanyi shughuli iliyokuwa inatarajiwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Wilaya ya Liwale iko katika Mkoa wa Lindi na ndiyo Wilaya pekee ambayo bado mpaka leo hii inatumia umeme wa mafuta na mashine zile tumezitoa Rufiji, mashine zile zimechoka. Nini kauli ya Serikali kuipatia umeme wa gesi Wilaya ya Liwale ili tuweze kuwa na umeme wa uhakika?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa katika umeme tunaotumia hapa nchini 50% ya umeme tunaotumia unatokana na rasilimali ya gesi.
Kwa hiyo, hata huko Liwale tunachofanya sasa hivi tunajenga miundombinu ya kusafirisha umeme kutoka Mtwara kuja Lindi utakaokwenda katika Wilaya za Liwale, Tandahimba, Nanyumbu pamoja na Masasi umbali wa kilometa 80 ili kupunguza umbali wa kilometa 206 zilizopo sasa. Lengo ni kuunganisha umeme wa gesi katika maeneo yote ya Mtwara na Lindi na maeneo ya jirani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa
Mbunge wa Liwale tunakuhakikishia kwamba kwa sasa hivi hata wananchi wa Liwale sasa wataanza kutumia umeme wa gesi.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Sambamba na Sheria ya Ndoa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliridhia Sera ya Wazee tangu mwaka 2003. Ni lini Serikali italeta sheria kamili ya wazee ili waweze kutambuliwa katika nchi yetu?
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli
kwamba tunayo Sera ya Wazee na sasa hivi tayari tumeshapeleka kwenye Sekretarieti ya Baraza la Mawaziri
mapendekezo ya kutengeneza Sheria ya Wazee ili kuhakikisha kwamba yale ambayo tumeyaweka katika Sera ya Wazee basi yanapewa nguvu ya kisheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ni lini? Ni mara tu baada ya kumaliza taratibu za kutengeneza Sheria hiyo katika
Baraza la Mawaziri tutaleta Bungeni tukiwa tayari.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali moja la nyongeza. Barabara ya Nangurukulu – Liwale, Nachingwea – Liwale, ni barabara ambazo zimo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi, lakini mara nyingi nimekuwa nikiuliza barabara hizi, naambiwa itajengwa, itajengwa; sasa wana-Liwale wanataka kusikia ni lini barabara hizi zitaingia kwenye upembuzi yakinifu na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua tunayoifanya sasa ni kutafuta fedha. Nimhakikishie Mheshimiwa Kuchauka, mara tutakapopata fedha, suala la upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara hii ambayo imeahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi tutaitekeleza.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Niseme tu nasikitika kwa majibu ambayo ni rahisi, majibu mafupi, majibu ambayo hayaoneshi matumaini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo Mheshimiwa Naibu Waziri...
...anasema ubinafsishaji wa matawi 22 yaliyokuwa National Milling tumepata shilingi bilioni 7.4, ni masikitiko makubwa sana; na hii inaonyesha moja kwa moja kwamba sisi huu umasikini umetuandama. kwa sababu kama tunaweza tukatupa…
..ni masikitiko makubwa sana. Msheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna matawi kama Plot 33, Plot 5, Tangold yale matawi sasa hivi yote ni ma-godawn. Watu walionunua matawi ya National Milling ambayo yanafanya kazi ni Bakheresa na Mohamed Enterprises peke yake, lakini matawi mengine yote yaliyobaki yamekuwa ma-godawn na ninyi mnasema mnaenda kwenye viwanda, mimi hapa sijapata kuelewa. Nini hatima ya hayo mashirika ambayo sasa hivi ni ma- godawn badala ya kuwa viwanda? (Makofi)
(b) Kwanza niseme wazi kwamba na mimi ni mmoja kwenye taaluma hii ya usindikaji wa nafaka. Nimefanya kazi National Milling si chini ya miaka 10. Kwa upande wa Kurasini mnamo tarehe 31 Aprili, 2005 waliletewa barua aliyekuwa Meneja pale kwamba kiwanda hicho akabidhiwe Mohamed Enterprises anayekaribia kununua, alikabidhiwa tu kwa sababu anakaribia kununua. Si hivyo tu, wafanyakazi waliokuwepo pale mpaka leo hii wanaidai Serikali hii zaidi ya shilingi milioni 234.3, bado hatima yao haieleweki na kesi imekwisha. Vilevile si hivyo tu, tarehe 20…Hazina wameitwa mahakamani hawataki kwenda, nini hatima ya wafanyakazi wale?
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza nini hatima ya hayo Mashirika ambayo yalikodishiwa na sasa sio viwanda ni ma- godown. Naomba kumkumbusha Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali ilishaanza mchakato wa kufanya tathimini ya viwanda vyote vilivyouzwa na ambavyo vimegeuzwa matumizi.
Mheshimiwa Waziri wa Viwanda alishasimama hapa na kusema na ndiyo kauli ya Serikali, kwamba vyote hivyo vitarejeshwa Serikalini na vitaendelea kufanya kazi, na vitatafutiwa wawekezaji na wataendelea kuviendesha viwanda hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili linalohusu hatima ya wafanyakazi, ameshasema kesi iko mahakamani, ikishakuwa mahakamani naomba nisiliongelee hapa na ni imani yangu kwamba kesi hiyo itaendeshwa na itafika mwisho mzuri.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza kuhusu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano. Nimekuwa nikisimama hapa mara nyingi naongelea Barabara ya Nangurukuru – Liwale na Barabara ya Nachingwea – Liwale. Majibu ninayoyapata ni kwamba barabara hizi zitajengwa katika kipindi hiki cha miaka mitano, lakini barabara hizo sasa hivi hazipitikia kutokana na mvua za masika zilizokatika sasa hivi. Je, nini commitment ya Serikali kwa kuwaokoa hawa Wanaliwale ili waweze kupata barabara inayopitika masika na kiangazi? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kuchauka ni Mjumbe wa Kamati yangu ya Miundombinu na kwa kweli michango yake tunaithamini sana katika Makati hiyo; na amekuwa akiongelea mara nyingi barabara hizi zote pamoja na ile ya kwenda Nangurukuru. Nimhakikishie Mheshimiwa Kuchauka, yale ambayo tumekuwa tukiyajadili katika Kamati ya Miundombinu, Serikali ina dhamira ya dhati ya kuyatekeleza. Hata hivyo, nimwombe, wala sio dhambi, pitia Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ataona nini Serikali iliahidi kwa ajili ya barabara hizi na nimhakikishie tutatekeleza kile ambacho tumeahidi.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuelekea kwenye nchi za viwanda; na ninavyofahamu mimi ili twende huko, lengo kubwa ni kuchakata mazao yanayolimwa hapa nchini; lakini kama ambavyo swali namba 206 lilivyojibiwa, sijaona mkakati unaowekwa kwenye zao la ufuta. Ni namna gani Serikali imejipanga kutangaza ili tupate wawekezaji kwenye kusindika mazao ya ufuta?
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua haya maneno ya mkakati na vipaumbele yanaleta shida. Nilivyosema kwenye swali la msingi Na. 206 nimesema, viwanda vidogo na viwanda vya kati ni viwanda tunavyoweza kuvimudu. Nikaenda zaidi nikasema sisi Waheshimiwa Wabunge tuwe wa kwanza, kwa sababu sisi ni watu ambao tunafuatwa na watu, ni influential, ukianzisha kiwanda wewe cha shilingi milioni 200, watu wa kwenu wote wakianzisha viwanda, viwanda vitatekelezwa. Ndivyo hivyo nilivyosema.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri anasema kwamba mpango mkakati mmojawapo ni kutangaza kuingiza hiyo tovuti na filamu. Hapa swali lilikuwa linataka kujua mkakati thabiti wenye dhamira ya kweli kwa sababu hapo wanaposema, hata barabara ya kufika kwenye hivyo vivutio hakuna. Sasa huu mkakati, hata hao watu unaoingiza kwenye filamu, watafikaje kule Kilwa ambapo kwenye hivi vivutio hamna barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Pwani ya Afrika Mashariki ni mahali ambapo kwanza walikuwa na currency yao, yaani walikuwa na pesa yao; ni Kilwa, lakini haya yote watu hawayajui.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa mfano, ukiangalia Vita ya Majimaji; asili ya vita hii ni Kilwa, lakini makumbusho ya Vita ya Majimaji yako Songea. Sasa Wananchi wa Kilwa walitaka waone, Serikali inafanya taratibu gani kuirudisha Vita ya Majimaji Kilwa na kuitangaza Kilwa kama sehemu ya Utalii? Hilo ni swali la kwanza.(Kicheko)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Kuchauka nafikiri wewe na mimi kwa pamoja tunafahamu kwamba historia ya kwamba Kilwa haifikiki au haipitiki ilikuwa labda zamani; lakini kwa sasa hivi ninavyofahamu na nafikiri Wabunge wengi wanafahamu, kama unazungumzia barabara ya kufika mpaka Kilwa; ni ya lami, kwa maana vivutio vya Mjini Kilwa, yale magofu pamoja na maeneo mengine ya utalii wa kiutamaduni pamoja na utamaduni wa kihistoria.(Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama anazungumzia Mbuga ya Selous, kufika ndani ya Hifadhi ya Selous, ni kweli kuna namna na haja ya kuboresha miundombinu ya kufika ndani ya Selous na kuzunguka ndani ya Selous yenyewe kwa maana ya barabara; lakini iko miundombinu ambayo ni maeneo ya malazi au facilities za malazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, upande mmoja ni jukumu la Serikali, kwa mfano kama barabara, lakini upande mwingine ni jukumu la taasisi binafsi ambazo sasa Mheshimiwa Mbunge usaidie Serikali mnapokaa kwenye Mabaraza kule ya Halmashauri kuweza kuona namna ambavyo mnaweza mkashirikiana na Serikali kuweza kuhamisha wawekezaji wakaweza kuweka vivutio ndani ya Selous.
Mheshimiwa Naibu Spika, pengine nimtaarifu tu Mheshimiwa Kuchauka kwamba mkakati anaoutaka mahususi sasa kwa ajili ya Kilwa yenyewe; sasa hivi tunakamilisha hadidu za rejea kwa ajili ya mkakati mahususi kabisa kwa ajili ya Kilwa. Siyo Kilwa peke yake, kwa ajili ya southern circuit. Huu ni utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Miaka Mitano ambao tunaposema kutekeleza Mpango wa Miaka Mitano, maana yake tunazungumzia diversification kwamba kutanua wigo wa vivutio vya utalii nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kupitia mkakati huo, tuna uhakika kwamba tunakwenda kuboresha mazingira ambayo yataboresha utalii ndani ya Selous lakini pia vivutio ambavyo viko Kilwa Mjini hasa vya utamaduni na kihistoria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la Vita ya Majimaji, hilo suala bado linajadiliwa. Wako upande mmoja katika Kambi nyingine wanasema ni muhimu zaidi kuzingatia kwamba historia ya Majimaji ina mizizi zaidi Kilwa, wengine wanasema ina mizizi zaidi Songea. Sasa nafikiri unatingisha kichwa kwa sababu hayo ni maoni yako, lakini nafikiri suala hili linajadilika, lakini hali ilivyo kwa sasa hivi, mazingira yaliyoko sasa hivi yanazingatiwa kwa mujibu wa historia hiyo hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri utakumbuka siku za nyuma tulikaa hapa tukawa tunazungumzia kuhusu suala la historia kwamba wengine wanasema historia inabidi ziandikwe upya, lakini hatuna sababu ya kuandika upya, lakini tutaweza kuweka utaratibu ulio makini kuweza kuweka suala hilo likakaa sawa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Kama ambavyo Halmashauri ya Itilima ilivyokuwa na tatizo la Hospitali ya Wilaya, Wilaya ya Liwale ni Wilaya ya zamani sana na lile jengo lake la Hospitali ya Wilaya limeshachakaa na limezidiwa uwezo. Kwa kutambua hilo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Liwale imetenga eneo kama hekari 50 hivi kwaili ya mradi wa hospitali mpya ya Wilaya ya Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutuunga mkono katika mradi huu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulikuwa wote site siku ile Liwale na mvua ilikuwa kidogo inanyesha na tumefika Hospitali yake ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wao Liwale pale wana hospitali ya Wilaya, lakini ni hospitali ya muda mrefu sana. Kama wazo hilo zuri lilivyo ambapo mnafikiria kujenga hospitali mpya Serikali haitoshindwa kuungana nanyi, lakini hayo mawazo lazima yaanze kwenu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndio maana kwa kuona umuhimu wa Serikali Mheshimiwa Rais alipita kule kutoa ahadi, na kwa sababu hiyo katika kile Kituo cha Afya cha Kibutuka kwa maagizo ya Mheshimiwa Rais, tutakifanyia ukarabati mkubwa Kituo cha Afya cha Kibutuka kwa kujenga theater pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo kubwa ni kwamba
kina mama wanaopatikana katika eneo lile waweze kupata huduma. Kwa hiyo, Serikali itakuwa tayari kushirikiana na mipango mizuri ya pale.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kunakuwa na matatizo mengi ya miradi mingi ya maji nchini ambayo haikamiliki kutokana na matatizo ya fedha, lakini mara nyingi tukiuliza hapa, nakumbuka Bunge lililopita, Mheshimiwa Naibu Waziri wa Wizara hii alikuwa anasema kwamba Wakurugenzi wetu wakamilishe taratibu za manunuzi, pesa zipo kwenye Wizara.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilipokwenda kwenye halmashauri yangu kwa mfano, nilienda kuulizia suala hili wakasema wameshaandika maandiko mengi kupeleka Wizarani, lakini mpaka leo hawajaletewa hizo pesa na miradi mingi imekwama . Sasa naomba kupata Kauli ya Serikali; ni nini Kauli ya Serikali kwa miradi ile ya maji iliyokwama kwenye halmashauri zetu mbalimbali hapa nchini?
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza; kulingana na fedha za utekelezaji wa miradi zinazopelekwa kwenye halmashauri; tumetoa mwongozo kwamba katika bajeti ambayo kila halmashauri imetengewa wanaweka vipaumbele, wakishaleta andiko Wizarani sisi tunaidhinisha wafanye manunuzi. Wakishafanya manunuzi wakaajiri mkandarasi au mhandisi mshauri tunapeleka fedha kulingana na certificate. Maeneo mengi, halmashauri nyingi zimefuata mwongozo huu na miradi inbaendelea kutekelezwa. Sasa namwomba Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge hili tukutane tuweze kuona, labda kuna tatizo mahususi katika halmashauri ya wilaya yake.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika,ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kutokana na kuharibikaharibika kwa mara kwa mara kwa kinu cha gesi pale Kilwa na kutokana na uchakavu wa mitambo ile, hitajio la Wilaya za Kilwa, Lindi pamoja na Liwale, I mean Kilwa pamoja na Rufiji pamoja na Liwale kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa ni muhimu sana.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba Waziri atueleze hapa ni nini kinachelewesha wilaya hizi kuongizwa kwenye Gridi ya Taifa kwa sababu ya uchakavu wa mitambo ya Kilwa kunafanya umeme usiwe wa uhakika katika Wilaya hizi tatu? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa maeneo ya Kilwa, Rufiji na maeneo ya Mkuranga hivi sasa hayapati umeme wa gridi na maeneo mengine ya karibu na pale, lakini hatua zinazofanyika sasa hivi tunajenga mradi wakusafirisha umeme kutoka Somangafungu ambao nimeutaja, lakini kutakuwa na Mradi wa Rufiji Stiegler’s Gorge ambao unaanza Disemba mwaka huu. Kwa hiyo, kinachochelewesha ni maandalizi ya ujenzi kabambe wa miradi mahususi ambayo itaunganisha wananchi wa maeneo yale na Gridi ya Taifa.
Mheshimiwa Spika, Mradi wa Stiegler’s Gorge na huu niliosema ambao ni wa kusafirisha umeme wa kutoka Somangafungu kupita Kinyerezi mpaka Dar es Salaam ndio pia, utawapatia nguvu ya kutosha ya umeme na kuunganisha kwenye Gridi ya Taifa, maeneo yote ya Rufiji, Kilwa pamoja na Mkoa wa Mtwara pamoja na Lindi. Kwahiyo, wananchi wa mikoa hii miwili niwahakikishie kwamba, ifikapo mwaka 2019/2020 tayari watakuwa wameshaunganishwa na Grid ya Taifa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa sababu tunataka tuingie kwenye Tanzania ya viwanda na Tanzania ya viwanda ni lazima iende sambamba na uwekezaji kwenye ardhi lakini uwekezaji kwenye ardhi unakumbwa na matatizo makubwa. Tatizo la kwanza vijiji vyetu vingi havijaingia kwenye matumizi bora ya ardhi, matokeo yake mwekezaji anakosa nafasi na hata pale ambapo vijiji vimeshaingia kwenye matumizi bora ya ardhi kuna tatizo kwenye Makamishna wa Kanda katika upatikanaji wa ardhi lakini sio hivyo tu, hata kwenye Ofisi ya Rais ambapo nako kuna matatizo...
Je, nini kauli ya Serikali kwa wawekezaji wanaohangaika kutafuta ardhi ya kufanya uwekezaji katika kilimo? (Makofi)
WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa rafiki yangu Alhaj ametaka kujua kauli ya Serikali. Tunalitambua tatizo la upatikanaji wa ardhi, ndiyo maana si mara moja Mheshimiwa Waziri Mkuu na Ofisi ya TAMISEMI wametoa maelekezo kwa mamlaka za Mikoa na Wilaya, watenge maeneo kwa wale walio tayari waweze kuwekeza mara moja. Nirudie, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, tengeni maeneo yule anayetaka kuwekeza msimsubirishe.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ilivyo kwenye matatizo ya mazao ya mbaazi vivyo hivyo kuna tatizo la zao la ufuta, lakini tatizo kubwa la mazao haya ni Bodi ya Mazao Mchanganyiko. Ni nini kauli ya Serikali katika kuiboresha hii Bodi ya Mazao Mchanganyiko iwe na mipango endelevu ya kuendeleza haya mazao ili wananchi wetu waweze kupata soko la uhakika?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa Wizara na Serikali inaendelea na mikakati ya kuboresha Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. Changamoto iliyopo kwa sasa ni namna gani tunaweza tukaanzisha utaratibu wa kusimamia mazao mengi ambayo hayana mfumo wa kuyasimamiwa. Kwa hiyo, kwa sasa Bodi inaendelea na mchakato wa kuangalia namna gani ya kuweza kusimamia kila zao kwa utaratibu wake kama ilivyo kwenye mazao mengine ya biashara. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali inafahamu hilo na linafanyiwa kazi, Bodi inajitayarisha kuangalia namna ya kusimamia siyo zao la ufuta tu lakini vilevile mazao mengine.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, nitoe shukrani kwa Serikali, wanasema kwamba usiposhukuru kwa kidogo basi hata kikubwa hutaweza kupata, kwa sababu nililalamika hapa sina hata kituo cha afya kimoja, lakini sasa hivi nimepewa pesa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha pili na pesa za kuboresha kile kituo cha afya cha zamani ambacho nilisema ni mfu, kwa hiyo nasema ahsanteni sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini bado Hospitali ya Wilaya ya Liwale ina tatizo la nursing officers na mpiga picha wa x-ray. Ni lini Serikali itaweza kutupatia watumishi hawa wa kada mbili; mpiga picha wa x-ray na nursing officers? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, ambalo kimsingi amekuwa akipigania sana wananchi wake na mimi najua na jana alikuwepo na majibu yaliyokuwa yametolewa aliyasikia. Kwa msisitizo na nimejibu katika swali kutoka kwa Mheshimiwa Kigoda kwamba ni vizuri tukaweza kutumia own source kama ambavyo wao wamefanya na katika maeneo ambayo wameajiri ni pamoja na hawa wataalam wa picha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, inawezekana, kama wenzetu wa Handeni wamefanya, Liwale tunaweza. Bahati nzuri kule sasa hivi hali ya kipato inakwenda juu kabisa. Kwa hiyo, ni namna tu ya kupanga kitu gani ni kipaumbele kwa ajili ya wananchi kupata huduma. Ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba kwa kupitia bajeti yake ikiruhusu tutaweza kuajiri na kupeleka watumishi wa kada ya afya.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nipate kuuliza swali la nyongeza.
Matatizo ya mawasiliano katika Halimashauri ya Wilaya ya Liwale na Wilaya nzima ile ni makubwa sana na ujio wa Kampuni ya Halotel pamoja na TTCL tuliona kwamba inaweza kuwa kama mkombozi kwa ajili ya mawasiliano katika Halmashauri ile. Kwa bahati mbaya zaidi, miradi ambayo ilikuwa tayari wananchi wametoa maeneo yao kwa ajili ya kujenga minara katika Kata za Mirui, Ngongowele, Mpigamiti, Mkutano, Ndapata na Igombe na Mtunguni miradi ile yote imesimama hatuwaoni tena wale Halotel…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini kauli ya Serikali juu ya kukwama kwa miradi hii katika hizo Kata nilizozitaja?
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna baadhi ya sehemu ambazo Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote na watoa huduma za mawasiliano wameendelea kupata changamoto mbalimbali katika kutekeleza miradi ya kuweka mawasiliano kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tumeendelea kushirikiana na Waheshimiwa Wabunge mbalimbali katika sehemu mbalimbali kuhakikisha kwamba mawasiliano yanawafikia wananchi kwa wakati. Kwa hiyo, namwakikishia Mheshimiwa Kuchauka kwamba hiyo miradi ambayo imekwama tunaifahamu na tunaifuatilia tutahakikisha kabla ya mwisho wa mwezi wa Juni, 2018 tutawatembelea sehemu hizo ili watu waweze kuwasiliana. Ahsante.
MHE. ZUBER M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vya Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ni vijiji ambavyo vimepakana na hifadhi ya Selous katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, lakini kuna mgogoro mkubwa sana wa ardhi kati ya Kikulyungu pamoja na Selous.
Je, ni lini Mheshimiwa Waziri utaweza kutatua mgogoro huu ambao umedumu zaidi ya miaka 10 na watu tayari washapoteza maisha?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika eneo hili kuna migogoro mingi na kuna eneo kubwa ambalo kwa kweli kuna matatizo. Naomba nikuhakikishie hata jana nilikuwa karibu na pori la Selous katika maeneo ya Mbwande nikishughulikia matatizo ambayo yanafanana na namna hii. Kwa hiyo, katika eneo lako hili la Mpigamiti pamoja na Kikulyungu ambako kuna matatizo naomba niseme kwamba ninalichukua tutaendelea kulifanyia kazi na tutashirikiana na wewe ili kuweza kutafuta ufumbuzi wa hili tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu kusudi wananchi wa eneo lako wapate kufaidika na wapate kufurahi. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Moja ya sababu zinazofanya ucheleweshwaji wa malipo ya korosho ni pamoja na tamko la Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, alitamka kwamba korosho zote za Mkoa wa Lindi na Mtwara zipitie Bandari ya Mtwara kitendo ambacho bandari ya Mtwara ilishindwa kusafirisha korosho hizo kwa wakati na wanunuzi wakaacha kulipa kwa sababu korosho zao mpaka ziingie kwenye maji ndipo waendelee kufanya malipo. Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, sababu ya pili; ni kwamba hata hayo makampuni mnayosema kwamba mnayadhibiti pale ambapo yanakuwa yanachelewesha kulipa lakini bado kuna mtindo wa hayo makampuni kubadilisha majina. Unalifutia jina kampuni hili, mwenye kampuni ni yule yule anatengeneza kampuni nyingine…
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Je, Serikali inatoa kauli gani namna ya kukabiliana na matatizo hayo?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kama alivyosema kwamba kitendo cha kuelekeza korosho ipelekwe nje kupitia Bandari ya Mtwara ilikuwa ni moja kati ya sababu ambazo zilipelekea ucheleweshwaji wa malipo na kuvuruga kwa kiasi fulani soko la korosho. Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo nimueleze Mheshimiwa Mbunge kwamba Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa na Serikali kwa ujumla walifanya hivyo kwa nia njema. Tulitaka vilevile kujenga Bandari ya Mtwara kama moja kati ya bandari zetu, kwa hiyo, ilikuwa ni kwa nia njema. (Makofi) Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vilevile hata ilipotokea changamoto ile ya mizigo kurundikana bandarini, Serikali ilikuwa rahisi kuchukua hatua na kuruhusu ipitie Bandari ya Dar es Salaam. Kwa hiyo, baadae tatizo hilo liliisha. Kuhusu hili la makampuni kutumia majina mbalimbali, ni tatizo kubwa, tunatambua kwamba unakuta mtu mmoja au watu wale wale wanakuwa na kampuni zaidi ya kumi, wana-bid katika soko lile lile. Lakini nikueleze tu kati ya mabadiliko makubwa ambayo tumefanya ni hilo la kuleta kanuni na utaratibu ambao ni lazima kuweka security bid ili baadaye ukishashinda tender baadaye huwezi kukimbia na kusema kwamba sitakuja kuchukua korosho. Kwa sasa ni lazima uchukue kwa sababu usipochukua, fedha zako tayari ulishaziacha na Serikali itawalipa wakulima.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kutokamilika kwa miradi ya maji katika Halmashauri zetu kumekuwa ni tatizo sugu, niliwahi kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri wakati huo ambaye sasa ndiyo Waziri alisema pesa Wizarani zipo ila watu wapeleke certificate. Ninasikitika kumwambia kwamba hapa ninayo makabrashi ambayo ni copy ya hizo certificate ambazo zimeshafika kwenye Wizara yake sasa ni zaidi ya mwaka mzima hizo pesa hazijawahi kutolewa, na kuna miradi kadhaa katika vijiji vya Kipule, Ngongowele pamoja na Mikunya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kauli ya Serikali ni lini miradi hii itakamilika ili wananchi wa vijiji hivi waweze kupata maji. (Makofi)
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa
Mwenyekiti, kwa sababu certificate, ni masula ya kiutendaji Mheshimiwa Mbunge, ninaomba baada ya Bunge hili leo tukutane, twende kwa watendaji tukaangalie certificate kama zipo, kama nilivyosema kwamba tayari nina fedha ili wiki ijayo tuweze kulipa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa utangulizi tu nipende kusema kwamba jibu ni jibu hata kama halikutosha kwa muuliza swali huwa ni jibu. Hii bla bla yote iliyotolewa kwenye aya ya pili mimi sioni kama ni jibu linalijitosheleza kwa sababu mradi huu umehujumiwa kwa kiwango kikubwa sana. Kwenye ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja kwenye Jimbo langu, mimi na Mkuu wetu wa Wilaya na Mkurugenzi wetu wa Halmashauri tulipanga ziara Mheshimiwa Waziri Mkuu akakague aone nini kimefanyika kwenye mradi ule. Hata hivyo, hao watu wa Kanda wa Umwagiliaji wakishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Lindi waliifuta hiyo ziara katika mazingira yasiyofahamika na ni kwa sababu tu huu mradi umehujumiwa kwa kiwango kikubwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, je, Serikali iko tayari sasa kama hii awamu wanayotaka kuisema awamu ya tatu, kutukabidhi Halmashauri mradi huu tuutekeleze badala ya kuwaachia hawa watu wa Kanda ambao wamekuwa wakiuhujumu mradi huu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kutembelea mradi huu ili aangalie pesa hizi shilingi milioni 746 za Serikali ambavyo zimepotea bila sababu zozote zile za msingi? (Makofi)
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na la mwisho, tuko tayari kuongozana na wewe kwenda kuangalia ule mradi. Kwanza nishukuru kwamba umekubali kwamba ule mradi tumetekeleza lakini mafuriko yalitokea, sasa kama tulivyojibu katika swali la msingi tutaunda timu ya wataalam tuipeleke kule iende ikachunguze na huo ndiyo utaratibu wa kisheria wa Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimuombe Mheshimiwa Mbunge tu kwamba Halmashauri ni taasisi ya Serikali, umwagiliaji ni taasisi ya Serikali, hawa wote wanafanya kwa niaba ya Serikali. Kwa sababu wote ni wa Serikali hakuna kitu chochote kwamba pengine Mkuu wa Mkoa alifuta ratiba ya Waziri Mkuu ili asije kuangalia mradi ule, tusilete mgongano kati ya Halmashauri na Idara ya Umwagiliaji iliyo chini ya Wizara ya Maji, zote ni Serikali.
Suala la msingi ni kwamba changamoto ipo, tushirikiane na Mheshimiwa Mbunge tutume timu ikaangalie na kama tulivyojibu kama kuna hujuma yoyote imetokea basi waliofanya hivyo watawajibishwa kwa mujibu wa sheria. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ninachotaka kujua TARURA ni chombo ambaco kimeundwa hivi karibuni, nataka kujua TARURA sasa kwa sababu barabara wanazoshughulikia ni zile zilikuwa zinashughulikiwa na Halmashauri chini ya Madiwani. Je, hiki chombo sasa kinasimamiwa na mamlaka gani kwa niaba ya wananchi, kwa sababu hawaingii kwenye Baraza la Madiwani?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba TARURA ni chombo ambacho kimeanzishwa hivi karibuni. Kimsingi taarifa ya kazi zinazofanyika taarifa yake inapelekwa kwenye chombo kinaitwa DCC na katika DCC Waheshimiwa Wabunge wote wanakuwemo kwenye kile chombo, lakini pia kila Mwenyekiti wa Halmashauri husika anahudhuria kwenye hicho kikao na ndiyo fursa ambayo kwa sasa hivi TARURA inatoa taarifa juu ya utekelezaji wa kazi zake.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama hiyo haitoshi, hata katika vipaumbele vya barabara ambazo zinaenda kutengenezwa ni wajibu wa Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani wote tunaidhinisha barabara ambazo ni vipaumbele, lakini TARURA inapelekewa kulingana na bajeti sasa wao ndio wanasema katika hizi barabara tunaenda kutengeneza barabara zipi, lakini fursa kama forum ya Waheshimiwa Madiwani bado ipo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza nataka kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu ya kuridhisha.
Lakini kwa niaba ya wananchi wa Dar es Salaam na hasa wa hili eneo la Kawe, huu mgogoro ni wa muda mrefu sana. Kama ambavyo Naibu Waziri anasema anataka kushirikisha sasa jamii kuona namna ya kuwapa fidia wale wamiliki wa mwanzo mimi naomba kwamba ushughulikiaji wa suala hili Mheshimiwa Naibu Waziri bado ni mdogo sana. Sasa nataka tu nipate majibu ya uhakika kwamba Mheshimiwa Naibu Wziri unawahakikishia nini watu wa Kawe juu ya upatikanaji wa ardhi ili waweze kuondokana na adha hii ya upatikanaji wa ardhi?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tatizo hili la migogoro ya ardhi Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana hii alishawahi kutuletea taarifa Wabunge hapa Bungeni kwamba tuorodheshe migogoro mingi kwenye majimbo yetu, lakini asilimia kubwa ya migogoro ile bado haijashughulikiwa, nini kauli ya Serikali juu ya kushughulikia migogoro ya ardhi nchini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza ameuliza tunawahakikishia nini wananchi hawa ili kuwapa maeneo mengine waweze kuwa na makazi. Nadhani kwenye jibu la msingi nimeeleza wazi, kwa sababu eneo lile walilivamia na kulikuwa na mashauri mahakamani na bado wananchi wale wakaonekana ni wavamizi. Hata hivyo kwa busara ya Serikali, kwa sababu tulishaona eneo lile limevamiwa kwa kiasi kikubwa, Wizara ikaamua kuwarasimishia, kwa hiyo walitakiwa kurasimishiwa ili waendelee kuwepo pale na wamiliki maeneo yale, lakini wale wananchi hawako tayari kurasimishiwa. Na tukumbuke eneo lile kisheria si la kwao, ni wavamizi na mahakama ilishatamka.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kama wao hawatakuwa tayari kwa zoezi ambalo Serikali imetaka kuwasaidia ili warasimishwe pale basi utaratibu mwingine Serikali haitasita kuchukua kwa sababu mahakama ilishatoa maamuzi na Serikali imeona iwasaidie kwa kuwarasimishia na wao wakae pale kihalali. Kwa hiyo, hatutakuwa na mpango mwingine nje ya pale waliponapo, kwa hiyo kama ni maeneo mengine itabidi wagharamie wenyewe kwenda kununua na waweze ku-settle kama ambavyo tunatoa viwanja kwa watu wengine.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili anaongelea habari ya migogoro; ni kweli tuliorodhesha migogoro mingi na iliundwa Kamati ya Wizara zaidi ya tano na migogoro ile imekuwa ikishughulikiwa katika kila Wizara na migogoro ambayo ilikuwa inaelekea kule, lakini tayari kuna ushauri ambapo kuna kamati iliundwa kwa ajili ya kutoa ushauri wa namna ya kuwa na ufumbuzi wa kudumu wa migogoro ile na tayari Kamati ile ilishamaliza kazi yake, italetwa mtaona namna ambavyo tunakwenda kushughulikia.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa migogoro mingine yote ambayo ilikuwa ndani ya uwezo wa Wizara husika, moja wapo ikiwa ni Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wizara ya Kilimo, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Maliasili na Utalii; wote tumeshiriki pamoja na wenzetu ambao walikuwa wameandaliwa kufanya kazi hiyo.
Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Wizara inafanyia kazi na muda si mrefu mtapata ufumbuzi wa kudumu ambao umepangwa kwa ajili ya kuondokana na migogoro hiyo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kama ambavyo Naibu Waziri ameitambua Kitowelo kwamba atatenga kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Vilevile eneo hilo liko ndani ya kijiji cha Lilombe, lakini tangu uchimbaji huu mdogo umeanza kijiji kile cha Lilombe hakijawahi kunufaika kwa lolote na Halmashauri nzima ya Liwale haijawahi kunufaika kwa lolote, kwa sababu vibali vya uchimbaji vinatoka Kanda, halafu wale wakitoka kwenye Kanda wanaingia moja kwa moja vijijini wanaanza uchimbaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, nini kauli ya Serikali juu ya manufaa wanayoyapata vile vijiji ambavyo tayari machimbo hayo yapo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nakiri jambo ambalo anazungumza na tumezungumza naye kama miezi miwili iliyopita, nikaomba sana nimuagize Mheshimiwa Mkurugenzi wake na Watendaji wa Vijiji ili watumie fursa hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachimbaji wote nchi nzima, wadogo na wakubwa wanatakiwa kutoa ushuru wa Halmashauri husika, wanatakiwa kuchangia maendeleo ya vijiji ambayo shughuli za uchimbaji zinafanyika. Kwa hiyo, nimuombe sana Mheshimiwa Mbunge ikiwezekana nitakafanya ziara huko tutaita mkutano chini ya Mkurugenzi wako, Watendaji wote wa Serikali ambao shughuli za migodi zinafanyika ili sasa Serikali za Vijiji vianze kunufaika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu ni kwamba kila kijiji ambapo kuna mgodi wa aina yoyote mkubwa na mdogo lazima wachimbaji hao washiriki katika shughuli za maendeleo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa ninasikitika tu kwamba hili swali halijajibiwa; kwa sababu hapa nilizopewa ni story tu, nimeona hapa zimepatikana story tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu tatizo letu Liwale ni kwamba Mji wa Liwale unategemea maji kutoka Mto Liwale na Mto Liwale sasa umekauka, kwa hiyo, shida yetu ni kutafuta chanzo cha pili mbadala cha maji. Sasa hapa Mheshimiwa Waziri anasema kwamba hatua ya awali yaani kwa muda mfupi wanakarabati matenki, wanakarabati chanzo cha maji na wananunua dira. Sasa unakarabati chanzo cha maji, unakarabati vipi? Mto umekauka unaukarabati vipi? Matenki unayokarabati unataka uweke nini na mita unazokwenda kufunga unataka zitoe nini? Hapo naona swali bado halijajibiwa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, katika muda mrefu wanasema wametenga shilingi bilioni 3.5 lakini hizi shilingi bilioni 3.5 kuna Halmashauri 14 zimewekwa hapa. Kwa nini sasa Mheshimiwa Waziri hajatenganisha kujua kwamba Halmashauri fulani ina kiasi gani maana kuzifumba hapa ni nini?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ninalouliza mo wamba, scheme ya Umwagiliaji ya Ngongowele itakamilika nini? Nimepewa story tu. Sasa nataka nijue hatua gani imefikiwa ili tuweze kupata chanzo cha maji mbadala kwa Mji wa Liwale, hilo ndio swali ambalo naomba niulize. Vilvile naomba nirudie, tunaomba mradi wa Ngongowele ukamilike. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kwenda na mimi kuangalia huo mradi?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, utangulizi umesema majibu yote ni story, sio story ndiyo ukweli ulivyo. Mto Liwale ambao ndiyo chanzo cha maji cha Mji wa Liwale unakauka kiangazi na ndio maana tunaweka sasa upembuzi yakinifu. Lakini nikwambie maana ya ukarabati, ukarabati ni kuongeza uwezo ndani ya huo ukarabati basi tutabaini ni eneo gani sasa baada ya mto kukauka tunaweza tukapata maji ambayo yatahakikisha yanahudumia Mji wa Liwale bila matatizo yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nije kwenye swali namba moja; hatua tunayoichukua ni kufanya upembuzi yakinifu, upembuzi yakinifu utabaini chanzo cha maji cha kudumu pamoja na huo Mto Liwale. Ikiwa siwezi kuanza kuzungumza utafiti utakaofanyika lakini baada ya kufanyika itabainisha ni wapi tutakuwa na maji ambayo yatakuwepo kwa miezi 12 ama kwa visima ama kwa kujenga bwawa ili yale maji yanapokuwa ni mengi kipindi cha kiangazi tuyapeleke kwenye bwawa tuyahifadhi ili tuweze kuhakikisha kwamba sasa Mji wa Liwale unakuwa na maji mwaka mzima. Ndio hatua tunayoichukua sasa hivi tunachukua hatua ya kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.
Mheshimiwa Mwenyekiti, umeuliza swali kuhusu mradi wa umwagiliaji utakamilika lini. Mradi ule ulikamilika, umepata madhara ya mafuriko. Sasa hivi tumepata fedha kutoka Serikali ya Japan, tunapitia miradi yote ambayo ilikuwa imekamilika lakini imepata matatizo mbalimbali yakiwemo ya kukosa maji, unakuta kwamba kilimo kinafanyika mara moja badala ya mara mbili. Kwa hiyo, tunafanya mapitio ya hiyo miradi ikiwemo mradi wako wa Ngongowele ili tuweze sasa kuhakikisha kwamba tunauimarisha ili wananchi waweze kunufaika na kile walichokitarajia. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Kama ilivyo Mahakama ya Kasulu ni chakavu, lakini Wilaya ya Liwale ni Wilaya ambayo ina umri wa miaka 42 mpaka leo haina jengo la Mahakama. Jengo linalotumiwa ni lile jengo ambalo lilikuwa Mahakama ya Mwanzo ambalo sasa hivi limechakaa limefika mahali ambapo mafaili yanafunikwa na maturubai. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuijengea Liwale Mahakama ya Wilaya?
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Wilaya ya Liwale itajengwa mwaka 2017/2018.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina misitu mikubwa miwili; kuna ule msitu ambao unahifadhiliwa na WMA (Ustawi wa Vijiji) na ule msitu wa Serikali ambao ni Msitu wa Nyera, Kipelele. Msitu huu ni msitu ambao tumeurithi kutoka enzi za Wakoloni, lakini mpaka leo harversting plan ya msitu ule haijatoka. Nini kauli ya Serikali kuharakisha harvesting plan ya msitu huu ili wananchi waweze kupata faida ya kuwepo kwa msitu huu wa Nyera, Kipelele? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika misitu miwili anayoizungumzia, labda niseme tu kwa ujumla, harvesting plan anayoizungumzia maana yake ni mpango wa uvunaji. Tunao mpango wa uvunaji ambao tumeupitisha hivi karibuni unaoeleza namna ambavyo tunaweza tukavuna misitu lakini tukizingatia uvunaji endelevu ili uvunaji usizidi kasi ya kukua kwa misitu na hatimaye tukajikuta kwamba tunamaliza misitu zaidi ya kuitunza na kuifanya iendelee kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wakati wowote ule Mheshimiwa Mbunge atakapopata nafasi aje Wizarani, tunaweza tukamwelekeza namna gani au tunaweza tukamwonesha harvesting plan jinsi ilivyo aweze ku-share na wananchi wa maeneo ambayo yanahusika kwa ajili ya matumizi ya wananchi wake.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Waziri anasema kwamba mpango mkakati mmojawapo ni kutangaza kuingiza hiyo tovuti na filamu. Hapa swali lilikuwa linataka kujua mkakati thabiti wenye dhamira ya kweli kwa sababu hapo wanaposema, hata barabara ya kufika kwenye hivyo vivutio hakuna. Sasa huu mkakati, hata hao watu unaoingiza kwenye filamu, watafikaje kule Kilwa ambapo kwenye hivi vivutio hamna barabara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo hivyo tu, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri kwamba Pwani ya Afrika Mashariki ni mahali ambapo kwanza walikuwa na currency yao, yaani walikuwa na pesa yao; ni Kilwa, lakini haya yote watu hawayajui.
Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kwa mfano, ukiangalia Vita ya Majimaji; asili ya vita hii ni Kilwa, lakini makumbusho ya Vita ya Majimaji yako Songea. Sasa Wananchi wa Kilwa walitaka waone, Serikali inafanya taratibu gani kuirudisha Vita ya Majimaji Kilwa na kuitangaza Kilwa kama sehemu ya Utalii? Hilo ni swali la kwanza. (Kicheko)
Swali la pili...
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza Mheshimiwa Kuchauka nafikiri wewe na mimi kwa pamoja tunafahamu kwamba historia ya kwamba Kilwa haifikiki au haipitiki ilikuwa labda zamani; lakini kwa sasa hivi ninavyofahamu na nafikiri Wabunge wengi wanafahamu, kama unazungumzia barabara ya kufika mpaka Kilwa; ni ya lami, kwa maana vivutio vya Mjini Kilwa, yale magofu pamoja na maeneo mengine ya utalii wa kiutamaduni pamoja na utamaduni wa kihistoria. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kama anazungumzia Mbuga ya Selous, kufika ndani ya Hifadhi ya Selous, ni kweli kuna namna na haja ya kuboresha miundombinu ya kufika ndani ya Selous na kuzunguka ndani ya Selous yenyewe kwa maana ya barabara; lakini iko miundombinu ambayo ni maeneo ya malazi au facilities za malazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, upande mmoja ni jukumu la Serikali, kwa mfano kama barabara, lakini upande mwingine ni jukumu la taasisi binafsi ambazo sasa Mheshimiwa Mbunge usaidie Serikali mnapokaa kwenye Mabaraza kule ya Halmashauri kuweza kuona namna ambavyo mnaweza mkashirikiana na Serikali kuweza kuhamisha wawekezaji wakaweza kuweka vivutio ndani ya Selous.
Mheshimiwa Naibu Spika, pengine nimtaarifu tu Mheshimiwa Kuchauka kwamba mkakati anaoutaka mahususi sasa kwa ajili ya Kilwa yenyewe; sasa hivi tunakamilisha hadidu za rejea kwa ajili ya mkakati mahususi kabisa kwa ajili ya Kilwa. Siyo Kilwa peke yake, kwa ajili ya southern circuit. Huu ni utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Miaka Mitano ambao tunaposema kutekeleza Mpango wa Miaka Mitano, maana yake tunazungumzia diversification kwamba kutanua wigo wa vivutio vya utalii nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kupitia mkakati huo, tuna uhakika kwamba tunakwenda kuboresha mazingira ambayo yataboresha utalii ndani ya Selous lakini pia vivutio ambavyo viko Kilwa Mjini hasa vya utamaduni na kihistoria.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la Vita ya Majimaji, hilo suala bado linajadiliwa. Wako upande mmoja katika Kambi nyingine wanasema ni muhimu zaidi kuzingatia kwamba historia ya Majimaji ina mizizi zaidi Kilwa, wengine wanasema ina mizizi zaidi Songea. Sasa nafikiri unatingisha kichwa kwa sababu hayo ni maoni yako, lakini nafikiri suala hili linajadilika, lakini hali ilivyo kwa sasa hivi, mazingira yaliyoko sasa hivi yanazingatiwa kwa mujibu wa historia hiyo hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri utakumbuka siku za nyuma tulikaa hapa tukawa tunazungumzia kuhusu suala la historia kwamba wengine wanasema historia inabidi ziandikwe upya, lakini hatuna sababu ya kuandika upya, lakini tutaweza kuweka utaratibu ulio makini kuweza kuweka suala hilo likakaa sawa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa swali la nyongeza. Halmashauri ya Mji wa Liwale ulikuwa na miradi ya maji wa vijiji 10, lakini mpaka sasa hivi vijiji vyote 10 vimeshatobolewa lakini vijiji vilivyofungwa miundombinu ya maji ni vijiji vitatu tu. Vijiji ambavyo sasa hivi vina maji ni Kijiji cha Mpigamiti, Barikiwa, pamoja na Namiu. Je, vile vijiji saba vilivyobaki lini watatoa pesa kwa ajili ya kujenga miundombinu kumalizia vile visima ambavyo tayari vimeshatobolewa?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa kwamba chanzo cha maji cha Mji wa Liwale kinatokana na Mto Liwale na ni kweli kwamba chanzo kile kidogo kimeleta shida. Katika bajeti ya fedha ya mwaka unaokuja tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya study ili tuweze kuimarisha chanzo au kutafuta chanzo kingine kuhakikisha vijiji vilivyobaki sasa vinapata maji bila wasiwasi wowote na hii itatekelezwa kwenye mwaka wa fedha unaokuja ambapo bajeti yake Mheshimiwa na yeye mwenyewe nafikiri aliikubali siyo kwamba aliikataa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale yenye kata 20 na kituo kimoja cha aya haina gari ya wagonjwa. Shida tuliyonayo ni kubwa sana ukizingatia mtawanyiko wa kata zetu zile pale Wilaya ya Liwale mwenyewe Mheshimiwa Naibu Waziri ni shahidi, umefika, umeona jinsi shida ya Wilaya ya Liwale ilivyo juu ya kupata gari la wagonjwa. Ni lini sasa Serikali itatupatia gari la wagonjwa katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Liwale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika fursa nikiwa nahudumu katika nafasi ya Naibu Waziri Ofisi ya Rais, TAMISEMI nimepata nafasi ya kwenda Liwale na tukakutana na Mheshimiwa Mbunge katika kazi nzima ya kujenga kituo cha afya na muitikio wa wananchi wa Liwale ni mkubwa sana katika kujitolea katika shughuli za maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie kwa spirit niliyoiona na hakika na mapato ambayo wanapata kutokana na zao la korosho na wakasimamia vizuri kabisa mapato ya kwao na kituo kile cha afya kikikamilika hitaji la kwanza la wananchi naomba nimuagize Mkurugenzi katika vipaumbele vyake vya kwanza ni pamoja na kuhakikisha kwamba wananunua gari la wagonjwa kwa sabbau wezo upo, pesa zikisimamiwa vizuri, kulikoni kuishia kugawana kama posho hakika uhitaji mkubwa wa gari la wagonjwa wafanye kama kipaumbele.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Liwale ni mji unaokua kwa kasi sana hasa baada ya korosho kufanya vizuri na kuna mradi wa kutafuta chanzo cha maji mbadala kwa Mji wa Liwale. Mradi ule sasa hivi una zaidi ya miaka minne umesimama. Nini kauli ya Serikali juu ya kuwapatia maji wananchi wa Mji wa Liwale? (Makofi)
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Ilani ya Chama cha Mapinduzi imeelekeza kwamba maeneo yote ya vijijini yatapata maji kufikia asilimia 85 na mijini asilimia 95. Mheshimiwa Mbunge naomba uvute subira kidogo, tarehe 7 mpaka 9 Mei, 2018 tutawasilisha bajeti yetu kwa hiyo miradi yako yote ambayo ilikuwa imekwama utapata kidogo maelekezo kule ndani na tutahakikisha kwamba mradi huu unatekelezwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza; wakati wa upanuzi wa Kiwanda cha Umeme cha Liwale wakati wanapanua ile plant yao, walichukua mashamba ya wananchi ambapo mpaka leo hii zaidi ya miaka mitano wananchi wale hawajui hatima ya malipo yao. Nini kauli ya Serikali namna ya kuwalipa wale wananchi mashamba yao?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Kuchauka kwa swali la nyongeza na ninampongeza pia kwa kazi zake, lakini nataka niseme kwamba suala la fidia kwa mashamba ambayo yamechukuliwa kwa upanuzi wa kituo cha kuzalisha umeme Liwale, naomba kwa kuwa kwa takwimu kwa sasa hivi sina, naomba nilichukue.
Naomba tu nimpe Mheshimiwa Mbunge taarifa ya nyongeza kwamba kwa sasa kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa laini ya msongo wa Kv 132 inayotoka Kituo cha Kuzalisha Umeme Mozambique, nataka nimthibitishie na jitihada ambazo zinaendelea za Wizara kuhakikisha Mikoa ya Kusini, Lindi na Mtwara inapata umeme kutoka Gridi ya Taifa kwamba kwa hivi karibuni Wilaya ya Liwale itapata umeme kupitia kituo hicho na kwamba hata yale matumizi ya mafuta ya kuzalishia umeme Wilaya ya Liwale yatapungua na umeme utapatikana kwa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la fidia nitalichukua, baada ya Bunge hili tutalifanyia mchakato wa kupata taarifa ya uhakika. Ahsante. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Awali naomba uelewe kwamba haya maswali tunayoyauliza hapa na sisi wawakilishi yanaulizwa kwa niaba ya wananchi wetu, kwa hiyo, hii ni kero ya wananchi. Sasa tunapopata majibu yasiyoridisha na majibu ambayo yana mkanganyiko, tunapata mashaka sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi wa Septemba, 2017 niuliza swali hili na Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana alitumia sekunde zisizozidi tano akaniambia Mahakama ya Wilaya ya Liwale itajengwa mwaka 2018. Sasa leo hii naambiwa itajengwa kwenye bajeti ya 2018/2019. Kwa nini wanakuwa na majibu ya kudanganya wananchi wakati sisi ni wawakilishi wao na hizi ni kero wanatupa ili wapate majibu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza…
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sambamba na Mahakama ya Wilaya ambayo nadanganywa kwamba itajengwa kwenye mwaka ujao wa bajeti, je, Serikali ina mpango gani kujenga Mahakama za Mwanzo katika Tarafa za Kibutuka na Makata? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba huduma za Mahakama zinawafikia wananchi wote nchi nzima kwa ukaribu na pasipo upendeleo wowote na ndiyo maana katika bajeti ambayo Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria ameisoma hapa tumeelezea mahitaji yaliyopo na mpango wa Serikali katika kuhakikisha kwamba Mahakama hizi zinajengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondelee hofu Mheshimiwa Kuchauka kwamba Serikali hii si Serikali ya kudanganya kama alivyokuwa ameainisha awali Mheshimiwa Waziri na mimi pia nimesema hapa leo ni kwamba Mahakama hii itajengwa na ipo katika mpango huo kwa sababu hivi sasa tumepata nafasi ya kuwa na ushirikiano mzuri na Chuo Kikuu cha Ardhi na Baraza la Nyumba la Taifa ambapo tunatumia teknolojia rahisi sana ya ujenzi wa Mahakama kupitia teknolojia ya moladi. Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba kama Serikali ilivyoahidi, Mahakama ya Wilaya ya Liwale itajengwa. Hivi sasa navyozungumza katika mpango wa bajeti ya mwaka huu tuna mpango wa kujenga takribani Mahakama za Wilaya 29. Kwa hiyo, Mheshimiwa atupe imani, Mahakama hiyo itajengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusu Mahakama za Mwanzo, ni kweli ni dhamira ya Serikali kuendelea kuzijenga Mahakama za Mwanzo nyingi kadri ya upatikanaji wa fedha kwa sababu kwa hivi sasa tuna upungufu wa Mahakama za Mwanzo takribani 3,304 nchi nzima. Kwa hiyo, nimuondolee hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba pindi pale bajeti itakaporuhusu na fedha zitakapopatikana Mahakama hizo pia zitajengwa ili kuwafanya wananchi wa Jimbo la Liwale waweze kupata huduma ya Mahakama kwa urahisi zaidi.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu yanayoridhisha ya Mheshimiwa Waziri, mgogoro huu, kama mwenyewe anavyokiri ni wa muda mrefu na mimi nimeshakwenda kwa Mheshimiwa Waziri wa Ardhi akaniambia kwamba mgogoro huu bado uko kwenye ngazi ya mkoa, watakaposhindwa ngazi ya mkoa watauleta Wizarani. Nimekwenda kwa Mkuu wa Mkoa ameniambia kwamba yeye ameshauandikia Wizarani kwa maana ya kwamba wameshashindwa.
Mheshimiwa Spika, hata h ivyo, mimi mwenyewe binafsi nimemuandikia Mheshimiwa Waziri kumjulisha mgogoro huu mpaka sasa hivi sijapata majibu yoyote. Sasa kutokana na huu mkanganyiko wa kauli za Serikali, Mkuu wa Mkoa anasema hili na Waziri anasema lingine, nini kauli ya Serikali juu ya mgogoro huu yaani nani kati yao yuko sahihi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, anasema mgogoro huu utashughulikiwa mwaka huu wa 2018/2019. Je, Mheshimiwa Waziri, yuko tayari kuandamana na mimi baada ya Mkutano huu twende akaangalie hali halisi? Kwa sababu tayari watu walishaanza kuchomeana ufuta, juzi hapa ufuta wa Kijiji cha Mirui umekatwa na wananachi wa kutoka Kilwa.
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya familia, napenda kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa namna ambavyo wameshiriki katika msiba huu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni wiki mbili tu kabla ya msiba nilikuwa kule na nimefika mpaka kwenye jimbo lake. Taarifa nilizozipokea kutoka mkoani, walisema migogoro yote walikuwa wameorodhesha na wakasema kama mkoa wameunda timu za kiwilaya wanashughulikia migogoro yao, itakapowashinda wataileta Wizarani na taarifa ya maandishi wamenipa.
Mheshimiwa Spika, nataka tu nimhakikishie kwamba pamoja na kwamba timu ya Wizara iko kule katika kushughulikia ule mgogoro, lakini pia mkoa ulijiridhisha na ukaniridhisha pia mimi nilipokuwa kule kwamba migogoro yao wanaisimamia wenyewe kwa sababu haijawashinda na wakikamilisha Wizara itakwenda kuweka mipaka, hasa katika yale maeneo ambayo yana utata wa mipaka.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Utekelezaji wa REA Awamu ya Tatu kwenye Mkoa wa Lindi tumepata Mkandarasi ambaye uwezo wake ni mdogo sana. Mpaka sasa hivi awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mradi huu ishafika nusu ya wakati wake lakini bado yuko kwenye Wilaya moja tu ya Ruangwa. Ni lini mkandarasi huyu ataweza kufika Liwale?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Kuchauka juu ya changamoto za utekelezaji wa miradi hii ya REA Awamu ya Tatu na mkandarasi. Lazima nikiri kwamba mkandarasi wa Mkoa wa Lindi State Grid kuna matatizo ambayo yanaendelea kufanyiwa kazi.
Kwa hiyo, nimthibitishie tu, hivi karibu Mkandarasi huyu zitakapoisha changamoto hizi atafanya kazi kama ilivyokusudiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapa tukutane na Mheshimiwa Mbunge na wote wa Mkoa wa Lindi ili tuweze kujadili suala hili. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Kusini unaozungumzwa ilikuwa uchangiwe pamoja na Wilaya ya Liwale, Nachingwea na Masasi kutokana na mikoa hii kuwa mbali na Makao Makuu ya Mikoa. Serikali kusitisha uanzishwaji wa Mkoa huu wa Selous, huoni kwamba ni kuwanyima haki ya kimsingi wananchi wanaokaa maeneo haya ambao wako mbali sana na Makao Makuu ya Mkoa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza katika swali lake ameongeza maeneo ambayo hayajawahi kujadiliwa; yapo maeneo aliyoyaongeza hapa kama Liwale na wengine wanazungumza Nanyumbu kwamba iwe katika sehemu ya Mkoa mpya wa Selous.
Katika majadiliano yaliyofanyika, maeneo hayo hayakutajwa kwamba ni sehemu ya mapendekezo ya Mkoa mpya. Sasa kwa sababu ni mapya basi naomba sana Mheshimiwa Kuchauka ayapeleke kwenye Mkoa wake wa Mtwara ili waweze kuyajadili kuanzia huko. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vilivyotajwa na Mheshimiwa Waziri kwamba, ndiyo vinavyochangia katika Wilaya ya Liwale kwa Selous, vijiji hivi ndivyo vilivyoanzisha mgogoro kwa sababu vijiji hivi vimepakana na Selous kwa Mto wa Matandu. Kwa nini Kikulyungu peke yake ndio ambayo imeonekana kwamba imeondoka Matandu na ndio maana wanakijiji Wakikulyungu waligoma. Sasa Mheshimiwa Waziri ninachotaka kujua je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kufuatana na Mheshimiwa Waziri wa Ardhi muende mkatafsiri GN ambayo inaitambua Pori la Akiba la Selous ukiachana na hii tangazo la mwaka 1974?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba tuko tayari kuongozana na Mheshimiwa Waziri pamoja na viongozi wengine wa Mkoa wa Lindi ili tushughulikie migogoro yote inayohusu mpaka wetu kule. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu la msingi Mheshimiwa Waziri amesema kwamba Bodi ya Mazao Mchanganyiko iko imara na haijatetereka. Naomba kuuliza kwa nini wakati tunaingiza zao la ufuta kwenye stakabadhi ghalani wasimamizi wakapewa Bodi ya Maghala badala ya Bodi ya Mazao Mchanganyiko?
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjibu Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Bodi kununua mazao na mfumo wa kuuza ni vitu viwili tofauti. Hata hiyo Bodi ya Mazao Mchanganyiko ikitaka kununua zao linalouzwa kwa mfumo wa stakabadhi ghalani, itabidi na wao waende wakanunue huko kwenye huo mfumo. Siyo kwamba Bodi ya Mazao Mchanganyiko maana yake ni mfumo wa stakabadhi ghalani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, Bodi na yenyewe itashiriki kununua kama wanunuzi wengine walivyo kwa kwenda kununua kwenye mfumo huo wa stakabadhi ghalani. Kwa hivyo, namwomba tu Mheshimiwa Mbunge asichanganye haya mambo, Bodi hii itafanya biashara ya kununua mazao na kuuza kwa kushindana na wafanyabiashara binafsi na watu wengine katika mazao mbalimbali.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 43 sasa, licha ya kukosa nyumba za Askari walioko kule hata kituo cha Polisi hatuna, umri wa miaka 43. Ni lini Serikali itatujengea Kituo cha Polisi cha Wilaya ya Liwale, kuondokana na adha ya kupanga kwenye nyumba ambayo wamepanga, nyumba yenyewe nayo ni mbovu? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Spika, ni sahihi. Liwale pia, inahitaji kuwa na kituo, niliwahi kuongea na Mheshimiwa Mbunge tukakubaliana kwamba, mara litakapomalizika Bunge twende pamoja mimi na yeye Jimboni kwake tuweze kushirikiana tuone jinsi gani tunaweza tukafanya ili kuharakisha huu mchakato wa ujenzi wa kituo hiki ikiwezekana kwa kuanzia kuwashirikisha wananchi na wadau mbalimbali wakati tukisubiri jitihada za Serikali za kukamilisha ujenzi wa kituo hiki zitakapokuwa zimekamilika. Kwa hiyo, ahadi yangu na Mheshimiwa Mbunge kama tulivyozungumza iko pale pale. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kabla sijauliza swali la nyongeza kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa Mawaziri wote wanaohusika kuona wahudumu kwenye wizara hii kwa kunipunguzia tatizo la wafanyakazi, baada ya kunipatia wafanyakazi sita kwenye kada hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya shida iliyopo wale wafanyakazi sita imekuwa kama tone la damu kwenye bahari. Kwa hiyo, shida iliyopo katika hospitali yetu ya Wilaya ya Liwale ni kubwa sana kiasi kwamba wauguzi wawili wanahudumia wodi tano kwa wakati mmoja, jambo hili ni baya sana vilevile linapunguza ufanisi wa kazi.
Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuniongezea wafanyakazi kwenye kada hii ya wauguzi ili kuongeza ufanisi kwenye hospitali ile ya wilaya?
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba tunajua na tunatambua mahitaji ya watumishi wa afya ikiwa ni pamoja na Manesi katika hospitali za Liwale. Pindi tutakapopata watumishi basi Wilaya ya Liwale ni moja ya wilaya ambayo na sisi tutaizingatia.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Baada ya tasnia ya korosho mwaka 2017 kufanya vizuri sana msimu uliopita, mwaka huu kumekuwa na matatizo ya mgogoro katika Mkoa wa Lindi kati ya Chama cha Ushirika cha Runali na Bodi ya Korosho. Jambo hili limefanya mpaka sasa hivi sulphur iwe bado haijafika katika Mkoa wa Lindi jambo ambapo limefanya sasa hivi mfuko mmoja wa sulphur kufika shilingi 70,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba Serikali itoe tamko, ni lini mtatuletea sulphur ili kupunguza bei ya sulphur ambayo imepanda baada ya kuwa na mgogoro kati ya Runali na Bodi ya Korosho?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna tatizo la kuchelewa kwa sulphur, lakini kutokana na swali lake alilouliza, mpaka sasa hivi ni kwamba Chama kile cha Runali kimeshaagiza tani 128 za sulphur, zimeshafika na zimeshasambazwa. Vilevile kwa faida ya wengine hata TANECU wameshaagiza tani 1,100 na tayari zimeshasambazwa na zinauzwa kwa shilingi 32,000. Nashukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kutokana na swali hili. Kwa sababu sasa Harvesting Plan imekamilika ina maana sasa Serikali inaenda kuanza kupata mapato kutokana na msitu huo. Hata hivyo, kama ilivyo watu wa baharini au ziwani, uchumi wao mwingi unategemea mali ya bahari na mali ya ziwa. Vilevile sisi tulio kwenye misitu uchumi wetu mkubwa unategemea mazao ya misitu. Sasa kwa nini Serikali mpaka leo hii ile cess haijapata kuongezwa kutoka asilimia tano tunayoipata kutokana na uvunaji huu wa misitu, angalau ifike asilimia 10 ili kuweza kuinua kipato cha Halmashauri tunazozunguka?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, TFS wamekuwa na tabia ya kutotoa ile responsibility kwa vijiji vyetu yaani ile incentive. Sio hivyo tu kuna mazao ambayo yamevunwa na wavunaji haramu ambayo yapo kwenye Halmashauri zetu kwa muda mrefu yanaendelea kuharibika. Je, Serikali haioni sasa inaweza kutoa kwenye Halmashauri husika yale mazao ambayo yamevunwa kwa haramu ili yaweze kunufaisha kwenye vijiji vyetu, kwa mfano mazao ya mbao, yanaweza kutusaidia kutengeneza furniture au viti, meza na madawati kwa ajili ya shule zetu na hospitali zetu?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, asilimia tano ya cess ambayo TFS wamekuwa wakitoa kwenye Halmashauri, iko kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa ya mwaka 1982 na sisi kama Wizara hatuwezi kuibadilisha na hatuwezi kuikiuka. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge kama anataka ibadilike anaweza kuanzisha mchakato huo, lakini kwa sasa maelekezo yetu ni kutoa asilimia tano.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, ni kweli kwamba maeneo ya Liwale kuna mbao nyingi ambazo zilikamatwa wakati wa Operation Tokomeza, na mbao hizo bado kesi zake ziko Mahakamani. Hata hivyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, mara uvunaji huu niliosema utakapoanza, tutawaelekeza TFS kuhakikisha kwamba wanatoa misaada kwenye shule zote ambazo ziko jirani na maeneo ya uvunaji.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mji wa Liwale ni Mji unaokua kwa haraka sana na una chanzo kimoja tu cha maji; na kutokana na mabadiliko ya tabianchi, chanzo kile hakitoshelezi tena. Je, ule mradi wa kutafuta chanzo mbadala cha maji kwa Mji wa Liwale, umefikia wapi?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, lakini na pili nimepata nafasi ya kufika katika Jimbo lake la Liwale. Pamoja na jitihada kubwa za Serikali zinazofanyika lakini kiukweli, Liwale kuna changamoto. Sasa sisi kama Wizara tulishawaagiza watu wetu wa rasilimali za maji katika kuhakikisha wanafanya utafiti wa kina ili tuweze kupata chanzo cha uhakika, tuweze kubuni mradi mkubwa ambao kwa ajili ya kutatua kabisa tatizo la maji Liwale. Nataka nimhakikishie sisi tutalifanya jambo hili kwa haraka ili wananchi wake wa Liwale waweze kupata maji ya uhakika.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nangurukuru-Liwale ni muhimu sana kwa wakazi wa Liwale, lakini siyo hivyo tu ni barabara iliyoahidiwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2015-2020. Je, Serikali inawaambia nini wana Liwale juu ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimpongeze tu Mheshimiwa Kuchauka kwa sababu namfahamu amekuwa akiifuatilia sana barabara hii, ni kilometa 230 kutoka Nagurukuru - Liwale. Niwahakikishie tu wananchi wa Liwale kwa ujumla wake, maana walikuwa wanajiona kama wako Kisiwani. Mheshimiwa Kuchauka anafahamu tunatoka Nachingwea, kilometa 129 kuja Liwale na tuko kwenye hatua ya usanifu. Namwomba Mheshimiwa Mbunge asiharakishe tu shughuli, tutakuja na pendekezo kwenye bajeti yetu inayokuja kwa ajili ya kusanifu barabara hii ya kutoka Nangurukuru - Liwale.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niliombe tu Bunge lako tutakapokuja na pendekezo hilo watupitishie ili twende kusanifu barabara hii ya Mheshimiwa Mbunge Kuchauka na hatimaye tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante wa majibu ya Serikali athari kubwa ya mgogoro huo ni kijiji cha Kikulyungu kuondolewa kwenye WMA ya Jumuiya ya Magingo na kwa majibu haya inaonekana mgogoro huu umefika mwisho.

