Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Catherine Nyakao Ruge

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. CATHERINE N. RUGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na suala la utawala bora; naomba kutumia fursa hii kuikumbusha Serikali ya CCM misingi ya utawala bora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Serikali na taasisi za umma kutekeleza majukumu yake kwa kufuata Katiba, Sheria na taratibu zilizowekwa. Taasisi za Serikali kusimamia rasilimali za umma kwa manufaa ya wananchi, kutengeneza mfumo wa kutoa haki bila upendeleo, kulinda demokrasia, kulinda amani, kulinda haki za binadamu, uwajibikaji, uwazi, utawala wa Sheria kufuta chain of command.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, Serikali ya Awamu ya Tano imeonesha upungufu mkubwa katika kufuata misingi ya utawala bora. Kwa mfano, sasa hivi kila kiongozi anatoa matamko kuanzia Rais, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakuu wa Polisi wa Mikoa, Wakurugenzi bila kufuata misingi ya utawala bora; tena matamko mengine yamekuwa hayatekelezeki na ya kudhalilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Wakuu wa Mikoa na Wilaya wamekuwa na mamlaka makubwa mpaka kufikia kuwaweka Wabunge ndani kwa personal interest. Napenda kuishauri Serikali kuzingatia misingi ya utawala bora ili tuweze kulinda amani, demokrasia na kutoa haki sawa kwa kila mwananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kuchangia hotuba ya TAMISEMI; nimesoma hotuba ya TAMISEMI na nimegundua upungufu katika sehemu tatu. Moja, hotuba hii haina jicho la kijinsia; pili, haina mnyambulisho wa data; tatu, haina consistency.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda ukurasa wa 12 wa hotuba hii inaonesha asilimia 49 ya pesa za maendeleo hazikwenda kwenye halmashauri. Napenda Waziri atakapokuja ku-wind up atueleze ni kwa nini pesa hizi hazikwenda wakati Serikali imekusanya mapato kwa asilimia 86.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda pia kuzungumzia suala la vijana na wanawake. Taarifa ya ajira kutoka National Bureau of Statistics inaonesha jumla ya watu 2,334,969 na youth employment rate is 13.7 percent kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2015/2016. Naomba kufahamu mkakati wa Serikali juu ya ajira kwa vijana. Serikali inasema vijana wajiajiri wakati hawana mitaji watajiajiri vipi? Mapato ya ndani ya halmashauri hayatoshi kuwapa vijana asilimia tano na wanawake asilimia tano. Ukiangalia ukurasa wa 23 wa hotuba ya TAMISEMI ni asilimia 15 tu ya vikundi vya vijana na wanawake waliweza kupata fedha hizo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri wangu; Serikali iwa- guarantee vijana ambao wamemaliza vyuo vikuu ili waweze kupata mikopo kutoka taasisi za fedha ili waweze kujiajiri kwa kutumia vyeti vyao.