Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kwenye Wizara tajwa hapo juu. Niishauri Serikali kwamba, iachane na mradi wa Bwawa la Lukuledi na badala yake iongezee nguvu Idara ya Maji ya MANAWASA ili iweze kufikisha maji safi na salama kutoka Masasi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la elimu bure. Suala hili liangaliwe kwa umakini, elimu bure imeshindwa kuangalia suala la quality badala yake inaangalia quantity. Kuna haja gani kufurahia idadi kubwa ya wanafunzi, lakini Walimu huna?

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la vituo vya afya na zahanati. Bahati mbaya sana kumekuwa na utata mkubwa juu ya ramani, Serikali iseme wazi kabisa juu ya suala hili, wananchi wanahitaji jengo la kupatia huduma. Pale Serikali itakapopeleka pesa basi ndipo ramani hizo zitumike, wananchi hawawezi kukamilisha na kupata huduma, ndiyo mahitaji. Nishauri kwamba, ramani ziendane na mahitaji ya eneo husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na tatizo kubwa sana la madeni ya wazabuni ambao walitoa vyakula na huduma mbalimbali kwenye shule na vyuo. Watu hawa wengine mpaka wamekufa kwa pressure, tuwalipe wazabuni hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la Wilaya ya Masasi. Zimetengwa pesa shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya. Nataka kufahamu kazi hii itaanza lini na itafanyika wapi?