(i) Sasa ni lini Serikali itakuja Kikulyungu kuwapa wananchi matokeo ya maamuzi haya na kuwapa kibali au kuwapa kibali au kuwapa hati ili waweze kurudishwa kwenye Jumuiya ya Magingo?

(ii) Na kwa sababu sisi tunaoishi kwenye maeneo ya hifadhi kumekuwa na uharibufu mkubwa sana wa mazao unaotokana na wananyama waharibifu kama tembo, nguruwe, na wananyama wengine waharibu. Na Serikali imekuwa ikitoa kitu kinachoitwa kifuta machozi sasa ni lini Serikali itakuja na marekebisho ya sheria ili badala ya kutoa kifuta machozi iwe wananchi wao wanapata fidia inayotokana na uharibifu wa mazoa ya mashambani?
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimuahidi kwa kuwa taarifa ya kamati ambayo ilienda kuhakiki mipaka imekamilika na ipo mezani kwangu, kwamba baada ya Bunge hili la Bajeti kuisha aidha nitaenda mwenyewe ama nitamtuma Mheshimiwa Naibu Waziri kwenda kuzungumza na wananchi wa kijiji cha Kikulyungu kwenda kuwapa matokeo ya taarifa ya kazi iliyofanywa na kamati iliyokuwa chini ya uzongozi wa Wizara ya Ardhi ambayo ili hakiki mpaka ule kwa hivyo ni lini baada ya Bunge la Bajeti kumalizika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili kuhusu Serikali kuachana na kulipa kifuata machozi ama pia na kifuta chasho kutokana na uharibifu wa unaofanywa na wanyama wakali na waharibifu badala yake tulipe fidia. Ngumu kwa Serikali kuji-commit kwamba itaanza kulipa fidia ya uhalibifu unaofanywa na wanyama wakali na wanyama waharibifu na sababu zipo wazi. Kwa mfano mnyama amesababisha umauti wa raia wa mwananchi huwezi kusema utalipa fidia ya mnyama kuua mwanadamu kwa sababu thamani ya mwanadamu haiweezi kulinganishwa na kitu chochote kile.

