Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Spika, nami nashukuru sana kwa kunipa nafasi ili niweze kuchangia. Kwanza nianze kutoa pongezi kwa Wizara ya Fedha. Wizara ya Fedha imeweza kufanya kazi kwa ufanisi mzuri sana. Bahati nzuri taarifa tuliyoisoma ipo wazi. Pale walipo-perform vizuri wanasema na pale wanapojua hawaja-perform wanasema. Huo ndiyo tunasema uwazi. Ndiyo maana kila mmoja anasema labda kwenye kilimo amepeleka asilimia kadhaa, ipo wazi; kuliko asingesema vitu ambavyo ame-perfom. Kwa hiyo, nimempongeza sana Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa uwazi huo.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili, Wizara ya Fedha ndiyo moyo wa Serikali, ndio moyo wa maendeleo ya nchi hii na ndiyo inayo-control mapato yote ya nchi hii. Ili Serikali i- perform vizuri, lazima Wizara ya Fedha ikae vizuri. Tunajua kwamba ili Serikali ifanye vizuri lazima makusanyo ya kodi yakae vizuri. Kuna Mbunge mmoja alisema kwamba Wizara hii inataja kodi tu, lazima itaje kodi tu kwa sababu isipotaja kodi haiwezi kupata fedha ya kuendesha shughuli za Kiserikali.

Kwa hiyo, nasema waendelee kutaja kodi tu ili na wananchi waelewe kwamba lazima wananchi walipe kodi ili Serikali ifanye vizuri kwenye miradi ambayo tunahitaji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukitaka kuangalia, wameeleza vizuri kwamba wanataka kupunguza umaskini. Nataka nijikite vizuri sana kwenye kupunguza umaskini. Wanataka wafanye ufuatiliaji kwenye vijiji ili waangalie umaskini umepungua percent ngapi? Tuna changamoto nyingi sana vijijini.

Mheshimiwa Spika, nataka niiombe Wizara ya Fedha, lazima isimamie vizuri kuhakikisha kwamba mahitaji ya wananchi kule vijijini kweli yanapungua. Nataka nitoe mfano mdogo tu, tukisema kupunguza umaskini kwa wananchi, lazima tuhakikishe miradi ile inayolenga wananchi inafanyika kiusanifu na kwa bei inayojulikana. Wengine wanasema, Serikali isifanye uhakiki, wanasema kila siku ni kuhakiki. Nasema kuhakiki kuongezeke kwa sasabu unaweza ukaona Serikali imelipa fedha nyingi sana lakini mradi wenyewe hauonekani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haiwezekani Serikali ikawa inatoa fedha nyingi, halafu mradi ule hauonekani. Kwa mfano, wanachimba kisima cha maji vijijini, wananchi hawajapata maji, lakini fedha zinaonekana zimetumika pale. Hii haitakubalika hata siku moja. Zamani miaka mitano iliyopita, unaweza ukaona wananchi wanahitaji maji pale kijijini, wanasema kwamba Mkandarasi ametumwa na Serikali, labda Wizara akachimbe kisima cha maji. Maji hajapata, unaenda kuangalia gharama kubwa pale zimetumika na wananchi hawajapata maji. Hii kweli itakubalika? Hii haiwezi kukubalika. Lazima tuone impact. Kama fedha zimetumika kwa ajili ya kuchimba kisima, basi wananchi wapate maji pale. Hilo lazima Serikali ihakikishe inafuatilia vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tuna changamoto kubwa sana. Kwa mfano miradi ya maji. Naiomba Serikali, miradi ya maji mpaka sasa hivi kama tunapunguza umaskini, basi tupunguze kwenye mradi ya maji, tuhakikishe wananchi wetu wote wamepata maji. Kuna Wakandarasi wengine bado wanadai fedha hazijalipwa. Kwa mfano, hata kwenye Jimbo langu, kuna kata moja ya Sawala, Mkandarasi sasa hivi kuna miezi sita alishasaini mikataba lakini mpaka leo hajapata fedha na mradi ule umesimama na wananchi wanataka impact ya maji. Kama tunapunguza umaskini, basi tuwapelekee maji.

Mheshimiwa Spika, kuna sehemu nyingine wananchi wanatembea kwa mguu kilomita nne au kilomita tatu wanatafuta maji. Sasa tusipokijita vizuri, hata hii perception ya kusema tunapunguza umaskini, tutakuwa hatujapunguza umaskini. Wananchi wanataka wapate maji. Namwomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha, wananchi wanataka kupata maji. Miradi ile ya maji ambayo tumetenga kwenye bajeti, basi wapeleke tuhakikishe inafanyika kwa ufanisi kama ilivyopangwa ili wananchi waweze kupata maji.

