Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naunga mkono hoja ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni. Napenda kupata majibu ya Serikali, je, unawezaje kuzalisha vyakula kwa wingi na kuingiza fedha kwenye miradi ya kilimo bila hali hiyo kwenda sambamba na uboreshaji wa miundombinu kama barabara na kadhalika. Ni lini Wizara hii itashirikiana na Wizara ya Ujenzi ili kuleta matokeo mazuri kwa wananchi hasa wa Jimbo la Mlimba.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujua Serikali inachukua hatua gani kwa Wawekezaji wa KPL wanaolima eneo dogo la shamba na maeneo mengine wanawakodisha wafugaji na wakulima. Pia kuhusu uhamishaji wa ubia na mali zilizopo na hadi sasa mali hizo hazipo, je zimepelekwa wapi?
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kupata majibu ya Serikali ni lini itamaliza migogoro iliyopo kwenye maeneo ya uwekezaji mfano Rupia, Ngalimila, ambako yameonyeshwa kwenye hotuba ya Wizara.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni lini Serikali itawasikiliza wafugaji waliopo Jimbo la Mlimba na kuwapa elimu ya ufugaji wa kisasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Jimbo la Mlimba lina mazao mengi ya biashara kama cocoa, ufuta, ndizi, mpunga, mahindi na kadhalika, ni lini Serikali itawapa elimu wakulima hao pia kuanzisha dirisha la mkopo kwa wakulima ili wakope na wasaidiwe utaalam wa kuboresha kilimo cha mazao hayo?
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kaya takribani 400 zenye hekari karibuni elfu moja zimeathirika na madawa ya Mwekezaji KPL, (kwa hisia zao) na Mheshimiwa Waziri ulifika na kuwapa matumaini utapeleka majibu ndani ya siku ya 21 tangu tarehe 4/5/2016 na hadi leo tarehe 4/5/2016 na hakuna majibu na wananchi hawatavuna kabisa, msimu wa kilimo umepita. Je, Serikali iko tayari sasa kupata idadi kamili ya watu walioathirika na kupeleka chakula cha msaada kwani hali ya chakula ni mbaya? Ahsante