Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, madini ni chanzo kizuri cha mapato kwa Taifa letu. Pongezi kwa Rais Mheshimiwa John Pombe Magufuli, Mawaziri wote na Makatibu wote wa Wizara kwa kazi nzuri ya kusimamia Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nashauri Serikali kama ifuatavyo:-

(i) Ifungue Ofisi za Utafiti kila Wilaya ili kufanya utafiti maeneo yote yenye viashiria vya madini.

(ii) Vibali vitolewe kwa watu wenye mitaji ya kutosha.

(iii) Usimamizi na ufuatiliaji wa walipa kodi katika sekta ya madini uboreshwa.
(iv) Elimu kwa wachimbaji wadogo wadogo itolewe na vifaa vya kuchimbia wachimbaji wadogo wapewe.

Mheshimiwa Naibu Spika, huo ni baadhi ya ushauri wangu kwa Serikali ili madini yetu yawe na faida kwa Taifa letu. Naunga mkono hoja.