Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Amb Dr. Diodorus Buberwa Kamala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. BALOZI DKT. DIODORUS B. KAMALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba nianze na kusema kwamba naunga mkono hoja lakini pia naomba nijikite kwenye changamoto ya kwanza ambayo Mheshimiwa Waziri ametueleza katika kitabu chake cha hotuba kwamba ndio changamoto kubwa ziko nyingine, lakini yenyewe ni ya kwanza ambayo ilichangia katika kutekeleza vizuri kama tulivyokusudia na changamoto yenyewe ni kwa sababu tuna wafanyabiashara walio kwenye sekta binafsi hawana sehemu maalum, hawatambuliki, kwa hiyo inakuwa ngumu kwa Serikali kukusanya kile ilichokusudia kukifanya. Kwa hiyo, ningependa kushauri mambo yafuatayo kuhusiana na jinsi ya kukabiliana na changamoto hiyo.

Kwanza, naishauri Serikali wakati umefika kwa kutumia Geographical Information System (GIS) katika kuwatambua wajasiliamali katika kukusanya kodi katika kujua nani amelipa na nani hajalipa. Ninaposema GIS sitaki sihitaji kusema maneno mengi kwa sababu ndio mfumo wa kisasa unaotumika, na habari nzuri hapa Tanzania wataalam wa kuandaa mifumo hii wapo na kuna kampuni moja ambayo imeandaa mfumo inaitwa Digital City Services Mheshimiwa Waziri utakuwa unafahamu kwa sababu nina uhakika wataalam wako wanajua kuhusu kampuni hii na kampuni hii imefanya kazi kule Njombe kuhusu property tax walipohamishia zile shughuli kwenda kule Wizarani hiyo project ikasinzia, lakini pia hivi sasa Manispaa ya Iringa ipo mbioni ku-adapt utaratibu huu kwa GIS. Sasa kama hili jambo lipo na linawezekana na mfumo huu ni mwepesi maana tunatumia simu tu, utaalam tuanao Mheshimiwa Waziri nashauri uangalie eneo hili na tuone jinsi gani tukatumia GIS katika kukabili changamoto hii.

Ushauri wa pili, Mheshimiwa Waziri unapoangalia wajasiriamali mfumo wetu wa kodi tatizo ninaloliona moja unavyomuangalia mama ntilie ndio hivyo hivyo unavyomwangalia mfanyabiashara mkubwa au kampuni kubwa kama TBL. Sasa unapokuwa na mfumo unaofanana katika ukusanyaji kodi huo huo unaupeleka kwa mfanyabiasha mkubwa kama TBL mfumo huo huo unaupeleka kwa majasiriamali mdogo, lazima utapata shida Mheshimiwa Waziri. Kwa hiyo, ushauri wangu na wataalam wapo wa kusaidia katika hilo tuandae tailor made regime kwa ajili ya informal sector. Tukifanya hivyo Mheshimiwa Waziri tutakuwa tumepiga hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa tatu ni kuhusu kodi katika economics nyepesi lazima iwe certain, lazima mtu awe anajua akiagiza bidhaa atalipa shilingi ngapi, sio baada ya kuagiza anapofika pale kuanza kulipa anakuta mambo yanabadilika, nasema hivyo kwa sababu tatizo kubwa tulionalo hapa ni kwamba unaweza kukaagiza vitu kwenye kontena lile lile, vitu kutoka sehemu ile ile, waagizaji tofauti lakini kila mtu anaambiwa kodi yake ya kulipa. Sasa hii sio sawa Mheshimiwa Waziri, kwa hiyo lazima tuweke utaratibu ambao utakuwa certain ili mtu yeyote mfanyabiasha anapoenda Dubai, anapenda China anapoenda popote duniani awe anajua akija pale bandarini alipa shilingi ngapi na hilo lisibadilike badilike. (Makofi)

