Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kunipa fursa hii kuchangia Mapendekezo ya Mpango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wabunge wengi wamezungumza ndani ya Bunge lako Tukufu walau kuna waliotoa mchango wa maana kuna wengine wameingiza kidogo siasa, lakini ndio maana ya Bunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nataka niende kwenye mpango na ninataka Dkt. Mpango unisikilize vizuri kweli kweli ukipitia hotuba yako ukurasa wa 34 ambapo unajadili changamoto za utekelezaji wa mpango wa maendeleo na bajeti:-

(i) Serikali inasema ugumu wa kukusanya kodi kutoka kwa wafanyabiashara waliopo katika Sekta isiyo rasmi kwa kuwa hawana sehemu rasmi za kufanyia huduma ya Kibiashara, hiyo ni moja Serikali imekiri.

(ii) Kutofikiwa kwa lengo la Kodi zinazotokana na ajira (Pay As You Earn) kilichosababishwa na kutofikiwa kwa malengo ya ajira mpya na kutokuongezeka kwa mishahara kwa wafanyakazi kama ilivyokuwa imetarajiwa haya Serikali inakiri. Hebu imagine Serikali ilikuwa inaanzisha chanzo haijui kama mishahara itaongezeka halafu leo tunakaa ndani tunajadili, Serikali yenyewe inakiri kwamba jamani tumeshindwa kwa sababu mishahara haijaongezeka kama tulivyokuwa tunatarajia tulikuwa tunapitisha mpango wa nini?

(iii) Sasa unakuja inakwambia kushuka kwa biashara za Kimataifa kulikopelekewa kutofikiwa malengo ya uagizwaji wa bidhaa kutoka nje, Serikali imekiri, watu wanazungumza yenyewe imekiri, imeandika ukurasa huu wa 35.

(iv) Upungufu wa Wafanyakazi na Vitendea kazi ndani ya Mamlaka ya Mapato Tazania yaani mpaka leo Serikali yaani wakusanyaji mapato hawana Vitendea kazi mnajadili nini yaani hapa tunajadili nini?

(v) Kupungua kwa misaada na mikopo nafuu kutoka kwa washirika wa maendeleo wakati wa utekelezaji wa bajeti.

(vi) Changamoto ya masoko na bei ndogo za mazao kwa wakulima, Serikali imekiri yenyewe mapungufu.

(vii) Kuendelea kuwepo kwa madai mbalimbali yakiwemo ya wakandarasi, watoa huduma, wazabuni na watumishi wa umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hebu fikiria malalamiko ya Serikali ambayo yalivyo genuine. Sasa kazi ya Bunge ambayo ilipaswa leo tuijadili hapa cha kwanza ilikuwa ni kwa namna gani tunaweza tukatoka hapa, that was number one. Mimi nimejaribu kupitia mpango hapa tangu jana napitia nimeangalia kila nikijaribu kuangalia sasa Serikali imekuja na mpango itautekelezaje mwakani kwa sababu mpango bila fedha ni kazi bure, is a nonsense. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hizi zote zinazopigwa hapa zitabaki kuwa stori tuu sasa unakuja kugundua, mimi wiki iliyopita, wiki mbili nilikuwa Rwanda kuna kitu nimejifunza na ningependa Tanzania ikajifunza. Nchi ya Rwanda kabla Mawaziri hawajateuliwa na Rais Kagame wanapewa perfomance contract unasema mimi Waziri wa Fedha nikiwa Waziri nitafanya moja, mbili, tatu, nne, tano, ukishindwa kutekeleza unaondoka automaticaly, hakuna mjadala.

Sasa leo kwetu humu ndani unakuta mtu analinda Uwaziri kwa kusifia sio kwa kutenda kazi, leo tukiwapima Mawaziri hapa tukasema Waziri gani number one na wa mwisho ni nani? Sisi wenyewe Wabunge tunajua nani anapiga porojo hapa ni waongo tu, nani wanamdanganya Rais tunawajua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, yaani tunawajua hapa wote ninyi mlivyo, sasa matokeo yake mtu anayejua kusifia sana ndio anayeonekana anafanya kazi, tunaliangamiza Taifa hili. (Makofi)

Sasa ukipitia hapa unaenda unaangalia mafanikio ya utekelezaji wa mpango unakuta Serikali imeandika pale kwamba ulipaji wa madai, eti Serikali mafanikio kulipa madai mlikuwa mnakopa mlikuwa hamjui hamtalipa? Yaani ipo kabisa kwenye hotuba ukurasa wa 31 eti madai, kulipa madai kweli jamani? Kwenye hotuba kabisa unaandika kabisa kabisa yaani na watu wanavuka kama hawaelewi unakuta mtu anakuja anaandika hapa kwamba huduma za maji, kwa mfano soma ukurasa wa 31 mimi imenishtua ndani ya miaka mitatu kwamba ukurasa wa 31 wa hotuba inasema; “Miradi 1595 ya maji vijijini imekamilika inayohudumia watu milioni 31,652,000” uongo uliotukuka, is a complete lie, kila Mbunge hapa analalamika maji watu milioni 31 jamani over sixty percent ya wananchi ndani ya miaka ya tatu kweli tunajadili mambo ya namna hii? A total lie. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mambo unaweza kuyakuta Tanzania tu lakini muangalieni mwenzenu Mheshimiwa Rais Kagame, Kagame is a different man, pamoja na matatizo yake mengine lakini nimeona ni mtu tofauti. Rais ana bodi ya ushauri ambayo inamshauri, hiyo ina vikao viwili tu, mwezi wa sita wanakaa Kigali, mwezi wa kumi wanakaa Washington, Marekani. Bodi yake aliyounda kuna Rais Clinton, kuna kina Tony Blair kuna ma-CEO wa makampuni makubwa yote yanamshauri kuhusu uchumi wa Rwanda. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna mradi unatekelezwa Rwanda bila kupitia level tatu za utathmini, anaitwa consultant number one, anakuja namba mbili, anakwenda namba tatu akishauriwa Rais Kagame hapo arudi nyuma ndio mtu akipinga atapotea katika mazingira ya kutatanisha, sio mawazo tu ambayo mtu mmoja anaweza akatoa wazo likaanza kutekelezeka halafu tathmini baadae, this is a nonsense, hatuwezi kuendesha nchi katika huo mfumo. (Makofi/Kicheko)

Sasa leo tuna SGR (reli), Kenya wakati wanaanzisha SGR walihakikisha wanapanua bandari ya Mombasa, that was they did Kenya, leo una SGR Tanzania bandari wanasema tunarekebisha gati one wakati mipango ya miaka yote tunapitisha ndani ya Bunge tumepitisha gati 13, gati 14 yamefutwa kwenye mpango sasa unategemea hii reli ikishakamilika fedha tunaturudisha vipi za miradi ya reli? Tumeshindwa kuiga Kenya wanavyofanya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo unasema mradi unaanza Disemba unakwenda mpaka Isaka sijui baada ya hapo unakwenda Makutupora wakati Rwanda mwenzako anakwambia Mradi wa SGR ataufadhili kwa kutumia PPP, wewe unasema nitaufadhili kwa kutumia fedha za ndani yaani unakuja kugundua yaani sijui tuna watu wa namna gani kwenye nchi yaani tuna watu they can not think unaweza kuwa Ph.D holder you can be a Professor lakini real life inakuwa determined na uwezo na capacity namna ambavyo mtu anavyoweza kutekeleza na kusikiliza. Kwa hiyo, mimi niliona nilisemee hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ukiifananisha na Rwanda ni vitu viwili tofauti strategically sisi tumezungukwa na nchi karibu tisa ambao hizi zote zinategemea Tanzania. Nchi ya Rwanda hawana rasilimali mtu atajenga hoja wanaiba Congo, lakini si kweli mtu anasema Rwanda ni kanchi kadogo si kweli mtu atakuja anahoja Rwanda kuna vision, Rwanda kuna commitment watu wako tayari kutumikia Taifa lao Tanzania hakuna commitment iko labda kwa mtu mmoja tu the rest ni blaa blaa tu kudanganya wananchi wa Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nilikuwa naomba Serikali inapokuja mwishoni ije na mpango, itueleze hapa namna gani tunaweza tukakusanya trilioni 22 ili tuweze ku- finance mpango, lakini ukiangalia hapa nilikuwa naangalia vilevile kwenye huo ukurasa uliokuwa unafuatia namna ambavyo mkakati wao hamna mkakati tutaimarisha TRA kwa kukusanya kodi yaani ni kile kile waje watuambie namna gani sasa tutapata fedha kwenye vyanzo vya uhakika ili nchi iweze kufaidika.