Kwa hivyo, hiyo ni bahati mbaya ambayo inakuwa imetokea tunachoweza kulipa pale ni kufuta machozi na sio fidia. Lakini thamani ya mazao vilevile ni ngumu kusema Serikali itaji- commit kulipa fidia balada ya kufuta jasho kwa sababu changamoto zilizopo ambazo zinahusiana na wanyama hawa kwenda kwenye maeneo ni nyingi wakati mwingine wananchi wanawafuata wanyama kwenye mapito yao ama kwenye mazalia yao ama maeneo ya mtawanyiko na wakati mwingine sisi viongozi tukiwemo Wabunge, madiwani tunahamasisha sana Serikali imege maeneo ya hifadhi ambayo kiuhasili ni lazima yatapitiwa na wanyama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, kusema Serikali itaji-commit kwa kweli kulipa fidia ni jambo gumu kwa sababu gharama itakuwa kubwa sana mwisho wa siku tutashindwa kutunza hizi maliasili ambazo sisi zote tunapaswa kuzilinda kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 27.

Kwa hivyo ninawaomba sana wa kwa Waheshimiwa Wabunge wote na wananchi wote watambue kwamba wanyamapori ni maliasili ya Taifa, ni utajiri, ni urithi wa Taifa letu na hatuwezi kwamwe kuacha kuilinda kwa ajili ya matumizi ya sasa na vizazi vijavyo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika mradi wa kutafuta chanzo cha pili cha mbadala cha maji ya Wilaya ya Liwale palitolewa shilingi milioni 300 na DDCIA walishaanza kufanya kazi hiyo lakini wamechimba visima viwili ambavyo vina uwezo wa kutoa maji lita 5,000 lakini visima vile vimetelekezwa mpaka leo.

Je, Serikali iko tayari kutoa fedha kwa ajili ya kwenda kufanya uendelezaji wa visima vile ambavyo viko katika Kijiji cha Makata na kijiji na Mikunya?
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza labda kwa nia njema kaisa katika kuhakikisha visima hivi vinakuwa endelevu labda baada ya saa saba nikutane na Mheshimiwa Mbunge na tuweze kufanya mawasiliano na wenzetu ili tangalie ni namna gani tunaweza tukasaidiana naye. Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Baada ya Mtwara kupatikana kwa gesi Mheshimiwa Waziri akatangaza kwamba Liwale nao tutapata umeme wa gesi kutoka Mtwara. Wakati ambapo Mheshimiwa Waziri anatangaza nikamwomba nikamwambia kwa umeme ule wa Mtwara nafuu Liwale wakatuachia umeme wetu wa mafuta, lakini jambo hilo halikutekelezwa, matokeo yake sasa Liwale umeme unapatikana kwa shida sana.

Je, Mheshimiwa Waziri anatuahidi nini sisi watu wa Liwale shida hii tunayoipata mwisho lini? Maana sasa hivi umeme haupatikani kabisa, unawaka masaa mawili au matano.
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushuruku kwa kunipa nafasi ya kujibu swali la nyongeza ya Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kupitia Chama cha Mapinduzi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Kuchauka ameelezea katika swali lake la nyongeza kwamba tulitoa ahadi ya kuunganisha Wilaya ya Liwale katika umeme wa gesi, lakini kwa sasa nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ni kweli kuwa Wilaya ya Liwale kwa mara ya kwanza imeunganishwa na grid ya Taifa kupitia Kituo cha Maumbika, lakini tunatambua changamoto iliyojitokeza katika maeneo mbalimbali ambapo tumeunganisha grid ya Taifa lakini inatokana na umbali wa kusafirisha umeme huyo kufikia katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Shirika la TANESCO lipo katika hatua ya manunuzi ya kifaa ambacho kitakuwa na uwezo wa kurekebisha hali hiyo ili isiendee. Kwa hiyo niwathibitishie wakazi wa Wilaya ya Liwale, wakazi wa mikoa ya Lindi na Mtwara ambao wameunganishwa kwenye grid ya Taifa, wakazi pia wa Mkoa wa Ruvuma na wakazi wa Biharamulo, Ngara kwamba tatizo ni muda na limepatiwa ufumbuzi na kwamba likishashughulikiwa wataona faida ya umeme wa uhakika ambao unatokana na grid ya Taifa, kuliko huu ambao ni wa mafuta ambao kwa kweli umelisaidia shirika kuokoa kiasi cha pesa na kuweza kuendelea kuwekeza katika maeneo mengine. Kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na kwa kuwa hivi karibuni kwenye tarehe 21 nitafanya ziara katika jimbo lake, nitatoa hayo maelezo. Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Awali ya yote, niishukuru Serikali kwa kuliona hili na kupandisha hadhi Hifadhi ya Selous, lakini baada ya kupandisha hadhi au baada ya Serikali kuimarisha uhifadhi katika hifadhi zetu suala la wanyamapori limekuwa ni shida sasa hivi, hasa wanyama kama tembo. Wanyama hawa sasa hivi wanasumbua kwenye maeneo yetu na niliuliza swali hapa kuhusiana na Serikali kuleta Muswada pengine kupata fidia wakasema haiwezekani, lakini bado suala la kifuta machozi hakipatikani. Je, Serikali ipo tayari kutupatia fedha hizi mapema iwezekanavyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maliasili inapozungumzia utalii Kanda ya Kusini, bado napata changamoto. Mwaka jana tumepata fedha kuendeleza utalii Kanda ya Kusini, lakini Wizara hii inapozungumzia Kanda Kusini wanazungumzia Morogoro, Mbeya na Iringa, lakini Mkoa wa Lindi, Mtwara na Songea hautajwi. Je, Serikali kwa upande wake inapozungumzia kukuza utalii ukanda wa kusini unaamanisha mikoa ipi? Ahsante sana.
NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo amekuwa akifuatia haki za wananchi wake hasa wanaoathirika na matatizo ya kuharibiwa kwa mali zao na kuhatarisha usalama wao na wanyama waharibifu kama tembo. Nilifanya naye ziara kwenye jimbo lake na tulifanya mikutano takriban mitatu na tulizungumza na wananchi hasa kwenye mgogoro wao wa mpaka na Selous.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni kweli kwamba tuliahidi hapa tutaleta marekebisho ya kanuni, kanuni zipo lakini Wizara yetu inazipitia upya ili kanuni hizo zinapokwenda kulipa fidia hiyo fidia iwe angalau na thamani kulingana na uharibifu uliofanywa kwa sababu zimekuwa za muda mrefu. Kanuni hizo zimekuwa ziko tayari na Mheshimiwa Waziri hivi karibuni alikuwa amealika wadau kuzipitia na mara baada ya wadau kupitia, tutazitangaza na zitaanza kutumia. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge ni kweli awali zilikuwa malipo yake ni kidogo, lakini tumezipita.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kuchelewa kwa kifuta jasho suala hili linahusisha taratibu na taratibu zinaanzia kwenye halmashauri yenyewe kwenye vijiji. Wataalam wetu wa vijiji wa kilimo wanapaswa kulifanya suala hili kwa haraka kwa kulipeleka kwa Afisa Wanyamapori wa Wilaya na baadaye linafika kwenye level yetu ya Wizara na kwa sababu ni la nchi zima, mara nyingi tumekuwa tukiangalia first in, first out. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, ni suala la utalii kusini, ni kweli imekuwepo tafsiri kwamba unaposema utalii kusini unamaanisha Lindi, Ruvuma na Mtwara, lakini tunapozungumzia kwenye Mradi wa REGROW ni utalii wa Nyanda za Juu Kusini. Sasa hivi Wizara yetu ipo katika hatua za mwisho za kuandaa utaratibu ambao tutafanya mkutano tena kama tulivyofanya na watu wa Nyanda za Juu Kusini ili kufungua utalii wa kusini kwa maana ya Mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma. Kwa hiyo nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge hatujasahau eneo hili, tunalifanyia kazi na Wizara inashirikisha wataalam kutoka vyuo vikuu mbalimbali katika kuangalia maeneo ambayo yanaweza kutuletea mafanikio ya haraka ikiwa ni pamoja na kufungua milango ya mikoa hii yote ambayo inapakana na bahari na hasa katika maeneo ambayo tuna mali kale nyingi kama maeneo ya Mikindani na Kilwa. Nakushukuru sana.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri na Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuongezea majibu kwenye sehemu ya swali la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka kwamba tunapozungumzia utalii Kanda ya Kusini, hatuzungumzii utalii wa Kanda ya Kusini ambayo ipo kwenye nyanda ya juu peke yake, tunazungumzia kusini kwa ujumla wake. Mradi wa REGROW pamoja na ku-include na pori la Akiba la Selous la zamani na sasa Nyerere National Park ambayo ipo kusini proper huku lakini pia imejikita kutengeneza Mji wa Iringa kama kama hub ya utalii, lakini mradi huu upo kwenye awamu hii ya kwanza awamu ya pili utatanua maeneo zaidi kwenye upande wa Kanda ya Kusini upande huo wa akina Mheshimiwa Zuberi Kuchauka.

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo kuna miradi mingine mikubwa inayoendelea kule ikiwepo Mradi wa SECAD lakini pia ikiwemo mradi wa kukifanya Kisiwa cha Kilwa Kisiwani ile malikale iliyopo pale kama kivutio cha kipekee. Pale tumewaelekeza TAWA ambao kwa sasa tumewapa dhamana ya kuwaendeleza utalii kwenye eneo hili Kilwa Kisiwani, wanunue boti ya kitalii ambayo itakuwa ya first class na business class, lakini pia wawekeze kwenye lodge ya kitalii ambayo itakuwepo katika eneo hilo la kisiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna mradi mkubwa utakuja pale kama wananchi watatoa ushirikiano, kuna zaidi ya trilioni moja itawekezwa pale katika eneo la fukwe zilizopo pale kusini kuanzia Kilwa mpaka Msimbati na hivyo tunaamini utalii wa fukwe unaweza ukakua kwa kiasi kikubwa sana katika eneo lile kama wananchi watatoa ushirikiano ili tuweze kuilinganisha Hifadhi ya Taifa ya Nyerere na fukwe zilizopo pale kusini. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Awali ya yote nitoe pole kwa wananchi wa nchi nzima hii ambao wamepata adha ya mafuriko hasa wa Wilaya yangu ya Liwale na Mkoa wa Lindi. Nawapa pole sana Mwenyezi Mungu aendelee kuwapa nafuu wakati huu wanahangaika na makazi yao.

Mheshimiwa Spika, suala la kilimo hakuna mtu ambaye hajui kwamba nchi yetu asilimia 75 ni wakulima lakini naona Serikali usimamizi wa kilimo wameachia Vyama vya Ushirika ambavyo havina uwezo wa kulisimamia. Mfano kwa suala la kuagiza vifaa au pembejeo wameachiwa Vyama vya Ushirika ambapo wao ndiyo wanaoingia mikataba na suppliers wa pembejeo hata kwenye mauzo. Kama Serikali mtaamua kuviachia Vyama vya Ushirika kusimamia kilimo basi tutendelea kusuasua kwenye kilimo.

Mheshimiwa Spika, mfano mzuri mwaka huu kwenye zao la korosho tumechelewa msimu tumekuja kuanza msimu mwezi wa kumi na moja wakati korosho wakulima wameshaanza kuzivuna tangu mwezi wa nane. Jambo hili mliliachia kwenye Vyama vya Ushirika matokeo yake tumechelewa kuanza msimu toka mwezi wa Novemba mpaka leo wakulima bado wana korosho.

SPIKA: Sasa swali.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Je, Serikali ipo tayari kusimamia mazao haya badala ya kuviachia Vyama vya Ushirika?
WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza si kweli kwamba tumeachia Vyama vya Ushirika kusimamia mazao. Mazao mengi hasa ya kimkakati yanasimamiwa na Bodi za Mazao ikiwemo Bodi ya Korosho na Vyama Ushirika vimekuwa vinakusanya hayo mazao na kuyapeleka sokoni kwa ajili ya kuuza kwa niaba ya wanachama si kwamba vinasimamia uzalishaji na hili tutaendelea kulifanyia kazi na tutaendelea kulisimamia.

Mheshimiwa Spika, lakini nilitaka kusema tu kwamba kama alivyosema Mheshimiwa Naibu Waziri tunataka mazao yote, pembejeo zote, kuanzia mbegu, mbolea viuadudu, hivi vyote vitakuwa vinasambazwa na sekta binafsi katika maeneo yote. Tunataka Watanzania watumie fursa hii kuona kwamba sasa ni wakati mwafaka kuna fursa ya kupeleka viuadudu vya korosho, pamba, kahawa na katika mazao yote tunataka sekta binafsi isambaze vitu vyote hivyo badala ya kutegemea Serikali. Serikali sisi tutasimamia kuratibu maendeleo ya zao na namna ya kutafuta masoko lakini siyo kusambaza pembejeo ni fursa kwa Watanzania.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niwaombe tu Mheshimiwa Kuchauka na Watanzania wote wanaotaka kusambaza sulphur huko kwenye zao la korosho, wanaotaka kupeleka viuadudu huko kwenye pamba, wanaotaka kupeleka kwenye kahawa, kwenye tumbaku sio Vyama vya Ushirika ni sekta binafsi. Sisi tutasimamia ubora wa usambazaji wa vitu hivyo ili viwafikie wakulima.

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na niwaombe Watanzania watumie nafasi hiyo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni wilaya ambayo ilianzishwa mwaka 75 leo ina umri wa miaka 45. Wilaya ile ina kata 20 lakini Mahakama mbili tu Mwanzo, na Mahakama ya Mwanzo ya Liwale Mijini ndio inayochangiwa na Mahakama ya Wilaya kwa maana kwamba Mahakama ya Wilaya hawana jengo. Lakini nilipouliza swali hili mwaka 2017 Mheshimiwa Kabudi akiwa hapo kwenye hicho kiti alisema mwaka 2018 inajengwa hospitali ya Wilaya. Je, Serikali kwenye majibu yale mlikuwa mnanidanganya?
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyoelewa ni kwamba huwa kunakuwa na jitihada za pekee, kama Waziri anatoa majibu, anafanya kila njia kuweza kuhakikisha kwamba inatekelezwa. Ningependa kurudi na kutazama rekodi za mazungumzo hayo na jitihada ambazo zilifanywa, lakini Liwale ni mahali ambapo kama ulivyoona mchakato wa kufungua Mahakama katika Wilaya za Lindi na Mtwara, umekuwa ukiendelea kwa kasi sana. Kama kulikuwa na ahadi kama hiyo, Wizara tungependa kufuatilia na Mahakama iendelee kujitahidi kutekeleza ahadi hizo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Nangurukuru - Liwale ni ya vumbi na kokoto lakini naishukuru Serikali mwaka huu tumetengewa fedha shilingi milioni 300 kuanza usanifu wa kina. Hata hivyo, mvua zilizonyesha mwezi uliopita zimelaza watu siku tatu barabarani. Ni nini mkakati wa Serikali kuifanya barabara hii ipitike majira yote? (Makofi)
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Mbunge Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama alivyosema mwenyewe tumetenga fedha kwa ajili ya kuifanyia usanifu wa awali na usanifu wa kina, malengo ni kuijenga kwa kiwango cha lami ili haya matatizo ya mvua yanapojitokeza yasije yakaleta athari kwa wananchi. Hata hivyo kwa vile umetuambia tutaifanyia kazi, hela ya emergency ipo ili tuweze kurudisha hiyo miundombinu wananchi waendelee kutumia barabara hiyo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni Wilaya kongwe yenye umri zaidi ya miaka 44 sasa; pamoja na kwamba Halmashauri wametenga eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi, lakini hadi leo Wilaya ya Liwale haina Kituo cha Polisi. Nini kauli ya Serikali namna ya kuwapatia wananchi wa Liwale ujenzi wa Kituo cha Polisi?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Kuchauka hiki kimekuwa ni kilio chake cha muda mrefu sasa, lakini nimhakikishie kwamba kilio chake siyo cha peke yake, hata sisi Serikali tuna kilio hicho hicho kuhakikisha kwamba Wilaya ya Liwale kulingana na umuhimu wake inapata Kituo cha Polisi. Kwa hiyo, nimhakikishie kwamba pale ambapo tutaweza kufanikiwa kupata fedha, basi tutajenga hicho Kituo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Vilevile napenda kutoa shukrani kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu ya msingi niliyosema shule hii ni shule pekee katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, shule pekee yenye inawachukuwa watu wenye mahitaji maalum, kwa takwimu hiyo utaona kabisa kwamba bado kuna tatizo la miundombinu, shule hii inahitaji mabweni na ndiyo maana inakuwa na takwimu ndogo ya walemavu kwa sababu walemavu wengi kutoka vijijini wanashindwa kumudu kuandikishwa kwenye shule hii kwa sababu ya ukosefu wa mabweni, lakini siyo hivyo hata wale walimu hao anaowataja...

