Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. BERNADETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpongeza Waziri kwa kuwasilisha vizuri hotuba hii na kazi nzuri wanayofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali kwa kuwa wasikivu. Waziri ametoa tamko Bungeni kuwa watumishi walioajiriwa kabla ya mwaka 2004, waliosimamishwa kazi sababu walikuwa na cheti cha darasa la saba hawana cha kidato cha nne warudishwe kazini. Nawapongeza Serikali kwa kuwarudisha kazini na kuwalipa mishahara yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo sasa ni wale walioajiriwa tangu mwaka 2004 na kuendelea wamesimamishwa, hawa hatma yao ni nini? Hawa ni watu wa hali za chini na kawaida, ni maskini, ni wanyonge, wametumikia nchi hii kwa zaidi ya miaka 10, je, Serikali itawasaidiaje kwa sababu hawa wa darasa la saba hawaajiriki tena. Fedha zao zilikatwa zikawekwa kwenye Mifuko ya Hifadhi za Jamii mfano NSSF, uwezekano wa kuajiriwa haupo sababu ni darasa la saba. Naomba ili kuwasaidia warudishiwe michango yao iliyo kwenye hii mifuko, Serikali inasemaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.
Ahsante.