Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kuchangia katika Bunge lako Tukufu angalau kwa maandishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza natoa pongezi kwa Mheshimiwa Rais, Waziri Mkuu na Mawaziri wote kwa kazi nzuri wanayoifanya. Napenda kumpongeza Waziri Jafo na Manaibu wote wawili, Katibu Mkuu na Watendaji wote chini ya Waziri wa TAMISEMI kwa kazi nzuri wanayofanya. Naishukuru Serikali kwa miradi yote ya maendeleo iliyotolewa kwa Mkoa wetu wa Morogoro, kutokana na Morogoro Vijijini kutokuwa na hospitali ya wilaya naiomba na kuishauri Serikali yangu kupandisha Kituo cha Afya Dutumi na kuwa hospitali ya wilaya, majengo yapo, iko kwenye baadhi ya majengo ambayo yaliachwa na wafadhili bila ya kukamilika, naomba Serikali ione jinsi ya kukamilisha majengo haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba hiki Kituo cha Afya Dutumi kiangaliwe kwa namna ya pekee kwani Wauguzi na Madaktari hawatoshi. Kituo hiki kinachukua takribani kata saba, lakini kata hizi ziko mbalimbali. Kwa sababu ya kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto, nawaombea wanawake wa Morogoro Vijijini gari la wagonjwa. Wanawake hawa wanapata shida sana kwa kuletwa kwenye kituo cha afya hiki. Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI tafadhali awasaidie wanawake wajawazito na watoto na watu wengine (wagonjwa) kwa kuwapatia gari la wagonjwa katika kituo hiki cha Dutumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa kutupatia hela za baadhi ya vituo vya afya katika Mkoa wetu wa Morogoro. Ombi langu licha ya kutokuwa na hospitali ya wilaya katika Wilaya ya Morogoro Vijijini, pia hatuna hospitali za wilaya katika Wilaya ya Mvomero na Gairo, pia Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ambayo inajengwa kuwa hospitali ya wilaya bado haijakamilika. Tunaomba hospitali za Wilaya katika Wilaya hizo nilizozitaja hapo huu na pia kukamilisha ambazo bado kukamilika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Mafiga kinatoa huduma kubwa. Akinamama wajawazito na hasa wanawake wanapenda kujifungulia katika Kituo cha Afya Mafiga. Tatizo wagonjwa wajawazito hasa akinamama wanaishi katika mitaa na kata za mbali, kiasi wakati mwingine hupatwa na matatizo ya uzazi, kwani hakuna gari la wagonjwa la kuwakimbiza kwenye kituo hicho cha afya. Mheshimiwa Waziri nawaombea gari la wagonjwa wanawake hawa wenye matarajio ya kujifungua salama na kupunguza vifo vya akinamama wajawazito na watoto. Gari lililopo ni la zamani na mara kwa mara ni bovu, pia linatumika kwenye vituo vingine vya afya katika Manispaa ya Morogoro.

Mheshimiwa, Mwenyekiti, Mkoa wa Morogoro tuna upungufu wa Walimu wa shule za msingi zaidi ya ……pia tuna upungufu wa Walimu wa sayansi 641 katika shule za sekondari. Naishauri Serikali izidi kuajiri Walimu wa sayansi mpaka shule za vijijini kadri Walimu wanavyohitimu vyuo. Pia ukosefu wa Walimu, nashauri kuwepo usambazaji wa Walimu hawa wa msingi sawasawa mjini na vijijini kadri nchi yetu inavyosonga mbele kwa miradi ya kisayansi ndivyo wanasayansi wanavyohitajika. Kwa hiyo, ombi na ushauri wangu, Serikali yangu ya Awamu ya Tano iliangalie suala hili la upungufu wa Walimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombi langu lingine ni kuhusu TARURA. TARURA wawezeshwe ili barabara za Manispaa Morogoro zitengenezwe. Barabara nyingine kwa sasa zina mashimo. Je, hao TARURA mbona hawaendi speed inayotakiwa mpaka barabara za vijijini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Taifa letu na hasa katika badhi ya mikoa na hasa mikoa inayozalisha sana mazao kuna utapiamlo uliokithiri pamoja za udumavu zaidi ya asilimia 42. Pia kumezuka tatizo la utapiamlo uliopitiliza, viriba tumbo. Nashukuru kwa Serikali kwa mikakati inayoiweka kuhusu masuala ya lishe na uhakika wa chakula Tanzania, tatizo hili bado ni tete kitaifa na hasa kwenye mikoa niliyoitaja inazalisha chakula kwa wingi. Naomba Serikali ilione hili ni tatizo la wananchi wake na izidi kulifanyia kazi na kuweka mikakati ya kutokana na tatizo hili kwa makundi yote ya Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, masuala ya lishe ni mtambuka, watu wengine wanawake kwa wanaume, pia mna Wabunge wengi hawajui masuala ya lishe. Ombi langu kwa kuanzia hapa Bungeni na kushirikiana na Serikali masuala ya lishe, uhakika wa chakula yaangaliwe kwa umakini. Namna hii tutakuwa na Taifa la watu wenye afya nzuri na wachapa kazi, pia lishe nzuri, inasaidia kupunguza magonjwa yanayotokana na utapiamlo wa aina yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nashauri kuwe na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Lishe na Uhakika wa Chakula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.