Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2017 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019 na Mapendekezo ya Serikali kuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili niweze kutoa mchango mkubwa katika Wizara hii, Wizara mama ambayo kwa kweli tunaitegemea.

Mheshimiwa Spika, katika Wizara hii mimi nina wasiwasi kidogo. Wasiwasi wangu ni kwamba juzi Mheshimiwa Mpango ameonesha kwamba bajeti hii ametoa punguzo kwenye viwanda, maana yake amewasaidia wafanyabiashara wa ndani, lakini ameishia hapo hakwenda mbali zaidi, hii mimi imenitia wasiwasi sana. Kwa kuwa hakwenda mbali zaidi ina maana kwamba karibu asilimia 70 ya wananchi wa Tanzania ni wakulima.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tulitegemea kuwa hiyo asilimia 35 ambayo ameiongeza kwenye ushuru au kodi maana yake sasa angerudi tena kwa wakulima wa nchi hii ambao ni wakulima wa alizeti, korosho, mahindi na karanga ili ahakikishe kwamba anawawezesha hawa Watanzania ili tupate raw material ya kwenda viwandani; lakini hilo hakulifanya Mheshimiwa Mpango. Kwa sababu hiyo sasa kunakuwa na ugumu wa jinsi ya kupata raw material katika hili.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimuombe Mheshimiwa Mpango atakapokuja atueleze, kwamba, je, kama amepunguza kwenye viwanda, akishapunguza au akishaongeza kodi kwenye raw material ambayo ni imported maana yake hivyo viwanda usipowezesha wananchi wa ndani vitakuwa stagnant, kwamba hakutakuwa na raw materials kutoka nje wala hakutakuwa na raw materials ambayo iko ndani. Itakuwa kama wanavyosema Wamakonde, kwamba, uchiteme wala uchimumunye, maana yake huwezi kusogea, utakuwa huna raw materials kutoka nje wala ya kutoka ndani.

Mheshimiwa Spika, maana yake ni nini sasa kama huna raw materials kutoka nje wala huna raw material ya ndani maana yake ni hivi viwanda vyote vitasimama kwa wakati mmoja na watatengeneza shida ambayo ni kubwa sana. Kwa hiyo aangalie namna atakavyovifanya hivi viwanda. Leo tunasema hapa kwamba amewasaidia wafanyabiashara, lakini sidhani kama amewasaidia wafanyabiashara, atakuwa amewaweka njia panda kwa sababu production ya ndani ya raw material kwa ajili ya viwandani, hamna njia yoyote au hajaweka process ambayo tutahakikisha kwamba tunapata.

Mheshimiwa Spika, nina wasiwasi kwa sababu mwaka jana wananchi walipolalamikia kuhusu upande wa kilimo alisema kwamba atasaidia wakulima, kwanza kwa kufanya importation in bulk kwa upande wa mbolea. Wale wananchi hawakusaidiwa, kwenye mambo ya bulk importation. Mwaka jana alichokifanya ni kupunguza ushuru, ule ushuru wa mazao kutoka asilimia tano hadi asilimia tatu. Alitengeneza nini baada ya pale? Maana yake ni kwamba waliopata nafuu ni wachuuzi, kwa sababu sheria inasema kwamba asilimia tano, maana yake kwamba ushuru utalipwa na mnunuzi, kwa hiyo unavyosema kwamba umepunguza hadi asilimia tatu unakuwa hukumsaidia mkulima na badala yake umemsaidia mnunuzi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo maana yake wakulima pale wakawa wamepigwa changa la macho ambalo hawakuliona, tukadhani kwamba, ok utafidia kwenye mambo ya importation.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka huu vile vile imetokea, Mheshimiwa Waziri amesema kwamba ok, sasa tunataka ushuru wa mazao, kwa mfano huu wa korosho, maana Sheria ya Korosho tunayo, anasema kwamba asilimia 35 ya mazao ya korosho yatakwenda kwenye Mfuko Mkuu na asilimia 65 itarudi tena kwenye Bodi ili kuwezesha wale wakulima wa korosho waweze kuhakikisha kwamba wanapelekwa kwenye taasisi kwa mfano Naliendele.

Mheshimiwa Spika, wakifanya tafiti zile huu ugonjwa wa mnyauko, maana yake hautakuwepo. Sasa anavyong’ang’ania pesa zote bilioni mia mbili, akitegemea kwamba mwakani atapata kutoka wapi? Nimwombe Mheshimiwa Dkt. Mpango, kwamba ni vizuri zile fedha za korosho ambazo anazo katika mfuko wake ambazo haku- release; maana leo mfuko wa sulphur unauzwa Sh.65,000, kwa hiyo ile production ya mwaka jana ambayo alipata bilioni mia tatu sitini na tano asitarajie mwaka huu kwamba atapata kwa sababu hiyo sulphur haipo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Waziri asitarajie kupata yai la dhahabu kwa kumchinja kuku mwenyewe badala ya kumwezesha yule kuku aendelee kutaga ili apate kidogo kidogo. Kwa hiyo natarajia kabisa mwaka huu inawezekana kabisa kwa namna yoyote asipate zile bilioni mia tatu sitini na tano; kwa hiyo, maana yake atatuweka katika hali ngumu sana Mheshimiwa Dkt. Mpango. Hebu afanye utaratibu kwa kuhakikisha kwamba hawa wakulima wanapata zile pembejeo za kilimo, ili mwakani aweze kupata fedha za kutosha.

