Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuishauri Serikali kuharakisha urasimishaji wa hati za maeneo ya wananchi ili kuwezesha kupata mikopo kiurahisi na kupunguza umaskini. Nashauri zoezi la utoaji huduma kwa wahitaji kupitia TASAF kuchunguzwa, kwani wataalam wengi hawana weledi katika utendaji. Watendaji wamesababisha misaada hiyo kuwaacha walengwa na kupewa wenye uwezo na hivyo zoezi hilo kukosa maana ya kuanzishwa kwake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kuwalipa watumishi waliostaafu stahiki zao kwani ajira inapokoma ni dhahiri mtumishi anakuwa na mipango yake ya kujikimu baada ya kustaafu. Hivyo, nishauri Serikali kuliona hilo kwani inaharibu taswira ya utumishi wa umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishauri Serikali kufungua milango ya uhamisho kwa watumishi wale ambao wanahitaji kuungana na familia pale mwenza mmoja anapohamishwa hivyo kuleta usumbufu kwa watoto ambao hawaelewi wabaki na mzazi yupi. Kumekuwa na usumbufu mkubwa kwa mtumishi anapotaka kuhama, kuambiwa atafute mtu wa kubadilishana naye, je asipopatikana huyo mtu hivyo mtumishi anakosa haki ya kuhama? Je, huo ni wajibu wa mtumishi au Serikali kutafuta jinsi ya kujua ni wapi mtumishi huyo atapangwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia watumishi wapate kozi fupi za kujengewa uwezo ili wapate uelewa mpana katika sehemu zao za kazi.