Mheshimiwa Spika, suala lingine, kwenye makusanyo. Serikali ijitahidi kufanya makusanyo. Lazima kwanza itengeneze urafiki na wafanyabiashara, TRA watoe elimu ya kutosha ili kuhakikisha kwamba kila mtu anayelipa kodi asione kama adhabu, aone ni wajibu wake kulipa kodi. Ili ajue kwamba ni wajibu wake kulipa kodi, lazima utaratibu wa ulipaji kodi uwe mzuri. Kuna point moja nimeipenda sana kwamba Wizara ya Fedha kushirikiana na TRA wanataka utaratibu mzuri wa kuhakikisha kwamba kila mtu anayelipa kodi asikwepe. Hiyo nimeipenda, huo ni mfumo mzuri wa kuhakikisha kwamba kila mtu analipa kodi, hiyo ni njia mojawapo. Hata hivyo, lazima tuhakikishe kwamba wale walipa kodi, tunajenga urafiki nao, tunawapa elimu, ili kila mmoja nayelipa kodi asione kama adhabu.

Mheshimiwa Spika, kuna masuala ya fedha zile zinazopelekwa kwenye Halmashauri za maendeleo. Naishauri Serikali kwa sababu wanapeleka quarterly, sijajua system ya kupeleka, lakini fedha ziende kwa muda unaotakiwa, on time. Unaweza ukaona Mkandarasi ameingia mkataba labda wa mwaka mmoja. Usipopeleka fedha on time kama mkataba unavyosema, matokeo yake ukichelewesha fedha, inatokea Mkandarasi baadaye anaanza kuidai Serikali, baadaye ule mradi bei inaongezeka, Serikali inaanza kulipa riba.

Mheshimiwa Spika, mradi wa shilingi bilioni moja baadaye inakuja kusomeka hata shilingi bilioni tano. Kwa hiyo, naiomba Serikali ipeleke fedha kwenye miradi mikubwa, kwenye Halmashauri kwa muda uliopangwa. Hii itasaidia sana kuhakikisha miradi ile inakwisha on time.

Mheshimiwa Spika, suala lingine nataka niipongeze Serikali kwenye point moja. Serikali kufikiri miradi mikubwa ya kimaendeleo ndani ya nchi yetu ndicho kinachotakiwa. Hatuwezi kuwa tunafikiri miradi midogo midogo tu halafu tunasema nchi itafikia uchumi wa kati, haiwezekani hata siku moja. Lazima ifikiri miradi mikubwa ambayo inajenga uchumi ndani ya nchi yetu. Kwa mfano, ule mradi wa umeme wa Rufiji ni mradi ambao utatutoa katika hali ya umaskini. Kwa sababu ule umeme tunaweza kuuza hata nje.

Mheshimiwa Spika, kwa mfano, Malawi watanunua, Zambia watanunua na nchi nyingine za East Africa wanaweza wakanunua umeme kutoka pale. Ndiyo nchi yetu itapata fedha za kigeni, ndiyo tutafikia uchumi wa kati. Ukisema kwamba unataka kufikia uchumi wa kati, wewe una plan kulimalima mboga, bustani na kadhalika, uchumi wa kati utaufikia wapi? Lazima tuwe na miradi ya kimkakati ambayo inaleta uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, point nyingine ambayo nimeiona, Serikali kufikiria kujenga reli, hiyo ni point kubwa ana katika nchi zinazoendelea. Hata ukienda Ulaya utakuta kuna reli zimejengwa standard. Kwa mfano, sasa hivi kuna standard gauge, ni kitu cha msingi sana. Kwa hiyo, nataka niwaambie, kama tuna-plan uchumi, lazima tufikiri vitu vya kiuchumi ambavyo vinaleta hela kubwa ili uchumi wa kati ufikiwe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna watu wengine wanakatisha tamaa, wanasema Serikali sijui haifanyi kazi. Sasa hivi tunaingia kwenye vitu vikubwa ambavyo ni pigo kubwa kwa uchumi ili kuinua uchumi wa nchi yetu. Tukitaka kupata fedha nyingi, lazima tufikiri vitu ambavyo vinaweza vikatuingizia. Hata wawekezaji wanapokuja, wanauliza vitu vya msingi. Kwa mfano, atauliza barabara, miundombinu ya umeme, maji, hospitali; wafanyakazi wakiugua wanatibiwa wapi? Hivyo ndivyo vitu wanavyouliza wawekezaji. Wewe huna barabara, umeme, maji wala hospitali halafu unasema unatafuta mwekezaji, utampata wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa Serikali inapobuni vitu vya msingi lazima tui-support na sisi Waheshimiwa Wabunge. Bila kui-support Serikali kwa vitu vya msingi hatutaendelea hata siku moja. Kwa hiyo, nataka nimwambie Mheshimiwa Waziri wa Fedha, akaze buti, afikiri vitu vya msingi ili nchi yetu iweze kusonga mbele. Hatuwezi kuwa tunarudi nyuma kila siku, Waheshimiwa Wabunge tunauliza maswali madogo madogo ambayo Serikali inaweza kutatua kwa muda mfupi sana. Kwa hiyo, tunafuta maswali sasa hivi.

