Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Prof. Jumanne Abdallah Maghembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. PROF. JUMANNE A. MAGHEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukua fursa hii kuzipongeza sana hotuba nzuri sana zilizotolewa na Mawaziri wetu wa Nchi, Mheshimiwa Suleiman Jafo na Mheshimiwa George Huruma Mkuchika. Mawaziri hawa mahiri wanafanya kazi nzuri sana, wao pamoja na wasaidizi wao wote. Hivyo, naunga mkono hoja zao zilizo Mezani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Mwanga ina baraka ya kuwa na milima mirefu katikati ya wilaya na tambarare mbili; moja Mashariki ya Milima katika Ziwa Jipe na moja Magharibi ya Milima ulipo Mji Mkuu wa Mwanga na Bwawa la Nyumba ya Mungu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali yetu ya Wilaya iko Usangi juu kabisa milimani. Awali mwaka 1980 tulipopewa hadhi ya Wilaya ya Mwanga, kilichokuwa Kituo cha Afya Usangi kilipandishwa hadhi kuwa Hospitali ya Wilaya, lakini tangu kipandishwe hadhi, hakijafanyiwa ujenzi na ukarabati ili kifikie kiwango cha hospitali ya wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu kwa Waziri wangu Mheshimiwa Suleiman Jafo; atume timu ya wataalam wafanye mahitaji halisi ya Hospitali ya Wilaya ya Mwanga iliyopo Usangi. Baada ya assessment hiyo aiunganishe hospitali hii kwenye vituo vya afya vinavyoboreshwa na World Bank ili itengenezwe, ipanuliwe na ipatiwe vifaa stahiki kama hospitali nyingine za wilaya. Tupatiwe Madaktari na wafanyakazi stahiki ili Hospitali ya Wilaya ya Mwanga ifanye kazi kama hospitali ya wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya TAMISEMI ihakikishe kuwa viongozi wote wa Idara ya Afya (15) waliohamisha ofisi zao toka Hospitali ya Wilaya Usangi na sasa wako Ofisini kwa Mkurugenzi wa Wilaya (DED) Mjini Mwanga, warudi hospitalini wakatoe huduma ya afya kwa wananchi badala ya kuwa Makarani wa DED. Uamuzi huu ulifanywa na BMW, lakini uamuzi haujatekelezwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.