Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nawapa pole viongozi wa CHADEMA zaidi ya 15 wakiwemo Wabunge wa Upinzani ambao wana kesi katika Mahakama zetu, kesi za kisiasa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpe pole na Mungu amponye Mheshimiwa Lissu ili aweze kurudi aendelee na majukumu yake. Pamoja na kwamba mpaka sasa ripoti ya tukio la Mheshimiwa Lissu Bunge halijaleta ripoti hii na malalamiko mengi yaliyopo nchini. Mfano, kupotea Ben Saanane na Mwandishi Azroy, kifo cha Aquilina, vifo vya watoto Kibiti na Tundu Lissu kupigwa risasi. Ni kwa nini Serikali inatoa majibu tata na kuacha wananchi wakibaki na sintofahamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Serikali kuendelea kukaa kimya inapelekea wananchi waamini kwamba Serikali hii ni Serikali isiyojali wanyonge na Serikali inayowaonea watu bila kuwasaidia wananchi na matatizo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uhuru wa kufanya mikutano ya hadhara. Serikali ina hofu gani kuzuia mikutano ya siasa. Hii inaonesha kuwa katika Serikali hii ya Awamu ya Tano inaogopa kufichuliwa udhaifu uliopo ndio maana inaogopa ukweli.