Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

Hon. Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 – Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza nishukuru na kupongeza Hotuba ya Waziri kwa maneno mazuri na jinsi ambavyo amejipanga na timu yake kwa ajili ya kufanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Kiteto tuna Kituo cha Polisi ambacho kimechakaa na ni muda mrefu, nataka niombe Waziri mwenye dhamana atakapopata muda basi tutembelee pale, tumpitie RPC wetu, twende pale tufanye kikao tuzungumze, tuone lile jambo tunaliwekaje, yawezekana tukafanya marekebisho ya muda wakati tunafikiria kufanya marekebisho ya muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema jambo moja la magereza. Niombe Kamishna wa Magereza, haya magereza mengi yangefanya shughuli za kilimo yangeweza kusaidia sana. Pale Kitengule Karagwe lile gereza kule Kagera kuna mvua ambazo ni za misimu yote miwili. Ningeomba hili gereza liweze kutumika kwa ajili ya kilimo cha kuzalisha mbegu kwa sababu wana mashamba makubwa na ni mazuri na hakuna contamination ya majirani kwa ajili ya kufanya ile pollution ya mbegu ili iweze kutoka mbegu nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe huyu Kamishna wa Magereza azungumze na watu wa ASA hiki kitengo chetu cha mbegu na mimi nitakwenda kama Mjumbe wa Kamati ya Kilimo kama kushauri kwa gharama zangu na timu ya kule ambayo ni ya kilimo ya magereza ili tuweze kukaa chini tuone tuainishe namna gani, hawa watu wanaweza kuzalisha mbegu kwa ajili ya Serikali na wananchi wetu na kwa ajili ya Serikali ili tuweze kupata mapato. Hata hivyo, gereza litapata faida kubwa sana kwa kuzalisha mbegu badala ya kuzalisha yale mahindi 60,000 au 70,000 ambao kwa sasa yawezekana haiwalipi kama magereza pia hailipi kama Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizungumzie juu ya suala la Uhamiaji. Uhamiaji wanafanya kazi nzuri na kubwa sana lakini shida kubwa wanayoipata, mimi naona kwenye bajeti hapa Mheshimiwa Waziri atakapokuja aniambie maana nimekusudia kushika shilingi. Hizi pesa alizowapangia ni pesa ndogo sana, hawa watu hawawezi kufanya kazi kwa kiwango ambacho wanafanya na shughuli nyingi walizonazo ambazo ni ku-contol mipaka yetu yote, kulinda ndani, kukamata wahalifu na wahamiaji haramu wakaweza kufanya hili jambo. Kwa bajeti hii hakuna kitu kitakachoendelea unless in between tuangalie ni namna gani Serikali inaweza kuongezea hawa watu bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naweza kutoa mfano mpakani tunao watu wengi ambao wanaingia, hizi nchi jirani ambazo tumepakana nazo kwa kuwa Tanzania tumepakana na nchi nyingi. Kuna malalamiko mengi ambayo watu wanaingia na kumetokea watu; Mheshimiwa Waziri mwenyewe anakumbuka alienda kuchoma silaha pale Kigoma, watu wameingiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, hawa watu wanapoingiza hizi silaha wanakutana na raia wetu wanakaa nao, wanazungumza, wanakula nao, wanahifadhi hizo silaha, leo uhamiaji wanapokwenda kukamata wananchi na baadhi ya Wabunge wanalalamika kwamba wale watu wamewaonea, its quite impossible, lazima Uhamiaji wachape kazi na waendelee wasirudi nyuma na wasikatishwe tamaa na wasonge mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kushauri juu ya jambo la Uhamiaji. Kuna haja ya Uhamiaji kukaa na Wabunge wa Mikoa ya mipakani, Kagera, Kigoma, Tunduma na kwingineko ili kunapotokea zile complains angalau waweze kukaa wakubaliane baadhi ya mambo ambayo technically lazima yafanyike kwa wananchi ili kudhibiti usalama wa wananchi na raia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumetokea malalamiko mara nyingi wanasema mtu amekamatwa, amehojiwa, ameshinda kituoni, amefanya nini. Labda niseme hiyo ndio kazi ya Uhamiaji waliosomea ni kukuita na kukuhoji na kukuruhusu urudi nyumbani au ulale ndani, hiyo ndio kazi waliosomea hakuna nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikueleze ukweli hatuna haja ya kukimbia na kuficha haya. Niliwahi kupigwa ile fomu ya kujaza ya uhamiaji, sasa nilipopewa kwanza nikajifikiria nikasema sasa hapa nafanyaje? Fomu ile kama sio raia wa Tanzania, niseme, huwezi kujaza ile fomu. Kama sio raia wa Tanzania halali ile fomu page ya kwanza tu chali, lazima uombe kwenda kukojoa mara mbili. Sasa ndio maana unaona…

T A A R I F A . . .

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, huyu naomba nisiendelee naye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachotaka kusema Idara ya Uhamiaji kazi yake ni kuita mtu, ni Mbunge uitwe, ni kiongozi wa dini uitwe, ni Waziri uitwe, wewe ukifika pale chukua fomu yako jaza ukimaliza tawanyika, unahofu nini? Unahofu nini na kulalamika kwamba kwa nini umehojiwa, unahofu nini? Kama una hofu it means wewe sio kweli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze Idara ya Uhamiaji, kwanza hii bajeti ni ndogo, ndio maana nasema nakusudia kushika shilingi, waongezewe pesa ili wakamate wengi, wahoji wengi. Maana kuna intervention ya watu wanaingilia kwenye hii mikondo na kutafuta kutengeneza umamluki na uharamia wa kutafuta hawa watu waendelee kupoteza laini, wanasema watu wanakufa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijawa Mbunge pale Dosidosi, Kiteto pale mpakani na Kongwa, nimefika pale Wahabeshi wamepita pale, mmoja kati yao akawa amezidiwa, ameumwa wherever kwenye gari, gari limeharibikia upande wa pili wakaisogeza, mtu wamemwacha porini amekufa na gari iko sealed. Leo unauliza watu wanakufa, wanaokufa ndio hao wanaotoka nje, sio Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka jana katikati, hapa Kiteto, Kongwa hii hapa, semitrailer imepaki pembeni, watu wameshushwa, ni Wahabeshi wamejaa gari zima wengine wame-faint, wengine wamekufa, hao hao ndio wanaokufa ambao sasa sisi hatuwezi, nchi au Uhamiaji au Polisi haiwezi kulaumiwa kwamba watu wanakufa, wanaokufa ni watu wa nje ambao still Tanzanian…

K U H U S U U T A R A T I B U . . .

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilichotaka kuzungumzia na huyo aliyenipa taarifa, hao wote wanaokufa mimi nilitarajia yeye atusaidie, aende aiambie polisi kwamba jamani kuna mtu amekufa hapa, ni Mtanzania, jamani fatilieni hili, kwa vyovyote vile atakuwa anawajua, huyu aisaidie polisi. Nataka kuishauri idara yetu hii iendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo nataka kushauri hawa watu wa NIDA wa vitambulisho. Kwenye hii mikoa ya mipakani watu wanazungumza lugha moja wanazungumza wanaelewana huku na huku, niombe kwamba… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kuisha kwa muda wa Mzungumzaji).