Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze mchango wangu kwa kutoa pongezi kwa hotuba nzuri inayogusa maisha ya Watanzania hasa walioko kwenye sekta ya madini. Hongera sana Mheshimiwa Angellah Kairuki, Waziri wa Madini bila kuwasahau Waheshimiwa Naibu Mawaziri wote wawili na watendaji wote wa Serikali. Hotuba imewatendea haki wananchi wa Jimbo la Busanda hasa wachimbaji wadogo wa madini wa maeneo yote ya Nyarugusu, Nyamyeye, Lwamgasa, Kaseme na Magenge.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ukurasa wa 49 na 50 hotuba imeongea bayana juu ya ujenzi wa mgodi wa mfano katika eneo la Lwamgasa. Tunashukuru sana kwa hatua iliyofikia ujenzi huu.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile napongeza kwa mpango wa Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupitia upya mkataba wa ubia kati ya STAMICO na Kampuni ya TANZAM 2000. Naunga mkono sababu za Wizara kuchukua hatua maana ni kweli kabisa kampuni hii imeanza kufanya kazi kwa muda mrefu, miaka nane sasa lakini hakuna uzalishaji wowote. Jambo hili limekuwa kero kubwa kwa wananchi wa maeneo husika maana maeneo mengi ya wananchi yamechukuliwa na mpaka sasa hawajalipwa fidia. Naomba Wizara ifuatilie suala hili kwani ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.