Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Serikali na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa jitihada mbalimbali za kuwezesha Wizara na Taasisi zake zote zinazotekeleza majukumu yake pamoja na changamoto zilizopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali ione namna ya kuongeza fedha katika Wizara na Taasisi zake ili majukumu ya kazi zao yatekelezwe kwa ufanisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji lipatiwe zana na vitendea kazi vya kisasa ili Jeshi hili liweze kukabiliana na majanga, maafa na matukio mbalimbali yanayotokea nchini yanayohitaji uokoaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Jeshi la Polisi lipatiwe vitendea kazi ili liweze kukabiliana na uhalifu na ulinzi wa nchi, wananchi na mali zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri kwamba wahamiaji haramu wakikamatwa warudishwe kwao au waachiwe waendelee na safari yao nje ya nchi yetu kuepusha mlundikano wa mahabusu katika Magereza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Askari yeyote ambaye anakiuka maadili ya kazi yake kwa kuchafua Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji na kadhalika, wachukuliwe hatua za kinidhamu ili kulinda heshima ya majeshi yetu hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, nawatakia utekelezaji mwema. Naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.