MWENYEKITI: Uliza swali basi Mheshimiwa.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, najenga hoja; je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kujenga mabweni kwenye shule hii ili watoto wanaotoka nje ya Halmashauri hii waweze kumudu kuingia shuleni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa sababu ya mahitaji ya wanafunzi hawa wanatakiwa wafuatiliwe kule wanapokaa manyumbani kwa sababu hawakai bweni kwahiyo panahitajika usafiri wa walimu hao kuwafuatilia kule wanapoishi kuona maendeleo yao namna gani wanavyo catch yale masomo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwanunulia vifaa kama vile mapikipiki hawa walimu watatu waliobaki ili waweze kumudu kuwafuatilia hawa watoto manjumbani kwao?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tunakubaliana na Mheshimiwa Mbunge, kwanza tunaunga jitihada za Mheshimiwa Mbunge katika kuhakikisha kwamba hawa wanafunzi wenye uhitaji maalum wanapewa kipaumbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge jana nilipata fursa ya kuongea na mkurugenzi na tukakubaliana kwamba hicho kiasi cha shilingi milioni 50 itatengwa kuanzia mwezi Desemba wakati tutakapokuwa wanafanya review ya bajeti yao kwa sababu na wanaona ni jambo la muhimu sana kuhakikisha watoto hawa wanakuwa katika mazingira yaliyo bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini katika swali lake la pili anaongelea swala zima la usafiri ili walimu waweze kwenda kupata fursa kwenda kuwabaini hata wanafunzi wengine ambao wanashindwa kujiunga kutokana na adha iliyoko huko, naomba ni muhakikishie Mheshimiwa Mbunge ni azma ya Serikali, siyo walimu peke yao ni pamoja watumishi wote ikiwepo wale wa Ustawi wa Jamii kuhakikisha kwamba tunawabaini watoto wetu wote bila kujali hali zao ili waweze kupelekwa katika maeneo ya kuweza kujufunza sawa na watoto wengine ambao hawana ulemavu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo Mheshimiwa Waziri amejibu mimi kwanza nimpongeze kwa majibu yake mazuri, lakini bado kuna tatizo la hawa watendaji wetu yaani kwa maana kwamba Wenyeviti wa Vijiji na Madiwani ni kwamba hawajapata semina, pamoja na kwamba sheria/sera bado haijaletwa ya ugatuzi wa madaraka lakini bado uko umuhimu wa kuwapa semina mara kwa mara ili waweze kujua mipaka yao ili waweze kuboresha utendaji wao wa kazi.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapa semina hawa watu, Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji ili waweze kufanya kazi vizuri? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, inawezekana kuna maeneo hawa viongozi hawajapata semina lakini ninachojua na maelekezo ya TAMISEMI ambayo na mimi nimesema nilikuwa Mwenyekiti wa Mtaa tulifanyiwa baada ya uchaguzi wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa wale viongozi wakishapatikana kabla ya kuanza kazi wanapewa semina ikiwa ni pamoja na kuapishwa, hawa wajumbe wanakula viapo vya uaminifu kwenye ngazi ya Halmashauri na wanapaswa kuapishwa na Mwanasheria Mkuu wa Halmashauri husika, hilo linapaswa kufanyika, kama kuna mahali halikufanyika nitaomba kwa sababu tunaenda kwenye uchaguzi wa mwaka huu tutalisimamia ili viongozi wakishapatikana wapate semina, waapishwe lakini kubwa zaidi ni lazima wajue mipaka yao ya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, yako majukumu na kuna tofauti kubwa kwa mfano ya Wenyeviti wa Mitaa na Wenyeviti wa Vijiji, Wenyeviti wa Mitaa ni waratibu wa shughuli za Serikali za Mitaa, wakati Wenyeviti wa Vijiji ni Serikali kamili wana maamuzi wanaweza hata wakachukua rasilimali za eneo fulani wakauza wakafanya miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hayo mambo tutayasimamia ili yaweze kufanyiwa kazi na naomba viongozi wetu wa Halmashauri na Mikoa wajipange, baada tu ya uchaguzi haitakiwi Mjumbe wa Serikali ya Mtaa au wa Kijiji au Mwenyekiti aanze majukumu yake bila semina, kiapo na mafunzo tutayazingatia na chuo chetu kikuu cha mafunzo ya Serikali za Mitaa za Hombolo kina nafasi hiyo na hata nyie Waheshimiwa Wabunge mnakaribishwa hata sasa mkitaka na wajumbe wenu mnawapeleka pale, tuna nafasi ya kutosha walimu waliobobea, karibu Hombolo Chuo cha Serikali za Mitaa wapate mafunzo ili wafanye kazi kwa kuboresha huduma za kijamii. (Makofi)
MHE.ZUBERI M.KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye Bandari ya Mtwara, lakini commitment ya Serikali katika matumizi ya bandari ile bado haijaonekana. Mfano leo hii kule kuna kitengo cha mafuta (kuna pump ya mafuta ambayo inatakiwa wananchi wa Kanda ya Kusini wote wachukulie mafuta kwenye bandari ya Mtwara lakini ukienda kwa wafanyabiashara bado wanalalamika kwamba mafuta ya Mtwara yako bei juu kuliko Dar es Salaam, matokeo yake watu wanatoka Songea, wanatoka Lindi, wanatoka Tunduru wanafuata mafuta Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, nini kauli ya Serikali namna bandari hii inaweza kutumika efficiently na sisi watu wa Kanda ya Kusini tukanufaika kwa kuwepo kwa bandari hii?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa
Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nini commitment ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kazi kubwa ya Serikali ni kutengeneza miundombinu na tayari commitment ya Serikali imeonekana kuiboresha Bandari ya Mtwara ili iweze kufanya kazi kama ilivyopangwa na ndiyo maana katika jibu langu la msingi sasa tunatangaza na kuitangaza Bandari ya Mtwara ili iweze kutumika kwa sababu sasa inauwezo wa kupokea meli zote kubwa na tungeshauri wafanyabiashara wote waweze kutumia bandari ya Mtwara na hasa wale wa Ukanda wa Kusini. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, sambamba na barabara ya Masasi – Nachingwea, barabara hii vilevile ina jina la Lukuledi
– Liwale yenye jumla ya kilometa 175 kwa maana kutoka Masasi mpaka Liwale kilometa 175. Barabara hii tayari imeshafanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Wanaliwale wanataka kusikia barabara Nachingwea – Liwale lini itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja kama nilivyosema tunatambua ni muhimu na zimeahidiwa kujengwa katika bajeti ambayo tutaanza kuijadili. Kwanza ni barabara ambayo ipo kwenye Mpango wa Miaka Mitano na tunategemea katika bajeti inayoanza itatengewa fedha ili ianze kujengwa.

Mheshimiwa Spika, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ya zao la kokoa iliyoko kule Mbeya ni sawasawa kabisa na changamoto ambayo zao la korosho kwenye Wilaya ya Liwale inakumbana nayo. Kwenye msimu uliopita 2018/2019 mikorosho yenyewe ilikuwa inakauka bila kujua sababu ni nini. Kwenye msimu huu uliopita kwa nje zinaonekana korosho ni nzima lakini ukizipasua kwa ndani zimeoza.

Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutuletea wataalam kwenye Wilaya ya Liwale waje kufanya tathmini au utafiti kujua ni nini changamoto za korosho Wilaya ya Liwale zinazosababisha wananchi wale wapate bei isiyoridhisha?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ufupi tu siyo tuko tayari, timu ya Wizara ya Kilimo leo ina wiki mbili ikishirikiana na watu wa TAFA na Naliendele. Timu hii wako Mkoa wa Mtwara na wengine wako Ruvuma kuangalia athari zilizojitokeza katika msimu uliopita ili tuwe tuna majibu sahihi ni athari za kimazingira ama kuna attack kwenye mimea yetu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza. Tatizo kubwa la masoko ya tumbaku linafanana kabisa na tatizo la soko la korosho, lakini mimi nimegundua tatizo hili linasababishwa zaidi na kuwepo kwa mdudu mmoja anaitwa Vyama vya Ushirika. Vyama vya Ushirika vimekuwa vikiyumbisha sana masoko kwa wakulima wetu.

Je, Serikali iko tayari kuleta sheria ya Vyama vya Ushirika ili kuvifanyia marekebisho kuondoa matatizo yaliyoko kwenye vyama hivi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kuchauka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali iko tayari kuleta sheria na tunafanyia mapitio sheria ya ushirika, lakini sio sahihi kufikiri kwamba mfumo wa ushirika ndiyo una haribu mfumo wa kuuza mazao, bali kuna washirika wanaoharibu vitu vya namna hiyo na Serikali imekuwa ikiwachukulia hatua. Lakini suala la sheria tuko kwenye mchakato na tutaileta Bungeni kuifanyia marekebisho. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale unakua kwa haraka sana na mahitaji ya maji yamekuwa ni makubwa na uhaba wa maji ni mkubwa sana. Bajeti iliyopita tuliletewa fedha shilingi milioni 100 kwa ajili ya kutafuta chanzo cha pili cha maji cha Mji wa Liwale lakini mpaka leo tunaambiwa DDCA hawana nafasi ya kuja Liwale. Ni lini Serikali watakuja sasa kutafuta chanzo cha pili cha maji kwa ajili ya Mji wa Liwale?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Liwale. Kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo anafuatilia na amekiri tumewapatia shilingi milioni 100. Nachoweza kumwambia hawa DDCA nitawasimamia na nitahakikisha ndani ya mwezi huu Aprili watakuja ili waweze kuona kwamba shughuli ambayo ilipaswa kufanyika basi sasa inaenda kutekelezwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza. Ni kwamba, Serikali yetu sasa hivi imeingia kwenye mfumo wa Serikali ya viwanda na uhamasishaji huu umekuwa mkubwa sana. Katika Wilaya ya Liwale viko viwanda vidogo vidogo kazi yake ni kusindika korosho, lakini wananchi wale wanashindwa kupata mali ghafi kwa sababu ya kuwa na mitaji midogo. Tunafahamu kwamba korosho, zinazalishwa, zinauzwa kwenye minada; na kwa sababu wale wawekezaji ni wadogo wadogo hawawezi kuingia kwenye mnada matokeo yake anapoingia kwa wananchi kwenda kununua korosho anaoneka wananunua kangomba.

Mheshimiwa Spika, je, sasa Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wale wadogo wadogo kupata mali ghafi hii ya korosho ili vile vikundi vyao vya kubangua korosho viweze kubangua kwa msimu mzima au kwa mwaka mzima?
NAIBU WAZIRI VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kutoka Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli usindikaji wa zao la korosho angalau sasa unaimarika kwa sababu sasa tumehamasisha uanzishaji na kufufua viwanda vingi vya kusindika korosho.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaweka utaratibu maalum baada ya kuona changamoto hiyo inayowapata wazalishaji au wabanguaji wa korosho wa viwanda vya ndani kutokana na ile changamoto ya kuweza kutokununua kwenye minada.

Mheshimiwa Spika, utaratibu uliopo ni kwamba wale wote wenye viwanda vya kuchakata au kubangua korosho ambao wanazalisha kwanza kabla ya kufungua msimu wa mnada huwa tunawapa kipaumbele wao kwanza, wanunue waweze kutosheleza mahitaji yao halafu zile korosho zinazobaki ndizo zitaingizwa kwenye mnada wa jumla. Lengo ni hilohilo kuwalinda, kulinda viwanda vyetu vya ndani ili viweze kupata raw material au malighafi ya kutosha kabla ya kuingia kwenye ile competition ya mnada mkubwa.

Mheshimiwa Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge wa Liwale kwamba hilo tutalichukulia kwa umakini sana kuhakikisha viwanda vyetu vya ndani vinapata malighafi za kutosha ili waweze kuzalisha kadri ya uweze ambao viwanda hivyo vimesimikwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, hii barabara siyo kwamba fedha Serikali hawana ya kujenga, ninachokiona hapa ni kwamba Serikali bado haijaamua kujenga hii barabara, kwa sababu zipo barabara zimefanyiwa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2018, mwaka 2017, mwaka 2016 zimeshajengwa na zingine zinajengwa. Lakini hii tangu mwaka 2014, ninaiomba Serikali iamue kwa maksudi kabisa kuikomboa Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Nachingwea ili iweze kufunguka nasi kiuchumi tuweze kuwa miongoni mwa watu waliopo duniani.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, moja ya vitu ambavyo vinaongoza katika kutengeneza hizi barabara kwa kweli ni uwezo wa Serikali kwa maana ya bajeti, lakini Ilani ya Chama cha Mapinduzi na ahadi za viongozi.

Mheshimiwa Spika, barabara ya Nachingwea - Liwale kwenye Ilani yetu ni kati ya barabara ambazo zipo kwenye usawa wa kilometa 7,500 ambazo zinatakiwa zikamilishwe usanifu wa kina kazi ambayo tayari imefanyika. Kwa hiyo ni hatua ya awali ambayo imefanyika na sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, usanifu tayari umekamilika kama ilivyoahidiwa kwenye bajeti mwezi Juni mwaka huu. Kwa hiyo, tayari Serikali imeshapiga hatua na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Liwale kwamba kwa kuwa tayari tumeshaanza kadri fedha zitakapopatikana naamini barabara hii itajengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali la nyongeza. Halmashauri ya Wilaya ya Liwale ina vijiji 76, vijiji 34 bado havijapatiwa umeme. Naona uzalishaji wa vijiji vifuatavyo mahitaji ya umeme ni makubwa sana; Kijiji cha Mlembwe, Lilombe, Kikulyungu, Mkutano, Mpigamiti, Ngorongopa, Ngongowele, Kimambi, Nahoro na Ndapata, vijiji hivi kwa sababu ya uzalishaji wake mahitaji ya umeme ni makubwa sana. Je, Serikali ni lini mtatupelekea umeme kwenye vijiji hivi ili kuwatia wananchi hamasa zaidi waweze kuzalisha zaidi mazao ya chakula na biashara?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza pia Mheshimiwa Kuchauka kwa sababu yeye ni mmojawapo wa Wabunge wanaofuatilia pia maendeleo ya majimbo yao katika maeneo mbalimbali katika likiwepo eneo la umeme. Kama nilivyosema hapo mwanzo ni kwamba vijiji vyote ambavyo havijapata umeme, kufikia Desemba, 2022 vitakuwa vimepatiwa umeme vikiwepo vijiji vyote alivyovitaja vya Jimbo la Liwale. Tunaomba aendelee kutusaidia na kusimamia utekelezaji ambao utafanyika katika maeneo yake.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni Wilaya ambayo iko mbali sana na makao makuu ya Mkoa ambako ni Lindi. Na pale Liwale hakuna kituo cha polisi kwa maana ya jengo hawana kabisaa, wanaishi kwenye nyumba ambayo ilipangwa na benki mpaka leo hii. Lakini, mwenyewe ni muhanga katika hili, mwaka huu mimi nimechomewa nyumba mbili na magari matatu wakati wa uchaguzi. Kimechangiwa sana na uhaba wa askari polisi na hatuna msaada wa karibu kutoka Liwale mpaka Nachingwea ni zaidi ya kilomita 120 mpaka Lindi zaidi ya kilomita 300. Sasa, je, Serikali ina mkakati gani kwanza, kutuongezea polisi Wilaya ya Liwale ikiwepo pamoja na majengo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza niko tayari kama ambavyo umenishauri kwenda kutembea Liwale, bahati mbaya kidogo sijafika Liwale. Lakini najitahidi katika kipindi hiki cha Bunge la Bajeti tunaweza tukatenga siku moja tukaenda Liwale kwenda kuangalia hiyo hali, halafu tutarudi tuje tuone sasa namna ya kufanya tathmini kuona namna ya kuweza kusaidia.

Mheshimiwa Spika, lakini, suala hili la uhaba wa askari mimi nadhani tuje pale pale, tuhakikishe kwamba tunaipitisha bajeti yetu, bajeti ambayo imezungumza suala zima la uajiri wa polisi, vijana hawa wa polisi, ili tuweze kuajiri. Tukikwamisha hii maana yake tutakuwa hatuna namna ya kufanya. Nakushukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina Kata 20 na vijiji 76, lakini bado upatikanaji wa maji ni wa shida sana hasa hasa kwenye vijiji vya Kihangara, Makata, Kikulyungu, Nahoro, Lilombe, Ngorongopa, Mkutano, Mtawatawa, Kimambi na Nanjegeja.

Mheshimiwa Waziri, ni lini vijiji hivi vinaweza kupatiwa maji safi na salama?
WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukimwona mtu mzima analia ujue kuna jambo. Mheshimiwa Mbunge wa Liwale amekuwa akilia sana juu ya suala zima la maji katika Jimbo lake. Sisi kama Wizara ya Maji tumewapatia fedha wakala wa Uchimbaji visima DDCA waende katika Jimbo lako la Liwale waende wakachimbe visima ili wananchi wako waweze kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu ya Serikali ambayo naweza kusema kwamba hayaridhishi. Kwanza ni-declare interest kwamba na mimi ni miongoni mwa waathirika, nimepoteza mali yenye thamani ya zaidi ya shilingi 301,516,000. Pia kuna nyumba zaidi ya sita zenye thamani ya shilingi 417,300,000; magari nane yenye thamani ya shilingi 299,700,000; pikipiki nane zenye thamani ya shilingi 22,100,000 na vifaa vya ndani vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 145,169,000. Jumla uharibifu huu umeigharimu halmashauri yetu zaidi ya shilingi milioni 886.

Mheshimiwa Naibu Spika, waathirika, kama nilivyosema, mimi mwenyewe ni mmoja wao, lakini yuko Musa Mkoyage, Hassan Liwango…

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kuchauka, hilo ni swali, uliza swali lako.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, sawa. Sasa swali langu; hivi ni kweli Serikali pamoja na uharibifu huu mkubwa haioni umuhimu wa wananchi hawa waathirika zaidi ya 15 angalau kuwashika mkono? Ni kweli nchi yetu inaongozwa kwa sheria pamoja na kanuni, lakini kuna mila na desturi ya kufikiria kwamba hawa watu wameathirika, hawana mahali pa kuishi, hawana namna nyingine yoyote ya kushiriki maendeleo ya nchi hii; kweli Serikali haioni umuhimu wa kuwashika mkono watu hawa? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. PASCHAL P. KATAMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, tukiri kwamba jambo lililofanyika siyo zuri na Serikali imelipokea kwa uchungu mkubwa. Kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema vizuri ni kwamba ni kweli nchi hii inaongozwa kwa mujibu wa sheria na sheria inayoongoza hapa ni Sheria ya Menejimenti ya Masuala ya Maafa ambayo ni ya mwaka 2015, yanapogeuka kuwa makosa ya jinai tayari inakuwa imeingia katika utaratibu mwingine. Ukisema ulipe fidia kwa watu ambao wamefanya uharibifu wa maji, kwa mfano, squandering of property, lakini pia kunakuwa na overt act kwa maana ya tendo ovu ambalo limekusudiwa, sasa tunaangalia ile mens rea na actus reus; kama tendo limefanyika ambalo kimsingi limevunja sheria maana yake hatua kali za kisheria lazima zichukuliwe kwa sababu ukilipa fidia kwa watu ambao wamefanya makosa maana yake tunachochea zaidi watu wengine kuleta madhara zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimpongeze sana Amiri Jeshi Mkuu na vyombo vyake vya ulinzi na usalama wakati wa uchaguzi au maafa lakini pia wakati wa sherehe zote za Kitaifa na nyakati zote kuna timu ambazo zimeandaliwa, kuanzia ngazi ya kata tunazo kamati ambazo zinahusika na kufanya upembuzi wa kujua kwamba hili ni janga na ni afa ambalo linahitaji kuweza kuingia katika perimeters za Sheria hii ya Menejimenti ya Masuala ya Maafa. Pia kwenye ngazi ya wilaya, tunao Wakuu wa Wilaya ambao wanaongoza Kamati za Ulinzi na Usalama, ambazo ndizo timu pia za maafa kwa ajili ya kufanya ile assessment.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwa suala hili lilivyojitokeza Liwale, moja kwa moja ni kosa la jinai. Kwa hiyo, hatua zitachukuliwa na kwa hatua ya sasa tayari evaluation imefanyika, nadhani tumeshauriana ameliona hilo, ni jinsi ambavyo tunataka sasa kuja kupata taarifa ya mwisho ya jinsi gani ambavyo madhara yalifanyika, watuhumiwa waliokamatwa na hatua kuchukuliwa zaidi ili kuweza kupeleka kesi zenye ushahidi mahakamani ili waweze kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunaendelea kusisitiza wananchi wote kufuata sheria, taratibu na kanuni katika maeneo yao. Niseme tu hili, imekuwa ikijitokeza mara nyingi kwenye uchaguzi, watu wanaposhindwa hawakubali kwamba wameshindwa matokeo yake anataka kufanya justification ya kutaka kuonesha kwamba yeye alikuwa na nguvu kwa hiyo wanatengeneza matukio ya kihalifu. Kumekuwa na timu ambazo wanaleta vijana kwa ajili ya kufanya uhalifu huo. Serikali iko imara, vyombo vya ulinzi na usalama viko imara, navipongeza kwa hatua ambazo wamekwishaanza kuzichukua na ambazo tunaendelea nazo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitumie fursa hii pia kupongeza Jeshi letu la Polisi katika kipindi cha uchaguzi limefanya kazi nzuri. Nipongeze Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, hata kwenye maafa haya lilihusika. Nipongeze pia vijana wa Scout lakini pia vijana wetu wa Red Cross ambao wamekuwa wakifanya kazi nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Hali ya madhara yanayotokana na wanyamapori yamekuwa ni makubwa sana. Leo hii kwenye Vijiji vya Ngumbu, Kibutuka, Kiangala na Ngatapa, wananchi wameshahama wamerudi majumbani kwao kutoka mashambani, baada ya tembo kumaliza mazao yote. Sasa naomba Serikali ituambie, je, ina mkakati gani wa kuhakikisha usumbufu huu wa wanyamapori unapungua hasa kwenye hivi vijiji vichache nilivyovitaja? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nianze kwa kuwapa pole wananchi wa Liwale, lakini pia niendelee kutoa pole kwa wananchi wengine wote wanaozunguka maeneo ya hifadhi, zikiwemo Hifadhi ambazo nimezitembelea jana za Mwanga na Same.

