Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Desderius John Mipata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. DESDERIUS J. MIPATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja kwa mchango ufuatao:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza Jeshi la Polisi kwa kazi nzuri ya kulinda amani na usalama. Nashauri pamoja na kazi nzuri inayofanywa, Polisi wasichukue sheria mkononi mwao kama vile anapotokea mhalifu badala ya kumpeleka Mahakamani hupigwa na kufia mikononi mwa Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vitendo hivi vimeshamiri na pia imetokea kwenye Jimbo langu Kijiji cha Kilambo, Kata ya Kala ambapo mtuhumiwa wa wizi kijana alipigwa na Polisi na akapoteza maisha. Haya yanatokea sehemu mbalimbali nchini na yanalalamikiwa sana. Nashauri Polisi wasitumie nguvu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yapo malalamiko kuwa watu wanapotea, wanatekwa na wengine hawajapatikana. Vitendo kama hivi siyo utamaduni wa Tanzania. Tanzania irejeshe taswira nzuri iliyojengeka miaka ya matumizi ya vyombo vya kutafsiri sheria, yaani Mahakama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napongeza kazi nzuri ya kuendelea kulinda raia na mali zao ambapo mpaka sasa raia na mali zao wapo salama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri Waziri anipe bati kwa ajili ya kuezeka kwenye vituo vya polisi vilivyojengwa na wananchi vya Tarafa ya Kate, Mji Mdogo wa Kate na Tarafa ya Wampembe, Kata ya Kala na Kijiji cha Mpasa wananchi wasikate tamaa maana wao wameona umuhimu wa kuwa na huduma ya Polisi lakini wameshindwa kuezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Polisi Nkasi hawana nyumba za kutosha. Pia Polisi Nkasi hawapati fedha ya mafuta na badala yake wanakuwa wanaomba omba wakipata dharura. Naomba Polisi Nkasi waongezewe gari ili ipelekwe Wampembe kwani ni mbali na Makao Makuu na ni mpakani.