Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

Hon. Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Madini

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kutoa mchango wangu katika Wizara hii muhimu, Wizara ya Madini. Ni kweli hii Wizara ndiyo inayosimamia rasilimali zetu muhimu sana ambazo Mwenyezi Mungu ametupatia sisi kama Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuwapongeza Waziri mwenyewe na Naibu wake wawili wanafanya kazi nzuri sana. Pia nimpongeze Katibu Mkuu na uongozi mzima wa Wizara. Hawa watu nimeshuhudia mwenyewe wanafanya kazi long hours. Walinipa appointment na mkutano na wao saa 2.00, nikauliza saa 2.00 ya asubuhi wakasema hapana ni saa 2.00 usiku. Kweli tumefanya mkutano saa 2.00 usiku mpaka midnight. Nilipotoka nikawauliza walinzi hivi hawa ndiyo style yao ya kufanya kazi wakasema ndiyo na tunategemea watatoka saa mbili baadaye. Kwa kweli hiyo ni ishara nzuri, hii Wizara ni mpya, ina mambo mengi mageni, inahitaji watu wenye moyo wa aina hii, hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia hata kwenye matokeo ya Wizara, tulitegemea wangekusanya kama shilingi bilioni 194 lakini kwa miezi tisa wamekusanya shilingi bilioni 225, hilo ni ongezeko kubwa sana. Kwa miezi tisa kama ni shilingi bilioni 225, nina imani kwa mwaka mzima kama makusanyo yanaendelea evenly kwa miezi itakuwa ni shilingi bilioni 300. Hili ni ongezeko kubwa ambalo ni karibu asilimia 54, kwa kweli huu ni utendaji mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na Kamati uchambuzi wao ni mzuri sana, umesema matokeo mazuri haya yametokana kwanza na udhibiti wa utoroshaji wa madini, pia ongezeko la mrabaha na kuna 1% ya makusanyo ambayo hiyo ni kodi mpya. Nafikiri imetuletea matokeo mazuri na mimi nafikiri tukijikita katika haya machache tu, kwa vile haya ndiyo yatakuwa makusanyo yenye uhakika kwa muda mrefu yatatuletea sustainable growth kwa muda mrefu kuliko yale one off ambayo labda tunategemea tutapata makusanyo kiasi hiki hayatatusaidia. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nikubaliane na maoni ya Kamati. Kwa muda mrefu tumeona utendaji wa STAMICO si mzuri. Mimi ningeomba sana Serikali katika hizi Wizara ingeangalia majukumu yao ya kimsingi, yale ambayo ni operational wayaache. STAMICO sasa hivi inapata hasara kubwa sana, madeni ya shilingi bilioni 60 na sijaangalia balance sheet yao huko inaonesha ina shimo la kiasi gani. Sasa ukiwa na hali ya namna hiyo huna haja ya kuyalea mashirika ya aina hii. Zile shilingi bilioni 8.6 ambazo wametengewa na Wizara nafikiri Wizara ingeangalia kupeleka mahali pazuri zaidi ambapo kutaisaidia Wizara kuongeza mapato na maduhuli ya shirika hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama walivyo-recommend Kamati, nafikiri hiyo migodi ambayo ilikuwa inaendeshwa na STAMICO wapewe Watanzania wazawa, wachimbaji wadogo wadogo na wachimbaji wa kati. Nina imani kuwa Serikali itapata mapato makubwa kupitia kwa hawa kuliko tukitegemea kuendelea na STAMICO. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile naomba kuikumbusha Wizara tu, nafikiri ilikuwa ni overlook. Kuna mgodi wa Niobium kule Mbeya unaitwa Panda Hill Niobium Project. Mgodi huu thamani yake ni dola kama bilioni 6.8, project nzima na tunategemea Serikali kama ukianza utaleta kodi kama ya dola bilioni 1.4 ambazo nafikiri ni pesa nyingi mno.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa nini nimelisema hilo? Ni kwa sababu huu mgodi si wa leo ni wa siku nyingi, uligunduliwa mwaka 1953. Hii kampuni mpya imepewa license ya mgodi huu mwaka 2013 na wameshawekeza zaidi ya dola milioni 28 sasa hivi walikuwa wanajipanga kuanza. Huu mgodi ni muhimu kwa Tanzania lakini ni mgodi pekee Afrika wa Niobium, migodi ya aina hii iko mitatu duniani; migodi miwili iko Brazil na mgodi mmoja Canada. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika biashara ya madini hatuko peke yetu inategemea speed ya kuingia sokoni. Nina imani huu mgodi ukianza haraka utailetea Serikali pesa nyingi sana. Dola bilioni 1.2 si ndogo, ni nyingi, zikiongezwa kwenye mfuko wa Serikali, nafikiri itaipunguzia mzigo hata Wizara ya Fedha tunapolia maji kuna hela huku zimebaki. Kwa hiyo, naiomba Wizara iharakishe process, kwanza ukiangalia Wizara ni mpya hii inaweza kuwa project kubwa ya kwanza ya madini kwa mwaka huu ukiachilia mbali za miaka mingi za dhahabu, almasi na tanzanite.

Mheshimiwa Naibu Spika, orodha ya madini ambayo nimeikuta pale nje kwenye maonesho ni kubwa mno, ni namna gani twende haraka sokoni. Madini vilevile yanaendana na teknolojia. Tusubiria dhahabu na tanzanite lakini teknolojia iki-change unaweza kukuta yakabaki kama mawe tu tunayoangalia huko nje milimani. Kwa hiyo, naiomba sana Wizara ijitahidi kufanya haraka ili hizi rasilimali zetu tuzitumie vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana.