Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu. Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Kilwa wapo vijana wawili wamechukuliwa na vyombo vya dola (Polisi), vijana hao ni Ndugu Ali Mohamed Shari na Ndugu Yusufu Kiduka. Vijana hawa tangu wamechukuliwa hawajulikani walipo, wazee wao wananiulizia na wamenituma wanataka kujua wapo wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, walikamatwa na Polisi tunahitaji wapelekwe Mahakamani. Pamoja na hawa waliokamatwa Kilwa, pia wapo wananchi wamekamatwa Wilaya ya Rufiji, pia nao hawajapelekwa Mahakamani na jamaa zao hawajui walipo, wengi wao ni viongozi wa Serikali na Chama cha Wananchi ambao ni hawa wafuatao:-

Ndugu Ziada Nongwa, Diwani Viti Maalum; Ndugu Moshi Machela, Mwenyekiti wa Kitongoji; Ndugu Jumanne Kilumike, Mwenyekiti Ikwiriri; Ndugu Kisinga Athumani, Mwenyekiti Kijiji na Katibu wa Vijana CUF; Ndugu Kazi Mtoteka, Mwenyekiti wa Kijiji; Ndugu Mtuku Astera, Katibu CUF, Kata Ikwiriri; Ndugu Khamisi Nyumba na mwanawe Katibu CUF, Wilaya ya Rufiji; Ndugu Blasil Linyago na Mkewe; Ndugu Baruti Kongoi, Ikwiriri; Ndugu Konjoma Mlanzi, Mfanyabiashara, Ikwiriri; Ndugu Abdala Mkuu na Ndugu Salum Mkuu, Mwenyekiti Mstaafu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri hawa wote wamekamatwa, lakini hawajapelekwa Mahakamani kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu. Mheshimiwa Waziri nahitaji kujua wapo wapi na lini watafikishwa Mahakamani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri katika majumuisho yako napenda kupata majibu. Mheshimiwa Waziri katika Wilaya ya Kilwa, Kijiji cha Chumo, siku ya Ijumaa tarehe 21 Julai, 2017, Polisi walivamia msikiti wa Ali Mchumo usiku na kushambulia kwa risasi za moto na kusababisha kifo cha muumini Ismaili Bweta na kupoteza jicho kwa muumini Mbaraka Saburi. Je, Serikali inasema nini kuhusu wahanga hawa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza shukrani.
Naomba kuwasilisha.