Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu ambaye amenipa uzima asubuhi hii. Vilevile napenda kuwapa pole wananchi wa Buyungu kwa kuondokewa na Mbunge wao. Mwenyezi Mungu atawapa subra katika kipindi hiki kigumu walichokipata.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia sina budi kumpongeza Mheshimiwa Naibu Waziri na Naibu wake, pamoja na Watendaji wake wote kwa bidii wanayoionyesha katika sekta hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania siyo nchi maskini lakini kuna baadhi ya wananchi na hata wawekezaji wanatuongezea umaskini. Madini tuliyonayo ni ya aina mbalimbali ambazo kama zitafuatiliwa vizuri, Taifa letu lingeneemeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna baadhi ya wachimbaji hawauzi bidhaa zao katika masoko husika ila wanauza katika njia za panya. Naomba Serikali iwe madhubuti, wachimbaji wakubwa na wadogo wauze bidhaa zao katika masoko yanayotambuliwa na Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna ajali za mara kwa mara zinatokea katika migodi ikiwamo wananchi kuangukiwa na kifusi au migodi kujaa maji. Serikali ina mkakati gani kuhakikisha hali hii ya hatari haitokei mara kwa mara?

Mheshimiwa Naibu Spika, madini ya pekee ambayo hayapo nchi yoyote duniani ni tanzanite. Madini haya Wakenya huyanunua sana na kuyapeleka nje na kujifanya kuwa wao ndiyo wachimbaji wa madini haya. Naiomba Serikali itangaze madini yetu na pia iieleweshe dunia kuwa tanzanite ni madini yanayopatikana Tanzania tu, siyo nchi yoyote katika dunia hii.