Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda kuchangia kuhusu wafanyakazi wanaolipwa kwa kifungu 5000 (mapato ya ndani) katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga (Mafinga TC). Kufuatia kugawanywa kwa Halmashauri ya Mufindi na kupatikana Mafinga TC, wafanyakazi wengi wanaolipwa kwa mapato ya ndani walipelekwa Mafinga TC. Mafinga TC tunatumia around Sh.12,000,000 kila mwezi kulipa wafanyakazi hao ambao miongoni mwao wako ngazi ya uandamizi. Hali hii imekuwa na changamoto kubwa mbili kwa Halmashauri ya Mafinga Mji na kwa watumishi.

(i) Kwa halmashauri, tunajikuta tunatumia kiasi cha Sh.120,000,000 kwa mwaka kulipa mishahara ya watumishi. Kama watumishi hao wataingizwa katika mfumo wa Hazina, fedha hiyo itasaidia katika shughuli za maendeleo.

(ii) Kwa watumishi, kutokana na mishahara yao kutegemea makusanyo ya ndani, wafanyakazi hawa wamekuwa wakichelewa kupata mishahara, hali hii imekuwa ikiathiri hata huduma zao za afya. Mara mbili mfanyakazi ameshindwa kupata huduma Hospitali ya Ikonde kwa sababu ilionekana kuwa michango ya bima ya afya haijawasilishwa. Baadhi yao waliokopa benki, marejesho yanacheleweshwa na kujikuta wakipigwa penati. Hali hii inawaathiri sana wafanyakazi hao, wanajihisi ni second citizen.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali itusaidie kuwaingiza watumishi hawa ili walipwe na Serikali Kuu. Yawezekana ni jambo ambalo lipo katika halmashauri nyingi, lakini naomba Mafinga TC tutazamwe kwa macho mawili. Kuna hoja kuwa Mafinga tuna mapato ya Msitu wa Sao Hill, lakini ukweli ni kuwa beneficiary wa Msitu wa Sao Hill ni Mufindi DC, hivyo, naomba mtusaidie.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ni kuhusu kupandishwa madaraja/vyeo watumishi. Kuna manung’uniko makubwa sana kuhusu kubadilishwa kwa tarehe za wao kupanda vyeo, baadhi yao walipanda mwaka 2015. Ni kweli kuwa maelekezo ya kuhakiki vyeti na suala zima la watumishi hewa, suala hili lilisitishwa, aidha, mishahara yao haikubadilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, waraka ulitoka kuwa barua au kupanda vyeo kusomeke kuanzia 1/11/2017 na wengine kuanzia tarehe 1/4/2018. Nafahamu yawezekana kutokana na suala la kibajeti Serikali inaona kuwa itakuwa na mzigo mkubwa wa kulipa malimbikizo. Hali hii inaweza kushusha morali ya watumishi. Kama Serikali haitawalipa malimbikizo ni miaka almost mitatu itapotea na hivyo kuathiri hata pension zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hekaheka nyingi za kuweka sawa masuala ya watumishi wa umma, nashauri na kupendekeza kuwa watumishi hao waangaliwe upya na vyeo vyao vizingatie tarehe ya awali ya kupanda vyeo. Ahsante.