Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 - Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu na Watendaji wote katika Wizara hii, hongereni sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali imalize migogoro ya ardhi ya muda mrefu inayosababisha wananchi kunyanyasika na kuwa maskini. Migogoro hiyo ni kama ifuatavyo:-

(1) Migogoro kati ya Hifadhi ya Uwanda ya Akiba na Vijiji vya Ilambo, Kilangawana, Maleza, Legeza, Kapenta, Mkusi, Mpande, Kawila na Kipeta.

(2) Mgogoro mwingine ni kati ya Mwekezaji wa Shamba la Malonje na wanachi wa Kata ya Msanda Muungano; tunaomba mgogoro huo ufike mwisho.

(3) Mgogoro wa Gereza la Molo na wananchi wa Kata ya Msanda Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naunga mkono hoja.