Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kuleta mkakati wa kuboresha vituo vya afya. Naomba kujua awamu nyingine ya fedha hizi, Mji wa Geita utapewa? Hii inatokana na kutokuwemo katika awamu ya kwanza. Geita Mjini haina hospitali hivi sasa kwa kuwa hospitali yetu ya wilaya kwa miaka minne imebadilishwa kuwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza sana Serikali kwa kukubali kuwarejesha Watumishi wa darasa la saba kazini. Naomba sana suala hili liwe kwa watumishi wote waliokumbwa na kadhia hili ikiwa ni pamoja na Manesi, Dereva na Idara zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kukabiliana na tatizo la upungufu wa Walimu, kwa kuwa hivi sasa tunapunguza Walimu wa sekondari kwenda msingi ni vyema taratibu za kuangalia kwa makini waliokusudiwa zifuatwe kwa kuwa hivi sasa kuna kukomoana. Pia ni muhimu sana wanaohamishwa wawe ni wale wenye Diploma kwanza kuepuka kutengeneza tatizo tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ubora wa elimu, naishauri Serikali hasa kwa elimu ya Sekondari kuacha kuchukua watoto holela wa darasa la saba. Kwa mfano, mwaka 2017 iwapo uwezo wa Serikali nchi nzima ni wanafunzi 200,000 wa mwaka wa kwanza basi mwaka unaofuata Serikali ichukue kwanza 200,000 na baadaye iongeze idadi iwapo tu inazo taarifa za uwepo wa nafasi zaidi kuliko hivi sasa kuchukua kama kokolo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ajira mpya; bado hakuna uwazi wa kutosha katika mfumo wa kuchuja watahiniwa kwa kuwa hivi sasa ni rahisi sana kwa Watendaji wa Idara ya Utumishi wanaokuja mikoani kuja na watu wao.