Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia hoja zifuatazo kwa Wizara mbili zilizowasilishwa Bungeni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikijinasibu kuwa inashughulikia rushwa. Manispaa ya Morogoro ujenzi wa barabara ya kilometa nne kutoka Kichangani – Tubuyu. Barabara hii imejengwa kwa fedha za mkopo wa World Bank ambayo tunatarajia fedha hizo zitalipwa na kodi za jasho la Watanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha kushangaza barabara hiyo kilometa moja imejengwa kwa kiasi cha shilingi bilioni 3.4 kwa kilomita nne, hivyo imegharimu 13.8 bilioni, wakati haina mto, korongo wala milima imenyooka kama rula.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya Madiwani walihoji matumizi mabaya ya barabara hiyo kwa fedha, matokeo yake rushwa za wazi zilianza kutolewa kwa Madiwani wa CHADEMA na CCM. Kuna kigugumizi gani katika kufuatilia ubadhirifu wa fedha waziwazi zilizotafunwa na wakandarasi wakishirikiana na watumishi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja hii niliileta Bungeni nikamuuliza swali Waziri wa TAMISEMI ambaye wakati huo alikuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI Mheshimiwa Jafo, Mheshimiwa Jafo mwaka jana alienda kuitembelea barabara hiyo na akaunda Kamati ya kufuatilia baada ya kutoridhika na pesa zilizotumika ikilinganishwa na thamani ya barabara yenyewe lakini cha kushangaza hadi sasa hakuna kitu kinachoendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ufisadi huu wa wazi wazi Serikali imeuona lakini hakuna hatua zozote zimechukuliwa. TAKUKURU wamehoji Madiwani wa Manispaa wamekiri kupokea rushwa kwa nini Serikali haichukui hatua?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wamevunja nyumba za wananchi Mtaa wa CCT Mkundi kwa madai ya kujenga kwenye hifadhi ya lami lakini wananchi hawa wana hati halali za viwanja pamoja na vibali vya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika Serikali ilipeleka huduma za maji, umeme, ujenzi wa shule, Ofisi ya Mtendaji wa Kata na wana vitambulisho vya makazi na walipiga kura. Sasa hivi Serikali inawahamishia wananchi wa Mtaa wa CCT katika Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero. Haki haikutendeka kwa wananchi na imesababisha usumbufu na taharuki.