Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

Hon. Salum Mwinyi Rehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali Pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020

MHE. SALUM MWINYI REHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nami naunga mkono hoja. Naomba nichangie na nishauri Serikali katika mpango huu, nikimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa kuwasilisha maoni yake. Nami naomba niwasilishe maoni ambayo naona yanaweza kuisaidia Serikali hii kuiondoa hatua moja kwenda hatua nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kubwa la mwanzo ambalo nataka kuanza nalo ni suala zima la uwekezaji katika bahari kuu. Nchi zote za visiwa na nyingine zilizozungukwa na bahari suala hili limekuwa kipaumbele na wenzetu limewatoa na ndiyo nguzo ya uchumi wao. Tanzania hatufaidiki hata asilimia moja katika maeneo ya uvuvi wa bahari kuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu ni huu, kama tumeweza kununua ndege, kwa nini tushindwe kununua long vessels mbili tu ambazo zitaweza kuongeza mapato zaidi ya shilingi bilioni 7.8 kwa kila bamvua. Wale wenzangu wa Pwani wanaelewa bamvua ni kipindi kile cha uvuvi tu kwa kila long vessel moja. Kwa hesabu za haraka nilizozipiga ni kwamba tukiwa na long vessels mbili tunahitaji wataalam katika mchakato mzima wa uwekezaji wa viwanda vya samaki na uvuvi wa bahari kuu karibu 3,640; lakini tunahitaji hard labor katika eneo hilo karibu wafanyakazi 48,000 wakati mmoja na hawa watakuwa wanafanya kazi kwa pamoja ambapo meli moja inakwenda Pwani, meli moja inapakua mzigo kutoka baharini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia sasa hivi ina mahitaji zaidi ya asilimia 67 ya samaki. Tuna demand kubwa in the world wa samaki aina ya tuna katika soko la China, Nordic countries, Japan. Sasa hivi samaki aina ya tuna wamepanda kutoka dola 8,000 kwa tani mpaka dola 18,000 kwa tani. Hiyo demand haijawahi kutokea duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ni sehemu ambayo sisi kama nchi tunakiwa tuiangalie. Nami nashangaa Doctor, kwa nini hili lisiwemo katika mpango wa sasa hivi? Tumechelewa sana, kwa sababu uwekezaji uliokuwepo hapa, input na output haziko sambamba, ni only two percent ya input, lakini una output ya 98% kwenye total production ambayo tunaweza tukaifanya katika maeneo hayo. Wewe ni mchumi na unaelewa hapa ni kitu gani tunachokizungumza. Naomba tufanye restructuring tuhakikishe kwamba tunakuwa na uwekezaji katika eneo hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili katika eneo hilo, tutaanzisha viwanda ambavyo vitaweza kuchakata hawa samaki. Tukiianzisha bandari moja ya uvuvi hapa nchini ambayo mwenzangu ameshaidokeza pale, inaweza kutuingizia mapato mengi sana. Kwa mfano, ukaguzi wa long vessel moja tu ambayo tutaipa leseni sisi kama Tanzania ni dola 40,000. Ndani ya nchi kwa mwaka mmoja tunaweza kusajili zaidi ya meli 40 au 100, ni kiasi gani ambacho nchi itaweza kuingiza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hivyo tu, kila meli moja inayokuja kukagua lazima ichukue vyakula ndani ya nchi, inaanzia tani 10 mpaka 17. Hizi ni fursa ya soko la bidhaa ambazo tunazalisha wananchi hapa, wakulima watakuwa wamepata sehemu ya soko na vyakula mbalimbali vitaweza kuuzwa kwenye maeneo hayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo hicho tu, niliwaambia watu, maji haya ya kawaida ambayo yanatiwa katika vile vyombo, kila meli moja tungeiuzia zaidi ya shilingi milioni mbili au shilingi milioni nne. Mbali na upande wa mafuta, tutaweza