Kwa taarifa yako Mheshimiwa Waziri wapo wananyabiashara wengi wa Tanzania wamaamua kutumia bandari za nchi nyingine kwa kuogopa kwamba watakapofika pale kwenye bandari yetu wataambiwa bei ambazo ndivyo sivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu wa nne ni utararibu wetu, hili ni jambo la capacity building tusitarajie kukamua maziwa kutoka kwa mfugo kama unafunga ng’ombe huwezi kukawa unapanga kukamua maziwa mengi bila kumlisha ng’ombe huyo vizuri. Nasema hivyo kwa sababu hawa wajasiriamali wetu hawa watalipa kodi kama wataweza kuwazeshwa masuala mbalimbali mojawapo ni vitu vidogo tu kwa mfano tulikiwapa simple skills za accounting wakazijua, unaweza ukaanzisha programu ya accounting system nyepesi tu ya kufundisha tu hata unawezana ukatumia hata wanafunzi ukitoa elimu hiyo kwa wajasiriamali wetu watawea kutambua nini wafanye ili waweze kulipa kodi vizuri na Serikali inanufaika na utaratibu huo.

Jambo lingine ni elimu ya kodi, tatizo kubwa tunalolipata katika biashara hizi wafanyabiasha wadogo wadogo/wajasiriamali au wataalam wetu wa kodi anapoenda kwa mfanyabiasha huyo anaanza kumwambia hiki mbona hujafanya, hiki hujafanya, kile hujafanya, hiki hujafanya, kwa hiyo na huyo kwa kuwa hajui basi anaishia kukimbia mwingine anaishia kujificha au kulazika kulipa kodi kubwa ambayo siyo, hii ni kwa sababu kutokuwa na elimu hiyo. Sasa kwa kuwa muelekeo Watanzania wengi watakuwa wajasiliamali wakati umefika katika mitaala ya elimu ya msingi kuanza kutoa elimu ya kodi. Mheshimiwa wa Waziri wa Elimu atusaidie katika hili lakini Serikali ijipange tuone ni kwa namna gani vijana katika shule za msingi kuanzia kule wanaweza kuanza kupata elimu ya kodi ili wanapofika kwenye kujiajiri isije kuwa jambo jipya.

Ushauri wangu mwingine ambao napenda niutoe haraka haraka lazima tu-simplify system yetu ya kodi, iwe nyepesi, lakini pia ambapo ni jambo dogo ukiliangalia upokuja kwenye kulipa kodi kuna suala la kandaa returns, kuna suala la manunuzi na mauzo, mfanyabiasha wa mchele kwa mfano anayefanya biashara ya mchele anapoenda kununua mchele wake ananunua maeneo mbalimbali huko vijijini na mara nyingi hizi risiti zinakuwa hazipo. Lakini ukimuuliza ya mauzo risiti atakuwa nayo ya mauzo unapomuuliza risiti ya manunuzi hana tatizo linaanza, lakini kwa mfano ukaenda pale Mwenge ukakutana na wafanyabiasha wa vinyago yule mfanyabiasha wa vinyago ukimuuliza risiti za mauzo anaweza kuwa nazo, lakini ukimuuliza risiti za manunuzi ya kinyago kile mpaka kimefikia pale hana, tatizo linaanza.

Mheshimiwa Waziri uanglie ni kwa jinsi gani tunaweza tukasimplifyeneo hilo ili kuweze kuondoa huo utata ambao unasumbua. Lakini pia ukienda kule Kanda ya Ziwa bidhaa nyingi tunatumia za kutoka nchi za jirani hakuna Special Economic Processing Zone na shauri izingatiwe na nishauri poa kule Kajunguti ambapo tulilikuwa tujenge uwanja wa kimataifa wa ndege sasa hatujengi, lakini tuweke Export Processing Zone, tukifanya hivyo tunaweza tukatumia lile eneo vizuri na kuendelea kupiga hatua.