Mheshimiwa Spika, hatupendi sisi Wabunge tukifika hapa tunauliza masuala ya maji, tunauliza kuhusu barabara ndogo ndogo, zahanati ndogo ndogo; Serikali inakuwa imeshatatua. Sasa ili kutatua lazima tujifunge mkanda. Bila kujifunga mkanda, kujibana vizuri hatuwezi kuendelea hata siku moja. Lazima Serikali ibane vizuri lakini ilete maendeleo, tuone impact. Siyo Serikali ibane halafu tuwe na njaa, hapana. Ubane vizuri, tunakula lakini tuhakikishe kila mmoja anafanya kazi kwa nafasi yake vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna suala lingine la utendaji kazi. Unaweza ukaona document moja inapelekwa kwenye ofisi, inazunguka miezi mitatu. Namwomba Mheshimiwa Waziri wa Fedha, document isizunguke. Mtu anatoka Halmashauri kule anafuatilia document hapa, inachukua siku mbili au tatu. Hii haiwezekani, unaweza ukaona gharama za ufuatiliaji wa document, inataka kukaribia mradi unaofuatiliwa. Hii inakuwa ni system mbaya sana. Kwa nini tusitafute system, mtu yuko Halmashauri kule, ana-lodge document yake mtaalam huko anasoma kwenye computer, analipa malipo, simple. Anaona hiki kipande nimeelezwa vizuri, ana
document.

Mheshimiwa Spika, mtu yuko Halmashauri kule ana- search tu document kwenye computer, mtaalam huku anasoma. Akishasoma ana-reply within the minute, yule kule atakuwa ameshaiona. Akishaiona, basi inajibiwa. Sasa mtu anaanza kufuatilia wiki moja, mbili, anafuatilia document. Hii inarudisha nyuma maendeleo. Kwa hiyo, nataka nihamasishe wafanyakazi, hasa wale wa Idara ya Fedha, kwenye hili wasimame vizuri, wasilimbikize kazi ambazo hazina msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la mwisho ni wastaafu. Kuna Mheshimiwa Mbunge aliuliza asubuhi kwamba wastaafu wao bado wanadai, wanalipwa kiasi kidogo sana. Wale wastaafu ni wa kuwaheshimu, wamefanya kazi nyingi sana mpaka sasa hivi nchi imefika hapa. Wewe mtu amestaafu, alifanya kazi nzuri, kwa nini usimlipe haki yake vizuri? Lazima tuhakikishe wale wazee ambao na wenyewe wanatuombea na sisi tufanye kazi vizuri, tuwalipe stahili zao kama inavyotakiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, haiwezekani mstaafu unamlipa Sh.50,000/=. Kama sheria inasema alipwe Sh.100,000/=, mlipe Sh.100,000/= yake. Kama inasema Sh.200,000/= mlipe Sh.200,000/= yake, sasa mzee amestaafu anafuatilia mafao kuna watu wengine hawajapata mafao mpaka leo inachukua miezi mitatu na zaidi na mtu anastaafu yuko kwenye system. Kwa nini anastaafu leo, kesho humlipi hela yake? Mtu yuko kijijini, kwa mfano yuko Mufindi, afuatilie Dodoma au Dar es Salaam wakati system inasoma. Kwa nini asilipwe on time? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naiunga mkono Serikali, naunga mkono hoja. Ahsante sana.