Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni ulinzi wa madini yetu. Kutokana na Serikali kuona ni vyema kulinda madini yetu kwa faida ya wananchi wa Tanzania imeweza kujenga ukuta huko Mererani. Napenda kujua, katika uchimbaji wa madini haiwezekani kutokea mtu kuruka ukuta huo huo chini kwa chini? Kuna mkakati gani wa kuhakikisha wachimbaji hao hawatokezi mbali nje ya ukuta huo? Kama ulinzi huo kwa tanzanite unafaa, je, Serikali ina mpango gani kuhusu migodi mingine ya dhahabu, kwa mfano Buzwagi na kwingineko?

Mheshimiwa Naibu Spika, madini ya ujenzi kodi zake ni za juu kiasi cha kusababisha wananchi kushindwa kugharamia ununuzi wa madini hayo kwa ajili ya ujenzi wa makazi bora na salama kwa wananchi. Napenda kuishauri Serikali kuliangalia hilo kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu madini ya Liganga na Mchuchuma, napenda kushauri Serikali kuharakisha mchakato wa uchimbaji kwani chuma au nondo tunazojengea sasa hivi siyo imara, zinatokana na vipande chakavu vinavyookotwa na kuyeyushwa, hivyo vinasababisha nyumba nyingi za kawaida kuporomoka na maghorofa pia. Naishauri Serikali kulishughulikia hili kwa ukaribu kwani nondo za nje ni ghali sana na za hapa ni dhaifu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu fidia kwa wananchi wanaopisha wawekezaji, natambua kwamba madini mengi huvumbuliwa na wananchi, hivyo badala ya kuwaondoa wazawa wangeongezewa uwezo kwa kukopeshwa vifaa vya uchimbaji ili waweze kujiongezea pato kwani wawekezaji wanapopewa uwekezaji hawataki kuwashirikisha wazawa wanawafanya vibarua na kuwanyanyasa. Niishauri Serikali iliangalie hili kwa faida ya wachimbaji wadogo wadogo kwani wanasaidia mzunguko wa fedha hapa nchini na kukuza uchumi wa nchi tofauti na wawekezaji wanatorosha fedha hii kwa manufaa ya nchi zao.