Mheshimiwa Spika, changamoto hii inasababishwa na wananchi kusogelea maeneo ya hifadhi, hasa maeneo yenye ushoroba, njia za wanyama pori hususani tembo, wanatembea kwa speed ndefu na wanatembea katika maeneo marefu na shoroba hizi zimezibwa na wananchi ambao wanafanya shughuli za kilimo lakini wengine wamejenga kwenye maeneo ambayo ni mapito ya wanyama.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaweka mkakati wa kufanya mafunzo kwa wananchi ya namna ya kudhibiti hawa tembo, lakini pia tunagawa vifaa, lakini pamoja na hilo tumeimarisha dolia za askari, kuhakikisha kwamba hawa wanyama wanapoingia kwenye maeneo ya wananchi basi askari wa doria wanakuwepo kwenye maeneo husika.

Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mbunge kwamba suala hili Serikali inalitambua na tunaendelea kufanya kazi na hatulali mchana na usiku tunahakikisha wananchi waishi kwa amani. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa na mimi nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyojibu kwenye jibu la msingi kwamba barabara hii inaharibika sana kutokana na malori hasa ya Dangote na malori ya gypsum. Lakini usafirishaji kama anavyosema ni kweli Bandari ya Mtwara imeboreshwa kwa kiwango kikubwa, lakini gharama ya usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye Bandari ya Mtwara na Bandari ya Dar es Salaam ni sawa sawa na ndiyo maana wafanyabiasha wana option kusafirisha mzigo kwa barabara kuja kusafirisha kwa Bandari ya Mtwara na ndiyo maana hata mafuta watu wa mafuta wameambiwa wachukulie Mtwara, lakini bado malori ya mafuta yanatoka Tunduru, yanatoka Liwale, yanatoka Nachingwea yana option kuja Dar es Salaam badala ya kuchukulia Mtwara.

Kwa hiyo, mimi naiomba Serikali sasa Serikali wataangalia namna yaku-adjust hizi bei ili iwe kivutio kwa Bandari ya Mtwara? (Makofi)
NAIBU WAZIRI UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Kwanza majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri mwenzangu ni sahihi lakini niongezee tu kusema kwamba tumeshafanya mazungumzo ni kweli barabara imeharibika kwa sababu ya mzigo mzito wa Dangote lakini pia na tungependa pia hata korosho zisafirishwe kupitia Bandari ya Mtwara. Tumefanya ziara pale, tulikuwa na changamoto ya gharama ambayo Dangote alilalamika tumefanya negotiation tumekubaliana kupunguza gharama hizo.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili wenzetu wa korosho wanasema kwamba kulikuwa hamna makontena tumewapa nafasi katika Bandari ya Mtwara ili waweze kuhifadhi korosho zao na kwa sababu hiyo tunaamini kwamba hata mazungumzo yakikamilika mzigo utapita sehemu kubwa pale. Tumeboresha Bandari ya Mtwara lakini pia na uwanja wa ndege unaboreshwa, kwa kweli barabara ile kwa namna ilivyo ikiendelea kutumika vile ilivyo watu wa Kusini wataendelea kupata gharama kubwa ya mizigo yao.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kuna shida kwamba hata uiharibifu wa barabara gharama yake ambayo inachangiwa
hatuwezi ku-replace kwa hiyo alternative njia nzuri ni kuhakikisha kwamba bandari ile inatumika vizuri na imeshaboreshwa tumetumia gharama kubwa zaidi, hayo mengine mazungumzo ya kiutawala itakamilika ili mizigo iweze kupita kwenye eneo hilo, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa na mimi nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kama alivyojibu kwenye jibu la msingi kwamba barabara hii inaharibika sana kutokana na malori hasa ya Dangote na malori ya gypsum. Lakini usafirishaji kama anavyosema ni kweli Bandari ya Mtwara imeboreshwa kwa kiwango kikubwa, lakini gharama ya usafirishaji wa mzigo kutoka kwenye Bandari ya Mtwara na Bandari ya Dar es Salaam ni sawa sawa na ndiyo maana wafanyabiasha wana option kusafirisha mzigo kwa barabara kuja kusafirisha kwa Bandari ya Mtwara na ndiyo maana hata mafuta watu wa mafuta wameambiwa wachukulie Mtwara, lakini bado malori ya mafuta yanatoka Tunduru, yanatoka Liwale, yanatoka Nachingwea yana option kuja Dar es Salaam badala ya kuchukulia Mtwara.

Kwa hiyo, mimi naiomba Serikali sasa Serikali wataangalia namna yaku-adjust hizi bei ili iwe kivutio kwa Bandari ya Mtwara? (Makofi)
NAIBU WAZIRI UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Kwanza majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri mwenzangu ni sahihi lakini niongezee tu kusema kwamba tumeshafanya mazungumzo ni kweli barabara imeharibika kwa sababu ya mzigo mzito wa Dangote lakini pia na tungependa pia hata korosho zisafirishwe kupitia Bandari ya Mtwara. Tumefanya ziara pale, tulikuwa na changamoto ya gharama ambayo Dangote alilalamika tumefanya negotiation tumekubaliana kupunguza gharama hizo.

Mheshimiwa Spika, lakini la pili wenzetu wa korosho wanasema kwamba kulikuwa hamna makontena tumewapa nafasi katika Bandari ya Mtwara ili waweze kuhifadhi korosho zao na kwa sababu hiyo tunaamini kwamba hata mazungumzo yakikamilika mzigo utapita sehemu kubwa pale. Tumeboresha Bandari ya Mtwara lakini pia na uwanja wa ndege unaboreshwa, kwa kweli barabara ile kwa namna ilivyo ikiendelea kutumika vile ilivyo watu wa Kusini wataendelea kupata gharama kubwa ya mizigo yao.

Mheshimiwa Spika, lakini pia kuna shida kwamba hata uiharibifu wa barabara gharama yake ambayo inachangiwa hatuwezi ku-replace kwa hiyo alternative njia nzuri ni kuhakikisha kwamba bandari ile inatumika vizuri na imeshaboreshwa tumetumia gharama kubwa zaidi, hayo mengine mazungumzo ya kiutawala itakamilika ili mizigo iweze kupita kwenye eneo hilo, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Liwale inazungukwa na Pori la Selous, lakini sasahivi mkakati wa Serikali ni kuimarisha utalii wa picha badala ya utalii wa uwindaji na sisi kwenye Kanda ya Kusini kuanzia ukanda wa Kilwa mpaka Tunduru hakuna lango la utalii wa picha.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kutuwekea sisi lango la utalii wa picha na sisi tuweze kunufaika na uwepo wa Selous?

SPIKA: Mheshimiwa kule Liwale unadhani lango lingeweza kukaa wapi kwa mfano?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, palepale Liwale Mjini ndio panafaa kwa sababu, Kambi ya Selou iko palepale Liwale.
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Kuchauka kwa maswali yake mazuri, lakini pia kwa kutambua wananchi wanaoishi Liwale. nimuahidi tu kwamba, mageti yanayohusiana na hii hifadhi yatafunguliwa kwa mwaka wa fedha 2021/2022 na mageti mengine yote.

Mheshimiwa Spika, hili naliongea kwa kujiamini kwa sababu, wiki iliyopita tu nilikuwa katika Mkoa wa Kilimanjaro, Same pamoja na Mwanga, pia kuna maombi hayo ya kufungua mageti mbalimbali kwenye Hifadhi ya Mkomazi. Kwa hiyo, niwaombe Waheshimiwa Wabunge kwenye maeneo yale ambayo yanahitaji kufunguliwa mageti ya ziada, ili kurahisisha watalii mbalimbali waweze kuingia na kurahisisha namna ya kuingia kwenye hifadhi, tutayafungua na bajeti hii itakayoanza keshokutwa imezingatia kufunguliwa kwa mageti hayo. Naomba kuwasilisha.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tofauti kubwa kati ya miradi ya upembuzi yakinifu wa barabara zetu ukilinganisha na ujenzi, kwa sababu zipo barabara ambazo zimefanyiwa upembuzi yakinifu tangu mwaka 2012 na bado hazijajengwa.

Je, Serikali haioni kwamba ipunguze miradi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ili barabara ambazo zimeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwanza zijengwe, kwa sababu haiwezekani mwaka 2012 ifanyiwe upembuzi halafu uje kuijenga 2025 useme kwamba utaijengwa kwa data zile zile, ni lazima itabidi ujenge kwa data zingine.

Je, huoni kama Serikali inapoteza fedha nyingi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana nae kwamba tukifanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa muda inakuwa ni gharama kwa sababu itabidi tuje turudie, lakini azma ya Serikali wakati tunafanya upembuzi na usanifu wa kina inakuwa ni kuijenga barabara kwa kipindi hicho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunavyosema kinachosumbua wakati mwingine ni upatikanaji wa fedha kwa kipindi hicho lakini ni muhimu tukafanya usanifu ili mara tunapopata fedha basi barabara hizo ziendelee kujengwa. Kwa hiyo, tutaendelea kufanya usanifu na kutafuta fedha. Ahsante.
MHE: ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili na mimi nipate kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naishukuru Serikali kwa kutupatia fedha kwa ajili ya maji ya Mji wa Liwale. Hata hivyo mpaka leo DDCA wametutia changa la macho, ni mwezi wa sita huu hawajaja; na Mheshimiwa Waziri ameniambia kwamba kuna uwezekano tukachukua watu binafsi wakaanza kuchimba pale. Lakini nimewasiliana na Mhandisi anasema asilimia 30 ya fedha hizo tayari DDCA walishachukua na walishaingia mitini.

Je, ni lini DDCA watakuja kutuchimbia maji Wilaya ya Liwale?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Zuberi ni jana tu tumeongea na Mheshimiwa Waziri amekupa hayo maelekezo. Kwa hiyo nipende tu kuongezea pale alipoongea bosi wangu kama alivyokuhakikishia, pale DDCA wanapozidiwa kazi basi watu binafsi tutawapa vibali ili waweze kuja kuchimba hivi visima. Na visima hivi mwaka ujao wa fedha ninaamini vitachimbwa na mambo yatakaa vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na fedha iliyochukuliwa na DDCA fedha ikichukuliwa maana yake ni lazima kazi ije ifanyike. Kwa hiyo kwa ile asilimia ambayo wamechukua lazima watakuja kufanya hiyo kazi.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, na mimi kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Iko barabara ya kiuchumi barabara ya ukombozi kwa Wilaya ya Liwale, barabara ya Nangurukuru - Liwale. Barabara hii bajeti ya mwaka jana ilitengewa fedha kwa ajili ya kufanyiwa upembuzi yakini na usanifu wa kina, na mwaka huu pia imetengwa kwenye kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Wana Liwale wangetaka kusikia, ni lini barabara hii itakwisha kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, na hatimaye kujengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika bajeti tuliyopanga, tunauhakikia tutakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara yote, lakini pia katika maeneo yale kofofi, tumemuagazi Meneja wa TANROADS ayape kipaumbele ili kuhakikisha kwamba yanatengenezwa vizuri ili yasiathiri kupita kipindi kile cha masika, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu. Barabara ya Nangurukuru - Niwale ni mwaka wa tano inatengwa fedha kwa ajili upembuzi yakinifu na usanifu wa kina…

NAIBU SPIKA: Uliza swali. Taja barabara unayotaka ijibiwe.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, Nangurukuru - Liwale, fedha hazijawahi kuletwa tangu zinatengwa miaka yote mitano.

NAIBU SPIKA: Swali lako ni nini?

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa barabara ya Nangurukuru - Liwale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, swali la nyongeza la mheshiiwa Kuchauko ndiyo lilikuwa swali la msingi na Serikali imetenda shilingi milioni 548.603 na tumesema taratibu zote zimekamilika na muda wowote inatangazwa.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru Serikali kwa majibu mazuri, na nimpongeze Naibu Waziri kwamba naye ameshafika Liwale kwa hiyo ninachokizungumza anakifahamu. Lakini hii sehemu ya pili anayosema kwamba Madiwani na Wabunge wanahusika, kwamba wanapata hizi taarifa, mimi nimekaa Liwale miaka sita, sijawahi kupata hii taarifa zikiletwa kwenye Baraza letu la Madiwani. Kwa hiyo jambo hili labda leo aagize hili jambo lifanyike lakini hili jambo halifanyiki kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu ya pili, kwamba Kamati hii ya Uvunaji anayeingia mwanakijiji ni Mwenyekiti wa Kijiji peke yake, sasa wanaovuna hesabu zinakuja pale wanaambiwa cubic meters yule mwanakijiji cubic meters hajui, magogo mangapi yanaondoka hajui, matokeo yake kuna magogo yale makubwa ambayo yana mashimoshimo wanayaacha, kwa hiyo uharibifu ni mkubwa sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa naomba kufahamu, ni lini Serikali italeta fedha za upandaji miti kwenye vile vijiji ambavyo vina uvunaji huo ambao mimi nausema kwamba ni uvunaji wa holela?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge kwamba Kamati hii ni Kamati ambayo inaundwa katika level ya Wilaya, lakini washiriki wa Kamati hii ni pamoja na Wenyeviti wa Vijiji na Watendaji wa Vijiji, pia inajumuisha Meneja wa Misitu ambaye anatoka Makao Makuu TFS lakini yuko pale Wilayani, kuna Afisa Misitu ambaye anakuwa ni mjumbe, vilevile kuna Afisa Tawala wa Wilaya ni mjumbe pia kuna Afisa Ardhi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninaitamka hii Kamati ili afahamu Wajumbe wanaoingia mule ambao sasa ndiyo wanapeleka taarifa kwenye Baraza la Madiwani kama taarifa ya wale wote tu waliopitishwa kwenye orodha ya uvunaji wa mazao ya misitu na anayekuwa Mwenyekiti wa Kamati hii ni Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya na Katibu ni Meneja wa Misitu anayetoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa hii inapokuwa imekamilika inapelekwa kwenye Baraza la Madiwani. Baraza la Madiwani Wabunge ni Madiwani, wanashiriki pia Mwenyekiti wa Halmashauri ni Diwani na hawa Wenyeviti na Watendaji wa Vijiji wanapopeleka maombi yao kwenye hii Kamati ya Wilaya tayari wanaonekana ni wajumbe ambao watapeleka tena kwenye WDC kama taarifa. Kwa hiyo taarifa hizi kuanzia level ya kijiji kwenda WDC na mpaka kufika kwenye Halmashauri, Mbunge na Mwenyekiti anakuwa ameipata kupitia Mabaraza yanayofanyika.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi niwaombe tu, kwa kuwa huyu Mjumbe ambaye ni Afisa Ardhi wa Wilaya anaingia kwenye hii Kamati na kama hafanyi hivyo basi anafanya makosa ni kwamba hii taarifa baada ya kukamilika inatakiwa ikasomwe kwenye Baraza la Madiwani ili Waheshimiwa Wabunge wafahamu lakini pia na Mwenyekiti wa Halmashauri afahamu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivyo kwa sababu Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana ya Mwenyekiti wa Halmashauri ama Mbunge, wale ni wasimamizi, hawawezi kuingia kwenye mchakato kama ilivyo maelekezo na miongozo ya uvunaji wa misitu.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ameongelea kuhusu fedha, ni kweli kulikuwa kuna changamoto ya fedha, tukipeleka kwenye Halmashauri, halmahsauri zilikuwa hazifikishi kwenye maeneo husika ambayo kunatakiwa kuanzishwa vitalu na kupandwa hii miti ili kuziba yale maeneo ambayo yamekwisha vunwa. Kwa sasa tutapeleka hizo fedha lakini tutaleta mwongozo mahsusi wa kuhakikisha fedha hizi zinawafikia wale tu ambao wanahusika na fedha hizi na siyo Halmashauri kuelekeza kwenye matumizi mengine.Naomba kuwasilisha.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza. Wilaya ya Liwale ni miongoni mwa wilaya kongwe lakini haina Kituo cha Polisi mpaka leo sambamba na nyumba za watumishi. Nami kutoka kwenye Mfuko wa Jimbo kutokana na shida hiyo, nimetoa shilingi milioni 10 kusaidia ujenzi wa Kituo cha Polisi. Nini kauli ya Serikali kuwasaidia wananchi wale wapate Kituo cha Polisi? (Makofi)
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kutoa shilingi milioni 10 kwa kupitia kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kituo. Nimhakikishie kwamba Serikali tutaelekeza Jeshi la Polisi kupitia utaratibu wa Mfuko wa Tuzo na Tozo kama ambavyo nimejibu katika swali msingi la Mheshimiwa Daniel Sillo ili uangalie uwezekano wa kutumia fedha hizo kuunga mkono jitihada za Mheshimiwa Mbunge katika kuhakikisha kwamba ujenzi wa kituo hiki unaendelea. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza nitoe shukrani kwa majibu mazuri ya Serikali juu ya swali langu, lakini nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Spika, kwani upo udanganyifu uliofanywa katika Kijiji cha Kibutuka na aliyekuwa mfanyakazi wa Tigo, alienda pale akadanganya wanakijiji kwamba, anahitaji eneo la kujenga mnara, baadaye wanakijiji walimpa bure wakitumia mukhtasari ule yule sasa hivi anekuwa ndio mnufaika wa kodi ya mnara ule badala ya kuwa wanakijiji waliopo katika kijiji kile.

Je, Serikali ina mkakati gani au ina kauli gani juu ya utapeli wa huyu mtumishi wa tiGO ambaye yeye anajifanya kwamba, ndio mmiliki wa lile eneo wakati aliliomba apewe bure?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; pamoja na kwamba, Vijiji vya Ndapata, Ndunyungu, Makata, Mtawatawa, Kipelele, Makinda na Nambinda havina mawasiliano ya kutosha. Nini mkakati wa Serikali wa kutuwashia ile minara ambayo tayari imeshawashwa kwenye baadhi ya vijiji hapa nchini?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika kipengele cha kwanza. Ni kweli kabisa changamoto ya udanganyifu uliojitokeza tunaifahamu, lakini tayari suala hili lilikuwa limeshafika mahakamani na lilikuwa limeshatolewa maamuzi.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu pia migogoro ya ardhi inapotokea kwa Sheria Na.2 ya Mwaka 2002, tunafahamu kabisa kwamba, hili linahusisha Wizara ya Ardhi moja kwa moja, lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa changamoto hii ambayo imejitokeza tutashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Ardhi, ili tuweze kujua namna gani tutatatua changamoto hii ambayo imejitokeza katika eneo husika.

Mheshimiwa Spika, vilevile swali la pili ni kuhusu minara ambayo haijawashwa. Ni kweli kabisa katika maeneo ya Jimbo la Liwale, kwanza kabisa labda tuseme kwamba, Serikali imefanya uwekezaji mkubwa sana katika ujenzi wa minara ndani ya nchi yetu, likiwepo Jimbo la Liwale. Ni takribani bilioni 19.56 imewekezwa katika minara 161 ambapo tunatarajia katika kipindi cha miezi miwili mitatu minara hii ambayo tayari imeshasimama itahakikisha kwamba, itakuwa imeshawashwa.

Mheshimiwa Spika, Serikali pia imefanya uwekezaji mwingine wa minara 127 ambayo iko katika hatua za civil works. Katika kipindi cha miezi miwili mitatu, tunaamini kabisa kwamba, minara hii itakapokamilika, naamini maeneo mengi yatakuwa yamepata ufumbuzi wa changamoto hizi za mawasiliano, likiwepo Jimbo la Mheshimiwa Kuchauka ambalo ni Liwale. Nakushukuru sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina umri wa miaka 47 sasa, haijawahi kuwa na jengo la Kituo cha Polisi ukiacha lile jengo ambao wamepanga lililokuwa la benki. Nini, kauli ya Serikali kuipatia Wilaya ya Liwale jengo la Polisi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunafahamu Wilaya kongwe hizi zimekuwa na vituo lakini chakavu sana. Sasa kwa bahati mbaya Liwale hawajawahi kuna nacho. Namwahidi kwamba katika bajeti ijayo tutaweka kipaumbele ili Wilaya yake ianze mchakato wa kujenga kituo chake cha Polisi kama zilivyo Wilaya nyingine za Tanzania Bara. Nashukuru. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kwa kweli vijiji hivi kama majibu ya msingi yanavyosema; ni kweli upimaji huu ulifanywa lakini walio wengi wanaolalamika ni kwamba upimaji haukuwa shirikishi. Kwa mfano, kuna mgogoro wa Mkutano na Kikunyungu, Kipelele, Nangumbu au Ngongowele na Ngunja. Wanachozungumza pale ni kwamba yale mawe wakati wanabeba kuna mahali walichoka wakayatunza mahali. Matokeo yake hawakurudi pale, kwa hiyo, yule aliyekuja kuchukua a-coordinate majira ya nukta akachukulia pale. Kwa hiyo, hicho ndiyo chanzo cha migogo mingi kwenye hivi vijiji ambavyo nimevitaja.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile kuna mgogoro kati ya Wilaya ya Kilwa na Wilaya ya Liwale kwenye Vijiji vya Nanjilinji na Milui. Mgogoro wake scenario yake inafanana na hiyo hiyo, kwamba wakati wanapima wakazi wa wilaya hizi mbili zote hawakushirikishwa. Sasa Je, Mheshimiwa Waziri yupo tayari kufuatana nami baada ya Bunge hili twende Liwale akatatue migogoro hii?
NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, juu ya changamoto iliyotokea ni kweli yako baadhi ya maeneo ambayo yana changamoto hizo. Nimwahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge tutapanga ziara twende tukakutane na wananchi wake ili kumaliza kero katika maeneo yake. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara inayotoka Mangaka Wilaya ya Nanyumbu - Nachingwea Tarafa ya Kilinalondo - Liwale katika Kata ya Ilombe, tumeshaiombea iingie TANROADS, lakini mpaka leo tunapigwa danadana.

Je, ni lini barabara hii itaweza kupandishwa hadhi kuwa barabara ya TANROADS kwa sababu barabara hiyo imepita katika wilaya tatu?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ameshasema Mheshimiwa Mbunge walishaomba na mchakato upo katika ngazi husika na wenye jukumu la kufanya hivi ni watu wa TANROADS, naamini sisi Serikali ni moja tutalifuatilia ili kuharakisha huo mchakato uweze kukamilika. Ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Liwale ilikuwa na gari moja tu ambalo kwenye Uchaguzi uliopita gari lile lilichomwa moto mpaka sasa hivi Wilaya nzima ile haina gari hata moja. Ni nini mpango wa Serikali kutupatia miongoni mwa hayo magari 78?
WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru kwa kuliweka vizuri.

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu sasa swali la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi kwamba magari haya yatakapokuja tutayapeleka katika maeneo ambayo yana mahitaji zaidi, kwa kweli maeneo ambayo yana mahitaji zaidi ni mengi kwa hiyo siyo rahisi kuweza kukamilisha kwa wakati mmoja kwa mwezi huu.

Kwa hiyo, niombe nikubaliane na Mheshimiwa Spika kwamba hoja za Waheshimiwa Wabunge tunajua ni za msingi, lakini magari yatakuja kwa awamu basi tutazingatia wapi kuna mahitaji zaidi.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu katika maswali yaliyopita ikiwemo na Mheshimiwa Mbunge Kuchauka kama itaangukia katika maeneo ambayo yana mahitaji zaidi na zaidi utapata mapema lakini nikuhakikishe kwamba tunafahamu na tunafanyia kazi. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale ilikuwa na mradi wa kimkakati wa stendi lakini fedha zililetwa zikarejeshwa baada kukwama kwenye manunuzi.

Je, fedha zile zitarejeshwa lini ili mradi ule uendelee?
NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla hatujabadilisha sheria na ninyi mnakumbuka mwaka jana, fedha zote ambazo zilikuwa zinavuka mwaka zilikuwa zinarejeshwa Hazina, maana yake mnatakiwa kuanza kuomba upya.

Kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba nimesikia maombi hapa ambayo ameyainisha na tutakwenda pale Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili kuona namna bora ya kusaidia kwa zile fedha ambazo awali zilikuwa zimeshapelekwa. Ahsante sana. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale haina Kituo cha Polisi na kwa kuliona tatizo hilo nimetoa fedha shilingi 10,000,000 kutoka kwenye Mfuko wa Jimbo kwa ajili ya kuanza ujenzi. Je, Serikali inatusaidiaje ili kuimarisha kituo cha Polisi cha Wilaya ya Liwale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Mbunge Kuchauka kwa kuchangia shilingi 10,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi Liwale, naomba nitoe ahadi kama nilivyosema katika swali lililopita kwamba maeneo yote ya Wilaya ambayo hayana Vituo vya Polisi ni mpango wa Serikali kuona kwamba Wilaya hizo zinapata Vituo vya Polisi, hivyo tutafanya tathmini kuona kiwango cha fedha kinachohitajika ili kushirikiana nae tuweze kukamilisha Kituo cha Polisi Liwale. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Liwale inazo barabara moja muhimu sana, barabara ya uchumi, barabara ya Mkombozi. Barabara hii nimeizungumza mara nyingi mno, barabara ya Nangurukuru Liwale. Wananchi wa Liwale wanataka kusikia barabara hii itajengwa lini kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara hii ilishakamilishwa kufanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina, Mheshimiwa Kuchauka atakubaliana nami kwamba Wizara ina mpango wa kuanza kuijenga barabara hii walau kwa awamu mwaka wa fedha unaokuja. Kwa hiyo, itategemea sana na upatikanaji wa fedha, lakini Serikali ina mpango kuianza kuijenga kwa kiwango cha lami.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza naishukuru Serikali kwa majibu mazuri yanayotia moyo. Hata hivyo majibu haya hajatoa takwimu; yaani hizi takwimu hazijaja na percent ili tuone ukubwa wa tatizo sisi kama wawakilishi wa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, mimi hapa nina takwimu ya chuo kimoja tu hiki cha MUHAS hapo Muhimbili. Mwaka 2022/2023 udahili, wanafunzi walioomba pale walikuwa 27,540; waliokidhi vigezo 19,287, lakini chuo kile kina uwezo wa kudahili wanafunzi 866 tu, ambayo ni 4% tu ya mahitaji: Je, hatuoni kwa trend hii kwamba tunakatisha tamaa vijana wetu kuendelea kusoma masomo ya Sayansi? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyowaelezakwenye majibu yangu ya msingi, tumeona ukubwa wa tatizo, ndiyo maana Serikali imeingia mkataba wa kuchukua mkopo huu. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari fedha hizi tumeshazipata na zinakwenda kutanua sasa wigo wa vijana wetu kuingia katika Masomo ya Sayansi. Amezungumzia suala la Muhimbili ambayo sana sana ni masomo ya tiba, lakini hapa tunazungumzia sayansi kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa takwimu zilizopo mwaka 2020 waliofanya mtihani wa kidato cha sita walikuwa ni 84,212; mwaka 2021 waliofanya mtihani wa form six walikuwa ni 88,273; na mwaka 2022 waliofanya mtihani wa form six walikuwa ni 94,456.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa takwimu hizi kama zaidi ya 40,000 wanakwenda kwenye masomo ya sayansi, yaani karibu asilimia 50 wanadahiliwa katika nyanja hiyo ya sayansi, bado tumesimama pazuri. Hata hivyo mradi huu unakwenda kutusogeza zaidi ya asilimia 70.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye Mji wa Liwale upo mradi wa kuupatia maji mji ule na tumechimba visima vitatu Kijiji cha Turuki, lakini mradi ule sasa umesimama kwa muda mrefu. Je, lini hatima ya mradi ule ili Mji wa Liwale upate maji safi na salama?
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tulifika Liwale, mwenyewe nilikwenda Liwale, lakini vile vile Mheshimiwa Waziri amekwenda Liwale na huu mradi uliosimama, naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge nitaufuatilia leo hii na baada ya Bunge hili naomba tuonane.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati tunatangaza Hifadhi ya Nyerere, National Park tayari kuna maeneo ya WMA, mfano kama Wma ya Magingo katika vijiji vya Mpigamiti, Barikiwa na Mlembwe tayari vimechukuliwa na TANAPA.

Je, ni lini Serikali itakuja kuhakiki hiyo mipaka ili yale maeneo yaliyokuwa yamehifadhiwa na vijiji yaendelee kuwa yanahifadhiwa na vijiji?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tu wananchi wa Liwale niwaahidi kwamba kwa kuwa taratibu za kuainisha mipaka ni kazi inayoshirikisha Wizara ya Ardhi pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii, tutaenda kuhakiki hiyo mipaka ili kuruhusu wananchi watambue maeneo yao na kisha yaendelee kuhifadhiwa vizuri.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kutokana na ripoti ya GST, Wilaya ya Liwale imeonekana kuwa na madini mengi sana ya dhahabu, kito na sapphire. Tayari wawekezaji wako kule na wachimbaji wadogo wameshaanza kazi, lakini Wilaya ya Liwale haina Ofisi ya Madini pale, matokeo yake wale wachimbaji wadogo na wawekezaji wengine wanakwenda Tunduru kuuzia madini. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka ofisi pale Liwale ili kuwarahisishia wachimbaji wadogo kupeleka madini yao Tunduru badala ya kuuzia Liwale?
NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sisi Wizara ya Madini tumeendelea kujenga masoko ya madini na kuanzisha vituo vya kuuza na kununua madini katika maeneo yote yenye madini nchini. Kwa hiyo nimhakikishie kwamba ni suala la muda tu katika mzunguko wetu kadiri mapato yanavyoruhusu, tutafika huko Liwale na tutajenga soko na tutahakikisha kwamba wachimbaji wake walioko huko wana masoko ya kuuzia madini yao kwa bei iliyo sahihi na bila kupunjwa na mtu yeyote.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru Serikali kwa kuonesha commitment ya kutaka kujenga stendi hii ya kisasa, lakini nimewasiliana na watu wa Halmashauri, wanasema kwamba kwa upande wa Halmashauri mchakato umeshakamilika kutoka kwenye ngazi ya Wilaya mpaka kwenye ngazi ya Mkoa. Sasa hivi Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kuwasiliana na watu wa TAMISEMI kwa kuona kwamba mradi huu umekwama kwenye ngazi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwa sababu kumebakizwa miezi miwili bajeti aliyoitaja hapo inakwenda kukamilika. Je, Mheshimiwa Waziri upo tayari kututengea tena fedha kwenye bajeti hii iwapo kama fedha zile za mwanzo zitakuwa bado hazijatumika? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kabla ya kujibu maswali hayo naomba nimpongeze sana Kaka yangu Kuchauka kwa kazi nzuri anayoifanya katika Jimbo la Liwale.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha na Mipango ipo tayari kuwasiliana na Wizara ya TAMISEMI nachukua nafasi hii nitoe maelekezo kwa wataalam wetu kufanya mawasiliano ya haraka sana kuona hadhi ya project hii imefikia wapi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, suala la pili kwa kuwa Serikali ina nia njema ya kujenga stendi ya kisasa, basi kama haikukamilika mwaka wa 2021/2022 basi bajeti inayokuja tutatenga tena fedha hiyo ili kusudi tuone mradi huo umekamilika. Ahsante. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Lakini kutokana na umuhimu wa shule hii, kama ilivyoelezwa hapa; kwamba ni ya muda mrefu sana; na naona hapa majibu yote yaliyotoka ni ya jumla jumla.

Mheshimiwa Spika, nachotaka kuomba ni commitment ya Serikali; je, Shule hii ya Kingurungundwa ni lini italetewa fedha kufanyiwa ukarabati? Kwa sababu hali ya shule hii ni mbaya zaidi kuliko hizo shule nyingine ambazo umezijumuisha kwenye majibu yao. Naomba kupata commitment ya Serikali, hii Shule ya Kingurungundwa ni lini italetewa fedha ili ifanyiwe ukarabati mkubwa?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI
ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo tulijibu katika jibu la msingi, kwamba, mpango wetu wa sasa ni kuzifanyia tathmini shule zote ikiwemo shule ya Kingurungundwa. Tukishamaliza mchakato; maana yake ni kuanzia mwaka huu wa fedha mpaka mwaka 2025/2026. Kwa hiyo, nimhakikishie tu kwamba tutafanya mapema iwezekanavyo ili kuhakikisha shule hiyo inafanyiwa ukarabati, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika Mji wetu wa Dar es Salaam kumejengwa barabara ya njia nane, lakini madereva wengi hawajui matumizi ya barabara ile.

Je, ni lini Serikali itaendesha mafunzo ya kutumia ile barabara kwa sababu unakuta guta limekaa kwenye highway badala ya kukaa kwenye barabara ya upande wa kushoto. Je, Serikali ni lini itatoa mafunzo rasmi?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama Wabunge wanafuatilia na wananchi kwa ujumla kazi inayofanywa na chombo chetu cha usalama barabarani (traffic police) wanatoa elimu kupitia vyombo vya habari kuhusu usafiri kwenye kipindi cha UBA, usafiri na uraia Tanzania. Pale hutoa mafunzo mbalimbali juu ya namna barabara zile zinavyotakiwa kutumika. Kwa gari yoyote inayokwenda mwendo mdogo au inaelekea kusimama inatakiwa itembee kushoto zaidi na gari ambayo inakwenda haisimami kwenye vituo vya karibu inatakiwa ipite kule kule ambako wanaita highway. Kwa hiyo elimu hii itaendelea kutolewa ili kuwe na matumizi sahihi ya barabara hizi, nashukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza napenda kutoa shukrani za dhati kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia matumaini, lakini hata hivyo namshukuru sana Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanznaia, Mama yetu Mama Samia Suluhu Hassan, tumepata fedha zile za UVIKO, tumejenga chujio na sasa hivi tunapata maji safi ka Mji wetu wa Liwale. Nina swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, vipo Vijiji vya Ngongowele, Makata, Mtatawa, Kihangala, Kipelele, Nguta, Mpengele, Ndapaka, Mlembwe na Nangano. Vijiji hivi bado havijapata maji safi na salama. Naomba kupata comfort kutoka Serikalini, ni lini wananchi wa vijiji hivi wataweza kufikiwa na mradi wa maji ili kutimiza ile azma ya kumtua Mama ndoo kichwani iweze kukamilika? Ahsante sana. (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Kuchauka Zuberi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, napenda kupokea shukrani zake na vile vile tumuombee Mheshimiwa Rais, kwa ababu adhma ya kumtua Mama ndoo kichwani hakika inatekelezwa maeneo yote.
Mheshimiwa Spika, vijiji alivyovitaja Mheshimiwa Mbunge tayari RUWASA Mkoa inafanyiakazi na mwaka ujao wa fedha tutavifikia kwa kila kijiji, kila tunapopata fedha kuhakikisha maeneo yote ya Liwale yanakwenda kupata maji safi na salama.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale iliahidiwa kujengewa Chuo cha VETA kwenye bajeti hii inayotekelezwa sasa. Mpaka leo hii imebakia miezi miwili bajeti inakwenda kwisha: Je, lini tutapewa fedha hizi tuweze kujenga chuo hicho?
NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari tumeshapeleka fedha za awali kwa ajili ya mobilization na zile kazi za mwanzo; na kazi nyingine za Geotechnical Survey, Topographical pamoja na ESIA (Environmental and Social Impact Assessment) tayari zimeshafanyika. Kwa hiyo, hivi sasa tunachokamilisha ni kupata matokeo ya tafiti hizi tulizokwenda kufanya. Baada ya matokeo hayo, tayari tutapeleka fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wa maeneo yote yale 63 tuliyoyataja.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, viko Vijiji vya Mtawatawa, Ndapata, Ndunyungu na Ndinda, ambavyo havina mawasiliano kabisa. Ni lini Serikali itaona umuhimu wa kupeleka mawasiliano kwenye vijiji hivyo?
NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wataalam wetu wameshafika katika maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja, na tayari katika orodha ya vijiji 2,116 tukitoka hapa Mheshimiwa Kuchauka tuonane ili niweze kukuonesha maeneo ambayo tayari umeyataja, yamo tayari kwenye utaratibu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Sera ya Taifa letu ni kuunganisha barabara za mikoa kwa lami, lakini sisi Mkoa wa Lindi haujaunganishwa na Mkoa wa Morogoro kwa barabara hata ya vumbi.

Je, Serikali inasema nini juu ya kuunganisha sisi Mkoa wa Morogoro na Lindi kwa barabara angalau ya changarawe pale Liwale na Mahenge?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge Kuchauka, kwamba mwaka huu wa bajeti tumependekeza kwanza tufanye upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kati ya Liwale, Ilonga hadi Mahenge ili hii barabara tuweze kuifungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara inapita kwenye Mbuga ya Selous, na limekuwa ni ombi kubwa sana la wanalindi akiwepo Mheshimiwa Kuchauka sasa tumeiweka kwenye mpango wa kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina. Kwa hiyo kama bajeti yetu itapita tuna uhakika hiyo kazi itakuwa imeanza kuunganisha Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Morogoro, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale pamoja na kwamba ni ya mwaka 1975 haijawahi kuwa na jengo la Kituo cha Polisi, lakini Serikali walituahidi kutujengea Vituo vya Polisi katika Kata za Kimambi, Lilombe na Kibutuka. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hii?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa
Spika, tumewahi kueleza hapa na naomba nirudie kwamba katika wilaya zetu hasa kwenye kata, mpango wa Serikali ni ku- support pale ambapo juhudi zimeoneshwa na wananchi na halmashauri zao za ujenzi wa vituo hivyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge akitusaidia kupitia Mfuko wa Jimbo, akaanzisha ujenzi, kwa vyovyote vile IGP kupitia fungu lake atatoa fedha za kusaidia kukamilisha vituo vyake. Kwa hiyo, nimtie moyo, hizi kata tatu ambazo zina changamoto za uhalifu, tuanze kwenye ngazi ya halmashauri na Mfuko wa Jimbo ili ngazi ya wizara kupitia Jeshi la Polisi liweze kusaidia kukamilisha, nashukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Gereza la Liwale pamoja na kwamba lina uzio wa miti, Mkuu wa Gereza amejenga nyumba tano za two in One na bado nyumba zile zimeishia kwenye linta. Je, Serikali haioni umuhimu wa kumwongezea fedha Askari yule ili wamalizie nyumba zile za maaskari?
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge, kwa wale wanaofanya juhudi kama Mkuu wa Gereza wa Liwale pamoja na juhudi za Mbunge ambaye anatoa fedha kwenye fungu lake kwa ajili ya kuliwezesha gereza hili, tutaendelea kuwa-support kwa kuwapa bajeti ili miradi kama hiyo iweze kukamilishwa ndani ya muda mfupi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Liwale kwenye bajeti ya 2018-2020 tulitengewa fedha kwa ajili ya kujenga stendi ya kisasa kama mradi wa kimkakati, lakini fedha zile zilirudishwa kutokana na sababu zisizojulikana. Je, ni lini Serikali itatuletea fedha hizo tena ili mradi ule wa kimkakati uweze kukamilika kwa wakati?
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Mohamedi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nafikiri Bunge lako lilipitisha hapa sheria ya kuhakikisha kwamba fedha zote ambazo zimeelekezwa katika miradi na kuvuka mwaka wa fedha ziendelee kubaki ili zitekeleze miradi ambayo imekusudiwa. Na jambo hili alilozungumza Mheshimiwa Mbunge maana yake sasa Ofisi ya Rais, TAMISEMI italifanyia kazi kulipitia ili ione namna bora ya kuhakikisha fedha zile zinarudi na kufanya kazi ambayo imekusudiwa, ahsante sana.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaja na swali la nyongeza kwanza nisikitike kwa majibu ambayo hayajaridhisha. Hayajaniridhisha mimi wala wananchi wa Liwale. Nina sababu zifuatazo; kwanza Wizara haikuzingatia umbali uliopo kutoka Liwale kwenda Nachingwea lakini vile vile haikuzingatia miundombinu ya usafiri uliopo kutoka Liwale kwenda maeneo iliyotajwa. Hata Mkoa wenyewe wa Lindi ukiuangalia ukubwa wake Wilaya ya Liwale ndiyo yenye eneo kubwa Mkoa wa Lindi. Takriban theluthi moja ya Mkoa wa Lindi iko Liwale. Sasa kuniambia kwamba Wilaya ya Liwale ina shughuli pungufu ya uchimbaji wa madini napata shida kukubaliana na jambo hilo. Hii ni kwa sababu kuna eneo kubwa sana ambalo linazungumzwa Wilayani Nachingwea, eneo la Kitowelo. Eneo hili la Kitowelo liko mpakani na Liwale...

MWENYEKITI: Mheshimiwa uliza swali la nyongeza.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Swali langu: -

(a) Je, Wizara hii ya Madini haiko katika mfumo ule wa kusogeza huduma kwa wananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana kama ingekuwa kwenye hiyo mpango wa kusogeza huduma kwa wananchi kwa karibu basi na sisi tungepatiwa Ofisi. Ile taasisi ya GST ilikuja Liwale ikakaa mwezi mzima ikakaa pale Liwale waliweka kambi Mpigamiti pale, mwezi mzima. Wamefanya utafiti wa madini lakini mpaka leo hatujapata sisi kama Wilaya, kupata hata kile kitabu cha matokeo yale ya uchimbaji wa madini. Matokeo yake sasa watu kutoka Kanda ya Ziwa ndio wanachukua vitalu kule kwa wingi sana kwa sababu matokeo yote yako hapa GST Makao Makuu.