kufanya biashara kubwa kabisa ya uwekezaji katika maeneo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti,katika kitu ambacho kinaweza kututoa ni hili suala la uwekezaji katika uvuvi wa bahari kuu. Kwa sababu meli, hii long vessel ndogo ya kawaida ina uwezo wa kuvua kuanzia tani 42,000 mpaka 105,000 na tunaweza kuinunua meli hii kwa dola za Kimarekani 450,000 na hizi mbili au zile kubwa zaidi tukainunua kwa dola 700,000 kitu ambacho kinawezekana kwa nchi. Kwa hiyo, naiomba Serikali ijielekeze huko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ambalo napenda nishauri ni eneo ambalo bado kama nchi uwekezaji wake hatujaufanya. Wenzetu nchi za nje na nchi nyingine ambazo ziko ndani ya eneo la Sahara zinawekeza kwenye research. Namwomba Mheshimiwa Dkt. Mpango aangalie suala hili la research. Nchi yoyote duniani haipigi hatua kama haikuwekeza kwenye research. Research hupotezi, ndiyo mwongozo utakaokupelekea kufikia yale malengo uliyokusudia. Tuna tatizo katika uwekezaji katika eneo hili, tunazungumza sana na kama Doctor kazi yako kubwa na wewe ilikuwa ni research lakini priority za maeneo ya research hazijakuwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mmoja kati ya Wajumbe wa Baraza na hayo malalamiko yapo katika kila eneo la research unaambiwa kwa kweli fedha katika maeneo hayo zinazokwenda kwa kiwango kidogo sana. Siyo tu kwenye research kwenye maeneo ya kilimo na mifugo lakini hata maeneo ya elimu na viwanda, huko kwenye viwanda bado hatujafanya utafiti wa kutosha tukagundua viwanda gani tunahitaji kama nchi? Tuwekeze kitu gani tuweze kutoka hapa? Je, tuwekeze kwenye viwanda vya chuma ambavyo vinapatikana ndani ya nchi au tuwekeze kwenye viwanda vya aina gani? Nafikiri hili nalo lionekane katika huu mpango, kuna vipaumbele katika maeneo hayo na litatutoa katika kipindi kifupi tu kijacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ambalo nataka kulizungumzia ni suala zima la utalii. Bado kama nchi sisi tunapata tip tu, hatufaidiki na fee zinazotokana na utalii. Wanaoshughulika na tasnia ya utalii wanaelewa, nchi yoyote ili ifaidike na utalii unatakiwa uwe na link ambayo itakuunganisha kutoka mtalii anapotoka na aweze kulipa ndani ya nchi. Watalii wetu wengi wanalipa kwao, wanalipa kwenye makampuni yao, wanakuja na travelling card ndani ya nchi hapa, hatufaidiki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba suala hili liangaliwe upya. Kwa kweli kiwango tunachokipata hapa nchini ni kidogo sana, tungeweza kupata zaidi ya mara 20 au 50 ya pato ambalo wanapata wenzetu na tungeweza kwenda kujifunza Mauritius na Seychelles, nchi ndogo watu wachache, lakini kipato chake kinachotokana na utalii ni kikubwa. Leo mtalii nchini kwetu mpaka kufika hapa, mchakato wote ule anatoa dola 15 lakini akiingia Seychelles kufanya utalii, mtalii yeyote lazima atoe dola karibu 160 za mwanzo hizo. Ni entry fee ambazo wao wamezitengenezea mazingira. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba twende tukafanye utafiti kwa wenzetu, tukae nao, watupe ujanja na mbinu tuweze na sisi kuwekeza katika hayo maeneo. Vivutio tulivyokuwanavyo vinalipa. Leo hii watalii ambao wanakuja katika maeneo yetu, kwa mfano, Ngorongoro ukiwazuia, kwa kweli yatakuwa maandamano makubwa. Sasa kama vivutio hivi potential viko nchini na tunaweza kuvi-control wenyewe, tuwe na usimamizi mzuri tupandishe kipato ambacho kitaweza kuleta tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaka kuzungumza kidogo suala la mbegu ambazo tunasema kwamba tunataka tuzizalishe ndani ya nchi, tuna tatizo.