Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Pili, naomba kuchangia maeneo yafuatayo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa nyumba za Polisi, kwa kuwa nyumba wanazoishi askari polisi zina hali mbaya sana mbovu na hazina hadhi ya kuishi askari polisi na kwa kuwa Serikali ina mpango wa kujenga nyumba 400, kila Mkoa na kwa kuwa Dodoma ni Makao Makuu ya Nchi, je, ujenzi wa nyumba hizo utaanza lini ikiwemo Wilaya ya Mpwapwa ambapo nyumba za Askari Polisi ni mbovu zimechakaa na hazifai kuishi askari ikiwemo jengo la kituo cha polisi ambapo wakati wa kipindi cha mvua paa linavuja sana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Gereza la Mpwapwa halina ukuta wa ngome na hivi sasa maaskari magereza wanajitolea kujenga ukuta (ngome) na mimi kama Mbunge nilichangia mifuko 25 ya cement. Je, Serikali imetenga shilingi ngapi kwa ajili ya ujenzi wa ngome ya gereza la Mpwapwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Uhamiaji, kwa kuwa passport zinabadilishwa na kwa kuwa sisi Waheshimiwa Wabunge hatujabadilishiwa, je, Idara ya Uhamiaji itabadilisha lini passport za Waheshimiwa Wabunge na hizi za sasa zinaruhusiwa kutumika kwa muda gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Zimamoto, kwa kuwa magari ya zimamoto katika miji mingi ni machache sana na matukio ya moto ni mengi hapa nchini. Je, ni Serikali itanunua magari ya kutosha kuzimia moto katika miji yote Tanzania ikiwemo Makao Makuu ya Nchi Dodoma. Je, Serikali haioni kwamba ipo haja Serikali kununua gari moja la kuzimia moto kila Wilaya?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja hii kwa asilimia mia moja.