Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Waziri kwanza nakupongeza kwa hotuba nzuri kuhusu Sekta ya Kilimo na Mifugo na naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja. Naomba nichangie maeneo machache.
Sekta ya Mifugo; Kwanza Wilaya ya Mpwapwa kuna taasisi tatu za Mifugo ambazo ni Taasisi ya Utafiti wa Mifugo ya Mpwapwa (TALIRI), Chuo cha Mifugo Mpwapwa (LITA), Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo (VIC).
Mheshimiwa Waziri, taasisi hizi zote tatu zinategemeana. Taasisi ya Utafiti wa Mifugo-Mpwapwa, ng‟ombe akiugua lazima apelekwe Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo ili achunguzwe anasumbuliwa na nini au Ng‟ombe akifa lazima wapeleke mzoga huo (VIC), Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo ili afanyiwe post-mortem ili kufahamu ugonjwa gani unasababisha ng‟ombe kufa. Vile vile Mpwapwa kuna Chuo cha Mifugo cha Mpwapwa na pale kuna wanafunzi zaidi ya 360,000 wote hawa wanatumia Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa kwa mafunzo ya vitendo.
Mheshimiwa Waziri kwa sasa, Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo (VIC) Mpwapwa imehamishiwa Dodoma Mjini na kusababisha Taasisi ya Utafiti wa Mifugo na Chuo cha Mifugo (wanafunzi wake) kukosa mahali pa kuchunguza mifugo na wanafunzi kukosa mahali pa kujifunzia kwa vitendo na inabidi wasafiri kuja Dodoma na ni gharama kubwa na ni mbali, pia hupoteza muda mwingi wa masomo.
Mheshimiwa Waziri, taasisi hizi zilijengwa kabla ya uhuru na wakoloni. Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI) ilianza mwaka 1905; Chuo cha Mifugo (LITA) kilianza mwaka 1936 na Taasisi hizi tatu zinategemeana. Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi alikataa Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa isihamishwe na kupelekwa Dodoma na mwaka 2015 wakati wa kampeni, Rais, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli alikataa isihamishwe Dodoma Mjini.
Mheshimiwa Waziri, suala la kusikitisha taasisi hiyo imehamishwa Dodoma Mjini na suala hilo la kuhamishwa taasisi hiyo limewafanya wananchi wa Wilaya ya Mpwapwa kukosa mahali pa kupeleka mifugo yao wagonjwa waweze kuchungwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ombi la wananchi wa Wilaya ya Mpwapwa, Taasisi ya Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo irudishwe Mpwapwa haraka kabla hawajamwona Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.