Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa, nichukue fursa hii kumpongeza Waziri na Naibu Mawaziri kwa kazi nzuri wanayofanya. Nimechangia kwa kuongea, hata hivyo ipo hoja nyingine muhimu ambayo sikuizungumza kwa sababu ya muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, azma ya Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Jemedari Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ni kuona sekta ya madini inatoa mchango stahiki katika uchumi wa Taifa letu.

Mheshimiwa Naibu Spika, azma hii ni nzuri lakini takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa Serikali haina wathamini (Government Valuer) wa madini wa kutosha na hali hii imesababisha wawekezaji na wachimbaji wa madini kutoa takwimu za thamani ya madini kadri wanavyoona inafaa. Nashauri Serikali isomeshe wathamini wa kutosha na naomba wakati wa kuhitimisha hoja Bunge lielezwe hatua zilizochukuliwa katika suala hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja.