Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Khalifa Mohammed Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Mtambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. KHALIFA MOHAMED ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuzungumzia changamoto za kiutendaji Polisi - Kaskazini Pemba kuhusu mafuta, vipuri na umeme. Polisi wetu wanapatiwa lita 900 badala ya mahitaji ya lita 3,000. Vilainishi (lubricants) na spare wanapewa shilingi milioni 1.5 badala ya shilingi milioni 4.5 ya mahitaji. Umeme wanapatiwa Sh.400,000 kwa mwezi wakati mahitaji ni shilingi milioni 2.4 kwa mwezi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jengo la Maofisa wa Polisi Wilaya ya Wete linavuja, jengo la utawala la Polisi Kaskazini Pemba ni chakavu, jengo la Askari Polisi - Konde ni chakavu, Bweni la Askari wetu ni bovu, nyumba za Askari FFU ni chakavu zinahitaji ukarabati wa miundombinu ya majitaka na makaro na kuezekwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni Maafisa na Askari kutolipwa mishahara kulingana na vyeo vyao kwa muda mrefu, wastaafu kuchelewa kulipwa mafao yao bila ya sababu ya msingi, kutolipwa posho mbalimbali kama za nyumba, upelelezi, nguo na malipo ya uhamisho huchelewa sana. Vile vile kuna uchache wa Askari ambapo Askari wengi wanahamishwa na kustaafu bila ya kupatiwa mbadala.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Ofisi ya Teknohama Mkoa ipatiwe vifaa vya kisasa pamoja na computer.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri asimamie upatikanaji wa stahiki za Idara ya Uhamiaji Makao Makuu kama vile vinywaji.