Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa fursa ya kuchangia.
Mheshimiwa Spika, ninapenda kupongeza hotuba nzuri sana aliyotoa Msemaji wa Kambi ya Upinzani, ambayo kusema kweli kama tuna Serikali sikivu, inapaswa itoke hapo kwamba imepata somo na iende iwatendee Watanzania haki. Imekuwa ni mazoea kuchukulia michango ya wapinzani kama mzaha, lakini mwisho wa yote tunaona dublication ya mambo yale yale ambayo tayari yamekuwa yametolewa tahadhari na upande wa Upinzani. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, akisema sasa zoezi la kubaini watumishi hewa kila mtumishi kuanzia Waziri mpaka chini hakuna shughuli nyingine ni kutafuta watendaji hewa. Tutaendesha hii Serikali kwa decree mpaka lini? Hapa ndiyo umuhimu wa instrument unapokuja.
Mheshimiwa Spika, tulikuwa Dar es Salaam katika ofisi ndogo za Bunge, wakaja wasomi ambao walikuwa wanajaribu kutupa orientation ya namna ya ku-scrutinize bajeti na namna ya kupanga bajeti, niliwauliza kitu kimoja, niliwaambia nchi hii uchumi wake unafanana na uchumi ulioanza kule kwenye nchi za Taiwani, Kuwait, Botswana, Vietnam, Rwanda, Singapore, Malaysia, Hong Kong na nchi nyingine, lakini leo hii hata Vietnam walikuja kuchukua mbegu ya korosho huku sasa hivi ni mzalishaji wa korosho dunia nzima. Nikawauliza hawa wasomi niambie muwe wakweli, hivi tatizo la mipango yenu tangu mwaka 1961 mpaka leo mwaka 2016, mipango yenu hakuna unaotekelezeka kutupa uchumi ambao ni endelevu wenye mashiko. Matatizo ni usomi wenu, vyuo mnavyosoma, walimu wanaowafundisha au matatizo ni yapi?
Mheshimiwa Spika, wale mabwana waliniambia Mheshimiwa Lwakatare wewe yaache tu hayo bwana. Lakini ninachofahamu tatizo ni mfumo, mfumo wa kiutawala hata angekuja malaika mwenye mipango mizuri ya uchumi ukamtumbukiza kwenye Chama cha Mapinduzi, wallah yote inakuwa mguu chini, mguu pande, mna matatizo! CCM ndiyo tatizo, mnawapotosha watu wa mipango yetu, mnawapotosha hata wanasheria.
Mheshimiwa Spika, najua huyu siyo Mwakyembe halali tunayemjua wa Chuo Kikuu, huyu ni wa kutengenezwa, amechongwa kutokana na mfumo uliopo, hawezi kutetea, huwezi kukurupuka, hawezi kuchomoka, hata AG hawezi, CCM is a problem, angekuwa bado babu yupo kule Loliondo tungewapeleka mkapate kikombe cha babu.(Kicheko/Makofi)
SPIKA: Mheshimiwa Lwakatare malizia.
MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Spika, Tanzania imekuwa ikiridhia mikataba na tumekuwa tunaletewa mikataba ya kuridhia na najua itaendelea kuletwa, ningeomba basi tunapoletewa mikataba, tuwe na political will, tuwe na utashi ambao ni wa dhati, na ambao unanuia kuwasaidia Watanzania pindi mikataba hiyo inaporidhiwa.
Mheshimiwa Wenje akiwa Bungeni hapa, aliitanabaisha Serikali madudu gani alikuwa anayafanya Ndugu Kabwe kule Mwanza, ninyi mkaona tu kwamba ni mchezo wa kuigiza, lakini juzi tu Makonda akampandia mtu yule yule na akalalamika kwa Rais na Rais akamfukuzia mtu kwenye jukwaa la shughuli nyingine kabisa ya kuzindua daraja. Jamani kuweni serious na hoja zinazotolewa na Upinzani.
Mheshimiwa Spika, katika mchango wangu ninaomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, msomi Mwakyembe na AG, kweli mpo pale kwa ajili ya kumsaidia Rais kama wasomi wazuri wa sheria ambao Taifa hili limewaamini mmeteuliwa kwa usomi wenu, mnakaa katika Baraza la Mawaziri kumshauri Rais kwa mambo yanayohusiana na sheria? Inapokuja kutoka kitu ambacho amekizungumza kwa kina Mheshimiwa Lissu ni aibu! Huo ndiyo ukweli maana yake kuna mtu tumbo limemletea shida barabarani akachepuka aende pembeni akaanza kujisitiri kidogo ili tumbo liwe released kidogo, sasa kwa kuwa watu wanapita anajifunika uso anafikiri hawamwoni kumbe mwili wote uko nje.
Mheshimiwa Spika, mambo haya ninaamini ukweli mnaujua, lakini pamoja na usomi wenu mnapotosha mambo maksudi kwa sababu ya hulka za kisiasa. Matokeo yake Rais mnamuweka katika matatizo makubwa, mnamweka katika tension ya ajabu, mpaka juzi, kwenye sherehe za walimu anasema anajuta kwa nini alivuta fomu, matokeo ni haya! (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa sababu kama Serikali inaendeshwa, bila instrument, Rais anajikuta maskini anafanya kila kitu. Kuagiza sukari yeye, kuipanga sukari yeye, wakati kuna Waziri mhusika wa shughuli hii, ni kwa sababu watu aliowateua wote kama yeye amejikuta katika mfumo huo, anakwenda kwa decree, ikizungumzwa majipu, kuanzia juu kwa Rais, Waziri Mkuu nani wote, majipu kila mmoja yuko kwenye majipu.
Mheshimiwa Spika, pamoja na mikataba ambayo imewahi kuridhiwa, kuna Mkataba wa nchi za SADC wa Utawala Bora na Uchaguzi wa Kidemokrasia ambao kimsingi pamoja na kusainiwa na viongozi wetu haujawahi kuletwa hapa ndani ya Bunge kuridhiwa.
Mheshimiwa Spika, ninaomba wakati Mheshimiwa Waziri na AG anatoa ufafanuzi, ni lini mnaleta mkataba huu uridhiwe? Najua hamtaki huu mkataba unayozungumzia masuala ya utawala bora na kuchungana katika demokrasia kupiga kura na uchaguzi hamtaki, ndiyo maana mwendelezo wa kuiba kura umeendelea, ndiyo maana matendo yanayofanyika Zanzibar wala hamuoni haya, mnayafanya makusudi kwa sababu ya kisingizio kwamba hamjaridhia mikataba ya namna hii. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, niwaeleze ukweli siyo kwamba Watanzania pamoja na kutowaonesha live nini tunachoongea siyo kwamba hawajui, ninawapongeza Wabunge wote ambao sasa wameamua kutafuta njia mbadala. Sasa hivi ma-group yote yanapata live, mambo yanayoendelea humu, hata CCM kuna ma-group ambayo tunaona na wao wana-post hotuba zao ili watu wajue wanasema nini, huo ndiyo unafiki uliopo humu.
Kwa hiyo, suala la kuzuia habari msifikiri kuzuia live coverage ya tv Watanzania hawapati taarifa!