Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. RUKIA KASSIM AHMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kuipongeza Serikali kwa jinsi wanavyojitahidi kuhakikisha kila wilaya inapata huduma stahiki kama vile elimu na afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mwalimu ni mtu ambaye inapaswa Serikali imuangalie kwa jicho la huruma sana. Mwalimu hana muda wa kufanya kazi nyingine ya kujitafutia riziki. Anafundisha darasani, wakati mwingine lina wanafunzi karibu 70 na anaporudi nyumbani hapumziki ana kazi ya kusahihisha madaftari mpaka anapomaliza keshachoka hawezi tena kufanya kazi nyingine. Hivyo basi, Mwalimu wa nchi yetu anabakia na umaskini mkubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utawala bora ni pamoja na kuheshimu kila mmoja anafanya kazi ambayo inamhusu. Nakusudia kuwa kama wewe sio kiongozi katika nafasi fulani basi huwezi kufanya kazi ile ambayo sifa yako kwa mujibu wa sheria na kanuni ya vyama vya siasa. Kuna Sheria ya Vyama vya Siasa Na. 5 ya mwaka 1992, Kifungu cha 8B(2) ni marufuku kujitambulisha kwa vyeo ambavyo sio vyako.

Mheshimiwa Spika, utawala bora ni pamoja na kuheshimina na kuhakikisha kila mmoja anafanya kazi ambayo inayomhusu. Nakusudia kuwa kama wewe sio kiongozi katika nafasi fulani, basi huwezi kufanya kazi ile ambayo siyo yako kwa mujibu wa sheria na kanuni ya vyama vya siasa. Kuna Sheria ya Vyama vya Siasa ni ya mwaka 1992 kifungu 8B(2) ni marufuku kujitambulisha kwa vyeo ambavyo siyo vyako.

Mheshimiwa Spika, tunaowaona baadhi ya watu wanasema vyama kwa nafasi ambazo siyo zao na Serikali haiwachukulii hatua stahiki. Hapa utawala bora ndiyo unakosekana. Tunaishauri Serikali, watu hawa wapo na wanajulikana wachukuliwe hatua za kisheria ili utawala bora upatikane.