Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kwenye Wizara ya TAMISEMI ambayo ni uti wa mgongo wa maendeleo ya nchi yetu. Maana ndio Wizara inayoratibu utendaji wa Wizara nyingine kwenye ngazi ya halmashauri na tawala za mikoa, lakini tumekuwa tukishuhudia baadhi ya utendaji usioridhisha na hivyo kukwamisha shughuli za maendeleo katika halmashauri zetu na Taifa kwa ujumla. Ni Wizara ambayo inahitaji kupewa kipaumbele na kuhakikisha bajeti tunazoziweka zinatolewa zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, je, halmashauri zetu zina rasilimali watu wenye uwezo na kazi walizopewa au wanawekwa tu kwa itikadi za vyama ili kulinda maslahi ya Chama cha Mapinduzi, Chama Tawala. Maana tumeona watendaji wengi wanakaa kwa maslahi ya Chama cha Mapinduzi na sio wananchi wote kwa ujumla bila kujali vyama vyetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukishuhudia kuporomoka kwa elimu yetu huku ikichangiwa na mambo mengi. Mojawapo ni uhaba wa madarasa, vyoo, nyumba za Walimu, maabara zisizo na vifaa vya maabara, ofisi za Walimu, kupandishwa madaraja Walimu ili waweze kuwa na motisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukisoma hotuba ya Waziri ukurasa wa 38 ameonesha kuwa tuna vyumba vya madarasa 123,044 ambapo kwa mwaka wa fedha 2,278, idadi ambayo ni ndogo sana na bado imeonesha changamoto ya upungufu wa madarasa kuwa ni 264,594. Kwa kasi hii tunahitaji miaka 116 ili kujenga hii na ikumbukwe tunavyosonga mbele population inaongezeka na idadi ya ya vyumba vilivyojengwa mwaka 2017/2018 havitajengwa kwa miaka ijayo kwa kuwa wananchi wamepunguza kasi ama wameacha kuchanga kufuatia kauli tata za viongozi. Mheshimiwa Rais alisema hamna michango mara Mawaziri wakasema ichangiwe kupitia DED. Leo hii tunaendelea kushuhudia wanafunzi wakisoma hadi 200 kwenye darasa moja, kinyume na sera ya elimu kwa darasa moja kuwa na wanafunzi 45, lakini hata idadi ya Walimu kwa wanafunzi, wanafunzi kwa kitabu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumeendelea kushuhudia jitihada za wananchi kama wale wa Jimboni kwangu Tarime Mjini wakijitolea sana kujenga madarasa na shule, lakini wanazuiliwa kuendelea kwa sababu za mgogoro wa ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana Mheshimiwa Waziri husika afike Shule ya Msingi Mturu iliyopo Uwanja wa Ndege Tarime Mjini ambao walikuwa wameshajenga madarasa sita na ofisi, lakini wamezuiliwa kwa sababu zisizo za msingi kwa sababu mmiliki wa lile eneo hana shida na ni mtu binafsi ambaye alipata eneo kinyume cha taratibu, lakini pia alishindwa kuendeleza kwa zaidi ya miaka thelathini. Tunaomba sana, tumejitahidi sana na wananchi wangu wana ari kubwa ya kujenga vyumba vya madarasa, vyoo na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tuna upungufu wa Walimu, nyumba za Walimu wanakaa mbali na wanaishi mbali na shule na wanatumia fedha zao kwa nauli na makazi, lakini wakati wa mvua wanashindwa kufika. Kingine ni motisha kwa Walimu hawa haipo kabisa, wanafundisha katika mazingira magumu sana; kutopandishwa madaraja, madeni ya likizo, nyumba za kulala, na kadhalika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa sekta ya afya tuna changamoto juu ya hospitali ya wilaya inayohudumia Wilaya tatu, Serengeti, Rorya na Tarime Halmashauri ya Wilaya, lakini unapofikia muda wa mgawo hii hospitali inakuwa treated kama hospitali ya mji inayohudumia wakazi wa Tarime Mjini tu. Mortuary yetu ni ndogo sana, Basket Fund tumepata shilingi milioni 11, wakati Kituo cha Nyarwana wanapata shilingi milioni 42. Hii si sawa na hata Waziri nilimweleza hili. Tunaomba sana watuongezee fedha pamoja na vifaa pamoja na Wauguzi. Hili ni tatizo kubwa sana na linasababisha upungufu wa dawa kwa sababu ya kupewa dawa ndogo kwa idadi ya halmashauri ya mji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, ni vituo vya afya katika mgawo wa shilingi milioni 500 sikupata, kwenye shilingi milioni 400 hatukupata, pamoja na kwamba tuliomba, hii si sawa kabisa. Tunahitaji ku-upgrade zahanati ya Magena kuwa Kituo cha Afya, Zahanati ya Gamasara kuwa Kituo cha Afya na kile kituo ambacho Kata ya Kenyamayoni wananchi wameanza kujenga, lakini hatujapata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana waangalie jiografia ya utoaji huduma, bado hizo zahanati zinatoa huduma kwa Kata za Jimbo la Rorya na Tarime Vijijini, mfano Gamasara, Nkerege inatoa huduma Kata za Tarime Vijijini.