Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nichukue fursa hii kumpongeza Waziri wa Wizara hii na Manaibu wake kwa kazi nzuri wanayofanya. Natoa shukrani zangu kwa kazi zifuatazo:-

(1) Kutoa fedha za jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Mkalamo;

(2) Kutoa fedha za uboreshaji wa Kituo cha Afya Kinyambuli (Tshs. 400m);

(3) Ujenzi wa Shule za Msingi (Kitumbili, Senene (TBA), Kibololo (TBA), Isanzu Secondary, Iguguno High School); na

(4) Kuleta wafanyakazi wa kada ya Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunashukuru kutengwa kwa Shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya. Pamoja na pongezi hizi naishauri Serikali kuona namna ya kutanzua changamoto zifuatazo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, afya; naomba idadi ya watumishi waongezwe. Naomba Wizara isimamie kwa karibu shilingi bilioni 1.5 za Hospitali ya Wilaya, Wizara imekuwa mbali na miradi hii ambayo inagharimu pesa nyingi Serikali. Pia tunaomba ambulance.

Mheshimiwa Mwenyekiti, elimu; miundombinu ya baadhi ya shule ni hafifu na haitoshelezi, naomba zipatikane pesa kusaidia wilaya mpya ya Mkalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukaguzi; tunaomba gari la ukaguzi, kwani ufaulu wa shule za msingi umeshuka kutokana na kutokuwepo ukaguzi (both) Waratibu wa Kata pamoja na Wilaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara (TARURA); baadhi ya maeneo ambayo ni muhimu kwa uchumi wa wilaya na Taifa hayafikiki. Tunaomba fedha za barabara Msingi – Yulansoni – Lyelembo, kilometa 25.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na tunawaombea mfanye kazi yenu nzuri.