(b) Je, Wizara ya madini iko tayari sisi kama Halmashauri kutupatia vile vitabu vya matokeo ya utafiti ule?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI K.n.y. WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la kwanza, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni Serikali ya wananchi, na nia yake kubwa ni kupeleka huduma kwa wananchi. Kama tulivyosema kwenye jibu la msingi, ni kwamba, ofisi zitafunguliwa kulingana na Wingi na uhitaji wa ofisi hizo kwenye maeneo hayo. Lakini pia nimemalizia kwa kusema Wizara itaendelea kuboresha huduma kwa wadau wake kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimuhalkikishie Mheshimiwa Kuchauka, mpaka sasa Tanzania ina masoko 42 ya kununua na kuuza madini, ina vituo 93. Kadri maeneo yanavyozidi kuongezeka na uhitaji unavyotokea huduma hii inazidi kusogezwa kwa wananchi. Hata katika Jimbo la Liwale watakwenda kutizama na kuona wingi na upana wa mahitaji ya ofisi hizi, na zitapelekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili; nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge; wananchi wa Liwale niliwashauri kutembelea ofisi za madini watapata hizo taarifa za madini yaliyopo kama ambavyo anasema, kwamba waliotoka sehemu za mbali wamepata taarifa hizo. Lakini pia ofisi itahakikisha inatoa taarifa hizo kwa sababu si za siri, kwa wananchi, ili waweze kuzi-access na kuweza kuingia kwenye maeneo hayo kuweza kuchimba madini ili kunufaika nayo. Sisi sote tunaohitaji kunufaika nayo.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ina WMA ya Magingo, lakini uanzishwaji wa TANAPA, ile Hifadhi ya Mwalimu Nyerere imeingia kwenye maeneo ya WMA ya Magingo katika Kitalu cha Nachengo, Kijiji cha Mpigamiti na Ndapata na Kimambi: Je, Serikali inachukua hatua gani kwenda kutatua migogoro hii iliyoletwa na uanzishwaji wa Hifadhi ya Mwalimu Nyerere?
NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaenda kuufafanua huo mpaka na kutafsiri mpaka ili WMA ziweze kufanya kazi zake na Hifadhi ya TANAPA iendelee na shughuli zake.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kituo cha Afya cha Ngongowele kilipata fedha za Matokeo Makubwa Sasa, tulipata shilingi milioni 250, mradi ambao umeshaisha; je, Serikali haioni imefika wakati kutupatia shilingi milioni 250 nyingine kumalizia kituo kile?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu kituo hiki cha afya cha Ngongowele kule katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale, Serikali itatenga fedha ya kumalizia kadiri ya upatikanaji wa fedha hizi na bajeti itakavyoruhusu.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na wimbi kubwa la kuhama watumishi kwenye Idara ya Afya kwenye Halmashauri hasa zile za pembezoni. Mfano Liwale tulipata watumishi 80 lakini watumishi wale leo ukienda kuwahesabu hata 15 hawafiki, wanahama 36 wanahamia wawili; je, Serikali ina mpango gani kudhibiti huo uhamaji wa watumishi holela?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, suala ambalo ananiuliza Mheshimiwa Kuchauka Serikali imelitambua na tayari tunaweka mikakati hasa kwenye ajira hizi ambazo wanaingia kazini muda siyo mrefu, kuona tutaweka mikakati ambayo itadhibiti hili la watu kuhama. Lakini pia nichukue nafasi hii kuwaeleza Wakurugenzi wa Halmashauri ambao ndio waajiri katika maeneo haya wahakikishe hawapitishi barua za watumishi ambao hawajathibitishwa kazini. Mtumishi anatakiwa walau akae miaka mitatu katika kituo chake kipya cha ajira, kwa hiyo, wafuate taratibu hizi, wasipitishe barua hizi ili watumishi hawa maana yake wameajiriwa kwenda kujaza upungufu ule ambao upo katika maeneo hayo. Sasa wanapopitisha barua hizi ili hawa wahame tayari wanazidisha upungufu katika maeneo haya.

Kwa hiyo, niliona nichukue muda kulizungumzia hili hapa ndani ili Wakurugenzi wetu wa Halmashauri ambao ni waajiri waweze kuelewa kufuata taratibu hizi za kiutumishi.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Liwale ndiyo wilaya pekee yenye kilometa chache sana za barabara za changarawe na tuna chini ya kilometa nne tu za lami. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuiongezea wilaya hii fedha za TARURA ili kuongeza ufanisi wa ujenzi wa barabara hizo? (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli Jimbo la Liwale lina changamoto kubwa ya barabara. Katika bajeti zetu za miaka mitatu mfululizo, Mheshimiwa Kuchauka ni shahidi kwamba bajeti imeendelea kuongezeka, lakini najua bado haitoshelezi kutokana na ukubwa na changamoto kubwa ya barabara.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kuboresha suala la kuhakikisha kwamba barabara hizo zinatengewa fedha zaidi ili ziweze kupitika vizuri zaidi, ahsante. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; Mji wa Nachingwea ni mji unaokua haraka sana. Upo Mradi wa Maji pale Nachingwea ambao tayari sasa hivi imeonekana mradi ule hautoshelezi. Je, Serikali iko tayari kutupatia fedha Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea ili kupanua Mradi ule wa Maji wa Mji wa Nachingwea?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kama ilivyo kwa Mji wa Nachingwea unakua haraka, Mji wa Liwale nao una mradi sasa una miaka zaidi ya miwili kwa ajili ya maji katika Mji wa Liwale. Je, Serikali ipo tayari kutupatia fedha ili tuondokane na adha ya maji pale Mjini Liwale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Amandus, kwa niaba yake yameulizwa na Mheshimiwa Kuchauka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu pesa Nachingwea kwa ajili ya kupanua mradi; nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, hili tunalifanyia kazi. Tayari lipo kwenye mipango kuhakikisha katika Mji wa Nachingwea wanapata huduma ya majisafi na salama na ya kutosheleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, pesa Liwale, nimelipokea, tutalifanyia kazi. Pia naomba kumpa taarifa, wale wawekezaji wetu walishafika Liwale, naamini atakuwa amewaona, watakwenda kufanya usambazaji wa visima vilivyochimbwa. Yote hii ni kuona kwamba jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kumtua mama ndoo kichwani Liwale nazo zinaweza kukamilika.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninashukuru kwa majibu mazuri yanayotia tumaini kutoka Serikalini. Vilevile ninashukuru kwenye ile barabara yangu ya Nachingwea – Liwale, tarehe 12 yule mkandarasi anaenda kukagua. Nashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya hivyo, nina maswali mawili; barabara hii niliyoitaja inayounganisha Morogoro, tayari TANAPA wameshaanza kuichonga. Sasa tunachotaka kujua; je, sisi tunaweza kuanza kupita hata kabla ya huo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina uliotajwa?

Swali la pili, tayari kwenye bajeti iliyopita tunayo barabara yetu ya Nangurukuru – Liwale kilometa 230. Tulishapewa kilometa 72 wananchi wa Liwale wanataka kujua ujenzi unaanza lini? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara hii ya Liwale kwenda Mahenge ambayo inapita katikati ya Hifadhi ya Mwalimu Nyerere, tumetenga fedha kama nilivyosema. Kwa maana ya kutumika kwa sasa waliofanya hiyo barabara ni wenzetu wa Maliasili na Utalii kwa shughuli zao, lakini sisi kama Wizara tunapokwenda kuifanyia upembuzi yakinifu ni kwa maana ya wananchi waweze kutumia.

Mheshimiwa Spika, tuna hakika kama tutakavyokuwa tumefanya usanifu, wenzetu wa maliasili watashauri ijengwe vipi ili iweze kutumika kama barabara ya kiulinzi, pia, iweze kuwahudumia wananchi wote wa Tanzania bila kujali ni wa hifadhi ama siyo hifadhi, ndiyo maana Serikali imetoa fedha ili kurahisisha mawasiliano kati ya wananchi wa Liwale na Mahenge. Kwa hiyo, itaanza kutumika na wananchi kama itakuwa imekidhi hivyo vigezo.

Mheshimiwa Spika, suala la pili; ni kwamba, Barabara ya Nangurukuru – Liwale tumetenga tuanze ujenzi mwaka huu kilometa 72 kuanzia Liwale kwenda Nangurukuru. Ninataka nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tayari taratibu za manunuzi za awali zimeanza ili barabara hii ianze kujengwa. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ninaishukuru Serikali kwa majibu mazuri yenye kutia matumaini, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Serikali imekiri kwamba upatikanaji wa pembejeo ndiyo shida mojawapo inayofanya zao hili lisilete tija iliyokusudiwa. Je, Serikali haioni pamoja na kwamba mwakani itatusambazia hizo mbegu bure, je na pembejeo zingine kama mbolea tutazipata?

Swali la pili, kwa kuwa tunayo Bodi ya Pareto, je, Serikali haioni umuhimu wa kuiwezesha hiyo Bodi ya Pareto kwa kuwaongeza bajeti na kuwaongezea watumishi?
NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema pamoja na usambazaji wa miche bora ambayo itasaidia katika kuongeza tija pia wakulima wa pareto wanaingia katika mpango wa mbolea ya ruzuku. Kwa hiyo ni wanufaikaji na watanufaika pia kupitia mbolea hii.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili kuhusu bajeti kwenye Bodi ya Pareto tunaendelea kulifanyia kazi suala hili, tumeendelea kuijengea Bodi uwezo tofauti na miaka miwili iliyopita, lengo letu ni kulikuza zao la pareto ambalo limekuwa na manufaa makubwa. Kwa hiyo, Bodi tutawajengea uwezo kuhakikisha kwamba bajeti yao inaongezeka pia. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Liwale unaoundwa na Kata tatu, Kata ya Likongole, Liwale Mjini na Nangando vipo vijiji zaidi ya kumi lakini vijiji vile vimegawanya, kuna vijiji vinalipa shilingi 27000 na kuna vinavyotakiwa kulipa shilingi 350,000. Je, Serikali haioni kwamba kwa sababu vyote hivi ni vijiji viingizwe kwenye kulipa shilingi 27000 ili kuweka usawa?
NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nifafanue kidogo jibu ni lilelile lakini niliongezee nyama kidogo.

Mheshimiwa wenyekiti, Wizara ya Nishati kupitia TANESCO tulibaini maeneo ya Vijiji na Miji kutoka kwenye taarifa za wenzetu wa TAMISEMI ndiyo waliotupatia taarifa za hapa ni mjini na hapa ni kijijini. Baada ya ku– implement hicho tulichokipata ndiyo yakatokea maoni mbalimbali kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge na wananchi. Tukaona ni vema tuende site wenyewe ili tukabaini, pamoja na kwamba enzetu wa TAMISEMI wamesema hapa ni mjini lakini maisha ya pale yanaonesha kuwa ni kijijini na hilo ndilo zoezi tunalolifanya na tukilikamilisha tutashirikiana na wenzetu wa TAMISEMI ili kuweka usawa kama ulivyoshauri Mheshimiwa Kuchauka ili wananchi waweze kulipa ile gharama ambayo wanaweza kuilipa kutokana na mapenzi na utashi mwema wa Serikali kuhakikisha kwamba inawahudumia wananchi wake salama.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa mara ya kwanza swali langu hili limepata majibu mazuri ya Serikali, imenitia tumaini, lakini bado ina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa sababu ya kituo hiki kuitwa kituo cha karibu cha usaidizi Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja Liwale alituahidi kutujengea kituo kwenye Tarafa ya Kibutuka na Kata ya Lilombe. Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa sababu jiografia ya Liwale kuwa ngumu hali ya usafiri ni mbaya sana, sasa je, Serikali iko tayari kutupatia gari kwa ajili ya maaskari wa kituo hiki?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, najibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge kuchauka kwamba ahadi zote zilizoahidiwa na viongozi wa Serikali zitatekelezwa. Sasa hivi tupo kwenye kufanya tathmini kuona wapi paliahidiwa ili tuanze sasa utekelezaji wa ahadi hizo. Kwa hiyo hicho ambacho kimeahidiwa Mheshimiwa awe na amani kitatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, kingine nimwambie ni kweli Serikali inafahamu umuhimu wa uwepo wa magari katika meneo mengi ambayo watu wanaishi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, kwanza tunafanya operation za mara kwa mara, lakini kufanya doria za mara kwa mara na kuhakikisha kwamba tunapambana na matukio ya kihalifu. Nimwambie tu Mheshimiwa kwamba katika gari ambazo zitafika tutahakikisha kwamba katika Jimbo la Liwale gari itakwenda ili iweze kusaidia wananchi kwa ajili ya kuweka hali ya amani na utulivu katika eneo hilo, nakushukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri amesema kwamba mwajiri wa Walimu hawa ni Mkurugenzi wa Halmashauri, lakini Mkurugenzi huyo wa Halmshauri amemnyima nafasi ya kukataa uhamisho wa mtumishi, jambo linalofanya watumishi wengi kuchukua namba tu kwenye hizi wilaya ambazo zipo pembezoni na kuondoka. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha Wakurugenzi wanakuwa na Mamlaka ya kuhamisha kulingana na wanavyoona nafasi inayopatikana?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kuchauka. Hili la kukataa uhamisho liko wazi, Waraka wa Katibu Mkuu Utumishi unaeleza wazi kwamba mtumishi wa umma anapoajiriwa atatumikia mwaka mmoja wa probation na baada ya mwaka ule anatakiwa kukaa katika kituo chake kipya cha kazi kwa muda usiopungua miaka miwili kabla ya kuomba uhamisho.

Mheshimiwa Naibu Spika, namna utaratibu ulivyo ni lazima mtumishi anapoomba uhamisho katika barua yake ile awaweke pale KK, Mkuu wake wa Shule, amuweke Afisa Elimu wa Wilaya, amuweke muajiri wake ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri na wale wote wanatakiwa kuweka comment pale, kama wanaona kuna uhaba wa watumishi katika maeneo yao, katika barua ile wanavyoandika imepitishwa, aandike kwamba kuna uhaba na huyu nashauri asihame. Barua ile inapofika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, wataangalia na zile comment za mwajiri na kuzifanyia kazi na kuhakikisha kwamba Mwalimu yule au mtumishi yule hatoki katika maeneo yale ikiwemo kule Liwale. Kwa hiyo naomba Mkurugenzi wa Liwale afuate utaratibu.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Wilaya ya Liwale ndiyo Wilaya katika Mkoa wa Lindi imepokea wafugaji wengi sana lakini hakuna miundombinu ya majosho wala malambo. Je Serikali iko tayari kutujengea majosho na malambo kwenye Kata ya Lilombe na Kata ya Ndapata, Kata ambazo ndizo zimetengwa kwa ajili ya kupokea wafugaji? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wilaya ya Liwale ni miongoni mwa Wilaya ambazo zipo katika mpango wetu katika huu mwaka. Kikubwa tutaangalia katika orodha ili tuone maeneo gani ambayo tutayapa kipaumbele. Ahsante.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwanza nishukuru Wizara kwa majibu mazuri yanayotia matumaini. Jambo hili linaenda kutatua tatizo kubwa la ununuzi, na hasa katika taasisi zetu za umma ambazo zinaingia kwenye ushindani ambazo zinashindwa kufanya manunuzi kwa sababu ya ushindani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa miradi mingi kwenye halmsahuri zetu sasa hivi inatekelezwa kwa force account na watu wanaoingia kwenye manunuzi ni watu ambao hawana taalum; Je, Serikali iko tayari kutoa mwongozo mahsusi ili kuongoza kuona namna gani hayo manunuzi yanayokwenda kufanya kusiwe na mgongano ambao sasa hivi nani ambaye anatakiwa kujibu maswali hayo ya ununuzi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ili kupunguza safari nyingi za maafisa ununuzi kwenda na kurudi kwa ajili ya kwenda kufanya manunuzi, Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza yale masurufi (imprest) kutoka milioni tatu ili kufika milioni kumi, kwa sababu sasa hivi hakuna bidhaa inayoweza kununuliwa kwa shilingi milioni tatu? Kwa hiyo matokeo yake wale maafisa manunuzi wanakwenda na kurudi zaidi ya mara tatu kwa bidhaa moja.
NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mohamed Kuchauka kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa ridhaa yako nijibu maswali yote mawili kwa pamoja. Taratibu, mwongozo na kanuni zinatolewa mara baada ya kutunga Sheria hiyo katika Bunge lako Tukufu. Hii ndiyo nafasi adhimu baada ya Muswada kuja Bungeni ya Wabunge kutushauri na kutuelekeza. Serikali yao ni sikivu sana tutaendelea kupokea ushauri huo na kuufanyia kazi, ahsante.

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa jambo la kuita watu wengi kwenye nafasi chache chache za usaili limekuwa ni jambo sugu na Serikali hamuwezi kulifanyia kazi; je, hamuoni sasa umefika wakati kuwapa posho angalau wale mnaowaita, ili waweze kujikimu wanapokuwa Dodoma?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, jambo analosema la kutoa posho kwa wanaoomba, hili ni jambo la kibajeti, lakini pia ni jambo la kisera. Kwa hiyo, tutakapokuwa tumejenga uwezo, Mheshimiwa Zuberi Kuchauka na Wabunge wote basi nalo pia litaangaliwa, lakini kwa sasa niseme jambo hilo ni gumu kidogo. (Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Wilaya ya Liwale kijiografia imekaa vibaya sana hasa kwa ulinzi tunayoahadi ya kujengewa vituo vya polisi kwenye Tarafa ya Kibutuka, Kata ya Lilombe na Kata ya Kimambi. Nini kauli ya Serikali juu ya kutekeleza ahadi hiyo ili kuimarisha ulinzi kwenye Wilaya yetu ya Liwale? (Makofi)
NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, japo hajaniambia ahadi ilitolewa na nani lakini nikiri tu, kwanza maeneo yote ya tarafa yanahitaji kuwa na vituo vya polisi vyenye hadhi ya kutimiza majukumu ya ulinzi na usalama wa wananchi na mali zao zikiwemo hizi tarafa ulizozitaja za Liwale kwa maana ya Kibutuka na tarafa hizo nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulingana na bajeti tuliyonayo tunakwenda kwa awamu. Kama tulivyokubaliana na Mheshimiwa Kuchauka tutafanya ziara Mkoa wa Lindi ili kuona uhitaji wa vituo hivi ili kuweka msukumo kwenye jeshi la polisi waweze kuvizingatia katika mipango yao ya ujenzi na ukarabati wa sekta nzima ya polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumekuwa na uhaba mkubwa wa watumishi katika Wilaya ya Liwale, lakini hata hivyo mgao tunapata watumishi, lakini idadi ya watumishi wanaohama na wanaohamia kubwa ni ile ambayo wanahama bila kufanyiwa replacement. Je, nini kauli ya Serikali juu ya kuhamisha watumishi bila kutupatia replacement kuziba nafasi hizo? Ahsante.
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tunatambua changamoto za maeneo ya pembezoni walimu wengi wanaoajiriwa huwa wanapenda kuhama na sasa hivi mkakati wa Serikali ni kwamba watu wote ambao tunawaajiri tunawapa na ile barua kwa maana ya commitment letter ambayo itawafanya wakae maeneo siyo chini ya miaka mitatu mpaka watakavyoomba kuhama. Lengo la Serikali ni kuhakikisha maeneo yote nchini yanakuwa na usawa wa walimu wote ambao tunawaajiri, ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kuniona kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mji wa Liwale ni mji unaokua kwa kasi sana na ni miaka 42 sasa umri wa mji ule, lakini una kilometa 1.8 tu za lami pale mjini. Je, Serikali iko tayari kutuongezea mtandao wa barabara ya lami kwenye mwaka huu wa bajeti?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKAO NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuambie tu kwamba Serikali iko tayari na tumetenga fedha na ninaamini eneo la Liwale ni sehemu ambayo tumewaanishia katika bajeti ya mwaka huu 2022/2023.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kata ya Miluwi iko umbali wa kilomita 80 kutoka Liwale Mjini ambako kuna hospitali ya wilaya na uhitaji wa kituo cha afya pale ni mkubwa sana na wananchi wameshaanza ujenzi wa kituo cha afya pale. Je, Serikali iko tayari kusaidia kwenye bajeti hii kuunga mkono juhudi zile za wananchi?
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza niwapongeze sana wananchi wa Kata hii ya Miluwi ambao wameanza kuchangia nguvu zao kujenga kituo cha afya na niwahakikishie kwamba Serikali itaendelea kuchangia katika hizo nguvu za wananchi ili kuhakikisha kwamba kituo hicho kinakamilika kwa awamu. Ahsante.
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa majibu ya kuridhisha.

Kwa kuwa barabara nyingi hapa nchini zimeshafanyiwa upembuzi yakinifu kwa muda mrefu sasa na hizo barabara zimeshakuwa ni nyingi sana; na bado ukiuliza unaambiwa tunatafuta fedha kwa ajili ujenzi.

Je, Serikali haioni kwamba imefika wakati sasa tusitishe kwanza kuendelea kufanyia upembuzi yakinifu tumalize hizi barabara ambazo tayari zimeshajengwa ili resource tulizonazo tumalizie hizi zilizojengwa ndipo tuendee kufanya upembuzi yakinifu?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, iko barabara inayotoka Masasi kwenda Nachingwea mpaka Liwale zaidi ya kilometa 158, barabara hii imeshafanyiwa upembuzi yakinifu zaidi ya miaka minane sasa.

Je, ni lini Serikali wataijenga barabara hii kwa kiwango cha lami?
NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuberi Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi kuzifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara ambazo tunaendelea nazo. Lakini pia naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba moja ya mahitaji ili barabara ziweze kujengwa kwa kiwango cha lami ni kujua gharama zake ili hata wakati Serikali inatafuta fedha inakuwa inafahamu gharama ya zile barabara, inakuwa inafahamu ni wananchi gani ambao watapisha ujenzi, lakini pia inasadia kuzuia wananchi wasijenge maeneo ambako barabara itapita.

Kwa hiyo, tutaendelea kufanya usanifu ili kuwa tayari tunapopata fedha tuanze kujenga badala ya kusubiri kuanza usanifu pale tunapokuwa tumepata fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, barabara aliyoitaja ya Masasi – Nachingwea hadi Liwale, katika bajeti hii tumetenga fedha kwa ajili ya kuanza kuijenga barabara kuanzia Masasi kwenda Nachingwea na Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili kipande cha Nachingwea kwenda Liwale, ahsante.