Mheshimiwa Spika, lingine, namsifu sana Mheshimiwa Mpango, kwamba ni mkusanyaji mzuri wa mapato. Hata hivyo Mheshimiwa Dkt. Mpango, halipi madeni kwa ma- supplier wa ndani. Asipowalipa ma-supplier wa ndani maana yake hakuna mzunguko wa fedha wa humu ndani, mzunguko wa ndani usipokuwepo, maana yake umaskini utakuwepo kila mahali, utakuwepo Arusha, utakuwepo Singida, Utakuwepo Dodoma, utakuwepo kila mahali. Kwa hiyo nimwombe sana alipe …

T A A R I F A . . .

MHE. AJALI R. AKBAR: Mheshimiwa Spika, nashukuru hiyo taarifa nimeipokea na hiyo taarifa vile vile Mheshimiwa Dkt. Mpango naomba aipokee; kwamba ule mchezo alioufanya, sasa hivi unatupeleka mahali pabaya. Zile fedha ambazo mwaka huu alipata, bilioni mia tatu sitini na tano, mwaka huu alitarajia labda angepata bilioni mia saba hizo fedha hatazipata tena. Maana yake si ajabu, ule mnyauko uko kule na mikorosho inakauka na ni mikavu sana.

Mheshimiwa Spika, namwombe Mheshimiwa Dkt. Mpango, in future, ahakikishe kwamba hawa wakulima na hizi taasisi zake hizi, hasa Naliendele au zile ambazo ni za kilimo ahakikishe zile fedha zinaenda mapema ili production kwa wakulima iende kwa wakati na uzalishaji uende kwa wakati ili waweze kupata fedha nyingi zaidi.

Mheshimiwa Spika, kama akiendelea kung’ang’ania hizi fedha, akiwa nazo mfukoni atazitumia mwisho hata hizo kidogo hatazipata Mheshimiwa Mpango. Nimwombe sana, najua TRA kama nilivyomwambia kwamba ni kweli anakusanya vizuri na atumie mbinu ambazo kwa kweli ni shirikishi kwa wafanyabiashara, maana TRA wanajifanya kana kwamba ni polisi, wanawatisha wafanyabiashara mpaka wale wafanyabiashara wanaogopa.

Mheshimiwa Spika, namwambia Mheshimiwa Waziri wenzake tulikusanya ushuru wa mazao lakini tulikuwa tunawashirikisha hawa wafanyabiashara kiasi kwamba ukienda mtu anakulipa yeye mwenyewe; usiende pale kwa vitisho. Aangalie hii Taasisi yake ya TRA iwe shirikishi na ishirikiane na wafanyabiashara ili akusanye mapato vizuri, isiwe kwamba wakiwaona TRA wanakimbia wanafunga maduka; huo si utaratibu wa kukusanya fedha. Naomba TRA wawe rafiki kwa wafanyabiashara ili mapato ya nchi yetu yapate kuongezeka na yeye mwenyewe itakuwa rahisi katika utendaji wake wa kazi, vinginevyo atakuwa anapata ugumu kila siku.

Mheshimiwa Spika, la pili, Mheshimiwa Dkt. Mpango, kwa hizi asilimia tano kuzipunguza mpaka asilimia tatu amezifanya halmashauri ziwe maskini. Leo halmashauri zinashindwa kulipia yale mahitaji muhimu. Anazitaka halmashauri leo zilipie bili ya maji, lakini ceiling yetu amepunguza ile kutoka asilimia tano hadi tatu, sasa hizo fedha zitatoka wapi ikiwa kila siku anatoa maagizo kwamba kuwe na miradi huko, fedha zinatoka wapi?

Mheshimiwa Spika, kana kwamba hiyo haitoshi halmashauri haziendelea kwa sababu hata hizi property tax amewanyang’anya, maana yake fedha zote sasa hivi badala ya kuwa kwenye Local Government ziko kwenye Central Government. Hii inamaanisha kwamba tunarudisha utawala wa kiimla, wa kizamani, kwamba hakuna ushirikishwaji katika miradi kutoka kwenye Local Government, miradi yote inatoka Serikali Kuu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimwombe Mheshimiwa Dkt. Mpango kwamba, arudishe utaratibu kama Mzee wetu Mwalimu Nyerere alivyokuwa amesema kwamba tunatoa madaraka mikoani, tunapeleka huko chini ili kuhakikisha wananchi wanashirikishwa katika mapato ili miradi hii iwe shirikishi, badala ya kila kitu kwenda Serikali Kuu; inakuwa ni ngumu kiutendaji; nimwombe sana awashirikishe wananchi katika hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo mchango wangu ni huo, ila nimwombe sana Mheshimiwa Mpango aache kung’ang’ania zile fedha za korosho, atoe release ili watu wapate kununua zile pembejeo muhimu za kimsingi za kilimo.

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.