Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, natanguliza shukrani zangu za dhati kwa Wizara hii, kwa kazi nzuri inayofanywa na watumishi wa Wizara hii kuanzia Waziri, Naibu Waziri, Katibu Mkuu, AGP na watumishi wote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wizara iwe inakumbuka ahadi zake Budget 2015/2016, 2016/2017, niliomba fedha za ujenzi wa vituo vya polisi, Nyamuswa na Mugeta.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ya makazi ya nyumba za askari polisi ni mbaya sana, tunaomba suala hili Serikali ilione na kulifanyia kazi haraka. Jimbo la Bunda ni wakulima wa pamba, naomba Kituo cha Polisi, Kata ya Haonyori, ambayo wakazi wake ni wakulima wazuri wa pamba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba askari watumie weledi wao wakati wa kufanya operation. Tarehe 12 Novemba, 2018, kulitokea mauaji ya watu wawili katika mapigano ya vijiji viwili, Remung’orori na Mekomariro lakini askari waliokuja kufanya operation katika tukio hili, walichukua bidhaa zote madukani, walikunywa bia zote katika baa na kupekua masanduku na kuchukua fedha clip zipo na tukio hili siyo zuri, askari watumie weledi.