Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Hon. Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka wa Fedha 2018/2019 – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa na Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, naomba nami nichangie haraka. Nilikuwa napitia jedwali la TAMISEMI katika pesa za ujenzi wa hospitali za Wilaya nimeshangaa sana kuona Manispaa ya Tabora haijawekewa hata shilingi moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama utakumbuka Mheshimiwa Waziri Madiwani kutoka Manispaa ya Tabora tulikuja ofisini kwake, moja kati ya maombi ambayo tulimwomba ni kuweza kutusaidia Hospitali ya Wilaya ijengwe. Nafahamu kwa nini amefanya hivi, akiamini kwamba Hospitali ya Kitete itaweza kutusaidia watu wa Manispaa ya Tabora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali ya Kitete ina matatizo mengi, hospitali ya Kitete ina changamoto nyingi. Kwanza haina Madaktari, mpaka sasa kati ya Madaktari tisa bingwa wanaotakiwa kuna Daktari mmoja peke yake. Ukimuuliza Daktari huyu ubingwa wake amesomea kwenye nini wala haelewi, lakini ni Daktari Bingwa peke yake ndiye aliyepo katika hospitali ya Kitete. Leo hospitali ya Kitete ni hospitali ya Rufaa, kwa hiyo wale wananchi wote wa Manispaa ya Tabora wanapokuwa wana matatizo wanakimbilia hospitali ya Kitete, imekuwa na msongamano mkubwa kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha ajabu pale kuna majengo ya chuo ambayo sasa yameanza kuchakaa, hebu atueleze atakapokuja ku-wind up ni lini yale majengo yatamaliziwa na watafungua kile chuo ili tuweze kuondokana na upungufu wa Madaktari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali hiyo ya Kitete ina jengo la ICU lakini hakuna mashine hata moja katika jengo hilo na ndiyo hospitali ya Rufaa, leo bado mnatuona kwamba watu wa Tabora hatuhitaji kupewa hospitali ya Wilaya tuendelee kutumia hospitali ambayo ina matatizo chungu nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hospitali ya Kitete wodi ya wazazi ni ndogo sana, kwa siku katika Hospitali ya Kitete inapokea akinamama 15 mpaka 17 wanaotaka kujifungua kwa kawaida, inapokea akinamama watano mpaka saba wanaokwenda kujifungua kwa operesheni, wodi ile haitoshi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunayo nafasi kubwa kwenye ile hospitali, tunaomba kwa sababu ni hospitali ya Rufaa lijengwe jengo kama lililopo Hospitali ya Mwananyamala ama lililopo pale Sinza ili liweze kusaidia akinamama hawa kuondokana na matatizo ya kuwa na msongamano wa hali ya juu. Wanawake pale wanalala chini, wanawake pale wanaenda kujifungua wanalala wawili na watoto wao, kwa kweli haiwezekani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungeomba badala ya kutubana, kutegemea hospitali ya Rufaa ambayo ina msongamano mkubwa, tunaomba nasi basi tutengewe fedha ili tuweze kujenga hospitali yetu ya Wilaya. Tunashukuru kwa pesa katika Wilaya ya Uyui na Wilaya ya Sikonge, tunaomba na Tabora Manispaa itengewe fedha ili tupate hospitali yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunahitaji pia standby jenereta; katika Hospitali ya Rufaa ya Kitete hakuna jenereta, hata kama mtu anafanyiwa upasuaji kama umeme unakatika na umeme wenyewe huu, haiwezekani na watu wanaweza wakafia na wengi wanakufa wakiwa wanafanyiwa operation kwa sababu umeme unakatika mara kwa mara. Tunaomba wamtusaidie hospitali ile angalau basi iwekewe standby generator ili kuokoa maisha ya Watanzania walio wengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie suala la elimu. Shule za zamani tunashukuru tumepiga kelele angalau zimefanyiwa matengenezo. Shule ya Tabora Girls, Shule ya Tabora Boys na Shule ya Mirambo, tunawashukuru sana kwa hilo lakini bado zipo changamoto. Ningeomba sana Mheshimiwa Waziri Tabora Girls wasichana wanalala chini kwa sababu vitanda vingi pale vimevunjika, wanaomba wasaidiwe angalau vile vitanda viweze kutengenezwa waweze kulala kwa nafasi. Pia Tabora Girls ina uhaba wa Walimu. Kwa hiyo, tunaomba watusaidie Ofisi ya Utumishi waajiri Walimu, wale waliowandoa wasiokuwa na vyeti waturudishi Walimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tunaomba na bado tutaendelea kuomba kama wanawake angalau kwenye shule kama hizi, basi wanawake wale mabinti waweze kusaidiwa taulo, kwa sababu waliopo katika shule hizi wengi ni wale ambao wazazi wao hawana uwezo, kwa wale ambao wazazi wao hawana uwezo waweze kusaidiwa taulo ili angalau wanapofika kwenye kipindi chao cha hedhi waweze kuwa salama na waweze kuendelea na masomo.