Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Korogwe Mjini; mpango mkakati wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe ulikuwa kujenga hospitali ya wilaya na kwa taarifa tulitengewa bilioni 1.5 lakini zimeondolewa na kupewa Korogwe Vijijini. Nimeridhika na maelezo ya Waziri kwamba imefanyika kwa nia njema baada ya kuona ipo Hospitali ya Wilaya Korogwe Vijijini kwenye Kata ya Magunga iliyopo mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, niombe unapohitimisha utamke wazi ndani ya Bunge kauli ya kukabidhi hospitali hiyo ili wananchi wa Korogwe Mjini wapate kusikia mabadiliko haya na kuzipeleka fedha, bilioni 1.5, Korogwe Vijijini ili kuondoa mkanganyiko uliopo. Hata hivyo, niiombe Wizara kunipoza kwa kunisaidia kunipatia fedha kwa ajili ya ujenzi na vituo vya afya; kata zilizo mbali na mji zina shida kubwa ya huduma ya afya nazo ni Kata ya Kwamsisi yenye vijiji sita na Kata ya Mgombezi vijiji vitano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitashukuru Mheshimiwa Waziri akinisaidia ili wananchi hawa wa vijiji hivyo waweze kupata huduma nzuri.